Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 38 of 38
    1. #1
      ukweli2's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th November 2011
      Posts : 50
      Rep Power : 389
      Likes Received
      39
      Likes Given
      11

      Default Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Habari za j2 wadau

      Kutoka kwa John Mnyika>>>>>....Leo saa saba hadi tisa alasiri,mkutano wa mtandaoni kutoa maoni juu ya suala la SSRA na NSSF! Mjadala utakuwa ktk: mnyika.blogspot.com!

      Mnyika: Nalazimika kukusanya maoni kwa hatua ya sasa kupitia njia ya mtandao kutokana na udharula wa hoja husika

      Source: Mnyika on Twitter

    2. RukaaJuu Final

    3. #21
      LORDVILLE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd June 2012
      Location : Imaginary island
      Posts : 1,323
      Rep Power : 615
      Likes Received
      117
      Likes Given
      141

      Default re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

    4. bob nasta's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th April 2011
      Posts : 24
      Rep Power : 413
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Hivi ni kweli kifungu cha mafao ya kujitoa kilichomekewa alafu naona wabunge kama wameipozea sana hii ishu au kwa vile wao hawamo hawaoni ni kwamba watu wengi watakufa haraka kwa sababu ya pressure ya hili jambo.

      Maoni yangu ni kwamba yaani kama ikishindakana kabisa basi angalau iwe mtu pale unapochukua mkopo nusu ya pesa yako iliyopo ndo ihesabibike kama umesha jiunga na huo mpango wao manake hiyo mikopo wanasema tu hawatoa hao na hili jambo kama litashindikana huko BUNGENI tunaomba tumjue mbunge mmoja mmoja nani kasema sheria hii iendelee na nani alikua anataka itolewe MANAANAKE HAPA NAPUMULIA JUU JUU IKIPITISWA TU MAUTI YAMENIKUTA

    5. #23
      bob68's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th February 2012
      Posts : 35
      Rep Power : 375
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default

      Muache kujipa majina hayo maana inaonyesha udhaifu wa kufikiria na kuamua wakati polisi hawapo hivyo bali wao wanapokea amri kwa wanao waongoza,umeonyesha udhaifu mkubwa sana kwa kuuliza ilo swali.futa ilo jina

    6. #24
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,488
      Rep Power : 6171
      Likes Received
      3059
      Likes Given
      1020

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Hivi hiyo sheria ilipitishwa na nanai? Siyo wabunge wetu akiwemo Mnyika? Hivi utaratibu wa kupitisha sheria ukoje?

      Hawakuona hayo mapungufu au walipitisha bila kusoma wakikimbilia posho? Kwa mtindo huu ni sheria ngapi za kikansamizi zinapitishwa na wabunge wetu kwa kuwa inaonekana huwa hata hawazisomi hadi tunaowakilishwa tunakuja kugundua kwamba wawakilishi wetu wametupeleka kusiko!

      Kama ni hivyo wao wanawakilisha nini sasa halafu wanakuja kujifanya ati wanawasilisha hoja kwa hati ya dharura. Wabunge wetu wanakosa utukufu na sipendi tena kusikia ati Bunge letu Tukufu; hakuna utukufu hapo.

    7. #25
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,488
      Rep Power : 6171
      Likes Received
      3059
      Likes Given
      1020

      Default

      Quote By LORDVILLE
      sasa kaka watu 300 wanasema YES, sasa mtu mmpja ukisema NO atakuelewa nani? haiitaj degree kuelewa jambo kama hili!!!
      Yeye alisemaje? Huwa namuamini sana kwa hoja hata kama haikupita lakini angesema tungemuelewa badala ya kuwa miongoni mwa waliopitisha anagutuka baada ya wawakilishwa kugundua udhaifu wa sheria.

