Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

    Report Post
    Page 7 of 7 FirstFirst ... 567
    Results 121 to 133 of 133
    1. #1
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 573
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Polisi katika manispaa ya mji wa Morogoro wamezuia operation sangara ya CHADEMA kwa sababu za kuwa hakuna askari wa kutosha kusimamia mikutano yao katika mkoa wa Morogoro.

      Lakini pamoja na makatazo hayo CDM wamedai wao wataendelea na mikutano yao kama kawaida kwa sababu haisuani na fujo wala vurugu na siku zote Polisi huwa hawawasaidii kwa lolote.

      Concern

      Jeshi la PolisiCCM liko kwa ajili ya kuzuia CDM sio kulinda

    2. Miaka 50

    3. #121
      Zipuwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Posts : 2,200
      Rep Power : 870
      Likes Received
      307
      Likes Given
      123

      Default Re: Mgongano wa Chadema na Polisi Morogoro:Nampongeza RPC Shilogile

      hata alichokifinya jana kamanda wa polisi Morogoro bado ni wa kikoloni hakuna jipya hapo hata angekuwa na master ya sheria bado anatumikia polissm
      Maisha yetu ni mafupi lazima tuyatete kwa namna yeyote ile!

    4. #122
      MATESLAA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2011
      Location : KINONDONI STUDIO
      Posts : 1,252
      Rep Power : 644
      Likes Received
      62
      Likes Given
      32

      Default Re: Mgongano wa Chadema na Polisi Morogoro:Nampongeza RPC Shilogile

      mi nadhani police wanaakili za kutosha lakini mwajili wao yani bosi wao hakuna kitu upepo mtupu kwa kifupi ni abunuasi
      NAZI AIMENYWI ....INAKUNWA

    5. mob
      #123
      mob's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2009
      Posts : 594
      Rep Power : 599
      Likes Received
      103
      Likes Given
      35

      Default Re: Mgongano wa Chadema na Polisi Morogoro:Nampongeza RPC Shilogile

      jAMAA ALIKUWA HAYUKO SERIOUS IWEJE ASEMA KUWA HAKUNA POLISI WA KUTOSHA KULINDA MKUTANO ILA TUMEKUJA KUONA KUNA POLISI WA KUTOSHA KATIKA KUZUIA MAANDAMANO.nA KAMA HAKUTUMIA BUSARA MORO INGEJEUKA KUWA KAMA MBEYA AU ARUSHA,vIVA CHADEMA TUTAFIKA TU KWA JAMBO HILI WANANCHI PIA WAKO NYUMA YENU
      Mpita Njia likes this.

    6. #124
      malaka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 996
      Rep Power : 644
      Likes Received
      237
      Likes Given
      66

      Default Re: Mgongano wa Chadema na Polisi Morogoro:Nampongeza RPC Shilogile

      Eti hakuna polisi wa kutosha kulinda mkutano. Wakat hao polisi waliomwagwa jana wapo zaidi ya mia. Hakuna kitu hapo walewale.

    7. #125
      PROFESA KYANDO's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th July 2012
      Posts : 83
      Rep Power : 360
      Likes Received
      6
      Likes Given
      5

      Default Mwananchi; chadema yakwama kufanya mkutano

      Chadema yakwama kufanya mkutano Send to a friend
      Sunday, 05 August 2012 00:15

      MKUU wa Operasheni wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Singo Benson, akizungumza na wanachama na wapenzi wa chama hicho katika ofisi za Wilaya za chama hicho kuhusu kuahirishwa kwa maandamano na mkutano wa chama hicho uliokuwa ufanyike jana mjini Morogoro . Picha na Juma Mtanda

