Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 32
    1. #1
      MAGAMBA MATATU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 392
      Rep Power : 490
      Likes Received
      204
      Likes Given
      1

      Default Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Shija Felician, Kahama | Mwananchi | Agosti 03, 2012

      WAKATI sakata la kupinga sheria mpya ya mafao ya watumishi wanaoacha kazi katika sekta mbalimbali likizidi kushika kasi, Kampuni ya African Barrick Gold Mines juzi iliufunga mgodi wake wa Bulyanhulu baada ya wafanyakazi wake kugoma wakipinga sheria hiyo.

      Habari zilizopatikana katika mgodi huo mkubwa hapa nchini kwa uzalishaji wa madini ya dhahabu na shaba, zilieleza kuwa chanzo cha kufungwa mgodi huo ni mgomo wa watumishi wanaofanya kazi ndani ya mashimo.

      Hivi karibuni Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Mifuko ya Pensheni Nchini (SSRA), ilifanya marekebisho ya mafao ya watumishi wanaoacha kazi ama kufukuzwa kulipwa stahiki zao mpaka watakapofikisha umri wa miaka 55au 60 hatua ambayo ilipingwa na watu wengi.

      Ofisa Uhusiano wa Kampuni hiyo Necta Foya, alisema shughuli zote za uzalishaji zimefungwa kwa masaa 48 ingawa zile za utawala zinazofanyika maeneo ya juu ya mgodi zinaendelea kama kawaida na baada ya muda huo watumishi wote waliosimama kazi wataitwa, na kwamba watakaoonekana kukubaliana na masharti wataendelelea na kazi.

      Kabla ya hapo uongozi wa mgodi huo uliwataka watumishi hao kuendelea na kazi wakati suala lao likishughulikiwa baada ya kubaini wengi wao waliandika barua za kuacha kazi wakipinga masharti ya malipo ya ya pensheni .

      Wafanyakazi wanaofanya kazi shimoni ndio wachimbaji wakuu wa madini katika migodi ya aina hiyo wakisaidiwa na mafundi mitambo, na hivyo kugoma kwao kufanya kazi kunaathiri uzalishaji kwa ujumla.

      Hata hivyo baadhi ya watumishi waliokumbwa na hali hiyo jana walikuwa wamezagaaa mjini Kahama wakionyesha wasiwasi wa kurudishwa kazini kutokana na mwajiri wao kuchukizwa na hali ya mgomo huo unaodaiwa kuisababishia hasara kampuni.

      Kwa mujibu wa Foya, leo wanatarajia kuongea na watumishi hao waliokuwa wamegoma baada ya masaa 48 kumalizika ambayo yalitolewa juzi wakati wa kufunga uzalishaji katika mgodi huo.


    2. #2
      segwanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th March 2011
      Posts : 1,452
      Rep Power : 709
      Likes Received
      359
      Likes Given
      0

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Watarudi kazini jk akikoroma

    3. #3
      Nyakageni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,574
      Rep Power : 1610
      Likes Received
      816
      Likes Given
      52

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      gud move! Washenzy hawa

    4. #4
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,974
      Rep Power : 761
      Likes Received
      284
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By segwanga View Post
      Watarudi kazini jk akikoroma
      wasiporudi wataajiriwa wengine kuziba pengo

    5. #5
      mmbangifingi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2011
      Posts : 2,574
      Rep Power : 863
      Likes Received
      455
      Likes Given
      2918

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Yeah na sehemu kubwa yaop c manual labour tu?
      Who Jah bless, No one Curse!


    6. #6
      jamii01's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2010
      Location : STREET
      Posts : 955
      Rep Power : 633
      Likes Received
      304
      Likes Given
      185

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      tanzania ni zaidi uijuavyo..hiyo sheria mbovu sana,na wasomi wetu ndiyo waliopitisha hiyo sheria..

    7. #7
      ITEGAMATWI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th January 2012
      Posts : 1,818
      Rep Power : 810
      Likes Received
      481
      Likes Given
      915

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Ni upepo tu unapita!!Liwalo na liwe !!! Kama unaona sheria hii haifai basi katafute kazi sehemu nyingine kwenye sheria unazozitaka!!! Haya ndiyo yatakuwa majibu ya viongozi wetu!!
      zululima likes this.

    8. #8
      WA-UKENYENGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2011
      Location : Inside a Smart Grid
      Posts : 2,491
      Rep Power : 5057
      Likes Received
      806
      Likes Given
      1903

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Quote By kookolikoo View Post
      wasiporudi wataajiriwa wengine kuziba pengo
      Hao jamaa kuwatrain si haba, itachukua muda tena itawalazimu kuwatafuta ambao nao wanaweza kujikuta wanagoma. Otherwise walete wageni ambao nao ni ghali vibaya sana.
      zululima likes this.
      "The usual conclusion is that you can't put a price on a human life. But you can if you must".

