Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Muungano wa Serikali 3 ni bora Sana

    Report Post
    Page 4 of 4 FirstFirst ... 234
    Results 61 to 62 of 62
    1. #1
      TAYADI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th July 2012
      Posts : 1,348
      Rep Power : 615
      Likes Received
      210
      Likes Given
      256

      Default Muungano wa Serikali 3 ni bora Sana

      Serikali 3 ni bora sana kwa sababu zifuatazo:
      (i) Ni muarobaini wa malalamiko ya kuonewa au kumezwa;
      (ii) Ni balance nzuri ya uwiano serikalini - 50 kwa 50 katika uwakilishi na gharama;
      (iii) Hujuma za kuingiliana ktk chaguzi na kulazimisha chama kimoja kiongoze pande zote mbili zitadhibitiwa kirahisi;
      (iv) Hoja ya muunda wa serikali kuwa sera za vyama tutakuwa tumeimaliza;
      (v) Gharama za uendeshaji zitapungua kwa zaidi ya 50%. Mfano mmoja, serikali ya Muungano (serikali 2) kwa sasa (siyo SMZ) inalipa wabunge zaidi ya 80 wa Zanzibar (yenye wapigakura pungufu ya laki 4 na 50 na ukubwa sawa na wilaya ya Sengerema). Kila mbunge akilipwa milioni 11 kwa mwezi (11x80) sawasawa na milioni mia 8 na 80. Muundo wa serikali 3 tutakuwa na wabunge 30 au 40 (15 au 20 toka kila upande kufanya kazi za muungano wakigharamiwa na pande zote 2) na wabunge Serikali ya Tanganyika wapatao 150. Huu ni mzigo mwepesi kwa walipa kodi wote. SERIKALI MBILI NI MZIGO!!!!!
      Uliza_Bei likes this.

    2. Miaka 50

    3. #61
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,442
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      4805
      Likes Given
      2871

      Default Re: Muungano wa Serikali 3 ni bora Sana

      Quote By Nonda
      Mkuu Nguruvi3

      Hii tuhuma imetolewa sana na Wazenj kuwa Tanganyika imejigeuza jina tu na kujiita Tanganyika. Leo umelithibitisha hilo.
      Kama ni kweli hili ulisemalo basi yapasa tuwaombe radhi wazenj kwa kuwafanyia hadaa.

      Halafu inakuwaje tena, tutake serikali moja?

      Kama Tanganyika ilijibadilisha jina tu basi mkuu Nguruvi3 hata kama na mimi ningekuwa Mzanzibari basi nisingejiita mtanzania.
      Kwa maneno uliyoyaandika hapa, mtanzania ni mtanganyika.

      Mkuu leo umethibitisha ukiini macho wa Muungano.

      Yaani Tanganyika haijafa wala serikali ya Tanganyika haijafa. Hili nalo neno!!!

      Haya wamekusikia?

      Mkuu unajua maana ya ulaghai? hadaa? Vipi utafanya biashara kihadaa hadaa halafu useme unapata hasara?

      Leo, mkuu naona umeamua kuimwaga siri hadharani.

      Tanganyika haikufa wala serikali ya Tanganyika haikufa!!!??? Ila ilibadili jina tu. Duhhh!!! Hii kiboko, kwa hiyo kwa miaka 48 ni usanii tu na mazingaombwe. Sasa napata idea kwa nini UAMSHO na wazanzibari wanapiga kelele siku zote.

      Kama ni hivyo, maana yake hakuna Muungano au haujawahi kuwepo muungano. Ni usanii kwenda mbele na mazingaombwe tu.

      Pasco alipokuja na mada yake ya ratification naona aliekewa mkwara wa nguvu.

      Kuna la ziada Mkuu Nguruvi3 ambalo unataka kulisema kutuelimisha zaidi? Masikio yetu yako tayari kupokea darsa. Funguka mkuu.
      Usisome juu juu nimeandika nikiwa 'sober'. Tanganyika ni sleeping general kwasababu ili uwe na muungano lazima uwe na vitu viwili au zaidi. Kwa vile tuna muungano basi Tanganyika ipo na Zanzibar ipo.
      Kwa walioanzisha muungano waliacha Zbar na madaraka yake kuchelea kuonekana imefutwa na Tanganyika.
      In other words Tanganyika is recessive unlike Zanzibar which is predorminant.

      Hoja hiyo ni kujibu kuwa Tanganyika haijafa kama mnavyosema ila siyo dorminant kwasababu ya Tanzania.
      Niliposema kile cha Tanganyika kiwe cha Tanzania nilikuwa na maana ile ile ya cha ZNZ kiwe cha Tanzani. Lakini ukweli usiohitaji kuhitimu darasa la 4C upo wazi kuwa utamuombaje mtu asiye nacho akupe kisichokuwepo?

      Nikupe mfano, Elimu ya juu si jambo la muungano, lakini likasemwa liwe la muungano ili Kumsaidia Mzanzibar.
      Ni kutokana na hilo ndiyo Maana Mzanzibar yoyote mwenye elimu kasomea bara, kuanzia Maalimu Seif Jussa na wengine walioandikishwa jana(vijukuu).

      Nishati siyo muungano lakini Tanganyika ikasema kile cha Tanganyika kiwe cha Tanzania, ndipo ukaona umeme wa bure unavuka kwenda Zanzibar. ZNZ haikutoa au kuwekeza hata senti tano juu ya gharama hizo. Pamoja hayo, kuanzia akina Jumbe hadi Wajuu , vitukuu na vilembwe hakuna anayejua bei ya umeme duniani ni mpaka atoke nje ya ZNZ.
      Sababu kubwa ni kuwa cha Tanganyika ni cha Tanzania iliyo na Zanzibar

      In short kile cha Tanganyika kilichofanywa kuwa cha Tanzania ni kwa faida ya mzanzibar kwasababu ZNZ haina cha kutoa. Nonda huo ni ukweli, ni free ride msione kama tusi.

      Mtakapoondoka kwa amani na si kukimbizwa na mashoka, nadhani siku si nyingi, mtakwenda bandari kupanda meli na mabegi, Tanzania au Tanganyika au Mzizima itakuwepo pale pale ndiyo tafsiri ya sleeping giant.

    4. #62
      kajima's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th December 2009
      Location : Mtwara, Tanzania
      Posts : 162
      Rep Power : 514
      Likes Received
      40
      Likes Given
      130

      Default Re: Muungano wa Serikali 3 ni bora Sana

      Natamani mtu achambue option zote tatu kwa faida na hasara halafu JF members wachangie na kisha tuchague ipi itakuwa mfumo bora wa muungano....

    Page 4 of 4 FirstFirst ... 234

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...