Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

    Report Post
    Page 3 of 27 FirstFirst 1234513 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 529
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Wanabodi, Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!Trend za Upepo wa Kisiasa kuelekea 2015, zinavuma kwa Kasi ya Ajabu kuelekea Direction ya Mabadiliko (The Wind of Change, is Sweeping Across Tanzania) na kila dalili inaonyesha na kuelekeza Chadema is gaining momentum and there is nothing to stop it kuchukua nchi mwaka 2015 iwapo...
      1. Hakuna ubishi kuwa siku zote, CCM imekuwa ikishinda chaguzi mbalimbali "kihalali" na mtaji wao mkubwa wa ushindi ni "watu".
      2. Hakuna ubishi kuwa CCM kama chama, kimechoka, dalili zote za chama kichovu kinachosubiri kifo, tayari, zimeisha jitokeza kwa CCM, kinachosubiriwa sasa its only a matter of time ni lini kitaangwa rasmi, hiyo 2015 naiona kama vile ni mbali, unless wamsimamishe their one and only jewel!.
      3. Hakuna ubishi kuwa wengi wa hao "watu", wamekuwa wakiichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda sana!, (waipende kwa lipi?), la hasha!, "watu" wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu!.
      4. Hakuna ubishi, kuwa wengi wa hao "watu" waliokuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu, sasa wameichoka, hivyo uchaguzi wa 2015, hawatachagua tena chama kwa mazoea, bali watachagua chama kwa "sababu"!.
      5. Hakuna ubishi kuwa Chadema, ndicho chama kinachokubalika zaidi kwa sasa kuliko CCM, hivyo ule mtaji mkubwa wa CCM iliyoutegemea kwa miaka nenda miaka rudi, sasa umehamia Chadema!.
      6. Kama ambavyo CCM imekuwa ikichaguliwa kwa mazoea tuu, na sasa CCM imechokwa, vivyo hivyo kwa sasa Chadema haina lolote la kukifanya kipendwe, bali kinapendwa kwa sababu "watu" wameichoka CCM!.
      7. Kama uchaguzi utaitishwa leo, Chadema itashinda kwa kishindo kikubwa cha ajabu, lakini ukiwauliza hao watakaokipa Chadema ushindi, ni sababu zipi za kuichagua Chadema, hawatakupa sababu yoyote zaidi ya kuichagua Chadema kwa sababu wameichoka CCM!.
      8. ili Chadema iweze kupata ushindi wa Tsunami kwa uchaguzi wa 2015, lazima Chadema ikubali kubadilika, isiendelee kuutegemea huu umaarufu wa muda kwa kushangiliwa na umati wa watu walioichoka CCM, bali Chadema sasa lazima iwape Watanzania sababu za kuichagua Chadema!.
      9. So far so good, Chadema is doing a good job chini ya Uongozi Shupavu wa Kamanda Mbowe na kinara wa M4C, Dr. Wibroad Slaa, Chadema is doing the right thing!. Doing the right thing alone, doesn't guarantee sweet clear victory for Chadema, it got to do things right!. Hii inamaanisha ili Chadema ishinde kwa kishindo kinachotakiwa, lazima ikubali kubadilika and start doing things right besides doing the right thing!.
      10. Hivyo ndugu zangu viongozi wa Chadema najua 2015 mmedhamiria kwa dhati kuchukua nchi kwa ushindi wa kishindo!, lakini ili lengo hili litimie, ni lazima kwanza mkubali kusikiliza, pili mkubali kuzifanyia kazi hizi hoja na tatu mkubali kubadilika!.

      Naomba kumalizia kwa nukuu kutoka kwa mmoja wa wanachama wetu humu jf.
      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Nitasema jambo moja zito- labda mbeleni nitaliangalia zaidi - ni wagumu sana kushaurika. Wametengeneza cocoon ya kujilinda kiasi kwamba ni vigumu sana kuweza kutoka ndani. Na kama kuna kitu kitakachosababisha waendelee kuwa wapinzani wa kudumu siyo kukosa ushauri au mawazo mapya bali kutokukubali kubadilika.
      Kwa wale wapenzi wa Chadema, for sure, Uchaguzi wa 2015, Chadema inaweza kabisa Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If "Itabadilika" and provided that CCM haitamsimamisha yule mgombea wangu!. Japo ni vema kuwa na great expectations on Chadema kuchukua nchi 2015, only if Chadema itabadilika, vinginevyo keep hopping for the best na kama Chadema haitabadilika, you better get prepared for the worst kwa sababu 2015 itakuwa ni CCM Tena!.NB. Msiniulize Chadema wabadilike nini, wahusika wameshaambiwa imebaki kusikiliza na kutekeleza!.Naomba kuwasilisha.Pasco.
      UP DATE 1.Kufuatia maswali mengi kuhusu Chadema wabadilike nini, naomba kumnukuu mmoja wa great thinkers wetu humu jukwaani
      Quote By Mchambuzi
      ‘The Country is Suffering From CCM Fatigue’. Kuna tofauti kubwa baina ya “Doing the Right Things” na “Doing things Right”, na ili ufanikiwe, nilazima kufanya yote mawili. Chadema has been doing the right things ambayo ni kutumia kikamilifu mapungufu ya CCM kujijenga kisiasa. Lakini tatizo linakuja kwenye “doing things right” Mbinu za upinzani zinazotumiwa na Chadema Hazipo Consistent na CoherentKwanza Chadema wanastahili pongezi kwa kuonyesha ukomavu wa kisiasa kwa kuwa politically active majira yote. Lakini pamoja na mafanikio haya, bado Chadema kinaonyesha udhaifu mkubwa kwenye mbinu inazotumia kuendesha siasa za upinzani. Mbinu za Chadema kwa kiasi kikubwa hazina consistency (uthabiti) na coherence kwani zinabadilika mara kwa mara. Hili ni tatizo, hasa pale chama kinapokuwa hakina mvuto unaotokana na itikadi bali masuala ya mpito Upinzani dhidi ya Itikadi ya CCM, lakini bila ya kutoa dira na itikadi mbadala iliyo practical – Chadema wamekuwa wanapinga sera nyingi za CCM bila ya kutoa itikadi na dira mbadala Ni muhimu nisisitize kwamba tatizo sio mbinu hizi za upinzani bali the inconsistency na incoherence katika hilo.

