Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tamko la Chama Cha Walimu(CWT)

    Report Post
    Page 8 of 8 FirstFirst ... 678
    Results 141 to 149 of 149
    1. #1
      Olesambai's Avatar
      Member Array
      Join Date : 31st July 2012
      Posts : 15
      Rep Power : 346
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Tamko la Chama Cha Walimu(CWT)

      Kufuatia hukumu iliyotolewa hapo jana na mahakama ya kazi ya kuwataka walimu kurejea kazini na kuwaamuru viongozi wa CWT kutangazia Umma kuwa mgomo umekwisha, Chama kimesema kitatoa tamko leo saa 4:00 asubuhi. Tamko hilo litaeleza kama chama kimeridhika na hukumu au wanakata rufaa. Taarifa hiyo haijaweka wazi kama walimu warejee kazini ama laa. Mtoa taarifa amewataka walimu kufuatilia vyombo vya habari saa 4 asubuhi. Nawaomba wadau mtakaopa updates mtuwekee humu. Karibuni.

      =============
      UPDATE
      =============
      Quote By tamuchungu


      Rais Chama cha Walimu nchini (CWT) Mwl. Gratian Mukoba akitoa taarifa ya chama hicho
      --
      UONGOZI wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT), umesitisha mgomo uliokuwa unaendelea nchini, hivyo kuwataka walimu kurejea kazini.

      Rais wa chama hicho, Mukoba amesema wameamua kusitisha mgomo, baada ya kuingiwa na hofu ya viongozi wao wa juu kuhofiwa kukamatwa.
      Quote By Losambo
      Chama Cha Walimu Tanzania-CWT-kimetangaza kusitisha rasmi mgomo wa walimu na hivyo kuwataka walimu wote nchini kurejea kazini mara moja kuanzia leo ili kutekeleza majukumu yao ya kila siku kama kawaida.

      Akitoa tamko la CWT kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku moja baada ya Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi kukiagiza Chama hicho kitoe maelekezo kwa wanachama wake kurudi kazini, Rais wa Chama hicho GRATIAN MUKOBA amesema walimu wanarudi kazini wakiwa wamekata tamaa kutokana na hukumu hiyo.

      Amefafanua kuwa walimu wanaporudi kazini bila kuwa na mawazo yaliyotulia, utendaji wao utaathirika hivyo Chama kinatoa wito kwa Serikali kukutana na CWT kwa haraka ili kuendeleza majadiliano ya Madai mapya ya Walimu.

      Kuhusu kulipa fidia ya hasara waliyoipata wanafunzi, Chama hicho kimesema kinasubiri taarifa rasmi ya Serikali kuhusu hasara hiyo kwa kuwa hakina uwezo wa kufahamu hasara waliyoipata wanafunzi.

      Kwa mujibu wa Mwalimu MUKOBA wenye uwezo wa kuwasilisha hasara hiyo ni mlalamikaji katika kesi hiyo ambaye ni Serikali.

      Hapo jana Chama hicho kilipongeza kauli ya Rais JAKAYA KIKWETE yakusema Serikali inajali na kuthamini mchango wa Walimu nchini"

      Mytake:

      Mara kwa mara nimekuwa nikiwaona viongozi wa CWT ni wasaliti na katu hawatawatoa walimu katika lindi la matatizo yao ambayo ni ya msingi mkubwa. Naamini wanaendekeza njaa maana wanayofanya hayaingii akilini kabisa.
      Hebi jionee tamko lao baada ya mahakama kusitisha mgomo halafu utarajie serikali itasikiliza madai yao. Kama wangetaka suluhu kwa amani kusingekuwa na haja ya kugoma huko ni kama kumtishia nyau mkubwa.

      Walimu mna kazi kweli.