    8. Miaka 50

    9. #26
      majorbanks's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Posts : 148
      Rep Power : 397
      Likes Received
      37
      Likes Given
      3

      Default

      Unatumia kiungo gani kuwaza?ukishajua alikuwa wapi kipindi icho then what?help yourself to discover how to think with your average mindset..!
      Quote By Polisi
      Atueleze kwanza wakati hii sheria inafanyiwa marekebisho bungeni mwezi Aprili alikuwa wapi? Kwanini hakuiinga kipindi hicho?
      Polisi likes this.

    10. #27
      Kibanga Ampiga Mkoloni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2007
      Location : Here! here!
      Posts : 4,800
      Rep Power : 1636
      Likes Received
      1195
      Likes Given
      1702

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Quote By Polisi
      Atueleze kwanza wakati hii sheria inafanyiwa marekebisho bungeni mwezi Aprili alikuwa wapi? Kwanini hakuiinga kipindi hicho?
      Naomba kumjibu mtoa maoni wa saa 3:56 swali lake: ‘mlikuwa wapi wakati haya yanapitishwa? Sio wapinzani, sio chama tawala... wote mlishiriki kutukandamiza.”, kwa kurejea taarifa yangu ya tarehe 3 Agosti 2012 kwa umma kuwa:

      “Ikumbukwe kwamba kifungu cha kufuta mafao ya kujitoa kilichozua mgogoro hakikuwepo wakati muswada uliposomwa kwa mara ya kwanza bungeni tarehe 1 Februari 2012 bali kiliwasilishwa kupitia jedwali la marekebisho ya Wizara lililowasilishwa tarehe 13 Aprili 2012 bila malengo na madhumuni yake kuelezwa kwa ukamilifu.

      Kupitishwa kwa kifungu hicho kumethibitisha maneno niliyoyatoa bungeni kuwa tumefika hapa tulipo kutokana na ‘uzembe wa bunge na wabunge’ na kwa hili pamoja na mchango nilioutoa bungeni kwa maandishi siku hiyo juu ya haja ya kuwa mfumo mpana zaidi wa pensheni na hifadhi ya jamii (universal pension and social security) pamoja na kuwa sikuunga mkono kifungu husika kilichoingizwa kinyemela naomba radhi kwa wananchi wa Ubungo na wafanyakazi kwa kutokuwasilisha jedwali la marekebisho kupinga kifungu hicho kuingizwa.

      Izingatiwe kuwa ili kurekebisha hali hiyo tarehe 27 Julai 2012 kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani niliitaka Serikali itoe maelezo maelezo kuhusu taarifa zilizotolewa bungeni tarehe 13 Aprili 2012 kuwa wafanyakazi ikiwemo wa migodini kupitia vyama vyao walihusishwa kutoa maoni yaliyopelekea kufutwa kwa fao la kujitoa (withdrawal benefits); suala ambalo Chama Cha Wafanyakazi wa Migodini (TAMICO) kililikanusha.

      Hata hivyo, Waziri wa Nishati na Madini wakati wa majumuisho ya Hotuba yake tarehe 28 Julai 2012 hakutoa majibu yoyote bungeni kuhusu suala hilo hali ambayo imesababisha migongano kuendelea katika migodi mbalimbali kuhusu madai hayo hali ambayo kwa taarifa nilizozipata tarehe 1 na 2 Agosti 2012 inaweza kusababisha migomo migodini. Kufutwa kwa fao la kujitoa kumelalamikiwa pia na wafanyakazi na wadau wa hifadhi ya jamii katika Jimbo la Ubungo na katika taifa kwa ujumla.

      Hata hivyo, suala hili na tukio husika litumike kama rejea ya bunge na wabunge kuikatalia Serikali kuwasilisha marekebisho yenye athari kubwa kipindi cha mwisho na hivyo wabunge kukosa fursa ya kupata maoni ya wananchi na pia Serikali itakiwe kuomba radhi kufuatia kulipotosha bunge kuwa wadau wa hifadhi ya jamii hususan wafanyakazi na vyama vyao walishirikishwa na kuridhia wakati ambapo wamejitokeza na kukanusha madai hayo yaliyotolewa na Wizara bungeni.

