Mbele ya Jakaya Kikwete, Joyce Banda alitamka kwamba Ziwa Malawi ni la Malawi kwa asilimia 100.
JK akatamka kwamba hajawahi kufikiri au kusogeza jeshi na yeye ndiye amiri jeshi mkuu.
JK hata hakuwa na haja ya kusema kwamba tuiachie suala hilo kamati maana wote tunajua na hata humu JF tumeeleza sana kwamba August 20, 2012, Kamati inayojumuisha mawaziri na wataalamu itakutana huko Mzuzu, nchin Malawi kwa suala hilo.
August 20, 2012 imefika, na ndiyo leo. Sasa, tukae tayari. Baada ya marais kutoa matamko, hali ya hewa humu imebadilika. Waliokuwa wa kwanza kukejeli ukweli kuhusu Heligoland na kuwasema wenzao wa malawi wameshindwa kabisa kumsema JK ni mmalawi.
Sasa, membe yuleyule aliyetetewa humu JF ni lazima tutajua leo atatamka nini. Membe aliyesema kuwa mpaka uko katikati ya Ziwa tena kwa mujibu wa Heligoland treaty sasa ni lazima atasema matokeo ya mkutano huo.
Mnaopitia thread zangu na mliosoma article ya Ansbert Ngurumo jana kwenye TANZANIA DAIMA hatuna tofauti sana. Ngurumo alishangazwa na kitendo cha kishujaa cha Joyce Banda kusema Ziwa malawi ni lote la Malawi kwa asilimia 100 na Kikwete akashindwa kusema asilimia za Tanzania kwa ziwa hilo.
Ngurumo anauliza, kama tuna asilimia sifuri katika ziwa hilo, sasa hayo majadiliano tunaenda kujadili nini? Tutaendaje kujadili ziwa la watu?
Ndizo hoja ambao humu mimi nimekuwa nikizitetea bila kutetereka jana, leo na kesho.
Sasa wakati mawaziri wanakutana huko Malawi leo, tuone ni nini kinaweza kutokea kwa kujikumbusha majibu yetu kuhusu mpaka wa Malawi:
*****
MAY 26, 1959
HANSARD YA BUNGE LIKIWA NA WANACHAMA WENGI WA TANU INASEMA HIVI:
Article II of the Anglo-German agreement of 1890.
The description of the southern boundaries of Tanganyika, which include the boundaries of Nyasaland, are as follows:
'from the point of confluence of the Rovuma River with the Msinje River, the boundary runs westward along the parallel of that point until it reaches Lake Nyasa, thence striking northward it follows the Eastern, Northern and Western shores of Lake Nyasa to the northern bank of the mouth of the River Songwe; it ascends that river to the point of its intersection by the 33rd degree of east longitude'.
*****
NOVEMBER 30, 1961:
Nyerere, then Prime Minister, set out the policies which Tanganyika would not adopt, once independent, towards international treaties concluded by Britain.
*****
JUNE 11, 1962:
HANSARD YA BUNGE LA TANGANYIKA HURU HUKU RASHID KAWAWA AKIWA EXECUTIVE PRIME MINISTER INASEMA HIVI:
In his reply the Prime Minister, currently Rashidi Kawawa, made three points:
(i) that no part of Lake Nyasa fell within German East Africa;
(ii) that since the boundary had not been altered by Britain after the assumption of the mandate, the Prime minister's statement of 30 November 1961 did not apply; and
(iii) that whatever the disadvantages to Tanganyika, the Government could not contemplate negotiations with either the Central African Federal Authorities in Salisbury or with Britain. 'If there are to be negotiations on this question', he concluded, 'they must be with the Government of Nyasaland itself and must wait the attainment by Nyasaland of full independence'.
*****
Hivyo, wanaojaribu kutudanganya kwamba Tanzania hatujawahi kulikataa ziwa hili kwa kusema siyo letu wajue kwamba wanaweza kufanikiwa wavivu wa kusoma na uvivu huo wa kusoma usidhaniwe kuwa ni ugonjwa ambao umeshateketeza watanzania wote.
Kwa hiyo, hakuna heado of government wa Tanzania yaani kuanzia Nyerere, Kawawa, Mwinyi, Mkapa aliyewahi kusema tuna asilimia hata moja ya Ziwa Malawi.
Na badala yake hapo juu tumeona Kawawa ndiye mtu pekee aliyesema tuna asilimia ngapi yaani alitamka wazi kwamba hatuna hata tone moja la maji ya ziwa hilo.
Hivyo, ingekuwa ni ajabu kwa Kikwete kujiunga na timu ya wajinga wanaodhani tuna hata asilimia yoyote ya ziwa wakati hansard hizi hasa ile ya JUNE 11, 1962 inaonyesha Kawawa akilitangaza ziwa siyo letu kwa hata tone moja.
Naona Kikwete amechoka kuumbuliwa na ushahidi wa hansard hasa kama ulivyotumika juzijuzi kwenye kesi ya Profesa Costa Mahalu.
Na zaidi ya yote, tusubiri matokeo ya leo kama ambavyo huwa tunakuwa na hamu ya kusburi update za kesi za mahamamani humuhumu JF na tuone ni nani atabadili kauli humu.
Viva ukweli, viva historian, viva wasio na uvuvu wa kusoma.

Reply With Quote
Follow Us Here