      Leo hii masuala ya uongozi na siasa yametawaliwa sana na misingi ya Ukanda, Ukabila na Udini. Inawezekana baadhi ya watu wasikubaliane na mimi katika hili, Ni vigumu kwa sasa kubaini masuala la udini, ukabila na ukanda yata ‘play out’ vipi katika siasa za CCM na Chadema 2015. Vinginevyo ni muhimu Chadema ikafanya marekebisho ya maana kwenye itikadi yake, kwani nje ya uchovu wa wananchi na CCM, nje ya agenda ya serikali ya CCM kutokuwa na maamuzi magumu kutatua matatizo ya nchi, na pia nje ya agenda ya ufisadi, Chadema haina ammunition ya kutosha kisera kuitoa CCM magogoni. Hili linahitaji kubadilika na ndio kete kuu ya Chadema 2015 itakayowaletea mafanikio yenye mashiko zaidi mbali ya vita dhidi ya ufisadi ambayo sio mwarobaini (panacea) ya matatizo ya wananchi walio vijijini.

      Ni mambo haya ambayo nadhani yakifanyiwa kazi na Chadema, basi yatazidi kujenga mazingira ya utayari kwa Chadema kushika madaraka ya nchi 2015 – kwani mbali ya “doing the right things”, pia watakuwa wametekeleza dhana ya “doing things right”
      NB. Kwa maswali yoyote kuhusu haya mambo ambayo Chadema inahitaji kubadilika, naomba uyaelekeze moja kwa moja kwenye thread husika hapa.CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015
      UPDATE 2: Input ya Mchambuzi.
      Quote By Mchambuzi

      Ningependa kuchangia kidogo kuhusu suala hili la rushwa, hasa kwa kujaribu kujengea hoja kwanini rushwa ni hoja ya ukombozi. Naungana na wewe kupinga hoja kwamba Ufisadi sio hoja ya kuwakomboa watanzania. As a matter of fact, vita dhidi ya Ufisadi/Rushwa na ile dhidi ya umasikini lazima viende kwa pamoja, vinginevyo kuendeleza vita dhidi ya umaskini huku vita dhidi ya ufisadi vikilega lega, juhudi za kutokomeza umaskini hazitazaa matunda na tutaishia tu kupoteza resources nyingi sana pamoja na muda mwingi bure kwenye vita dhidi ya umaskini ambavyo havitamalizika.

      Mabadiliko yoyote ya kisiasa, kijamii na kiuchumi yenye kulenga kuletea faida wananchi walio wengi hayawezi kufanikiwa bila ya kutokomeza rushwa; Rushwa/Ufisadi ni ‘an infection’ kwenye juhudi za Maendeleo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ndio maana hata kwenye kwenye international development community, Suala la Rushwa/Ufisadi limeanza kuchukuliwa kama ‘a development issue’ & ‘a development imperative’;

      Kwanini Rushwa ni hoja ya kuwakomboa watanzania?

      Rushwa covers a wide spectrum, kuanzia rushwa ndogo ndogo/petty corruption to large scale/grand corruption. Tukianza na Petty corruption, ili mtanzania aweze pata huduma za msingi kabisa zinazosimamiwa na Bureucrats/Administrators kama vile Uhamiaji, Polisi, Ardhi, Elimu n.k, bila ya kutoa ‘kitu kidogo’, normal bureaucratic procedures can’t be accomplished; Mwalimu Nyerere alipokuja na kauli mbiu ya TANU dhidi ya Rushwa kwamba RUSHWA NI ADUI WA HAKI, SITATOA WALA KUPOKEA RUSHWA, aliliona hili kwani MASKINI HAWEZI KUPATA HAKI katika jamii inayoendeshwa kwa rushwa, na maskini tanzania ni zaidi ya 80% na hawa wanasubiria ukombozi kwa miaka 50 sasa;
      Mpaka hapa, hoja kwamba rushwa sio hoja ya kuwakomboa watanzania inajishikilia wapi?

      Tukiangalia aina nyingine ya rushwa - Large scale/Grand Corruption, hii inatokea pale ambapo a considerable amount of money inatolewa kama hongo ili kuwapatia watu fulani fulani preferential treatment au access kwa Rasilimali za watanzania ambazo walipewa na Mungu. Nyerere alitueleza kwamba ili kufanikiwa katika Maendeleo, moja ya vitu muhimu tunavyohitaji ni ARDHI, vingine vikiwa ni watu, siasa/sera safi, uongozi bora n.k. Tumeshuhudia jinsi gani wageni wanajinyakulia ardhi kwa kutoa rushwa huko kwa watawala; tunazidi kuona jinsi gani wawekezaji wanawawekea watawala mamilioni ya dola kwenye mabenki huko Uswisi na kupewa miradi ya madini, mafuta, gesi….miradi ambayo ina kila sura ya kijambazi na unyang’anyi kwani HAKI YA MUNGU aliyopewa mtanzania (rasilimali) inakuwa HAKI YA MZUNGU.
      Pia kwa mfano mwingine huu mdogo tu, hoja kwamba Rushwa sio hoja ya kuwakomboa watanzania inajishikilia wapi.

