Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

    Report Post
    Page 1 of 8 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 154
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7367
      Likes Received
      6152
      Likes Given
      22273

      Default PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Wanabodi,

      Kila nipatapo fursa, sipendi kabisa kukosa kipindi cha Maswali na Majibu ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo, Kayanza, Peter Pinda, ile leo nilikikosa kipindi hiki.

      Lakini kupitia taarifa za habari, nimemsikia Mhe. Pinda, akisema kuwa ni jukumu la wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuhakikisha CCM inashinda chaguzi zote ili CCM iendelee kutawala milele!.

      Naombeni wajuzi wa masuala ya utawala, mnirekebishe if I'm wrong!, Kuanzia kwa rais JK na wanasiasa wengine wote ambao japo wamechaguliwa kwa tiketi za vyama, ukishakuwa mtumishi wa umma, paid by taxpayers money, jukumu lako kuu sasa ni kuutumikia umma na sio chama chako!.

      Hii inamaanisha rais JK, japo ameshinda kwa tiketi ya CCM, na anaongoza serikali ya Tanzania, na wakati huo huo yeye ndiye Mwenyekiti wa CCM, amechaguliwa kuiongoza Tanzania na Watanzania na sio na wana CCM, hivyo anaongoza serikali ya Tanzania kwa niaba ya Watanzania na kwa manufaa ya Watanzania wote, na sio kwa manufaa ya wana CCM!. (Of the people, by the people and for the people).

      JK ndiye rais wa Chadema, ndiye rais wa CUF na ndiye rais wa wasio na vyama kama sisi!. Yeye ndiye rais wa Dr. Slaa, yeye ndiye rais wa Prof. Lipumba, yeye ndiye rais wetu sisi wote kama Watanzania, ni rais wa waliomchagua na pia rais wa wasiomchagua, anatakiwa kufanya kazi kwa kutanguliza maslahi ya taifa mbele na sio maslahi ya chama chake cha CCM!.

      Kauli ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda bungeni leo kuwa Wakuu wa wilaya na mikoa, wako pale kuhakikishe CCM inashinda chaguzi zote ili itawale milele, haiwezi kupita bila kupingwa!. Hi inamaanisha kuwa viongozi hawa, wako kwa ajili ya kuilinda na kuitetea status quo ya CCM ili iendelee kutawala milele!. This is very wrong kwa tafsiri sahihi ya Public Servants!. Kwa kauli hii ya Pinda, it goes without saying kuwa wakuu wa majeshi yetu, Polisi wetu, mahakama zetu na wakuu na vyombo vya dola, na vyombo vya kiserikali, wanateuliwa ili wahakikishe CCM haishindwi na inaendelea kutawala milele!.

      Public Servant, ni mtumishi wa umma, ma RC na ma DC ni viongozi wa serikali, kwa maana hiyo ni viongozi wa umma, na watatimiza majukumu yao kwa maslahi ya umma na sio kwa maslahi ya CCM. Ndio maana Mhe. Tundu lissu aliwakataa hawa wasihusishwe ile tume ya katiba na juzi akasisitizwa hawapaswi kuwamo bungeni!.

      Hata wabunge wa kuchaguliwa, ni watumishi wa umma, japo wanateuliwa kwa tiketi za vyama vya siasa, wanachaguliwa na wananchi na sio na vyama vyao, hivyo wakishashinda ubunge, wanakuwa ni watumishi wa watu na sio watumishi wa vyama vyao, hivyo wanapaswa kutekeleza majukumu yao ya kibunge kwa maslahi ya wananchi na sio kwa maslahi ya vyama vyao!. Kama ni kweli, majukumu ya ma RC na ma DC ni kuhakikisha CCM haishindwi, hii ina maana kubwa zaidi katika mustakabali wa mabadiliko halali ya serikali!.

      Binafsi yangu, nimesikitishwa na kauli hiyo, and to be honest, nilikuwa na very high hopes kuhusu Pinda, lakini sasa nimeamini, he is good for nothing!, a very disapointing PM!. Kwa vile CCM ni chama tawala, hivyo public servants wana jukumu la kuhakikisha CCM inashinda na kutawala milele!.