    9. #9
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By kookolikoo View Post
      wasiporudi wataajiriwa wengine kuziba pengo
      mfungo ukiisha wataletwa toka IRAN

    10. #10
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By ITEGAMATWI View Post
      Ni upepo tu unapita!!Liwalo na liwe !!! Kama unaona sheria hii haifai basi katafute kazi sehemu nyingine kwenye sheria unazozitaka!!! Haya ndiyo yatakuwa majibu ya viongozi wetu!!
      generally,,,,uende NCHI NYINGINE,TUNAKUTAKIA KILA LA KHERI UENDAKO
      ITEGAMATWI likes this.

    11. #11
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Kundi la kwanza kulaumiwa hapa ni BUNGE,,,,,,yaan ndo limezidi kujiharibia kwa kuruhusu hii sheria,,,,,,,

    12. #12
      pembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 342
      Rep Power : 506
      Likes Received
      94
      Likes Given
      346

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Mimi binafsi sielewi kwa nini wabunge wetu waliptisha shera hii. Huenda haiwagusi wao lakini kwa wengi wetu hi sheria ni kandamizi kishenzi hata senti zako usizipate unapoacha kazi wanategemea utaishi kwa kudra ya Mola? chako ni chako upewe uangalie ustaarabu mwingine maana mpaka miaka 60 utakuwa umesahau una salio mahali!

    13. #13
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,988
      Rep Power : 2594
      Likes Received
      641
      Likes Given
      777

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Mambo si kesho, mbona hawa wameanza mapema?
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    14. #14
      Mzito Kabwela's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th November 2009
      Location : MPUMBULI
      Posts : 7,524
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1133
      Likes Given
      8

      Default re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      JK chaguo la Mungu

    15. #15
      Mayunga6's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th January 2012
      Posts : 95
      Rep Power : 392
      Likes Received
      15
      Likes Given
      11

      Default

      Quote By segwanga View Post
      Watarudi kazini jk akikoroma
      hakuna ki2 km hcho.
      yani pimbi amkoromee panya kula viazi?impossible.

    16. #16
      Zimamoto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 347
      Rep Power : 434
      Likes Received
      89
      Likes Given
      33

      Default Re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Amini usiamini, ipitishwe isipitishwe; sheria haitatekelezeka.

    17. #17
      waya's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 31st July 2012
      Posts : 6
      Rep Power : 348
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Hivi wakati hii sheria inapitishwa wabunge walikuwa wapi na je hawakuiona hasara zake?maana nilisikia kuwa wao wakimaliza muda wao wanapata mafao yao.je wale wabunge wanaokuwa mbele kutetea maslahi ya wanyonge walikuwa wapi?
      FirstLady1 and nkikiki like this.

    18. #18
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 15,052
      Rep Power : 3723
      Likes Received
      3621
      Likes Given
      5885

      Default Re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Quote By segwanga View Post
      Watarudi kazini jk akikoroma
      kumbuka mwajiri atapata hasara sana kwani hata wakirudi production haifanyiki kunakuwa na mgomo baridi..ni mwajiri gani atapenda kuendesha kampuni kwa hasara?
      Acha tu huyu Mama SSRA aendelee kuchezea vichwa vyetu
      Mohamedi Mtoi likes this.
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..
      Hadi tufike 2015 tutakuwa tumekoma

    19. #19
      Wachovu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 245
      Rep Power : 1121
      Likes Received
      55
      Likes Given
      0

      Default Re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Quote By FirstLady1 View Post
      kumbuka mwajiri atapata hasara sana kwani hata wakirudi production haifanyiki kunakuwa na mgomo baridi..ni mwajiri gani atapenda kuendesha kampuni kwa hasara?
      Acha tu huyu Mama SSRA aendelee kuchezea vichwa vyetu
      Wasubiri JK awatume vijana wake wawapeleke Mwabepande

    20. #20
      Kakubilo Kasota's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th March 2012
      Posts : 166
      Rep Power : 400
      Likes Received
      53
      Likes Given
      21

      Default Re: Mgodi wa Barrick (Bulyanhulu) wafungwa; kisa NSSF na PPF, wafanyakazi wako tayari kupoteza kazi!

      Huku ndio sekta binafsi bwana, kwa taarifa yenu, huyo mama Irene ameisha toa tamko tayari na kusema watu wa migodini hii sheria haiwahusu so wataendelea na utaratibu wa zamani kama kawa, for your infor, hawa watu wa migodini wameisha badiri sheria za mafao mara nyingi tu,

      Wao wakiacha kazi wala hawalazimiki kusubiri hiyo miezi 6 yenu, yaani yeye akimalizana tu na mwajiri hata kabla hajafika nyumbani kwake anawahi NSSF/PPF na fomu zake, baada ya week 1-4 pesa yake inakuwa imeisha toka, huwezi kuwapeleka mahakamani because sio waajiriwa wa serikali, kwani hamkusikia lile tamka la meneja rasilimali watu wa mgodi wa Geita?

      Aliwaambia hawa watu wa SSRA kuwa mtalazimika kulipa fidia ya mgomo uliotokea hapa, hasara yote mwatakiwa kuibeba na jamaa aliishia kuomba msamaha tu, hawa sio madaktari wala walimu!
      Mohamedi Mtoi and mjasiria like this.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...