Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

    Report Post
    Page 4 of 5 FirstFirst ... 2345 LastLast
    Results 61 to 80 of 82
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,106
      Rep Power : 19193
      Likes Received
      8049
      Likes Given
      26489

      Default Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Utangulizi


      Mtafiti mmoja kutoka Argentina, Boaventura Santos de Sousa, aliwahi kuandika kwamba ‘mwandishi ingawa huandika kuhusu yaliyopita huwa anajaribu kueleza yaliyopo, siyo yaliyopita. Lakini, kwa kufanya hivyo, huwa pia anajiweka mbali na hali ya sasa na kwa hakika anaandika kwa ajili ya siku zijazo’.


      Muungano wa Zanzibar na Tanganyika umepita katika masaiba kadhaa tokea kuasisiwa kwake takriban miaka 45 iliyopita lakini mtikisiko ulioukumba katika siku za karibuni ni mkubwa sana. Ni mkubwa kwa sababu umegusa kiini cha Muungano huu ambapo suala linaloulizwa ni iwapo kwa kule kukubali kushirikiana katika baadhi ya mambo, je, Zanzibar na Tanganyika zimejifuta na hivyo kupoteza hadhi zake kama nchi? Hilo limekuwa ndiyo suala kubwa linaloulizwa na Wazanzibari hasa baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutamka Bungeni kwamba Zanzibar si nchi.


      Hakuna awezaye kubisha kwamba tokea kuasisiwa kwake, Muungano huu umejengeka kutokana na misingi ya khofu, kutiliana shaka na kutokuaminiana baina ya pande mbili zinazouunda, ambako wakati mwengine kumepelekea hata kutishia uhai wa Muungano wenyewe.


      Muungano umekuwa gumzo kuu katika takriban kila mjadala wa katiba na siasa katika nchi yetu. Umejitokeza na kujionyesha hivyo katika mwaka wa mwanzo wa Muungano kuhusiana na sakata la kuwa na Ubalozi wa iliyokuwa

      Ujerumani Magharibi kwa upande wa Tanganyika na Ubalozi wa iliyokuwa Ujerumani Mashariki kwa upande wa Zanzibar, kuhusiana na uwakilishi wa Zanzibar katika Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki na uanzishwaji wa Benki

      Kuu ya Tanzania (BOT) mwaka 1964 – 1966, wakati wa kuunganisha vyama vya ASP na TANU kuunda Chama Cha Mapinduzi (CCM) mwaka 1977, katika mjadala wa marekebisho ya Katiba wa 1983/84 na hatimaye kujiuzulu kwa

      Rais wa pili wa Zanzibar Sheikh Aboud Jumbe, wakati wa kuondolewa katika Uwaziri Kiongozi kwa mwandishi wa makala haya na hatimaye kufukuzwa katika CCM na wenzake 6 mwaka 1988, katika harakati za madai ya kutaka

      kura ya maoni kuhusiana na Muungano huo mwaka 1989/90, wakati wa mjadala wa kuanzishwa vyama vingi mwaka 1991, katika sakata la Zanzibar kujiunga na Umoja wa Nchi za Kiislamu (OIC) mwaka 1993, wakati wa mjadala wa

      G-55 kudai kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano mwaka 1994, katika mjadala wa marekebisho ya 11 na 14 ya Katiba ya Muungano mwaka 1994/95, wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 1995 na ule wa 2000 na karibuni kabisa kuhusiana na suala la matarajio ya ugunduzi wa mafuta visiwani Zanzibar na harakati za kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki.


      Ukiondoa kuibuka kwake katika mijadala mikubwa ya kikatiba na kisiasa nchini, kwa upande mwengine katika uendeshaji wa shughuli za Serikali za kila siku, ‘matatizo na vikwazo kadhaa ya kiutawala na kiutendaji’ vimekuwa vikiripotiwa kila mara kwamba vinakwamisha uimarishaji wa Muungano.


      Tume na Kamati kadhaa zimeundwa kuainisha matatizo ya Muungano na kupendekeza njia za kuyatatua. Serikali ya Jamhuri ya Muungano imeunda Tume na Kamati zifuatazo, miongoni mwa nyingi, kuhusiana na masuala haya:



      1. Kamati ya Mtei
      2. Tume ya Jaji Francis Nyalali (1991)
      3. Kamati ya Shellukindo (1994)
      4. Kamati ya Shellukindo 2 ya kuandaa Muafaka juu ya Mambo ya Muungano baina ya SMZ na SMT.
      5. Kamati ya Jaji Mark Bomani (1995)
      6. Kamati ya Jaji Robert Kisanga (1998)
      7. Kamati ya 'Harmonization'
      8. Kamati ya Masuala ya Simu (Kamati ya Kusila)



      Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) nayo kwa upande wake iliunda Kamati zifuatazo kwa madhumuni hayo hayo:



      1. Kamati ya Baraza la Mapinduzi (Kamati ya Amina) ya 1992
      2. Kamati ya Rais ya Kupambana na Kasoro za Muungano (Kamati ya Shamuhuna) ya 1997
      3. Kamati ya Rais Kuchambua Ripoti ya Jaji Kisanga (Kamati ya Salim Juma Othman)
      4. Kamati ya Kuandaa Mapendekezo ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya Kero za Muungano (Kamati ya Ramia) ya 2000
      5. Kamati ya Baraza la Mapinduzi juu ya Sera ya Mambo ya Nje
      6. Kamati ya Rais ya Wataalamu juu ya Kero za Muungano ya 2001
      7. Kamati ya Baraza la Mapinduzi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki
      8. Kamati ya Mafuta
      9. Kamati ya Madeni baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Muungano wa Tanzania
      10. Kamati ya Suala la Exclusive Economic Zone (EEZ)
      11. Kamati ya Masuala ya Fedha na Benki Kuu
      12. Kamati ya Rais ya Masuala ya Simu (1996 –1999)
      13. Kamati ya Baraza la Mapinduzi juu ya matatizo na kero za Muungano na taratibu za kuyaondoa (2004)



      Ukiacha Tume, Kamati na Ripoti hizo, kuanzia mwaka 1985 kulianzishwa utaratibu wa Kamati ya Pamoja ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Waziri Kiongozi wa Zanzibar pamoja na Mawaziri wa Serikali zetu mbili ambao ulitarajiwa uwe ndiyo jukwaa la kuzungumzia matatizo kutoka kwa washiriki wakuu wa Muungano huu na kuyapatia ufumbuzi unaofaa. Utaratibu huu uliachwa kwa muda mrefu lakini sasa umerejeshwa upya kufuatia agizo la Rais Jakaya Kikwete alilolitoa katika mkutano na mawaziri na watendaji wakuu wa Serikali yake huko Ngurdoto, Arusha mwezi Februari, 2006.


      Mikutano, Makongamano, Semina na Warsha vimefanywa kujadili masuala haya na kupendekeza hatua za kuchukuliwa. Wasomi na wanafunzi wamefanya tafiti kadhaa na kujipatia shahada na stashahada hadi ngazi ya Ph.D juu ya Muungano lakini bado matatizo yako pale pale na yanaongezeka kila kukicha.


      Yanayoonekana na kuelezwa kama matatizo, mapungufu, dosari, kasoro na, kwa msamiati wa sasa, kero yamekuwa ndiyo yale kwa yale. Nini basi kiini cha haya? Na vipi tutayatatua?


      Mimi nimeamua kutoa changamoto kupitia waraka huu kwa kuitazama historia ya Muungano, jinsi ulivyoundwa, matatizo yanayoukabili, nafasi na hadhi ya Zanzibar katika Muungano na nini khatima ya Zanzibar na mustakbali wa Muungano huko tuendako. Nitakayoyaeleza yanaweza yakaonekana ni machungu kwa wakati huu wa sasa lakini kama asemavyo Santos de Sousa yanaweza yakawa ndiyo ufumbuzi kwa siku zijazo.




      Asili na Sababu za Muungano


      Maoni yanayotolewa kuhusu asili na sababu za Muungano yamekuwa yakitofautiana mno. Wapo wanaouleza Muungano huu kuwa ni wa pekee katika bara la Afrika, kwani ndiyo pekee ulioweza kudumu katika kutimiza azma na malengo ya kuleta umoja wa Afrika (Pan-Africanism),[2] na pia wapo wanauona kuwa ni ‘jaribio la kusisimia la ukoloni mdogo wa nchi moja ya Kiafrika kuiteka na kuitawala nchi nyengine ya Kiafrika.’[3]


      Kutokana na maelezo na hoja nyingi na zinazokinzana kuhusu asili na sababu za Muungano, si rahisi kusema moja kwa moja kuwa maelezo yepi au hoja ipi ni sahihi. Utangulizi (Preamble) wa Mkataba wa Muungano wenyewe unataja sababu kuu ya kuunganisha nchi za Zanzibar na Tanganyika kuwa ni ‘maingiliano ya muda mrefu ya watu wa nchi mbili hizi na mahusiano yao ya kidugu na kirafiki … na … kuendeleza umoja wa watu wa Afrika.’ Lakini miaka 45 sasa baada ya uzoefu wa Muungano huu, Wazanzibari wanajiuliza kweli haya ndiyo madhumuni ya Muungano huu?


      Wazo la kuungana linaweza kurudishwa nyuma tokea zama za harakati za ukombozi wa nchi za Afrika. Waasisi na wakuu wa harakati za kupigania Uhuru waliiona mipaka ya nchi zao iliyowekwa na wakoloni kuwa ni ‘mbinu za kibeberu’ zilizotekelezwa kwa ajili ya manufaa na maslahi yao. Kutokana na hisia hizo, mazungumzo ya kuanzisha aina fulani ya umoja miongoni mwa nchi huru za Afrika yalitawala duru za siasa katika miaka ya 5o na 60.


      Nadharia mbili zilijichomoza. Ya kwanza, ikishadidiwa na Kwame Nkrumah wa Ghana, ilikuwa ikitaka kuasisiwa kwa nchi moja tu ya Afrika nzima iliyoungana ikiwa na Serikali moja kwa bara zima. Nadharia hii ilipingwa na baadhi ya viongozi, wakiongozwa na Julius Nyerere waTanganyika, ambao walisisitiza haja ya kuanza na miungano ya maeneo (regional unions) chini ya mfumo wa Shirikisho badala ya kuwa na mpango wa Serikali moja.[4]


      Katika kulifikia lengo hilo, viongozi wa kisiasa wa nchi tatu za Afrika Mashariki – Kenya, Ugandana Tanganyika – walikuwa wakifanya mikutano ya mara kwa mara kipindi chote cha kati ya mwaka 1961 na 1963 kuona jinsi gani wanaweza kutimiza ndoto hiyo. Mfumo wa Muungano uliokuwa ukiandaliwa ulikuwa ni ule wa Shirikisho. Tamko la Pamoja la viongozi hao lilisema:


      “Sisi, viongozi wa wananchi na Serikali za nchi za Afrika Mashariki … tunayakinisha nia zetu kuhusu kuwepo kwa Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki. Mkutano wetu wa leo unasukumwa na hisia za umoja wa Afrika (Pan-Africanism), na siyo tamaa za maslahi binafsi ya eneo hili. … Ijapokuwa Zanzibar haikuwakilishwa katika mkutano huu, tunapaaswa kuweka bayana kwamba nchi hiyo inakaribishwa kushiriki kikamilifu katika mikutano yetu kwa ajili ya uundwaji wa Shirikisho .”[5]


      Lakini Umoja wa Afrika (Pan-Africanism) hauonekani kuwa ndiyo dhamira pekee au kama ndiyo dhamira halisi ya Muungano. Wengi wanaamini, na mimi nikiwa mmoja wao, kwamba dhana hiyo ilitumiwa tu kuficha njama za muda mrefu za Nyerere kutaka kuimeza na kuitawalaZanzibar. Katika mwaka 1961, wakati Tanganyika inakaribia kupata Uhuru wake, Nyerere alinukuliwa akisema:


      “If I could tow that island [Zanzibar] out in the middle of the Indian Ocean, I would do it … I fear it will be a very big headache for me.”[6]


      Yaani, “Kama ningekuwa na uwezo wa kuvikokota visiwa vile [Zanzibar] na kuvitupa nje kabisa, katikati ya Bahari ya Hindi, basi ningefanya hivyo … Nakhofia vitakuja kuniumiza kichwa sana”.