      Hii inamaanisha hata kama 2015, Watanzania wataamua kuivote out CCM kupitia njia halali ya ballot box, hao public servanys wenye jukumu la kuitumia serikali mpya ya chama kitakachoshinda, wako kwenye mind set ya kuhakikisha lazima CCM inashinda, na jee ikitokea CCM ikashindwa, jee watakabidhi madaraka kwa mshindi halali?!, jee majukumu yao yatabadilika or what does Pinda exactly meant?!.

      Kusema ukweli, civic education kuhusu multipartism, inatakiwa kuanzia juu ndipo ishuke chini kwa wananchi wa kawaida!.

      Sasa ndio nimeanza kuelewa, no wonder kwa nini jina la Pinda, halitajwi kabisa kabisa katika presidential materials!. Maliza tuu term yako kwa amani, ukaiendeleza ile kampuni yako ya P & P, nami nitakutangazia sana ile asali yako, ila nakuomba Tanzania yetu utuachie kwa amani, hii sio Tanzania ya CCM, CHADEMA au CUF!. Tanzania ni ya Watanzania wote.

      Kiukweli, mabadiliko yakija, hizi nafasi za ma DC na ma RC ndizo ziwe za kwanza kufutiliwa mbali!.

      Very Disapointed!.

      Pasco.

      NB. Pasco wa jf, ni Mtanzania wa kawaida ambaye sio mwanachama, mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa!. Ni mshabiki wa Utanzania kwa maslahi ya Taifa mbele!.

      Last edited by Pasco; 17th August 2012 at 12:17.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Papizo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Location : What for??
      Posts : 3,296
      Rep Power : 1233
      Likes Received
      400
      Likes Given
      2244

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Huyu mzee sijui hata kwa nini alipewaa uwaziri maana saa zingine namuona kama hajui nini anafanya maana mambo yake tu anaoneken mfata upepo kutoka mjengoni....
      Pasco likes this.

    4. #3
      Informer's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 29th July 2012
      Posts : 232
      Rep Power : 502
      Likes Received
      354
      Likes Given
      67

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Pasco kakangu,

      Unajua fika kuwa watumishi wengi serikalini wanafanyishwa kazi kwa mtindo huu.

      Kwangu sishangai, na bado tunajigamba tuna demokrasia. Kauli hii wengi mliitarajia toka kwa Nape au Mukama, sasa ndio mjue tuna ombwe la uongozi kama taifa.
      Pasco, muchetz and mmbangifingi like this.

    5. #4
      kibogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Location : MBEYA
      Posts : 1,682
      Rep Power : 693
      Likes Received
      419
      Likes Given
      312

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      MKP Ameisha fikia ukomo wa kufikiria hawezi kuwa na jipya
      Pasco likes this.

    6. #5
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,087
      Rep Power : 41562
      Likes Received
      5986
      Likes Given
      1052

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Tulisema hapa tangu anaapishwa, kwamba huyu jamaa bomu, watu wakaona tunaendekeza tahariri.

      Sasa mnaona.

      Na zaidi ya Pinda, tatizo ni system iliyomlea Pinda, maana huyu ni graduate wa UDSM aliyefanya kazi Usalama miaka mingi, akakaa kwenye corridors of power Ikulu huko, akagombea ubunge akapata, akapewa u PM.

      Sasa inaonekana institutions zetu zote hizi hazijaweza kumuandaa vizuri kwa kazi hii.

      Kuanzia elimu ya chini mpaka ya juu shahada ya sheria, usalama, Ikulu, bungeni, uwaziri, mpaka uzoefu wa miaka yote hiyo aliyokuwa PM, bado anacheza makidamakida mpaka leo.

      Pathetic.
      Pasco, Nyamizi, Nyunyu and 7 others like this.
      Banda lishavunjika, jogoo kaondoka. Vifaranga hangaika, kumtoa nyoka.


