Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

    Report Post
    Page 1 of 6 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 114
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Wanabodi,

      Katika thread moja humu jukwaani, nimekutana na mchango wa mwana jf huyu

      Quote By jogi
      mkuu Pasco, Nikubaalie japo mara hii tu kuwa, tatizo linalotumaliza ni zimwi CCM.
      Kutokana na kauli hiyo, nimekuwa inspired kuandika kidogo kuhusu adui mkuu wa Tanzania wengi wakidhani ni CCM, kumbe sio, bali adui mkuu wa Watanzania ni huyu nimtajae hapa chini na headline imejielekeza kwa Chadema, simplt because ndicho chama pekee so far chenye kuonyesha mwelekeo wa matumaini ya uwezekano wa kulipatia taifa letu la Tanzania, ule ukombozi wa pili wa kweli wa Mtanzania!.

      Mkuu Jogi, japo umeniomba "Nikubaalie japo mara hii tu kuwa, tatizo linalotumaliza ni zimwi CCM". Samahani sana, sikukubalii, kwa maoni yangu,

      1. Tatizo kubwa la Watanzania sio au adui mkubwa wa Tanzania sio CCM, CCM is just the vehicle, haikujiweka hapo ilipo, imewekwa, hivyo tatizo sio CCM iliyowekwa, bali tatizo ni walioiweka CCM hapo ilipo!. That simply means, tatizo ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani and it plays games on us again and again na sisi tukiendelea kuiweka madarakani again and again na sitashangaa kama hata 2015, tukairudisha tena!.

      2. Hii dhana ya kudhania adui mkubwa wa Tanzania ni CCM, is a wrong concerpt, na ndilo kosa kubwa la wapinzani, katika chaguzi zote za nyuma kuelekeza concetration ya mashambulizi yote kwa CCM wakijihesabu ndie adui yao mkubwa, hivyo ku miss the real target ya adui halisi ni nani!.

      5. CUF baada ya kujaribu mara 3 ikashindwa, ikaamua kutumia principle ya "if you can't beat them, join them", kwa mara ya 4 katika uchaguzi wa 2010, ikakubali yaishe, ikawajoin ndani ya SUK katika ndoa ya kukubali kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM, at the same time, its fighting from within, and is hitting them very hard kwa mtindo wa "kikulacho" na kikundi cha "uamsho" ni matokeo chanya ya kipigo from within, hivyo kwa 2015 upande wa Zanzibar CUF ni njia nyeupe!.

      6. Kwa sasa, angalau Chadema, kupitia M4C, imeshagundua adui halisi anayewakosesha ushindi, na sasa imejielekeza kwa wananchi ambao ndio wenye maamuzi ya mwisho na wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu, hivyo concetration ikiwekwa kwenye "changing mindset ya wenye maamuzi, kuacha kuchagua kwa mazoea tuu, bali kuchagua kwa sababu. Wananchi, watafunguka macho, na hawatakuwa na sababu tena ya kuendelea kuichagua CCM!.

      7. Mara baada ya uchaguzi wa 2010 na mafanikio makubwa upande wa Chadema, kwenye ile mada yangu ya "CCM Imechokwa, Chadema Haijajipanga", niliwaeleza kuwa wapinzani bado hawajipanga mkao wa kushika dola, lakini kwa kwa sasa kupitia M4C, Chadema wanaonyesha dalili za kujipanga japo bado wanakabiliwa na madhaifu haya na yale, yakiwemo, lile koti la ukanda, udini, ukabila na ubinafsi wa "umimi" etc.

      8. Kwa leo naomba nisiingie tena kwenye udini, ukanda na ukabila wa Chadema, bali naomba nijikite kwenye ubinafsi au "umimi" kwa Chadema kujiamini kupita kiasi kuwa peke yao wataweza!, nilisema peke yao hawawezi, na leo nasema te na na tena, "Chadema peke yenu hamuwezi Kuiondoa CCM Madarakani" kwa sababu hili CCM ni dubwana kubwa sana ambalo haliwezi kung'oka bila umoja ambao ni nguvu ya Watanzania wote wenye kuliutakia mema taifa hili.

