Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 30
    1. #1
      mpigauzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th July 2012
      Posts : 276
      Rep Power : 400
      Likes Received
      70
      Likes Given
      174

      Default Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Peter Saramba, Arusha
      MAJAJI watatu wa Mahakama ya Rufaa, Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Masati Septemba 20,mwaka huu watapitia kurasa 990 zenye hoja 42 zilizowasilishwa na aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema kupinga kuvuliwa ubunge.

      Awali katika rufaa yake iliyowasilishwa mahakamani kupinga hukumu ya kumvua ubunge iliyotolewa na Jaji Gabriel Rwakibarila Aprili 5, mwaka huu, Lema kupitia kwa wakili wake, Method Kimomogoro aliwasilisha kitabu cha rufaa chenye kurasa 985 na hoja 18 zinazoeleza kwanini anapinga hukumu hiyo, kabla ya kuongeza kitabu kingine cha kurasa tano na hoja za ziada 24 Julai 3, mwaka huu.

      Pamoja na kubeba kumbukumbu zote za mwenendo wa shauri namba 13/2010 na vielelezo vyote vilivyowasilishwa mahakamani na pande zote mbili za wadai na wadaiwa, kitabu hicho cha kurasa 990 pia kimebeba maelezo ya kina na hoja za kuishawishi mahakama ya rufaa kumpa nafuu Lema kwa kutengua hukumu hiyo.

      Kwa mujibu wa kumbukumbu za kimahakama, tayari walalamikaji Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo wamejibu hoja zote za rufaa kupitia kwa mawakili wao Alute Mughwai na Modest Akida.

      Akizungumza kwa njia ya simu jana, Wakili Kimomogoro alithibitisha kukamilisha taratibu zote za kisheria kuhusu rufaa ya mteja wake na kilichosalia ni kusubiri tarehe ya kusikilizwa na uamuzi.

      Kwa mujibu wa hati ya rufaa hiyo, hoja ya kwanza hadi nne zinapinga uamuzi wa Jaji Aloyce Mjulizi aliyesikiliza shauri hilo katika hatua za awali kwa kutupa pingamizi za awali zilizowasilishwa na upande wa utetezi kwenye kesi ya madai namba 13 iliyofunguliwa na wapiga kura watatu waliopinga ushindi wa Lema.

      Miongoni mwahoja hizo ni kuwa wadai, Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo hawakuwa na haki kisheria kufungua shauri hilo kwa sababu hakuna haki yao iliyovunjwa kisheria kama wapiga kura.

      Lema anadai aliyekuwa na haki kisheria kulalamikia kauli na maneno ya kashfa na udhalilishaji anazotuhumiwa kutoa kwenye mikutano yake ya kampeni ni aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Batilda Burian ambaye pamoja na kutajwa na mashahidi wote wa wadai, hakufika mahakamani kuthibitisha madai hayo licha ya umuhimu wa ushahidi wake.

      Serikali katika shauri hilo liliwakilishwa na wakili wa serikali, Timon Vitalis na Juma Masanja waliodai aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Batilda Burian ndiye alikuwa na haki kisheria kulalamikia ushindi na maneno ya kashfa yanayodaiwa kutolewa dhidi yake na Lema hoja ambayo Jaji Rwakibarila alitupilia mbali katika hukumu yake iliyozua mjadala baada ya kudaiwa kuvuja kabla ya kusomwa.

      Hoja ya tano hadi 18 zinapinga hukumu ya Jaji Rwakibarila ambapo katika suala la hukumu yake kukosa hadhi kisheria, wakili Kimomogoro anadai hakutolea maamuzi athari za wadai kushindwa kuwasilisha mahakamani CD zinazomwonyesha Lema akitoa maneno ya kashfa na udhalilishaji walizodai kuwa nazo katika hati yao ya madai.

      Kimomogoro anadai Jaji alikosea kwa kutotumia hata kesi moja kama rejea kati ya kesi kadhaa zilizotajwa na mawakili wa pande zote mbili za wadai na wadaiwa.

      Jaji Rwakibarila ambaye ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga pia anadaiwa kukosea kisheria kwa kukubali na kuegemea ushahidi wa mdomo pekee katika hukumu yake bila kuwepo ushahidi wa mazingira, Video wala maandishi kuunga mkono ushahidi wa mdomo.

