Re: Harakati za Chadema na mbinu za kuchukuwa dola

By
Ritz
Wanabodi.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, kinafanya harakati na mbinu kuchukuwa dola lakini kuna mapungufu mengi sana ambayo ni kikwazo bahati mbaya Chadema wenyewe hawatambui hivyo vikwazo ndani ya chama chao..
Chadema bado wanategemea wanachama wasiotabirika, wanachama wake ni wale wanaoingia wakati wa mikutano ya hadhara na maandamano, Chadema wamekosa uhalali wa mtawanyo wa wanachama hai katika kila kona ya nchi.
Chadema baada kupata mafaniko katika uchaguzi mkuu uliopita wamejikuta wakihodhi wajibu wa jamii kisiasa kwa niaba ya vyama vingine wakihisi kwamba wao ni bora zaidi mbele ya jamii kuliko vyama vingine vyote nchini..
Chadema mpaka sasa hawajawa na uhakika wa jinsi ya kumpata kiongozi wa juu katika nafasi ya Mwenyekiti au Urais kutoka kanda nyingine, Chadema kimeweza kupata umaarufu kisiasa lakini bado wanakabiliwa na tatizo la umakini, uzoefu na mbinu nina hakika uteuzi wa mgombea urais kutoka Chadema ataleta mtarafuku mkubwa ndani ya chama hicho viongozi wa Chadema kutoka kanda zingine hawataafiki mgombea urais atoke eneo moja tu kila uchaguzi.
Chadema inasumbuliwa na kasumba ya ubinafsi na upendeleo wa kifamilia, Chadema wamejikuta wakipiga teke demokarasia ndani ya chama chao na wabunge wake wa viti maalum wengi wao wanatoka katika koo za waasisi wa chama.
Mkuu Ritz una maoni mazuri na chokonozi juu ya CDM ambayo yatasababisha Mnakasha hasa kuhusu nafasi ya mgombe Urais na Uenyekiti wa CDM. Ila sasa subiri haki kutoka kwa jamaa wa CDM ambao wanadhani kila anayeikosoa CDM basi ni mgomvi wao.
CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.
Follow Us Here