Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nape azungumzia Harambee ya CHADEMA, wamjibu na kusema kakurupuka!

    Report Post
    Page 37 of 37 FirstFirst ... 27353637
    Results 721 to 734 of 734
    1. #1
      Return Of Undertaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 696
      Rep Power : 553
      Likes Received
      483
      Likes Given
      0

      Default Nape azungumzia Harambee ya CHADEMA, wamjibu na kusema kakurupuka!

      NA MWANDISHI WETU

      CCM imesema imesikitishwa na iliouita usanii mkubwa unaofanywa na Chadema, kuwahadaa Watanzania kwa kufanya harambee kwa lengo la kuhalalisha mabilioni ya chama hicho yanayodaiwa kutolewa na wafadhali kutoka mataifa tajiri duniani.

      Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye aliyasema hayo leo, Agosti 12, 2012, wakati akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba jijijni Dar es salaam.

      “Itakumbukwa mara kadhaa Chadema wamekuwa wakiitisha harambee za kisanii kwa kujaribu kuwahadaa baadhi ya Watanzania kwa kuwaomba wakichangie chama hicho huku viongozi wa chama hicho wakijua kuwa tayari wameshapata mabilioni toka kwa wafadhili wao. Mfano mzuri wa usanii huu ni juzi siku ya Jumamosi, Agosti 10, 2012, kwenye hoteli ya Serena ambapo walifanyika kiini macho cha harambee na kurushwa moja kwa moja na kituo kimoja cha televisheni." alisema Nape.

      Alisema ,umekuwa ni utamaduni wa Chadema kuhadaa watu kwa kuitisha harambee za kisanii kina wanapokuwa wameshapewa mabilioni ya fedha na wafadhili wao, ili mradi wahalalishe kuwa fedha wanazotumia zimetokana na michango ya watanzania wakati si kweli.

      Nape alisisitiza kuwa CCM wanao ushahidi kuhusu zinakotoka fedha na mikataba wanayoingia Chadema na wafadhili hao na kudai kuwa kama hawatasema wenyewe basi yeye (Nape) ipo siku atawasaidia kwa kutaja wafadhili hao na kuanika hadarani mikataba hiyo.

      “Tunao ushahidi wa kutosha unaoonyesha mabilioni waliyopewa Chadema juzi na wafadhili kutoka nje ya nchi kwa lengo la kuendeleza operesheni zao mbalimbali nchini. Cha kushangaza badala ya kuwaambia wanachama wao na Watanzania kwa jumla mikataba na wanakoyapata mabilioni haya, wanawahadaa kwa kuwachangisha na kugeuza mapato hayo mtaji wa baadhi ya watu binafsi ndani ya chama”, Alisema Nape

      Nape alidai kwamba, siri kubwa inayofichwa kuhusu mikataba na mabilioni wanayopewa Chadema ni kwa sababu wanaotoa fedha hizo wana ajenda ya kunyemelea rasilimali za nchi hii zinazoanza kuonyesha matumaini ya kuwepo kwa wingi ili wapate kizikwapua kwa urahisi kupitia mgongo wa chama hicho.

      "Kwanini mabilioni hayo yanatolewa kwa Chadema wakati huu ambapo sasa Tanzania imo katika kufanya utafiti na ugunduzi wa rasilimali mbalimbali zikiwamo gesi na mafuta? Na Je ufadhili huu kwa Chadema licha ya kufichwa sana na kufanywa siri, una nia njema kwa nchi yetu na rasilimali za nchi yetu? Kwanini ufadhili huu wa mabilioni unafanywa siri ya watu wachache hata ndani ya chama chenyewe?", Nape alihoji.

      Alisema, hatua hiyo ya Chadema itaitumbukiza Tanzania katika machafuko yasiyoisha, kama ambavyo inashuhudiwa katika baadhi ya nchi zenye rasilimali kama madini ambako nchi zenye utajiri wa fedha zilijipenyeza kupitia walioitwa wapambanaji wa uhuru na haki katika nchi hizo na hadi sasa hakuna amani.

      "Migogoro mingi tunayoshuhudia hasa katika nchi zinazoendelea pamoja na kuwepo sababu zingine lakini moja ya chanzo kikubwa ni uwepo wa utajiri wa rasilimali mbalimbali ambapo mataifa makubwa huzitamani na njia pekee ya kuzipata kwa urahisi ni kuchochea migogoro ya ndani na hivyo kuwa rahisi kupora rasilimali hizo wakati wenye nchi wanahangaika katika migogoro na kuachwa wakiwa masikini wa kutupwa huku waadhirika wakubwa wa migogoro na vita hivi vikiwanufaisha wakubwa.” Alisema Nape.