      9. Kabla ya kauli ya majuzi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda kule bungeni, nilikuwa najua ma RC na ma DC ni watendaji wakuu wa serikali mikoani na wilayani baada ya kutenganisha zile kofia mbili za chama kushika hatamu za kuiongoza serikali, kumbe wamevua tuu hizo kofia na kutovaa sare, lakini kiutendaji kumbe wako pale kuhakikisha CCM inatawala milele!, hivyo bila joint foces, hakuna jinsi ya kuipumzisha CCM na ni kweli itatawala milele!.

      10. Chadema na wapinzani wengine wote wa ukweli, ni lazima wa join forces kutafuta the common working grounds na wenzenu wengine wote mu work together towards a common enemy hata na nyinyi wenyewe kwa wenyewe lazima mkubali kushirikiana kwa kukubali kutokubaliana kwa hayo madogo madogo lakini lazima mkubaliane kwenye kubwa la msingi kwa kukubali "umoja ni nguvu" vinginevyo matokeo ya 2015 yatakuwa ni yale yale ya, vyama vile vile, na watu wale wale!.

      11. Mfano, japo CUF ni mke wa CCM kwa upande wa Zanzibar, hiyo ni "marriage of convinience", hivyo inavunjika wakati wowote "conveniences" zikimalizika, hivyo Chadema inacho kibarua kigumu cha kum..ngoza huyu mke wa mtu kwa kumhakikishia akikubali kutoka nje ya ndoa, yeye sasa hatakuwa mke tena, bali atageuka mume na 2015 ni yeye sasa ndie atageuka kidume na kumuoa huyo mume aliyenae sasa kwa sababu mume huyo ategeuzwa mke!.

      12. Hakuna ubishi kuhusu nguvu ya CUF kule Zanzibar na Chadema itake isitake, ipende isipende, ili kujihakikishia njia nyeupe ya kuwa mpangaji wa magogoni kwa 2015, ni lazima ikubali kuisupport ya CUF kwa upande Zanzibar ili CUF nao wakubali kuisupport Chadema huku bara!. Chadema wakae chini na CUF, waainishe maeneo ya strong holds za kila mmoja na kuachiana maeneo hayo ili 2015, kuepuka kumfaidisha kunguru kwa vita vya panzi!.

      13. Voting statistics

      Registered Voters 20,137,303
      Total votes 8,626,283
      % Turnout 42.84
      Valid votes 8,398,394
      Spoilt votes 227,889
      % Spoilt votes 2.64
      Table source

      Commonwealth 2010, 31.
      Results

      Candidate Party Votes % Vote
      Jakaya Kikwete Chama Cha Mapinduzi (CCM) 5,276,827 62.83
      WP Slaa Chama Cha Demokiasia na Maendeleo (CHADEMA) 2,271,941 27.05
      Ibrahim Lipumba Civic United Front (CUF) 695,667 8.28
      Peter Mziray Kuga Progressive Party of Tanzania (PPT-MAENDELEO) 96,933 1.15
      Rungwe Hashim Spunda National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi) 26,388 0.31
      Muttamwega Bhatt Mgaywa Tanzania Labour Party (TLP) 17,462 0.21
      Yahmi Nassoro Dovutwa United People's Democratic Party (UPDP) 13,176 0.16
      Total 8,398,394 99.99
      Table source

      Commonwealth 2010, 31.

      14. Kwa mujibu wa data hizo, JK amechaguliwa kura milioni 5 tuu kati ya watu milioni 40!. Waliojiandikisha ni milioni 20, lakini waliopiga kura ni milioni 8 tuu!, hii inamaanisha kuna watu milioni 12, ambao walijiandikisha lakini hawakupiga kura kwa sababu mbalimbali, ikiwemo wale waliokata tamaa na kuona kupiga kura ni wastage of time, hata upige vipi kura, matokeo ni yale yale lazima CCM ishinde, hivyo kuliko kupoteza muda wakaachana kabisa na kupiga kura!

      15. Suppose 2015, Watanzania tutakuwa Milioni 50 wenye sifa za kupiga kura ni milioni 35, hawa wote wakihamasishwa kujiandikisha na kujitokeza kupiga kura, mgombea wa CCM atajipatia kura zao zile milioni 6 za wanachama wao kwa mujibu wa tovuti ya CCM, halafu hizo kura milioni 29 zimuangukie mgombea wa upinzani, hata NEC ya CCM, wachakachue vipi, there will be no way out!, hivyo adui yetu mkubwa sio CCM, bali ni Watanzania wanaipigia kura CCM!.

      Wasalaam.