      Mtu anayetoa hoja kwamba rushwa sio hoja ya kumkomboa watanzania ni dhahiri anawatusi mamilioni ya watanzania waliotaka mabadiliko mwaka 1995 wakati wa Augustine Mrema na NCCR Mageuzi kwani nchi ilikuwa inanuka rushwa, jambo ambalo hata Nyerere alilisema sana; Kama tunaamini katika demokrasia, hasa katika dhana ya nguvu ya umma, umma ule kumuunga mkono Mrema kutokana na msimamo wake dhidi ya Rushwa ni maana kwamba Rushwa ni Hoja ya kumkomboa Mtanzania; Vile vile, katika nyakazi hizi, Chadema imejinyakulia umaarufu na kuungwa mkono na watanzania wengi sana (kwa mamilioni) kwani watanzania wengi wanaona hoja ya rushwa ina mashiko;vile vile the fact kwamba CCM inazidi kupoteza mapenzi mioyoni mwa watanzania wengi ni ushahidi tosha kwamba rushwa ni hoja ya kuwakomboa watanzania;

      Nchini Tanzania rushwa imeshaota mizizi, na its ‘negative effects’ imesha – multiply kwenye jamii. Katika Tanzania, Rushwa/Ufisadi umepelekea mamilioni ya watanzania kupoteza matumaini na hali zao za maisha, umezaa cynicism, hali ya kutoaminiana kwani watanzania wengi sasa wanaamini kwamba rushwa/ufisadi is a ‘norm’. Ufisadi/rushwa unazidi ku-undermine our social values kwa sababu watu wengi wanaona ni rahisi na inalipa kujiingiza katika shughuli za ufisadi/rushwa kuliko kutafuta shughuli au ajira halali;

      Rushwa/ufisadi umeshapelekea mmomonyoko wa uhalali wa serikali ya CCM in the eyes ya watanzania wengi kwani mbali na madhara ya Ufisadi ambayo yanawanyang’anya watanzania ile HAKI YA MUNGU na kugeuzwa kuwa HAKI YA MZUNGU, vile vile petty corruption inapunguza kwa kiasi kikubwa sana ‘effective delivery’ ya huduma za kijamii, na ni ahadi juu ya upatikanaji wa huduma za namna hii ndio ilipelekea watanganyika wengi kuiunga mkono TANU miaka ya 1950s na hatimaye kuisaidia TANU kutekeleza malengo yake ya ukombozi wa nchi;

      Given all this, mtu anaweza vipi kuja na hoja kwamba Rushwa sio hoja ya kuwakomboa watanzania? Wakati tunazidi kushuhudia madhara ya rushwa/ufisadi katika upatikanaji wa huduma za kijamii kwa watazania walio wengi? Na pia jinsi gani ufisadi/rushwa unapelekea watanzania kuporwa HAKI YAO KUTOKA KWA MUNGU (Rasilimali) na inageuzwa kuwa HAKI YA MZUNGU?
      Quote By Mchambuzi
      Cha kuzidi kushanganza zaidi ni pale CCM (tofauti na TANU) kinapogeuka kuwa ni chama cha kujiuma uma kuhusu suala la rushwa/ufisadi. Pengine tunapoteza muda kujadili hoja hii kwamba rushwa sio hoja ya kuwakomboa watanzania bila ya kujua kwamba kumbe ina mahusiano na kujiuma uma kwa CCM; I don’t know, Lakini yetu macho na masikio.
      UPDATE 3: CLOSING REMARKS YA MKUU NGURUVI3

      Quote By Nguruvi3
      Mkuu, kama nilivyoahidi nipo. Ingawa mjadala unaonekana kufungwa hakika sitasita kutupa neno moja au mawili hasa kujibu hoja yako ya kuwa inaonekana nakubaliana na Pasco.

      Ni kweli nakubaliana naye kwa asilimia kubwa sana hata kama si mia moja. Na sababu za kufanya hivyo ni:
      1. Kama alivyosema CCM imechokwa, si tu imechokwa bali imechokwa na matendo yake. Chama kilichopo madarakani miaka 50 hakionekani kuwa tumaini kwa Wananchi, badala yake kimegeuka kuwa genge la waporaji na waporaji hao kulindwa kwa kura za wananchi licha ya kuwa uporaji ni wa kodi zao.

      2.Wananchi wametafuta mbadala kwa miaka mingi na hakika 'ndele' ya kupendwa imeangukia Chadema.
      Ndele hiyo inatokana na jitihada hasa zilizofanyika bungeni kuuonyesha umma wapi tatizo lilipo.
      Yule mama aliyehojiwa Iringa yeye alisema 'Anaipenda chadema kwasasababu kama si wao, yeye asingejua uhuni na udhalimu unaoendelea nchi hii'.Hadi hapo Chadema wame win nyoyo za watu kwa kutambua kuwa wapo wanaosimama nao.

      3.Mikutano inayoendelea ya M4C ni jambo sahihi, lakini haitoshi tu kuwa sahihi ni lazima ifanyike kwa usahihi.
      Mfano, je kila baada ya mkutano kuna ufuatiliaji wa kuimarisha chama eneo husika? Au ni kugawa kadi tu na kukusanya watu na kama ni hivyo je huo ni usahihi hata kama jambo lenyewe ni sahihi?

      4.Juzi tumeona picha za CDM mji mwema. Tena viongozi wakionekana kuwa makini. Aliyeleta picha ni mkereketwa wa Chadema na haikuwa na maelezo nini kimesemwa. Mkutano ni jambo sahihi, je, wamelifanya kwa usahihi? Jibu ni hapana kwasababu hawajawasiliana na umma kama ilivyokuwa mwazoni.
      Wamekuwa 'out of touch' kwa public kama walivyo kwa JF.
      Tayari wameshau ngazi iliyowapindisha na hiyo tu ni tatizo.

      5.Pasco amesema lazima wawe tayari kukubali ushauri, na ushauri tuliwahi kutoa kwa kitengo cha mawasiliano ya umma 'public relationship' na ni wazi hawajaufanyia kazi. Hapo nakubaliana na Pasco kuhusu hoja hiyo.

      6.Uwajibikaji; Tumeona panga la Arusha na Mwanza kwa madiwani.Uamuzi huo ni sahihi, lakini je wameufanya kwa usahihi? Jibu ni ndiyo na hapana. Ni ndio kwasababu wale wanaoleta vurugu wanapaswa kushughulikiwa.
      Ni hapana kwasababu sheria au taratibu zinapindwa kila mara. Kama CDM ilikuwa tayari kupoteza madiwani wa Arusha na wa Mwanza hadi kufikia kupoteza hatamu za umeya katika grassroot level, imeshindikanaje kwa CDM kukubali kupoteza ubunge kwa utaratibu ule ule wanaoutumia? Mbunge mmoja na madiwani 9 ni nani muhimu katika kuimarisha chama.

