Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 30
    1. #1
      Mystery's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 8th March 2012
      Posts : 609
      Rep Power : 484
      Likes Received
      213
      Likes Given
      150

      Default Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Tumeshuhudia tokea Mwangosi auawe kinyama na polisi, septemba 2, mwaka huu, na jinsi, jeshi hilo la polisi, lilivyojitahidi kwa juhudi zote, kujifanya kuwa wao hawakuhusika, badala yake wakadai, kuna kitu kizito kimerushwa toka kwa wafuasi na viongozi wa Chadema, lakini kwa jinsi Mungu alivyo mkuu, aliwapa ujasiri wapiga picha, wakapata picha zenye ushahidi wa wazi, kuwa polisi ndiyo wamehusika na mauaji hayo. Sasa wasiwasi wa wananchi wengi ni kuwa huyo polisi waliyemfikisha mahakamani, wamelazimika tu kumfikisha mahakamani, kutokana na shinikizo kubwa sana la vyombo vya habari na wananchi, pamoja na wanaharakati. Sasa kutokana na mlolongo wa matukio, kama vile kumfikisha mtuhumiwa mahakamani na gari la kifahari, la Land Cruiser, polisi kuzuia kabisa, mtuhumiwa huyo, asipigwe picha na paparazi. Vile vile, kitendo cha Kamuhanda kutoshtakiwa na kuendelea na kazi, wakati inafahamika wazi kuwa yeye, ndiye aliyesimamia hiyo operesheni ya mauaji ya Mwangosi. Kwa mazingira hayo nadhani ipo haja kwa wanaharakati na wanasheria wazalendo, kutoa taarifa ya kuwa hatuna imani na mahakama hiyo, kama mashahidi wa kesi hiyo, ndiyo hao hao mapolisi, wanaozuia hata mtuhumiwa asipigwe picha! Kwa hiyo nadhani ingekuwa vyema, wanasheria wazalendo wakaangalia vifungu vya sheria, vinavyoweza kuruhusu kesi hiyo, ihamishiwe mahakama ya kimataifa,ya the Hague, ambako tunaamini haki itaweza kutendeka

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Mlyafinono's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Posts : 131
      Rep Power : 385
      Likes Received
      42
      Likes Given
      1

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Hatakama watazuia haki kutendeka lakini Damu ya Mwangosi haiwezi kwenda bure katika midomo ya ardhi.They will pay for it

    4. #3
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,020
      Rep Power : 956
      Likes Received
      333
      Likes Given
      33

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mystery
      Tumeshuhudia tokea Mwangosi auawe kinyama na polisi, septemba 2, mwaka huu, na jinsi, jeshi hilo la polisi, lilivyojitahidi kwa juhudi zote, kujifanya kuwa wao hawakuhusika, badala yake wakadai, kuna kitu kizito kimerushwa toka kwa wafuasi na viongozi wa Chadema, lakini kwa jinsi Mungu alivyo mkuu, aliwapa ujasiri wapiga picha, wakapata picha zenye ushahidi wa wazi, kuwa polisi ndiyo wamehusika na mauaji hayo. Sasa wasiwasi wa wananchi wengi ni kuwa huyo polisi waliyemfikisha mahakamani, wamelazimika tu kumfikisha mahakamani, kutokana na shinikizo kubwa sana la vyombo vya habari na wananchi, pamoja na wanaharakati. Sasa kutokana na mlolongo wa matukio, kama vile kumfikisha mtuhumiwa mahakamani na gari la kifahari, la Land Cruiser, polisi kuzuia kabisa, mtuhumiwa huyo, asipigwe picha na paparazi. Vile vile, kitendo cha Kamuhanda kutoshtakiwa na kuendelea na kazi, wakati inafahamika wazi kuwa yeye, ndiye aliyesimamia hiyo operesheni ya mauaji ya Mwangosi. Kwa mazingira hayo nadhani ipo haja kwa wanaharakati na wanasheria wazalendo, kutoa taarifa ya kuwa hatuna imani na mahakama hiyo, kama mashahidi wa kesi hiyo, ndiyo hao hao mapolisi, wanaozuia hata mtuhumiwa asipigwe picha! Kwa hiyo nadhani ingekuwa vyema, wanasheria wazalendo wakaangalia vifungu vya sheria, vinavyoweza kuruhusu kesi hiyo, ihamishiwe mahakama ya kimataifa,ya the Hague, ambako tunaamini haki itaweza kutendeka
      wangekuruhusu ukapiga izo picha, zingesaidia lolote kwenye ushahidi? kwa wao kuzuia kupiga picha, je? kuna defect yeyote kwenye ushahidi? uliwauliza watoe sababu yeyote ya kwanini wanazuia kupiga picha na kwanini wamemleta kwa escort ya landcruiser na ulinzi kabambe wa polisi? pengine wangekuwa na sababu maalumu kukueleza na ungepata jibu hukohuko wala usingeleta hapa.