      Mrufani pia anadai Jaji alikosea kwa kutumia viwango na vigezo tofauti kwa mashahidi wa upande wa wadai na utetezi kwa kukataa ushahidi wa Lema na mashahidi wake kwa madai kuwa walikuwa na maslahi kwa sababu ni wanachama na viongozi wa Chadema lakini akaukubali ushahidi wa wadai na mashahidiwao waliothibitika kuwa ni wanachama na viongozi wa CCM kutengua matokea.

      Lakini kwa mujibu wa wakili Kimomogoro, Lema na viongozi wa juu wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe, hoja ya msingi iliyofanya wakate rufaa ni kitendo cha Jaji Rwakibarila kutumia kifungu cha 114 cha sheria za uchaguzi kwa kuagiza taarifa za hukumu hiyo kupelekwa kwa Mkurugenzi wa uchaguzi ikimaanisha Lema hataruhusiwa kupiga wala kupigiwa kura kwa kipindi kisichopungua miaka mitano kinyume na makosa aliyoshtakiwa nayo.

      SOURCE: Mwananhi 20 Aug 2012

    2. Miaka 50

    3. #2
      politiki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Posts : 1,378
      Rep Power : 1342
      Likes Received
      728
      Likes Given
      130

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      hawa majaji wawili siwafahamu lakni huyu Salum Masati ni jaji wa siku nyingi na majaji wa siku nyingi si ajabu akawa na kadi ya CCM mfukoni mwake. Aloyce Mujulizi amekula pesa za ccm huku akitoa hukumu iliyovunja kwama kwa kukataa ushahidi wa viongozi wa chadema kwa sababu wao ni chadema huku akikubali ushahdi wa viongozi wa ccm akiwemo musa mkangaa yaani ni kichekesho
      Hofstede likes this.

    4. #3
      mpigauzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th July 2012
      Posts : 276
      Rep Power : 400
      Likes Received
      70
      Likes Given
      174

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Wakuu hawa Majaji waliosikiliza kesi hii wana walakini. Kama huyu Mujuluzi amechambuliwa vizuri katika ripoti ya Tundundu Lissu.

      JAJI ALOYSIUS MUJULIZI

      Jaji Aloysius Mujulizi alikuwa miongoni mwa watu ishiriniwalioteuliwa Majaji wa Mahakama Kuu mwezi Februari, 2006. Kabla ya uteuzi wake,Jaji Mujulizi alikuwa wakili wa kujitegemea katika kampuni ya mawakili yaIshengoma, Masha, Magai & Mujulizi Advocates (IMMMA) ya Dar es Salaam.Kampuni hii ya mawakili ndiyo iliyoshiriki katika kuanzishwa kwa kampuniiitwayo Deep Green Finance Co. Ltd. mnamo tarehe 18 Machi 2004. IMMMA Advocatesvile vile walikuwa mawakili wa Tangold Ltd.

      Makampuni haya mawili yanatuhumiwa kutumika kupitishiamabilioni ya fedha zilizoibiwa Benki Kuu ya Tanzania kati ya mwaka 2005 na2006. Kwa mfano, katika kipindi kifupi cha miezi minne kati ya Agosti 1 naDesemba 10, 2005 kampuni ya Deep Green Finance ilipokea jumla ya shilingi10,484,005,815.39 kutoka akaunti ya kulipia madeni ya nje (EPA) iliyokuwa BenkiKuu ya Tanzania. Katika kipindi hicho hicho, kampuni ya Tangold Ltd. ililipwadola za Marekani 13,736,628.73 kutoka kwenye akaunti hiyo ya EPA. Nyarakazilizowasilishwa BRELA na mawakili wa IMMMA Advocates na kusainiwa na Gavana waBenki Kuu wa wakati huo Daudi Ballali tarehe 20 Mei 2005 zinaonyesha kwambaTangold Limited ilikuwa kampuni ya kigeni kutoka Jamhuri ya Mauritius. Hayayote yalitokea wakati Jaji Mujulizi akiwa wakili mwenza wa IMMMA Advocates.
      MpendaTz and Kipigi like this.

    5. #4
      Marire's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 2,264
      Rep Power : 966
      Likes Received
      611
      Likes Given
      0

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Hukumu ya lema hata kwa mimi nisiyejua sheria ni komedi mwanzo hadi mwisho,namshauri lema adili na maombi zaidi kwani Mungu ndiye mweza ya yote!