      7.Taratibu zinazowaangukia madiwani kwanini zisitumike kutuliza mtafaruku uliopo BAVICHA?
      Ikifika hapo tofauti kati ya CDM na CCM inayowafukuzu makatibu wa matawi na kuwaacha wahalifu NEC na CC haipo.
      Inaonekana kama Chadema wanafanya kazi kwa template ya CCM.
      Kwa staili hiyo wananchi wataonaje tofauti ya vyama hivi katika kusimamia taratibu zao kabla ya kupewa madaraka!

      Hapo ndipo niliposema Chadema lazima iwe na clear demarcation iliwatu waone mbadala walio na matumaini nao.
      Ni lazima kuwe na demarcation katika kutoa misimamo ya mambo ya kitaifa. Chadema kama chama pinzani na tegemo kwa wakati mfupi ujao inapaswa kuwa mstari wa mbele katika kujibu, kupendekeza na kunyumbulisha hoja zinazohusu utaifa.
      Mfano, nini msimamo wa Chadema kuhusu muungano?

      8.Chadema wanapaswa kusimama kama taasisi na si kundi la watu fulani maarufu. Taasisi ina namna ya kupanga na kushughulikia mambo yanayohusiana nayo. Suala la Iringa ni mfano mzuri tu. Imewachukua wiki moja kukabiliana na uharibifu wa taswira ya chama uliohusishwa na tukio. In fact kauli ya Mbowe ilikuwa 'damage control' badala ya statement. Tatizo lisiloonekana kwa wengi ni hili la kutokuwa taasisi kikamilifu na ni ngumu kuliona kirahisi.

      9.Kama Chadema hawatajipambanua kama Chama kinachosimamia na kueleza sera zake basi ipo siku wananchi watasema tofauti iko wapi? Hawa wanatenda wale wanakosoa nini kilitakiwa kifanyike!
      Kwa maneno mengine ukosoaji pekee hautoshi ni lazima kuwepo na makusudi ya kueleza sera zao.

      Chadema isimamie sera zake na kuzieneza na si kubaki katika makabrasha au kukaa kimya zikiporwa.
      Hoja kama ya katiba, utawala wa majimbo wameziacha zimeporwa na sasa kuonekana kama za CCM.
      Kwanini hili linatokea? Hoja ya katiba ilikuwa sahihi, je ilifanywa kwa usahihi?

      Kwa ufupi, Chadema sasa kimekuwa na ni wakati kiongoze. Hoja za kukubaliana na CCM kama ya katiba haionyeshi mbadala. Kwangu mimi CDM walikuwa na hoja na waliwaacha wananchi porini. Nitty gritty!
      Pamoja na ukosaoaji sasa ni wakati waeleze wao wana matarajio gani kwa njia gani, rasilimali gani na kipaumbele gani.

      Vinginevyo wananchi watasema 'better the devil you know than the angel you don't know'.
      The simple way CDM could counter act this arguement is to set a clear goal, and make a clear distinction between the past and the future.

      CLOSING REMARKS.
      Wababodi, baada ya 25 pages each with twenty posts, with a total 500 Posts Plus, imethibitika pasi shaka kuwa uchaguzi wa 2015, Ikulu ni ya Chadema, hivyo sasa kuelekea 2015, kila dalili zinaelekeza Chadema kuchukua nchi, ila kwa maoni ya wengi serious waliochangia thread hii (ukiondoa wale wa ushabiki), wengi wamekubali Chadema iko on the right track, ila ili kutimiza lengo hilo la kubisha hodi ikulu, na kukubaliwa kuwa mpangaji rasmi wa jengo lile, lazima Chadema ikubali kubadilika, apart from doing the right thing kama inavyofanya sasa, it got to do things right!.

      Baada ya maneno haya, sasa kwa heshima na taadhima naomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa hawa wafuatao.
      1. Mkuu Mkandara, topic yako ya ndio was the inspiration ilionifanya kuanzisha hii thread na niliepuka kukutaja wala kukuquote popote kwa sababu maalum. Asante kwa kujitanabaisha kama mwana Chadema ambaye uko tayari kusimama na ukweli, "no matter what"
      2. Mzee Mwanakijiji , ile quote yako niliyoitumia humu, imekuwa kama ndio "colabo" ya hit single kwa mwanamuziki mchanga, kumshirikisha "star mkubwa" ili atoke!, ndivyo ilivyokuwa hii thread, imefikisha record hits kwa mada yangu yoyote kufikisha posts 500 in two days, hii ndio mara yangu ya kwanza, na naamini kuna wachangiaji walichangia thread hii kwa ajili ya quotation yako. Ingawa wewe binafsi hukuchangia kwa sababu ambazo ninazifahamu fika, thanks for being you, who you are!.
      3. Mkuu Mchambuzi, ule uzi wako wa ndio the subject matter ya hii mada, kwa jinsi ninavyokusoma humu, naamini wewe ni genius kwenye politics zetu, kama Chadema wanakusoma na kuzifanyia kazi hoja zako, 2015, hatuzungumzii ushindi wa Chadema, bali how big the margin is, kati ya mshindi na mshindwa!.
      4. Mkuu Nguruvu3, wewe ni other political genius wetu humu, nilikufahamu kupitia theory yako ya "demage control" na kuendelea kukufuatilia kule kwenye Jukwaa lako, hii closing remarks yako, ni faraja kubwa kwangu, kuendelea kuibua topic ambazo sio popular kwa wana jf wengi, ila huu ndio ukweli halisi ambapo siku zote, kweli itasimama.
      5. Na mwisho, napenda kuwashukuru, wachangiaji wote mlioungana nami katika mada hii, ni vigumu kumtaja kila mtu, lakini shukrani za pekee ziende kwa wachangiaji changamoto akiwemo Mag3, J Mushi, Nicholas, na wengine wengi ambao japo hatukubaliani, lakini tumeishia kukubali kutokubaliana na hii ni healthy kwenye mjadala wowote. Mimi pia ni binadamu kama binadamu wengine, huwa nakwazika na kuwakwaza wengine, na especial kwenye mada yoyote inayomhusu "yule mgombea wangu"! tusameheane na tuzidi kusonga mbele kwa maslahi ya taifa.