      Kwa upande mwingine kufutwa kwa mafao ya kujitoa msingi wake haupo kwenye marekebisho ya sheria yaliyofanyika tarehe 13 Aprili 2012 pekee bali ni udhaifu katika mfumo mzima wa kisera na kisheria wa hifadhi ya jamii nchini hali ambayo inahitaji wadau kutaka mabadiliko makubwa.”

      Tuendelee na mkutano.
      John Mnyika
      For the Holy Quran says in Sura 42, verse 41: 'All those who fight when oppressed incur no guilt, but Allah shall punish the oppressor, Come the day.

    11. #28
      Jodoki Kalimilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Location : Ihayabuyaga
      Posts : 2,284
      Rep Power : 894
      Likes Received
      783
      Likes Given
      1484

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Quote By king kong iii
      mnyika yupo jf aje na huku achukue maoni.

      1.fao la kujitoa liwepo kwa sababu mifuko ya hifadhi za jamii ya tz haifanyi kazi kama huko usa wanapotaka kufatisha hyo sheria ya kuzuia kuchukua fao la kujitoa....wao social security inawalinda incase ukipoteza ajira unakuwa unalipwa

      2.mifuko ya hifadhi za jamii iwe inawapa bonus ya faida wanayopata kwenye uwekezaji.

      3.katika kipindi ambacho mtu anafanya kazi aruhusiwe kukopa fedha zake kwa riba nafuu (5%) @lst nusu na awe anakatwa kila mwisho wa mwezi.

      4.serikali isiwe na mamlaka ya kuiingilia hyo mifuko kwani ssra ipo,na hao wakurugenzi wapunguziwe mishaara na posho!! Haiwezekani mkurugenzi analipwa mil25 p.m na posho hadi 1.5m kwa siku,come on!!!
      pia mazingira ya tanzania ni tofauti na ulaya hivyo anytime hata hao waliopo kwenye ajira ya kudumu kuna kipindi huwa kuna ridandansi

    12. #29
      Jodoki Kalimilo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Location : Ihayabuyaga
      Posts : 2,284
      Rep Power : 894
      Likes Received
      783
      Likes Given
      1484

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Kimbunga

      Mie mwenyewe mhanga wa hili ukitaka kitu chako kipite ukiweke kwenye m issue jedwali ambayo mengi hayasomwi kwa kuwa watz wengi hawapendi namba hivyo wanasoma NARRATIVE tu ikifika kwenye majedwali ni wabunge wenyewe ndio wanaibua hivyo kwa kuwa wengi si wasomaji wakiambiwa JEDWALI na 1 mnasemaje wao wanaitikia IMEPITA na mwisho wa siku wanapitisha

    13. #30
      tusichoke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2011
      Posts : 660
      Rep Power : 544
      Likes Received
      78
      Likes Given
      8

      Default

      Kimbunga

      Dah kweli siasa imetukaa vibaya au watu hatufuatilii bunge, mimi ninachojua mnyika na wenzake wachache wako makini ktk kila hoja na huwa hawaungi mkono kirais,tatizo kila wanapoonyesha kutetea wananchi kuna wabunge wanasema wanatafuta umaarufu sasa leo mnyika unamlaumu kwa kosa gani, kijana yupo smart ktk hoja nyingi na anasimamia anachokiamini siku zote

    14. #31
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,488
      Rep Power : 6171
      Likes Received
      3059
      Likes Given
      1020

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Quote By tusichoke
      Dah kweli siasa imetukaa vibaya au watu hatufuatilii bunge, mimi ninachojua mnyika na wenzake wachache wako makini ktk kila hoja na huwa hawaungi mkono kirais,tatizo kila wanapoonyesha kutetea wananchi kuna wabunge wanasema wanatafuta umaarufu sasa leo mnyika unamlaumu kwa kosa gani, kijana yupo smart ktk hoja nyingi na anasimamia anachokiamini siku zote
      Mkuu mimi najua Mnyika yupo smart katika masuala mbalimbali lakini kwa hili wala. Nakumbuka CDM walikuwa makini kwenye suala la sheria ya mchakato wa katiba na wakatoka nje kuonyesha hasira zao. Mwishowe Rais alikubali na sheria ikafanyiwa marekebisho.

