Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

    Report Post
    Results 1 to 10 of 10
    1. #1
      Paparazi Muwazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd December 2007
      Posts : 310
      Rep Power : 648
      Likes Received
      70
      Likes Given
      0

      Default Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Werema alimjibu Mnyika bungeni kuwa bunge halina nafasi katika kushughulikia mgogoro kati ya serikali na walimu kwa kuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kuingilia kazi za muhimili wa serikali.

      Werema aliyasema hayo baada ya Mnyika kudai kwenye mchango wake kuwa kwa kuwa mahakama imehukumu kuwa Serikali na walimu warejee katika majadiliano kwa kuwashirikisha wataalamu wa masuala ya kazi, ni muhimu wataalamu hao wateuliwe na bunge au kamati husika ya kudumu ya Bunge.

      Mnyika alisema ni lazima chombo cha tatu kiingilie kati kwa kuwa tayari walimu na serikali walishashindwa kukubaliana katika hatua ya usuluhishi na kudai kuwa chombo hicho kwa mujibu wa katiba ya nchi ibara ya 63 ni bunge ambalo ndilo lenye mamlaka ya kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi.

      Mnyika alidai kuwa suluhisho la mgogoro huo na Serikali baada ya kupanua wigo wa mapato kufuatia marekebisho ya muswada wa sheria ya fedha iwasilishe bungeni bajeti ya nyongeza yenye kuweka vipaumbele katika masuala ya msingi ya taifa.

      Mnyika alidai kuwa chanzo cha mgogoro huo ni bajeti finyu ya serikali na chombo chenye kupitisha bajeti ni bunge hivyo linapaswa kuingilia kati hoja ambayo ilipingwa na Werema kwa madai kuwa mgogoro huo unaohusu walimu na serikali na kwamba mahakama imeshaamua warejee kwenye majadiliano hivyo bunge kuingilia kati ni kuvunja katiba ya nchi na kuingilia mihimili mingine ya dola.

      Kwa upande mwingine, Werema alimkosoa Mnyika kuwa mahakama haikusema kwamba serikali imevunja katiba. Werema aliyasema hayo wakati akijibu madai ya Mnyika aliyoyatoa bungeni kuwa katika kipindi cha mgomo wa walimu wapo viongozi na watendaji wa serikali waliokiuka ibara ya 4 na 107 A za katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliyoapa kuilinda na kuhoji hatua ambazo zimechukuliwa na serikali kufuatia hali hiyo.

      Aidha Jaji Werema amekemea tabia ya wanasiasa kuwapotosha wafanyakazi na kuwataka pia wasifanye mikutano nao.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Zipuwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Posts : 2,197
      Rep Power : 869
      Likes Received
      307
      Likes Given
      123

      Default Re: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      Ngoja wanasheria waje !
      Maisha yetu ni mafupi lazima tuyatete kwa namna yeyote ile!

    4. #3
      fundimchundo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd July 2010
      Posts : 70
      Rep Power : 462
      Likes Received
      20
      Likes Given
      70

      Default Re: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      Quote By Kobello
      Acha ushabiki wa kijinga!
      Bunge linaingiaje kwenye huu mzozo? Eleza, usipotoszhe mada.
      This is too low!!!!!
      Bunge ndiyo nafasi (forum) ya Wananchi kupanga na kupitisha mapato na matumizi ya Serikali yao!
      Unakumbuka jinsi Bajeti ya Uchukuzi ilivyokataliwa mwaka jana ikabidi Serikali ijipange upya?
      The same could have been done juu ya bajeti ya ELIMU.
      Tatizo kubwa ni kwamba Wabunge hawaathiriwi na migomo ya Walimu kwa kuwa watoto wao hawasomi shule zilizo chini ya Serikali wanayoisimamia!
      Tatizo hili lingekuwa linawagusa, moto ungewaka Bungeni.
      Talk of Wabunge na uzalendo!

