Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Zitto ni maporomoko ya mto Nile - hayazuiliki kwa kifusi!

    Report Post
    Page 9 of 9 FirstFirst ... 789
    Results 161 to 162 of 162
    1. #1
      TUNTEMEKE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th June 2009
      Location : Mombasa
      Posts : 4,504
      Rep Power : 11337
      Likes Received
      323
      Likes Given
      236

      Default Zitto ni maporomoko ya mto Nile - hayazuiliki kwa kifusi!

      Nimeshawishika kuandika uzi huu kumfananisha ndugu yangu kabwe zuberi zitto na maporomoko ya nile ambayo maji yake husafiri kwa nguvu ya ajabu sana.
      katika vipindi tofauti tofauti na kwa sababu tofauti tofauti, zitto amekuwa akishambuliwa na maadui zake hasa kutokana na misimamo yake, kwa kipindi kirefu watu wengi walishawishika kuamini kuwa uzalendo wa zitto umetoweka.

      kadri siku zinavyoenda na kadri mtiririko wa matukio unavyoonyesha ni dhahiri nyota ya kijana huyu haiwezekani kuzimwa kwa majungu kama ilivyotakiwa iwe. mtiririko wamatukio unamfanya zitto aonekane kuwa ni shujaa na mzalendo wa kweli katika taifa hili.

      pamoja na kuwa anasimama kidete bungeni kuwatetea masikini na walala hoi wenzetu lakini amekuwa akiyafanya mengi zaidi na zaidi. leo nitataja machache tu.

      1. ni zitto ndiye aliyekuwa mbunge wa kwanza Tanzania tangu mwaka 2000 kupeleka hoja binafsi bungeni ambapo alipeleka hoja ya BUZWAGI ILIYOMLETEA MISUKISUKO

      2. ni zitto ndiye mbunge wa kwanza tanzania tangu kuanzishwa kwa dunia kusimamishwa kushiriki bunge kwa madai ya kusema uwongo bungeni kisa kufichua siri ya waziri wa nishati na madini kwenda kusaini mkataba nje ya nchi kipindi ambacho rais ametangazab marekebisho ya sheria za madini.

      3. ni zitto huyu huyu aliyelishauri taifa kuinunua mitambo ya dowans ili kunusuru nchi isiingie kwenye mgao wa umeme, wakati huo mitambo hiyo ilikuwa ikiuzwa kwa dola elf 40 tu. lakini kwa unafiki wa wanasiasa wetu na wanafiki wachache walishirikiana kuupotosha umma na kusema zitto amehongwa. kitu cha kusikitisha miaka mitatu baadae mitambo ile ile sasa imeuzwa kwa dola mil120 na wanafiki wote wameufyata hakuna tena mzalendo hapo. kwenye hili zitto leo ni shujaa. na mitambo imebadilishwa jina inaitwa symbions na inatuuzia umeme kila kukicha na serikali imeshindwa kesi mahakamani na inatakiwa kuwalipa dowans zaidi ya dola mil50

      4.ni zitto ndiye aliyeongeza ushawishi wa kuwavutia vijana wengi hapa nchini washiriki kikamilifu siasa na kujiona kuwa nao wanaweza na mpaka leo wamepatikana wabunge wengi wa chadema ambao ni vijana. wabunge kama wenje, silinde, highness na sugu ni mfano wa wabunge walioshinda kati ya vijana wengi waliogombea.

      5. ni zitto pekee ndiye kiongozi wa kitaifa wa chadema aliyezunguka sehemu kubwa ya nchi kipindi cha uchaguzi mkuu kwenda kuwanadi wagombea ubunge wa majimbo mbali mbali-ukiondoa slaa aliyekuwa mgombea urais. mbowe yeye alijifungia hai na maeneo machache ya mkoa wa kilimanjaro.

      6. ni zitto ndiye aliyeasisi operesheni ya wabunge kukataa kupokea posho ya kushiriki vikao bungeni ambapo amekutana na vipingamizi vingi na upinzani mkali kutoka kwa wabunge wa upinzani na ccm.