      kuhusu kutokuwa na imani na mahakama husika, unataka watu waikatae mahakama hiyo kwamba hawana imani nayo halafu shauri lipelekwe mahakama ipi? kwani mahakama ile ya wilaya/mkazi ndiyo yenye mamlaka kusikiliza shauri la mauaji?....kwaakili yako unafikiri mahakama ile ndiyo itakayosikiliza kesi hiyo?

      kwa ushauri na kufahamishana ni kwamba, pale ile kesi haitasikilizwa na mahakama ile, labda kwa direction ya High court ikaliwe pale kama ni RM kwa extended power. ila shauri lile lipo pale wakati uchunguzi unaendelea, upelelezi ukikamilika vijalada vitafungwa na accused atakuwa committed to the High court...yaani pale PI yake itakapofungwa...hapo lipo kwaajili ya committal proceeding tu...na si vinginevyo...kwahiyo usiwe na wasiwasi, wala usipotezee watu muda kujadili hili, kwasababu mahakama itakayosikiliza shauri lile siso ile ya wilaya/mkazi, ni mahakama kuu na kutakuwa na majaji sio mahakimu, na kama upande wa mashitaka hawataridhika kuna nafasi kukata rufaa hadi court of appeal.

      kuhusu mashahidi kuwa ni polisi...hapana, sio polisi peke yake, hata wewe kama una maelezo yeyote yatakayosaidia kwenye ushaidi nenda pale polisi iringa katoe maelezo watakuweka kwenye folio C na utakuwa shahidi mzuri tu, hata wale polisi waliopiga picha na wananchi wa kijiji kile kama hawatakataa kutoa maelezo watakuwa mashahidi wazuri tu wakichukuliwa maelezo. hivyo si polisi peke yao watakaotoa ushaidi....kama hujaelewa chochote uliza nitakujibu.
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    5. #4
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,020
      Rep Power : 956
      Likes Received
      333
      Likes Given
      33

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mlyafinono
      Hatakama watazuia haki kutendeka lakini Damu ya Mwangosi haiwezi kwenda bure katika midomo ya ardhi.They will pay for it
      wewe ndio umeongea point, mahakama za hapa duniani si mahakama za haki. kuna sababu nyingi tu, hata ushahidi na mashahidi vinaweza kuharibiwa na kesi kufa. kuna mambo mengi yanaweza kufanya kesi isishinde. sasa, cha kuelewa ni kwamba, mhukumu mkuu ni Mungu aliye juu, aliyeumba mbingu na dunia na kila mtu aliyepo duniani, huyo ndiye anayeweza kuhukumu na kutoa kisasi. imeandikwa kisasi si cha mwanadamu, kisasi ni changu mimi Mungu, ....ina maana kwamba, wanadamu hatuwezi kutoa kisasi kikakolea, anayejua kutoa kisasi na kuhukumu na hukumu ikakolea na ikawa ya haki, ni Mungu aliye juu...huyu ndiye hakimu na jaji wa kila mtu. auae kwa upanga atakufa kwa upanga....lakini yote katika yote, hapo ndio utamshangaa Mungu, ANASAMEHE, ANA REHEMA, REHEME ZA MUNGU NI KUU KULIKO DHAMBI ZETU...the mercy of the Lord is greater than our sins....na Mungu angehesabu maovu, nani angesimama? sisi sote tu watenda dhambi,....ukigeuka na kutubu kwa kweli, Mungu anakusamehe hata kama umetenda dhambi nyekundu kama damu....huu ni ujjumbe kwa polisi wote ambao walishiriki yale mauaji na hawajakamatwa labda wamejificha au wamefichwa akafikishwa tu yule mmoja mahakamani....kama hamtatubu na kuacha, damu ya huyo inalia mbele za Mungu....tubuni basi.
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    6. #5
      Ronal Reagan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 2,627
      Rep Power : 958
      Likes Received
      615
      Likes Given
      256

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Kuna mahakama mbili hapa, moja lazima itatenda haki...je waijua ni ipi? Ni Mahakama ya Wananchi.

