Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

    Report Post
    Results 1 to 20 of 20
    1. #1
      mharakati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 931
      Rep Power : 572
      Likes Received
      258
      Likes Given
      243

      Default Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Baada ya kufuatilia historia ya mgogoro huu nimepata wazo kwamba Tanzania ilikua na historia ya kipekee ya kushughulikia tatizo hilo wakati wa serikali ya Bakili Muluzi (94-2004).

      Muluzi alikua ni rais ambaye alikuja kua na uhusiano mzuri sana na Tanzania na uhusiano mzuri wa kikazi na Rais mstaafu Mkapa.

      Mkapa ambaye alikuwa anajua tatizo hili kwa undani kama kiongozi wa muda mrefu wa ngazi za juu, angepaswa kutumia muda huo kuanzisha mazungumzo ya kutatua hili tatizo kwa kuongea na serikali "rafiki" ya Malawi ya wakati huo baada ya kuondolewa kwa Kamuzu Banda (aliyekua mtu mgumu kuongea nae lolote la maana).

      Kama kawaida viongozi wetu wamekua hawana malengo ya muda mrefu yenye manufaa ya taifa wanatumikia miaka 10 yao halafu wanajenga mahekalu ya kustaafu na wananchi mtajijua wenyewe. Sera ya nje ya Tanzania baada ya kumalizika kwa vita ya baridi ya dunia imebaki kua shambolic to say the least. Hatuna dira wala mipango ya kimkakati ya kutumia jiografia (geo politics) kutetea na kujilinda kimaslahi katika eneo hili lenye migogoro isiyoisha.

      Sasa hivi na matatizo ya kiuchumi duniani na siasa za ushindani za Malawi kuna uwezekano wa kuendelea kupata reactionary leaders au populist leaders kama huyu Banda na kale kadirisha kalikokuepo miaka ya 94-2004 kua ndiyo kamefunga kabisa.

      Mungu ibariki Tanganyika yetu,


      Mharakati

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Nicholas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 5,017
      Rep Power : 3621
      Likes Received
      1285
      Likes Given
      2142

      Default re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Kuanza msingizia aliyeondoka wakati aliyepo pia anapaswa dili nalo ni Ishara kuwa limeshakomaa na kumwogopesha. Kwani kiapo cha kuilinda katiba kinampeleka kulinda mipaka inayosemwa na Katiba yetu bila kusema kuwa kama ilianzishwa na presidaa mwingine basi asihusike.

      Makubaliano yalianza Long time, ila kama kawaida ya mazungumzo ya nchi na Nchi huwa hayaishi utawala mmoja,la utawala fulani unaweza kuwa na advantages zaidi au hata disadvantages zaidi ya mwingine.

      Wamalawi wameanza endeleza upande wao so taratibu wataongeza na kuwapa mikataba mataifa ya nje. Sasa baadaye mazungumzo yanaweza tibuliwa. Tanzania mkija juu mnajikuta mataifa makubwa yakilinda vitega uchumi vyao na hivyo kusaidia maadui zetu. Na tayari zoezi la kudilute watu linaendelea kwa kasi sana. Watu wanaoana na wabongo wasiojua malengo ya wenzao katika mipaka yetu.

      Na hili ni sehemu nyingi za nchi.Sijui kama SERIKALI IMEWAHI FANYA OPINION POLL KUJUA MAKABILA YA MPAKANI KAMA YANAPENDA KUWA UPANDE GANI WA NCHI. sijui kama waliwahi wauliza masai wa bongo, Jaluo au hata warombo kuwa wangependa TZ au Kenya, Waangaza na nchi za Rwanda na burundi, wanyaKyusa, wanyasa, na wengine wanoanzia katika border la DRC, zambia, Malawi, na Mozambique.

