Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 37
    1. #1
      Zak Malang's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th December 2008
      Posts : 4,835
      Rep Power : 1922
      Likes Received
      187
      Likes Given
      2

      Default Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Mwandishi wa habari mahiri, mhariri na wakili wa kujitegemea, Nyaronyo Mwita Kicheere, ambaye wakati fulani alikana jina lake hilo na kusema kuanzia sasa anaitwa Ridhiwani Jakaya Kikwete, ameamua kuwapasha ukweli wahariri wenzake nchini. Akiandika katika mtandao wa wanabidii, Nyaronyo (RIZ) amesema wahariri wanajikomba kwa serikali na amewataja baadhi yao kwa majina. Hili hapa ndivyo alivyoandika:

      ndugu wanamabadiliko,
      mimi nakubaliana na wale wanaosema dk nchimbi alialikwa jangwani. nimelazimika kuingilia kati na kutoa ushahidi wa kiapo kwa vile naona kama vile ukweli hausemwi. maoni yangu ni kwamba watu wakubali ukweli hata kama unauma na ukweli wenyewe unapatikana kutokana na ushaidi wa mazingira (circumstantial evidence):

      KIAPO CHENYEWE;
      MIMI nyaronyo mwita kicheere, mtu mzima, mpagani na mkazi wa tungi, kigamboni, dar es salaam, tanganyika territory (pamoja na sehemu za ziwa nyasa), NAAPA kwa mizimu ya nyamongo na KUTAMKA yafuatayo:
      1. KWAMBA mimi nyaronyo mwita kicheere, nilikuwepo, nilishiriki na nilichunguza kwa makini nyendo za watu fulani fulani kwenye maandamano ya wanahabari yaliyofanyika jumanne wiki hii kwa hiyo nafahamu ukweli wa haya ninayoyaeleza hapa chini.
      2. KWAMBA baada ya kuandamana kutoka ofisi za channel ten hadi viwanja vya jangwani hatukukuta maandalizi yoyote ya maana pale viwanjani jangwani kwa maana kwamba hakukuwepo jukwaa wala vipaza sauti.
      3. KWAMBA muda mfupi tu baada ya kuwasili zilisikika sauti na minong'ono ya chinichini hasa ya akina mama wakipinga ujio wa dakitari wetu mtukuka nchimbi na kwamba kwa sababu ya ufupi wake nchimbi hakuwa ameonekana kwa wengi wala kufahamika kuwa alikuwapo.
      4. KWAMBA mimi binafasi nilichukua jukumu la kuwahoji wale wanahabari wa kike, kama huyo nchimbi wanayemlalamikia ni nani, na yuko wapi, na kaja kufanya nini pale jangwani kama yeye si mwanahabari.
      5. KWAMBA wanahabari wale wa kike walinielekeza mimi pamoja na wenzangu tuliokuwapo jirani nao mtu waliyedai ni dakitari mtukuka nchimbi na wakadai kuwa mtu yule hakuwa na lolote la kuuambia ummati ule wa wanahabari kwa sababu wauaji ni serikali na nchimbi ni sehemu ya serikali.
      6. KWAMBA mimi pamoja na wenzangu tuliokuwa tumesimama jirani na wanahabari wale wa kike tulisaidia kusema na kupaza sauti kuwa nchimbi hahitajika kwenye mkutano ambao serikali ilikuwa inalaaniwa kwa vitendo vya watendaji wake na hasa polisi ambao wanapaswa kulinda amani, mali na uhai wa raia lakini wao wanashiriki kuua!
      7. KWAMBA nchimbi kwa kujiamini kabisa alitukonyeza kuashiria kufahamiana sana na sisi na kwamba yeye ni mwenzetu. zipo ishara, vitendo na mwonekano (body language) vinavyoashiria kuwa mhusika ni mwenyeji tena alwatan na hivyo hababaiki wala kuterereka na yanayotokea mfano ukonyezaji.
      8. KWAMBA kitendo cha kutukonyeza badala ya kuondoka viwanjani jangwani kilituudhi wandishi na hasa wanahabari wa kike ambao waliongeza sauti zao kumkana nchimbi na kumtaka aondoke jangwani ili kuwaacha wanahabari waomboleze peke yao kifo cha mwenzao.
      9. KWAMBA pamoja na kelele za "nchimbi ondoka kuongezeka", msemaji wa jukwaa la wahariri (charles misango) alipopanda kwenye rundo la udongo lililogeuzwa jukwaa kutokana na kutokuwepo maandalizi ya maana naye nchimbi alimfuata jirani na kupanda jukwaa lile la rundo la udongo kama mtu aliye tayari kutoa hotuba.