      Nakufikia hapa, naomba sasa ku declare rasmi, mjadala huu, umefungwa rasmi!
      this Topic is officially Closed by the thread starter!!
      Last edited by Pasco; 20th January 2013 at 14:00.

    2. FemaTV & Radio

    3. #41
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,865
      Rep Power : 1976
      Likes Received
      2332
      Likes Given
      3018

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Wachagga wapo wengi sana zomba ngoja ni kumwagie list.

      [1] Anthony G Mbassa huyu ni mchagga wa Biharamulo magharibi

      [2] Prof Kulikoyela Kahigi huyu ni mchagga wa Bukombe Shinyanga

      [3] Simon Peter Msigwa huyu ni mchagga wa Iringa Mjini

      [4] Yohana Natse huyu ni mchagga wa Karatu

      [5] Halima Mdee huyu ni mchagga wa Kawe Dar

      [6] Zitto Z kabwe huyu ni mchagga wa Kigoma kaskazini

      [7] John Shibuda huyu ni mchagga wa Maswa mashariki

      [8] Joseph Mbilinyi huyu ni mchagga wa Mbeya mjini

      [9] David Silinde huyu ni mchagga wa Mbozi magharibi Mbeya

      [10] Mustafa Akonnay huyu ni mchagga wa Mbulu

      [11] Meshack Opulukwa huyu ni mchagga wa Meatu Shinyanga

      [12] Said Arf Amour huyu ni mchagga wa Mpanda Rukwa

      [13] Vicent Kiboko Nyerere huyu ni mchagga wa Musoma mjini

      [14] Ezekia Wenje huyu ni mchagga wa Nyamagana Mwanza

      [15] Tundu Lissu huyu ni mchagga wa Singida Mashariki

      [16] John Mnyika huyu ni mchagga wa Ubungo Dar

      [17] Salvatory Machemuli huyu ni mchagga wa Ukerewe........

      Mkuu zomba kama wachagga wameenea kila pembe ya Tanganyika ni kwanini wasishike dola haa ha ha ha wanchekesha!!!!!!.




      Quote By zomba
      Hivi chadema itashinda kwa kura za kina nani? wachagga? wako wangapi nchi hii?
      Last edited by Ngongo; 13th September 2012 at 15:40.
      Albedo, Pasco, MpendaTz and 9 others like this.

    4. #42
      amba.nkya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2010
      Location : Downtown
      Posts : 292
      Rep Power : 534
      Likes Received
      43
      Likes Given
      47

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By zomba
      Hivi chadema itashinda kwa kura za kina nani? wachagga? wako wangapi nchi hii?
      kuna wanyakyusa, wahehe, waha, wanyamwezi, wasukuma, wakurya, na wengine kibao, sema jingine...Zombi
      Pasco likes this.
      The Figther never gives up!

    5. #43
      JUST's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2010
      Posts : 377
      Rep Power : 503
      Likes Received
      149
      Likes Given
      31

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      mimi huwa nafurahi sana nikiona ushauri wa watu kwa chadema hivi unasema kibadilike Je uliwapa ushauri wakati hawajakubalika ili wakubalike? kama sio waunge mkono kwa kuhamasisha jirani na ndugu zako ili tusaidie kuondoa mfumo mbovu uliopo, tuacheni kuwapanikisha viongozi wa chadema kilchopangwa na mungu kamwe binadamu hawezi kukitengua atachelewesha tu na kwa maono yangu ilicheleweshwa toka 1995 na sasa 2015 ndi mwisho.

      hakuna mabadiliko hakuna maendeleo na watanzania naombwa wahamasishwe kuichoka CCM sababu nyingine baadae. ukimchoka mume au mke si unachukua hatua na sababu zitatolewa mbele ya vikao vya wanafamilia?
      Pasco and MpendaTz like this.

    6. #44
      Dangire's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : Dar
      Posts : 179
      Rep Power : 420
      Likes Received
      35
      Likes Given
      3

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By zomba
      Hivi chadema itashinda kwa kura za kina nani? wachagga? wako wangapi nchi hii?
      akili za magamba.....hivi bado unaamini kuwa cdm ni chama cha wachaga! ajabu.kama ni hivyo, ukichanganya wachaga wote walio ndani ya ccm na vyama vingine vyote, kisha ongeza wakristo wote, kisha watz wote, cdm itakuwa bado haijaingia madarakani? ........kumbuka..cdm ni chama kisicho na dini wala kabila.
      Pasco likes this.

    7. #45
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,165
      Rep Power : 1531
      Likes Received
      758
      Likes Given
      591

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By Pasco
      Wanabodi,
      Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!

      Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!

      Trend za Upepo wa Kisiasa kuelekea 2015, zinavuma kwa Kasi ya Ajabu kuelekea Direction ya Mabadiliko (The Wind of Change, is Sweeping Across Tanzania) na kila dalili inaonyesha na kuelekeza Chadema is gaining momentum and there is "nothing" to stop it kuchukua nchi mwaka 2015 iwapo...
      1. Preamble yako ni fedheha kwa kila mtu si CDM itayochukua nchi bali ni kwa wapiga kura watakaokabidhi nchi kwa chama cha mabadiliko

      2. Neno "______ kwa kishindo" ni kauli mufilisi inatokana na nguvu ya ziada inayotumika kwenye kuhalalisha matokeo ya kura knyume cha wapiga kura na wala si hiari ya wapiga kura.

      Kwenye mazingira, upepo unazuiliwa na upandaji miti. Kipindi tulicho nacho chama tawala kinaweza kupanda miti kuzuia upepo. Kinachotakiwa ni dhamira ambayo HAWANA kwa hiyo upo sahihi.

      Ila "!... Only If...!"!; iwapo..." haya maneno haya "uswi". Kumbuka unapopanda mahindi mbegu inaoza halafu inachipua hakuna suala la "iwapo". Na mabadiriko haya yapo uje upepo, mvua, jua; SUALA kama ulivyoliweka ni kuchokwa chama tawala na dhamira zake mufilisi. Sitegemei chama kitakachochukua nchi kifanye miujiza. Nategemea kitakuwa na changamoo nyingi ila kitakuwa na mikakati shirikidhi, ya ukweli na yenye dhamira safi.
      Pasco likes this.
      Ukweli utakuweka huru daima

    8. Miaka 50

    9. #46
      Deus F Mallya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th July 2011
      Posts : 467
      Rep Power : 488
      Likes Received
      321
      Likes Given
      65

      Default

      Quote By Pasco
      Wanabodi,
      Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!