      Pasco.

      NB. Pasco wa JF, sio mwanachama, mfuasi wala mshabiki wa chama chochote cha siasa, bali ni Mtanzania wa kawaida mwenye kuweka mbele maslahi ya taifa.
      Last edited by Pasco; 20th August 2012 at 19:46.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      only83's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Dodoma-Mjengoni
      Posts : 4,157
      Rep Power : 1846
      Likes Received
      1431
      Likes Given
      1539

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      NB. Pasco wa jf, sio mwanachama, mfuasi wala mshabiki wa chama chochote cha siasa, bali ni Mtanzania wa
      kawaida mwenye kuweka mbele maslahi ya taifa.
      Hoja yako ni njema ila hii kauli hapo juu ndio uwa inaniacha hoi..ati Pasco wa JF sio mwanachama wala mshabiki wa chama cha siasa...huu ni unafiki, ukweli ni kuwa unaweza usiwe mwanachama au mfuasi wa chama chochote ila lazima uwe na hisia za chama fulani..kwa asili ya binadamu ni ngumu kuwa at the between. Jaribu kuacha unafiki huu nadhani hoja zako zitakuwa bora zaidi. Ukweli ni kuwa hoja yako ina mashiko, isipokuwa unafiki weka pembeni.
      Kaa la Moto, Pasco, Mboko and 1 others like this.
      "Problems can not be solved by the same level of thinking that created them"
      "Matatizo hayawezi kutatuliwa na uwezo ule ule mdogo wa watawala wa CCM walioyasababisha"




    4. #3
      ChiefmTz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2008
      Posts : 1,478
      Rep Power : 861
      Likes Received
      109
      Likes Given
      36

      Default

      Pasco

      Mkuu chukua tano umenena ukweli ambao wenye makengeza hawataki kuuona.
      Pasco likes this.

    5. #4
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,852
      Rep Power : 2331
      Likes Received
      2858
      Likes Given
      5512

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pasco,

      Naogopa kusema kuwa wewe ndiyo una makosa.

      Kwa haraka haraka na kwa kutumia KATIBA zetu hizi za Tanzania zilizo na matundu mengi kama Mipaka yetu ya nchi, nasikitika kukuambia kuwa CCM IMEJIWEKA MADARAKANI na si kuwa TUMEIWEKA MADARAKANI.

      Tukianzia na uchaguzi wa Rais, ni wewe ulitutangazia matokeo siku kadhaa hata kabla ya uchaguzi. Ukatuambia na maandalizi ya kumuapisha KIKWETE (siyo RAIS) kuwa Rais kwa muhula wa pili yameshaanza (tulishangaa hata wageni waalikwa kuwepo). Hii haikujalisha kama ameshinda au kashindwa kwa sababu katiba ya Tanzania, MTU AKITANGAZWA NA TUME KUWA NDIYO RAIS, basi imetoka na huwezi kwenda kupinga matokeo hayo popote pale. Nina imani ingelikuwepo kifungu hicho, sasa hivi uchaguzi ungelirudiwa tena na watu kufungwa..... (wafungwe na nani? Majaji waliochaguliwa na Kikwete? Jaji gani aamue uchaguzi urudiwe wakati wamewekwa hapo na huyo huyo Kikwete? Polisi gani apeleleze? Usalama gani wa Taifa apeleleze? Takururu gani apeleleze ... wakati Maboss wote wamewekwa na Kikwete/Mwenyekiti wa CCM???)

      Hapo unaona kuwa Mduara unafunga kama wimbo wa P-SQUARE (If you do me, I do you). JWTZ gani aje juu wakati ndiyo hao akina Shimbo na mtani wangu Mwamunyange walikuwa kwenye mkutano wa MBAYUWAYU?

      CCM ni kama mashidano ya ngumi na CHAMPION. Ukitaka kumshinda, mpeleke chini kwa KNOCK OUT maana vinginevyo utaambiwa mmetoka droo na hapo mshindi bado ni YEYE.

