Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Zitto Kabwe on Magic FM: Tuhuma za Rushwa, Posho za wabunge na Mbio za Urais 2015

    Report Post
    Page 6 of 6 FirstFirst ... 456
    Results 101 to 108 of 108
    1. #1
      Makutano Show's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd August 2012
      Location : Dar es Salaam, Tanzania
      Posts : 21
      Rep Power : 346
      Likes Received
      65
      Likes Given
      81

      Default Zitto Kabwe on Magic FM: Tuhuma za Rushwa, Posho za wabunge na Mbio za Urais 2015

      Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe leo kuanzia saa tisa mchana atakuwa katika kipindi cha Makutano Magic FM kinachoendeshwa na Fina Mango ambapo atazungumzia na kutoa ufafanuzi kuhusu shutma za rushwa zilizolitikisa Bunge hivi karibuni ikiwa ni pamoja na yeye kudaiwa kuwa mmoja wa wabunge waliohongwa ili kutetea madudu ya Tanesco.

      Pia atazungumzia suala la mbio za Urais 2015 na posho kwa wabunge.

      Wana-JF mnaruhusiwa kuuliza maswali na kutoa maoni ambayo yatasomwa katika kipindi.

      Karibu.
      Quote By Kunta Kinte
      Amejibu ifuatavyo, kwa baadhi nitakayokumbuka

      - Urais, ni kweli ana nia ya kugombea pamoja na kwamba hajasema atagombea 2015,
      - Anashangaa katiba yetu kuweka umri wa mgombea urais uwe 40, wakati baadhi ya nchi jirani ni 35
      - Anapigania nyimbo za wasanii kwenye milio ya simu wapate 50% sasa hivi wanapata kiduchu - 7%?
      - Amekataa kujibu swali la posho na mishahara ya wabunge - kasema aulizwe spika
      - Kwa nini hayupo na wenzie kwenye operation sangara, kasemawamepeana ratiba na pia alikuwa ana ahadi ya kuhudhuria hicho kipindi cha Fina
      - Mwanasiasa ampendaye amesema Halima Mdee, Spokesperson - Bibi Titi Mohamed,

      Hayo ndio baadhi ya niyakumbukayo
      Quote By nngu007
      JUMAPILI, AGOSTI 05, 2012 | EVANS MAGEGE

      *Asema hajawahi kutangaza mwaka
      *Akiri ni vigumu bila baraka za chama
      *Aahidi kumuunga mkono atakayeteuliwa
      *Masha naye aibuka, autolea macho ubunge


      JINAMIZI la urais linaendelea kumwandama Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA).

      Hali hiyo imetokana na mwanasiasa huyo machachari kushindwa kuweka wazi mwaka wa uchaguzi ambao atagombea urais kama ambavyo amekwisha kutangaza.

      Zitto alipatwa na kigugumizi hicho jana alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha Makutano kinachorushwa na radio ya Magic FM ya Dar es Salaam.

      Zitto alihojiwa kuhusu masuala mbalimbali na katika suala la urais aliendelea kusisitiza kuwa anautaka ingawa alishindwa kutaja mwaka ambao atatekeleza azma yake.

      Zitto alisema suala la kugombea urais ni azma yake kutoka moyoni na kueleza kuwa yeye ni tofauti na wanasiasa wengine ambao hulitaka jambo kwa kisingizio cha kutumwa na watu wengine.

      “Ni kweli nautaka urais jambo ambalo nataka Watanzania wajue, mimi sikusema ni lini lakini nia yangu ipo…iwe mwaka 2015, 2020 au 2025.

      “Dhamira yangu nataka siku moja kuliongoza taifa langu, kama mwanasiasa mkomavu huu ni uamuzi wangu kutoka moyoni, sijatumwa wala kuagizwa na mtu yeyote.

      “Siamini katika kauli za kutumwa, kuombwa wala kuagizwa ila kwa mwanasiasa anayejiamini katika uongozi lazima athubutu kuweka dhamira ya kweli katika kuongoza wananchi,”alisema Zitto.

      Hata hivyo, Zitto alisema pamoja na dhamira yake hiyo, ataendelea kufuata sheria na taratibu ambazo ni pamoja na kupata ridhaa ya chama chake cha CHADEMA.

      Zitto ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisema hadi hivi sasa chama chake hakina mgombea urais na kueleza kuwa muda ukifika suala hilo litakuwa bayana.

      Zitto alisisitiza kuwa hana ubinafsi juu ya hoja hiyo na kusema kuwa mwanachama yeyote atakayeteuliwa kupeperusha bendera katika wadhifa huo yuko tayari kumuunga mkono.

      Akizungumzia suala la tuhuma za rushwa linalohusisha wabunge kuhongwa na kampuni na baadhi ya makampuni ya mafuta, Zitto alirejea msimamo wake wa kupinga kuhusika katika rushwa.

      Zitto alisema binafsi yake anaiamini tume iliyoundwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda katika kushughulikia sakata hilo kwa kusema kuwa ripoti ya tume hiyo itabainisha ukweli iwapo anahusika au laa.

