Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

    Report Post
    Page 1 of 7 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 133
    1. #1
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 577
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Polisi katika manispaa ya mji wa Morogoro wamezuia operation sangara ya CHADEMA kwa sababu za kuwa hakuna askari wa kutosha kusimamia mikutano yao katika mkoa wa Morogoro.

      Lakini pamoja na makatazo hayo CDM wamedai wao wataendelea na mikutano yao kama kawaida kwa sababu haisuani na fujo wala vurugu na siku zote Polisi huwa hawawasaidii kwa lolote.

      Concern

      Jeshi la PolisiCCM liko kwa ajili ya kuzuia CDM sio kulinda


    2. #2
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,532
      Rep Power : 18655
      Likes Received
      3624
      Likes Given
      2380

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Polisi wakusimamia hawapo, lakini mkutano ukifanywa, polisi wakuwasambaratisha wapo. Tanzania ni zaidi ya tuijuavyo!

    3. #3
      Mzizi wa Mbuyu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2009
      Posts : 3,387
      Rep Power : 1311
      Likes Received
      590
      Likes Given
      430

      Default

      Quote By dosama View Post
      Polisi katika manispaa ya
      mji wa Morogoro wamezuia operation sangara ya CHADEMA kwa sababu za kuwa
      hakuna askari wa kutosha kusimamia mikutano yao katika mkoa wa
      Morogoro.

      Lakini pamoja na makatazo hayo CDM wamedai wao wataendelea na mikutano
      yao kama kawaida kwa sababu haisuani na fujo wala vurugu na siku zote
      Polisi huwa hawawasaidii kwa lolote.

      Concern

      Jeshi la PolisiCCM liko kwa ajili ya kuzuia CDM sio kulinda
      Sasa utaona kituko.. Polisi wa kuvunja mkutano huo wa kukaidi agizo la polisi kuwa hawatoshi watakuwa wengi mno!
      othorong'ong'o and mecy like this.

    4. #4
      Jembe Ulaya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th October 2008
      Posts : 414
      Rep Power : 625
      Likes Received
      95
      Likes Given
      127

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Polisi watatangaza mikutano ni batili. Hawataisogelea, lakini wananchi wataogopa kwenda, mahudhurio yatakuwa pungufu. Azma yao itakuwa imetimia. Usalama wa Taifa unafanya kazi yake waliotumwa.
      CHADEMA CHAWEMA CHAWEZA!

    5. #5
      Mzito Kabwela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th November 2009
      Location : MPUMBULI
      Posts : 7,524
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1133
      Likes Given
      8

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Chadema hawana kazi nyingine ya kufanya zaidi ya hizo operation mbuzi?


    6. #6
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,988
      Rep Power : 2594
      Likes Received
      641
      Likes Given
      777

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Kama hawatoshi wakalale. Hawana umuhimu katika mikutano ya CDM. CDM hawana fujo, ila wanapochokozwa na Policts.
      Last edited by Fredrick Sanga; 3rd August 2012 at 09:07.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    7. #7
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,542
      Rep Power : 1269
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      29

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By Filipo View Post
      Polisi wakusimamia hawapo, lakini mkutano ukifanywa, polisi wakuwasambaratisha wapo. Tanzania ni zaidi ya tuijuavyo!
      Si ndo hapo... Wakifanya mkutano utaona defender tatu zinaletwa zote zimejaa polisi hii nchi bana
      mecy likes this.
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    8. #8
      pembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 342
      Rep Power : 505
      Likes Received
      94
      Likes Given
      346

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Cdm tunaomba bendera kwani ni alama tosha ya utambulisho wa uwepo wenu. Operesheni zikipita bila kucha alama wananchi tunawasahau kila tunapoona kijani kinapepea!

    9. #9
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,555
      Rep Power : 1066
      Likes Received
      1288
      Likes Given
      621

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By Janatu Firdaus View Post
      Chadema hawana kazi nyingine ya kufanya zaidi ya hizo operationmbuzi?