      Quote By nngu007
      JUMAMOSI, AGOSTI 04, 2012 05:38

      NA GABRIEL MUSHI


      *CWT yatangaza rasmi kurudi darasani
      *Yakusudia kukata rufaa ngazi za juu
      * Mukoba asisitiza madai yao yako palepale
      *Alia na polisi wanaotisha walimu waliogoma

      HATIMAYE Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kimesalimu amri na kutangaza kusitisha mgomo wa walimu uliodumu kwa siku kadhaa nchi nzima.

      Kutokana na kauli hiyo, CWT imewataka walimu wote kurudi kazini ili kutekeleza agizo la Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, lililotolewa juzi mjini Dar es Salaam.

      Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alisema pamoja na mambo mengine, hukumu hiyo imewakatisha tamaa kwa kiasi kikubwa, hivyo wanajipanga kwa ajili ya kukata rufaa.

      Alisema maagizo yaliyotolewa na mahakama yatekelezwa na CWT, baada ya kuipitia kwa umakini hukumu hiyo.

      “Leo (jana), nimewaita kwa ajili ya kutekeleza sehemu ya maagizo ya Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, yaliyotolewa na Jaji Sophia Wambura kwenye Shauri Na. 96 ya mwaka 2012. Katika hukumu hii, mahakama imeagiza chama kitoe maelekezo kwa wanachama wake kurudi kazini kuanzia leo (jana) Agosti 3, mwaka huu.

      “Kwa maelekezo hayo, chama kinawaagiza wanachama wake kurudi kazini kuanzia leo (jana) kutekeleza majukumu yao ya kila siku, maagizo mengine ya mahakama yatatolewa maelekezo, baada ya kupitia hukumu kwa makini na kupata ushauri wa wakili wetu na wanachama watajulishwa,” alisema.

      Alisema kuhusu kulipa fidia ya hasara waliyoipata wanafunzi, chama kinasubiri taarifa rasmi ya Serikali, kwa kuwa CWT haina uwezo wa kufahamu hasara waliyopata wanafunzi.

      Alisema mwenye uwezo wa kuwasilisha hasara hiyo, ni mlalamikaji katika kesi hiyo, ambaye ni Serikali.

      “Kwa kuwa hukumu hii, imewakatisha tamaa walimu wanarudi kazini, huku mwajiri wao akionyesha kutowajali kutokana na madai yao kutopewa kipaumbele katika kuboresha maslahi yao.

      “Walimu wanamwangalia mwajiri wao ambaye ni Serikali amewapuuza akifahamu kuwa kwa vyovyote vile atakimbilia mahakamani…hii haijafuta cheti cha kutopatikana kwa suluhu ya mgogoro wa Julai 25, mwaka huu, haiondoi ukweli kwamba maslahi ya walimu ni duni.

      “Pamoja na walimu kuendelea kupuuzwa na mwajiri wao kwa kuwapa maslahi duni, chama kitaendelea na majadiliano na Serikali kuhusu nyongeza ya mishahara na posho kama kilivyowasilisha. Chama kina imani hukumu hii imetoa somo kwa mwajiri ili atambue umuhimu wa kuzungumza na walimu wote nchini,” alisema.




      KUKATA RUFAA
      Kuhusu kukata rufaa, alisema chama hicho kinawasiliana na wakili wake ili kuona uwezekano wa kukata rufaa.

      “Baadhi ya vipengle vya hukumu, vinahitaji ufafanuzi wa Mahakama ya Rufaa ili kuondoa utata wa kisheria, wanachama wanaombwa kuwa wavumilivu wakati huu.

      “Kwa sababu mahakama, imetuonea kwa kipengele wanachodai tulitoa muda kwa Serikali kabla ya kuitisha mgomo katika siku za mapumziko, wakati wao wenyewe walishawahi kutoa saa 3:48 usiku,” alisema.



      WATAKA KULINDWA
      Kuhusu usalama wao, Mukoba alisema katika kipindi cha mgomo baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya, waliamuru wanachama wa CWT na viongozi wake kukamatwa bila na sababu za msingi.