      “Kwa sasa tumekuwa katika taifa la majungu, uwongo, fitna na tuhuma zisizokuwa na maana na haya yamekuwa kama maisha ya kawaida ya wananchi.

      “Nadhani kwa hili tusiliongelee sana na tuiachie tume iliyoundwa kuchunguza jambo hili ifanye kazi kwa uhuru mkubwa..kwani inatakiwa kutoa majibu yake ndani ya siku 14…msihofu majibu yatatoka tu hivu karibuni,”alisema Zitto.

      Zitto pia alisisitiza kuwa yeye siyo mla rushwa na wala hajawahi kula rushwa.

      Mwanasiasa huyo kijana anadaiwa kuwa na utajiri mkubwa na baadhi ya mali anazodaiwa kuwa nazo ni pamoja na ujenzi wa kasri unaoendelea Mbezi Dar es Salaam na magari ya kifahari.

      Katika mahojiano hayo, Zitto alikanusha madai hayo akisema maneno yote hayo yaliyoibuka ni fikra hasi juu ya nafasi yake ya uenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC).

      “Dhamana niliyonayo katika POAC inawajenge watu sura tofauti ya labda najinufaisha na madaraka yangu katika kamati hiyo…nasimamia mashirika zaidi ya 290, kwa hiyo wanafikiri Zitto ni tajiri.

      “Na kama vile haitoshi ule msimamo wangu kupinga posho za ubunge nayo ilifanya wengi wachukie …lakini nitaendelea na msimamo wangu ule ule.

      “Kuhusina na mali zangu ..mimi si tajiri kama wengi wanavyodhani, sina Range Rover, Hammer au jumba la fahari kama watu wanavyozusha.

      “Mimi ninajenga Kigoma, Dar es Salaam sina nyumba, sina kiwanja achilia mbali kiwanja sijawahi kuomba kiwanja Dar es Salaam wala Dodoma, hilo kasri nitakuwanalo wapi?.

      “Nakumbuka siku hiyo mambo haya yaliibuka ilikuwa siku ambayo bajeti ya Nishati na Madini ilikuwa inawasilishwa ….na katika wakati mwengine siku hiyo hiyo, mishahara na posho mpya kwa wabunge zilianza kutoka, hivyo basi wabunge wengi walichangia jambo hilo hadi wengine wasiopenda kuzungumuza siku hiyo walizungumza,” alisema Zitto.

      Alipohojiwa juu ya kiasi kipya cha posho na mshahara Zitto alikataa katu katu kuzungumzia hoja hiyo na kusema kuwa mtu wa kuulizwa ni Spika wa Bunge, Anne Makinda.

      Wakati huohuo, aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha alisema bado anayo dhamira ya kuwania tena ubunge katika jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza.

      Masha aliangushwa na mbunge wa sasa jimbo hilo, Ezekia Wenje wa Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2010 na hivyo kupoteza ubunge pamoja na uwaziri.

      Masha ambaye alikuwa akihojiwa katika kipindi hicho alisema bado anayo dhamira ya kugombea tena kiti hicho cha ubunge wa Nyamagana lakini hajaamua atafanya hivyo lini.

      Alisema kuwa hawezi kutangaza ni lini atafanya hivyo lakini iwapo wananchi wa jimbo hilo watamuhitaji kugombea uchaguzi ujao wa 2015 atafanya hivyo.

      “Nikigomea tena sitashindwa …suala la kutaka kugombea ni lazima lakini kwa sasa nafanya biashara zangu binafsi…najipanga nitarudi tena katika siasa,” alisema Masha.

    2. FemaTV & Radio

    3. #101
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 528
      Rep Power : 537
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Zito kabwe asafisah hali ya hewa-asema sio mla rushwa, anashirikiana na chama kukijenga

      Kama kawaida mimi napenda kutoa maoni ya kile ninachoona ni sawa bila kufuata ushabiki wowote wa chama pamoja na kwamba mimi ni mfuasia wa chama kimoja tu humu ndani ya Jamhuri.
      Zitto ni kiongozi amabaye anaonekana kuwa na kiu kubwa ya mafanikio, huenda anataka ikiwezekana yaje kesho. Tabia na mwenendo wake vinanipa kuamini kuwa Ifikapo mwaka 2020 pengine atakuwa na uzoefu wa kutosha kuongoza nchi hii. Si maanishi umri bali Utulivu wa ki-utu uzima bado hajaufikia. Hata tatizo kuu ninaloliona kwa raisi wetu wa sasa ni hilohilo. yaani kakosa utulivu wa ki-utu uzima. Utulivu huu hauji kwa kuishi miaka mingi, wala kwa kufanya kazi mda mrefu. Sharti uzaliwe nao kisha uendelee kukomaa taratibu kwa kadiri unavyoishi. Zito anao ila nadhani mpaka 2018 utakomaa lakini si 2015