    5. #4
      TEMILUGODA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2012
      Posts : 954
      Rep Power : 557
      Likes Received
      134
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By mkigoma
      huwezi kumlinganisha kipanya(mnyika) na tembo (werema) uwezo wa kuchambua sheria, werema ni masters na mnyika form six, werema yupo sahihi.
      huo ndio weledi wako!

    6. #5
      Tuyuku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 658
      Rep Power : 559
      Likes Received
      139
      Likes Given
      16

      Default Re: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      kuna chombo kilichoundwa kisheria CMA ndicho kinachosuluhisha migogoro ya wafanyakazi, walimu wakiwemo. Chombo hicho kikishindwa, kama ni mgogoro wa maslahi wafanyakazi wanapewa haki ya kugoma kwa kufuata utara tibu uliowekwa kisheria. Kama ni mgogoro wa haki, CMA inatoa uamuzi ambao rufaa yake hupelekwa mahakama kuu divisheni ya kazi. Upand ucporidhika inakwenda mahakama ya rufaa.

      Kwa msingi huu Werema yupo sahihi. Bunge ndo lililoutengeza utaratibu huo.

    7. Miaka 50

    8. #6
      MARCKO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th June 2011
      Posts : 1,412
      Rep Power : 684
      Likes Received
      153
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Kobello
      Acha ushabiki wa kijinga!
      Bunge linaingiaje kwenye huu mzozo? Eleza, usipotoszhe mada.


      Wewe bado hujaisoma ccm vyema ndio maana unamwambia aache ushabiki.

    9. #7
      msnajo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 665
      Rep Power : 555
      Likes Received
      75
      Likes Given
      92

      Default

      Quote By fundimchundo
      This is too low!!!!!
      Bunge ndiyo nafasi (forum) ya Wananchi kupanga na kupitisha mapato na matumizi ya Serikali yao!
      Unakumbuka jinsi Bajeti ya Uchukuzi ilivyokataliwa mwaka jana ikabidi Serikali ijipange upya?
      The same could have been done juu ya bajeti ya ELIMU.
      Tatizo kubwa ni kwamba Wabunge hawaathiriwi na migomo ya Walimu kwa kuwa watoto wao hawasomi shule zilizo chini ya Serikali wanayoisimamia!
      Tatizo hili lingekuwa linawagusa, moto ungewaka Bungeni.
      Talk of Wabunge na uzalendo!
      This gave you credibility. I like the way you hit the point. If our government is not part of the problem, automatically it cant be part of the solution!!
      fundimchundo likes this.

    10. #8
      LE GAGNANT's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 1,228
      Rep Power : 709
      Likes Received
      222
      Likes Given
      184

      Default Re: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      Tatizo huu muhimili wa mahakama unatumiwa kisiasa. Serikali ikiona kuna jambo imelishindwa inatumia mahakama kujilinda, kukandamiza haki na kukomoa wale inaowaona ni maadui zake.
      SI VYOTE VING'AAVYO NI DHAHABU

    11. #9
      Aristides Pastory's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2012
      Posts : 347
      Rep Power : 437
      Likes Received
      58
      Likes Given
      0

      Default Re: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      ....WEREMA mawazo yake dhaifu...

      ....MH.MNYIKA mawazo yake ni ya Kizalendo na Kishujaa zaidi...

    12. #10
      Naytsory's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 724
      Rep Power : 759
      Likes Received
      127
      Likes Given
      2

      Default Re: Mnyika Vs Werema: Nani yuko sahihi kuhusu mgogoro wa Serikali na Walimu?

      Ninyi mnaoitetea Serikali katika mgogoro wa walimu mmekosa uzalendo kwa watoto wa Watanzania na Taifa kwa ujumla, wanaf. Mashuleni hawafundishwi kama inavyotakiwa na hata wanaofaulu kwenda sekondari hawajui kkk, halafu kuna mijitu inashabikia na kushangilia kama mazuzu hatua zilizochukuliwa na serikali ambayo haijatoa suluhu kwa mgogoro huu ambao utaendelea kuwaumiza watoto wetu. Au kwa kuwa watoto wako shule za English medium na nje ya nchi?

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...