      10. KWAMBA hapo ndipo uzalendo ulipowashinda wandishi na kilichofuata ni biashara inayofahamika kwetu wote wanahabari, mashushushu (ambao siku ile hawakuwa wanahesabika pale jangwani kwa wingi wao), mapolisi na wananchi kwa ujumla.
      11. KWAMBA baada ya sakata lile la kumwondoa nchimbi mkutanoni na akaondoka kwa aibu zote zinazoweza kuelezeka, wandishi wa itv walimfuata pembeni na kumhoji na baadaye siku hiyo kumwonyesha na kumtangaza nchimbi eti wakitaka kujua sababu za yeye kuvamia maandamano ya wanahabari.
      12. KWAMBA kwa uelewa wa mtu wa kawaida, itv wanashukiwa kuhusika na kumwalika nchimbi jangwani. kwa nini wamfuate mtu kumhoji baada ya kumtimua? unamtimua wa nini kama unamhoji na kumtangaza si bora ungemwacha basi akahutubia wandishi halafu mkapata habari ya kuonyesha na kutangaza kama lengo na nia yenu itv ilikuwa habari za nchimbi na siyo maombolezo ya mwangosi? kitendo hiki hakivumiliki na kilitudhalilisha sana wanahabari. mnamfukuzaje mtu halafu mnamkimbilia kumlamba miguu?
      13. KWAMBA ninakumbuka kuwa hii si mara ya kwanza itv kufanya jambo la kinafiki na la hovyo kama hili. huko nyuma, wandishi waliwahi kukubaliana kutomquote wala kumwandika waziri Mkuchika hata angefanya nini duniani hapa. lakini siku mkuchika alipokuwa anahutubia jambo fulani na akatamka mema kadhaa kumhusu mwenyekiti wa IPP r.a.mengi maamuzi ya wanahabari yalitupiliwa mbali na mkuchika akatangazwa na kuonyeshwa kwenye runinga za itv na ipp akimsifia bwana mkubwa bila kujali mgomo uliokuwepo!
      14. KWAMBA pamoja na itv mtu mwingine ninayemtuhumu na kumshutumu kwa kumwalika nchimbi ni katibu wa jukwaa la wahariri bw. nevil meena. huyu bwana alitoa hotuba nzuri sana lakini akamalizia hotuba yake na maneno mabaya sana.
      15. KWAMBA meena alisikika akisema; hatuna ubaya na nchimbi, tunampenda nchimbi, hatuna ugomvi na serikali, hatuna ugomvi na polisi! jamani mwenye mkanda na akausikilize vizuri. sasa kama wanahabari hawakuwa na ugomvi na serikali maandamano ya nini? kama wanahabari hawana matatizo na polisi je matamko na kulaani alikuwa analaaniwa nani na kwa nini? kama wanahabari hawakuwa na tatizo na nchimbi je kwa nini walimtimua? mimi nina mashaka makubwa sana kuwa huyu bw. meena ndiye alimwalika nchimbi.
      16. KWAMBA nyie wahariri kupitia kwa katibu wenu mlikuwa mnajipendekeza kwa nchimbi kwa nini? nyie wahariri mlikuwa mnajifanya wazuri kwa nchimbi eti wabaya ni wanahabari wanaomtimua nchimbi mlikuwa mmeahidiwa nini? si bure, mpaka mkajitoa bila aibu vile kumtukuza nchimbi, serikali na polisi kupitia kwa meena baada ya kutoa hotuba ya kulaani na kukerwa na serikali na polisi, hakukuwa bure kuna jambo. mlimwahidi aje na mtampatia nafasi ya kuongea naye kwa kujua 2015 yaja kajiingiza kichwa kichwa na kaja kweli.
      17. KWAMBA baada ya hotuba zile kabla hatujaondoka jangwani nilikaa jirani na wahariri fulani (nawakumbuka watatu, jesse kwayu wa nipashe, bakari machumu wa the citizen na dennis msacky wa mwananchi) na hapa jesse kalikoroga kwa kuhoji "hivi nchimbi hawezi kuelewa mahali pa kuhudhuria na wapi kutohudhuria?"
      18. KWAMBA kwa mshangao wa wengi dennis msacky alijibu kwamba nchimbi kagain political capital! jibu hili lilipingwa na wote, jesse, bakari nakumbuka hata mimi nilipinga. tukajaribu kumwonyesha msacky namna alivyoaibika nchimbi na hakupata ujiko wowote huku yeye aking'ang'ana "ehe huoni yeye kafika hapa ni waziri pekee aliyekuja hii ni njema ni political capital"! hakuna aliyemsikiliza na sote kwa pamoja tulimbamiza hadi akakubali kuwa rafiki yake kachemka. nasikia dennis ni rafiki yake kipenzi dk nchimbi. nami nasema namtilia shaka sana dennis kuwa naye alihusika kumwalika nchimbi jangwani.
      kicheere, tungi kigamboni tanganyika territory