    7. Miaka 50

    8. FJM
      #6
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,168
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5318
      Likes Given
      4585

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Kwa maana hiyo wakuu wa mikoa na wilaya wanatumikia chama cha siasa (CCM). Mashangingi, mishahara na posho zao zinatoka kwenye CCM au hazina?

      NB: From now on, wakuu wa mikoa na wilaya ni fair game, si viongozi wa serikali tena bali ni makada wa chama cha siasa. Hivyo, wananchi wana haki ya kuwasikiliza/kuwapuuza kama wanavyofanya kwa wana-CCM wengine i.e Nape & co. Naona giza!
      Jasusi and Pasco like this.

    9. #7
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,144
      Rep Power : 21610
      Likes Received
      13477
      Likes Given
      17780

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      CCM wana viongozi aina kadhaa wa kadhaa

      1,kuna wezi ambao ni wachapakazi kidogo

      2.wezi wazembe

      3.wachapakazi but uwezo mdogo


      sasa Pinda ndo group la mwisho
      na wanaonekana better kulinganisha na wengine
      Pasco, Nyamizi, Nyunyu and 5 others like this.
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    10. #8
      Bitabo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2011
      Posts : 1,375
      Rep Power : 661
      Likes Received
      447
      Likes Given
      261

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Mkuu Pasco
      Mh Pinda yuko sahihi kwa mfumo wa nchi yetu maana tumerithi ule wa chama kimoja.
      Ukiangalia kwa ukaribu, RC na DC ni baadhi ya wajumbe wakuu wa CCM kwenye maeneo yao ya kazi. lakini huwezi kuona wanakuwa wajumbe wa vikao vya opposition parties.
      Na hii ndo kazi yao kubwa honestly. Ameongea ukweli japo ni mchungu but in reality kama uko mikoani, utaona ndo ukweli.

      RC na DC hawatakiwi tena kwenye katiba mpya. Tunahitaji RAS na DAS na DED tu. Ukiingia kwa undani, hata DAS hana kazi ya muhimu.

      Pinda amewafungua masikio watu wengi na itasaidia kwenye maoni ya katiba watu kulijadili jambo hili.

      pole for being dissapointed Pasco, ila huo ndo ukweli. kama huamini toka da uje uishi kwenye mikoa mingine. Utauona huu upuuzi kwa uwazi kabisa
      Uovu wa siku moja, unaondoa wema wa MWAKA MZIMA

    11. #9
      Informer's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 29th July 2012
      Posts : 232
      Rep Power : 502
      Likes Received
      354
      Likes Given
      67

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      FJM,

      Wapinzani wanatakiwa ku-capitalize katika hili. Hutuhitaji wakuu wa Mikoa/Wilaya. Binafsi sioni umuhimu wa watu hawa zaidi ya kuliingiza taiga ktk gharama zisizo na kichwa wala miguu.
      Pasco, FJM and Mzalendo JR like this.

    12. #10
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Pasco, mkuu wangu hivi kweli wewe ulitegemea vinginevyo? Si afadhali huyu mtoto wa mkulima Mizengo Kayanza Peter Pinda kaweka wazi mjue kabisa kwamba mfumo uliopo ndio umetufikisha hapa tulipo na ndivyo itakavyokuwa hivyo jiandaeni..

      Mh. Pinda anaweza kabisa kusema uongo wowote kuwapaka mafuta, lakini ukweli unabakia kuwa kipenzi cha Mungu. Pinda kasema wazi nini wanakitaka hivyo ni kujumu la vyama vya upinzani kuzipata salaam hizo. Politically anaweza kuwa wrong lakini ndivyo inavyokuwa..Tujifunze mara ngapi mkuu wangu.
      Pasco, Nyunyu and muchetz like this.
      Exploration of reality

    13. #11
      kelvito's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th May 2012
      Posts : 388
      Rep Power : 521
      Likes Received
      97
      Likes Given
      74

      Default

      Sikumbuki ni lini nilikubaliana na pinda kwa lolote!
      Pasco, REMSA and Original like this.