      “Baadhi yao, wamefikishwa mahakamani kwa kuhamasisha mgomo wa walimu, chama kina wasiwasi kuhusu usalama wa viongozi na wanachama walioshiriki na kuhamasisha mgomo wa walimu.

      “Chama kinatoa rai, kwa Serikali na vyombo vya dola, wakiwamo maofisa usalama na makamanda wa polisi wa mikoa na wilaya, kuhakikisha viongozi wa chama na wanachama waliohamasisha mgomo wanakuwa salama bila kudhurika.



      MAZUNGUMZO NA SERIKALI
      Alisema walimu wanarudi kazini bila kuwa na mawazo yaliyotulia, juu ya utendaji wao wa kazi.

      “Chama kinatoa wito kwa Serikali, kukutana na CWT haraka kuendeleza majadiliano ya madai ya walimu, msimamo wetu tangu mwanzo ulikuwa ni kujadiliana na Serikali kupitia kwa msuluhishi, aliyeteuliwa na Tume ya usuluhishi na uamuzi.

      “Tatizo lilikuwa ni serikali ambayo haikuwa tayari kuzungumza na CWT, ushahidi umeonekana kuwa muda wa siku 50 za mgogoro huu, hakuna mwakilishi wa Serikali aliona umuhimu wa kukutana na viongozi wa CWT kuzungumza nao, badala yake waliamua kutumia vyombo vya habari kukishambulia chama.

      “Chama kinashauri Serikali ichukue hatua za haraka kutibu majeraha ya walimu kwa kujadiliana na CWT kuhusu madai yao na kufuta barua zote zilizosambazwa kwa walimu kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua za kinidhamu,” alisema.

      Julai 30, mwaka huu, CWT kiliitisha mgomo wa walimu nchi nzima ili kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao ambayo ni nyongeza ya mshahara kwa asilimia 100, posho ya walimu wanaofundisha masomo ya sayansi asilimia 55, walimu wa sanaa 50 na mazingira magumu 30. Lakini Rais Jakaya Kikwete akihutubia taifa katika utaratibu wake aliojipangia, alisema Serikali haina uwezo wa kulipa madai ya walimu kutokana na bajeti ndogo iliyopo
      .

    2. Miaka 50

    3. #141
      Dr. Wansegamila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Location : Kwetu pazuri
      Posts : 345
      Rep Power : 2082
      Likes Received
      143
      Likes Given
      88

      Default Re: Rais wa CWT anapaswa kujihuzuru kwa mgomo batili alioutangaza

      Quote By OSOKONI
      Walimu wanatakiwa ajira zao zipitiwe upya, kuna mtu aliwahi kushauri wanafunzi wakifanya mtihani walimu nao wafanye mtihani huohuo pia!!"kwa ishu seriou kama hii" hilo neno sikulielewa
      Naunga mkono hoja mkuu........
      'HAKIMU AKIWA FISI, HUKUMU YA MBUZI NI KIFO'

    4. #142
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,639
      Rep Power : 1111
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      758