    4. #102
      Pendael laizer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th January 2012
      Posts : 945
      Rep Power : 560
      Likes Received
      90
      Likes Given
      5

      Default Re: Zito kabwe asafisah hali ya hewa-asema sio mla rushwa, anashirikiana na chama kukijenga

      Aache uropokaji wa kiaina manake anajiona yeye ndiye top.. Ajenge chama chake kwanza urais baadaye

    5. #103
      Ally Kanah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Posts : 780
      Rep Power : 559
      Likes Received
      37
      Likes Given
      35

      Default

      Quote By Crucifix
      Hayo maneno kayasemea wapi na kamsemea nani?
      Magic Fm akihijowa na Fina Mango katika kipindi kipya kiitwacho MAKUTANO
      kinepi_nepi likes this.

    6. #104
      Ally Kanah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Posts : 780
      Rep Power : 559
      Likes Received
      37
      Likes Given
      35

      Default

      Quote By Radhia Sweety
      Hizi habari nyingine bwana hatari tupu. Yaani mtu anajitungia tu maneno yake na kuyarusha JF. Na kwasababu JF imejaa watu wa kuchangia chochote hata kama kimetoka uvunguni, basi ndiyo hivyo tena watu wachangia tu uzi.
      http://www.youtube.com/watch?v=mHBD9WlIZB
      Na

      http://www.youtube.com/watch?v=yEK5o...e_gdata_player

      Sasa povu litaacha kukutoka hapo ndipo ZZK aliposemea
      kinepi_nepi likes this.

    7. #105
      kinepi_nepi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2007
      Posts : 878
      Rep Power : 1209
      Likes Received
      223
      Likes Given
      118

      Default Re: Zito kabwe asafisah hali ya hewa-asema sio mla rushwa, anashirikiana na chama kukijenga

      Quote By Crucifix
      Hayo maneno kayasemea wapi na kamsemea nani?
      Magic FM akihojiwa na Fina Mango
      Quote By Radhia Sweety
      Hizi habari nyingine bwana hatari tupu. Yaani mtu anajitungia tu maneno yake na kuyarusha JF. Na kwasababu JF imejaa watu wa kuchangia chochote hata kama kimetoka uvunguni, basi ndiyo hivyo tena watu wachangia tu uzi.
      Sina historia ya kutengeneza habari angalia record yangu, sina sababu yeyote ya kumtungia au kumzushia mtu, ninaheshimu sana utu wa mtu. Zito kasema kwa akauli yake na kwasababu yuko humu usijali atakuja mwenyewe akiona inafaa.

      Quote By Ukwaju
      Kasema wapi na lini? maana humu sasa itaanza habari, chanzo hatukijui, mm huyu jamaa namkubali lkn akitokeza tena TUNTEMEKE mara Shose Genda huelewi nani ni nani ndo maana mm nakimbia hizi story sasa
      Quote By Pendael laizer
      Aache uropokaji wa kiaina manake anajiona yeye ndiye top.. Ajenge chama chake kwanza urais baadaye
      Inawezekana haropoki ila anasema anachokiamini, tuwe na uwezo wa kumwelewa wakati mwingine sio rahisi wote wakawa sawa. Misimamo inatofautiana.
      Quote By Desi Mangola
      Magic Fm akihijowa na Fina Mango katika kipindi kipya kiitwacho MAKUTANO
      Asante sana Mkubwa umenisaidia sana
      "Power never takes a back step only in the face of more power. Nobody can give you freedom, equality or justice or anything. If you're a man, you take it."

    8. Miaka 50

    9. #106
      kinepi_nepi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2007
      Posts : 878
      Rep Power : 1209
      Likes Received
      223
      Likes Given
      118

      Default Re: Zito kabwe asafisah hali ya hewa-asema sio mla rushwa, anashirikiana na chama kukijenga

      Quote By Precise pangolin
      Napia akumbuke kwa sasa urais sio size yake
      Kama kaweza kuwa mbunge anaweza kuwa Raisi, Sioni sababu ya yeye kutokuwa Raisi zaidi ya logistics na labda timing anayotumia zaidi ya hapo he is ok.
      "Power never takes a back step only in the face of more power. Nobody can give you freedom, equality or justice or anything. If you're a man, you take it."

    10. #107
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 528
      Rep Power : 537
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Zito kabwe asafisah hali ya hewa-asema sio mla rushwa, anashirikiana na chama kukijenga

      Quote By Desi Mangola
      umempatia kwelikweli huyu jamaa, Badala ya kuuliza chanzo anakandia, haya akandie na hapo tena

    11. #108
      Ally Kanah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Posts : 780
      Rep Power : 559
      Likes Received
      37
      Likes Given
      35

      Default

      Quote By salosalo
      umempatia kwelikweli huyu jamaa, Badala ya kuuliza chanzo anakandia, haya akandie na hapo tena
      Watu kama hao wanaoutumiwa dawa yao ndio hiyo Mkuu

    Page 6 of 6 FirstFirst ... 456

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...