Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

    Report Post
    Page 7 of 9 FirstFirst ... 56789 LastLast
    Results 121 to 140 of 175
    1. #1
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,422
      Rep Power : 10874
      Likes Received
      3801
      Likes Given
      426

      Post Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Kiongozi wa upinzani nchini ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amefanyiwa hujuma kubwa mkoani Morogoro kwa kufukuzwa chumba cha kulala wageni ndani ya chuo cha ufundi VETA, Mikumi Kilosa.

      Kiongozi huyo ambaye alikabidhiwa chumba hicho na viongozi wa CHADEMA kikiwa kimelipiwa kila kitu na akaingia lakini ghafla akaja Meneja wa hoteli hiyo Jacob Sumary na kumtaka Kiongozi huyo wa upinzani nchini kuondoka mara moja kwenye hoteli hiyo kwa sababu tayari ilishalipiwa na mtu mwingine.

      Kwa ustaarabu mkubwa na kutokutaka mabishano Dr Slaa aliondoka.

      Pia katika hatua nyingine umeme ulizimwa mji mzima wa Mikumi jana kuanzia asubuhi hadi usiku katika kile kilichoonekana ni hujuma ya Tanesco ili Dr Slaa ashindwe kuhutubia,hata hivyo mbali na kukosekana umeme mikutano ya Dr Slaa ilifurika umati mkubwa wa watu huku kiongozi huyo akiwaambia maelfu ya watu atawahutubia hata bila vipaza sauti.

      Vitendo hivyo vya kihuni alivyofanyiwa Dr Slaa viliwachukiza wananchi wengi wa Mikumi na kusema watalipa kisasi kwa kuindoa CCM madarakani kupitia sanduku la kura.

      Source: Nipashe/Mwananchi




    2. FemaTV & Radio

    3. #121
      Wayne's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2009
      Posts : 448
      Rep Power : 598
      Likes Received
      78
      Likes Given
      20

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By MKUU ROMBO
      Aiseeee baba yangu hayo ni majaribu tu hata Yesu alijaribiwa cha msingi Dr Slaa songa mbele tu sisi tupo nyuma yako
      Mkulu

      Hapana...tupo bega kwa bega
      ALL TEMPTATIONS ARE FOUND EITHER IN HOPE OR FEAR

    4. #122
      ZeMarcopolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2008
      Posts : 7,191
      Rep Power : 5038
      Likes Received
      2426
      Likes Given
      2224

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Swali la kizushi: Hivi Slaa alikuwa na mama Junior au peke yake?
      "To greed, all nature is insufficient"

    5. #123
      MR. ABLE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Posts : 1,265
      Rep Power : 612
      Likes Received
      580
      Likes Given
      486

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Msiyashangae haya mambo yanayoratibiwa na kufanywa na CCM dhidi ya CHADEMA au dhidi WANANCHI WANYONGE NA MASIKINI.
      Ni kwamba hali waliyonayo kwa sasa hawa ccm hawafai hata kufuga bali ni kuwasaka kokote walipo na kuwaangamiza kabisa. cheki evolution yao;

      TUSHIRIKIANE KWAPAMOJA WAPENDA MABADILIKO NA WANACHADEMA KWA UJUMLA KUMUANGAMIZA HUYU MNYAMA MBAYA KABISA CCM IFIKAPAO 2015.

      Pipooooooooooooooooooooooooooo ooooooooz?????????????????????

    6. #124
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,606
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2866

      Default Dk. Slaa afanyiwa ‘umafya’



      Meneja wa hoteli amnyang�anya chumba
      Umeme wakatika, Tanesco wakana hujuma

      Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa, amefukuzwa katika nyumba ya kulala wageni ndani ya Chuo cha Ufundi Stadi (Veta) Mikumi, Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni sababu za kisiasa ikiambatana na kuzimwa kwa umeme kwa mji mzima kwa saa zaidi ya 12 ili kudhibiti mikutano yake ya hadhara anayoifanya.

      Dk. Slaa ambaye aliwasili majira ya saa 8.00 mchana mjini Mikumi akitokea tarafa ya Malinyi, wilayani Ulanga, Morogoro, katika Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) ikiwa ni mwendelezo wa Operesheni Sangara, alifikwa na udhalilishaji huo baada kuonyeshwa chumba chake lakini baadaye akanyang’anywa.