      Default Re: Rais wa CWT anapaswa kujihuzuru kwa mgomo batili alioutangaza

      Quote By naggy
      Kwa maoni yangu, rais wa chama cha waalimu ndg. Gratias Mkoba na kaimu katibu mkuu mwl. Oluoch wanapaswa kujihuzuru kwa kuandaa mgomo ambao kwa tafsiri yangu ulikuwa ni kiini macho, hawakuwa na dhamira ya dhati ya kuwataka waalimu wagome kwa kuishinikiza serikali kuwapa waalimu madai yao. Nina sababu zifuatazo kwa kusema haya: 1. kama viongozi waandaji wa mgomo, sikutegemea kukiukwa kwa masharti ya mgomo na hivyo kuufanya mgomo ni halari kisheria. Kitendo cha kutoa masaa 48 siku ambazo si za kazi, upigaji kura bila kuwepo afisa wa kazi, na makosa mengine yaliyoufanya mgomo uwe batili binafsi siamini kama hawakujuwa sheria ila walifanya makusudi kwa sababu zao binafsi. Naamini kabisa wanasheria wapo, wangeweza kuwatumia kwa ishu seriou kama hii kama wao ni wajinga wa sheria. Wametuzalilisha waalimu kwa kutafsiriwa kuwa mambo yetu ni ya ovyo ovyo. 2. kuwadanganya na kuwaaminisha waalim, ambao ni wanachama wao kuwa mgomo ni halari, umefuata misingi na taratibu zote za kisheri, na kwamba wasiwe na wasi wasi, kila wakati walipohojiwa katika vyombo vya habari unaonyesha kuwa viongozi hawa ni waongo na si watendaji. Waalimu watashindwa tena kuitikia matamko yao ya migomo kwa kuwa hawatakuwa na uhakika na maneno yao. wakiendelea kutuongoza kamwe mgomo wowote utakaotangazwa hautafanikiwa. 3. Uongozi wa juu wa CWT chini ya mr. Mkoba haukufanya maandalizi ya mgomo ipasavyo kwa kuwashirikisha wanachama wake wote ambao ndio wagomaji. Hakuna elimu ya uamusho iliyotolewa kwa wanachama na ndiyo maana mwitikio wa mgomo haujaweza kutikisa sana. Najuwa wadau wa elimu, hasa waalimu wenzangu mnasababu nyingine nyingi za kumfanya huyu mtu ajihuzuru. Naomba tuziweke zitusaidie kumtoa huu jamaa, hana lolote juu ya maslahi ya waalimu.
      Nilikuwa najiuliza inakuwaje watoto wetu wanamaliza shule hawajui kuandika na kusoma, kumbe jibu ndio hili! Mwalimu unakosa umakini mdogo tu wa kuandika kitu rahisi kama hiki je likija swala la taaluma la kutumia akili na weledi inakuwaje??kama kweli wewe ni mwalimu rudi darasani haraka kajifunze tena kuandika na kiswahili kwa ujumla! pole sana kumbe ndio maana hata migomo haifanikiwi kutokana na kuwa na walimu wa aina hii!!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    5. #143
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,639
      Rep Power : 1111
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      758

      Default Re: Rais wa CWT anapaswa kujihuzuru kwa mgomo batili alioutangaza

      Quote By ZeMarcopolo
      Usimraumu uyu. Inabidi kwanza umuhone mwalim wake! yeye piya ni matokeho ya mwalim.
      Wewe ni mwalimu au pia ni matokeo ya walimu hawa??
      Mtego likes this.
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    6. #144
      ZeMarcopolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2008
      Posts : 7,205
      Rep Power : 5041
      Likes Received
      2438
      Likes Given
      2229

      Default Re: Rais wa CWT anapaswa kujihuzuru kwa mgomo batili alioutangaza

      Quote By OSOKONI
      Wewe ni mwalimu au pia ni matokeo ya walimu hawa??
      Mkuu, that was meant to be a joke!
      "To greed, all nature is insufficient"

    7. #145
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,639
      Rep Power : 1111
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      758

      Default Re: Rais wa CWT anapaswa kujihuzuru kwa mgomo batili alioutangaza

      Quote By ZeMarcopolo
      Mkuu, that was meant to be a joke!
      Thanks very much for clarification maana nilishaanza kupiga mahesabu niuze ng'ombe wangu niwahamishie watoto wangu wakasome hata somalia kuna nafuu!!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!