      Adui wa Tanzania wapo wengi ila namba moja ni CCM (kama 40%) ila ndiye mwenye asilimia nyingi. Huyo akiondoka, bado kutakuwa na kazi kubwa sana ya kuwaondoa hawa wengine wengi ila wadogo wadogo - Katiba, Polisi, Takururu, Usalama wa Taifa, Mahakama, Bunge, Umasikini, Elimu ya uraia, kusoma na kuandika, Muungano na Zanzibar nk nk.
      Mkuu Jogi, japo umeniomba "Nikubaalie japo mara hii tu kuwa, tatizo linalotumaliza ni zimwi CCM". Samahani sana, sikukubalii, kwa maoni yangu,

      1. Tatizo kubwa la Watanzania sio au adui mkubwa wa Tanzania sio CCM, CCM is just the vehicle, haikujiweka
      hapo ilipo, imewekwa, hivyo tatizo sio CCM iliyowekwa, bali tatizo ni walioiweka CCM hapo ilipo!. That simply
      means, tatizo ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani and it plays games on us again and again na sisi
      tukiendelea kuiweka madarakani again and again na sitashangaa kama hata 2015, tukairudisha tena!.

      2. Hii dhana ya kudhania adui mkubwa wa Tanzania ni CCM, is a wrong concerpt, na ndilo kosa kubwa la
      wapinzani, katika chaguzi zote za nyuma kuelekeza concetration ya mashambulizi yote kwa CCM wakijihesabu
      ndie adui yao mkubwa, hivyo ku miss the real target ya adui halisi ni nani!.
      Last edited by Sikonge; 20th August 2012 at 12:37.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    6. #5
      maria pia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th July 2012
      Posts : 304
      Rep Power : 403
      Likes Received
      31
      Likes Given
      65

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      nitarudi
      Pasco likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,852
      Rep Power : 2331
      Likes Received
      2858
      Likes Given
      5512

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Hivi kulikuwa na haja gani ku-quote HABARI NZIMA na unakuja kuandika kimstari kimoja? HEBU angalia mwenzako hapo juu.
      Quote By ChiefmTz
      Mkuu chukua tano umenena ukweli ambao wenye makengeza hawataki kuuona.
      Pasco and Excellent like this.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    9. #7
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,852
      Rep Power : 2331
      Likes Received
      2858
      Likes Given
      5512

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Sikieni hii kauli ya mwanasheria mkuu wa serikali dhidi ya takukuru/dr hosea


      NI KUHUSU SHERIA KUIKWAZA TAKUKURU KUWASHTAKI VIGOGO WA UFISADI

      Kizitto Noya
      MWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema amesema Sheria ya Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru), ni nzuri na kwamba haipaswi kufanyiwa mabadiliko kama ambavyo imekuwa ikidaiwa.

      Jaji Werema aliliambia gazeti hili jana kuwa haoni haja ya sheria hiyo kufanyiwa mabadiliko sasa kwa kuwa haina tatizo na ipo kutekeleza misingi ya utawala wa Sheria.

      "Mimi nakubaliana na Sheria hii ya (Takukuru) kwamba iendelee kuwapo. Hakuna haja ya kuifanyia mabadiliko sasa. Ni nzuri kwa kuwa inazingatia misingi ya utawala wa sheria," alisema Jaji Werema.

      Kauli ya Jaji Werema inapingana na ile iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah kwamba sheria hiyo imekuwa ikiwakwaza kuwashughulikia wala rushwa wakubwa, kwani majalada ya kesi zilizokwishafanyiwa uchunguzi yamekwama kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP).

      From: http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la...-dr-hosea.html

      Habari ndiyo hiyooo. Hao ndiyo utegemee watangaze Matokeo na kusimamia UCHAGUZI.
      Jasusi, Kaa la Moto, Pasco and 1 others like this.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    10. #8
      Sabung'ori's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th July 2011
      Posts : 822
      Rep Power : 560
      Likes Received
      233
      Likes Given
      16

      Default

      Sikonge

      ...naunga mkono hoja(LIKE)...
      Sikonge and Pasco like this.

    11. #9
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default

      Quote By only83
      Hoja yako ni njema ila hii kauli hapo juu ndio uwa inaniacha hoi..ati Pasco wa JF sio mwanachama wala mshabiki wa chama cha siasa...huu ni unafiki, ukweli ni kuwa unaweza usiwe mwanachama au mfuasi wa chama chochote ila lazima uwe na hisia za chama fulani..kwa asili ya binadamu ni ngumu kuwa at the between. Jaribu kuacha unafiki huu nadhani hoja zako zitakuwa bora zaidi. Ukweli ni kuwa hoja yako ina mashiko, isipokuwa unafiki weka pembeni.
      Only83, mimi kiukweli wa toka ndani ya moyo wangu sio mwanachama, sio mfuasi na sio mshabiki wa chama chochote!.