      Mbaya zaidi ni kwamba Tanzania haijaendeleza sana mikoa ya pembeni kiasi cha raia wa huko kuona kuwa nchi za Jirani ndio wana maendeleo zaidi. Watu wa mipaka yetu huwa hawajiamini mbele ya wenzao.Utakuta wanahofia vitu kama Kiingereza na majengo na bidhaa za viwanda vya nchi jirani.

      Serikali kama haijui haya ni siku wamalawi wanasema zipigwe hata kuwa za watu serikali legelege inashangaa watu kuikataa Tanzania

      Jamani pro Kikwete tunaomba muanze maisha mapya term ya Kwanza ilishapita sasa mambo ya kila kitu kusingizia Mkapa au hata wasaidizi wake ni udhaif na woga. Plse toeni alternative solutions kam Presidaa ataona anweza zitumia basi kazi ianze.
      Last edited by Nicholas; 5th August 2012 at 17:34.
      Mindi and mharakati like this.
      SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.

    4. #3
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,209
      Rep Power : 3556
      Likes Received
      3058
      Likes Given
      462

      Default re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By mharakati
      Baada ya kufuatilia historia ya mgogoro huu nimepata wazo kwamba Tanzania ilikua na historia ya kipekee ya kushughulikia tatizo hilo wakati wa serikali ya Bakili Muluzi (94-2004). Muluzi alikua ni rais ambaye alikuja kua na uhusiano mzuri sana na Tanzania na uhusiano mzuri wa kikazi na Rais mstaafu Mkapa. Mkapa ambaye alikua anajua tatizo hili kwa undani kama kiongozi wa muda mrefu wa ngazi za juu, angepaswa kutumia muda huo kuanzisha mazungumzo ya kutatua hili tatizo kwa kuongea na serikali "rafiki" ya Malawi ya wakati huo baada ya kuondolewa kwa Kamuzu Banda (aliyekua mtu mgumu kuongea nae lolote la maana).

      Kama kawaida viongozi wetu wamekua hawana malengo ya muda mrefu yenye manufaa ya taifa wanatumikia miaka 10 yao halafu wanajenga mahekalu ya kustaafu na wananchi mtajijua wenyewe. Sera ya nje ya Tanzania baada ya kumalizika kwa vita ya baridi ya dunia imebaki kua shambolic to say the least. Hatuna dira wala mipango ya kimkakati ya kutumia jiografia (geo politics) kutetea na kujilinda kimaslahi katika eneo hili lenye migogoro isiyoisha.

      Sasa hivi na matatizo ya kiuchumi duniani na siasa za ushindani za Malawi kuna uwezekano wa kuendelea kupata reactionary leaders au populist leaders kama huyu Banda na kale kadirisha kalikokuepo miaka ya 94-2004 kua ndiyo kamefunga kabisa.


      Mungu ibariki Tanganyika yetu,


      Mharakati

      Wakati huo na wewe ULIKUWA IKULU? Sababu inaonyesha ya kuwa ULIKUWA UNASIKILIZA MIKUTANO YOTE YA

      MKAPA NA MULUZI na INAONYESHA HAWAKUZUNGUMZIA LAKE NYASA...

      INA ONYESHA HATA wewe haujui DIPLOMASIA, ni kulalama kama kawaida ya Mwananchi wa Tanganyika halafu

      Jasho halikutoki Unajinyamazia... hautaki Matatizo... Unajua Mbunge wako nakula PESA KIUFISADI Utalalamika

      Halafu Utatulia Ukija Uchaguzi Utamchagua huyo huyo...