      Nape alitoa mwito kwa Watanzania kuwa ni muhimu macho na ulaghai huo wa Chadema na wafadhili wao na kukitaka chama hicho na wafadhili wao kama kweli wana nia njema na Tanzania, waweke wazi mashariti ya ufadhili huo wa mabilioni ya fedha ili Watanzania wote wajue kama yana manufaa kwao au la hasa ikizingatiwa kuwa vyama vya siasa hapa nchini vinaendeshwa kwa fedha za walipa kodi, hivyo Watanzania wana haki ya kujua.

      Pamoja na kuwataka kuweka wazi mashariti yanayoambatana na mabilioni hayo Nape aliwataka Chadema waseme hadharani wenyewe kwamba wamepewa mabilioni hayo, na kuwataka waache mara moja kuwahadaa Watanzania na kujaribu kujipachika kuwa ni Chama cha wanyonge kinachotegemea kujiendesha kwa michango ya watanzania huku wakiendelea kuchukua mabilioni kwa siri kutoka nje.

      “ Wasipowaeleza watanzania ukweli , tutawasidia kuwaeleza watanzania ukweli wa kiasi halisi cha mabilioni haya, walikozitoa na mikataba waliyoingia. Lengo la hili ni kuhakikisha kuwa nchi yetu haiwekwi rehani kwa uroho wa madaraka wa baadhi ya wana siasa.” Nape alisema.

      Nape akawaasa wanasiasa, kuendesha siasa za nchi kwa kuzingatia uzalendo na kukwepa kudumbukia kwenye tamaa za madaraka kujisahau na kuwa tayari hata kuweka nchi rehani, hasa kipindi hichi ambapo ugunduzi wa rasilimali mbali mbali hasa madini, gesi na mafuta vikiwa vinashika kasi nchini na kwamba ugunduzi huo uwe baraka kwa nchi badala ya laana na kuwa chanzo cha kuiuza nchi.
      Quote By John Mnyika
      Katika mitandao ya kijamii kumesambazwa habari zikimnukuu msemaji wa CCM kutoa madai mbalimbali ya uzushi katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu CHADEMA baada ya CHADEMA kuendelea kutekeleza mikakati na mipango yake ya kuwaunganisha watanzania kupitia falsafa ya ‘nguvu ya umma’ katika kuchangia vuguvugu la mabadiliko (M4C) katika maeneo mbalimbali nchini.

      Nitatoa tamko kamili na kueleza hatua za ziada baada ya kupata taarifa iliyotolewa kwa ukamilifu, hata hivyo kuhusu madai yaliyokwisha sambazwa kwenye mitandao ya kijamii na CCM nachukua fursa hii kutoa kauli ya awali kama ifuatavyo:

      Kuibuka huku kwa CCM na kufanya propaganda chafu ni ishara ya kwamba CCM inaumizwa na namna ambavyo watanzania wanajitokeza kuunga mkono CHADEMA kwa hali na mali hivyo CCM sasa inatapatapa kujaribu kudhibiti wimbi la mabadiliko kwa kutumia siasa chafu. Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete anapaswa kueleza watanzania iwapo mikakati hiyo michafu ina baraka zake na za serikali anayoiongoza kwa kurejea pia madai yaliyotolewa na Waziri wa Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu) Steven Wassira kuwa CHADEMA itasambaratishwa katika kipindi cha mwaka mmoja kwa mbinu mbalimbali.

      CCM kwa kuwa imekuwa na kawaida ya kufanya usanii kuhalalisha fedha haramu kama ilivyofanya kwenye chaguzi zilizopita baada ya viongozi waandamizi wa CCM na makada wake kuchota fedha za chafu kifisadi kama zile za kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na vyanzo vingine vichafu na kuzisafisha kupitia harambee za hadaa zilizofanywa na CCM kwa nyakati mbalimbali; inataka kuichafua CHADEMA inayopata fedha kutoka vyanzo halali kwa njia za wazi ili kukatisha tamaa umma wa watanzania unaochangia vuguvugu la mabadiliko.

      Viongozi wa CCM wameamua kujidanganya, kuidanganya Serikali yao na kujaribu kuwapotosha watanzania lakini CHADEMA inatambua kwamba watu wachache wanaweza kudanganyika kwa muda mchache lakini si watu wote wakati wote; na kwamba watanzania wa leo kwa uwingi wao hawawezi kudanganyika na uzushi wa kijinga wa CCM.

