Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

    Report Post
    Page 5 of 6 FirstFirst ... 3456 LastLast
    Results 81 to 100 of 107
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,502
      Rep Power : 46710
      Likes Received
      16360
      Likes Given
      8419

      Default Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi



      Daraja ya Kagera (Kyaka) lililobomolewa na Idi Amin na vikosi vyake pamoja na majengo yaliyobomolewa nakubakia majeraha ya vita.


      • Wanasiasa wanaotoa lugha ya vita hawana hekima na ni hatari
      • Wengine wanatafuta ujiko wa kisiasa
      • Tusizungumzie vita kama hatuko tayari kupigana
      • Vita si lelemama


      Na. M. M. Mwanakijiji

      Sikutegemea kama Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje Bw. Lowassa kutoa kauli ambayo ikiunganishwa na ile ya Sitta na ya Membe inazidi kuchochea hali ya kutotafuta suluhu. Wote hawa watatu bila ya shaka wanasema kutokana na nafasi zao lakini pia yawezekana wanasema kwa sababu wote watatu wanatajwa vile vile kama wagombea watarajiwa wa urais mwaka 2015. Hata hivyo nazipima kauli hizi kwa jambo la kwanza na si kwa hilo la pili.

      Vita si jambo dogo na si jambo la mzaha kama watu wengine wanavyochukulia. Nimeona tangu Wamalawi walipozungumza suala la kudai "ziwa zima" la Nyassa kuwa ni lao baadhi ya watu wetu mwitikio wao wa kwanza umekuwa ni "tupeleke majeshi" au "tupeleke vijana wetu" na sasa leo Lowassa ananukuliwa na vyombo vya habari mbalimbali kuwa JWTZ liko tayari kwenda vitani na Malawi kuhusu suala hili. Hili ni jambo la kusikitisha na kushangaza.

      Kufikiria vita siyo jambo dogo na wala si jambo la kutafuta ujiko au siasa. Ni sawa na kuamua kushika bunduki na kumuelekezea mtu. Polisi huwa wanaambiwa kuwa usielekeze Bunduki kama hauko tayari kuitumia. Wale ambao wanabeba silaha (nao ni raia) wanajua kabisa kuwa hutoi silaha kibindoni kama hauko tayari ku-pull the trigger. Maana ya yote haya ni kuwa kutoa silaha na kuishika mkononi siyo suala la ubishoo, urembo au kujionesha kuwa unaweza.

      Tusipokemea hili la wanasiasa mwisho tutaona watu wanaanza mazoezi ya kutuonesha vifaa vya kivita ili kuwapiga mkwara wa Malawi. Na kweli wapo ambao wanatamani kuona "vijana wetu" wanaanza kuelekea mpakani au kwenye ukingo wa Ziwa Nyassa ili kutuma ujumbe kuwa tuko tayari. Sasa hili ni zuri na linasisimua akili na hisia za "kizalendo". Lakini tusije kuwa ni mambo ya Wag the Dog ambapo ili kushinda uchaguzi timu ya wanamkakati wa kampeni waliamua kutengeneza 'vita isiyokuwepo' ili kupoteza mawazo ya wapiga kura.

      Ninachoogopa zaidi ni kuwa wakati watawala wetu tumewabana kuhusu uongovi wao mbovu, sera zao zilizoshindwa na ukosefu wa maono usiokoma suala la mgogoro wa Ziwa Nyassa limewapa 'gia' ya kutokea na sasa hata watu waliokaa kimya wakati wananchi wetu wanauawa nakudhalilishwa na vyombo vya usalama wanasimama pasi ya kuomba radhi na kutaka tusimame nyuma yao. Nimeshangaa kuona Lowassa leo ameweza kukutana na vyombo vya usalama na kupewa taarifa zinazohusu vita lakini huyu huyu hajakutana na vyombo hivi wakati maisha ya wananchi wetu yanahatarishwa na vyombo hivi. Alikuwa wapi kwenye matukio ya Arusha, Mbeya (Tukuyu), Tarime na Songea? Kote huku hakuonesha kujali sana lakini leo ameibuka na kuonesha kuwa ana uwezo wa kufuatilia vyombo vya usalama?

      Kama nilivyosema hapo juu vita si lelemama kama baadhi ya watu wanafikiria. Najua wapo ambao wanafikiria kuwa vita dhidi ya Uganda ilikuwa ni uamuzi wa haraka na papara. Wengi (labda vijana zaidi) wanakumbuka tu maneno ya "nia tunayo na sababu tunayo" lakini ni wachache (hata wazee yumkini) wanaokumbuka kuwa kabla ya kufikia maneno hayo Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alielezea juhudi mbalimbali za kutatua mgogoro wetu na Uganda licha ya "chokochoko" zilizoanza miaka karibu mitano nyuma. Kwa Tanzania kwenda vitani ilikuwa ni uamuzi wa mwisho pale ambapo njia zote za amani na kidiplomasia ziliposhindwa.