      Ndio maana nilipo waambia CCM wamechokwa na niliwaambia na jinsi ya kujinasua toka mchoko iliopo na walianza kujinasua japo wanajizamisha kwenye tope zito zaidi!.

      Nilipowaambia Chadema hawajajipanga, niliwaelekeza na jinsi ya kujipanga japo niliambulia kutukanwa sana, ujumbe ulifika na kujipanga kumeanza!.

      CUF nao walipofunga ndoa yao na CCM kwa kula kiapo cha kuitekeleza ilani ya CCM, niliwaambia that is the begining of an end of era for CUF bila kujua kuwa kumbe walifunga tuu ndoa of "canvenuence" kwa principle ya " if you can't beat them, join them" na sasa ndio wana hit'em hard from within!.

      Kwa mujibu wa kazi yangu mimi ni daiwaka kama taxi driver, wote ni abiria wangu, ukitokea mzigo wa CCM, napiga kazi, watakaosema mimi CCM na waseme.

      Ukitokea mzigo wa Chadema au CUF mimi napiga tuu kwa maslahi ya taifa mbele na kuziacha siasa za vyama nyuma.
      Mantaleka likes this.

    12. #10
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default

      Quote By Sikonge
      Pasco,

      Naogopa kusema kuwa wewe ndiyo una makosa.

      Kwa haraka haraka na kwa kutumia KATIBA zetu hizi za Tanzania zilizo na matundu mengi kama Mipaka yetu ya nchi, nasikitika kukuambia kuwa CCM IMEJIWEKA MADARAKANI na si kuwa TUMEIWEKA MADARAKANI.

      Tukianzia na uchaguzi wa Rais, ni wewe ulitutangazia matokeo siku kadhaa hata kabla ya uchaguzi. Ukatuambia na maandalizi ya kumuapisha KIKWETE (siyo RAIS) kuwa Rais kwa muhula wa pili yameshaanza (tulishangaa hata wageni waalikwa kuwepo). Hii haikujalisha kama ameshinda au kashindwa kwa sababu katiba ya Tanzania, MTU AKITANGAZWA NA TUME KUWA NDIYO RAIS, basi imetoka na huwezi kwenda kupinga matokeo hayo popote pale. Nina imani ingelikuwepo kifungu hicho, sasa hivi uchaguzi ungelirudiwa tena na watu kufungwa..... (wafungwe na nani? Majaji waliochaguliwa na Kikwete? Jaji gani aamue uchaguzi urudiwe wakati wamewekwa hapo na huyo huyo Kikwete? Polisi gani apeleleze? Usalama gani wa Taifa apeleleze? Takururu gani apeleleze ... wakati Maboss wote wamewekwa na Kikwete/Mwenyekiti wa CCM???)

      Hapo unaona kuwa Mduara unafunga kama wimbo wa P-SQUARE (If you do me, I do you). JWTZ gani aje juu wakati ndiyo hao akina Shimbo na mtani wangu Mwamunyange walikuwa kwenye mkutano wa MBAYUWAYU?

      CCM ni kama mashidano ya ngumi na CHAMPION. Ukitaka kumshinda, mpeleke chini kwa KNOCK OUT maana vinginevyo utaambiwa mmetoka droo na hapo mshindi bado ni YEYE.

      Adui wa Tanzania wapo wengi ila namba moja ni CCM (kama 40%) ila ndiye mwenye asilimia nyingi. Huyo akiondoka, bado kutakuwa na kazi kubwa sana ya kuwaondoa hawa wengine wengi ila wadogo wadogo - Katiba, Polisi, Takururu, Usalama wa Taifa, Mahakama, Bunge, Umasikini, Elimu ya uraia, kusoma na kuandika, Muungano na Zanzibar nk nk.
      Mkuu Sikonge, CCM is a wrong target the right target ni " people" na sio CCM, in targeting the people you'll hit them all including CCM kwa sababu iko among the people!. Ukiitarget CCM, you will only hit CCM and miss the people wanaoichagua CCM hivyo to miss the point and the target,2015 watu wataichagua tena CCM na tena na tena mpaka ilitimie ile miaka 100 tulioelezwa humu!.