      Ni ukweli ulio wazi kwamba CHADEMA imekuwa ikifanya harambee kwa uwazi kwa nyakati mbalimbali katika kumbi na katika mikutano ya hadhara ikiwemo ya vijijini ambapo michango hutolewa kwa uwazi, aidha michango kwa njia ya simu inaweza kufuatiliwa na kuthibitisha bila shaka yoyote kwamba watanzania wameamua kuchangia mabadiliko ya kweli.

      Madai ya CCM kuwa CHADEMA imepokea au itapokea mabilioni ya shilingi kutoka mataifa ya nje ni ya uzushi na narudia kwa mara nyingine tena kuitaka CCM itaje majina ya serikali, taasisi ama makampuni ya nje ambayo CCM inadai kwamba CHADEMA imepokea mabilioni ya shilingi katika siku za karibuni au inatarajia kupokea.

      Badala ya CCM kuisingizia CHADEMA ilipaswa CCM ieleze watanzania orodha ya vigogo wa Serikali inayoongozwa na wanachama waandamizi wa CCM ambao wanaelezwa kuwa na akaunti nchini Uswisi na nchi zingine wakituhumiwa kupewa fedha za kifisadi kutoka kwa makampuni ya utafutaji wa mafuta, gesi asili pamoja na uchimbaji wa madini.

      CCM ilipaswa ieleze watanzania sababu za kuendelea kusuasua kujivua magamba ya ufisadi kinyume na maazimio ya CCM yaliyofikiwa baada ya msukumo wa CHADEMA kutaja orodha ya mafisadi kwa kuwa kati ya mafisadi hao ni pamoja na viongozi wa CCM walioiingiza nchi katika mikataba mibovu.
      Quote By John Mnyika
      WanaCCM mtanisamehe, lakini imenibidi kutoa kauli hii ya awali kufuatia madai ya uzushi na ya kijinga yaliyotolewa na Msemaji wa CCM dhidi ya CHADEMA

      Madai kama haya yanaendelea kudhihirisha kuwa taifa letu limefika hapa lilipo kwa pamoja na sababu zingine ‘upuuzi wa CCM’. CHADEMA haijawahi kufadhiliwa mabilioni kutoka nje, michango kwenye M4C iwe ni kwenye kumbi za hoteli au vijijini tunapochangiwa na wananchi wenye kutaka mabadiliko ya kweli ni ishara ya imani ambayo watanzania wanayo kwa CHADEMA.

      Badala ya CCM kuisingizia CHADEMA kuwa inafadhaliwa na mataifa ya nje kupora rasilimali za nchi ikiwemo mafuta na gesi yanapaswa kupuuzwa kwa kuwa CCM ndio inao wajibu wa kuwatajia watanzania viongozi wa Serikali na CCM waliongiziwa mabilioni Uswisi kuingia mikataba mibovu ya rasilimali za nchi yetu.

      Aidha, CHADEMA imekuwa mstari wa mbele kuwataja kwa majina wanaoingia mikataba mibovu ikiwemo kwenye madini, CCM kwa kuwa ilikubali kuwa ina magamba ya ufisadi irejee kwenye orodha ya mafisadi na kuchukua hatua ya kujivua gamba badala ya kufanya siasa chafu dhidi ya CHADEMA.

      Majibu zaidi mnaweza kuyasoma kwenye mnyika.blogspot.com na kuendelea kuunganisha nguvu ya umma kupitia CHADEMA katika kuwezesha Tanzania kupata uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya taifa letu na watu wake wote bila kujali itikadi. Hakuna Kulala, Mpaka Kieleweke
      Dr. Slaa: Nape kakurupuka!

      *Aponda hoja zake, adai hazina tija
      *Mjumbe NEC naye amshangaa


      KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa, amesema kamwe hawezi kujibizana na hoja za kukurupuka zilizotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye.

      Kauli ya Dk. Slaa, imekuja siku moja tu baada ya Nape kukituhumu Chadema kuwa kimekuwa kikiendesha harambee za kukusanya fedha, jambo ambalo ni sawa na usanii mtupu.

      Akizungumza na MTANZANIA mjini Dar es Salaam jana, Dk. Slaa alisema Nape si saizi yake kisiasa na wanachokifanya CCM ni kuweweseka na jinsi chama chake, kinavyozidi kukubalika kwa Watanzania.