      Leo viongozi wetu tena wakubwa na wenye dhamana nzito zaidi wanazungumza kana kwamba tumeshindwa kabisa kutafuta njia za amani na za demokrasia na sasa wanataka kuifanya Malawi kama wanavyofanyia wananchi wetu. Wananchi wakiandamana wanapigwa virungu na kuuawa na wakigoma wananyamazishwa kwa ghafla. Na hata mazungumzo wanataka yawe kwa masharti yao. Matokeo yake wamejenga fikra wanaweza kum-bully mtu yeyote, vyovyote, na kwa lolote kiasi kwamba wanataka kuanza kuibully Malawi. Hili linafanywa kwa sababu moja tu kuwa Tanzania ni kubwa kuliko Malawi na inawezekana ina uwezo mkubwa wa kuishinda Malawi.

      Wanaozungumza hivi wanafikiria vita inapigwana na wingi wa watu tu na vitu. Vita ni mikakati na mbinu lakini vile vile vita ni kujitoa muhanga. Tunapozungumzia lugha ya vita sijui kama tunafikiria viongozi wetu wanaweza kuhamasisha taifa kama ilivyokuwa miaka ya 1970 ambapo watu walichangia kuku, mbuzi na ng'ombe. Wangapi kati yetu leo watakuwa tayari kutoa magari na mabasi yao kwenda vitani? Wangapi wataamua kwa hiari yao kwenda kupigana chini ya viongozi hawa hawa? Itakuwaje kama watu wakiwa vitani kashfa kubwa ya ufisadi nyumbani inanguruma tena (mafisadi kwa asili hawabadiliki).

      Tunapozungumzia vita tunazungumzia maisha ya watu kuuawa. Watu wasifikiri kuwa tukienda vitani na Malawi au nchi nyingine yoyote jirani basi tutakuwa kama tunamsukuma mlevi. Ni wangapi wanafikiria kulipuliwa kwa miji yetu inayozunguka ziwa Nyassa? Mbamba Bay, Kyela, Tukuyu, Rungwe, Mbeya, hata Songea? Kweli kina Lowassa wanapozungumza lugha ya vita wanafikiria kabisa kuwa tumesahau jinsi Amin alivyolipua Mwanza? au ndio viongozi wetu hata historia tena wamesahau? Au watu wamesahau jinsi tulivyolazimika kuchimba mahandaki na kufanya mazoezi ya kujihami hadi kuwa na kuku ndani kwa ajili ya kukimbia nao kwenye mahandaki? Au watu wameshasahau jinsi Idi Amin alivyoweza kuua mamia ya watu wetu pale vikosi vyake vilipovuka Mutukula na kuingia Kagera?

      Ninachosema ni kuwa ipo haja ya haraka ya viongozi wetu kuonesha hekima ya kukwepa lugha ya vita. Si kwa sababu hatuna uwezo wa kupigana na Malawi (naamini tunao tena mkubwa na naamini tunaweza kushinda) lakini bado hatujawa na sababu ya kufanya hivyo. Watu kudai "ziwa zima" wakati sisi tumejenga bandari na watu wetu wanavua na kuishi kwenye ziwa hilo na tuna meli miaka nenda rudi na Wamalawi hawajarusha hata baruti ni jambo la kutufanya tufikiri. Kama kweli Wamalawi wangekuwa wanataka vita au ugomvi mbona wao sababu "wanayo" kuwa tumeingilia Ziwa lao na tunafanya vitu kinyume cha sheria?

      Wamalawi walipozungumza kwa lugha ya Vita mara moja walitambua kuwa hakuna sababu ya ku-escalate tension kwenye eneo hilo hasa kwa vile tayari tumeshawahi kuwa na tension sana. Ndio maana Waziri wa Mambo ya Nje aliamua kupunguza makali ya lugha ya vita. NI wakati kwa viongozi wa TAnzania nao kupunguza ukali usio wa lazima na kuchochea lugha ya vita. Na sisi wananchi tusiuziwe kirahisi vita kwani ina gharama kuliko watu tunavyoweza kufikiria. Ikumbukwe vita ya Uganda iliigharimu Tanzania kuliko watu wengi wanavyojua na imeacha mojawapo ya majeraha makubwa katika mwelekeo wa uchumi wetu ambayo hadi leo tunasikia maumivu yake. Sijui kama tunataka vita nyingine hasa kwa sababu ambazo ni za kidiplomasia na kisiasa.

      Hekima itusukume kufikiria mara mbili. Tutoe nafasi kwa diplomasia na mazungumzo ya amani na nina uhakika wa Malawi kama ni watu wa amani watanyosha mkono wa amani. Njia mojawapo kama tukitaka na sisi kutumia mbinu za diplomasia ni hilo nililosema kwenye mada nyingine badala ya kupeleka vifaru na askari wetu karibu na Ziwa Nyassa na sisi tuanze utafiti kwenye eneo tunaloamini ni letu na kuwaacha Wamalawi wafanye kwenye eneo lao. Kama wanafanya hivyo kwenye sehemu ya eneo letu basi tuna sababu ya kuhakikisha hizo 'incursions' hazitokei na hapo ikibidana kuweka boti zenye silaha kuhakikisha hayo hayatokei.