      Lets now deal with the source and not outcome, CCM sio msingi, bali ni matokeo tuu, watu ndio msingi, ukideal na matokeo ukaacha msingi, msingi utaendelea kutoa matokeo yale yale!.

    13. #11
      Ng'wanangwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th August 2010
      Posts : 5,969
      Rep Power : 1642
      Likes Received
      1129
      Likes Given
      409

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pasco

      na wewe kumbe umekaririshwa kwamba chadema kuna ukanda, udini, ukabila na ubinafsi wa "umimi"?

      unaweza kuthibitisha kwa mifano?
      Kaa la Moto and Pasco like this.
      CCM HAIKUBALIKI ...TUSHIRIKIANE KUITOKOMEZA...

      REST IN PEACE, DR.D.D. HAULE...Wema hawana Maisha

    14. #12
      Temple's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 17
      Rep Power : 363
      Likes Received
      14
      Likes Given
      13

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pasco,
      Hayo mawanzo ya kutaka consensus kati ya vyama vya upinzani ni nzuri, lakini kumbuka yalitaka kuisambaratisha CHADEMA kwa sababu hakika ulikuwa mpango wa CCM ku penetrate katika vyama hivyo. CHADEMA kiliamini hivyo na kuwa baadhi ya waandishi wa habari na baadhi ya vyombo vya habari vilipewa task hiyo kuhakikisha CHADEMA inaingia mkenge. Uchaguzi mdogo wa Tarime ulidhihirisha hivyo. Hata hivyo siingilii mawazo yako kuwa CCM is too strong kwa CHADEMA peke yake kuitoa. Kwa mimi naiona is not strong that much ila baadhi ya watu kuto mini mabadiliko kama ilivyo kwa Rais wa Syria kwa sasa.
      Pasco likes this.

    15. #13
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,852
      Rep Power : 2331
      Likes Received
      2858
      Likes Given
      5512

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pasco,

      CCM ni WATU na siyo Chombo. System ni WATU na siyo Chombo.

      Ukishamfahamu ADUI wako vizuri, utajua tu jinsi ya Ku-deal naye.

      Ndiyo maana wakati ZITTO anatamba kuwa anataka kuwa RAIS na hayo maneno anayasema akiwa Bungeni au Mitaani, M4C wapo vijijini wakiishambulia CCM kwenye Mioyo ya watu.



      Emancipate yourselves from mental slavery; - CCM
      None but ourselves can free our minds.

      Have no fear for atomic energy,
      'Cause none of them can stop the time.
      How long shall they kill our prophets,
      While we stand aside and look? Ooh!
      Some say it's just a part of it:
      We've got to fullfil the book.

      Quote By Pasco
      Mkuu Sikonge, CCM is a wrong target the right target ni " people" na sio CCM, in targeting the people you'll hit them all including CCM kwa sababu iko among the people!. Ukiitarget CCM, you will only hit CCM and miss the people wanaoichagua CCM hivyo to miss the point and the target,2015 watu wataichagua tena CCM na tena na tena mpaka ilitimie ile miaka 100 tulioelezwa humu!.

      Lets now deal with the source and not outcome, CCM sio msingi, bali ni matokeo tuu, watu ndio msingi, ukideal na matokeo ukaacha msingi, msingi utaendelea kutoa matokeo yale yale!.
      Jasusi, BAK, Pasco and 1 others like this.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    16. #14
      zimmerman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 334
      Rep Power : 484
      Likes Received
      258
      Likes Given
      66

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pasco, unajua mada zako unazipanga vizuri, unaziandika vizuri na unazifafanua vizuri kwa lugha rahisi kiasi kwamba hata kama kimantiki si kweli watu wengi wanaweza kukubaliana na hoja zako? Ndivyo ilivyo hata kwa hoja yako hii ya leo.

      Kiukweli kulekea elfu mbili na kumi na tano adui mkubwa wa Chadema ni…..CCM.

      Mimi si mwandishi mzuri hivyo nitaenda straight to the point.

      1. Well, kuhusu watanzania kuichagua CCM over and over again, wewe unatarajia nini? The whole system is fine-tuned kuiweka CCM madarakani na kimsingi hilo ndilo linalowapa kiburi baadhi ya wasemaji wa CCM kwamba “CCM ipo ili kutawala milele…” na mwingine kuongeza kwamba “ni heri afe kuliko kuona Chadema inatawala…” We unadhani hii ni exercise in political rhetoric tu? Wanamaanisha wanayoyasema na kiukweli kuna kila sababu ya watawala wetu wa sasa na makada wa CCM kutopata hamu au kuogopa kabisa kuona upinzani unachukua serikali. Sababu zinajulikana.