    5. #4
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,820
      Rep Power : 2967
      Likes Received
      2425
      Likes Given
      3501

      Default re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By mharakati
      Baada ya kufuatilia historia ya mgogoro huu nimepata wazo kwamba Tanzania ilikua na historia ya kipekee ya kushughulikia tatizo hilo wakati wa serikali ya Bakili Muluzi (94-2004). Muluzi alikua ni rais ambaye alikuja kua na uhusiano mzuri sana na Tanzania na uhusiano mzuri wa kikazi na Rais mstaafu Mkapa......
      Mharakati, ..this is very interesting lakini umesahau kwamba JK alikuwa waziri wa mambo ya nje for 10 yrs wakati Mkapa akiwa Raisi. ..je, JK alimshauri nini Raisi wake, au alifanya jitihada gani kushughulikia tatizo hilo? mbona hatukumuona JK akijishughulisha kutatua mgogoro huu kama anavyofanya Benard Membe sasa hivi??

    6. #5
      NusuMutu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Location : Mpulungu
      Posts : 421
      Rep Power : 471
      Likes Received
      74
      Likes Given
      20

      Default re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      lakin jamani rais si anaapa kuilinda katiba ambayo ina-define nchi na mipaka yake? Akishindwa kuilinda na sehemu ya nchi ikamegwa na 'mama' tumfanyeje?

    7. Miaka 50

    8. #6
      maandamano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th March 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 1,052
      Rep Power : 626
      Likes Received
      354
      Likes Given
      915

      Default re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      jk anapenda kurefer vitu alivyofanya na marais waliopita lakini hasemi inflation imevunja rekodi katika awamu yake!na hili anataka kumbwagia mkapa?!

    9. #7
      rodrick alexander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Posts : 705
      Rep Power : 508
      Likes Received
      170
      Likes Given
      333

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Tanzania tumekuwa wadhaifu juzi nilimsikia mbunge mmoja wa Kagera Ntukamazima anamuulizwa swali waziri wa afrika mashariki kwanini mifugo ya wanyarwanda ikivuka kufata malisho inarudishwa waziri akamjibu ana safari ya huko na atakutana nawiri mwenzake watajadili na yeye anakaribishwa nimeshangaa badala ya kutetea watanzania anatetea wageni ingawa tukiangalia jina lina asili ya huko huko
      Jasusi likes this.

    10. #8
      Mbozib's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th April 2012
      Posts : 358
      Rep Power : 430
      Likes Received
      43
      Likes Given
      5

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Wa TZ kazi tunaya hu Jk kila kitu kina mshinda angalia wasomali wanavyo pitishwa hapa kama mbuzi , wafugaji toka rwanda wanachungia mifugo yao kwenye mashamba yetu kule kagera .lakini jamaa kanyamaza tu ndio maana hata huyo mama wa malawi anatudharau sasa.

    11. #9
      Msalagambwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th July 2012
      Posts : 537
      Rep Power : 453
      Likes Received
      178
      Likes Given
      530

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Jina tu linaonyesha ni mzamiaji.
      Ntukasomething
      Quote By rodrick alexander
      Tanzania tumekuwa wadhaifu juzi nilimsikia mbunge mmoja wa Kagera Ntukamazima anamuulizwa swali waziri wa afrika mashariki kwanini mifugo ya wanyarwanda ikivuka kufata malisho inarudishwa waziri akamjibu ana safari ya huko na atakutana nawiri mwenzake watajadili na yeye anakaribishwa nimeshangaa badala ya kutetea watanzania anatetea wageni ingawa tukiangalia jina lina asili ya huko huko

    12. #10
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,159
      Rep Power : 24268
      Likes Received
      4671
      Likes Given
      2295

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Tatizo lipo kwa Jk na jeshi lake. Mkapa ameongoza vizuri kamaliza.

    13. #11
      Bejajunior's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th September 2011
      Location : Chuga...
      Posts : 169
      Rep Power : 421
      Likes Received
      37
      Likes Given
      85

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Sera ya uhusiano mwema iangaliwe vizuri maana tuendako majirani tunaowalinda watakuja "kutunawisha" ili tule. Kama hatutatoa mawazo stahiki ku-deal na hili swala.
      "Never try to make life simple by simplifying yourself."