      Endapo juhudi hizi za kuonesha sisi ni watu wa amani hazitapokelewa na kama juhudi za kidiplomasia zitashindwa na Wamalawi watapuuzia kabisa madai yetu na kuanza kutenda kanakwamba hatuna la kusema basi ni wakati huo Watanzania waandaliwe kwa kitu ambacho kinaweza kutokea - vita. Na hili lisizungumzwe na kila "dick, tom and harry" kwa sababu wanavaa suti za vyeo mbalimbali. Mtu pekee wa kuweza kulizungumzia hili kama uwezekano ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

      Endapo tutaacha wanasiasa ambao wanatafuta ujiko kwenye macho ya wananchi walizungumzia na kututia hamasa wakati wao wenyewe hawatoenda vitani na yawezekana hawana mtoto au ndugu hata mmoja JWTZ basi tutajikuta tunapelekwa vitani kisiasa na siyo kwa sababu tunatishiwa au tunajihami. Ni matumaini yangu viongozi wa upinzani (CHADEMA) hawatoingia mtego huu wa kuzungumza lugha ya vita. Hili waachiwe CCM na mashabiki wake mpaka pale ambapo juhudi zao za kisiasa zitakpokuwa zimeshindwa basi waseme tunaenda vitani na hapo viongozi wa upinzani watolee maoni na msimamo wao. Wapinzani wasizungumze lugha ya vita bali ya amani.

      Ndio maana kwa upande wangu ninaangalia sana watu wanaotaka kuwa ma-amiri jeshi wakuu, tusipoweza kuwaangalia wanavyoweza kutumia hekima watu hawa watakuja kutupeleka vitani na tukajikuta tunapigana na tukiulizwa tunapigania nini hatujui kumbe watu walitukaniana mama zao na taifa likaingizwa vitani. Na matumaini yangu JWTZ halitaingia kwenye hili suala la kisiasa na kidiplomasia. Tunataka JWTZ letu litakapozungumza iwe ni baada ya tangazo rasmi la vita nje ya hapo JWTZ iwaache wanasiasa wafanya mambo yao.

      Siasa na Diplomasia vikishindwa tujiandae kwa ushindi wa Kivita. Hapo ndio tutoe silaha zetu kibindoni na kuzielekeza kwani tutakuwa tayari kuzitumia.

      MMM
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. FemaTV & Radio

    3. #81
      Sheba's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th May 2009
      Posts : 199
      Rep Power : 553
      Likes Received
      83
      Likes Given
      34

      Default

      Quote By Matola
      Na wewe huwe na busara, huwezi kuquote uzi mzima halafu unareply mistari miwili hujui unawapa shida wanaotumia simu unnecessary? kwa nini usimmention Mzee Mwanakijiji??
      Kwa nini unatumia simu? Hilo sio tatizo langu ni lako.

    4. #82
      SALOK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2011
      Location : Some where!!
      Posts : 1,169
      Rep Power : 621
      Likes Received
      222
      Likes Given
      207

      Default

      Quote By masauni
      umesema vyema sana nakubaliana na wewe asilimia mia. Lakini nikusahihishe kidogo tu kuwa tanzania haina uwezo wa kuipiga malawi nina huakika na hilo.
      Pili ikitokea vita nina tamani sana tanzania ishindwe (mimi ni mtanzania ninaipenda sana nchi yangu tanzania.). hii inchi ya mafisadi ikipigwa then naamini kabisa itakuwa nchi ya watanzania baada ya vita.
      unakusudia mama, baba, dada, na wazee wauawe tu kwa vita ama unaamini mafisadi ndo watakao pigana!? Fikiri ndugu!!

    5. #83
      kwila's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 7
      Rep Power : 361
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Tatizo ni kuwa Wamalawi tangu uhuru wanajua kuwa ziwa lote ni lao, hata ramani zao zote zinaonyesha hivyo, pia utafiti hajauanzisha Joyce, tangu mtangulizi wake utafiti ulifanyika katika ziwa lote, wanachoshangaa kwa nini Watanzania wamesubiri wakati wa Joyce kudai ziwa, mbona hawakudai wakati Bingu anafanya utafiti

    6. #84
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,502
      Rep Power : 46710
      Likes Received
      16360
      Likes Given
      8419