      Trend za Upepo wa Kisiasa kuelekea 2015, zinavuma kwa Kasi ya Ajabu kuelekea Direction ya Mabadiliko (The Wind of Change, is Sweeping Across Tanzania) na kila dalili inaonyesha na kuelekeza Chadema is gaining momentum and there is to stop it kuchukua nchi mwaka 2015 iwapo...

      1. Hakuna ubishi kuwa siku zote, CCM imekuwa ikishinda chaguzi mbalimbali "kihalali" na mtaji wao mkubwa wa ushindi ni "watu".
      2. Hakuna ubishi kuwa CCM kama chama, kimechoka, dalili zote za chama kichovu kinachosubiri kifo, tayari, zimeisha jitokeza kwa CCM, kinachosubiriwa sasa its only a matter of time ni lini kitaangwa rasmi, hiyo 2015 naiona kama ni mbali sana!.
      3. Hakuna ubishi kuwa wengi wa hao "watu", wamekuwa wakuichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda sana!, (waipende kwa lipi?), la hasha!, "watu" wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu!.
      4. Hakuna ubishi, kuwa wengi wa hao "watu" waliokuwa kuwa wakiichagua CCM kwa mazoea, sasa wameichoka, hivyo 2015, hawatachagua tena chama kwa mazoea, bali watachagua chama kwa "sababu"!.
      5. Hakuna ubishi kuwa Chadema, ndicho chama kinachokubalika zaidi kwa sasa kuliko CCM, hivyo ule mtaji mkubwa wa CCM iliyoutegemea kwa miaka nenda miaka rudi, sasa umehamia Chadema!.
      6. Kama ambavyo CCM imekuwa ikichaguliwa kwa mazoea tuu, na sasa CCM imechokwa, vivyo hivyo kwa sasa Chadema haina lolote la kukifanya kipendwe, bali kinapendwa kwa sababu "watu" wameichoka CCM!.
      7. Kama utaguzi utaitishwa leo, Chadema itashinda kwa kishindo kikubwa cha ajabu, lakini ukiwauliza hao watakaokipa Chadema ushindi, ni sababu zipi za kuichagua Chadema, hawatakupa sababu yoyote zaidi ya kuichagua Chadema kwa sababu wameichoka CCM!.
      8. ili Chadema iweze kupata ushindi wa Tsunami kwa uchaguzi wa 2015, lazima Chadema ikubali kubadilika, isiendelee kuutegemea huu umaarufu wa muda kwa kushangiliwa na umati wa watu walioichoka CCM, bali Chadema sasa lazima iwape Watanzania sababu za kuichagua Chadema.
      9. So far so good, Chadema is doing a good job kwa sababu M4C is doing the right thing!. Doing the right thing alone, doesn't guarantee sweet clear victory for Chadema, it got to do things right!. Hii inamaanisha ili Chadema ishinde kwa kishindo kinachotakiwa, lazima ikubali kubadilika and start doing things right besides doing the right thing!.
      10. Hivyo ndugu zangu viongozi wa Chadema najua 2015 mmedhamiria kwa dhati kuchukua nchi kwa ushindi wa kishindo!, lakini ili lengo hili litimie, ni lazima kwanza mkubali kusikiliza, pili mkubali kubadilika kwa kuzikiliza hoja zinazotolewa kuhusu Chadema na kuzifanyia kazi!.


      Naomba kumalizia kwa nukuu kutoka kwa mmoja wa wanachama wetu humu jf.



      Kwa wale wapenzi wa Chadema, ni vema kuwa great expectations on Chadema kuchukua nchi 2015, only if Chadema itabadilika, vinginevyo keep hopping for the best and get prepared for the worst kama Chadema haitabadilika na 2015 itakuwa ni CCM Tena!.

      NB. Msiniulize Chadema wabadilike nini, wahusika wameshaambiwa imebaki kusikiliza na kutekeleza!.

      Naomba kuwasilisha.

      Pasco.



      Namba 9 nakukumbusha Mkuu uendelee kuichangia M4C ili iweze kutekeleza malengo yaliyopangwa.. Vinginevyo; Message Sent!.
      Pasco likes this.

    10. #47
      JUST's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2010
      Posts : 377
      Rep Power : 503
      Likes Received
      149
      Likes Given
      31

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By magino
      haya mawazo ni mazuri sana, hata mm ni mpenzi wa CDM tusipojirekebisha katu Ikulu hatuioni!!! tusiwe wepesi wa kuwaambia wezetu wameongea pumba ili hali mawazo ni mazuri na ya kutujenga.... ni hayo tu kwa leo!!!
      hembu wekeni mambo ya wao kujirekebisha mbona hamueleweki. huwa napenda kusema watanzania wa leo sio wa jana na hawadanganyiki wala hawachaganywi tena. na kama unaipenda CDM si uende makao makuu ukatoe hayo mapungufu ili warekebishe na uingie kwenye kumbukumbu za mchango waku katika kukisaidia.
      Pasco likes this.

    11. Ame
      #48
      Ame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Location : Global Citizen
      Posts : 1,513
      Rep Power : 1184
      Likes Received
      650
      Likes Given
      2615

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By Pasco
      Wanabodi,
      Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!

      Kwa wale wapenzi wa Chadema, ni vema kuwa great expectations on Chadema kuchukua nchi 2015, only if Chadema itabadilika, vinginevyo keep hopping for the best and get prepared for the worst kama Chadema haitabadilika na 2015 itakuwa ni CCM Tena!.

      NB.
      Msiniulize Chadema wabadilike nini, wahusika wameshaambiwa imebaki kusikiliza na kutekeleza!.

      Naomba kuwasilisha.

      Pasco.