      VIONGOZI, POLISI WAKUBALIANA UFANYIKE AGOSTI 8 KILOSA, FFU WAMWAGWA MITAANI KUDHIBITI WAFUASI
      Venance George, Morogoro
      BAADA ya mvutano wa siku mbili baina ya Jeshi la Polisi na Chadema kilichopanga kufanya mkutano mjini Morogoro jana, pande hizo mbili zilikubaliana kuwa mkutano wa kwanza ufanyike Agosti 8, mwaka huu Mikumi, wilayani Kilosa.Makubaliano haya yanakuja kufuatia mazungumzo baina ya viongozi wa Jeshi la Polisi mkoani Morogoro na wale wa Chadema kuwa, kwa vile maonyesho ya Nanenane mkutano huo usongezwe mbele na ufanyike wilayani Kilosa Agosti 8, mwaka huu.
      Awali Jeshi la polisi lilizuia kwa madai kutokana na kuwapo mgomo wa walimu nchini ambao ulisitishwa kwa amri ya mahakama Alhamisi iliyopita pamoja na kwamba, jeshi hilo halitakuwa askari wa kutosha na kusimamia matukio hayo.
      Hata hivyo, kabla ya kufikiwa makubaliano jana hayo askari wengi wakiwagwa mitaani kudhibiti wafuasi wa Chadema kuandamana na kufanya mkutano wa hadhara.
      Wakiwa na mabomu ya kutoa machozi, magari yenye maji ya kuwasha, silaha za moto na virungu, vikosi hivyo vilikabiliana na baadhi wafuasi hao kwenye mitaa mbalimbali mjini hapa na kufanikiwa kuwatia nguvuni baadhi yao.
      Hali hiyo ilitokana na wafuasi hao kumiminika kwenye ofisi za Chadema mjini hapa kwa ajili ya kuandaa maandamano hadi kwenye Viwanja ambavyo walitarajia kufanyia mkutano wa hadhara.
      Wafuasi hao wa Chadema pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali walishiriki kwenye vuguvugu hilo ambalo chama kimelipa jina Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), licha polisi kutoa onyo kuwa wasithubutu kufanya maandamano na mikutano hiyo, kwa kile walichodai ni kutokuwa na askari wa kutosha wa kutoa ulinzi.
      Jana asubuhi, Jeshi la polisi lilitawanya askari wake kwenye mitaa mbalimbali ya Mji wa Morogoro na barabara zote za kuingia na kutoka katika mji huo.
      Magari yenye maji ya kuwasha pamoja na yale yaliyopakia askari wa FFU, yalionekana yaranda randa katika mitaa ya Mji wa Morogoro huku yakipeperusha bendera za rangi nyekundu kuashiria hali ya hatari.
      Taarifa zilizopatikana mjini hapa zilidai kuwa vikosi hivyo vya askari zaidi ya 200 waliletwa hapa kutoka mikoa ya Dodoma na Dar es Salaam na kuungana na wenzao wa Morogoro.
      Hata hivyo, hali hiyo haikuwaogofya wafuasi na wapenzi wa Chadema, kwani walionekana wakiendelea na maandalizi ya kujikusanya huku wengi wao wakiwa wamevaa sare na kubeba bendera za chama hicho.

      Wafuasi hao walionekana wakiwa katika makundi kwa makundi wakielekea kwenye ofisi za wilaya za Chadema zilizoko Mtaa wa Kingo.
      Hali hiyo iliwafanya baadhi ya polisi waliokuwa katika mitaa mbalimbali kuanza kuwakamata baadhi yao hususan pale walipoonekana kuwa katika makundi makubwa.
      Kitendo hicho kiliibua jazba na kuwafanya baadhi ya wafuasi kutoa maneno makali ya kulilaani jeshi hilo.
      Hali hiyo ilionekana kuwatia zaidi hamasa wafuasi hao ambao waliendelea kujikusanya kwa kwenye ofisi za chama huku wakihimiza kuwa waandamane na ikiwezekana wakabiliane na yeyote atakayewazuia.
      Kutokana na sakata hilo, polisi liliomba kukutana na viongozi wa Chadema wa mkoa na taifa ili kujadiliana nao.
      Akizungumza na wafuasi na wanachama walifulika katika ofisi hizo baada ya majadiliano na polisi, Mkuu wa Operesheni za Chadema, Singo Benson Kigaila alisema kuwa, Jeshi la Polisi limewaomba kukubali kubadilisha ratiba na kupanga nyingine kadri chama hicho kitakavyopendekeza.
      Aliongeza makubaliano yatakwenda sambamba kuwachia huru bila masharti wafuasi zaidi ya 10 walikuwa wamekamatwa pamoja na magari ya chama hicho.
      Alisema Jeshi la polisi limeomba maandamano na mkutano huo uliopangwa kufanyika jana usitishwe kupisha shughuli za maonyesho ya wakulima ya Nane Nane, Kanda ya Mashariki yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, mkoani hapa.

      Alisema kuwa, kufuatia makubaliano hao waruhusiwa kufanya uzinduzi M4C kuanzia Jimbo la Mikumi, wilayani Kilosa Agosti 8 mwaka huu na kuendelea katika majimbo mengine tisa yaliyosalia.
      Hata hivyo, Chadema imepanga kufanya mkutano mkubwa katika Jimbo la Morogoro mjini ambao utawahusisha viongozi wa kitaifa na wabunge Agosti 18, mwaka huu.
      Kwa mujibu wa Chadema, maandamano hayo yatapambwa na watembea kwa miguu waliobeba mabango yenye ujumbe mbalimbali.