      Acha uzushi...ni Operation Sangara sio mbuzi.
      REMSA likes this.
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    10. #10
      thatha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 7,281
      Rep Power : 0
      Likes Received
      239
      Likes Given
      1

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By dosama View Post
      Polisi katika manispaa ya mji wa Morogoro wamezuia operation sangara ya CHADEMA kwa sababu za kuwa hakuna askari wa kutosha kusimamia mikutano yao katika mkoa wa Morogoro.

      Lakini pamoja na makatazo hayo CDM wamedai wao wataendelea na mikutano yao kama kawaida kwa sababu haisuani na fujo wala vurugu na siku zote Polisi huwa hawawasaidii kwa lolote.

      Concern

      Jeshi la PolisiCCM liko kwa ajili ya kuzuia CDM sio kulinda
      Kwani wewe ulichokusudia ni kutujuza agizo la polisi au ktoa concern yako?

    11. #11
      thatha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 7,281
      Rep Power : 0
      Likes Received
      239
      Likes Given
      1

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By Mkirua View Post
      Acha uzushi...ni Operation Sangara sio mbuzi.
      Nadhani yuko sahihi kuuliza hinvyo, is too much. Wakumbuke kibaya Chajitembeza na kizuri chajiuza.

    12. #12
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,555
      Rep Power : 1066
      Likes Received
      1288
      Likes Given
      621

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By thatha View Post
      Kwani wewe ulichokusudia ni kutujuza agizo la polisi au ktoa concern yako?
      All of the above..
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    13. #13
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,555
      Rep Power : 1066
      Likes Received
      1288
      Likes Given
      621

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By thatha View Post
      Nadhani yuko sahihi kuuliza hinvyo, is too much. Wakumbuke kibaya Chajitembeza na kizuri chajiuza.
      Kama una uhakika povu la nini??
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    14. #14
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,988
      Rep Power : 2594
      Likes Received
      641
      Likes Given
      777

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      CDM Mshughulikie Morogoro mpaka kieleweke, Hata vile viwanda vilivyobinafsishwa kwa wakubwa vinafugiwa mbuzi. huu mkoa unahitaji ukombozi wa jumla.
      mecy likes this.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    15. #15
      DALLAI LAMA's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st February 2012
      Posts : 3,122
      Rep Power : 0
      Likes Received
      741
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Janatu Firdaus View Post
      Chadema hawana kazi nyingine ya kufanya zaidi ya hizo operation mbuzi?
      that wy DHAIFU alisema chama cha msimu..kazi ya chama cha siasa ni kuzungumza na wanachama.ulitaka wakeshe baa?

    16. #16
      Baba V's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Location : Planet Nibiru
      Posts : 11,577
      Rep Power : 42530
      Likes Received
      5091
      Likes Given
      4370

      Default

      Quote By Janatu Firdaus View Post
      Chadema hawana kazi nyingine ya kufanya zaidi ya hizo operation mbuzi?
      na zitawanyoosha hivyohivyo pamoja na umbuzi wake!

    17. #17
      Wi-Fi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Location : 6°49′24″ S 39°16′10″ E
      Posts : 1,180
      Rep Power : 692
      Likes Received
      331
      Likes Given
      196

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By Janatu Firdaus View Post
      Chadema hawana kazi nyingine ya kufanya zaidi ya hizo operation mbuzi?
      hebu toa mapendekezo yako kwamba wafanye kazi gani tofauti na iyo, izo ni opereshen sangara tu, sangara akiwa mkubwa kama mbuzi wewe utazikwa ukiwa hai
      Most discoveries happened by accident!