    14. FJM
      #12
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,168
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5318
      Likes Given
      4585

      Default re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Quote By Informer

      Wapinzani wanatakiwa ku-capitalize katika hili. Hutuhitaji wakuu wa Mikoa/Wilaya. Binafsi sioni umuhimu wa watu hawa zaidi ya kuliingiza taiga ktk gharama zisizo na kichwa wala miguu.
      Sidhani kama PM anaelewa madhara ya hiyo kauli yake kwa CCM. Kwa bahati mbaya sana, viongozi wengi serikalini na hata ndani ya ccm wako nyuma sana. Sintofahamu inayoondelea ni kwa sababu wananchi wamepiga hatua lakini wakubwa wanazidi kucheza zilipendwa. Viongozi wanaonekana kufanya mambo ya aibu sana na unaposikia kauli kama hii ya Pinda you have to ask yourself kama alikuwa holiday sayari nyingine ambayo hakupata mawasaliano toka Tanzania au the 'dear leader' is simply out of it?
      Pasco and muchetz like this.

    15. FJM
      #13
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,168
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5318
      Likes Given
      4585

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Quote By Bitabo

      Mh Pinda yuko sahihi kwa mfumo wa nchi yetu maana tumerithi ule wa chama kimoja.
      Ukiangalia kwa ukaribu, RC na DC ni baadhi ya wajumbe wakuu wa CCM kwenye maeneo yao ya kazi. lakini huwezi kuona wanakuwa wajumbe wa vikao vya opposition parties.
      Na hii ndo kazi yao kubwa honestly. Ameongea ukweli japo ni mchungu but in reality kama uko mikoani, utaona ndo ukweli.

      RC na DC hawatakiwi tena kwenye katiba mpya. Tunahitaji RAS na DAS na DED tu. Ukiingia kwa undani, hata DAS hana kazi ya muhimu.

      Pinda amewafungua masikio watu wengi na itasaidia kwenye maoni ya katiba watu kulijadili jambo hili.

      Bitabo, hapa ndipo watu wanaona dhulma na matumizi mabaya ya kodi za walalahoi. Kwa miaka yote ishirini tangu mfumo wa vyama vingi viingie, tumeendelea kugharamia makada wa propaganda. Sasa hivi tuna wakuu wa wilaya 130 na ushee, wakuu wa mikoa 27 hapo kila mtu ana shangingi, anapata allowance kila kukicha. Tunapata faida gani?

      Huu uvundo ni wa kusafisha kwenye hii katiba mpya, but for now they should be treated kama makada wengine wa CCM!
      Pasco likes this.

    16. #14
      Original's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2012
      Posts : 324
      Rep Power : 426
      Likes Received
      66
      Likes Given
      265

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Kwa kauli ya Pinda ina maana kwamba kuanzia usalama wa taifa, polisi, jeshi, mahakama vipo kuhukikisha ccm inatawala milele huku wakitumia pesa ya watanzania?, huo ni upumbavu uliopita kiasi.
      Jasusi, Pasco and chiborie like this.

    17. #15
      Al Adawi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th February 2011
      Posts : 46
      Rep Power : 426
      Likes Received
      13
      Likes Given
      63

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Quote By Mkandara
      Pasco, mkuu wangu hivi kweli wewe ulitegemea vinginevyo? Si afadhali huyu mtoto wa mkulima Mizengo Kayanza Peter Pinda kaweka wazi mjue kabisa kwamba mfumo uliopo ndio umetufikisha hapa tulipo na ndivyo itakavyokuwa hivyo jiandaeni..

      Mh. Pinda anaweza kabisa kusema uongo wowote kuwapaka mafuta, lakini ukweli unabakia kuwa kipenzi cha Mungu. Pinda kasema wazi nini wanakitaka hivyo ni kujumu la vyama vya upinzani kuzipata salaam hizo. Politically anaweza kuwa wrong lakini ndivyo inavyokuwa..Tujifunze mara ngapi mkuu wangu.
      Kiongozi Mkandara,
      Unafahamu hata yule Jemadari Jacki Zoka anahudhuria vikao vya juu vya CCM? Unaiona hatari ya kuwa kama alivyosema Mkuu Pasco kuwa wenye Nchi siku wakiamua kuipiga chini CCM, basi uwezekano ni mkubwa yakawa yale ya Kibaki na Wakenya,2008. Safari ni ndefu bado.
      Last edited by Al Adawi; 21st August 2012 at 18:17.
      Mkandara, Peasant, Pasco and 2 others like this.