      Imani hii inatiliwa nguvu na mahusiano ya karibu na ya muda mrefu yaliyokuwepo kati ya chama kilichokuwa kikitawala Tanganyika, TANU, na ASP ambacho kilishika hatamu za utawala baada ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964, mwezi mmoja tu baada ya Zanzibar kupata uhuru wake kutoka Uingereza hapo Desemba 10, 1963. Zilikuwepo taarifa tokea mwaka 1959 kwamba TANU na ASP zitakaposhika madaraka zitaziunganisha nchi mbili hizi kuwa Jamhuri moja.


      Wakati juhudi za kuanzisha Shirikisho la Afrika Mashariki zikiwa zinafifia, Nyerere aliona fursaZanzibar ambayo hakutaka kuipoteza. Katika mazungumzo ya siri kati yake na Rais Abeid Amani Karume wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, wakakubaliana kuziunganisha nchi mbili hizi. Hakukuwa na ushirikishwaji wa aina yoyote ule wa wananchi wa nchi hizi mbili katika maamuzi haya makubwa. Usiri uliogubika hatua hii kubwa unafichuliwa na si mwengine bali Nyerere mwenyewe pale aliposema:


      “[Tanganyika] tulipeleka polisi wetu Zanzibar. Baada ya kuyashinda matatizo kadhaa tukaungana. Sisi wenyewe kwa khiyari zetu tulikubaliana kuungana. Karume na mimi tulikutana. Peke yetu wawili tu tulikutana. Nilipomtajia wazo la Muungano, Karume hakufikiri hata mara mbili. Pale pale alinitaka kuita mkutano wa waandishi wa habari kutangaza azma yetu. Nilimshauri asubiri kidogo kwani ilikuwa bado ni mapema mno kuweza kuviarifu vyombo vya habari.”[7]


      Taarifa hizi ziliendelea kubaki kuwa siri hadi tarehe 26 Aprili, 1964 pale Redio ya Tanganyika ilipotangaza kwamba siku hiyo Marais wawili hao watakutana katika Bunge la Tanganyika kubadilishana Hati za Muungano ambazo zimeunganisha Zanzibar na Tanganyika kuwa Jamhuri moja. Hivyo inaonekana wazi kwamba tokea awali Muungano huu ulikosa ridhaa ya watu. Haukuwa Muungano wa watu, ulioundwa na watu, kwa maslahi ya watu. Bali ulikuwa na umeendelea kuwa ni Muungano uliosimamishwa kwa ridhaa ya watawala pekee.




      Kiini cha matatizo ya Muungano


      Ukitazama kwa jicho la sheria, kiini cha matatizo ya Muungano kinatokana na tafsiri ya Mkataba wa Muungano (Articles of Union) wa 1964. Hizi ndizo hati zinazounda, kupitia mkataba wa kimataifa, Jamhuri ya Muungano. Suala kubwa lililoumiza na linaloendelea kuumiza vichwa vya wengi na hivyo kuendelea kuulizwa ni mfumo gani wa Muungano ulikusudiwa kuwekwa na Mkataba huu? Ni muungano wa moja kwa moja (unitary) au wa shirikisho (federal)?


      Mfumo uliopo sasa ambao ulianza kutekelezwa 1964 ni ule wa serikali mbili – ile ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Zanzibar. Tanganyika haikuwekewa serikali yake tofauti; madaraka yake kwa yale mambo yasiyo ya Muungano yalielezwa kwamba yatasimamiwa na kuendeshwa na Serikali hiyo hiyo ya Jamhuri ya Muungano. Hata hivyo, uhalali wa kisheria wa muundo huu umeendelea kuhojiwa na hata kupingwa kwamba hauwakilishi ipasavyo makusudio yaliyomo katika Mkataba ulioanzisha Muungano wenyewe.


      Mkataba wa Muungano wenyewe hauelezi bayana aina au mfumo wa muungano inaouanzisha lakini uko wazi kuhusiana na mgawanyo wa madaraka (distribution of power) inaouweka na idadi ya mamlaka (number of jurisdictions) zitakazokuwepo. Ibara ya (iii) (a) ya Mkataba huo inaanzisha ‘Bunge na Mamlaka ya Utendaji’ (Parliament and Executive) ndani ya na kwa ajili yaZanzibar ikiwa na mamlaka kamili kuhusiana na mambo yote yasiyo mambo ya Muungano kwaZanzibar. Kwa upande mwengine, Ibara ya (iv) ya Mkataba huo inaanzisha ‘Bunge na Mamlaka ya Utendaji’ (Parliament and Executive) ya Jamhuri ya Muungano ikiwa na mamlaka kamili katika eneo lote la Jamhuri ya Muungano kuhusiana na mambo ya Muungano na, pia, ikiwa na mamlaka kamili ndani ya, na kwa ajili ya Tanganyika kuhusiana na mambo yote yasiyo mambo ya Muungano kwa Tanganyika. Kwa hivyo, katika sehemu ya pili, mamlaka mbili tofauti zimechanganywa pamoja.


      Mjadala mkubwa na mkali umekuja kuhusiana na tafsiri ya Ibara hiyo ya (iv) na kule kuchanganya kwake mamlaka mbili hizo.


      Haya si masuala ya kisheria tu kama ambavyo baadhi yetu wanataka tuamini (ingawa nayo ni muhimu mno kama ilivyodhihirika hivi karibuni), bali pia ni masuala ya kisiasa kwa vile yanahusisha uwezo wa maamuzi, madaraka na mamlaka, na zaidi mchango wa gharama za uendeshaji na mgawanyo wa rasilimali na mapato kati ya wahusika wakuu. Mambo haya, katika uzoefu wa nchi za wenzetu, ndiyo yaliyopelekea kuvunjika kwa miungano yao kwani huzaa kutiliana shaka na kutokuaminiana. Kwa vile yanachukua sura ya kisiasa (kutokana na sababu nilizozitaja), haya hayana chama wala itikadi kama nitakavyoonyesha huko mbele. Kamaalivyowahi kusema Prof. Issa Shivji:


      “Ultimately, the question of the Union is primarily a political question and no amount of rhetoric about blood and cultural ties will matter when it comes to realpolitik.”[8]


      Yaani, “Mwisho wa yote, suala la Muungano linabakia kimsingi kuwa ni suala la kisiasa, na inapofikia kwenye siasa hasa, hotuba na kauli kali za jazba kuhusiana na mahusiano ya damu na ya kidugu, zote hazitafaa kitu.”


      Kwa hakika, kinyume na inavyojaribiwa kuonyeshwa na wengi kwamba Tanganyika imepoteza kila kitu katika muundo huu wakati Zanzibar imekabidhi sehemu tu ya madaraka yake, muundo wa Serikali mbili umepelekea wengi

      kuamini kwamba kilichofanyika ni kiini macho tu kwani ni Zanzibar iliyokabidhi sehemu muhimu ya mamlaka yake (mahusiano ya nchi za nje, ulinzi na usalama, uraia, kodi na ushuru, sarafu, nguvu kuu za kuendeshea uchumi na

      mengineyo) kwa Tanganyika na kisha Tanganyika ikajigeuza jina na kujiita Jamhuri ya Muungano. Na haya si maoni ya ngumbaru (kwa lugha ya Mwalimu Julius Nyerere) bali ni maoni ya watu wazito wakiwemo aliyekuwa Spika wa

      Bunge na ambaye sasa ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa ambaye alisema kwa jinsi mambo yalivyofanyika, Zanzibar inaonekana kama vile ni‘invited guest’ (mgeni aliyealikwa) katika Muungano.[9] Naye

      msomi mashuhuri ulimwenguni, Prof. Ali Mazrui alisema baada ya Muungano Zanzibar imepoteza kila kitu muhimu wakatiTanganyika imebadilika jina tu na kuwa Tanzania huku ikiwa na mamlaka zaidi lakini ikibaki na Rais wake, nembo yake ya Taifa, wimbo wake wa Taifa na hata kiti chake katika Umoja wa Mataifa.[10]




      Mkataba wa Muungano haujafuta Serikali ya Tanganyika


      Katika makubaliano ya kimataifa yaliyounda Muungano, ambayo hata hivyo katika muda wote wa uhai wa Muungano yamekuwa hayafuatwi, hakuna kifungu hata kimoja kilichotoa au kuagiza kwamba Serikali ya Tanganyika ifutwe kwa

      mujibu wa makubaliano hayo. Serikali ya Tanganyika, kama ilivyo ile ya Zanzibar, imelindwa na kifungu cha (v) kinachosomeka kwamba: “The existing laws of Tanganyika and of Zanzibar shall remain in force in their respective territories”.Kinachosemwa hapa ni kwamba “Sheria zilizopo za Tanganyika na za Zanzibar zitaendelea kufanya kazi na kuwa na nguvu katika maeneo yao.”


      Wataalamu wa katiba na sheria wanafahamu kwamba katiba ndio sheria mama ya sheria zote za nchi. Hivyo Katiba ya Tanganyika imelindwa na inapaswa kuwepo na Serikali yake iwepo, pamoja na viongozi wake kuwepo na

      kusimamia mambo yasiyo ya Muungano. Katiba na sheria zaTanganyika ndizo zilizotakiwa zitumike katika eneo la Tanganyika kwa yale mambo yaliyokuwa hayamo kwenye Muungano kama ambavyo Katiba (au kabla ya hapo Matangazo ya Kikatiba –Constitutional Decrees) na sheria za Zanzibar zinavyotumika katika eneo la Zanzibar kwa yale mambo ambayo si ya Muungano. Hiyo ndio tafsiri ya ‘maeneo yao’.


      Wazanzibari wanafahamu kwamba Serikali ya Tanganyika imefutwa kwa makusudi na Bunge laTanganyika kinyume na Makubaliano ya Muungano ili kujipa nafasi kuitumia Serikali ya Muungano, kama kwamba ndio Serikali ya Tanganyika. Lengo ni hatimaye kuiuwa Serikali yaZanzibar na kufanya Tanganyika mpya ikiwa na jina jipya la Tanzania lenye mipaka mipya, yaani kuwa nchi moja yenye Serikali Moja.


      Hiyo ndio ghilba iliyofanywa na viongozi wa Tanganyika mara baada ya kuwekwa saini makubaliano. Kwa kusaidia kufichuwa ukweli wa hadaa hii, msomaji anashauriwa asome Sheria Na. 22 ya mwaka 1964 inayoitwa “Union of Tanganyika and Zanzibar Act, 1964.”


