Fikiri kabla ya kutenda. Nidhairi kuwa viongozi wetu wana ufinyu wa fikra, ili jambo haliingii akilini na linasikitisha sana kuwa na viongozi kama hawa. Inakuwaje? Ikulu tuna muuzia Marekani. Watanzania niwajibu wetu kulikomboa taifa ili tuachane na ushabeki wa chama.
Ni wajibu wa kila mmoja wetu kusimama na kulitetea na kulikomboa taifa letu ambalo kwasasa liko katika mikononi mwa wanyang’anyi. Pili ningependa kila mtanzania ajue kuwa Tanzania hatuko huru bali uhuru wa bendera. Tatu ikumbukwe kuwa viongozi wetu ni madikteta, mfano mzuri tuangalie Kigamboni ambayo imeuzwa, imeuzwa kwa lidhaa ya nani?
Kama sio udikteta, nimatumaini yangu kuwa kila kitu kinachofanyika viongozi wetu ujiuliza kuwa watatufanyeje hawa zezeta? Ili linaonesha kuwa huu ni udikteta usiokuwa na mfano, wana Kigamboni wana atimiliki za maenoe yao lakini hawakuusiswa katika sakata la kuuzwa sehemu yao. Lakini ili ni kwasababu yao serikali kujua uhozo wanaofanya katika nchi hii na sisi kukaa kimya.
Tena wanapokuja katika kapeni tunawapa ridhaa ya kuongoza taifa tena kama vile hatuoni uhozo wao. Naili inabidi tuliangalie kwa umakini.. Ndugu zangu watanzania ili tusiliachie wananchi wa Kigamboni ilinatuhusu sisi pia kama watanzania wazalendo na wapenda haki.
Ninapenda viongozi wajue ni wajibu wao kama viongozi kabla ya kufanya kitu chochote kinacho husu wananchi wanaokaa katika eneo ilo au lolote kwanza wakubaliane kabla ya kutenda/kufanya kitu chochote. Hapa inasemekana hakuna mwananchi mwenye haki katika nchi hii.
Wananchi swala la Kigamboni tusiwaachie kigamboni tu. Ili ni swala la kitaifa tuachane na uzezeta wa kushangilia eti Tanzania itakuwa kama Ulaya, ndugu zangu mtegemea cha nduguye ……………………… kwanini tusifaye yetu? Kama tunataka tuwe kama Ulaya tutakuwa kama Ulaya kwa kulinda na kusimamia mali za taifa letu.

Reply With Quote
Follow Us Here