    14. #12
      Mzizi wa Mbuyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2009
      Posts : 3,217
      Rep Power : 1273
      Likes Received
      531
      Likes Given
      404

      Default

      Quote By Mungi
      Tatizo lipo kwa Jk na jeshi lake. Mkapa ameongoza vizuri kamaliza.
      Jeshi la cha nazi ni matatizo matupu wamepoteza mwelekeo!
      Sasa angalia u.p.u.m.b.a.v.u huu wa kusingizia waliomtangulia ilhali na yeye alikuwa waziri wa mambo ya nje kwa miaka 10!

    15. #13
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 511
      Rep Power : 750
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Hebu tuangalia, kwanini mgogoro huu unakuja kipindi hiki wakati huu ambapo Bi Kiroboto wa Marekani anatembelea Malawi? Hakuna uhusiano kweli?

      Ushahidi uliyopo na wa uhakika ni kuwa marekani wame eye-mark eneo hilo ka Nyanda za Juu Kusini likiwemo eneo lijulianalo kama Rungwa-Ruaha Landscape ambapo linahusisha mito mikuu ya kusini nyanda za juu, milma yake na hasahasa bonde la ufa na huu ni mpaka Ziwa Nyasa.

      Serikali ya Marekani ndiyo inayofadhili mpango mzima wa hifadhi za wanyama pori za maeneo haya ikiwemo ufadhili wa utafiti na upanuzi wa Ruaha National Park ambapo wazee wetu kule bonde la Ihefu waliondolewa.

      Pia NGOs nyingi za Kimarekani zimejikita maeneo haya ikiwemo NGO ya Jeshi la Serikali ya Marekani ijulikanayo kama Walter Reed. Kwa hali ya uchumi wa Malawi, uchumi ambao imefika mahali hawana motuary na walikosa hata mafuta ya kuendeshea majenereta wakati wa mazishi ya raisi wao.

      Ni nchi ambayo ina hali mbaya kiuchumi kuliko maelezo, lakini watu wake hawasikiki kimataifa (isipokuwa yawezekana tukaanza kusikia ukizingatia Bi Kiroboto kaenda huko na inaonekana serikali ya wababe hawa ikawa na vested interest).

      Hakuna safari ya Bi Kiroboto wao kwenda kwa nchi masikini kama Malawi ambayo hailipi, sina uhakika na upendo wowote wanaotaka kuunyehsa kwa nchi hii kama ilvyo Tanzania kwetu, ambapo mpaka yule gwiji wa migogoro duniani alirudi hata baada ya kustaafu. Kuna siri kubwa bila shaka- What a morden neo-colonialism we are already traped in.
      mharakati likes this.

    16. #14
      mharakati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 931
      Rep Power : 572
      Likes Received
      258
      Likes Given
      243

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By JokaKuu
      Mharakati,

      ..this is very interesting lakini umesahau kwamba JK alikuwa waziri wa mambo ya nje for 10 yrs wakati Mkapa akiwa Raisi.

      ..je, JK alimshauri nini Raisi wake, au alifanya jitihada gani kushughulikia tatizo hilo? mbona hatukumuona JK akijishughulisha kutatua mgogoro huu kama anavyofanya Benard Membe sasa hivi??
      Nafikiri Jk kama waziri wa enzi hizo anayeshughulikia sera ya nje na maslahi ya nje ya taifa anahitaji lawama kwa kiasi chake..ila kama serikali nzima, Mkapa atabeba political responsibility kwa sababu hatuna notes za vikao vya vyote vya baraza la mawaziri haswa kwenye mambo ya usalama wa mipaka na sera ya nje kwa hiyo hatuna uhakika kama Jk aliwahi kumshauri boss wake au la?

      Mkapa kama na aliyekua na uhusiano na Muluzi angeanzisha mazungumzo ambayo yangeendelezwa katika ngazi ya mawaziri baada ya mahead of state kuyapa heshima haya mazungumzo.