      Alisema CCM, wamekuwa wakikurupuka kutoa hoja ambazo hazina msingi na badala yake zimekuwa na mrengo wa kuwachanganya Watanzania.

      “Kwanza napenda kusema Nape si saizi yangu … hoja zake zote nazipuuza, zimejaa propaganda na uchochezi kwa Watanzania.

      “Inashangaza kusikia watu hawa wanatuhumu chama chetu, eti kinapokea fedha chafu, inashangaza kuona wao ndio polisi, usalama wa taifa na Benki Kuu (BoT), sasa inakuwaje wanaacha fedha hizi zinaingia nchini?” Alihoji Dk. Slaa.

      Alisema inaonyesha wazi namna ambavyo Nape amekosa hoja za msingi za kuwaambia Watanzania.

      Alisema atafurahi kusikia Nape anataja mataifa ambayo yamekuwa yakitoa fedha kuifadhili Chadema, kwani kufanya hivyo kutasaidia kupunguza propaganda.

      Alisema kuna sheria ya kudhibiti fedha chafu ambayo imepitishwa na Bunge, sasa inakuwaje utekelezaji wake unakuwa mgumu.

      “Nawaomba Watanzani watuelewe tunachofanya, kwani kuendelea kuwasikiliza watu hawa tunapotezea mud wetu.

      “Watanzania wanatakiwa kufahamu, kuwa umoja wa utaifa unavurugika kutokana na uchochezi kutoka kwa viongozi au watu waliopewa dhamana ya kusimamia na kulinda amani.

      “Nimechoshwa na kujibu hoja za kitoto na hii itakuwa ni mara ya mwisho kwangu kumjibu Nape, kwa sababu hoja zenyewe hazina mashiko kwa wananchi.

      “Nasema hivyo, kwa sababu watu hawa wanakurupuka kutoa hoja zisizokuwa na mantiki yoyote…hawana hata makabrasha ya ushahidi wa maneno wanayoyasema …sijui ni aina gani ya viongozi?” alihoji Dk. Slaa.

      Juzi Nape alikutana na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam na kudai CCM, imeshtushwa na kasi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuendesha harambee za kukusanya fedha kila kukicha, kitendo ambacho ni sawa na usanii.

      Alisema, CHADEMA kimekuwa kikiendesha usanii huo, licha ya ukweli kuwa, kinapokea mamilioni ya fedha kutoka mataifa ya nje.

      Alisema CCM, imesikitishwa na kushangazwa na usanii unofanywa na CHADEMA, kwa kuwahadaa Watanzania, kwa kufanya harambee ili kuhalalisha uwepo wa mabilioni ya fedha wanazopewa na wafadhili wao nje ya nchi.

      ‘‘Umekuwa utamaduni wa chama hiki kuhadaa watu kwa kuitisha harambee za kisanii, baada ya kupewa mabilioni ya fedha na wafadhili wao, ili mradi wahalalishe fedha wanazotumia zimetokana na michango ya Watanzania, wakati si kweli.

      “Tunao ushahidi wa kutosha unaoonyesha fedha walizopewa na wafadhili kutoka nje ya nchi, kwa lengo la kuendeleza operesheni mbalimbali nchini. Cha kushangaza, badala ya kuwaambia wanachama wao na Watanzania ukweli wa haya, wanaanza kuwahadaa kwa kuwachangisha na kugeuza mapato haya, mtaji wa baadhi ya watu binafsi ndani ya chama.

      “Hebu tujiulize, kwa nini mabilioni haya yanayotolewa kwa Chadema wakati huu, ambao nchi yetu inaendelea kufanya utafiti na ugunduzi wa rasilimali mbalimbali, zikiwamo mafuta na gesi? Je, ufadhili huu licha ya kufichwa sana na kufanywa kwa siri, una nia njema kwa nchi yetu na rasilimali za nchi yetu?” alihoji Nape.

      “Ni muhimu Watanzania tukawa macho na ulaghai huu na tunawataka wafadhili wao kama kweli wana nia njema na nchi yetu, waweke wazi masharti ili Watanzania watambue fedha hizi zina manufaa au la,” alisema Nape.

      MJUMBE WA NEC

      Katika hatua nyingine, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema anashangazwa na kauli za Nape.

      “Nimeshangazwa mno na kauli hii, nimeshtushwa kusikia eti kuna mataifa ya nje yanayotoa fedha nje kwa ajili ya kuisaidia Chadema…kumbuka Serikali yetu zaidi ya asilimia 30 tunapewa na wafadhili.