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Quote By Bra-joe
      Mipaka ya nchi lazima ilindwe kwa gharama zote. Swala hili siyo la kisiasa ni la Taifa, hapa wa Tz wote viongozi na wananchi wote wake kwa waume tunatakiwa kuacha itikadi zetu za vyama na kuwa kitu kimoja.
      Umoja wa namna hiyo unafaa kwenye nchi za madikteta. Rais aliingize taifa vitani kwa sababu ambayo ingeweza kuepukika na sote tushabikie kwa sababu ya kuonesha "umoja"? Kama Malawi wangekuwa na nia mbaya tusingeweza kujenga bandari Mbambabay wala kuwa na meli na boti na uvuvi wa maelfu ya Watanzania kwenye ziwa hilo. Kama Malawi wanaoamini kuwa ziwa lote ni lao hawajaamua wala kutishia kwenda vitani kwa sababu tunatumia maji ya ziwa "lao" iweje sisi leo recklessly tuzungumzia mambo ya vita kwa sababu tu wao wanafanya exploration? Hawajazuia meli zetu, hawajaanza kufukuza wavuvi wetu kutoka ziwani?
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    7. #85
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,502
      Rep Power : 46710
      Likes Received
      16360
      Likes Given
      8419

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Quote By Democracy999
      Mwanakijiji kumbe una chuki kwa Lowassa na unaonekana LIVE, mbona unamtaja sana yeye kuliko Sitta alietangulia kwa kauli dhaifu ya eti hatutishwi na malawi?
      Sitta alizungumza kama kwa niaba ya JWTZ? Sitta ana madaraka gani katika mambo ya ulinzi na usalama ukimlinganisha na Lowassa?
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    8. Miaka 50

    9. #86
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,502
      Rep Power : 46710
      Likes Received
      16360
      Likes Given
      8419

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Quote By Ben Saanane
      Watu wengi wanadhani Diplomasia hufanikiwa bila Millitary Background.Diplomasia na hatua za kijeshi nyuma ya pazia ndiyo DIPLOMASIA yenyewe.Hili nililijadili sana kwenye thread iliyopita
      sasa hivi hakuna sababu ya kuzungumzia mambo ya military background ya kina Lowassa. Mambo ya kuzungumzia tuna uwezo, vifaa na teknolojia kuweza kupigana na Malawi yanakuja vipi? Diplomasia ambayo mtu kawekewa silaha kichwani ni diplomasia gani? Hamuwezi kuwa na diplomasia kama wote mmelekezeana silaha. La kwanza ni kuweka silaha chini ili kuzungumza.

      Wote tunajua Malawi ina jeshi na TZ inajeshi na tunajua kuwa majukumu ya majeshi haya ni kulinda mipaka. Haiitaji watu kuringishiana majeshi.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    10. #87
      Murrah's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Location : Tarime
      Posts : 191
      Rep Power : 442
      Likes Received
      40
      Likes Given
      9

      Default Suluhisho la Mpaka na Malawi

      Nashauru Serikali kuruhusu safe passage ya walechoka na wanchari Toka (Tarime) wanaopigana turaise jeshi twende Malawi tukagine huko hii haitakuwa mara ya kwanza kufanya hivyo tawala zote zilizotangaliwa zilifanya hivyo, ila tutakachoteka ni halali yetu. Kwa kufanya hivyo serikali itakuwa imejiondelea mizigo miwili kwa mara moja. Isitoshe most Malawian accept poofters, so we can bit them hand down

    11. #88
      KOMBESANA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2009
      Posts : 525
      Rep Power : 610
      Likes Received
      114
      Likes Given
      1460

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Mwanakijiji rafiki MWEMA<
      Tutakubaliana kwamba diplomasia ya kutatua migogoro haimaanishi kuwa taifa au jamii haina nguvu za kijeshi za kupambana na mvamizi.Maana yangu ya diplomasia ni kule kutambua kwamba vita ni gharama kubwa kwa pande zote tena kwa miaka mingi kiasi kwamba Sun Tzu anatuarifu kwamba hakuna mshindi wa vita!
      Hizi kauli za Waheshimiwa Sitta, Lowassa,na Membe ni kauli za kujaribu kufukia OMBWE la kiuongozi lililo wazi kwa yeyote kwa maneno yanayofanana na yale ya aliyekuwa Waziri wa Habari wa Kamandoo Saddam kuwa Jeshi lao lingewachinja Wamarekani wote waliojipeleka Baghdad!Kilichotokea ni historia .Tuwe makini na kauli hizi za kujitafutia jina kwamba eti Fulani anafanania fanania na Chief -in -Command Mtarajali!Diplomasia itumike, International Law itumike na baada ya hapo busara ISIYOKUWA YA WAHESHIMIWA Sitta,Membe,Lowassa na hata AMIRI JESHI MKUU WA SASA, itumike kabla ya option hatari isiyo ya ushindi ya VITA!