      Hii nyingine ijue fika hukumu kuu/rufaa imeshatolewa na wananchi kuwa Polisi, kwa niaba ya serikali ambayo nayo kwa niaba ya CCM imekuwa ikitekeleza ukatili na mauaji kwa kisingizio cha (vurugu za) kisiasa. Kwa hivyo CCM hadi polisi wamehusika na kifo cha Mwangosi. PERIOD.

    7. Miaka 50

    8. #6
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Sasa wewe unaongelea haki au upendeleo?

      Kwani askari aliyeshikwa yeye hana haki zake?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    9. #7
      raymg's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 643
      Rep Power : 475
      Likes Received
      143
      Likes Given
      15

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      kwa jinsi mtuhumiwa anavyofikishwa mahakaman bila kuonekana sura....ninahisi sio mwenyewe huenda n pandikizi kutoka kwenyebaadhi ya mageraza nchi waliokua watumike kwenye issue ya Ulimboka.....

    10. #8
      raymg's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 643
      Rep Power : 475
      Likes Received
      143
      Likes Given
      15

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mlyafinono
      Hatakama watazuia haki kutendeka lakini Damu ya Mwangosi haiwezi kwenda bure katika midomo ya ardhi.They will pay for it
      how...

    11. #9
      Mag3's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 3,536
      Rep Power : 1804
      Likes Received
      2458
      Likes Given
      2497

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Ubungoubungo
      blah, blah, blah....kama hujaelewa chochote uliza nitakujibu.
      Ubungoubungo unakumbuka hili uliloliandika?
      Quote By Ubungoubungo
      hapo hamna cha fotoshop, inaonyesha wazi kabisa marehemu amemshikilia RPC hapo...na polisi anamuelekezea bunduki ya bom la machozi marehemu aliyelala chini, sasa mtuambie, huyu aliyezungusha mikono kwa RPC si marehemu? na aliyezungushiwa mikono si sura ya RPC kwa wale wanaomfahamu?..je kama ilishafika kipindi marehemu akazungusha mikono kwa rpc live hivyo, ni vipi kama utasema bom lililipuliwa baada ya rpc kuondoka yeye hakutoa maelekezo ya kumwacha marehemu asipigwe au aliona kuna habari ya utata itatokea ambayo marehemu anayo akaagiza afyatuliwe? tujue nini hapa sasa?
      Haki itatendeka vipi kama ushahidi wenyewe ndio kama huu uliotolewa hapo nyuma na Ubungoubungo? Halafu unadai kuwa kama yupo asieelewa, mwenye majibu ni wewe, duh! Why dont some people just shut up and disappear!
      Jasusi likes this.
      The true sign of intelligence is not knowledge but imagination.
      Education is what remains after one has forgotten what one has learned in School
      -Albert Einstein.


    12. #10
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,020
      Rep Power : 956
      Likes Received
      333
      Likes Given
      33

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mag3
      Ubungoubungo unakumbuka hili uliloliandika?

      Haki itatendeka vipi kama ushahidi wenyewe ndio kama huu uliotolewa hapo nyuma na Ubungoubungo? Halafu unadai kuwa kama yupo asieelewa, mwenye majibu ni wewe, duh! Why dont some people just shut up and disappear!
      yap, niliandika mimi mwenyewe, lakini unachotakiwa kujua ni kwamba, kuna principle of complimentarity ambayo itachukua si chini ya mwaka mmoja hata icc kuamua kutia timu. na pia kwa kosa kama hili, ninachofikiri ni kwamba, local courts ndio zitashughulikia kulingana na ingredient za makosa yale manne ukilinganisha na tukio hili. you are the one who should shut up and disappear forever. unachotakiwa kuelewa ni kwamba, suala hili icc haitalipokea, hata kama haki haitatendeka hapa ni kwamba, waendesha mashitaka wetu/ AG/DPP watatakiwa kukata tu rufaa na si vinginevyo, halikubaliki kwenye vigezo ya icc....you need to understand and shut up, and disappear forever too.
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    13. #11
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,020
      Rep Power : 956
      Likes Received
      333
      Likes Given
      33