      “Naamini kusaidiwa na mataifa si ajabu, kwa sasa hata sisi CCM tunasaidiwa na mataifa ya nje ambayo ni rafiki zetu kifedha na kiutawala.

      “Naamini Nape ni kiongozi mkubwa ndani ya chama, hii mikataba anayosema angeitaja ningefurahi sana… huu ni udhaifu mkubwa kwa kiongozi wangu, huu ni mwendelezo wa kujenga majungu na fitina,

      …hoja yake ya kusema atawataja ni miujizi, kwa sababu hii si mara ya kwanza kwake, kuibuka na maneno ya aina hii… nadhani kiongozi katika chama kikubwa na tawala wanapaswa kukaa chini na kutafakari kabla ya kuongea,” alisema mjumbe huyo.


      CHANZO: Mtanzania - Agosti 14, 2012


    2. #721
      maghambo619's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th August 2012
      Posts : 171
      Rep Power : 379
      Likes Received
      25
      Likes Given
      26

      Default

      Quote By Advocate Jasha View Post
      Baada ya kauli ya Nape ya kua CHADEMA wamekua wakipokea fedha chafu na kuzisafisha kwa kupita michango ya wananchi ya kua pesa hizo zitaiweka CHADEMA madarakani na watowaji wa pesa hizo wanawinda rasilimali zetu ,gesi na mafuta ambayo kuna dalili ya kugunduliwa.Kitu amabacho kimeonekana kwa kauli yake,mbali ya kutokua na mantiki ni kichekesho.Kwa sababu ni CCM ambayo iko madarakani imekua ikitumia pesa chafu katika kampeni zake,kuwalazimisha wafanyabiashara na walalahoi kuichangia bila ridhaa yao,kuuza rasilimali zetu dhahabu,almasi na ufisadi mwingine mwingi.
      Kwa kauli ya Nape inaonyesha ya kua CCM imeisha kata tamaa ya kurudi madarakani kwa hiyo kwa mawazo yake nikwamba CHADEMA ikichukua madaraka itaendeleza mfumu uliokua ukitumiwa na CCM,kuuza rasilimali zetu ili kupata pesa chafu kiiendesha.Hivyo sivyo,wakati CHADEMA kinakusanya pesa na michango toka kwa wananchi pamoja na ruzuku wanayoipata ,wanaitumia kuwaelimisha walalahoi kuhusu haki zao na uozo wa CCM na utawala kwa ujumla.Wakati CCM ruzuku,pesa chafu,michango ya kuwalazimisha wafanyabiashara na pesa inayoptikana kiufisadi,kwanza wanajinufaisha wao watawala na kiasi kidogo kinachobaki wanakitumia kuwarubuni kwa kuwanunua fulana na,khanga,kofia pilau n.k.
      kwa hali ilivyo hivi sasa pesa hazitoshi na wanaionea Wivu CHADEMA kwa walivyojipanga na kuanzisha uzushi usio na kichwa wala miguu.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
      naam, inauma sana uhai unapoitoka ccm. Afu wale wanaoitwa machizi na waropokaji wanaposhika hatamu! Haleluyah!!

    3. #722
      Jackbauer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : CTU
      Posts : 4,919
      Rep Power : 1703
      Likes Received
      1367
      Likes Given
      284

      Default Re: Kwa hili ccm na nape mkubali vyanzo na matumizi ya fedha ccm na chadema yanatofautiana

      hivi ccm walivyochangisha fedha kupitia simu za mkononi kipindi kile ilikuwa inaficha fedha haramu?kama huu ndio mchezo wenu msidhani kila chama ni hivyo.
      You may succeed in silencing me but that silence comes at a price-Alex litvinenko

    4. #723
      ntamaholo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Location : Mwilavya
      Posts : 4,119
      Rep Power : 1391
      Likes Received
      919
      Likes Given
      412

      Default Re: Dr. Slaa amjibu Nape!

      Quote By Rejao View Post
      ................
      Hivi vyote ni vitu visivyo na mashiko kwa sasa. Chamuhimu kwa sasa ni kuongelea mambo ya maendeleo na namna ya kujikomboa kifkra na kiuchumi.[/QUOTE]

      ukombozi upi wa KIFIKRA unaozungumzia Rejao? Hivi na wewe unauhitaji ukombozi wa kifikra? mbona juzi tu ulisherehekea MwanzaHALISI kupigwa life ban? wacha kujikorogao kuwa na msimamo wewe.