      Sheria hii ilipitishwa na Bunge la Tanganyika Aprili 25, 1964, siku moja kabla Muungano kuanza kufanya kazi. Ilikusudiwa kuthibisha kukubalika Muungano huo wa Tanganyika na Zanzibarupande wa Tanganyika (ratification). Kifungu cha (viii) cha Makubaliano ya Muunganokinaagiza ifanyike hivyo kwa pande zote mbili za Muungano.


      Inasikitisha kusoma katika kifungu Na. 2 cha sheria hiyo kwamba:


      “Existing law means the written and unwritten law as it exists immediately before Union Day but does not include the Constitution of Tanganyika in so far as it provides for the Government of the Republic of Tanganyika or any declaration or law or any provision which expires with effect from commencement of the Interim Constitution”.


      (“Sheria iliyopo maana yake ni sheria iliyoandikwa na isiyoandikwa kama ilivyo kabla tu ya siku ya Muungano lakini haijumuishi Katiba ya Tanganyika kwa mintaraf ya kuiweka kwake Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika au tamko, sheria au kifungu chochote ambacho kinafutika kwa kuanza kufanya kazi Katiba ya Muda (ya Muungano)).”


      Kwa hivyo, wakati Bunge la Tanganyika linapitisha sheria ya kuridhia, ratify, kuwepo kwa Muungano kwa upande wa Tanganyika, sheria hiyo ilianza kupinga vifungu vya makubaliano hayo. Mfano mwengine ni kifungu Na. 7 cha sheria hiyo kinachosema:


      “On the commencement of the Interim Constitution of the United Republic of Tanganyikaand Zanzibar, the Constitution of Tanganyika will cease to have effect for the Government of Tanganyika as a separate part of the United Republic”.


      (“Itapoanza kufanya kazi Katiba ya Muda ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika naZanzibar, Katiba ya Tanganyika itasita kuwa na maana kwa Serikali ya Tanganyika kamasehemu moja ya Jamhuri ya Muungano.”)


      Kwa maneno mengine, sheria ambazo zilitakiwa zitumike kwa Tanganyika kwa mambo ambayo si ya Muungano zilipewa maana mpya kwamba eti zisijumuishe Katiba ya Tanganyika.


      Jambo moja lililo wazi, pamoja na hatua hii ya kuifuta Katiba ya Tanganyika, ni kwamba kule kuendelea kutambua kuwepo kwa sheria nyengine za Tanganyika bado kunamaanisha kuwepo kwa mamlaka ya Tanganyika ambako sheria hizo kwa mambo yote yasiyo mambo ya Muungano ziliendelea na zinaendelea kutumika hadi leo.


      Zaidi, inapaswa ifahamike kwamba kufuta Katiba ya Tanganyika kulikofanywa na vifungu vya sheria hii hakukubadilisha makubaliano yaliyokwishatiwa saini kati ya Serikali mbili zilizounda Muungano, yaliyosema kwamba sheria za nchi mbili hizi zitaendelea kutumika katika maeneoyao. Bunge la Tanganyika, na hata hili la Muungano, halikuwa na mamlaka kutafsiri vifungu vya Mkataba wa Muungano.


      Utaratibu wa kisheria ni kwamba kama Mkataba ulitakiwa kutafsiriwa basi ni walioandika rasimu ya mkataba huo ndio walipaswa kutoa tafsiri ya vifungu vyake, tafsiri ambayo ingepaswa iwe sehemu ya Mkataba huo. Na wala makubaliano yale hayakufuta wadhifa wa Rais wa Tanganyika. Si hivyo tu, bali pia Katiba ya Muungano ambayo ilitakiwa iwe ya muda tu kwa mwaka mmoja(interim) ilikuwa ni ile ya Tanganyika iliyofanyiwa marekebisho kwa ajili ya kutumika kwa Serikali ya Muungano.


      Haikuruhusiwa kutumika kuiongoza Tanganyika kwa sababu Tanganyika ilikuwa na Katiba yake na Rais wake. Mwalimu Nyerere alikuwa na vyeo viwili, Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Makubaliano na Katiba ya Muungano na Rais wa Tanganyika kwa mujibu wa Katiba ya Tanganyika, kama alivyokuwa Mzee Karume ambaye alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Makubaliano na Katiba ya Muungano na akaendelea kubaki kuwa Rais wa Zanzibar kwa mujibu wa Tangazo la Katiba ya Zanzibar (Constitutional Decrees).


      Hivyo ndivyo makubaliano yalivyo hadi hii leo. Waliobadilika ni watu tu. Kufanya vyenginevyo ni kinyume na makubaliano yale na ndio sababu ya migogoro ya Muungano. Yaliyofanyika ni ujanja uliokuwa hauna nia njema kwa Zanzibar kama alivyosema Prof. Issa Shivji, mtaalamu wa Katiba wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.


      “Lakini yote ya kuepusha Serikali ya Tanganyika kuwepo yalifanywa kwa makusudi kabisa, ili itumike Serikali ya Muungano kama ndio Tanganyika. Katika Sheria ile Na. 22 ya 1964, Rais wa Tanganyika amejipa madaraka ya kutunga na kutoa maagizo yanayohusu Muungano kwa kutumia amri (decrees) za sheria ya Tanganyika.
      Siku ile inapopitishwa sheria ile zilipitishwa pia Decrees mbili zilizotokana na vifungu Na. 6 (3), cha 8 na cha 5 cha sheria hiyo Na. 22 ya 1964, yaani The Provisional Transitional Decree 1964, na ile ya Interim Constitution Decree 1964 ambazo zote hazikuwa halali maana ni Decrees zilizopitishwa na Bunge la Tanganyika zilizotokana na Sheria Na. 22 ya 1964 ya Tanganyika.”


      Miongoni mwa mambo yaliyodhihirisha kuwa hakukuwa na nia njema katika Muungano huu tokea awali ni pale wafanyakazi wa Serikali ya Tanganyika wote walipopandishwa vyeo kwa pamoja na kuwa wafanyakazi wa Muungano kama kifungu cha 3 (1) cha Provisional Transitional Decree kinavyosema:


      “Every person who holds office in the service of the Republic of Tanganyika immediately before the Union Day, shall on Union Day be deemed to have been elected, appointed or otherwise selected to the corresponding office in the service of the United Republic.”


      Yaani kila mfanyakazi aliyekuwa wa Serikali ya Tanganyika mara kabla ya siku ya Muungano kufumba na kufumbuwa, pengine kwa uchawi wa kifimbo cha Mwalimu Nyerere, anakuwa mara moja mfanyakazi wa Serikali ya Muungano kuanzia siku ya Muungano. Huu tuuiteje kama si ujambazi wa kikatiba (constitutional banditry)?


      Vivyo hivyo, kifungu cha 6 (i) cha Decree kinasema mara tu baada kuanza Muungano, Mahkama ya Tanganyika na Majaji wake wote nao watakuwa ndio Mahkama na Majaji wa Jamhuri ya Muungano kinyume na Makubaliano ya Muungano. Mpaka leo Katiba zote mbili hazitambuwi Mahkama (ukiondoa Mahkama ya Rufaa) kama ni suala la Muungano. Nembo ya Tanganyikainatumika kama nembo ya Serikali ya Muungano na Idara ya Mwanasheria Mkuu wa Tanganyikainachukuliwa kama Idara ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Muungano.


      Haya yote hayamo na ni kinyume na Makubaliano ya 1964. Yote haya na kile kifungu cha 7 cha Sheria Na. 22 ya 1964 kinachofuta kuwepo kwa Serikali ya Tanganyika hayakubadilisha na wala hayana mahusiano na Makubaliano ya Muungano ya 1964. Yote haya yalifanywa na Bunge la Tanganyika kwa maslahi ya Tanganyika nje ya Makubaliano.


      Aliyekuwa Spika wa Bunge na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Mheshimiwa Pius Msekwa, analifahamu vyema suala hili. Katika waraka wake alioutoa kwenye Semina kuhusu Muungano hapo Hoteli ya Mkonge, Tanga tarehe 25—27 Februari 1994 anasema:


      “The Transitional Decree, 1964 published on 01/05/64, transferred persons who were holding office in the public service of the Republic of Tanganyika to the corresponding office in the public service of the United Republic of Tanzania. By the same decree the High Court of Tanganyika also became the High Court of UnitedRepublic of Tanzania and the public seal of Tanganyika became public seal of theUnited Republic.”


      Athari za hatua hizi kwa Zanzibar ziko wazi. Tanganyika imejigeuza Tanzania na imechukua mamlaka ya mambo muhimu ya Zanzibar huku ikijipa hadhi ya kuwa juu ya Serikali ya Zanzibarkinyume na Mkataba wa Muungano. Hii ndiyo siri ya viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kung’ang’ania mfumo wa Serikali mbili na kukataa kata kata mabadiliko yoyote ya mfumo huo kwani Tanganyika inanufaika nao kwa kuwa yenyewe ndiyo imekuwa ‘Muungano’. Kukubali muundo wa Serikali tatu ni kuzifanya Tanganyika na Zanzibar ziwe na hadhi na fursa sawa katika Muungano, jambo ambalo Tanganyika hailitaki maana kulikubali ni kukubali kupoteza fursa zote inazozipata hivi sasa kwa kujikweza kwake na kujifanya kuwa ndiyo ‘Muungano’.


      Ushahidi wa wazi wa hoja yangu hii ni kwamba mtu anapoangalia taasisi zote za Muungano zilizoundwa chini ya Katiba au sheria za Muungano ambazo zinazikutanisha Serikali mbili zilizopo sasa, ataona kuwa wajumbe wanaowakilisha upande wa Serikali ya Muungano wote ni kutoka Tanganyika. Hoja inayojitokeza ni kwamba Serikali ya Muungano ni ya shirika ambapoZanzibar ni sehemu ya ushirika huo, kwa nini basi wajumbe wanaowakilisha Serikali hiyo ya Muungano watoke upande wa Tanganyika peke yake? Jawabu ni rahisi. Serikali ya Muungano kwa hakika ni Serikali ya Tanganyika iliyojivika joho la Muungano.


      Rais Jakaya Kikwete amekaririwa hadharani akisema matatizo ya Muungano hayatokani na muundo bali yanasababishwa na viongozi. Hoja, maelezo na mifano niliyoitoa hapo juu inatosha kumuonyesha Rais kwamba kauli yake si sahihi. Vyote viwili – muundo na pia kukosekana kwa nia njema upande wa viongozi – ni sababu za kuwepo kwa matatizo yasiyokwisha ya Muungano.


      Sisi katika CUF tumesema wazi kwamba kuna haja ya kuuimarisha Muungano wetu kwa kurekebisha kasoro hii ya msingi. Njia ya kufanya hivyo ni kuzionyesha wazi wazi mamlaka zote tatu zilizomo katika Mkataba wa Muungano ili kuondosha khofu za kudhani mmoja anafaidika katika muundo huu na mwengine anakandamizwa. Serikali ya Zanzibar ionekane wazi wazi, Serikali ya Tanganyika ionekane wazi wazi, na Serikali ya Muungano ionekani wazi wazi. Hapo hapatakuwa na hofu ya mkubwa kummeza mdogo, wala mdogo kupendelewa na kupewa uwakilishi unaozidi kiwango chake.