    18. #18
      HIMO ONE's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th September 2010
      Posts : 129
      Rep Power : 468
      Likes Received
      6
      Likes Given
      4

      Default Taarifa za kiitelijensia zazua balaa

      MKUTANO WAO WAPIGWA MARUFUKU,WENYEWE WASEMA LAZIMA UFANYIKE
      Joseph Zablon
      CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeingia tena katika mzozo na Jeshi la Polisi nchini, baada ya mkutano wake uliopangwa kufanyika mjini Morogoro kuzuiwa kwa maelezo kwamba, hakuna askari wa kutosha wa kuuwekea ulinzi.

      Pamoja na zuio hilo, Chadema wanasema lazima mkutano huo ufanyike kwa maelezo kwamba sababu zilizotolewa na polisi siyo za msingi na zina ajenda ya kuhujumu kampeni yao waliyoiita ‘vua gamba, vaa gwanda’.

      Mvutano huo unatishia amani mji wa Morogoro na viunga vyake, ikiwa Chadema wataendelea na msimamo wao huo, hali polisi wakitumia nguvu kuzuia mkutano huo na mingine midogo katika kata 28 iliyoombwa isifanyike.

      Chadema kiliwahi kuingia katika mvutano na polisi katika baadhi ya matukio makubwa ambayo ni pamoja na katika miji ya Mwanza huku mapambano ya jijini Arusha yakisababisha mauaji.

      Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Dar es Salaam jana, Mkuu wa Operesheni wa Chadema, Benson Kigaila alisema kuwa wamepokea taarifa ya polisi ya kuwataka wasifanye mkutano huo, lakini wao kama chama hawatarudi nyuma.

      "Mkutano wetu upo palepale na utahudhuriwa na viongozi wote wa kitaifa, wakiwamo wabunge wetu wote na utafunguliwa na Mwenyekiti wa wetu wa Taifa, Freeman Mbowe," alisema Kigaila.

      Kigaila alisema mikutano hiyo ni ya kukiimarisha chama na inaratibiwa na chama na sio polisi hivyo, kwa jeshi hilo walikuwa wanatoa taarifa na kuomba ulinzi na sio kulitaka liwapangie utekelezaji wake.

      "Mkutano ni makubaliano ya ndani ya chama na ajenda yetu ni kuwahamasisha Watanzania kujiunga na chama na ni sehemu ya operesheni Sangara," alisema Kigaila na kuongeza kuwa, maandalizi kwa ajili ya mkutano huo yamekamilika.

      Zuio la mkutano
      Kigaila alisema zuio la mkutano huo limetokana na barua yenye kumbukumbu Namba MRG/SO.7/2/A/219, ya Agosti Mosi mwaka huu kutoka kwa Kamanda wa Polisi Morogoro kwenda kwa Katibu Chadema wilaya.

      Kigaila alisema baada ya kujitokeza hali hiyo aliwasiliana na kamanda wa polisi na walimuomba wafanyie mkutano wao eneo la Mvomero ombi ambalo pia lilikataliwa kwa madai kuwa haiwezekani kutokana na mgomo wa walimu.

      "Mara waseme kuna Nane nane, CCM nao wana mkutano Morogoro hivyo haiwezekani, tunapomwambia tukafanyie Mvomero anadai kuna mgomo wa walimu sasa hoja yake ipi hapa tunashindwa kumuelewa," alisema Kigaila.

      Alidai ni wazi jeshi hilo linatumika kwa manufaa ya kisiasa kwani yeye anavyofahamu ni kwamba ikiwa kuna vyama viwili vinavyotaka kufanya mikutano yake, basi hupangiwa maeneo tofauti.

      "Kama wengine wakipanga eneo fulani basi sheria inataka chama kingine kifanye mkutano wake mita 500 kutoka walipo wenzao,” alisema.

      Kigaila alisema mkutano wao huo utafuatiwa na mingine katika kata 28 za mji huo kabla ya kuelekea katika miji ya Iringa, Dodoma, Manyara na Singida na awamu inayofuata itahusisha mikoa ya Tabora, Shinyanga, Simiyu na Mwanza.