    6. #5
      Kima Mchanga's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Location : Dynamic
      Posts : 4,508
      Rep Power : 11227
      Likes Received
      610
      Likes Given
      446

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Kila la heri kamanda Lema.
      Daudi Mchambuzi likes this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,341
      Rep Power : 872
      Likes Received
      382
      Likes Given
      309

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      watapiga sana chenga ila Mwisho wa siku style zote zitaisha na watamuachia ubunge wake
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    9. #7
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,525
      Rep Power : 1798
      Likes Received
      655
      Likes Given
      0

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Mhimili wa mahakama umeingiliwa na wana siasa,wana kazi kubwasana kuwageuka kwanza na kuwafanya wana siasa wajue wao si ma boss zao kwa kuwaambia nini cha kufanya na wawe huru, wakishamalizana na wana siasa, itabakia kutekeleza sheria kama msumeno ila kwa sasa hakuna lolote, haki itapindishwa tu, angalia Hukumu ya Segerea na Ubungo; Segerea wamebebwa kabisa na Ubungo bado hawamaini kuwa Haki ilitendeka wamekata rufaa wakijua huko mbele watamzima bwana mdogo!

    10. #8
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,632
      Rep Power : 1110
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      756

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Ugumu wa hukumu hii kuwa ya haki upo hapa majaji wote ni wateuliwa wa rais jk ambaye Lema anamtuhumu kuwa ndio chanzo au ana mkono kwenye kuvuliwa ubunge baada ya juhudi za jk kumshawishi lema agombee Arusha kupitia CCM kushindwa (rejea kikao cha Lema na JK huko Oysterbay) Je majaji wataweka weledi mbele au maslahi binafsi mbele??? lets wait and see!!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    11. #9
      Daffi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2011
      Location : Arachuga
      Posts : 2,935
      Rep Power : 987
      Likes Received
      516
      Likes Given
      239

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Watazunguka kote kwa hila ila ukweli wa mambo utabaki palepale kuwa Lema ni mbunge halali wa Arusha mjini!Hata wangerudia uchaguzi mara mia,bado hawataweza badili upepo wa kisiasa hapa Arusha!Lema atabaki kuwa mbunge halali wa Manispaa/jiji la Arusha.

    12. #10
      LiverpoolFC's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2011
      Posts : 6,705
      Rep Power : 11284
      Likes Received
      1483
      Likes Given
      574

      Default

      Hilo liko wazi kwa 100%

      Mi cjui ni kwamba hawajui kusoma hata alama ya nyakati

      Quote By Daffi
      Watazunguka kote kwa hila ila ukweli wa mambo utabaki palepale kuwa Lema ni mbunge halali wa Arusha mjini!Hata wangerudia uchaguzi mara mia,bado hawataweza badili upepo wa kisiasa hapa Arusha!Lema atabaki kuwa mbunge halali wa Manispaa/jiji la Arusha.
      Daudi Mchambuzi and Daffi like this.

    13. #11
      MVUMBUZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th January 2011
      Posts : 2,586
      Rep Power : 1089
      Likes Received
      684
      Likes Given
      374

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Sisi tunamtakia ushindi Lema na tunamwombea Mungu aweze kumshindia

    14. #12
      Hodarism's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 89
      Rep Power : 377
      Likes Received
      13
      Likes Given
      3

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      kwa mahakama hizi na majaji wa JK hakuna jipya

    15. #13
      Daudi Mchambuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 6,196
      Rep Power : 1955
      Likes Received
      3000
      Likes Given
      13644

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      may God bless Godbless Lema.
      only83 likes this.
      "Serikalii hii ni IMPOTENT kuanzia yule wa juu hadi walioko chini" by Dr. Slaa

    16. #14
      Emeka Anyaoku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Posts : 430
      Rep Power : 443
      Likes Received
      134
      Likes Given
      0

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Lema hakika ur alwayz on our mind.

    17. #15
      Chakunyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Location : Masasi
      Posts : 751
      Rep Power : 561
      Likes Received
      134
      Likes Given
      283

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Kila la kheri mh. G Lema.

    18. Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42
      Wataruka sana lakini watatua tu!




