Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanakijiji wamkataa mwekezaji

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,153
      Rep Power : 3544
      Likes Received
      3037
      Likes Given
      460

      Default Wanakijiji wamkataa mwekezaji

      Burhani Yakub, Tanga






      WAKAZI wa Kijiji cha Kwedikwabu, Kata ya Kwamsisi, wilayani Handeni, wamemuomba Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa kuingilia kati sakata la mwekezaji mmoja kutoka Dar es Salaam kuvamia eneo lao lenye ukubwa wa ekari 2,000.


      Akizungumza kwa niaba ya ujumbe wa wanakijiji hao waliofika ofisi za gazeti hili mjini hapa, Ramadhani Bakari alisema walishtuka baada ya kuona watu wakifyeka eneo kutayarisha shamba hatua iliyowalazimisha kuwafukuza.


      “Tulishtuka baada ya kuona kuna watu porini wakifanya kazi ya kufyeka, tulipowakamata walimleta mwekezaji huyo ambaye alijitetea kuwa, ameuziwa na mzee mmoja wa kijijini tukamwambia umetapeliwa kwa sababu hukufuata taratibu,” alisema Bakari.


      Alisema walipomfukuza alirejea Dar es Salaam, lakini baadaye alirudi tena kijijini na kuanza kufyeka huku akisisitiza kuuziwa eneo hilo.


      Bakari alisema baada ya kurejea tena kijijini, wananchi waliomba uongozi wa kijiji kuitisha mkutano mkuu ambao uliamua kumkataa mwekezaji huyo, huku akipewa amri ya kuondoka mara moja.


      Akizungumzia suala hilo kwa simu, Mtendaji wa kijiji hicho, Juma Shaaban alikiri wanakijiji kumkataa mwekezaji huyo katika mkutano huo kwa kupiga kura nyingi za kutaka aondoke.Shaaban alisema baada ya uamuzi wa mkutano mkuu wa kijiji aliwasiliana na Polisi Kituo cha Mkata, walipelekwa askari na kumuamuru aondoke kwani wanakijiji hawamtaki.


      “Mkutano mkuu wa kijiji ulifanyika Julai 8, mwaka huu wananchi walipiga kura nyingi za kumkataa, nikapeleka taarifa hadi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni,”alisema.

      Chanzo: Mwananchi

    2. Miaka 50

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,153
      Rep Power : 3544
      Likes Received
      3037
      Likes Given
      460

      Default Re: Wanakijiji wamkataa mwekezaji


      Hawa ndio Wanakijiji wanaojua kuwa Muungano ndio utakao linda Ardhi yao; Hawana Mchezo...

      Hawana Mchezo wamemuondoa Mwekezaji na Wamemuita Mkuu wa Mkoa kumueleza hayo, hii ndio inavyotakiwa

      People's Power; Wa Gezaulole wangeungana pamoja sidhani ardhi yao ingebwa kurahisi na Mabosi wa Serikali Kuu na

      Watoto Wao Wapendwa. Wakulima wetu wana NGUVU bado na wana kura sababu wengi bado wapo vijijini...

    4. #3
      zungupori's Avatar
      Member Array
      Join Date : 30th July 2012
      Location : Hapa na pale
      Posts : 71
      Rep Power : 356
      Likes Received
      6
      Likes Given
      15

      Default Re: Wanakijiji wamkataa mwekezaji

      nahisi hili sakata halijaisha, sikilizia mwana hii nchi ni kupandisha dau tu. Iwapo huyo mwekezaji ana interest tosha na eneo hilo, wanakijiji itabidi wawe prepared for kiinimacho. Kwani huyu mwekezaji ni mzungu au mbongo? For the villagers sake I hope a mzungu is not involved sababu sarakasi mbili tatu watu weweee, unalose focus kabla hujajiju kihamba kimehamishwa

    5. #4
      Father of All's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2012
      Posts : 3,093
      Rep Power : 1044
      Likes Received
      1828
      Likes Given
      3343

      Default Re: Wanakijiji wamkataa mwekezaji

      Huyo si mwekezaji ni mwizi wa kawaida. Usishangae hata akawa rais au mawaziri wake hata mkuu fulani wa mkoa kama si mbunge au mfanyabiashara aliyewatia kapuni watawala. Walipaswa wamchome moto huyo sawa na wanavyowafanyia vibaka. Wanakijiji hakikisheni mnafunga hata barabara na kuhakikisha hamfanyiwi huo ujinga.

    6. #5
      King'asti's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th November 2009
      Location : The Jungle
      Posts : 17,112
      Rep Power : 28887
      Likes Received
      11616
      Likes Given
      4783

      Default Re: Wanakijiji wamkataa mwekezaji

      Wananchi hawajamkataa mwekezaji, wamekataa kuibiwa ardhi yao! Huu ni upotoshaji wa habari.

      Taratibu za kuuza ardhi za kijiji inapaswa kuboreshwa. Na viongozi waache tamaa! Siku hizi hata hatua 20x20 shurti kijiji kihusike na kuna fees za kulipa. Ila mamlaka ya viongozi wa kijiji inahitaji limit. Isitoshe sheria inataka ununuzi na uwekezaji wa 50+ acres EPZA wahusishwe.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Omonto wa-hene's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 147
      Rep Power : 388
      Likes Received
      39
      Likes Given
      37

      Default Re: Wanakijiji wamkataa mwekezaji

      Hapa wala hakuna kilichofanyika. Angekuwa ngozi nyeupe ninyi nyoooote mngeufyata tu na kuishia kulalama kwenye vyombo vya habari huku mtasha wa watu akiendelea kufyeka, kuvuna magogo, kuchimba mahandaki na kuondoka na wake zenu kwenda kustarehe nao fukweni. Pambaf nyie!!!

    9. Study Abroad

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...