      7. ni zitto pekee ambaye ndio mbunge peke yake asiyepokea posho za vikao hapa tanzania kati ya wabunge wote wanaojidai leo hii ni wazalendo.

      8. ni zitto aliyeasisi na kulisimamia sekeseke la uwajibikaji la kukusanya sahihi 70 za kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na kumlazimu rais avunje baraza la mawaziri.

      9. ni zitto aliyewaunganisha wasanii wa bongo fleva na injili kuvunja mikataba yao na kampuni za simu ili waongezewe malipo kutoka 7% ya sasa wanayolipwa.

      10. ni zitto pekee aliyetangaza hadharani kuwa anataka kuwa rais wa taifa hili na kwamba uwezo wa kufanya hivyo anao, uzalendon wa kufanya hivyo anao na uadilifu wa kufanya hivyo anao. zitto ndio mwanasiasa pekee ambaye hafanyi siri dhamira yake ya kuutaka urais, na wala hasubiri ajitokeze kwa kushtukiza hapo baadae, lakini pia inaonyesha haitaji mfumo wa kizamani wa kubembeleza uombwe ili kugombea urais. kwa hili nina hakika amejiongezea maadui wengi ndani ya chama chake na nje ya chama chake.

      kwa hayo niliyoyataja na yawezekana mengine mengi nimeyasahau. kuna kila sababu ya huyu jamaa kuundiwa mazengwe mbalimbali ili kuondoa credibility yake.

      imefahamika pia wapinzani wake wa ndani ya chama chake wameanzisha kikundi maalumu walichokipa jina na OPERESHENI CHAFUA ZITTO..

      kwa hayo machache nawatakia mjadala mwema wakuu.
      narudia tena:- zitto ni maporomoko ya nile hayazuiliki kwa kifusi.

    2. FemaTV & Radio

    3. #161
      Al Zagawi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Location : Tabora
      Posts : 832
      Rep Power : 685
      Likes Received
      160
      Likes Given
      51

      Default Re: Ukweli na uwazi chadema aliyemsafi anyoshe kidole juu__zitto funga mlango

      Quote By Froida
      Zitto ni Kanika tena matambala kumbe Tumtemeke aka Magindu aka Zitto unafanya biashara ya kitoto hii thread mwanzo ilianzishwa na Magindu umeedit kila neno kwenye chanzo cha uzi huu ili kusuit maneno ya wachangiaji ,kumbe ni kweli ZZK ni kazi yako ya kujiandikia na kujijibu mwenyewe shame shame kwa hiyo umebadilisha title na kuiweka Tuntemeke kwa sababu unaamini wewe ni kijogoo your a deaf stupid
      upuuzi mtupu...hivi unajua hata ulitaka kuandika nini???!!!
      ...........Uwanja wa siasa katika nchi karibu zote za Kiafrika, ni uwanja uliotekwa na majambazi ambao wanafanya wanachotaka, vile wanavyotaka..........Jenerali Ulimwengu, Raia Mwema Namba 278.

    4. #162
      dogojanja 87's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 272
      Rep Power : 414
      Likes Received
      44
      Likes Given
      25

      Default Re: Zitto ni maporomoko ya mto Nile - hayazuiliki kwa kifusi!

      HABIB MCHANGE a.k.a Tuntemeke katika harakati zake za kukibomoa chama imara mara baada ya kuenguliwa kwenye Uchaguzi wa BAVICHA kwa tuhuma za rushwa ya wazi mchana kweupe na ushahidi wa MPESA pesa zilipotokea na aliowatumia,mpaka leo hajakana popote.Ndie huyhuyu alieliuza jimbo la kibaha mjini kwa njaa njaa zake.. huyu anatumika na kulipwa ujira mdogo na watu wenye tamaa kali ya madaraka..

    5. Miaka 50
    Page 9 of 9 FirstFirst ... 789

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...