      Ume amua kumtosa mzee wa watu siyo? M4C si mchezo haya we karibu.....Lakini CDM is peoples power haiendeshwi kwa matakwa ya individuals bali ya public!
      Pasco likes this.

    12. #49
      mzeelapa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2010
      Posts : 542
      Rep Power : 557
      Likes Received
      71
      Likes Given
      70

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Napata tatizo moja, TANU na baadae CCM wametawala tangu 1961 kufikia mwaka 1995 alipong'atuka Nyerere. Wakati huo hawakuwepo mafisadi, wala rushwa,sijui wauwaji, mikataba mibovu and so and so....na nchi haikuendelea na tumeendelea kuwa masikini. CDM wanachoongelea ni matatizo hayo hapo juu kama kwamba yakiondolewa na umaskini utakwisha. Kwa vile siamini hilo, naomba nifahamishwe CDM itafanya nini cha ajabu hapo 2015 kama wataingia madarakani? Naona sasa haziongelewi sera bali kuondoa mambo yanayotokana na matukio yanayojitokeza...! Nipeni ushawishi niichague CDM hapo 2015. (ila sasa hivi siandamani ng'o niko kwenye kujitafutia riziki)!!
      Pasco likes this.

    13. #50
      JUST's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2010
      Posts : 377
      Rep Power : 503
      Likes Received
      149
      Likes Given
      31

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By amba.nkya
      kuna wanyakyusa, wahehe, waha, wanyamwezi, wasukuma, wakurya, na wengine kibao, sema jingine...Zombi
      kama CDM ni ya wachaga na kwasababu wachaga wameweza kufanya mambo yao vizuri na kupata maendeleo naona si vibaya tukawakabidhi na nchi sio mbaya?
      Pasco and Ame like this.

    14. #51
      LINCOLINMTZA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th March 2011
      Location : Opposite The JF Web Page
      Posts : 1,360
      Rep Power : 696
      Likes Received
      352
      Likes Given
      216

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By magino
      haya mawazo ni mazuri sana, hata mm ni mpenzi wa CDM tusipojirekebisha katu Ikulu hatuioni!!! tusiwe wepesi wa kuwaambia wezetu wameongea pumba ili hali mawazo ni mazuri na ya kutujenga.... ni hayo tu kwa leo!!!
      Nimekubalina na wewe dada, lakini Avatar yako yaweza kuwachanga watu wakafikiri wako Jukwaa la MMU.
      Pasco likes this.
      Love everybody, trust no body. If you can not convince them, confuse them. If you can not teach them, cheat them.

    15. Ame
      #52
      Ame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Location : Global Citizen
      Posts : 1,513
      Rep Power : 1184
      Likes Received
      650
      Likes Given
      2615

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By mkomatembo
      Chadema sio rahisi kushinda, kwa sababu imeonesha dhahiri kuwa ni chama cha kanisa, sisi waislamu hatuwapi kura zetu , hilo lazima walijue, sasa watashinda kwa kura za kina nani?
      Vipi kama nature itasababisha watu wa dini moja (mf. wote waisilamu) tu wakawa ndiyo wagombea mta imba koras ipi tena?
      Pasco likes this.

    16. #53
      sembuli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Posts : 599
      Rep Power : 487
      Likes Received
      243
      Likes Given
      167

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      umekunywa nini leo pasco?
      Sikubaliani na namba 6: si kweli kuwa CDM inapendwa sababu tu CCM imechokwa,,!
      Nguvu kubwa ya CDM ni vijana “TAIFA LA LEO” Ambao 1977 wakati ccm inaanzishwa ama hawakuwepo au walikuwa watoto wa miaka 1-8 . Hivyo Hoja ingekuwa CCM IMECHOKWA basi wazee ambao relatively ni wengi ccm kuliko CDM ,wote wangekuwa CDM maana walikuwa nayo tangu 1977 ilipo anzishwa.

      My opinion: CDM Inapendwa kwa sababu sera zake zinajibu maswali ,mahitaji na matarajio ya vijana wa taifa hili,
      1: Ukosefu wa ajira kwa vijana.
      2: kupiga vita ufisadi kwa vitendo.
      3:uwajibikaji .
      4: sera mbadala ya mikopo ya elimu ya juu
      5:bei nzuri ya mazao ya kulima na uhuru wa masoko
      6:pembejeo kwa urahisi bila ukilitimba kama ilivyo sasa.
      Hayo na mengine mengi ndio yanatuvuta wananchi na vijana CDM, Si kuchoka ccm pekee ingekuwa kuchokwa basi republican na democrat vya marekani visingekuwepo hadi leo kutokana na ukongwe wa zaidi ya karne kadhaa
      Fidel80, Pasco, zumbemkuu and 1 others like this.
      There are two ways to slide easily through life; to believe everything OR to doubt everything; Both ways save us from thinking- Alfred korzybski

    17. #54
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By IBRAAH
      hadi leohujajua sababu za watz kukichagua chadema? sababu ni hiz hapa
      1.wananchi waliahidiwa maisha bora lakin imekuwa kinyume chake
      Mkuu Ibra, ni kweli kabisa CCM ilichaguliwa kwa ahadi ya kuleta "Maisha bora kwa kila Mtanzania" na kiukweli haikutekeleza, hivyo 2015 hautaichagua kwa sababu hii!. Hii ndizo kura za "kuchokwa kwa CCM" ambazo Chadema itazivuma kama imeokota!. Lakini Jee, Chadema wamekuahidi nini kuhusu hayo maisha bora?, Jee tukishaipiga chini CCM kwa sababu ya hasira za kukosa maisha bora, wako watakao ichagua Chadema ili tuu kuiadhibu CCM, lakini watu makini zaidi, na hawawezi kuichagua Chadema kwa sababu tuu ya kuichoka CCM, bali wataichagua Chadema kwa sababu Chadema imesema itafanya A,B,C, D kuwapatia Watanzania maisha bora ambayo CCM wameshindwa!. Ndio maana nimewaambia viongozi wa Chadema, kusema tuu kuwa CCM ni mbaya, hakutoshi, wasema wao watafanya nini and how?, lazima sasa wabadilike, watupe sababu za kuichagua Chadema!.
      Quote By IBRAAH
      4.kwa miaka 50 tangutupate uhuru chama kukaa madarakan kimeshindwa kutatua kero mbalimbali za wananchi kama vile ujenzi wa shule,nyumba za watumishi,zahanati,upatiakanaj i wa dawa na watumishi. Sababu hizo zinatosha kukipigia kura
      Na hapa pia nakuunga mkono, ni kweli CCM kimeshindwa kutatua kero ya umasikini, ujinga, maradhi, rushwa na ufisadi kwa Tanzania ndani ya miaka 50 iliyopita. Chadema kupitia M4C, is doing the right thing, kuzunguka nchi nzima kuwafungua macho Watanzania jinsi CCM ilivyoshindwa kutatua kero mbalimbali za Watanzania, kueleza tuu kuhusu kero ni one thing, sasa Chadema inatakiwa ibadilike, "not only doing the right thing, but also doing the things right" kwa kuwaeleza Watanzania yenyewe itafanya nini kinyume cha ilichofanya CCM ili kuwapa Watanzania sababu ya kuichagua Chadema!.

