Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Smz yaombwa kuzipatia ufumbuzi kero za muungano kabla ya katiba mpya

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 719
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default Smz yaombwa kuzipatia ufumbuzi kero za muungano kabla ya katiba mpya



      Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeombwa kuyapatia ufumbuzi matatizo ya muungano yanayolalamikiwa na Zanzibar kabla ya kuanza kwa katiba mpya ya Jamhuri ya muungano Tanzania.
      Mwakilishi wa kuteuliwa Ali Mzee Ali amesema taasisi kama vile benki kuu BOT, mamlaka ya mapato Tanzania TRA na taasisi nyingine zinalalamikiwa na upande wa pili wa muungano kwa madai ya kukwamisha maendeleo ya uchumi wa Zanzibar.
      Akichangia hotuba ya bajeti ya wizara ya fedha, uchumi na mipango ya maendeleo katika kikao cha baraza la wawakilishi amesema muundo wa taasisi hizo haziko katika mfumo wa muungano na kusababisha matatizo kutokana na utendaji wake kufimbiwa macho na serikali zote mbili.
      Hivyo ameiomba serikali ya mapinduzi Zanzibar kupitia vikao vya kutatua kero za muungano kuyapatia ufuimbuzi matatizo hayo kabla ya kuanza kwa katiba mpya
      Nae mwakilishi wa jimbo la Kwamtipura Hamza Hassan Juma ameiomba serikali kuingilia kukwama kwa zaidi ya gari 500 za wafanyabiashara wa Zanzibar katika bandari ya Dar es Salaam.
      Amesema tatizo la wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili limechangia kukwama kwa gari hizo, hivyo iko haja ya kwa serikali kulipatiwa ufmbuzi wa haraka.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Ruge Opinion's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2006
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,058
      Rep Power : 890
      Likes Received
      149
      Likes Given
      79

      Default Re: Smz yaombwa kuzipatia ufumbuzi kero za muungano kabla ya katiba mpya

      Magari ya Wazanzibari kwa nini yanapitia Dar es Salaam. Bandari yenu ina matatizo gani? Au Wazanzibari wanapitisha magari yao Dar ili kukwepa kero za Muungano Zanzibar? Nisaidieni. Kichwa kinazunguka.
      Loosing is a starting point to success

    4. #3
      Kamundu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2006
      Posts : 1,371
      Rep Power : 914
      Likes Received
      296
      Likes Given
      9

      Default Re: Smz yaombwa kuzipatia ufumbuzi kero za muungano kabla ya katiba mpya

      Zanzibar kama mnakumbuka wakati wa awamu ya mwinyi ilikiwa sehemu ya kupitisha vitu bila kulipia kodi hata sasa hakuna utaratibu wa kuzuia vitu visivyolipiwa kodi kupitia zanzibar na ndiyo maana bandari ya Zanzibar inapunguza umashuhuri hasa kwa wakusanya kodi. Kama Zanzibar wanataka kila kitu kiwe pande zote je muungano unamuhimu gani sasa si bora muwe na nchi inayojitegemea kwa asimila 100% TRA na BOT zitasaidia nini kwa Tanzania badala ya gharama tu?. Tusikoangalia wataanza kusema bandari ya Zanzibar ni huru haina kodi n.k huwezi kuwa na nchi moja na sheria mbili ni wakati wa kufanya uamuzi mmoja je Zanzibar inataka kuwa nchi moja ya Tanzania au inataka kuwa nchi pekee 100% na iwe na mipaka na tuachane kwa nia moja lakini huu muungano wa matatizo kila siku hausaidii nchi yeyote maana Wanzanzibar wanafikiri wanaonewa na Wabara wanafikiri wanafanya mengi bila sababu. Tuweke mipaka ya security na mikataba ya kijeshi na tutengane au tuungane kama nchi moja. Serikali mbili, tatu ni upuuzi mkubwa.

    5. Miaka 50

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...