    12. #89
      KANA KA NSUNGU J's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th July 2012
      Posts : 23
      Rep Power : 348
      Likes Received
      10
      Likes Given
      0

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Mwana kijiji Nakuheshimu sana kwa makala zako.Lakini kwa hili nafikiri umeteleza tena sana.Si vyema kwa wakati huu kuonyesha kile unacho onyesha.Maana naona watu wengine wasio ishi katika maeneo husika baada ya kusoma comments zako wanasema bora tuwaachie wamalawi hilo ziwa.
      Suala la mpaka wa TZ na Malawi ni la kihistoria na umewahi leta hata mtafaruku kwenye mabunge ya Uingereza kipindi cha ukoloni mkongwe.Serikali yetu pia imeanza mazungumzo kwa mda mrefu pia.Ukianzia kwa awamu ya kwanza ilishindikana baada ya kuona Mawali ina sera tofauti na Tanzania ambapo sera ya TZ ilikuwa ni kusaidia nchi za afrika kujitawala wakati malawi ilikuwa ni maswahiba wa makaburu.Hali hiyo kwa malawi imeendelea mpaka leo hii maana nchi nyingi za africa zinapinga vikwazo vyo ulaya na marekani kuhusu Sudani na nchi zingine lakini Joyce Banda anaunga mkono.Pia nchi za Africa zimeukataa ushoga lakini malawi imeukubali na sababu ni kutaka tu misaada.
      Wakati wa awamu ya nne, kumekuwepo na mazungumzo ya nchi hizi mbili ambayo yanaongozwa na wataalam wa mambo haya kwa nchi zote mbili.Lakini cha ajabu ni kuwa pamoja na mazungumzo hayo kuendelea, wenzetu tayari wameingiza makampuni yao kwenye eneo linalogombaniwa pamija na kuambiwa wasitishe shughuli hiyo, sasa hapa ulitegemea amirijeshi wa Tanzania akampigie magoti Joyce ambembeleze?
      Kuna jinsi tofauti za ustarabu wa watu inabidi ujue.Kwa mkuu wa nchi kama Rais, jinsi anavyo tembea, kuongea , kukaa ,facial expression, gestures na body language ni lazima iwe tofauti na mwananchi wa kawaida kama mimi na wewe.Hiyo ni elimu ya kidiplomasia ambayo viongozi wetu hupewa.Mfano Obama anavyo wapiga piga mgongoni viongozi wenzie wa nchi nyingine si kuwa anafanya kwa bahati mbaya, hilo ni jambo alilofundishwa na limepangwa kuwa hivyo.Yeye kama baba wa dunia, kama wamarekani wote wanavyo amini ni kama vile baba anampongeza au kumtuliza mtoto wake kwa kumpigapiga mgongoni.
      Pia viongozi hawa wakubwa wakikutana ni lazima watazamane usoni kwa msisitizo na macho makavu huku maki "shake mikono".Sasa hapo kama raisi wako akianza kuangalia chini au pembeni na anajiuma vidole ndo itaonekana watanzania wote mabwege maana kumbuka hapo anaiwakilisha nchi.
      Pia jinsi ya kukaa wanapoongea pia ina mpangilio wake na mwisho ni kuwa hata kuingia kwenye mikutano, huwa kwa kwa maana ile ile wanajitahidi kuwa watu wa mwisho.Obama asingependa awe wa kwanza kuingia alafu Raisi toka malawi ndo awe wa mwisho, mara nyingi hapo kuna kuwa na busara kubwa za waandaaji wa mikutano hutumika.
      Juzi juzi tu wamalawi walikuja juu baada ya kuona Raisi wao Joyce akimsalimia malkia Elizabeth kama vile anachuchumaa wakati wote ni Head of states.Si tu wamalawi walichukia bali watu wote duniani walishangaa na HII NDIO SABABU WAMALAWI WAKO AGGRESSIVE SASA HIVI MAANA WANADHANI KILA MTU SASA ANATAKA KUINYANYASA MALAWI KWA SABABU WANAONEKANA KUDHARAULIWA KWA SABABU YA HICHO KITUKO.
      Kwa sababu hiyo hiyo , linapokuja swala la kuvamiwa mpakani, kiongozi wa nchi(au anayesema kwa niaba ya Raisi) hatakiwi awe na maneno ya kuremba ni kutoa maneno makavu na straight kama Membe,Sitta na Lowassa walivyo tamka.Hii haimaanishi wametangaza vita ila ni maneno ya kawaida kwenye position zao na siasa/diplomasia za kimataifa.Ndo maana hata Malawi hawajaomba msamaha ila wametumia lugha laini kuwa wataendelea na mazungumzo ila hawataacha utafiti maana ni eneo la kwao.Publicly wametunishiana misuri hivyo lakini nakuapia watakapo kaa kuongea, si kama ulivyo sikia waki tunishiana misuri.Hapo kila mtu alikuwa anaonyesha kuwa ni baba mlinzi imara kwa watoto wake hata kama kiukweli hana huo uwezo.
      Ninacho furahi kwa viungozi wetu, wametumia maneno mazuri kama vile "Tutatumia kila linalowezekana kuhakikisha kuwa tunatatua matatizo haya kwa njia za mazungumzo (eg mazungumzo ya kiusuluhishi na mahakama) na kama itatulazimu basi jeshi letu limejipanga vizuri sana" Hii ni kauli ya kistaarabu mno lakini ya kiuongozi.Si ya kutangaza vita bali ya kutaadharisha upande wa pili kuwa suluhu ni muhimu sana kwa sababu bila hiyo suluhu kuna option nyingine itakayo tugharimu wote(sisi na malawi)
      Kumbuka, kama wamalawi wataachwa waendelee na utafiti, halafu wakaanza kuchimba mafuta na gesi, basi itakuwa ni vigumu sana kuwatoa kwenye mpaka huo maana watakuwa tayari wamesha onja "Black gold (mafuta)"
      Sasa huoni kwamba baada ya hizo kauli malawi wameanza kulegeza kamba na wamesha anza kutuliza raia wake kwa kuwaambia wewe watulivu maana serikali yao itafanya mazungumzo na serikali ya TZ?
      Maana siku chache hapo nyuma tulipata shida sana kwa sisis tulio na access ya kufika malawi na kufanya nao mawasiliano ya mara kwa mara nao.Wengi wa Raia walikuwa wana tutukana sana na kueleza jinsi jeshi la malawi nililvyo imara na kwamba wako tayari kwa vita.Lakini baada ya kauli hii naona hao hao raia wame "panick"