      Operesheni hiyo itaendelea katika miji ya Mara, Kagera na Geita kabla ya kurudi kumalizia mikoa iliyokuwa imesalia Kusini na ni operesheni ya kawaida ya kuhamasisha watu kujiunga na chama hicho

      Taarifa ya polisi
      Kulingana na taarifa hiyo (ambayo Mwananchi limeona nakala yake), sehemu yake inasomeka: “Rejea barua yako ya Julai 30, 2012 ya kutoa taarifa na kuomba ulinzi kwa ajili ya maandamano na mikutano ya hadhara mliyokusudia kufanya K/Ndege Agosti 4, 2012 na Agosti 5 kwa Kata 28”.

      "Katika tarehe zilizoainishwa hapo juu Chama cha Mapinduzi (CCM), wamekusudia kufanya mikutano ya hadhara ya wanachama, wapenzi na makada wao katika maeneo hayo hayo," inasema taarifa hiyo.

      Inaongeza kuwa Agosti mosi hadi 10 mwaka huu, maadhimisho ya sherehe za Nane Nane yanaendelea katika Mkoa huo na kama vile haitoshi, katika tarehe zilizoanishwa, mgomo wa walimu wa shule za msingi na sekondari unaendelea nchi nzima.

      Sehemu ya taarifa hiyo iliongeza kwamba, kutokana na sababu hizo shughuli zote zinahitaji ulinzi na usalama ambao utasimamiwa na polisi, hivyo kutokana na mgawanyo uliopo wa askari itakuwa vigumu kusimamia shughuli zote kwa wakati mmoja.

      "Kwa mantiki hiyo, kamanda wa polisi Mkoa wa Morogoro amesitisha mikutano ya hadhara na maandamano hayo kwa mujibu wa kifungu namba 43 (1-6) cha sheria za Polisi na polisi wasaidizi sura 322 kama ilivyorekebishwa mwaka 2002," inabainisha barua hiyo.
      “SKILFULL AND CONFIDENCE IS UNCONQUERED ARMY”

    19. #19
      Crucifix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 1,571
      Rep Power : 806
      Likes Received
      431
      Likes Given
      321

      Default Sijawaelewa polisi kuhusu mkutano wa CDM

      Nimesoma habari kuwa polisi wamekataza mkutano wa CDM Morogoro kisa na sababu hawana polisa wa kutosha kulinda mkutano huo. Hadi hapa ninaelewa. Nisipoelewa ni pale polisi wanaposema watatumia nguvu kuzuia mkutano huo. Ina maana kama CDM watakusanyika polisi watawatawanya na kuwasambaratisha.

      Nisichokielewa - kama hawana polisi wa kutosha kulinda amani, hao wa kusambaratisha watawatoa wapi? Kipi kinahitaji nguvu zaidi baina ya kusimamia amani na kutuliza amani?

      Nielekezeni wenye kujua mambo hayo
      LORDVILLE likes this.
      Jesus, Adoramus te. Dominus meus et Deus meus

    20. #20
      rugo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th June 2012
      Posts : 27
      Rep Power : 358
      Likes Received
      11
      Likes Given
      1

      Post Zuio la Mkutano wa CHADEMA MORO

      Sababu zilizotolewa na jeshi la polisi kuzuia mkutano wa CHADEMA huko Morogoro, je zina mashiko? Sababu zenyewe ni kwamba; walivyotaka kufanyia Moro mjini wakaambiwa CCM pia wana mkutano, wakaomba kwenda kufanyia Mvomero, wakaambiwa haiwezekani kwa sababu kuna mgomo wa walimu. Sasa kama kuna mgomo wa walimu, ina maana mkutano wa CCM hautaathiriwa na mgomo wa walimu, au mgomo wa walimu upo Mvomero tu?

      Nawasilisha.
      Last edited by rugo; 3rd August 2012 at 09:38. Reason: add details

    Page 1 of 7 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...