      Haya kujikomboa kiuchumi kutawezekana vipi wakati CCM wameiba na kuweka shekeli za kutosha uswiswi? Si walipuliwe na kama serikali ina utashi iwapeleke mahakaman kitu ambacho si rahisi, kwani naamini na wewe kwa unavyowatetea wezi, lazima una commision yako.
      UTUMISHI WA HAKI, NI SULUHISHO LA MAOVU YOTE

    5. #724
      mgashi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 227
      Rep Power : 408
      Likes Received
      61
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By Rejao View Post
      Babuuuuu....kumbe bado upo kwenye ulingo wa siasa? Naona story zako ni zile zile za Tangold, Kagoda na Meremeta! Don't you have something new? Badilika bana, tumeshaichoka hiyo mistari yako. Jitahidi uje na swaga nyingine.
      Sema umeichoka ww kama ww na mafisadi wenzio mkimsikia dr kaongea kijasho kinawatoka lakini kwa walio wengi bado tunamuhitaji sana.

    6. #725
      Muke Ya Muzungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th June 2009
      Posts : 1,906
      Rep Power : 3861
      Likes Received
      180
      Likes Given
      31

      Default NaPe: Usimfukuze Mwizi wa Kuku Kwa Panga Wakati Zizi Lako Limejaa Ng'ombe Wa Kuibwa

      Bw. Nape, kama mzungumzaji mkuu wa chama chetu, umekuwa ukipigia kelele harambee za chadema ukiziusisha na hela haramu. Kama mwana CCM anayeitakia chama chetu mema, tatizo siyo hela za chadema, tatizo ni mafisadi ndani ya ccm na serikali yake. Kuna taarifa za uhakika kwamba viongozi wengi sana ndani ya chama chetu wanaiba sana hela za walipa kodi na kuzipeleka uswisi. tafadhali sana utupatie majina ya hawa vigogo ndani ya ccm....vinginevyo utakuwa unaendeleza ujuha. Zizi lako limejaa na Ng'ombe wa wizi huku unamfukuza mwizi wa kuku na panga

      Tafadhali wapigie chadema kelele ukishataoa ufafanuzu kuhusu hela za uswisi
      desmondtutu likes this.


    7. #726
      Henge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2009
      Posts : 5,440
      Rep Power : 1678
      Likes Received
      920
      Likes Given
      1673

      Default Re: NaPe: Usimfukuze Mwizi wa Kuku Kwa Panga Wakati Zizi Lako Limejaa Ng'ombe Wa Kuibwa

      Quote By HonorableMP View Post
      Bw. Nape, kama mzungumzaji mkuu wa chama chetu, umekuwa ukipigia kelele harambee za chadema ukiziusisha na hela haramu. Kama mwana CCM anayeitakia chama chetu mema, tatizo siyo hela za chadema, tatizo ni mafisadi ndani ya ccm na serikali yake. Kuna taarifa za uhakika kwamba viongozi wengi sana ndani ya chama chetu wanaiba sana hela za walipa kodi na kuzipeleka uswisi. tafadhali sana utupatie majina ya hawa vigogo ndani ya ccm....vinginevyo utakuwa unaendeleza ujuha. Zizi lako limejaa na Ng'ombe wa wizi huku unamfukuza mwizi wa kuku na panga

      Tafadhali wapigie chadema kelele ukishataoa ufafanuzu kuhusu hela za uswisi
      Mkuu wewe mbona unaonekana ni mbunge mzuri wa ccm kuliko wenzako woote!
      HONGERA SANA TUNATAKA WATU KAMA NINYI NDANI YA CCM ACHANA NA MAVUVUZELA! KAMA NAPE!
      TUKIWAKAMATA MAFISADI NCHI ITAYUMBA by PINDA

    8. #727
      Muke Ya Muzungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th June 2009
      Posts : 1,906
      Rep Power : 3861
      Likes Received
      180
      Likes Given
      31

      Default Re: NaPe: Usimfukuze Mwizi wa Kuku Kwa Panga Wakati Zizi Lako Limejaa Ng'ombe Wa Kuibwa

      Nape vuvuzela tu. hana ubavu wa kuwataja mabilionea. Chadema anawaonea kwa sababu ni wanyonge

    9. #728
      afwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th October 2010
      Posts : 823
      Rep Power : 602
      Likes Received
      112
      Likes Given
      131

      Default Re: NaPe: Usimfukuze Mwizi wa Kuku Kwa Panga Wakati Zizi Lako Limejaa Ng'ombe Wa Kuibwa