      Kwa hili Mkapa bado anaonekana kama ana lawama zaidi, Jk angeshauri tu ila marais ndiyo walitakiwa wakutane kwanza na kuset parameters za mazungumzo.

    17. #15
      mharakati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 931
      Rep Power : 572
      Likes Received
      258
      Likes Given
      243

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By nngu007

      Wakati huo na wewe ULIKUWA IKULU? Sababu inaonyesha ya kuwa ULIKUWA UNASIKILIZA MIKUTANO YOTE YA

      MKAPA NA MULUZI na INAONYESHA HAWAKUZUNGUMZIA LAKE NYASA...

      INA ONYESHA HATA wewe haujui DIPLOMASIA, ni kulalama kama kawaida ya Mwananchi wa Tanganyika halafu

      Jasho halikutoki Unajinyamazia... hautaki Matatizo... Unajua Mbunge wako nakula PESA KIUFISADI Utalalamika

      Halafu Utatulia Ukija Uchaguzi Utamchagua huyo huyo...
      Kaka jazba haijengi ila kubomoa, sina minutes za mikutano ya Muluzi na Mkapa, ninachojua ni Mkapa kwa sababu anatoka kusini alijaribu kuanzisha hii habari ya mizigo ya Malawi ipate corridor pale Mtwara kupitia Mbamba bay kitu ambacho labda kama Rais mstaafu Mkapa angepata miaka mingine 10 angefanikisha labda..

      Hata kama aligusia mgogoro haikua priority ya sera ya nje ya Tanzania kwa sababu sisi wafuatitiliaji wa mambo ya kimataifa hatujawahi sikia kitu kama summit au task force ya kufuatilia hii kitu, kama mazungumzo ya siri yalikuaeop hayakupewa kipaumbele chake.

    18. #16
      manucho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Posts : 561
      Rep Power : 469
      Likes Received
      79
      Likes Given
      0

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Wamalawi wapewe ziwa waendelee na shughuli zao wanazozitaka kwa sababu tanzania wakiachiwa hiyo sehemu ya huo mpaka wanaosema umepita katikati mwanchi wa kawaida ambaye ndiyo mtanzania halisi atafaidi nini?

      Kama gesi asilia inatoka hapo Mtwara lkn gharama za umeme na maisha ndiyo zinapanda kila siku na wanaopandisha ni hao wachache kwa maslahi yao, kwahiyo hata hapo malawi wanang'ang'ania kwa maslahi yao hao wachache.

      Halina faida yoyote kwa mtanzania, wamalawi wapewe ziwa lao tu

    19. #17
      mharakati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 931
      Rep Power : 572
      Likes Received
      258
      Likes Given
      243

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By Nicholas
      Kuanza msingizia aliyeondoka wakati aliyepo pia anapaswa dili nalo ni Ishara kuwa limeshakomaa na kumwogopesha .Kwani kiapo cha kuilinda katiba kinampeleka kulinda mipaka inayosemwa na Katiba yetu bila kusema kuwa kama ilianzishwa na presidaa mwingine basi asihusike........
      Pro-kikwete, he he ..nway, mi naona kila administration ina unique historical opportunities za kulinda na kujenga taifa kwa faida za vizazi vingi vijavyo. Mkapa alikua nazo, Jk amekua nazo na yeye atakuja kulaumiwa akimaliza muda wake kwa kutokua makini sana na hili au lile.

      Mkapa alikua na nia nzuri tu ya kuwaweka wamalawi karibu na tanzania kiuchumi kwa kufungua miundo mbinu ya kusini kwa ajili ya mizigo na biashara za malawi na hii ingewafanya kufikiria mara mbili mbili kuanzisha mzozo wowote na Tz..