    8. #146
      ZeMarcopolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th May 2008
      Posts : 7,205
      Rep Power : 5041
      Likes Received
      2438
      Likes Given
      2229

      Default Re: Rais wa CWT anapaswa kujihuzuru kwa mgomo batili alioutangaza

      Quote By OSOKONI
      Thanks very much for clarification maana nilishaanza kupiga mahesabu niuze ng'ombe wangu niwahamishie watoto wangu wakasome hata somalia kuna nafuu!!
      Hahahahahahahahahahahah mkuu umenichekesha sana! Idea siyo mbaya aisee, kama vipi wapeleke madogo wakapige shule ughaibuni...
      "To greed, all nature is insufficient"

    9. #147
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,639
      Rep Power : 1111
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      758

      Default Re: Tamko la Chama Cha Walimu(CWT)

      walimu ni disgrace na disappointment kwa kada ya academicians wa Tanzania! hawajui wanachokifanya!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    10. #148
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,283
      Rep Power : 3571
      Likes Received
      3079
      Likes Given
      465

      Default Walimu wasalimu amri; CWT yatangaza rasmi kurudi darasani

      JUMAMOSI, AGOSTI 04, 2012 05:38

      NA GABRIEL MUSHI


      *CWT yatangaza rasmi kurudi darasani
      *Yakusudia kukata rufaa ngazi za juu
      * Mukoba asisitiza madai yao yako palepale
      *Alia na polisi wanaotisha walimu waliogoma

      HATIMAYE Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kimesalimu amri na kutangaza kusitisha mgomo wa walimu uliodumu kwa siku kadhaa nchi nzima.

      Kutokana na kauli hiyo, CWT imewataka walimu wote kurudi kazini ili kutekeleza agizo la Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, lililotolewa juzi mjini Dar es Salaam.

      Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alisema pamoja na mambo mengine, hukumu hiyo imewakatisha tamaa kwa kiasi kikubwa, hivyo wanajipanga kwa ajili ya kukata rufaa.

      Alisema maagizo yaliyotolewa na mahakama yatekelezwa na CWT, baada ya kuipitia kwa umakini hukumu hiyo.

      “Leo (jana), nimewaita kwa ajili ya kutekeleza sehemu ya maagizo ya Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, yaliyotolewa na Jaji Sophia Wambura kwenye Shauri Na. 96 ya mwaka 2012. Katika hukumu hii, mahakama imeagiza chama kitoe maelekezo kwa wanachama wake kurudi kazini kuanzia leo (jana) Agosti 3, mwaka huu.

      “Kwa maelekezo hayo, chama kinawaagiza wanachama wake kurudi kazini kuanzia leo (jana) kutekeleza majukumu yao ya kila siku, maagizo mengine ya mahakama yatatolewa maelekezo, baada ya kupitia hukumu kwa makini na kupata ushauri wa wakili wetu na wanachama watajulishwa,” alisema.

      Alisema kuhusu kulipa fidia ya hasara waliyoipata wanafunzi, chama kinasubiri taarifa rasmi ya Serikali, kwa kuwa CWT haina uwezo wa kufahamu hasara waliyopata wanafunzi.

      Alisema mwenye uwezo wa kuwasilisha hasara hiyo, ni mlalamikaji katika kesi hiyo, ambaye ni Serikali.

      “Kwa kuwa hukumu hii, imewakatisha tamaa walimu wanarudi kazini, huku mwajiri wao akionyesha kutowajali kutokana na madai yao kutopewa kipaumbele katika kuboresha maslahi yao.

      “Walimu wanamwangalia mwajiri wao ambaye ni Serikali amewapuuza akifahamu kuwa kwa vyovyote vile atakimbilia mahakamani…hii haijafuta cheti cha kutopatikana kwa suluhu ya mgogoro wa Julai 25, mwaka huu, haiondoi ukweli kwamba maslahi ya walimu ni duni.

      “Pamoja na walimu kuendelea kupuuzwa na mwajiri wao kwa kuwapa maslahi duni, chama kitaendelea na majadiliano na Serikali kuhusu nyongeza ya mishahara na posho kama kilivyowasilisha. Chama kina imani hukumu hii imetoa somo kwa mwajiri ili atambue umuhimu wa kuzungumza na walimu wote nchini,” alisema.




      KUKATA RUFAA
      Kuhusu kukata rufaa, alisema chama hicho kinawasiliana na wakili wake ili kuona uwezekano wa kukata rufaa.