      Uvunjwaji wa Mkataba wa Muungano


      Mbali na suala la muundo wa Muungano, maeneo mengine mengi yanayogusa msingi wa Mkataba wa Muungano yaliendelea kuvunjwa na Serikali ya Tanganyika ikivaa joho la Muungano.


      Kifungu cha (viii) cha Mkataba wa Muungano kinaweka sharti kwamba Mkataba huo hautokuwa halali hadi pale Bunge la Tangayika na Baraza la Mapinduzi likishirikiana na Baraza la Mawaziri la Zanzibar yatakapopitisha sheria za kuridhia Mkataba huo. Upo ushahidi wa kutosha kwamba Bunge la Tanganyika lilikutana na kuuridhia Mkataba huo tarehe 25 Aprili, 1964. Hakuna ushahidi wowote kwamba Baraza la Mapinduzi likishirikiana na Baraza la Mawaziri la Zanzibaryalikaa kuuridhia Mkataba huo. Kwa hakika ushahidi ulioibuliwa na Prof. Issa Shivji katika kitabu chake cha karibuni kabisa, Pan-Africanism or Pragmatism? Lesssons of Tanganyika-Zanzibar Union umeweka wazi pasina chembe ya wasiwasi kwamba Mkataba huo haujaridhiwa na upande wa Zanzibar hadi hii leo. Ndiyo kusema, Mkataba wa Muungano haujapata uhalali wa kisheria hadi leo.


      Kifungu cha (iii) cha Mkataba wa Muungano kiliorodhesha mambo 11 tu ambayo ndiyo yaliyokubaliwa na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika kuwa mambo ya Muungano. Hata hivyo, kipindi cha miaka 45 ya Muungano kimeshuhudia mambo hayo yakiongezwa isivyo halali kwa kutumia chombo kisicho na mamlaka ya kufanya hivyo yaani Bunge la Muungano na sasa kufikia 23 lakini ukiyanyumbua yanafikia 35. Ikumbukwe kwamba kila hatua ya kuongeza mambo ya Muungano maana yake ni kuchukua mamlaka ya Zanzibar na kuyahaulisha kwa Serikali ya Muungano ambayo kama tulivyokwisha onyesha kwa hakika hasa ni Serikali ya Tanganyika.


      Kifungu cha (vii) cha Mkataba huo kinataka Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mashauriano na makubaliano na Makamu wa Rais ambaye pia ni Rais wa Zanzibar kuunda Tume ya Katiba kwa lengo la kutayarisha rasimu ya Katiba ya Kudumu ya Muungano na baadaye kuifikisha rasimu hiyo mbele ya Bunge la Katiba (Constituent Assembly) litakalokuwa na wajumbe idadi sawa kati ya Zanzibar na Tanganyika kama watavyokubaliana viongozi hao wawili. Hatua hii muhimu sanakikatiba ilitakiwa itekelezwe ndani ya kipindi cha mwaka mmoja tokea tarehe ya Muungano. Hadi hii leo hakuna Tume ya Katiba iliyoundwa wala Bunge la Katiba lililoundwa na kuitishwa kwa madhumuni ya kupitisha Katiba ya Kudumu ya Muungano. Kilichofanyika ni kuwa siku moja kabla ya kumalizika mwaka mmoja uliotakiwa, Bunge la Muungano lilitakiwa kupitisha sheria ya kuahirisha kwa muda usiojulikana tarehe ya kutekelezwa kwa hatua hii na hadi leo imesahaulika kabisa.


      Lakini mbali na dhoruba hizo dhidi ya Mkataba wa Muungano, rungu kubwa zaidi ambalo ndilo lililotumika kuimaliza Zanzibar lilikuwa ni kule kuunganishwa kwa vyama vya ASP na TANU na kuzaliwa CCM huku ikijipa madaraka juu ya vyombo vyengine vyote vya maamuzi katika nchi ikiwemo Serikali na Bunge na Baraza la Wawakilishi. Chini ya dhana ya Chama kushika hatamu(Party Supremacy) iliyoasisiwa na Mwalimu Nyerere kwa lengo la kujilimbikizia madaraka yeye na Chama alichokuwa akikiongoza kama milki yake binafsi, CCM iliweza kutoa maagizo na maamuru mazito bila ya kujali madaraka ya Serikali ya Zanzibar yaliyotolewa kupitia Mkataba wa Muungano na hivyo kujinyakulia uwezo wote wa kuitawala Zanzibar ipendavyo huku viongozi wa Zanzibar wanaohoji wakituhumiwa kwamba wanapinga nidhamu ya Chama.




      Matatizo yatokanayo na kiini cha tatizo


      Kiini cha tatizo la msingi la Muungano ambalo kwa mtazamo wa CUF ni muundo wake unaotokana na tafsiri potofu ya Mkataba wa Muungano (Articles of Union) ndicho kimepelekea kujitokeza kwa matatizo mengine katika miaka 45 hii na ambayo yanaongezeka kila uchao.


      Mtu anapoangalia matatizo au hizi zinazoitwa kero atagundua kuwa karibu yote yanatokana ama na mshirika mmoja (mara nyingi Zanzibar) kutokuuamini au kuutilia shaka upande mwengine, au mshirika wa pili (mara nyingi Tanganyika ikivaa joho la Muungano) kuamini kwamba ina haki ya moja kwa moja kuamua na kutekeleza mambo fulani bila ya kulazimika kupata ridhaa ya upande wa pili ambao inahisi kama imeubeba tu. Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa tatizo linarudi kwenye muundo. Zanzibar haifahamu mamlaka ya Muungano katika Serikali ya Muungano yanaishia wapi ambapo mamlaka kwa mambo yasiyo ya Muungano kwa ajili yaTanganyika yanaanza. Tanganyika nayo kwa ‘kuwemo’ kwake katika Serikali ya Muungano kunaifanya ‘ishindwe kufahamu’ ni vipi na wapi Zanzibar inapata mamlaka ya kuhoji mambo ambayo ‘yameshatamkwa’ kwamba ni ya Muungano hata kama hayakuwemo katika Mkataba wa asili wa Muungano. Hali hii inaonekana katika kila kile kinachoitwa ‘kero’ za Muungano.


      Mifano inaweza kutolewa kwa takriban mambo yote, lakini kwa madhumuni ya waraka huu tuchukue mifano ya mambo matatu yafuatayo yanayozusha malalamiko:



      1. Umilikaji wa Mafuta na Gesi asilia.




      1. Uchangiaji katika gharama za Muungano na mgawanyo wa mapato yanayotokana na Muungano.




      1. Uwakilishi wa Zanzibar katika Bunge la Muungano.



      Umilikaji wa Mafuta na Gesi asilia


      Kwanza, kuingizwa kwake katika orodha ya mambo ya Muungano (kama ilivyo kwa mambo mengi yaliyoongezwa baadaye) hakukufuata taratibu za Serikali ya Muungano (ambayo pia ni Serikali ya Tanganyika kwa mambo yasiyo ya Muungano) kuishauri na kupata ridhaa ya Zanzibar. Pili, Zanzibar inataka kujua ikiwa mafuta yanapaswa kuwa suala la Muungano na hivyo mapato yatakayopatikana yanufaishe pande zote mbili, kwa nini madini mengine yanayopatikana Bara kama vile dhahabu, almasi au tanzanite hayakufanywa pia kuwa ya Muungano na hivyo kunufaisha pande mbili pia? Kwa hivi sasa, ambapo si mambo ya Muungano, mapato yake yanaponufaisha Tanganyika peke yake, yanaingia katika mfuko (account) upi wa matumizi? Tatu, ikiwa mapato yatakayopatikana kutokana na mafuta yataingia katika mfuko wa Muungano, kuna uhakika gani wa kutumika kwa shughuli za Muungano tu wakati hakuna mifuko tofauti ya fedha kwa shughuli za Muungano na zile za Tanganyika zisizo za Muungano?


      Uchangiaji katika gharama za Muungano na mgawanyo wa mapato yanayotokana na Muungano


      Je, mtu anaposema Zanzibar haichangii gharama za uendeshaji wa vyombo na taasisi za Muungano kwa sababu tu Serikali ya Zanzibar haitoi fungu la fedha na kuliingiza katika Serikali ya Muungano, Tanganyika ambayo hata

      Serikali haina inachangia vipi na kiasi gani? Ikiwa mchango wake unatolewa na Serikali ya Muungano, kwani hii siyo serikali ya shirika ambapoZanzibar ni mbia? Vipi basi Zanzibar itakiwe ichangie mara mbili kwa kutumia hadhi mbili

      tofauti? Na ikichangia (iwapo itachangia), ina uhakika upi kwamba itakachotoa hakitatumiwa na Serikali ya Muungano kwa shughuli za Tanganyika zisizo za Muungano ikitumia mamlaka yake kwa madhumuni hayo? Vivyo

      hivyo kwa mapato yatokanayo na vyombo na taasisi za Muungano, tunajua Zanzibar inapata mgao wake na kiasi chake kimewekwa wazi (ingawa hakikubaliki kwa Wazanzibari). Masuala yanakuja: Yale mapato yanayobaki katika

      Serikali ya Muungano, kuna kipi cha kuonyesha mpaka wa matumizi yake kwa Muungano na kwa shughuli za Tanganyikazisizo za Muungano? Uadilifu na uwajibikaji wa matumizi yatokanayo na mgao huu wa mapato utaonekana vipi?


      Uwakilishi wa Zanzibar katika Bunge la Muungano

      Wananchi wengi wa Tanganyika wanahoji vipi Zanzibar iliyo ndogo na ambayo ina watu wasiozidi milioni moja inawakilishwa na wabunge wa kuchaguliwa 50 wakati Dar es Salaam yenye wananchi wengi zaidi ina wabunge wa kuchaguliwa 7 tu? Wabunge hawa

      wanashiriki mijadala yote ya Bunge ikiwemo ya mambo yasiyo ya Muungano (ambayo kwa usahihi yatakuwa ni mamlaka ya Tanganyika kwa mambo yasiyo ya Muungano yanayosimamiwa na Serikali ya Muungano). Wanapata wapi uhalali wa kufanya hivyo

      wakati Wazanzibari hawapangiwi shughuli hizo (kwa mfano elimu, afya, kilimo, maji, umeme, habari, michezo, biashara, viwanda,

      serikali za mitaa n.k.) na Serikali ya Muungano wala hawasimamiwi katika mambo hayo na Bunge la Muungano? Uko wapi mpaka wa mamlaka ya Wazanzibari katika ushiriki wa Bunge hilowakati wao wana Serikali yao inayopanga na Baraza la Wawakilishi lao linalosimamia mamboyao kama hayo yasiyo ya Muungano?


      Mifano hii inatosha kuonyesha kwamba karibu matatizo yote, kama si yote, yanatokana na mkanganyiko na mgongano wa maslahi kati ya pande mbili ambao nao unasababishwa na mfumo usio wazi kuhusiana na mgawanyo wa madaraka kati ya mamlaka tatu za Muungano zinazotambuliwa katika Mkataba wa Muungano.


      http://mfumokristo.blogspot.com/2012...akbali-wa.html
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Study Abroad

    3. #61
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,106
      Rep Power : 19193
      Likes Received
      8049
      Likes Given
      26489

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Ibambasi
      Aisee,

      Mi kuna kitu nashindwa kuwaelewa wa-ZNZ, kama Muungano hamuutaki kwa nini mnakosa uthubutu wa kutoka? Ikiwa hayo ndiyo maoni yenu kwa nini msitumie vyombo vyenu, mf. BLW kuomba kuondoka katika Muungano?
      Quote By Mkandara
      Hawawezi maana ndio unawaweka Mjini..
      Quote By JokaKuu
      Mkandara,


      ..Tunatakiwa tuvunje mahusiano yoyote yale ya KIKATIBA.