      Quote By HonorableMP View Post
      Bw. Nape, kama mzungumzaji mkuu wa chama chetu, umekuwa ukipigia kelele harambee za chadema ukiziusisha na hela haramu. Kama mwana CCM anayeitakia chama chetu mema, tatizo siyo hela za chadema, tatizo ni mafisadi ndani ya ccm na serikali yake. Kuna taarifa za uhakika kwamba viongozi wengi sana ndani ya chama chetu wanaiba sana hela za walipa kodi na kuzipeleka uswisi. tafadhali sana utupatie majina ya hawa vigogo ndani ya ccm....vinginevyo utakuwa unaendeleza ujuha. Zizi lako limejaa na Ng'ombe wa wizi huku unamfukuza mwizi wa kuku na panga

      Tafadhali wapigie chadema kelele ukishataoa ufafanuzu kuhusu hela za uswisi
      Ni mtazamo wa kimageuzi ndani ya CCM! One needs to amplify this!

    10. #729
      TOWNSEND's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th May 2011
      Location : kwa ngulelo
      Posts : 1,160
      Rep Power : 643
      Likes Received
      201
      Likes Given
      31

      Default Re: NaPe: Usimfukuze Mwizi wa Kuku Kwa Panga Wakati Zizi Lako Limejaa Ng'ombe Wa Kuibwa

      Hizo za uswisi tunazitaka bwana nape na zile chenchi zetu za nguzo za umeme feki toka south kumbe ni za mufindi hii sio uzushi ni waziri wako npe alisema bungeni ....cha ajabu kabisa hakna hata mmoja alie chukuliwa hatua madhubuti ktk hili la wai kabisaaaaaa ccm hakuna msafi hata kama ni shehe au askofu ni balaa tpu mmesikia zile shule wanao iba umeme
      For tommorow belonging to those people who prepared fo it

    11. #730
      kupelwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th August 2011
      Location : DAR-ES-SALAAM
      Posts : 477
      Rep Power : 491
      Likes Received
      129
      Likes Given
      31

      Default Re: NaPe: Usimfukuze Mwizi wa Kuku Kwa Panga Wakati Zizi Lako Limejaa Ng'ombe Wa Kuibwa

      Quote By HonorableMP View Post
      Bw. Nape, kama mzungumzaji mkuu wa chama chetu, umekuwa ukipigia kelele harambee za chadema ukiziusisha na hela haramu. Kama mwana CCM anayeitakia chama chetu mema, tatizo siyo hela za chadema, tatizo ni mafisadi ndani ya ccm na serikali yake. Kuna taarifa za uhakika kwamba viongozi wengi sana ndani ya chama chetu wanaiba sana hela za walipa kodi na kuzipeleka uswisi. tafadhali sana utupatie majina ya hawa vigogo ndani ya ccm....vinginevyo utakuwa unaendeleza ujuha. Zizi lako limejaa na Ng'ombe wa wizi huku unamfukuza mwizi wa kuku na panga

      Tafadhali wapigie chadema kelele ukishataoa ufafanuzu kuhusu hela za uswisi
      tatizo si nape , tatizo ni chama kwa ujumla.chama ni pamoja na uongozi, wanachama, rasilimali, na mifumo ya kuendesha chama.Mfano chama hichi hicho bado kinadagnya kuwa itikadi yake ni kuwajali wakulima na wafanyakazi, lakini ni kweli ccm bado inamjali mkulima na mfanyakazi?leo kuna tatizo la bei ya pamba kwa kanda ya ziwa.wakulima hawa wameingia gharama nyingi kwa kutegemea bei ingekuwa kama msimu wa mwaka jana.lakini bila kutegemea msimu unaanza mwenyekiti wa bodi ya pamba dr.festus limbu mbunge wa magu(ccm); akatangaza bei ya T.shs 600/= kwa kilo, je ccm kama inawajali na kuwatetea wanyonge imefanya nini kuwasaidia wauze kwa bei waliokuwa wanaitegemea na shs 1000/=?nakumbuka kwenye mdororo wa uchumi duniani serikali iliingiza triaoni 1.7 kusisimua uchumi, japo mpaka leo hatujui pesa hizo zilienda wapi, kwanini isichukue jukumu la kuwasaidia kama enzi hizo z mdororo wa uchumi?pia kama nape hawezi kusema lolote hili la kuteremka bei ni sidicate wa wenye viwanda vya kuchambua pamba na wanunuzi wa pamba, je nape kasema nini badala ya kuwatetea.je kwa hili kweli tunawajali wakulima?nape yupo kama kichwa box wenye chama wametuli wanamuendesha kwa remote , na kumwacha anapayuka