      uthibitisho:
      mimi nyaronyo mwita kicheere nathibitisha kwamba yote niliyoyasema hapo juu hasa aya ya 1 -18 ni kweli tupu na si kitu kingine bali ukweli mtupu.
      kicheere, tungi kigamboni tanganyika territory

      ubaya ni kwamba ukweli huu unalifanya jukwaa la wahariri kuwa jukwaa la wanafiki hata kama si wote ni wanafiki. watu wako kwenye jukwaa kugain materially na politically. yaani kujiweka katika good books of government!!!!!!!! usiku mwema
      August, jmushi1, Kinyungu and 11 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Dr. Wansegamila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Location : Kwetu pazuri
      Posts : 345
      Rep Power : 2082
      Likes Received
      143
      Likes Given
      88

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      We really have a long way to go!!
      'HAKIMU AKIWA FISI, HUKUMU YA MBUZI NI KIFO'

    4. #3
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,953
      Rep Power : 754
      Likes Received
      281
      Likes Given
      147

      Default

      Mambo hayo!

    5. #4
      activist's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th April 2008
      Posts : 108
      Rep Power : 588
      Likes Received
      33
      Likes Given
      0

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Msaki ni alikuwa Mwalimu wangu Tumaini! Namfahamu fika! Ni mtu wa kujipendekeza kwa systeme sana!

    6. #5
      white wizard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2011
      Posts : 477
      Rep Power : 501
      Likes Received
      114
      Likes Given
      12

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      huyu bwana ni noma!ndio watu tunao wataka na sio wale wanafiki.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Kachanchabuseta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2010
      Posts : 2,977
      Rep Power : 1054
      Likes Received
      440
      Likes Given
      1133

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Quote By SPANNER
      3. KWAMBA muda mfupi tu baada ya kuwasili zilisikika sauti na minong'ono ya chinichini hasa ya akina mama wakipinga ujio wa dakitari wetu mtukuka nchimbi na kwamba kwa sababu ya ufupi wake nchimbi hakuwa ameonekana kwa wengi wala kufahamika kuwa alikuwapo.
      Hapo kwenye RED Daktari wetu??????

      Hizo bangi


    9. #7
      Duduwasha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 2,620
      Rep Power : 6249
      Likes Received
      523
      Likes Given
      418

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Nape keshapenyeza System yake Mule Umoja ni Mgumu kumbe kwenye Tansnia ya Habari hata Star Tv wanaogopa kutangaza Mada watakazozitoa Baada ya Wiki sababu Mada Huibiwa na Wenzao... Unafiki uishe basi wana habari iwe kama Boti za Zanzibar walikuwa hivi hivi hadi baadae wakaelewana

    10. #8
      Ta Kamugisha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th May 2011
      Posts : 1,045
      Rep Power : 3609
      Likes Received
      268
      Likes Given
      23

      Default

      Quote By Kachanchabuseta
      Hapo kwenye RED Daktari wetu??????

      Hizo bangi

      kaka unatuchosha kureplay kwenye topic nzima, wengne twatumia simu, kuwa na busara na uwe mwelewa, nukuu kpande kdogo unachotaka kuongelea na c story nzima, hii c kwako pekeyako hata wale wenye tabia kama yako

    11. #9
      josefast's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th December 2011
      Location : Mtaa wa chini
      Posts : 86
      Rep Power : 394
      Likes Received
      4
      Likes Given
      32

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      hilo nalo neno! Nchimbi alipata aibu ya mwaka bila shaka baada ya pale alikwenda kuomboleza kwa kilio cha samaki

    12. #10
      Ubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 1,151
      Rep Power : 589
      Likes Received
      204
      Likes Given
      185

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Siku zote bame game ikianza ni kwamba mambo si salama.

    13. #11
      MPIGA ZEZE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th May 2011
      Posts : 579
      Rep Power : 521
      Likes Received
      205
      Likes Given
      200

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Tanganyika Territory inahitaji watu kama wewe. Ila kazi bado tunayo kama 'political capital' ndo za aina hii!!!! mediocre cabinet ministers & journalists!!!

    14. #12
      chumvichumvi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2010
      Location : Kwenye Mapambano
      Posts : 356
      Rep Power : 531
      Likes Received
      42
      Likes Given
      42

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      wakili pitia nakala yako vizuri utaona mapungufu as hata ww pia wamtukua huyu waziri husika

    15. #13
      WAHEED SUDAY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2011
      Posts : 2,846
      Rep Power : 2972
      Likes Received
      479
      Likes Given
      318

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Quote By Kachanchabuseta
      Hapo kwenye RED Daktari wetu??????