      Ili Chadema wayaweze yote hayo, kwanza lazima ikubali kusikiliza kuhusu mapungufu yake, iyafanyie kazi na kuyatekeleza!. (Naombeni msiniulize mapungufu ya Chadema), viongozi wa Chadema wameisha ambiwa sana, imebaki kwanza kusikia, pili kutekeleza, 2015, ikulu ni yao!,

      Kinyume cha hapo, CCM itaendelea, na Chadema waki miss hii golden opportunity ya 2015!, then Chadema kitakuwa ni chama cha kudumu cha upinzani, just imaginethe scanerio ya uchaguzi wa 2015, kama yule kamanda wangu wa CCM ndie ataongoza mapambano, Chadema bila kuja na credible reasons kwa nini kichaguliwe, CCM itapeta tena kwa kishindo, na nawaombeni sana tafadhali msirudi humu kulia lia na kususa as if hamkuambiwa!.

      Pasco.

    18. #55
      Jibaba Bonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2008
      Posts : 1,003
      Rep Power : 763
      Likes Received
      145
      Likes Given
      61

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Pasco! Pasco!!! hivi msimamo wako hasa ni upi? Au unapima upepo? Hapa ulimaanisha nini?

      http://www.jamiiforums.com/tanzania-2010-2015/314614-kuelekea-2015-kama-ccm-itamsimamisha-edward-lowassa-then-2015-ni-ccm-tena.html
      Pasco likes this.

    19. #56
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By Dangire
      akili za magamba.....hivi bado unaamini kuwa cdm ni chama cha wachaga! ajabu.kama ni hivyo, ukichanganya wachaga wote walio ndani ya ccm na vyama vingine vyote, kisha ongeza wakristo wote, kisha watz wote, cdm itakuwa bado haijaingia madarakani? ........kumbuka..cdm ni chama kisicho na dini wala kabila.
      Hapo ndio pazuri.
      Pasco likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    20. #57
      winner forever's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2012
      Location : Port of Spain
      Posts : 551
      Rep Power : 558
      Likes Received
      101
      Likes Given
      88

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By zomba
      Hivi chadema itashinda kwa kura za kina nani? wachagga? wako wangapi nchi hii?
      Unazidi kuiweka CCM kwenye tope kwa hoja zako nyepesi kama hizi,tembelea morogoro,mbeya,iringa ruvuma,mtwara etc uwaone watanzania wa leo

    21. #58
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By amba.nkya
      kuna wanyakyusa, wahehe, waha, wanyamwezi, wasukuma, wakurya, na wengine kibao, sema jingine...Zombi
      Muengueni Shibuda kugombea Uenyekiti muone hao.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    22. #59
      Mzizi wa Mbuyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2009
      Posts : 3,202
      Rep Power : 1270
      Likes Received
      531
      Likes Given
      404

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Unatusumbua tu bwana!!! CCM imekufa bwana!! itashindaje!!?
      Pasco likes this.

    23. #60
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kuelekea 2015: Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

      Quote By Ngongo
      Wachagga wapo wengi sana zomba ngoja ni kumwagie list.

      [1] Anthony G Mbassa huyu ni mchagga wa Biharamulo magharibi

      [2] Prof Kulikoyela Kahigi huyu ni mchagga wa Bukombe Shinyanga

      [3] Simon Peter Msigwa huyu ni mchagga wa Iringa Mjini

      [4] Yohana Natse huyu ni mchagga wa Karatu

      [5] Halima Mdee huyu ni mchagga wa Kawe Dar

      [6] Zitto Z kabwe huyu ni mchagga wa Kigoma kaskazini

      [7] John Shibuda huyu ni mchagga wa Maswa mashariki

      [8] Joseph Mbilinyi huyu ni mchagga wa Mbeya mjini

      [9] David Silinde huyu ni mchagga wa Mbozi magharibi Mbeya

      [10] Mustafa Akonnay huyu ni mchagga wa Mbulu

      [11] Meshack Opulukwa huyu ni mchagga wa Meatu Shinyanga

      [12] Said Arf Amour huyu ni mchagga wa Mpanda Rukwa

      [13] Vicent Kiboko Nyerere huyu ni mchagga wa Musoma mjini

      [14] Ezekia Wenje huyu ni mchagga wa Nyamagana Mwanza

      [15] Tundu Lissu huyu ni mchagga wa Singida Mashariki

      [16] John Mnyika huyu ni mchagga wa Ubungo Dar

      [17] Salvatory Machemuli huyu ni mchagga wa Ukerewe........

      Mkuu zomba kama wachagga wameenea kila pembe ya Tanganyika ni kwanini wasishike dola haa ha ha ha wanchekesha!!!!!!.
      Kwani hao walikuwa wapi mwaka 2005 na 2010? mbona Mbowe aligaragazwa vibaya sana, uchaguzi uliofatia akaona huyu Jakaya Mrisho Kikwete si size yake akamuomba Slaa amsaidie, nae akagaragazwa vibaya sana na hao vibaraka wenu si walikuwepo au umesahau?
      Pasco likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    Page 3 of 27 FirstFirst 1234513 ... LastLast

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...