      Baada ya kuwasili hotelini hapo, Dk. Slaa alikabidhiwa funguo ya sehemu ya kufikia kutoka kwa Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare, na kuingia chumbani, muda mfupi baada ya kuingia katika chumba hicho alitokea meneja wa hoteli hiyo, Jacob Sumary, na kumueleza kuwa sehemu hiyo imeshawekewa ‘oda’ na wateja wengine na hivyo kutakiwa kuondoka katika eneo hilo mara moja.

      Hata hivyo, Dk. Slaa alihoji sababu za mmoja wa walimu wa Veta kuacha majukumu yake na kujipa jukumu la kuhudumia hoteli kwa kumhudumia eneo lenye vyumba vitatu lenye thamani ya Sh. 75,000 kwa kila chumba kimoja Sh. 25,000.

      Meneja huyo alishikilia kumtaka Dk. Slaa aondeke hotelini hapo kwa kuwa yeye hakuwa na taarifa za ujio wake. Dk. Slaa alitii na kuondoka.

      Naye Sumary alipofuatwa na NIPASHE jana kwenye hoteli hiyo kuzungumzia kitendo cha kumnyang’anya Dk. Slaa malazi, alikataa kuzngumzia suala hilo.

      Awali alisikiliza NIPASHE ikimuuliza juu ya hatua alizochukua na kutaka kujua ni kwa nini, lakini alisema hawezi kuzungumzia suala hilo na kukata simu yake.

      Akizungumzia hali hiyo katika mkutano wa hadhara, Dk. Slaa alisema kuna mipango imefanywa kwa nia ya kumdhoofisha katika kampeni za kuwakomboa Watanzania.

      “Kama mimi nafanyiwa mambo hayo kwa suala dogo la malazi tu na serikali ya CCM, je nyinyi wengine mtafanyiwaje? Mnapaswa kujifikiria mara mbili,” alisema Dk. Slaa.

      Ghafla umeme ulizimwa katika mji wa Mikumi hali iliyotafsiriwa kuwa ni muendelezo wa hujuma zinazofanywa dhidi ya Chadema, kwani wananchi walidai mji huo haukuwa na tatizo la umeme.

      “Watanzania wa leo siyo wa jana. Zimeni umeme. Hata mfanye nini tutaendelea na mkutano na wananchi watatusikiliza tu. Lakini nitakula nao sahani moja waliofanya hivi,” alisema Dk. Slaa.

      Hata hivyo, kukatika kwa umeme huo kuliongeza mori kwa wakazi wa Mikumi kutokana na kuongezeka kwa wingi katika mkutano huo na kukemea vitendo vilivyofanywa na serikali dhidi ya Dk. Slaa.

      Akizungumza kwa njia ya simu na NIPASHE, Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Morogoro, Deogratius Ndamugaba, alisema kukatika kwa umeme kulitokana na hitilafu za kawaida na siyo hujuma au msukumo wa kisiasa.

      “Kukatika kwa umeme Mikumi siyo kwa sababu ya Chadema ila ni feeder ya Mikumi iko nje tangu saa 12.45 jioni. Nguzo imeanguka na inapaswa kubadilishwa na sehemu yenyewe ni porini. Kuna giza na Chui,” alisema Ndamugaba.

      Alisema amekuwa akijaribu kuwasiliana na vyombo vya habari ili kuwapa taarifa wananchi wa Mikumi.

      Alisema utendaji kazi wa eneo hilo kwa muda huo ulionekana kuwa mgumu na kwamba, tayari mafundi wa Tanesco walikuwa katika eneo la tukio kufanya marekebisho.

    7. #125
      YAGHAMBA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th August 2012
      Posts : 376
      Rep Power : 417
      Likes Received
      91
      Likes Given
      724

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      kamzushie baba mwana.......
      Quote By ZeMarcopolo
      Swali la kizushi: Hivi Slaa alikuwa na mama Junior au peke yake?

