Last edited by zumbemkuu; 6th August 2012 at 11:43.
"watakaotubeza na kututukana wasameheni wanahitaji ukombozi wa fikra" Mh.G.Lema
Suluisho ni kuwa na serikali nne. Ya zanzibar, tanganyika, malawi, na ya muungano - TAZAMA
waseme wameuziwa nani tumsweke ndani.
Wasiwasi wangu ni kwamba huyo naibu spika wa bunge la malawi atakuwa amekuja kushuhudia reaction ya watanzania baada ya wao kutamka bayana kwamba ziwa nyasa ni lao lote.
Kwa kutambua kwamba leo ministry of Foreign affairs wanafanya presentation ya budget yao basi wakaona waje kushuhudia kwa macho yao msimamo wa nchi ya Tanzania na wananchi wake kupitia chombo chetu cha bunge.
Sasa kama wabunge wetu wasipoonyesha kwa dhati kwamba hawawezi kuruhusu kamwe uchokozi wa aina yoyote kutoka kwa malawi, na wakaendelea kutema mipasho bungeni, basi atarudi kwao na kuwaambia waendelee na uytafiti wao kama kawaida.
Honesty is a very expensive GIFT. Do not expect it from cheap people.
Sisi hatuna na hatujawahi kuwa na urafiki na malawi huyu mama wa malawi antaka kujaribu kila kitu hata sumu anataka kuionja! Yeye kama hajui umuhimu wa ardhi ya Tanzania ni lazima sasa tumuoneshe kuwa yeye ni kilaza wa siasa za kimataifa
Pure Matrimony >> Purity starts here (Quran 24:26)
My loyalty is to reason,and as a reasonable person I reserve the right to change my mind when presented with new information that alters my perspective" Njiwa"ᵀᴴᴱ'ᴼᴿᴵᴳᴵᴻᴬᴸ✯
"watakaotubeza na kututukana wasameheni wanahitaji ukombozi wa fikra" Mh.G.Lema
Soon ntakuwa wa Malawi mie.....
Labda Mwanangu pia atakuwa adopted na Mwimbaji Madonna....
Malawi njooni haraka basi.......................
Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).
Nimeupenda sana huo wimbo..ngoja niweke mashairi yake hapa wadau msome:
MISS TANZANIA-SOLO THANG"[Ubeti wa Kwanza]Baba yake alikuwa mkoloni kipindi huyu Miss mwali
Mchonga alikata utepe lakini hakuvinjari
Sababu alikua busy kumlinda na geti kali
Kumbe wenzake wanabinjuka, kushtuka akakaa mbali
Demu alikua na heshima kabla haijatangazwa Rukhsa
Chukua Chako Mapema ukimkonyeza tu umegusa
Ana kifua kimebetuka sio maziwa ni madini
Kayaacha wazi, watu wanashika hapo ndio anaponiudhi mimi
Watu wanagonga tu Ikulu tena kwa mitindo huru
Kavu kavu bila kinga hajali vinavyodhuru
Kawa shangingi na amedata hana uwoga wa kunguru
Anapenda sana chapaa haimtoshi kodi na ushuru
Ana kijungu matata laini kama nyanya masalo
Anatingisha Afrika nzima na mzigo Kilimanjaro
Usimchezee kwa vidani sio pete sio hereni
Anamiliki tanzanite kama ardhi ya Mererani
Sura dhahabu inaita kama amezaliwa Geita
Tatizo ndio kicheche kila mwanaume ndio amepita
Hata Benja hakutoka Kapa huyu demu hajatulia
Kama rushwa ndio kikwapa ananuka na kunukia[Kiitikio]
Miss Tanzania
Nakupenda ila hujatuliaa
Vitendo vyako sitojivunia
Sifa yako kubwa umefulia
Miss Tanzania[Ubeti wa Pili]
Bora angebaki kuwa modo kama Flavian Matata
Ila demu amejiachia kisa anaendekeza bata
Sitachoka kuwakilisha jinsi anavyoniacha hoi
Juzi juzi kaopolewa na Handsome Boy
Kabla hapo shoga zake wote kashawaona mabwege
Sababu hawana dira na yeye ameshahongwa ndege
Anafaa kuwa Miss Dunia maandalizi longolongo
Tatizo anakula sana akijamba ni Songosongo
Mara ghafla kanenepa kumbe mimba B.O.T.