      2. Dhana kwamba adui mkubwa wa watanzania si CCM bali ni sisi wenyewe siyo sahihi sana. Ni kweli kwamba kuna vi element fulani vya utamaduni wa kitanzania vinavyotubakisha sana nyuma lakini adui mkubwa ni yule anayecapitalize kwenye udhaifu wetu ili kuendelea kutunyonya na kutukandamiza. CCM haina huruma, haina tofauti na mkoloni wa kiarabu au kijerumani aliyetumia ukarimu wetu, upole wetu na kukosa elimu kwetu ili kujinufaisha juu ya migongo yetu. Ni kweli, hata hivyo, kwamba njia ya kumshinda adui wa namna hii ni kusambaza elimu ya uraia. Hii inatusaidia sana kuongeza ukali kidogo tunapodai haki zetu za kikatiba na kumpinga hasa pale anapoleta uhuni na ndicho Chadema wanachofanya.
      Jasusi, Kaa la Moto, Pasco and 6 others like this.

    17. #15
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,531
      Rep Power : 1263
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      28

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Good point... Watu wana njaa shida na taabu nyingi lakini utashangaa ccm wanafanya mkutano watu wanajaa na kuwasikiliza na bado wanawapigia kura. Nini ambacho ccm inataka kutuambia ambacho hatujasikia kwa miaka hii 50?
      Pasco and muchetz like this.
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    18. MTK
      #16
      MTK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th April 2012
      Posts : 928
      Rep Power : 4494
      Likes Received
      300
      Likes Given
      329

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pasco nakupa 4/10; your diagnosis(kutambua ugonjwa) may be right lakini perscription(kutibu) is off track!!

      Hebu tusaidie ni vyama gani ambavyo unaviona viko focused enough kuunganisha nguvu na CDM kuelekea ufanisi, na pia shauri watumie formula gani kufanikiwa kwa sababu wamejaribu mara nyingi wamekwama kutokana na baadhi ya udhaifu uliouainisha hapo juu!

      Binafsi naamini CDM haina sababu ya kuhangaika na vyama vya siasa bali kukusanya nguvu za umma na makundi ya vyama vya wafanya kazi, wakulima na wafugaji, taasisi zisizo sa kiserikali na wanaharakati mbalimbali bila kusahau diaspora(watanzania wanaoishi nje ya nchi)

      Kampeni za Sangara na vuguvugu la M4C na nyingine zitakazofuata kuelekea 2015 zinakusudia kufanikisha uamsho huo; watanzania wajitambue na kuchukua hatua mahsusi.

    19. #17
      SoNotorious's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2011
      Posts : 750
      Rep Power : 507
      Likes Received
      184
      Likes Given
      241

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      It is not a war against ccm or cdm, it is a war against YOU.
      Kaa la Moto and Pasco like this.

    20. #18
      Yonjolo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th January 2012
      Posts : 80
      Rep Power : 386
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Sikonge
      Pasco,

      Naogopa kusema kuwa wewe ndiyo una makosa.

      Kwa haraka haraka na kwa kutumia KATIBA zetu hizi za Tanzania zilizo na matundu mengi kama Mipaka yetu ya nchi, nasikitika kukuambia kuwa CCM IMEJIWEKA MADARAKANI na si kuwa TUMEIWEKA MADARAKANI.

      Tukianzia na uchaguzi wa Rais, ni wewe ulitutangazia matokeo siku kadhaa hata kabla ya uchaguzi. Ukatuambia na maandalizi ya kumuapisha KIKWETE (siyo RAIS) kuwa Rais kwa muhula wa pili yameshaanza (tulishangaa hata wageni waalikwa kuwepo). Hii haikujalisha kama ameshinda au kashindwa kwa sababu katiba ya Tanzania, MTU AKITANGAZWA NA TUME KUWA NDIYO RAIS, basi imetoka na huwezi kwenda kupinga matokeo hayo popote pale. Nina imani ingelikuwepo kifungu hicho, sasa hivi uchaguzi ungelirudiwa tena na watu kufungwa..... (wafungwe na nani? Majaji waliochaguliwa na Kikwete? Jaji gani aamue uchaguzi urudiwe wakati wamewekwa hapo na huyo huyo Kikwete? Polisi gani apeleleze? Usalama gani wa Taifa apeleleze? Takururu gani apeleleze ... wakati Maboss wote wamewekwa na Kikwete/Mwenyekiti wa CCM???)