    8. Miaka 50

    9. #126
      Unstoppable's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 940
      Rep Power : 612
      Likes Received
      330
      Likes Given
      2041

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By OTIS
      Kuna jambo watu hawalisemi.
      Kuna sababu tena ya msingi sana.
      uamuzi wa kumfukuza ulikuwa sahihi.
      Tukiweka siasa pembeni; mteja siku zote hafukuzwi; anatafutiwa alternative hata kama ni kosa la mteja, unless kama ameiba.

      Huyu mwenye hotel/guest ame-risk sana business yake kufanya kitu kama hiki (kama ni kweli amesukumwa na siasa). Unaweza kumnyanyasa mtega mmoja lakini akawa na influence ya-kukufanya ukose wateja 100.

      Only in Tanzania mteja sio mfalme. Pamoja na kuwa guest na hotel nyingi bado owner anakuwa na kiburi? Daah! Kaazi ipo.

    10. #127
      Unstoppable's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 940
      Rep Power : 612
      Likes Received
      330
      Likes Given
      2041

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By Sipendi Ubepari
      Hayakuhusu. Nyie mmefanya hila zenu, subirini umma uwahukumu kwa maovu
      Mimi nashangaa kama huyu Slaa sio tishio kwao kwanini wanaangaika naye hivyo? Wamwache tu aongee kwenye hiyo mikutano wananchi wataamua wenyewe. Hizi dalili sio nzuri kwakweli kwa CCM in a long run; it is just a short pleasure.

    11. #128
      Unstoppable's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 940
      Rep Power : 612
      Likes Received
      330
      Likes Given
      2041

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By Ronn M
      Kama inafikia hatua ya kuzimiana umeme, thats too much!
      It's unbelievable kwamba mambo yote muhimu yanasimama kwasababu tu ya ubabe/ushindani wa kisiasa. Sijui priorities zetu watanzania zikoje. Aah! inachosha.

    12. #129
      EmeraldEme's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th March 2012
      Posts : 113
      Rep Power : 385
      Likes Received
      18
      Likes Given
      38

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      What a shame....
      ''If you don't stand for something you will fall for anything" -Malcolm X

    13. #130
      Unstoppable's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 940
      Rep Power : 612
      Likes Received
      330
      Likes Given
      2041

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By Ulukolokwitanga
      Huyo hotel meneja angeonekana wa maana kama angepandisha bei ya chumba ili apate Presidential price. Ndio maana bongo ni vigumu sana kutofautisha meneja wa hotel, mhudumu wa hotel, mhudumu wa bar na meneja wa bar; wote akili zao sawa tu.
      Well said. Ndio maana watu wengi wanapoteza opportunity zaku-make profit/business hivi hivi bila kufikiri. Wakati wengine tukiwa kwenye business tunawaza how to maximize profit; wengine wanawaza kwingine kabisa. Huyu mtu ajue tu kwakumfukuza Slaa hajamkomoa, bali amewasaidia business competitors wake kwakuwapa business ya Slaa & Co. Inawezekana asijali sana kwasababu sio owner wa VETA; na uzalendo wake nao ni zero hivyo haoni pride yoyote VETA ikifanikiwa. Kweli mwenye macho haambiwi tazama!

    14. #131
      Lawrence Luanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th November 2011
      Posts : 604
      Rep Power : 499
      Likes Received
      51
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      wanaogopa moto ila utawaunguza tuuu wakae mkao wa kuungua.

    15. #132
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,422
      Rep Power : 10874
      Likes Received
      3801
      Likes Given
      426

      Default

      Quote By Unstoppable
      Mimi nashangaa kama huyu Slaa sio tishio kwao kwanini wanaangaika naye hivyo? Wamwache tu aongee kwenye hiyo mikutano wananchi wataamua wenyewe. Hizi dalili sio nzuri kwakweli kwa CCM in a long run; it is just a short pleasure.
      Kwa kweli hiki kitendo walichofanya CCM kimewadhalilisha sana.

    16. #133
      Indume Yene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Chumbani
      Posts : 2,144
      Rep Power : 4952
      Likes Received
      332
      Likes Given
      310

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Yaani kweli viongozi wa Tanzania hawako responsible. Inawezekanaje kutesa raia wengine kuwakosesha huduma ya umeme kwa ajili ya kumkomoa mtu mmoja Dr. Slaa?? Grrrhh.....Sioni kama wamemkoa Slaa hapo, kama ni kulala si angeweza kujiegesha kwenye kiti chake ndani ya gari yake!!!