      "KAMA HAWATANIRUDISHIA UBUNGE WANGU, DR. SLAA ATAGOMBEA JIMBO LA ARUSHA MJINI" ---Godbless LEMA
      RICARDO KAKA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 26th May 2012
      Posts : 236
      Rep Power : 399
      Likes Received
      72
      Likes Given
      39

      Defaultdata-cfstyle="display:none" id="progress_4464395" style="display:none;visibility:hidden;" data-cfsrc="template/JamiV1/default/misc/progress.gif" alt="" /> Reply With Quote


    19. #17
      Malafyale's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2008
      Posts : 1,151
      Rep Power : 780
      Likes Received
      292
      Likes Given
      22

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Quote By politiki
      hawa majaji wawili siwafahamu lakni huyu Salum Masati ni jaji wa siku nyingi na majaji wa siku nyingi si ajabu akawa na kadi ya CCM mfukoni mwake.
      Politiki,ktk majaji hao 3 aliye makini zaidi ni Jaji Salum Masati!Kumbuka ndiye yeye aliyekubaliana na Mtikila kwenye kesi ya wagombea binafsi kwenye dissident yake kuwa"kwa vile katiba inasema kila mtu ana haki ya kupigiwa kura na kupiga kura kukataa wagombea binafsi ni kuwanyima haki zao za kikatiba za kupigiwa kura"

      Jaji Masati ni jaji makini sana!

    20. #18
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,357
      Rep Power : 18617
      Likes Received
      3520
      Likes Given
      1707

      Default

      Quote By mpigauzi
      Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Peter Saramba, Arusha
      MAJAJI watatu wa Mahakama ya Rufaa, Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Masati Septemba 20,mwaka huu watapitia kurasa 990 zenye hoja 42 zilizowasilishwa na aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema kupinga kuvuliwa ubunge.

      Awali katika rufaa yake iliyowasilishwa mahakamani kupinga hukumu ya kumvua ubunge iliyotolewa na Jaji Gabriel Rwakibarila Aprili 5, mwaka huu, Lema kupitia kwa wakili wake, Method Kimomogoro aliwasilisha kitabu cha rufaa chenye kurasa 985 na hoja 18 zinazoeleza kwanini anapinga hukumu hiyo, kabla ya kuongeza kitabu kingine cha kurasa tano na hoja za ziada 24 Julai 3, mwaka huu.

      Pamoja na kubeba kumbukumbu zote za mwenendo wa shauri namba 13/2010 na vielelezo vyote vilivyowasilishwa mahakamani na pande zote mbili za wadai na wadaiwa, kitabu hicho cha kurasa 990 pia kimebeba maelezo ya kina na hoja za kuishawishi mahakama ya rufaa kumpa nafuu Lema kwa kutengua hukumu hiyo.

      Kwa mujibu wa kumbukumbu za kimahakama, tayari walalamikaji Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo wamejibu hoja zote za rufaa kupitia kwa mawakili wao Alute Mughwai na Modest Akida.

      Akizungumza kwa njia ya simu jana, Wakili Kimomogoro alithibitisha kukamilisha taratibu zote za kisheria kuhusu rufaa ya mteja wake na kilichosalia ni kusubiri tarehe ya kusikilizwa na uamuzi.

      Kwa mujibu wa hati ya rufaa hiyo, hoja ya kwanza hadi nne zinapinga uamuzi wa Jaji Aloyce Mjulizi aliyesikiliza shauri hilo katika hatua za awali kwa kutupa pingamizi za awali zilizowasilishwa na upande wa utetezi kwenye kesi ya madai namba 13 iliyofunguliwa na wapiga kura watatu waliopinga ushindi wa Lema.

      Miongoni mwahoja hizo ni kuwa wadai, Mussa Mkanga, Agnes Mollel na Happy Kivuyo hawakuwa na haki kisheria kufungua shauri hilo kwa sababu hakuna haki yao iliyovunjwa kisheria kama wapiga kura.

      Lema anadai aliyekuwa na haki kisheria kulalamikia kauli na maneno ya kashfa na udhalilishaji anazotuhumiwa kutoa kwenye mikutano yake ya kampeni ni aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Batilda Burian ambaye pamoja na kutajwa na mashahidi wote wa wadai, hakufika mahakamani kuthibitisha madai hayo licha ya umuhimu wa ushahidi wake.