      Yalielezewa kuwa yatasindikizwa na misafara ya baiskeli, pikipiki, magari na helikopta ya chama hicho.

      Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Faustin Shilogile alithibitisha kufikiwa kwa makubaliano hayo na kwamba, jeshi hilo litandelea kuimarisha ulinzi popote mikutano hiyo itakapofanyika.


    8. RukaaJuu Final

    9. #126
      Emma.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 865
      Rep Power : 521
      Likes Received
      111
      Likes Given
      0

      Default Re: Mwananchi; chadema yakwama kufanya mkutano

      Asante kwa kutujulisha M4C DAIMA ITASONGA MBELE

    10. #127
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,484
      Rep Power : 19785
      Likes Received
      4302
      Likes Given
      1248

      Default Re: Mwananchi; chadema yakwama kufanya mkutano

      Asante kwa taaarifa

    11. #128
      sir.JAPHET's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Posts : 608
      Rep Power : 474
      Likes Received
      90
      Likes Given
      43

      Default Re: Mwananchi; chadema yakwama kufanya mkutano

      Tuesday, 24 July 2012 21:03

      Aidan Mhando
      CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimepokea wanachama wapya 256 kutoka vyama vya CCM, Cuf, na TLP kutoka katika Kata nne za Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro. Hayo yalibainishwa na Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Kilombero , Moses Kisenime katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari.

      Kisenime alisema wanachama hao walipokelewa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Taifa (Bavicha), John Heche wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara jimboni humo.

      Alisema Mwenyekiti huyo wa Bavicha taifa aliwapokea wanachama hao katika mikutano minne aliyofanya katika Kata ya Ifakara, Mang’ula, Msolwa na Mkamba.

      “Kutokana na mikutano yetu tunayoifanya mkoani Morogoro tumeweza kupokea wanachama 214 kutoka CCM, Cuf 28 na TLP wanachama 14,” alisema Kisenime.

      Akizungumza kwa niaba ya wenzake aliyekuwa balozi wa nyumba kumi katika Kata ya Mkamba, Mussa Katanduki alisema ameamua kuhama kutoka chama cha CCM kwa madai kuwa chama hicho kimekosa mueleko na maadili ya uongozi.

      “Sijalazimishwa na mtu kuhamia Chadema lakini kutokana na mambo yalivyo ndani ya CCM kwa ihari yangu nimeamua kuungana na chama hiki ili kuweza kuendeleza mapambano ya kutetea haki za wanyonge,” alisema Katanduki.

    12. #129
      MtamaMchungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Posts : 1,540
      Rep Power : 807
      Likes Received
      710
      Likes Given
      64

      Default Re: Mwananchi; chadema yakwama kufanya mkutano

      Wana askari wa kupiga watu virungu, lakini kulinda watu hawana.

    13. #130
      chuwaalbert's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th September 2010
      Posts : 295
      Rep Power : 499
      Likes Received
      52
      Likes Given
      129

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Dhaifu at work!

    14. #131
      Mkekuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 700
      Rep Power : 499
      Likes Received
      84
      Likes Given
      0

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Kanda ya kati m4c lini?ratiba ilionyesha ni leo,ila sioni dalili yeyote.msiwatenge wana makao jamani.

    15. #132
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,127
      Rep Power : 14289
      Likes Received
      4015
      Likes Given
      3273

      Default Re: Mwananchi; chadema yakwama kufanya mkutano

      hawa polisi hawajui kama kuanzia mwaka 2015 mwishoni watakuwa wanatupigia salute Chadema
      Quote By MtamaMchungu
      Wana askari wa kupiga watu virungu, lakini kulinda watu hawana.
      Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X Nasubiri 'breaking news... '





    16. #133
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,632
      Rep Power : 1110
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      756

      Default Re: Polisi yazuia Operation Sangara ya CHADEMA Morogoro kisa hakuna Askari

      Quote By Kaka mwisho
      ndugu yangu hapa ni sehemu ya kutoa habari na kupata taarifa. Kwahyo acha umbumbu wako.
      Wewe sio mbumbumbu tu ila ni imbecile huwa sipendi matusi and I never argue with stupid, silly people like you tafuta size yako uwatukane, kite wewe!!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    Page 7 of 7 FirstFirst ... 567

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...