      Lakini katika hili mimi sikuwasikia hata kidogo. Nimemsikia Mnyika baada ya wawakilishwa kulalama. Ladda walisoma lakini wakawa na kiwi ya macho hawakuona madhara ya hii sheria kwa jamii.
      CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.

    15. #32
      GAMAH's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th July 2012
      Posts : 37
      Rep Power : 350
      Likes Received
      2
      Likes Given
      20

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      where were you when the bill was passed??? mmetuchosha nyi aghhhhhhhhh

    16. #33
      fikirikwanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 642
      Rep Power : 498
      Likes Received
      149
      Likes Given
      17

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Tunakuunga mkono mnyika na jitihada za kuondoa wizi wa SSRA na mashirika yake

    17. #34
      TOWNSEND's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th May 2011
      Location : kwa ngulelo
      Posts : 1,117
      Rep Power : 630
      Likes Received
      196
      Likes Given
      31

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Quote By GAMAH
      where were you when the bill was passed??? mmetuchosha nyi aghhhhhhhhh
      aliogopa matusi ya ag na spika wangemwambia anawashwa washwa na ile sauti ya spika akisema nafikiri wanaosema ndio wameshinda

      For tommorow belonging to those people who prepared fo it

    18. #35
      MILLIONS MOVEMENT's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd August 2012
      Posts : 111
      Rep Power : 365
      Likes Received
      31
      Likes Given
      13

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Suala hili ni muhimu kujadiliwa kwa manufaa ya wanachama, go Mnyika mtafute na JAFU kwani tayari amepita migodini kukusanya maoni hili ni kwa ajili ya wanachama wa mifuko hii na wala sio la kisiasa kama wengine wanavyotaka kupotosha hapa jamvini

    19. #36
      livingafrican's Avatar
      Member Array
      Join Date : 11th June 2009
      Posts : 20
      Rep Power : 511
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Watanzania kwa lawama ndo wenyewe. Hata kama Mnyika alikuwepo wakati inapitishwa na yeye alipitiwa kwa mfano haimaanishi kwamba ndo akae kimya. Kagundua kosa,amejipanga kupambana upya na huo ndo ujasiri tunaohitaji. kila la heri Mnyika

    20. #37
      Polisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2010
      Posts : 1,533
      Rep Power : 737
      Likes Received
      359
      Likes Given
      234

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Quote By majorbanks
      Unatumia kiungo gani kuwaza?ukishajua alikuwa wapi kipindi icho then what?help yourself to discover how to think with your average mindset..!
      Watu wengine hamuwezi kuongea kwa utaratibu? niambie alikuwa wapi then uone nitakahouliza
      ''Taabu Huisha Bali Ujinga Hudumu''

    21. #38
      Polisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2010
      Posts : 1,533
      Rep Power : 737
      Likes Received
      359
      Likes Given
      234

      Default Re: Mnyika na Mkutano wa mtandao kutoa maoni juu ya SSRA na NSSF

      Quote By Asha Abdala
      We Polisi, si uende huku ulipoelekezwa kwenye mkutano ukamuulize hilo swali akujibu? Ndio nyinyi mnaalikwa kutoa maoni mnakacha mikutano halafu wengine wakifanya maamuzi kwa niaba yenu mnalalamika na kupinga baadaye.

      Asha
      Asante mpenzi
      ''Taabu Huisha Bali Ujinga Hudumu''

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...