      Serikali katika shauri hilo liliwakilishwa na wakili wa serikali, Timon Vitalis na Juma Masanja waliodai aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Batilda Burian ndiye alikuwa na haki kisheria kulalamikia ushindi na maneno ya kashfa yanayodaiwa kutolewa dhidi yake na Lema hoja ambayo Jaji Rwakibarila alitupilia mbali katika hukumu yake iliyozua mjadala baada ya kudaiwa kuvuja kabla ya kusomwa.

      Hoja ya tano hadi 18 zinapinga hukumu ya Jaji Rwakibarila ambapo katika suala la hukumu yake kukosa hadhi kisheria, wakili Kimomogoro anadai hakutolea maamuzi athari za wadai kushindwa kuwasilisha mahakamani CD zinazomwonyesha Lema akitoa maneno ya kashfa na udhalilishaji walizodai kuwa nazo katika hati yao ya madai.

      Kimomogoro anadai Jaji alikosea kwa kutotumia hata kesi moja kama rejea kati ya kesi kadhaa zilizotajwa na mawakili wa pande zote mbili za wadai na wadaiwa.

      Jaji Rwakibarila ambaye ni Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga pia anadaiwa kukosea kisheria kwa kukubali na kuegemea ushahidi wa mdomo pekee katika hukumu yake bila kuwepo ushahidi wa mazingira, Video wala maandishi kuunga mkono ushahidi wa mdomo.

      Mrufani pia anadai Jaji alikosea kwa kutumia viwango na vigezo tofauti kwa mashahidi wa upande wa wadai na utetezi kwa kukataa ushahidi wa Lema na mashahidi wake kwa madai kuwa walikuwa na maslahi kwa sababu ni wanachama na viongozi wa Chadema lakini akaukubali ushahidi wa wadai na mashahidiwao waliothibitika kuwa ni wanachama na viongozi wa CCM kutengua matokea.

      Lakini kwa mujibu wa wakili Kimomogoro, Lema na viongozi wa juu wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe, hoja ya msingi iliyofanya wakate rufaa ni kitendo cha Jaji Rwakibarila kutumia kifungu cha 114 cha sheria za uchaguzi kwa kuagiza taarifa za hukumu hiyo kupelekwa kwa Mkurugenzi wa uchaguzi ikimaanisha Lema hataruhusiwa kupiga wala kupigiwa kura kwa kipindi kisichopungua miaka mitano kinyume na makosa aliyoshtakiwa nayo.

      SOURCE: Mwananhi 20 Aug 2012
      Hapo kwenye kumpa nafuu bado sijaelewa. Inaonekana kama anaomba hisani na sio kudai haki!

      Na hapo mwisho kwenye red ndio tatizo hasa. Na ilifanywa makusudi!

    21. #19
      Radhia Sweety's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 1,333
      Rep Power : 0
      Likes Received
      640
      Likes Given
      4

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Lema appears to be of more help to his party now working as a non-MP partyman than when he was serving as an MP. In just a few months he's been out the Parliament, for instance, he's managed to raise funds and win new members for his party from places as far as UK and US--and that he certainly couldn't have achieved had he still been an MP. Additionally, nobody will deny the fact his current across-the-country campaign to promote his party's policies and undermine those of CCM has really proved to be so damaging to the goverment well being that JK is said to be contemplating giving him back his post. Instead of him keeping alive the unrealistic dream of winning his appeal against the verdict that blocked him from the assembly, I propose he focus on the task arguably imperative and profitable he is currently embarking on of strengthening the party health at the grassroots level and setting the public against the CCM rulers.

    22. #20
      miti's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th June 2012
      Posts : 111
      Rep Power : 371
      Likes Received
      10
      Likes Given
      16

      Default Re: Lema apinga kuvuliwa ubunge kwa hoja 42

      Lema ni kichwa na tunamkubali sana hata ccm wanamkubali na ndio maana wameamua kumvua ubunge na kumsimamisha asigombee tena zaidi ya hiyo miaka 5. Lema komaa nao ni bora arusha kusiwe na mbunge hata kama ikifika mwaka 2015 kuliko jimbo lichukuliwe na ccm. Poa endelea kuwaburuza hadi haki ipatikane wakizingua tena kata rufaa nyingine .hadi kieleweka.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...