      ..ZNZ wanataka mamlaka kamili kujiamulia mambo yao.


      ..Hawataki kuwepo na mamlaka yoyote ile itakayokuwa juu ya Raisi wa Jamhuri ya watu wa ZNZ.


      ..Ukileta masuala ya Raisi wa muungano, tayari unakuwa umekwenda kinyume na matamanio, na matarajio, ya Wazanzibari.


      ..Kuhusu ZNZ kuwa free-port hilo waachiwe wa-ZNZ waamue wenyewe wakiwa nje ya muungano.


      ..Lakini pia ukumbuke kwamba na sisi wa-Tanganyika tunataka kuanzisha viwanda vyetu na kuwa kama India na China. Sasa ukituletea free-port hapo ZNZ na kufanya ndiyo kichaka cha ukwepaji kodi, nini itakuwa hatima ya viwanda vyetu huku Tanganyika??


      ..Zaidi, kama muelekeo ni Tanganyika kuwa dampo la bidhaa za India na China, kwanini hiyo free port isiwe Tanga au Mtwara badala ya ZNZ?? Sote tunaelewa kwamba soko liko Tanganyika,DRC,Burundi,Rwanda, and beyond. Katika mazingira hayo kwanini bidhaa iteremshwe ZNZ halafu ipakiwe tena kwenye boti umbali wa masaa kadhaa kuletwa Tanganyika??




      ..Mwisho, nadhani wa-Tanganyika tuanze kufikiria jinsi ya kuboresha hali yetu ya kiuchumi na kijamii. Mara nyingi sana naona viongozi wa Tanganyika wako kimbelembele kutatua matatizo ya wa-ZNZ na kuwaacha wa-Tanganyika waki-suffer.


      ..Mfano mmoja ni habari zilizochapishwa magazetini hivi karibuni. Iliripotiwa kwamba serikali imemtengea Dr.Bilali bil 32 kwa ajili ya maendeleo ya ZNZ. Wakati huohuo serikali ikatenga sh bilion 19 kwa ajili ya elimu ya msingi na sekondari kwa Tanganyika nzima.


      ..Haki ya Mtanganyika iko wapi? Lini mmesikia wa-ZNZ wakitupatia mabilioni ya fedha kwa ajili ya maendeleo ya Tanganyika?? MUUNGANO UVUNJWE HATA KESHO, LET ZNZ GO!!!
      Quote By Nguruvi3
      Hakuna Mtanganyika anayeitaka ZNZ kwa taarifa yako. Ndiyo maana sisi hatutaki serikali 3, mkataba, mkataba wa Uswiss, Muungano wa CUBA na Marekani wala mahusiano maalumu.

      Kama unafuatilia maoni ya katiba, kila mahali WZN wanataka serikali 3 kwasababu ZNZ ni tegemezi Kwa Tanganyika ndani na nje ya muungano. Kiuchumi tunaweza kuimaliza ZNZ kabisa. Mathalani Tanga ikiwa bandari huru, ZNZ kwisha!

      Jussa wa CUF juzi katika gaezti la Habari leo ameikiri kuwa wanataka serikali 3. Jussa ni Mzanizbar Mshirazi mwenye asili ya Uarab, ndevu na rangi ya dhahabu siyo feki wala zao la utumwa lakini bado amekiri wanataka serikali 3.

      Maalimu Seif hapo juu amebaki anababaika na serikali 3 au mkataba, hivi huo si ushahidi kuwa wanaong'ang'ania muungano ni wao. Huyu alikuwa waziri kiongozi lakini hana uthubutu wa kusema vunja muungano. Salimin alishindwa seuse Seif

      Lakini pia tunawezaje kuwazuia WZN ili hali wana Rais, Makamu wawili, BLW, Baraza la Mapinduuzi, Wabunge, Mwanasheria, Baraza la Mawaziri, Mahakama kuu na ya rufaa ya kwao, wimbo, bendera ya taifa. Unapokuwa na vitu kama hivyo ukashindwa kuvitumia kisheria kuvunja muungano basi ujue kuna jambo na tatizo.

      Tunasema hivi wanaong'ang'ania ni WZNZ 350,000 wanaoishi Tanganyika.
      Leo ZNZ ikivunja muungano hakuna athari zozote Tanganyika, hakuna

      Tumewaambia ondokeni, wao hawataki wanasema serikali 3, mkataba n.k. Juzi gazeti la Habri leo la tarehe 7 Makamu wa pili wa Rais ametusoma hapa JF na kuwaambiwa WZNZ kuwa hawana elimu ya kile wanachokidai. Amesema wanaosema serikali 3 au mkataba ni kwa mambo gani hawasemi akiwemo Waziri kiongozi mchochezi wa zamani Maalim Seif Shariff Hamada Mshirazi

      Tumewaauliza manguli akiwemo Maalim Seif watuatajie nini wanachodhani kiwe cha Muungano, wote wanazunguka zunguka hakuna mwenye hoja yenye mashiko.

      Wanaogopa kusema hivi, hawana bajeti ya kutosha, hawana ardhi ya kutosha, hawawezi kujilinda kiusalama, na kwamaba ustawi wa ZNZ unategemea soko la watu milioni 40 wa Tanganyika siyo Comoro, Kenya au Uganda.
      Sasa hivi ZNZ ina access na nchi hizo nje ya muungano hawana mpaka na mwingine isipokuwa Tanganyika.

      LET ZNZ GO! HATA IKIBIDI USIKU HUU KUAMKIA KESHO. WE DON'T NEED ZNZ IOTA!
      Msikilize Baba wa Taifa Mwalim Nyerere ailisema hivi ( Katika mwaka 1961, wakati Tanganyika inakaribia kupata Uhuru wake, Nyerere alinukuliwa akisema:


      “If I could tow that island [Zanzibar] out in the middle of the Indian Ocean, I would do it … I fear it will be a very big headache for me.”[6]


      Yaani, “Kama ningekuwa na uwezo wa kuvikokota visiwa vile [Zanzibar] na kuvitupa nje kabisa, katikati ya Bahari ya Hindi, basi ningefanya hivyo … Nakhofia vitakuja kuniumiza kichwa sana”.) sasa inawaumizaVichwa Kisiwa Cha Zanzibar Wa Tanganyika.Mkuu.@
      Ibambasi Mkuu Mkandara Mkuu JokaKuu Mkuu Nguruvi3
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    4. #62
      Nonda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th November 2010
      Location : Gongo La Mboto
      Posts : 5,797
      Rep Power : 1858
      Likes Received
      933
      Likes Given
      367

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Zanzibar pushes to join island alliance to confront climate change


      The East African archipelago of Zanzibar is attempting to win “environmental independence” from Tanzania by joining an organisation that promotes the sustainable development of islands in the Indian Ocean.
      Zanzibar has lodged a formal membership application with the Indian Ocean Commission (IOC), a regional cooperation body whose current members are Comoros, Mauritius, Seychelles, Madagascar and Reunion.

      Although Zanzibar is a semi-autonomous part of Tanzania, officials in the archipelago’s own government, as well as some scientists, maintain that the isles have different needs from the mainland in dealing with climate change.

      Backers of Zanzibar’s entry into the IOC argue that membership will help it deal more effectively with environmental threats. Parts of the islands suffer from beach erosion, flooding and high salinity in arable land, which is itself scarce.


      The United Nations has recognised that “small island developing states” (SIDS) have particular needs and vulnerabilities in regard to sustainable development and climate change. Three IOC members – Comoros, Mauritius and Seychelles – are recognised as SIDS.

      Zanzibar hopes to gain status as a non-UN member of SIDS through the IOC, in order to gain much-needed technical and financial support to adapt to climatic change.

      Observers say the challenge facing Zanzibar will be to persuade the mainland government of the United Republic of Tanzania (URT), which represents Zanzibar in almost all international climate change negotiations, to allow the isles to gain recognition as one of the SIDS in order to deal with climate change issues, rather than remaining part of the Group of 77 nations, of which Tanzania is a founding member.

      Sanju Deenapanray, an IOC official, noted that the G-77 “seemingly caters for comparatively bigger economies like China and India among other countries ... (rather) than small island economies.”

      Terezya Huvisa, environment minister in the Tanzanian government, said she could not say whether Zanzibar’s move to join IOC was valid until the issue had been discussed at a quarterly meeting between the vice-presidents of the URT and Zanzibar, due around the middle of the year.

      Huvisa added that while the environment was not officially a union matter, the precedent was to treat environmental issues of Zanzibar and the mainland jointly.

      “This matter will have to be discussed jointly for Zanzibar to join the IOC,” she said.

      Kelly Horton, an environmental scientist with Earth Systems Africa, argued in a 2011 research paper on “Climate Change Governance in Zanzibar: The Need for Environmental Autonomy", that Zanzibar’s vulnerability to climate change is worsened by its inability to present its specific challenges in the international arena.

      According to Horton, while Zanzibar in general “self-funds attendance at international environmental meetings, it is unable to push a small-island agenda, falling under the wing of the Tanzanian mainland, who do not represent SIDS interests.”

      She said Zanzibar “requires specialist skills and support to effectively adapt to challenges of climate change,” which can include sea level rise and more extreme weather.

      link Zanzibar pushes to join island alliance to confront climate change - AlertNet

    5. #63
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By MziziMkavu
      Msikilize Baba wa Taifa Mwalim Nyerere ailisema hivi ( Katika mwaka 1961, wakati Tanganyika inakaribia kupata Uhuru wake, Nyerere alinukuliwa akisema:


      “If I could tow that island [Zanzibar] out in the middle of the Indian Ocean, I would do it … I fear it will be a very big headache for me.”[6]


      Yaani, “Kama ningekuwa na uwezo wa kuvikokota visiwa vile [Zanzibar] na kuvitupa nje kabisa, katikati ya Bahari ya Hindi, basi ningefanya hivyo … Nakhofia vitakuja kuniumiza kichwa sana”.) sasa inawaumizaVichwa Kisiwa Cha Zanzibar Wa Tanganyika.Mkuu.@
      Ibambasi Mkuu Mkandara Mkuu JokaKuu Mkuu Nguruvi3
      Hivi nikujibu mara ngapi hotuba hiyo? nadhani kuna hoja zangu nyingine huzisomi maana nilishaandika mwanzo tu wa mada hii..
      JokaKuu likes this.
      Exploration of reality

    6. #64
      Ibambasi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th July 2007
      Location : Iponyamakalai - Isungang'holo
      Posts : 724
      Rep Power : 753
      Likes Received
      118
      Likes Given
      762

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Mkandara
      Alaaa hata mfano basi au naposema mke wewe unachukulia nawatukana kwa sababu uwezo wa mwanamke ni hafifu kwenu hivyo ni matusi?.. Wahi futur isifanye kufur, mimi bado hadi saa tatu usiku. Ukirudi utayakuta yamejaa tele kama pichi..