      Hapo unaona kuwa Mduara unafunga kama wimbo wa P-SQUARE (If you do me, I do you). JWTZ gani aje juu wakati ndiyo hao akina Shimbo na mtani wangu Mwamunyange walikuwa kwenye mkutano wa MBAYUWAYU?

      CCM ni kama mashidano ya ngumi na CHAMPION. Ukitaka kumshinda, mpeleke chini kwa KNOCK OUT maana vinginevyo utaambiwa mmetoka droo na hapo mshindi bado ni YEYE.

      Adui wa Tanzania wapo wengi ila namba moja ni CCM (kama 40%) ila ndiye mwenye asilimia nyingi. Huyo akiondoka, bado kutakuwa na kazi kubwa sana ya kuwaondoa hawa wengine wengi ila wadogo wadogo - Katiba, Polisi, Takururu, Usalama wa Taifa, Mahakama, Bunge, Umasikini, Elimu ya uraia, kusoma na kuandika, Muungano na Zanzibar nk nk.
      Nakugongea "like" mkuu. Kama watanzania walionesha nia njema kwa nchi yao kwa kukipiga chini chama cha mapinduzi ni dhahiri kabisa bwana pasco unawakosea watanzania na unapaswa utuombe radhi.

      Mimi naamini tulifanya sehemu yetu lakini kwa bahati mbaya wao ccm wameushikilia mpini kwa mabavu yote.

      Kama mtu ana roho mbaya huwa haichukiwi roho bali mwili wa huyo mtu utahesabika kuwa ni mbaya tu.
      ccm ni janga la uhai wa watanzania.
      Sikonge and Pasco like this.

    21. #19
      TUMBIRI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 1,856
      Rep Power : 3633
      Likes Received
      1114
      Likes Given
      283

    22. #20
      Wilawela's Avatar
      Member Array
      Join Date : 16th November 2011
      Posts : 80
      Rep Power : 395
      Likes Received
      28
      Likes Given
      454

      Default re: Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!

      Pascal nakubaliana nawe kwa kusema umoja ni nguvu na utengano ni udhaif.

      Lakini kumbuka 1995 CDM walijiunga na NCCR mageuzi wakamsapoti Mrema na Kukubaliana kuachiana majimbo ya Ubunge Kumbuka arusha Mjini Makongoro Nyerere alitakiwa amwachi Mzee Mtei as pe MoU ilikiukwa, 2000 Bob Makani baada ya kuvuta fomu aliambiwa amwachi Prof.Lipumba na alifanya hivyo lakini matokeo yake hawakuachiana Ubunge wala Udiwani!

      Miaka yote hiyo CDM wamekuwa wakiwachia CUF urais,ubunge uwakilishi nk, lakini mara zote wamesalitiwa! Unajua mfano last election mambo yalikuwa safi kwa CDM na magumu kwa CUF lakini likaja wazo ya "KURA ZA HISANI KWA KIKWETE MWISLAM MWENZETU NA KUEPUSHA NCHI KUTAWALIWA NA PADRI" uzuri kila kitu hadharani(rejea kanda za wanazuoni wa kiislam) sasa mazingira kama hayo toa Strategies za kuunganisha nguvu na kupata UMOJA.

      Maana wewe unaweza kuwaza very Objectively mwenzio so Subjectively! Maana hata sasa CUF wanasema rais atoke Zenj kwa nia hiyo hiyo!
      10. Chadema na wapinzani wengine wote wa ukweli, ni lazima wa join forces kutafuta the common working grounds na wenzenu wengine wote mu work together towards a common enemy hata na nyinyi wenyewe kwa wenyewe lazima mkubali kushirikiana kwa kukubali kutokubaliana kwa hayo madogo madogo lakini lazima mkubaliane kwenye kubwa la msingi kwa kukubali "umoja ni nguvu" vinginevyo matokeo ya 2015 yatakuwa ni yale yale ya, vyama vile vile, na watu wale wale!.
      Jasusi and Pasco like this.

    Page 1 of 6 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...