      Hii inaonyesha watu waliopewa dhamana ya uongozi hawako ethical. Hasira za wananchi zaweza kuwasulubu kama hawatakuwa makini na majukumu yao.
      makundi4619 likes this.

    17. #134
      Man 4 M4C's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd August 2012
      Posts : 464
      Rep Power : 826
      Likes Received
      64
      Likes Given
      15

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Hakika mambo haya yanaumiza sana,ila Mungu alimpa Mfalme Daudi nguvu hata akampiga Farao kwa jiwe na Kombeo. Ipo siku ccm watashangaa,wananchi wanaona! Wameona msitu wa mabwepande,vifo vya watu mbalimbali,manyanyaso ya walimu na madaktari,na wafanyakazi. Mungu atawasimamia wote wanaopigania haki. Mtawaliwa wa leo ndiye mtawala wa kesho.

    18. #135
      makundi4619's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2012
      Posts : 485
      Rep Power : 443
      Likes Received
      135
      Likes Given
      388

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Vitendo kama hivi vinazidi kukipa umaarufu CHDEMA na kukidhoofisha CCM bila kujua. Aliye nyuma ya mpango kama huu hana uwezo mkubwa wa kufikiri

    19. #136
      makundi4619's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2012
      Posts : 485
      Rep Power : 443
      Likes Received
      135
      Likes Given
      388

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By only83
      Huyo meneja anapaswa kushikwa jina na sura yake...baada ya ukombozi 2015 atashughulikiwa kulinga na matendo yake.
      Hakuna sababu ya kuwa na visasi kwa wapuuzi kama hawa wenye akili za kitoto. Kutakuwa na mambo mengi mno ya kimsingi ya kushughulikia. CCM ikiondoka madarakani ni kama ndiyo taifa limepata uhuru kwanza kwa maana ya kujipanga upya karibu katika kila sekta. Hebu angalia sheria, utumishi wa umma, polisi, usalama wa taifa, elimu, afya, maji, kilimo, nishati, miundombinu, nk shida tupu

    20. #137
      makundi4619's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2012
      Posts : 485
      Rep Power : 443
      Likes Received
      135
      Likes Given
      388

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Quote By MWANA WA UFALME
      Nafikiri ni wakati sahihi sana kufikiria swala la camping facilities na generator kwenye mikutano kama hii.

      Tatizo kama kuna kitu chochote unakitegemea kutoka kwenye current system kufanikisha kazi ya kisiasa, watakitumia kama strategy ya kukukomoa.

      Mara nyingi tunashuhudia mikutano ya cdm inaporushwa live kwenye tv, umeme unakatwa etc,

      Camping vogn ambayo inaungwa kwenye gari kwa nyuma ni bei rahisi sana na inakuwa na facilities zote za nyumba. Its just an advice maana as we approach 2015 there will be alot of gorrilla tactics
      Ninakubaliana na wewe umetoa ushauri mzuri sana. Na kwa kuongezea wakiwa na facility kama hiyo, wajipange kiulizi kwa kuwa hawa magamba ni hatari sana

    21. #138
      Mkekuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 700
      Rep Power : 499
      Likes Received
      84
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      Magamba kuwa wajanja basi,mbona mmeishiwa technic kiasi hicho duh poleni sana.

    22. #139
      Nyakageni's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,248
      Rep Power : 0
      Likes Received
      769
      Likes Given
      52

      Default Re: Dr Slaa afanyiwa hujuma Morogoro

      After hardship comes relief!

    23. #140
      Catherine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Location : Dar
      Posts : 1,241
      Rep Power : 595
      Likes Received
      739
      Likes Given
      208

      Default

      Quote By only83
      Huyo meneja anapaswa kushikwa jina na sura yake...baada ya ukombozi 2015 atashughulikiwa kulinga na matendo yake.
      mtamfanyaje? Sidhani kama cdm ni chama cha kulipa visasi. Ila hotel ya kizembe hiyo, si sehemu nzuri ya kufikia. Kama dk slaa wameweza mnyan'ganya funguo sie wengine kajamba nani hata makofi tutapigwa na huyo manager.

    Page 7 of 9 FirstFirst ... 56789 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...