      Haya niseme mke wangu miye sio wako, hawezi kuleta fedha alizoahidiwa na mwanamme ndani ya nyumba pasipo kushauriana nami. Na usichukulie naposema Mke ukaona nawadhalilisha nyie maana kwangu mke mume sote ni wamoja, uwezo sawa na nafasi sawa ndani ya ndoa tena mwanamke ana mamlaka zaidi. Ningekuwa mwanamke ningesema Mume wangu hawezi kuleta hela alizoahidiwa nje na mwanamke kuziingiza nyumbani. Halafu Hivi ni nani naibu waziri wa Membe vile?..
      Kwi kwikwiiiii!!

      Bob Mkandara we mkororfi sana, yaani kumpa huo mfano wa mke tu Mzizimkavu tayari jazba ishampanda! By the way hizo ndizo hoja za Wa-ZNZ mpaka unashidnwa kuelewa wakiwa wenyewe free and autonomous kama wanavyotaka sijui watajiongozaje!
      Mkandara likes this.

    7. #65
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Nonda
      Zanzibar pushes to join island alliance to confront climate change


      The East African archipelago of Zanzibar is attempting to win “environmental independence” from Tanzania by joining an organisation that promotes the sustainable development of islands in the Indian Ocean.
      Zanzibar has lodged a formal membership application with the Indian Ocean Commission (IOC), a regional cooperation body whose current members are Comoros, Mauritius, Seychelles, Madagascar and Reunion.

      Although Zanzibar is a semi-autonomous part of Tanzania, officials in the archipelago’s own government, as well as some scientists, maintain that the isles have different needs from the mainland in dealing with climate change.

      Backers of Zanzibar’s entry into the IOC argue that membership will help it deal more effectively with environmental threats. Parts of the islands suffer from beach erosion, flooding and high salinity in arable land, which is itself scarce.


      The United Nations has recognised that “small island developing states” (SIDS) have particular needs and vulnerabilities in regard to sustainable development and climate change. Three IOC members – Comoros, Mauritius and Seychelles – are recognised as SIDS.

      Zanzibar hopes to gain status as a non-UN member of SIDS through the IOC, in order to gain much-needed technical and financial support to adapt to climatic change.

      Observers say the challenge facing Zanzibar will be to persuade the mainland government of the United Republic of Tanzania (URT), which represents Zanzibar in almost all international climate change negotiations, to allow the isles to gain recognition as one of the SIDS in order to deal with climate change issues, rather than remaining part of the Group of 77 nations, of which Tanzania is a founding member.

      Sanju Deenapanray, an IOC official, noted that the G-77 “seemingly caters for comparatively bigger economies like China and India among other countries ... (rather) than small island economies.”

      Terezya Huvisa, environment minister in the Tanzanian government, said she could not say whether Zanzibar’s move to join IOC was valid until the issue had been discussed at a quarterly meeting between the vice-presidents of the URT and Zanzibar, due around the middle of the year.

      Huvisa added that while the environment was not officially a union matter, the precedent was to treat environmental issues of Zanzibar and the mainland jointly.

      “This matter will have to be discussed jointly for Zanzibar to join the IOC,” she said.

      Kelly Horton, an environmental scientist with Earth Systems Africa, argued in a 2011 research paper on “Climate Change Governance in Zanzibar: The Need for Environmental Autonomy", that Zanzibar’s vulnerability to climate change is worsened by its inability to present its specific challenges in the international arena.

      According to Horton, while Zanzibar in general “self-funds attendance at international environmental meetings, it is unable to push a small-island agenda, falling under the wing of the Tanzanian mainland, who do not represent SIDS interests.”

      She said Zanzibar “requires specialist skills and support to effectively adapt to challenges of climate change,” which can include sea level rise and more extreme weather.

      link Zanzibar pushes to join island alliance to confront climate change - AlertNet
      @Nonda, Mkuu wangu jaribu sana kufikiria nje ya box halafu utaelewa kwamba Zanzibar haihitaji kujiunga na chombo chochote ktk maswala ya Maendeleo yake isipokuwa maendeleo yao yataletwa na Wazanzibar wenyewe..Vyombo vyote hivi vinaundwa na watu wa nje kwa malengo ya kibiashara. hawakusaidii wewe ila wewe ni teja lao na ndio maana jumuiya hizi zinazidi kuongezeka kila kukicha. Na lengo kubwa ni kuzitumia nchi maskini kukopesha mtaji, technologia on sale na kuwaweka ktk utumwa wa mikopo na misaada ambayo sasa hivi ndio ngazi kuu ya utajiri kwa nchi tajiri.

      Huyo mtaalam mmoja tu anapokuja zanzibar analipwa zaidi ya Usd 10,000 kwa mwezi zaidi ya malipo anayopokea kwao ama Mzanzibar aliyezaliwa na kukulia hapo akijua hata mabadiliko ya vipindi bila kufumbua macho. Huyu mtaalam unamlipia wewe na sio shareholders waliounda SIDS. Elewa hiyo SIDS ni watu wamebuni biashara na wanategemea kutengeneza fedha kutoka kwa wateja wake wa Comoros, Mauritius, Seychelles, Madagascar, Reunion na sasa Zanzibar..Nyie mtakuwa mateja tu, hawa jamaa hawawasaidii isipokuwa mnauziwa huduma ya elimu zao ktk technologia badala ya kuwafundisheni elimu ya technologia, ili kesho muifanye kazi hiyo wenyewe..

      Hiyo IMF kupitia UN ni kitega uchumi cha Marekani na shareholders ndio maana hukuona Greece au Spain wakipewa Mkopo na IMF..watajikopeshaje?.. wao wanatafuta nchi mazuzu kama siye, na hakuna mfuko wowote unaweza kusaidia wananchi technical and financial support ati kwa jili ya climate change pasipo wewe kulipia kwa gharama kubwa. Mimi nakuuliza hivi, Kwa nini Wazanzibar wasijifunze wenyewe elimu hiyo? Kwa nini sisi tunategemea zaidi ahadi za mikopo na misaada hata ya elimu badala ya sisi wenyewe kupeleka vijana wetu wakajifunze mabadiliko haya?. Pengine nakuomba pitia hapa IMF upate kuwasoma jinsi gani mashirikisho haya yanavyotengeneza fedha badala ya kusaidia nchi maskini.

      Nachoweza kubaliana na wewe ni Tanzania kujiunga na OIC ikiwa kweli mikopo yao ina nafuu maana riba ndio hasidi wa maendeleo ya nchi zote maskini. Na inasikitisha sana leo hii duniani hapa tunajiita nchi za kiislaam wakati tunachukua mikopo yenye riba iwe Saudia ama Afghanstan ukienda IMF the list ni kubwa sana toka imeanzishwaiowanachokifanya ni kubadilisha jina tu..Hata hizo benki nchini wanachokifanya ni kibaya zaidi ya riba..

      Wanatumia fedha za watu kuwekeza lakini faida inatokana na thamani ya hisa inavyopanda inakatiwa riba, hivyo wallstreet, mikopo, misaada yote hii ni haramu. Tena niseme ukweli kama tunafuata dini haswa, basi hutakiwi hata kuweka fedha zako Benki maana hawa wanafanya biashara kubwa kwa kukuwekea fedha zako kwa malipo madogo kabisa..

      Benki za Kiislaam ni sawa na NSSF au PPF wanavyofanya kazi unaweka fedha zao leo miaka kumi baadaye imeshuka thamani na ndivyo ulipoumia wewe, halafu unajiuliza kwa nini NSSF isiwajengee hata nyumba wanachama wake kuongeza thamani za fedha zao. Isiwape mikopo ya kusomesha watoto wao ama mambo yanayoijenga jamii badala ya kuiweka ktk mashaka zaidi kwa kuhujumu nguvu zao kubwa walizoweka ktk miaka 40 ya kuajiriwa. Huu ni wakati wetu sisi kuamka na sio kuendelea kulala ktk usingizi mzito wa kusubiri misaada na sijui UAE wametuahidi bil200..
      Last edited by Mkandara; 10th August 2012 at 17:43.
      Nonda likes this.
      Exploration of reality

    8. Miaka 50

    9. #66
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,248
      Rep Power : 3039
      Likes Received
      3033
      Likes Given
      4113

      Default

      Quote By MziziMkavu
      Hakuna Kiongozi wa Serikali iliyopo Madarakani anaye zungumzia Kuvunjika kwa Muungano mpaka sasa mkuu Mkandara. Wanaye Zungumzia Suala la Kuvunja Muungano ni wananchi walala hoi Masikini

      Wazawa wa KiZanzibar ndio wanaotaka huo Muungano uvunjike wananchi wamechoshwa na Kero za Muungano mimi niliwahi kuwauliza Wa Zanzibar munachotaka kitu gani wakasema hatutaki Muungano tunachotaka tuwe huru wa kujiamuliwa mambo

      yetu wenyewe nikasema lakini nyinyi mupo wachache mpaka suala hilo walikubali Wenzenu wa Tanganyika walinirukia kiasi cha kutaka kunipiga na kusema kwenda zako wewe na hao Wa Tanganyika sisi tumesha choka na huo Muungano wenu

      tunachotaka tuwe huru Hatuutaki huo Muungano sasa Mkuu ikiwa kama ni wewe uliye wahoji hao Wa Zanzibar na hawautaki huo muungano utasema kitu gani Mkuu Mkandara
      Kwa nini mlichagua viongozi wasiowakilisha mawazo ya wananchi??

      Huo ndo ukenge wenyewe sasa.
      Nimesoma majibizano yako na Mkandara, nakushauri kwanza uache ku- copy na ku- paste maandiko ya watu bila aknowledgement.

      Pili, rudi bongo ukamrithi shekhe Yahaya, huna kitu... Si unajua ninafagamu uzuri profession yako?? Rudi utapata wateja.

      Acha siasa, post picha tu ndo unaweza.

    10. #67
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,248
      Rep Power : 3039
      Likes Received
      3033
      Likes Given
      4113

      Default

      Quote By Mkandara
      Hivi nikujibu mara ngapi hotuba hiyo? nadhani kuna hoja zangu nyingine huzisomi maana nilishaandika mwanzo tu wa mada hii..
      Mkuu Mkandara, wala aihitaji mtu anayefikiria nje ya box kuweza kujua ni kwa nini baadhi ya hawa majirani zetu wabafikiri kujiunga na jumuia fulani fulani ndo maendeleo yatakuja.... Hii ni akili ndogo ikifikiria vitu vidogo.
      Akili ya kufikiria kupewa, kusaidiwa, and the like!!!

      Wanawezaje kuchagua viongozi wasiotetea kuvunjika kwa mungano kama ndio watakacho wazanzibar??
      Hawa si ndio walimtukana Mh Tundu Lisu?? Wakamdhihaki?

      Sasa wa Zanzibar ndo akina nani kama viongozi wao wanasema mengine??
      Mkandara likes this.

    11. #68
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,818
      Rep Power : 2965
      Likes Received
      2417
      Likes Given
      3484

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Mkandara

      Nachoweza kubaliana na wewe ni Tanzania kujiunga na OIC ikiwa kweli mikopo yao ina nafuu maana riba ndio hasidi wa maendeleo ya nchi zote maskini. Na inasikitisha sana leo hii duniani hapa tunajiita nchi za kiislaam wakati tunachukua mikopo yenye riba iwe Saudia ama Afghanstan ukienda IMF the list ni kubwa sana toka imeanzishwaiowanachokifanya ni kubadilisha jina tu..Hata hizo benki nchini wanachokifanya ni kibaya zaidi ya riba..
      Mkandara,

      ..suala la OIC linakuzwa tu kwasababu za kisiasa.