Kumbe demu aligawa EPA watu wamepiga hafu jii
Alizugwa na akaunti hewa kuwadi Bwana Bilal
Mara mdomo naye kazimwa bila hata picha ya kaburi
Kinachomponza huyu shawty utulivu sifuri
Ila hakuna anayepinga kwamba huyu demu ni mzuri
Mixer siasa na biashara demu ameshakuwa chotara
Mishe za Dar akimaliza Mjengoni anakwenda lala
Kadri miaka inavyokwenda demu anazidi fulia
Kumbe weupe ni mkorogo ona mwili sasa umefifia
Demu kazidi umalaya wacha mabwana wamteme
Haogopi kuliwa mtungo kisa anagawa umeme[Kiitikio][Ubeti wa Tatu]Wadaku walishamfuma anakula denda na Richmond
Dowans akazidi kete akamvisha pete ya diamond
Binti masikini akanasa bwana mshenga ndio Lowasa
Shemeji hataki hata picha ndio tabia gani sasa
Ndoa ilifungwa kwa vifijo vigogo wakala pizza
Keki nzima wale wao share yetu si ni giza
Sio hayo demu ana mengi ya kuchukiza
Malighafi ashazinadi for sale anajiuza
Mtaani ilivuma rumor demu kawa mama huruma
Uchumi umefungwa drip maendeleo ndio kali homa
Mali asili ndio kitasa kila ufunguo ndio unapita
Toka alipovunja ungo nusu karne imeshapita
Mapenzi kafanya mradi anamegwa na mafisadi
Amani kwa time bomb binti amekumbatia radi
Vitendo vyake vibaya vinafanya adharaulike
Tabia Katiba sio Msahafu ndio useme isibadilike
Mikosi inayomkuta ndio kwanza anatabasamu
Hajali waliomzunguka kama nao binaadamu
Mbagala walimbaka mpaka akamwaga damu
Na juzi Gongo la Mboto kaanza kujamba mabomu[Kiitikio]"
Mi naona ingefaa kama wangeuza ikulu yaani pango la wala rushwa. Maana maamuzi yote ya kipuuzi yanatoka mle. Wameshindwa kukanusha kuwa hata watekaji wa Ulimboka walitoka mle. Badala yake wanafungia magazeti. Kama wana ubavu waje waifunge JF waone walichoona akina Gaddafi.
Tanzania tukiingia vitani Malawi itakuwa koloni letu. Malawi nikuichapa kwa siku saba tu.Halafu hata walie hatuwapi uhuru si wameyataka wenyewe. Kiherehere chao cha kujitanua kitawaponza. Hebu nawazidishe chokochoko tuifute nchi inayoitwa Malawi au Nyasa na iwe mkoa wa Tanzania.
Acheni unazi wa kijinga usio na tija nyinyi! mnavijua vita au mnavisikia? Hivi hizo bangi huwa mnachanganya na gongo la...au.....? Muwapige wamalawi kwa sababu zipi? kuhoji mipaka waliyoachiwa kisheria na wakoloni sawa na sisi tulivyoachiwa? Ukweli ni kwamba katika mzozo wa Malawi nchi zote ziko sahihi na kinachotakiwa ni busara hata kidogo tu, yaani kuvuta viti, kukaa pamoja na kuelewana mbele ya mashuhuda (AU/UN); na hili la Zanzibar limetokea wapi? wamefanya nini hadi muwagawe vipande vipande? Kwani ni koloni la Tanganyika lile? Zanzibar ni taifa huru lililoridhia kwa hiyari yake kuungana na taifa jingine kwa maslahi ya nchi mbili. Wana uwezo wa kuamua kujitoa kama walivyoamua kujiunga na sisi. Licha ya kuwa na eneo dogo na watu wachache; wanasimama kama taifa lenye hadhi sawa na Tanganyika, Kenya, Marekani au nchi yoyote unayoifahamu na kwa taarifa zenu walevi wa namna hiyo Zanzibar si taifa dogo sana kiasi hicho kwani kuna nchi zina watu elfu kumi na zina hadhi sawasawa na Marekani na Uingereza! Sasa sina shaka kwamba chokochoko baina ya pande hizi mbili mara nyingi huchochewa na walevi msiojua kabisa athari za vita. Kelele za namna hii zikikutana na watu wa aina yenu kule ndiyo yanatokea yanayotokea! Mungu ibariki Tanzania, dumisha amani na umoja!
Last edited by mchillo; 7th August 2012 at 06:22.
Heri ujinga wa mtu mzima kuliko busara za kichaa
Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika, Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, nisaidie kwa jambo hili kwanza, hivi Uamsho ni nani nchi hii, je nao pia wanaimba Mungu Ibariki Tanzania, Dumisha Uhuru na Umoja.....Tanzania na watu wake, je uamsho nao huwa wanaimba wimbo huu kwa kusisimka? Makanisa yaliyounguzwa huko zenj ni kwa ajili ya nini, Pili umoja ni nguvu na utengano ni uzaifu kwa kuna ubaya gani, kuwa na taifa moja - mbona wilaya za Iringa zimepelekwa Njombe, vijiji na wilaya za mwanza na kagera vimekuwa Geita, kwa nini Zenji isiwezekane, maana ni umoja huo huo?
Follow Us Here