    12. #731
      Man KKK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Location : Ndani ya Laptop
      Posts : 789
      Rep Power : 521
      Likes Received
      94
      Likes Given
      46

      Default Ccm: Dk. Slaa anazeeka vibaya

      KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nauye amemshukia Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbrod Slaa, kufuatia kauli aliyoitoa mkoani Morogoro kwamba Chama Cha Mapinduzi kimekuwa kikiingiza silaha nchini.
      "Kauli hii inaonyesha ni vipi Dk. Slaa ameanza kuzeeka vibaya, na sasa kazi ya siasa inamshinda hivyo awaachie vijana" alisema Nape na kuongeza kwamba anatambua kuwa uzee siyo laana kama unamwingia mtu vizuri.

      Akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, mtaa wa Lumumba, Dar es Salaam, Nape amesema, mbali na kuzeeka vibaya, hatua ya Dk. Slaa kuizushia CCM kwamba imekuwa ikiingiza siala kinyemela ni dalili kwamba ameona kuwa sasa operesheni ya mikutano ya Chadema hasa ya Morogoro zinazorota.

      Kwa mujibu wa Nape, Dk. Slaa amesikika akitangaza mjini Morogoro kwamba, CCM imekuwa ikiingiza siala nchini na kuwapa vijana wazitumie wawapo kwenye makambi ya Umoja wa Vijana wa CCM.

      "Kwanza huyu Mzee inaonyesha ni jinsi gani ufuatiliaji wake wa mambo ni vinyu, kutoa madai kwamba tumeagiza siala kinyemela kwa ajili ya makambi ya vijana wetu, wakati inafahamika kwamba wakati huu CCM imo katika uchaguzi mkuu hatuwezi kabisa kuandaa wala kufanya makambi ya vijana", alisema Nape.

      "Kutokana na kauli hizi za uzushi, tunazitaka mamlaka zinazosimamia ulinzi na usalama kumtaka Dk. Slaa awapatie ushahidi wa kina kuhusu mtu au tasisi yoyote ambayo inaingiza silaha nchini kinyemela, na kama ushahidi wake utawezesha kupatikana yeyote basi ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria", alisema.

      "Huyu Mzee imekuwa kawaida yake kuandaa uongo kila anapoona kwamba anakabia kushindwa katika operesheni au mipango yake au ya Chama chake kisiasa. Wakati ule wa Uchaguzi mkuu, alipoona kwamba atashindwa, alizusha kwamba CCM imeingiza kura nchini kutoka nje ya Nchi, lakini ikabainika kuwa ni uzushi", alisema.

      Alisema, hatua ya Dk. Slaa kuzusha uongo ni njama ya kuandaa fujo zitakazofanywa watu walioandaliwa na Chadema, kufanya fujo mitaani wakati wa mikutano wa chama hicho mkoani Morogoro. " sasa anatoa uongo huu, ili watu wao waliokusanya watakapofanya fujo azushe kwamba ni vijana waliotumwa na CCM".


    13. #732
      mamajack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 1,153
      Rep Power : 587
      Likes Received
      275
      Likes Given
      71

      Default Re: Nape azungumzia Harambee ya CHADEMA, wamjibu na kusema kakurupuka!

      nape yule mpuuzi au????kawaida yake kubisha,na mie naamini atakuwa ndiye muhusika mkuu wa mpango mzima,
      ndiyo maana mkama anataka kuachia ngazi.

    14. #733
      kiliochangu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 23rd February 2012
      Posts : 111
      Rep Power : 391
      Likes Received
      11
      Likes Given
      8

      Default Re: Nape azungumzia Harambee ya CHADEMA, wamjibu na kusema kakurupuka!

      Mchezo mchafu wa CCM tumeuzoea. Bora CDM kuliko CCM walioiba na kukwapua fedha za watazania kupitia Kodi na Bili kubwa za Umeme ili kuendesha chama Tunaomba azungumzie suala la kupandisha Malipo ya Unit za Luku na ukusanyaji wa fedha hizo kuendesha CCM. Watanzania sio wajinga ila hawapendi makuu. Tunayaelewa hayo.

    15. #734
      Mkekuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 716
      Rep Power : 506
      Likes Received
      86
      Likes Given
      0

      Default Re: Nape azungumzia Harambee ya CHADEMA, wamjibu na kusema kakurupuka!

      Vuvuzela kazini.

    Page 37 of 37 FirstFirst ... 27353637

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...