      ..kinachogombaniwa hapo siyo mikopo isiyo na riba, bali haki ya ZNZ kuweza kujiunga na jumuiya/vyombo vya kimataifa.

      ..Tanzania[Tanganyika & Zanzibar] tuna mahusiano ya kidiplomasia,kiuchumi,kibiasha ra, na mataifa[Kuwait,Saudia,Qatar,Oman,Iran] mengi sana wanachama wa OIC.

      ..kama ni masuala ya mikopo isiyo na riba basi tunaweza kupata mikopo hiyo kupitia bilateral agreements.
      Mkandara likes this.

    12. #69
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,412
      Rep Power : 2881
      Likes Received
      4759
      Likes Given
      2824

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Hili la OIC ni sababu tu za Wazanzibar. Sina hakika wanaogopa riba kwa misingi ya dini au riba kwa maana ya kuongezeka deni.

      Ukisoama makala na maoni ya wasomi wengi wa ZNZ wanachotaka ni ZNZ yenye madaraka kamili. Yaani uwezo wa kuwa na mahusiano na vyombo vya kimataifa kama IOC, EAC, SADC,UN n.k.
      Wanataka wawe na balozi zao, tayari wana wimbo wa taifa, bendera, rais n.k.
      Wanataka wawe na jeshi lao (Ingawa gharama atalipa Mtanganyika)

      Sasa kinchonishangaza ni pale wanaposema wanataka mkataba au serikali 3. Ukiwa na mkataba au serikali 3 ni wazi utapoteza baadhi ya mamlaka kamili. Hivi jamani Wazanzibar wanajua wanataka nini?
      Makamu balozi Idd Seif amewaeleza wazi kuwa hawakuandaliwa kujadili muungano maana hawajui nini wanataka iwe mkataba au serikali 3.

      Sasa hivi wanataka kujiunga na hiyo SID, cha kushangaza walijiunga na IMO (Int maritime org)kama kawaida yao hawalipi bili wanasubiri Sumatra
      Mimi nimewachoka hawa jamaa na hakika Nyerere aliposema watoswe hakukosea, ni headache!

      Wakuu Mkandara, Joka kuu mumesikia CUF sasa baada ya LET ZNZ GO! wanarudisha majeshi nyuma,sasa wanataka muungano wa serikali 2 kama kawaida, wamekataa 3 kwa kujua kuwa ni pasu kwa pasu na hawana ubavu. Wameona hawana hoja ya mkataba kwasababu Tanganyika haihitaji mkataba. Ukweli ni kuwa ZNZ haiwezi kukimbia muungano, kama wangeweza wangefanya hivyo kitambo
      Mkandara and JokaKuu like this.

    13. #70
      MTWA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th August 2009
      Location : Somewhere in the Universe
      Posts : 842
      Rep Power : 666
      Likes Received
      41
      Likes Given
      19

      Default

      Quote By Ibambasi
      Kwi kwikwiiiii!!

      Bob Mkandara we mkororfi sana, yaani kumpa huo mfano wa mke tu Mzizimkavu tayari jazba ishampanda! By the way hizo ndizo hoja za Wa-ZNZ mpaka unashidnwa kuelewa wakiwa wenyewe free and autonomous kama wanavyotaka sijui watajiongozaje!
      wakishakuwa wenyewe mara moja watatwangana maana hawataelewana kabisa. kumbuka always nature does not favor all people equally. baba alishasema wakishabagua wataendelea tu adi wenyewe na watoto wao

    14. #71
      morenja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Posts : 294
      Rep Power : 426
      Likes Received
      56
      Likes Given
      8

      Default

      Quote By Ibambasi
      Aisee,

      Mi kuna kitu nashindwa kuwaelewa wa-ZNZ, kama Muungano hamuutaki kwa nini mnakosa uthubutu wa kutoka? Ikiwa hayo ndiyo maoni yenu kwa nini msitumie vyombo vyenu, mf. BLW kuomba kuondoka katika Muungano?
      ni kweli kwanini hawa wa zanzibar hawaishi kulalamika .siwajitoa !! .hakuna kitu tunaitaji kutoka zanzibar .let znz go

    15. #72
      Nonda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th November 2010
      Location : Gongo La Mboto
      Posts : 5,797
      Rep Power : 1858
      Likes Received
      933
      Likes Given
      367

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Mkandara
      @Nonda, Mkuu wangu jaribu sana kufikiria nje ya box halafu utaelewa kwamba Zanzibar haihitaji kujiunga na chombo chochote ktk maswala ya Maendeleo yake isipokuwa maendeleo yao yataletwa na Wazanzibar wenyewe..

      Nachoweza kubaliana na wewe ni Tanzania kujiunga na OIC ikiwa kweli mikopo yao ina nafuu maana riba ndio hasidi wa maendeleo ya nchi zote maskini. Na inasikitisha sana leo hii duniani hapa tunajiita nchi za kiislaam ..
      Mkuu Mkandara.
      Uache kukurupuka...soma kwa makini hiyo taarifa niliyoibandika.
      Unaona umeleta suala la OIC, jumuiya ya kiislamu...makala inazungumzia OIC hii;the Indian Ocean Commission (IOC), a regional cooperation body whose current members are Comoros, Mauritius, Seychelles, Madagascar and Reunion.

      Unaona basi, umepata na trela la Jokakuu, Nguruvi3 na wengineo.

      Ni wazi kuwa hukuisoma hiyo makala na kuelewa maudhui yake.

      Kilichonigusa mimi katika hiyo makala ni usanii wa kiutendaji/ muungano wetu unavyoendeshwa.
      Ona hii:Terezya Huvisa, environment minister in the Tanzanian government, said she could not say whether Zanzibar’s move to join IOC was valid until the issue had been discussed at a quarterly meeting between the vice-presidents of the URT and Zanzibar, due around the middle of the year.

      Huvisa added that while the environment was not officially a union matter, the precedent was to treat environmental issues of Zanzibar and the mainland jointly.

      “This matter will have to be discussed jointly for Zanzibar to join the IOC,” she said.

      Kweli Maendeleo huletwa na wananchi wenyewe na wanapopata viongozi wazalendo wenye muono wa maendeleo. Lakini TZ inapata ufadhili wa asilimia ngapi vile wa bajeti yake?

      Je Tanzania inahitaji misaada ili kujiletea maendeleo yake?
      Je Tanzania inahitaji wafadhili ili ilete maendeleo?

      Mkuu Mkandara , Tatizo la Tz ni usanii mwingi, mazingaombwe ni mengi na ufisadi wa hali ya juu. Na muungano umetumika katika pande zote mbili kuwa NDIO SABABU YA KUTOKUENDELEA kwa TZ.

      Lakini usanii au mazingaombwe ambayo yameniacha mie hoi, bin taabani ni kupotea kwa jina Tanganyika.

      Siku tutakayoweza kuifuta serikali ya Zanzibar bado jina la sehemu litaendelea kuwa Zanzibar au vipi?
      Sasa tumeifuta serikali ya Tanganyika(tumekasimisha madaraka yake kwa serikali ya muungano) sasa basi hata jina pia la sehemu inayoitwa Tanganyika linapotea?
      Umesikia hata siku ya uhuru, tunasema uhuru wa Tz bara?

      Mimi huishia kusema huu ni Muungano wa mazingaombwe.
      Mkandara and JokaKuu like this.

    16. #73
      Dezo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th July 2012
      Posts : 15
      Rep Power : 346
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      wewe kama unapiga ban piga tu lakini hoja ndo iyoiyo kuna mkowa gani duniani unoujuwa wewe una hivyo vitu nilivyokutajia? Kwa hivyo nani anaongea pumba? nakwatarifa yako mimi ni Mzenji halisi sijapata hata siku moja kushangiria simba wala yanga wala nyinginezo bora nishangirie nguruwe.
      Nonda likes this.

    17. #74
      Nonda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th November 2010
      Location : Gongo La Mboto
      Posts : 5,797
      Rep Power : 1858
      Likes Received
      933
      Likes Given
      367

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Dezo
      wewe kama unapiga ban piga tu lakini hoja ndo iyoiyo kuna mkowa gani duniani unoujuwa wewe una hivyo vitu nilivyokutajia? Kwa hivyo nani anaongea pumba? nakwatarifa yako mimi ni Mzenji halisi sijapata hata siku moja kushangiria simba wala yanga wala nyinginezo bora nishangirie nguruwe.
      Mkuu Dezo
      Bila shaka kama umesoma threads/ mada mbali mbali hapa JF utagundua kuna watu wapayukaji, wenye lugha za kuudhi nk. Vile vile kuna watu wana lugha asali kama Mkuu Mkandara, Jokakuu, Nguruvi3.

      Inaonesha kulingana na idadi ya post zako bado wewe ni mpya. Je umejiunga JF ili upigwe ban? Au kuchangia na kuelimisha wengine kwa kile unachokifahamu au kushawishi wengine kwa kile unachokiamini?

      Hutopungukiwa na chochote utakapotumia lugha njema, ya upole ,ya staha na kutumia lugha hiyo kujenga hoja ambayo itaonesha weledi wako katika jukwaa la siasa.

      Kunasihiana ni jambo zuri.Punguza munkri, jenga hoja ili tuelimike/ tuelimishane.
      "Jf ni darsa kwenda mbele"Nguruvi3.

      Na kwa pale tutakapotofautiana kimtazamo au kwa hoja basi tukubaliane kutokubaliana bila kudhalilishana.

      Karibu sana JF, ndugu Dezo.

      Kuwa wewe ni mzenji halisi au vyenginevyo si muhimu sana katika mijadala, la muhimu ni hoja yako na kile unachokitetea.
      JokaKuu likes this.

    18. #75
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,818
      Rep Power : 2965
      Likes Received
      2417
      Likes Given
      3484

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Nonda,

      ..inawezekana Mkandara amechanganya IOC na OIC.

      ..mimi niliona kule kwenye post yako ukizungumzia IOC but I didnt have anything to contribute.

      ..maoni yangu yalikuwa ni majibu kwa Mkandara kuhusu suala la OIC.

      ..kwa kweli i am leaning on kuunga mkono tujiunge na chombo hicho ili kumaliza malumbano ya muda mrefu.

      ..but at the same time ninapenda kutoa angalizo kwamba tayari tuna mahusiano ya kibalozi na nchi nyingi zilizoko ktk OIC.

      ..sina uhakika kama hicho tunachokifuata OIC hakiweza kupatikana thru' bilateral agreements na mataifa wanachama wa OIC kama, Kuwait,Iran,Saudi Arabia etc etc.

    19. #76
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,412
      Rep Power : 2881
      Likes Received
      4759
      Likes Given
      2824

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Ahalan Nonda,
      Nadhani suala la nini kiwe cha muungano na kipi kisiwe sasa hivi ni tata zaidi.
      Ni tata kwasababu ZNZ imejitengenezea utaratibu wa kuchagua kipi ni chake na kipi ni cha muungano kwa manufaa yake zaidi.