      Nawasilisha Hoja

    13. #90
      Matola's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 12,514
      Rep Power : 19750
      Likes Received
      5443
      Likes Given
      3640

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Quote By Sheba
      Kwa nini unatumia simu? Hilo sio tatizo langu ni lako.
      Hivi unajijuwa kama wewe ni mjinga? ni wapi nilipokwambia mimi natumia simu?
      Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.

    14. #91
      Kima Mchanga's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Location : Dynamic
      Posts : 4,496
      Rep Power : 11225
      Likes Received
      605
      Likes Given
      446

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Umaarufu wa viongozi kwa gharama ya maisha ya watanzania haukubaliki hata kidogo!
      Do what you feel in your heart to be right-for yot will be criticized anyway.You will be damned if you do,and damned if you don't

    15. #92
      H1N1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th May 2009
      Posts : 1,356
      Rep Power : 779
      Likes Received
      290
      Likes Given
      288

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      MMM pamoja na maelezo yako fasaha,binafsi naona kama taifa tupo vitani tayari,tena vita kubwa na ghali kuliko vita ya kugombea mipaka ya ziwa moja tu. adui wetu mkuu kama taifa ni uongozi dhaifu na wa kifisadi wa taifa letu,uongozi unaoamini manunuzi ya magari ya kifahari kwenye barabara mbovu,uongozi unaoamini kwenye starehe kuliko afya na elimu.
      Hii vita ni kubwa na ni ghali sana.
      Watz tusitamani wa kuombea vita nyingine, tutumie nguvu zetu tulizonazo kwa mtu mmoja mmoja kwa nafasi yake pale alipo hata ndani ya majeshi yetu ili tushinde hii vita tuliyonayo kwanza,hayo mambo ya mpaka na malawi yaweza subiri ikibidi hata miaka 100 ijayo hadi tumalize na tushinde hii vita inayotukabili kama taifa.

    16. #93
      August's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2007
      Posts : 2,744
      Rep Power : 1162
      Likes Received
      251
      Likes Given
      2511

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Kauli ya Sitta haikuwa kali na ya kuogofya, bali ilikuwa kauli ya -re-assure wananchi wa tanzania usalama wao, na iliongelewa mahali panapostahili, bungeni baada ya suala hili kuulizwa na zaidi akasema kauli rasmi ya serikali itatolewa na waziri wa mambo ya nje.
      kauli zisizo faa zimetolewa na watu wawili walio fuatia, Koka la Mdimu na Kamati ya Ulinzi. Mdimu akiwa katika wizara tena inayo shughulikia diplomasia angekuwa mtu wa kwanza kuongelea hilo kuliko kuweka msisitizo wa vita, na mtu anaye kimbilia vita inaonyesha ni mtu dhaifu wa hoja au wa uhalisi wa jambo lenyewe, na si jambo jema kwa kiongozi wa namna hiyo kujaribu kudhalilisha nchi nyingine in public, mambo mengi yange fanyika behind the scene hii ndio inaitwa diplomasia. sasa tunavyo raise tension tunaonekana ni Taifa linalo penda kupigana pigana tu, na kauli ya kamati ya ulinzi na usalama nayo haikupaswa kutolewa,kwani hatujafikia huko? hatujasikia hata risasi moja toka upande wa pili kurushwa au raia au askari wetu kuuliwa au kunyanyaswa au hata vifaa vyetu kuharibiwa, na kama wanavyo sema watu walio karibu na mpakani kila mtu anaendelea na shughuli zake na uhusiano wetu bado upo mzuri kibiashara na kiujirani mwema. nafikiri Raisi anatakiwa kufanya reshufle ndogo huyu wa mambo ya nje ameisha jichafua na hili na kuichafua serikali yetu, na wa kamati ya ulinzi na usalama apewa naye kamati nyingine, na ni vizuri Raisi akatoa kauli iliyo nzuri kushusha hii tension tulio Raise bila sababu yoyote ili kuimarisha uhusiano wetu na watu wa Malawi.kwanza inakuwa ni sawa sawa na kugombania vifaranga ambavyo hata havijazaliwa -mafuta/gesi ya aslia?