      "It's dangerous to be Sincere, unless you are also stupid. "

    18. #16
      Escobar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th September 2011
      Posts : 330
      Rep Power : 454
      Likes Received
      201
      Likes Given
      146

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Nishaona dalili za kupasuana hapa! Kama wakuu wa mikoa na wilaya watapewa nafasi ya kupiga kampeni huku wengine wananyimwa vibali vya kukusanyika itakuwa ni sababu tosha ya amani kuanza kutoweka! Am worried
      Pasco, Manager and chiborie like this.
      The only white man you can trust is a dead white man, "ROBERT MUGABE"


    19. #17
      MAMMAMIA's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 25th February 2008
      Location : Near You
      Posts : 3,794
      Rep Power : 3256
      Likes Received
      1496
      Likes Given
      1206

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Watu husema, ukitaka kumuua mwendawazimu (unaweza kumuita silly, mzembe, dhaifu), usinyanyue mkono wako bali mpe kitanzi atajimaliza mwenyewe. Kamanda Lissu amempa kitanzi Pinda amejimaliza mwenyewe, ni suala la muda tu.

      Kwa kauli hiyo, ni kuwa zile ahadi zaviongozi wetu kuwa "nitawatumikia Watanzania bila ubaguzi" inakuwa ni uongo ndani ya kiapo kitakatifu. Ikiwa wakuu wa wilaya na mikoa, jeshi, polisi, mahakama (wote kama watumishi wa umma) wapo kwa ajili ya kuhakikisha kuwa CCM inashinda Liwalo naliwe, na mbaya zaidi wapo hapo walipo kwa mishahara na marupurupu ya jasho la Watanzania, hii ni dhuluma na wizi wa mchana. Nani atakayekuwa na imani tena na watumishi wa umma, akiwemo yeye Pinda? IKO HAJA YA KUREJESHA KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NA WAZIRI MKUU HUYU.

      Ninachosema, kwa ithibati ya maneno ya Pinda (anayepindisha haki ya Watanzania kuwa dhuluma kwa Watanzania), CCM imezidi kukosa uhalali wa kuiongoza Tanzania.
      Pasco, ral and KIJOME like this.
      "JF - SAUTI YA WASIO NA SAUTI ............ na wapayukaji"

    20. #18
      bullet's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2009
      Location : East London
      Posts : 365
      Rep Power : 563
      Likes Received
      116
      Likes Given
      129

      Default

      Quote By Escobar
      Nishaona dalili za kupasuana hapa! Kama wakuu wa mikoa na wilaya watapewa nafasi ya kupiga kampeni huku wengine wananyimwa vibali vya kukusanyika itakuwa ni sababu tosha ya amani kuanza kutoweka! Am worried
      Hivi hawa ma RC na DC si ndio Anna Kilalgo aliwatetea kuwa wawemo katika uratibu wa katiba mpya? Fikiria sasa ni upendeleo kiasi gani kwa CCM watakao uonyesha! Vyeo hivi vifutwe kabisa ndani ya katiba
      Pasco and chiborie like this.

    21. #19
      Nyenyere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 1,864
      Rep Power : 0
      Likes Received
      485
      Likes Given
      689

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Mkuu Pasco you have a point. Mimi mchango wangu ni mfupi tu. Vipi kuhusu ukweli kwamba makamanda wa JWTZ nao huteuliwa kuwa ma-RC na DC? Kumbe jeshi pia hutumika kisiasa?
      Pasco likes this.

    22. #20
      Magesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2012
      Posts : 1,172
      Rep Power : 1003
      Likes Received
      264
      Likes Given
      1

      Default Re: PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!

      Serikali imechoka
      Pasco likes this.

    Page 1 of 8 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...