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By raymg
      kwa jinsi mtuhumiwa anavyofikishwa mahakaman bila kuonekana sura....ninahisi sio mwenyewe huenda n pandikizi kutoka kwenyebaadhi ya mageraza nchi waliokua watumike kwenye issue ya Ulimboka.....
      walimficha kwako au walimficha na kwa waendesha mashitaka pale mahakamani....wewe ulitaka umwone halafu kiongezeke nini kwako au katika kusaidia kesi....kama ni pandikizi au la, nani kati yako wewe na hakimu aliyetakiwa kudetermine?
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    14. #12
      Mag3's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 3,536
      Rep Power : 1804
      Likes Received
      2458
      Likes Given
      2497

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By raymg
      kwa jinsi mtuhumiwa anavyofikishwa mahakaman bila kuonekana sura....ninahisi sio mwenyewe huenda n pandikizi kutoka kwenyebaadhi ya mageraza nchi waliokua watumike kwenye issue ya Ulimboka.....
      Hivi yule muuaji mwingine aliyeitwa Ukiwaona Ditopile Mzuzuri naye alikuwa akifunikwa sura asitambulike kila wakati alipokuwa akifikishwa mahakamani?
      Jasusi and Mystery like this.
      The true sign of intelligence is not knowledge but imagination.
      Education is what remains after one has forgotten what one has learned in School
      -Albert Einstein.


    15. #13
      Mag3's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 3,536
      Rep Power : 1804
      Likes Received
      2458
      Likes Given
      2497

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Ubungoubungo
      yap, niliandika mimi mwenyewe, lakini unachotakiwa kujua ni kwamba, kuna principle of complimentarity ambayo itachukua si chini ya mwaka mmoja hata icc kuamua kutia timu. na pia kwa kosa kama hili, ninachofikiri ni kwamba, local courts ndio zitashughulikia kulingana na ingredient za makosa yale manne ukilinganisha na tukio hili. you are the one who should shut up and disappear forever. unachotakiwa kuelewa ni kwamba, suala hili icc haitalipokea, hata kama haki haitatendeka hapa ni kwamba, waendesha mashitaka wetu/ AG/DPP watatakiwa kukata tu rufaa na si vinginevyo, halikubaliki kwenye vigezo ya icc....you need to understand and shut up, and disappear forever too.
      icc imeingiaje hapa...
      The true sign of intelligence is not knowledge but imagination.
      Education is what remains after one has forgotten what one has learned in School
      -Albert Einstein.


    16. #14
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,020
      Rep Power : 956
      Likes Received
      333
      Likes Given
      33

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mag3
      icc imeingiaje hapa...
      what do you mean....inaingiaje wapi...mbona haueleweki, funguka tukueleweshe.
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    17. #15
      Ubungoubungo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2008
      Posts : 2,020
      Rep Power : 956
      Likes Received
      333
      Likes Given
      33

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mag3
      Hivi yule muuaji mwingine aliyeitwa Ukiwaona Ditopile Mzuzuri naye alikuwa akifunikwa sura asitambulike kila wakati alipokuwa akifikishwa mahakamani?
      kufunikwa vile ni kosa kisheria? kuna madhara gani umepata au haki gani umenyimwa kisheria?
      Haya yote ni ubatili mtupu, hakuna jipya hapa duniani!

    18. #16
      Mag3's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 3,536
      Rep Power : 1804
      Likes Received
      2458
      Likes Given
      2497

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Ubungoubungo
      what do you mean....inaingiaje wapi...mbona haueleweki, funguka tukueleweshe.
      Unieleweshe! nani? wewe? thanx but no thanx...
      Quote By Ubungoubungo
      kufunikwa vile ni kosa kisheria? kuna madhara gani umepata au haki gani umenyimwa kisheria?
      Jibu swali na kama huwezi kaa kimya...niliuliza kama Ukiwaona Ditopile Mzuzuri naye alikuwa akifunikwa sura.
      The true sign of intelligence is not knowledge but imagination.
      Education is what remains after one has forgotten what one has learned in School
      -Albert Einstein.