      Kufuati akauli ya waziri Huvisa nasimama kumtetea kuwa ni sahihi
      ''Huvisa added that while the environment was not officially a union matter, the precedent was to treat environmental issues of Zanzibar and the mainland jointly''

      Namtetea kwa hoja zifuatazao:
      1. Mfano, Baraza la mitihani lilikuwa suala la muungano kuanzia kutahini hadi kuchaguliwa na kupata huduma za mikopo. Kwasababu za hisia tu za hujuma, WZNZ wameanzisha baraza lao la mitihani. Hili si tatizo.

      Tatizo ni kuwa kuchaguliwa kwa wanafunzi kujiunga na vyuo vikuu kunategemea viwango vya NECTA kama chombo chenye madaraka Tanzani. Kulipiwa mikopo na matumizi ni jukumu la wizara ya elimu ya juu Tanzania ambapo WZNZ wanafaidika bila ubaguzi. Sasa mtu akikuuliza hivi suala la elimu ya juu ni la muungano au la, hapo hakuna jibu

      Hakuna jibu kwasababu ZNZ wameamua kuunda baraza lao kwa manufaa yao.
      Wanafunzi wao watakapokataliwa kujiunga na vyuo vikuu itaonekana wanaonewa. Wanafunzi watakaponyimwa mikopo inaonekana wanaonewa. Kwahiyo suala limebaki hewani. Lipo hewani kwasababu ZNZ wanataka kuwepo sehemu zote.

      2. ZNZ imejitoa kusimamia vyombo vya baharini chini ya SUMATRA na kuunda chombo chao ZMO.
      Chombo hiki kinasajili meli kwa kutumia sheria za ZNZ (kama zipo).

      Tukienda International Maritime Organization, ada za uanachama zinalipwa na muungano.
      Maana yake ni kuwa ZMO haipo tayari kukabiliana na majukumu yake ya uanachama IMO Kama ZNZ bali JMT.

      Sasa mtu akiuliza hili ni suala la muungano au la, hakuna jibu. Kama jibu litakuwepo basi litakuwa na majibu mawili:
      a) ZMO ni chombo huru kwa WZN na si suala la muungano
      b) ZMO ni sehemu ya muungano kwasababu ada zake zinalipwa na JMT.

      Katika mazingira hayo ni vigumu sana kusema suala la mazingira ni la muungano au la.
      Hata kama tutafumba macho na kusema si la muungano bado kuna maswali yanakuja.

      Mkuu wa shughuli za mazingira nchini ni ofisi ya Makamu wa Rais ambayo inashikiliwa na Mzanzibar na uchaguzi wake umezingatia Uzanzibar wake.
      Endapo tutasema si suala la muungano, basi ofisi ya makamu wa Rais mazingira itakuwa ya Tanganyika, hapo inaondoa uhalali wa makamu wa Rais kutoka ZNZ kuongoza ofisi za Tanganyika.
      Haiwezekani mkuu wa ofisi hiyo aazimwe kutoka ZNZ na siyo apatikane kutoka ZNZ.

      Ofisi ya makamu wa Rais wa JMT imepewa billioni 32 kwa ajili ya ZNZ ikiwa ni pamoja na kuangalia mazingira ambayo ni jukumu la muhimu la ofisi hiyo. Kama ZNZ inapewa pesa za mazingira kutoka JMT kwanini iseme si suala la muungano?
      Kwanini wasikane pesa kwanza kabla ya kujiunga na hicho chombo cha mazingira inachokusudia?

      Na mwisho,Nonda nitajie suala moja tu ambalo ZNZ inaridhika kuwa ni la muungano bila ulalamishi. Just one!
      JokaKuu and Nonda like this.

    20. #77
      Nonda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th November 2010
      Location : Gongo La Mboto
      Posts : 5,797
      Rep Power : 1858
      Likes Received
      933
      Likes Given
      367

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Nguruvi3
      Ahalan Nonda,
      Nadhani suala la nini kiwe cha muungano na kipi kisiwe sasa hivi ni tata zaidi.
      Ni tata kwasababu ZNZ imejitengenezea utaratibu wa kuchagua kipi ni chake na kipi ni cha muungano kwa manufaa yake zaidi.

      Kufuati akauli ya waziri Huvisa nasimama kumtetea kuwa ni sahihi
      ''Huvisa added that while the environment was not officially a union matter, the precedent was to treat environmental issues of Zanzibar and the mainland jointly''

      Namtetea kwa hoja zifuatazao:......

      Na mwisho,Nonda nitajie suala moja tu ambalo ZNZ inaridhika kuwa ni la muungano bila ulalamishi. Just one!
      Mkuu Nguruvi3
      Ahlan wasahlan.

      Mkuu imekuwa kawaida yako kusema maneno mengi hata pale ambapo hakuna ulazima wa kufanya hivyo.

      Pili kumtetea kiongozi anayevurunda/ anayeongeza utata katika hali tata sioni kuwa ni jambo la busara. Hata kama sababu ni mtu wetu/ wako.
      Huviza amekiri kuwa environment si jambo la muungano kumtetea haisaidii kupunguza kero za muungano bali ni kuziongeza. Na ndio usanii wenyewe au mazingaombwe yenyewe. Vipi utakwapua madaraka ambayo si yako? Viongozi wa aina hii wanatuletea fujo/ mizozo na kelele ambazo si za lazima.

      kwa hiyo, mwishowe tutasema ili kutatua kero ya mazingira basi tulifanye mazingira kuwa jambo la Muungano au vipi?
      UAMSHO au Zanzibar wakilalamika ,tunajisemea ,"hawa hawaachi kulalamika!"

      Ingekuwa vyema ,tungewashauri hawa wasanii wetu wasitutengenezee utata zaidi badala ya huu uliopo.

      Ama kujibu suali lako ni kuwa katika maandishi, hotuba, makongomano na wale niliowahi kuwasikia wanasema mambo ya muungano wanayoyakubali ni yale 11 yaliyo katika mkataba wa awali wa muungano.

      Ulalamishi wa Zanzibar unakuja pale wanapohisi kuwa katika utekelezaji huwa kuna ujanja ujanja au kuwaweka pembeni. Au mtu kama Kaviza anapojichulia mamlaka ambayo si yake.

      Nakumbuka zamani kulikuwa na mambo ya nje tu, ili kuwapiga mkwala ZNZ wasipumue kama wanavyosema ,tukaongeza na ushirikiano wa kimataifa. Natumai unanifahamu hapa.

      Mkuu nguruvi3, nasoma katika michango yako mara nyingi unakuja na masimulizi ya jussa na Seif sharif. Nafikiri kupendelea kero za muungano ziendelee kwa sababu tu unawatwisha lawama hawa kuwa ndio wanaouharibu muungano ni wazi unajaribu kuficha ukiinimacho wa muungano wenyewe, kuanzia uundwaji, ukuaji wa mambo ya muungano, jinsi ya usiri wa uendeshwaji wa muungano wenyewe na utata mwingi katika mamlaka na mipaka ya mamlaka hayo baina ya mambo ya muungano na yale yasio ya muungano.

      Lakini pia unakuja na hoja ambazo unaona kila anaesema kuna kasoro katika Muungano huu kuwa ni mzanzibari na hivyo kuishia kutetea hata kile ambacho kwa dhahiri ni udhoofishaji wa muungano wenyewe.

      Kusema kuwa wizara ya Tanganyika imepewa Mzanzibari aongoze hili kwa mtazamo wangu ni kosa kubwa,tena ni katika kuongeza kero za muungano.Hatupaswi kulibariki.Na linapasa likemewe na tutake kasoro hizi zirekebishwe. Tukifanya hivi tutakuwa tunawasaidia wasanii (viongozi)wetu katika kuweka bayana mgawanyo wa madaraka/mamlaka, lakini pia kuheshimu mgawanyo wa madaraka/mamlaka hayo na kulinda haki ya/ za kila upande wa muungano.

      Pia naona ni kosa kubwa kutumia hoja hii kuwa wizara ya Tanganyika inapewa Mzanzibari kwa hiyo, ni sawa tu kukwapua madaraka/ mamlaka ya Zanzibar hata kwa yale mambo ambayo si ya muungano. Huku ndio kuvurunda kwenyewe, mwisho huwa ni fujo tu na manung'uniko.Tunaishia katika Muungano usioeleweka...muungano wa mazingaombwe!
      Nguruvi3 likes this.

    21. #78
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,412
      Rep Power : 2881
      Likes Received
      4759
      Likes Given
      2824

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Nonda,
      Niwie radhi kama ninapojaribu kuanisha maana niliyokusudia kunakukwaza. Hayo ni mapungufu ya ubinadamu kutokana na jinsi gani mtu analiangalia bandiko la mwenzake.

      Wapo pia wanaoshukuru kwa jinsi ninavofafanua hoja zangu. Sisi wengine si wandishi hasa lakini hiyo isituzuie tusiseme ya moyoni. Kuvumiliana ndio ubinadamu na hakika hakuna mtimilifu miongoni mwetu.

      Nimemtetea Huvisa kawasababu ya mambo niliyoyaeleza ambayo hukuyajibu. Ni utata huu ndio unamfanya awe makini katika kutoa majibu. Nadhani ulikusudia aseme mazingira si ya muungano. Kama tutatoa kauli rahisi hivyo, ipo siku ataibuka waziri na kusema ulinzi na usalama si mambo ya muungano. Huoni utata hapo? Huvisa makosea nini katika hiyo sentesi?

      Niliposema wizara ya muungano kushikwa na Mzanzibar nilimaanisha kuwa wizara hiyo iliyochini ya makamu wa rais ni ya muungano na inashughulikia mazingira. Sasa kama WZNZ wanasema hilo si suala la muungano, basi na wazikatae pesa(bilioni 32) wanazopewa kwa ajili ya mazingira kutoka sehemu ya muungano ili wawe huru kwa kila jambo.

      Hoja yangu ni kuwa, huwezi kukubali mimba halafu umkatae mama mwenye mimba!
      Na hapa ndipo nimekuuliza elimu ya juu ni muungano? kama si muungano iweje WZNZ wasome kwa pesa za muungano?
      Nimeuuliza SUMATRA ni muungano, kama si muungano iweje ZMO isilipe ada zake IMO?

      Hebu nipe majibu ya ndiyo au hapana unayotaka tuyatoe, ili usiandike maneno mengi hata pale pasipo na ulazima.

    22. #79
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,669
      Rep Power : 0
      Likes Received
      537
      Likes Given
      272

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Nguruvi3
      Joka kuu,hata tukijifanya hamnazo bado nafsi zetu zitatusuta!

      Tukienda mezani sisi kama Tanganyika tupo fit kila mahali, tutawauliza wenzetu ehe! mnataka tushirikiane nini? Hawana jibu maana jibu litapoteza maana halisi ya kushirikiana. Wataogopa kusema tusaidieni na hapo hoja zitakufa......
      Kwani Znz ilikuwaje kabla ya muungano?

    23. #80
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,412
      Rep Power : 2881
      Likes Received
      4759
      Likes Given
      2824

      Default Re: Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

      Quote By Tume ya Katiba
      Kwani znz ilikuwaje kabla ya muungano?
      Ilikuwa ZNZ, yenye Sultani na karafuu.
      JokaKuu likes this.

    24. FemaTV & Radio
    Page 4 of 5 FirstFirst ... 2345 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...