      Hii ninachisema ilikua ni wazo zuri na ingebidi liende sambamba na maongezi ya kisiasa ya kutatua mgogoro kwa spidi nzuri kwa sababu serikali ya wakati ule ya malawi ilikua karibu sana na tz na hapa tungepata favorable conditions.

      wataalamu wanasemaje unaingia kwenye majadiliano ukiwa kwenye nafasi ya kupata zaidi kulingo mwenzako (you go into negotiations in a position of relative strength). Tanzania ya wakati ule ilikua kwenye nafasi kuliko sasa na hatukufanya lolote. Na hapa ndiyo namlaumu BM

    20. #18
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,209
      Rep Power : 3556
      Likes Received
      3058
      Likes Given
      462

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By mharakati
      Kaka jazba haijengi ila kubomoa, sina minutes za mikutano ya Muluzi na Mkapa, ninachojua ni Mkapa kwa sababu anatoka kusini alijaribu kuanzisha hii habari ya mizigo ya Malawi ipate corridor pale Mtwara kupitia Mbamba bay kitu ambacho labda kama Rais mstaafu Mkapa angepata miaka mingine 10 angefanikisha labda..

      Hata kama aligusia mgogoro haikua priority ya sera ya nje ya Tanzania kwa sababu sisi wafuatitiliaji wa mambo ya kimataifa hatujawahi sikia kitu kama summit au task force ya kufuatilia hii kitu, kama mazungumzo ya siri yalikuaeop hayakupewa kipaumbele chake.

      Sasa Unaongea vizuri unaweka neno LABDA Kama, LABDA Ange... HIYO ni BORA

      Sina Jazba sikipendi Chama Cha Mafisadi ila Habari uliyotuwekea ni kama vile ulikuwapo hapo wakati hao Marais

      wakijadiliana.... Sasa nimekubali na hiyo LABDA kama, LABDA ange.... HIYO INGEPASWA kuwa kwenye Main Story

    21. #19
      mharakati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 931
      Rep Power : 572
      Likes Received
      258
      Likes Given
      243

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Quote By nngu007

      Sasa Unaongea vizuri unaweka neno LABDA Kama, LABDA Ange... HIYO ni BORA

      Sina Jazba sikipendi Chama Cha Mafisadi ila Habari uliyotuwekea ni kama vile ulikuwapo hapo wakati hao Marais

      wakijadiliana.... Sasa nimekubali na hiyo LABDA kama, LABDA ange.... HIYO INGEPASWA kuwa kwenye Main Story
      usibadilishe theme yangu kaka, nimesema Labda kama angekaa miaka 10 mingine labda angebadilisha, ina maana miaka 10 yake hakufanya wala kuchukulia uzito hili jambo zaidi ya wazo la bandari ya mtwara kupitisha mizigo ya malawi.( kitu ambacho ni kizuri kupunguza uhasama kwa kukuza mahusiano ya kibiashara, lakini ingebidi hili wazo liendane na diplomasia ya kujaribu kutatua tatizo lililokuepo).

      ujue ukitaka kuelewa utaelewa tu, usipotaka hautaelewa kaka, jaribu kuangalia na kuelewa kabla ya critique

      **Angalia gazeti la leo the citizen, mbunge zambi anaongelea haya haya niliyosema**

    22. #20
      Songambele's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2007
      Posts : 746
      Rep Power : 741
      Likes Received
      74
      Likes Given
      189

      Default Re: Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Serikali ya Mkapa inabeba lawama

      Sasa kama malawi wanagombea ziwa mbona hawajiulizi hayo maji yanayojaza ziwa yanatoka wapi na mbona mito mikubwa inayokusanya maji kutoka umbali mrefu iko bongo land, hivi hili bara limekumbwa na nini jamani manake viongozi wake hatujui wanatumia nini kufikiri.

      Huyo waziri wa Malawi anajambisha tu na mziki wetu hawauwezi kabisa kama vipi wakichafue wauone mziki wenyewe na tunaichukua nchi yetu.

      Mie sioni sababau yeyote ya huu mjadala its obvious mno.
      You can't fight ignorance with knowledge!

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...