    17. #94
      mgen's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 18th November 2010
      Posts : 5,579
      Rep Power : 3942
      Likes Received
      711
      Likes Given
      148

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Mkuu! Isije ikawa plan ya ccm ili kusiwepo uchaguzi 2015? kwa kisingizio cha hali ya hatari? manake lolote linawezekana kwa viongo wa aina ya hata nyasi mtakula?

    18. #95
      kanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 726
      Rep Power : 568
      Likes Received
      288
      Likes Given
      409

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Mwanakijiji nakuunga mkono, mimi nitakuwa mtu wa mwisho kuunga mkono vita hii ya kipumbavu.Vita ta Kagera Iddi Amini nusra atusamabaratishe, Muulize Kamanda yeyote aliyepigana vile vita atakwambia kuwa Id Amini alikuwa strong, kosa kwamba alikosa nguvu ya wananchi Entebbe na Kampala na vikundi vya waasi wengi waliokuwepo enzi hizo kama Museveni,Obotte na wengineo.WANANCHI WASIWAPE KIBURI VIONGOZI DHAIFU UJINGA WA KUSHABIKIA VITA.

    19. #96
      Nicholas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 5,014
      Rep Power : 3620
      Likes Received
      1285
      Likes Given
      2142

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Mwanakijiji umenena vyema, ila kuongea amani si mara zote kuna lead results kuwa amani.Huwezi amini this time CCM wamepiga bao,ingawa sijui kama kweli walipanga hivyo au ni coincidence.

      Hawa majirani zetu si wote wana akili timamu, kama wana timamu baso huwa wanazipeleka wanapojua.SI mara moja mipaka huwa majirani wanaingia na kufanya wapendalo na kuondoka, wamekuwa wakifanya jitihada nyingi sana hata kujaribu dilute watu wetu ili wajihalalishie mipango yao mirefu.

      Hawa jamaa Lugha ya Vita imekuwepo malawi long time.Na hawa jamaa ndio walikuwa uchochoro wa makaburu kufuata wapigananaji waliokuwa wameweka kambi sehemu mbalimbali Tanzania, Zambia, na hata Mozambique.So nadhani hicho kibarua chao kimewaingia sana kiasi wanajiona kuwa Tanzania ya rais anayeonekana kuwa dhaifu na watu hawezi linda nchi .Pia wanadhani wametushika by surprise.

      Nikirudi katika view zangu, Serikali sijui ni kwa woga au intentional wamepunguza tension at least by now.Na hao jamaa walio nyuma ya malawi pengine wamepiga mahesabu wakaona Bora waje Bonga kuchukua mikataba kuliko kuleta vita na wao wajiute pande zote mambo yanasimama au kupewa tabaka lingine.SI unajua tena Wakituboa wanajua china huwa hapati shida tubaka.Wakati waziri Membe akionyesha jumuia ya Kimataifa kuwa sisi bado tupo katika kusimamia Majadiliano.Ghafla akatokea Lowasa ambaye naye si wa serikali ila wanajua alichosema kama Mwenyekiti wa kamati Muhimu na mtarajiwa katika kugombea kupitia CCM.Yaani haina tofauti ya kumpa mtoto kauli ya kumfurahisha mbele ya wageni na kwa ujanja ukampa sura ya mauaji.Then ukamwambia twende nyumbani.

      Wamalawi wanapenda vita, wamalawi wanawa judge watanzania kwa kuangalia elimu na maendeleo ya watu walipakana nao wanaona kuwa pengine nchi mzima imechoka hivyo, nchi nzima ina watu wasiokuwa na elimu na pengine wajinga.Hawa vibaraka wa makaburu na wasaliti wa Africa si watu w akuamini sana,pamoja na umasikini wao.Sasa nadhnai ndio kipindi cha Tz kuweka wapelelezi wa kudumu huko na ikibidi tuanze pandikiza viongozi wetu, ili tuje wasignisha mikataba kirahisi na wasije ingia tena kwetu.