    19. #17
      kimeloki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th July 2012
      Posts : 554
      Rep Power : 456
      Likes Received
      56
      Likes Given
      6

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      kamhanda na polis wake wana kesi ya kujibu lini na wapi time will tell

    20. #18
      ndyoko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 4,505
      Rep Power : 1706
      Likes Received
      1199
      Likes Given
      1916

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Mystery
      Tumeshuhudia tokea Mwangosi auawe kinyama na polisi, septemba 2, mwaka huu, na jinsi, jeshi hilo la polisi, lilivyojitahidi kwa juhudi zote, kujifanya kuwa wao hawakuhusika, badala yake wakadai, kuna kitu kizito kimerushwa toka kwa wafuasi na viongozi wa Chadema, lakini kwa jinsi Mungu alivyo mkuu, aliwapa ujasiri wapiga picha, wakapata picha zenye ushahidi wa wazi, kuwa polisi ndiyo wamehusika na mauaji hayo. Sasa wasiwasi wa wananchi wengi ni kuwa huyo polisi waliyemfikisha mahakamani, wamelazimika tu kumfikisha mahakamani, kutokana na shinikizo kubwa sana la vyombo vya habari na wananchi, pamoja na wanaharakati. Sasa kutokana na mlolongo wa matukio, kama vile kumfikisha mtuhumiwa mahakamani na gari la kifahari, la Land Cruiser, polisi kuzuia kabisa, mtuhumiwa huyo, asipigwe picha na paparazi. Vile vile, kitendo cha Kamuhanda kutoshtakiwa na kuendelea na kazi, wakati inafahamika wazi kuwa yeye, ndiye aliyesimamia hiyo operesheni ya mauaji ya Mwangosi. Kwa mazingira hayo nadhani ipo haja kwa wanaharakati na wanasheria wazalendo, kutoa taarifa ya kuwa hatuna imani na mahakama hiyo, kama mashahidi wa kesi hiyo, ndiyo hao hao mapolisi, wanaozuia hata mtuhumiwa asipigwe picha! Kwa hiyo nadhani ingekuwa vyema, wanasheria wazalendo wakaangalia vifungu vya sheria, vinavyoweza kuruhusu kesi hiyo, ihamishiwe mahakama ya kimataifa,ya the Hague, ambako tunaamini haki itaweza kutendeka
      Hivi wauaji wa Imran Kombe walishanyongwa au badoooo? Jibu la hili swali litatupa picha kamili ya mwenendo mzima wa hii kesi na matokeo yake!
      “If you can not get what you love, then love what you have”

    21. #19
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,619
      Rep Power : 2891
      Likes Received
      3837
      Likes Given
      12224

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By ndyoko
      Hivi wauaji wa Imran Kombe walishanyongwa au badoooo? Jibu la hili swali litatupa picha kamili ya mwenendo mzima wa hii kesi na matokeo yake!
      Wako huru, na wamepewa bonge la ardhi katika Tanzania yetu ya amani na mshikamano.
      Mag3 likes this.

    22. #20
      ndyoko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 4,505
      Rep Power : 1706
      Likes Received
      1199
      Likes Given
      1916

      Default Re: Kesi ya Mwangosi, vigumu sana haki kutendeka!

      Quote By Jasusi
      Wako huru, na wamepewa bonge la ardhi katika Tanzania yetu ya amani na mshikamano.
      Basi hakuna hata haja ya kuhangaika na kesi ya hawa wahuni wa Polisi. Tungojee muda ukifika tuyafukue maovu yote kuanzia ya deep green, epa hadi hii ya mwangosi. Kiutaratibu Polisi mwenye cheo anapotoa kauli inakuwa ni amri. Yule Polisi aliyekuwa kamkumbatia mwangosi akiwazuia wenzake wasimuadhibu alikuwa akiwaambia kuwa anamjua yule ni mwandishi lakini wale constable walipuuza kauli ya afande wao wakaendelea kumuadhibu Mwangosi. Ni wazi kuwa walikuwa wakitekeleza amri na maelekezo waliyopewa na mkubwa zaidi ya jamaa aliyekuwa akiwakataza wasimpige Mwangosi!
      Lyimo, Jasusi and Mag3 like this.
      “If you can not get what you love, then love what you have”

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...