      Hizo bangi

      Mkuu hapa mwandishi katumia lugha ya kilemba cha ukoka wala usiwe na wasiwasi, elewa maudhui ya mwandishi kwanza
      Lokissa likes this.
      Just a charcoal, don't expect anything white

    16. #14
      Mwana Mpotevu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th September 2011
      Posts : 1,973
      Rep Power : 857
      Likes Received
      909
      Likes Given
      878

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Nashukuru Kicheere kwa kuthibitisha kile nilichokiandika juzi kuhusu Meena kumwalika Nchimbi ingawa wengine hawataki kuamini.
      Don't break the LAW, just Bend It!

    17. BAK
      #15
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,633
      Rep Power : 44971
      Likes Received
      8386
      Likes Given
      8363

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Tafakuri Jadidi
      Ridhiwan na Salma Kikwete wanapopita bila kupingwa….!

      Johnson Mbwambo

      Toleo la 258
      12 Sep 2012





      • Ni zama za mama na mwana


        TOLEO lililopita niliandika makala kwenye safu hii iliyobeba kichwa kinachosomeka: Tumsaidie Sitta kuona asichokiona CCM. Katika makala hiyo nilijaribu kueleza namna chama tawala, CCM, kilivyopoteza mvuto kwa wananchi kwa sababu ya ukaidi wake wa kukataa kubadilika na kujirekebisha.
        Nilieleza kwamba CCM ya sasa ni kivuli cha CCM asilia ya enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, na kwamba sasa kimepoteza kabisa mwelekeo kwa kugeuka kuwa chama cha matajiri kilichowatelekeza wakulima na wafanyakazi.
        Nilijaribu kutoa mifano ya mambo ya hovyo yanayotokea hivi sasa ndani ya chama hicho, ambayo enzi za Mwalimu Nyerere usingeweza hata kufikiria kwamba yanaweza kutokea – mambo kama vile viongozi kutoleana bastola hadharani, nk!

        Leo, niendeleze kidogo tafakuri hiyo kwa kutoa mfano mwingine wa sasa wa kitu kinachotokea ndani ya chama hicho na kukubalika ambacho enzi za Mwalimu hakikuonekana sana katika mienendo ya chama hicho.

        Nazungumzia tabia za watawala wa sasa ndani ya chama hicho kubebana kindugu au kifamilia katika chaguzi za chama. Hali hii pia imeanza kuonekana ndani ya serikali yake, kwenye ajira muhimu za makampuni, na hata katika duru za biashara kubebana kindugu ndio umekuwa wimbo wa wakubwa.

        Raia Mwema - Ridhiwan na Salma Kikwete wanapopita bila kupingwa

      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    18. #16
      Tuyuku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 658
      Rep Power : 560
      Likes Received
      139
      Likes Given
      16

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      safi sana Nyaronyo

    19. #17
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,483
      Rep Power : 1116
      Likes Received
      470
      Likes Given
      962

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Nyaronyo wewe kweli ni mtanzania halisi ndio watu tunaowahitaji ukweli mbele, utaifa mbele hela inakuja tu kama Mungu amekuandikia fanya kazi kwa uadilifu utapata haki yako na utaitumia kwa manufaa ya taifa na familia yako kwa ujumla. Hongera sana Mungu azidi kukupa ujasili kama huu uliouonyesha

    20. #18
      Mzee Mukaruka's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th June 2012
      Posts : 86
      Rep Power : 366
      Likes Received
      18
      Likes Given
      19

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Kweli kabisa poti! Tuko nawe hadi kieleweke, kama sio leo basi ni hapo 2015! Hili ni kwa kila mpenda haki wa nchi yetu Tanganyika.

    21. #19
      Josephine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th September 2010
      Posts : 699
      Rep Power : 730
      Likes Received
      756
      Likes Given
      134

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Nimeipenda hii.

      Nilimuona namna alivyokuwa akijikanyaga katika kongamano la wanaharakati TGNP.
      This guy ni DANGER.

      ndiyo maana nasema CCM wamefanikiwa katika maeneo mengi kuwagawa watu hasa maeneo yote yenye kushughulika na Taaluma.Madaktari,Walimu na Waandishi.Ni ngumu kutoka inahitaji viongozi jasiri na kanunu kubadilishwa za uanachama katika vyombo husika.

      Nitaendelea kusisitiza,CCM mtajaribu kote,but Chadema kiboko yenu.Hamuwezi,Hamtaweza na Tutawamaliza.
      KIJOME likes this.
      Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shahuri la wasio haki;wala hakukusanyika katika njia ya wakosaji;wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

    22. #20
      tatanyengo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th March 2011
      Posts : 931
      Rep Power : 599
      Likes Received
      221
      Likes Given
      186

      Default re: Nyaronyo M. Kicheere: Wahariri waoga, au wanajipendekeza kwa Nchimbi!

      Kila idara katika nji hii in watu wanaojipendekeza na watu wa system.But hilo lisitukatishe tamaa katika harakati za ukombozi.
      'Our Problems can be solved,our challenges can be met'- Obama

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...