      MCHEZO HAPA UMEKUWA STICK AND CARROT.Ila Malawi na watanzania wameona stick, wangine wameona carrot.So magamba wameshaonyesha kufanikiwa zuia vita kabla ingawa sijui kama kweli waliplann hivyo, au katika kigugumizi kama cha EPA ,Mh EL akapiga hizo za nishikeni nisimvunje.Jamaa wakapata ujumbe kuwa wakajipange upya au waachane na hiyo habari.SOmetimes kuzuia vita ni kuingia full mkoko, adui mwenyewe akajiulize, au hata kichapo ch amwanzo kimfanye akajiulize kama kuna uwezekano wa kuchinda kwa chochote.
      SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.

    20. #97
      Ben Saanane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th January 2007
      Posts : 6,726
      Rep Power : 32786
      Likes Received
      4994
      Likes Given
      6456

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      sasa hivi hakuna sababu ya kuzungumzia mambo ya military background ya kina Lowassa. Mambo ya kuzungumzia tuna uwezo, vifaa na teknolojia kuweza kupigana na Malawi yanakuja vipi? Diplomasia ambayo mtu kawekewa silaha kichwani ni diplomasia gani? Hamuwezi kuwa na diplomasia kama wote mmelekezeana silaha. La kwanza ni kuweka silaha chini ili kuzungumza.

      Wote tunajua Malawi ina jeshi na TZ inajeshi na tunajua kuwa majukumu ya majeshi haya ni kulinda mipaka. Haiitaji watu kuringishiana majeshi.
      Kinachofanyika ni kitu cha kawaida kabisa kwenye medani za siasa za kimataifa.Kauli kama hizi zina detterence effect.
      Pia hii ni siasa ya kimataifa na tunakosea sana pale tunapoamini kwamba diplomasia inaweza kufanikiwa bila shinikizo.Suala la kuweka majeshi chini au kutoongelea millitary strength pia tutakosea na watu hawaelewi kwamba hata wakati wa vita Diplomasia bado inafanyika
      Kutatua migogoro kwa njia ya kidiplomasia kuna:
      -Kushawishi kabla ya kufikia hatua ya kutishana
      -Kukirimu/kuhonga kwa ushawishi wa raslimali au mamlaka
      -Lobbying ya kutafuta sapoti kwa jumuiya ya kimataifa
      -Shinikizo la kijeshi au shinikizo la vikwazo vya kiuchumi(coercion)
      -Ama vyote kwa pamoja

      Pia kinachofanyika ni kuondoa sasa hofu wananchi na kuongeza ari ya jeshi na kama nilivyosema kuleta detterence effect kwa nchi hasimu.Hii ni propaganda ya kidiplomasia na haiepukiki
      Wametuonyesha Jeuri ya ukaburu,tuwaonyeshe jeuri ya Umkhontho we sizwe kupitia Red Brigade.Tukiwaonyesha woga wetu, itakua silaha imara zaidi kwao kutumaliza-Ben Saanane

    21. #98
      August's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2007
      Posts : 2,744
      Rep Power : 1162
      Likes Received
      251
      Likes Given
      2511

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      tatizo ni haya matamko ya kulinda mipaka kuwa inajirudia rudia, alicho tamkaa Sitta bungeni ilikuwa inatosha, waziri wa mambo ya nje yeye alipopata nafasi ya kutoa official statement ya serikali alitakiwa kukazia hiyo diplomasia ya kutatua kwa mazungumzo,na kuwepo kwa exit strategy , mfano tukienda mahakama ya kimataifa tukashindwa na wewe ulisema utatumia jeshi itakuaje? pia kumbuka tunazungumzia siku hizi economic diplomacy,sas mtu mnaye pigana nae mtaongea naye nini mambo hayo, tusichukulie Malawi tunaishi nayo sikumoja bali maisha yetu yote. Mbona wao waliweza kumzuia Raisi wao kutoa hotuba na waziri wa mambo ya nje akatoa kauli ya ki-diplomasia, kwamba mazungumzo yanaendelea, hayo ya tarehe 27/07/12 na ujumbe wao wa bunge umekuja. Sasa ni vizuri Raisi wetu akafanya ziara Malawi au akatoa neno kupunguza mumkari huu.

    22. #99
      Ronal Reagan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 2,627
      Rep Power : 958
      Likes Received
      615
      Likes Given
      256

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Sharti mojawapo ni lazima hawa watatu watoe watoto wao wa kiume kuwa mstari wa mbele ktk vikosi ikiwa tutaingia vitani. Vita si mchezo!

    23. #100
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,131
      Rep Power : 41571
      Likes Received
      6038
      Likes Given
      1054

      Default Re: Wanasiasa na Lugha ya Vita: Hekima ya kupunguza sababu ya kuingia vitani na Malawi

      Quote By Ronal Reagan
      Sharti mojawapo ni lazima hawa watatu watoe watoto wao wa kiume kuwa mstari wa mbele ktk vikosi ikiwa tutaingia vitani. Vita si mchezo!
      Kwani wa kike hawawezi kupigania nchi yao?
      Banda lishavunjika, jogoo kaondoka. Vifaranga hangaika, kumtoa nyoka.


    Page 5 of 6 FirstFirst ... 3456 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...