      “Baadhi ya vipengle vya hukumu, vinahitaji ufafanuzi wa Mahakama ya Rufaa ili kuondoa utata wa kisheria, wanachama wanaombwa kuwa wavumilivu wakati huu.

      “Kwa sababu mahakama, imetuonea kwa kipengele wanachodai tulitoa muda kwa Serikali kabla ya kuitisha mgomo katika siku za mapumziko, wakati wao wenyewe walishawahi kutoa saa 3:48 usiku,” alisema.



      WATAKA KULINDWA
      Kuhusu usalama wao, Mukoba alisema katika kipindi cha mgomo baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya, waliamuru wanachama wa CWT na viongozi wake kukamatwa bila na sababu za msingi.

      “Baadhi yao, wamefikishwa mahakamani kwa kuhamasisha mgomo wa walimu, chama kina wasiwasi kuhusu usalama wa viongozi na wanachama walioshiriki na kuhamasisha mgomo wa walimu.

      “Chama kinatoa rai, kwa Serikali na vyombo vya dola, wakiwamo maofisa usalama na makamanda wa polisi wa mikoa na wilaya, kuhakikisha viongozi wa chama na wanachama waliohamasisha mgomo wanakuwa salama bila kudhurika.



      MAZUNGUMZO NA SERIKALI
      Alisema walimu wanarudi kazini bila kuwa na mawazo yaliyotulia, juu ya utendaji wao wa kazi.

      “Chama kinatoa wito kwa Serikali, kukutana na CWT haraka kuendeleza majadiliano ya madai ya walimu, msimamo wetu tangu mwanzo ulikuwa ni kujadiliana na Serikali kupitia kwa msuluhishi, aliyeteuliwa na Tume ya usuluhishi na uamuzi.

      “Tatizo lilikuwa ni serikali ambayo haikuwa tayari kuzungumza na CWT, ushahidi umeonekana kuwa muda wa siku 50 za mgogoro huu, hakuna mwakilishi wa Serikali aliona umuhimu wa kukutana na viongozi wa CWT kuzungumza nao, badala yake waliamua kutumia vyombo vya habari kukishambulia chama.

      “Chama kinashauri Serikali ichukue hatua za haraka kutibu majeraha ya walimu kwa kujadiliana na CWT kuhusu madai yao na kufuta barua zote zilizosambazwa kwa walimu kujieleza kwa nini wasichukuliwe hatua za kinidhamu,” alisema.

      Julai 30, mwaka huu, CWT kiliitisha mgomo wa walimu nchi nzima ili kuishinikiza Serikali kutekeleza madai yao ambayo ni nyongeza ya mshahara kwa asilimia 100, posho ya walimu wanaofundisha masomo ya sayansi asilimia 55, walimu wa sanaa 50 na mazingira magumu 30. Lakini Rais Jakaya Kikwete akihutubia taifa katika utaratibu wake aliojipangia, alisema Serikali haina uwezo wa kulipa madai ya walimu kutokana na bajeti ndogo iliyopo
      .

    11. #149
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,283
      Rep Power : 3571
      Likes Received
      3079
      Likes Given
      465

      Default Re: Walimu wasalimu amri; CWT yatangaza rasmi kurudi darasani


      Waalimu Wangejaribu Style Nyingine... Wangefikiria kwanza kuna shule NYINGI PRIVATE; WATOTO WA WAKUBWA WOTE

      Wanasome NJE YA NCHI; SIO KAMA ZAMANI ENZI ZETU... Kwahiyo Matakwa yao yawe Madogo sio Nyumba ya Ghorofa...

      Hata Kama Mama Kikwete alikuwa Mwalimu ni enzi hizo sasa hivi ana dunda ile shule ya UTURUKI; hatoki Jasho tena

      Waalimu Mfukuzeni Kiongozi wenu wa Chama Cha Waalimu hafai...

    Page 8 of 8 FirstFirst ... 678

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...