Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyasa!
Kama Tanzania inaamini nusu ya Ziwa Nyasa ni mali yake kwanini wanasubiri kuwabembeleza Wamalawi kuhusu suala la kusitisha utafiti wa mafuta ili kupisha majadiliano? HIvi tumekuwa wasahaulifu hivi kiasi kwamba hatujui suala hili nusura litulete katika vita na Kamuzu Banda?
Tanzania inaamini mpaka wake na Malawi umepita kwenye Ziwa Nyasa. Sasa kama hii ni imani ya Kikwete na Membe na serikali yetu kwa ujumla kwanini wanataka kupoteza muda wa kuwashawishi Wamalawi? Jambo rahisi ni Serikali kuanza utafiti wa mafuta na gesi kwenye "upande wetu" na kutoa kibali kwa makampuni ya kimataifa kufanya hivyo. Wamalawi watafanya nini?
Unless tuna jeshi lisiloweza kulinda mipaka yetu! Kama Wamalawi wameweza kuingia "nusu yetu" ni nini kinatuzuia kuwazuia? Si Idi Amin naye alisema sehemu ya ardhi yetu ni yake akateua hadi Mkuu wa Wilaya?
Lakini nani anafikiri kuna kiongozi anayeweza kusimama vikali hivi? Watu wameng'ang'ania ati JWTZ lilinde mitambo ya umeme ya Tanesco! na mipaka analinda nani?
[email protected] Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By Bukyanagandi
Mkuu yaani suala hili la Ziwa Nyasa ni kama michezo ya Mickey Mouse, buzz word hapa ni discrepancy, discrepancy even more discrepancies!! Waingereza walicho kuwa wanafanya hapa ni kuchezea lugha TU katika azma yao ya kuchanganya watu akili.
Kama kweli report na ramani zilizo tolewa na Serikali ya kikoloni ya Nyasaland kati ya mwaka 1920 - 30 ilionyesha mpaka huko katikati ya ZIWA, alafu cha ajabu Waingereza hao hao kati ya mwaka 1933-34 kwa upande wa Tanganyika walifanya kimaksudi kuonyesha kwenye maaadishi kwamba mpaka huko katikati ya ziwa lakini kwenye ramani wanaonyesha kwamba mpaka huko ufukweni mwa ziwa!! Hii maanake nini, walikuwa na ajenda gani ya SIRI?
Mkuu hivi Nyasaland ilikuwa ni koloni au Protectorate, sasa kama Waingereza walikuwa wanatawala Nyasaland na Tanganyika at the same time kwa nini walikuwa wanazungumzia suala hili with a folked tongue?
Mkuu hebu angalia statements hizi hapa chini zinavyo ji-contradict!
" I n his review of the legal evidence, Brownlie notices earlier discrepancies in the CARTOGRAPHY of the Lake, both before the I 9 I 4- I 8 war, and perhaps more significantly in the description and depiction of the boundary under the Mandate. Thus between 1924and 1932 the British Annual Report on Tanganyika refers, although not always EXPLICITLY, to a CENTRE LINE as the Lake BOUNDARY. In 1933 and 1934a DISCREPANCY appears between THE TEXT, which refers TO A CENTRE LINE, and the MAP which shows the EASTERN SHORE BOUNDARY!!!!.
Then from 1935 until 1938, as in the post-World War II reports to the Trusteeship Council, both TEXT and MAP refer to the eastern shore line. Official reports and maps produced in the Nyasaland Protectorate during the 1920and 1930 also SHOW A MIDDLE LINE!!!!!!!. "
Waingereza bwana! Mtu unaweza kufikili suala zima walilichukulia kama watu wanao andikia URL ya wikipedia ambayo kila mtu yuko free kuongezea, kumodify au kupunguza maadishi.
Iwapo lina mkanganyiko hivi, basi inawezekana kabisa tunaweza gawana pasu kwa pasu, ila nitakuwa na amani kama jamaa zetu (serikali) itakuwa inakusanya reference kama hizi kwa ajili kuweka mambo sawa iwapo ubishi utaanza. Ila Jamaa zetu (serikali)nao hawaaminiki, wanaweza kuchukua hii issue kama deal na wakapewa cha juu na kuacha ziwa linakwenda, maana issue hii ina reference nyingi sana.
Inawezekana kabisa Waingereza walifanya hivyo kwa kuamini kuwa Tanganyika haitakuwa yao (wanayo kwa dhamana ya UN) na Malawi ni yao ya kudumu, ndio maana wakachakachua
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By Nguruvi3
Hapa umechanganya vitu viwili, haki ya nchi na uzembe wa nchi. Haki ya nchi ni pamoja na kulinda eneo lake. Hiyo haihusiani na uzembe wa kutumia rasilimali wa nchi yetu.
Huwezi kwenda kulala kwa jirani yako eti kwasababu baba mwenye nyumba ni mlevi!
Nitofautishie kati ya hapo nilipo-bold;
Mpaka Malawi wameweza kufikia hapo walipo katika issue ya Ziwa Nyasa, Tanzania ilikuwa au inafanya nini kuilinda haki hiyo?
Pili, Tanzania au watanzania tuna haki na rasilmali zetu, kwani zinafaidisha wageni kuliko sisi?
Na kwa mfano wako wa baba mlevi, asipoilinda na kuijali nyumba yake na mipaka ya nyumba yake, jirani akiingia ni tatizo la nani?
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By bdo
Iwapo lina mkanganyiko hivi, basi inawezekana kabisa tunaweza gawana pasu kwa pasu, ila nitakuwa na amani kama jamaa zetu (serikali) itakuwa inakusanya reference kama hizi kwa ajili kuweka mambo sawa iwapo ubishi utaanza. Ila Jamaa zetu (serikali)nao hawaaminiki, wanaweza kuchukua hii issue kama deal na wakapewa cha juu na kuacha ziwa linakwenda, maana issue hii ina reference nyingi sana.
Inawezekana kabisa Waingereza walifanya hivyo kwa kuamini kuwa Tanganyika haitakuwa yao (wanayo kwa dhamana ya UN) na Malawi ni yao ya kudumu, ndio maana wakachakachua
Hapo kwenye nyekundu mkuu - tumefika hapa tulipo kwa sababu hiyo hiyo Waingereza walijuwa fika kwamba Tanganyika wataitawala kwa dhamana ya UN, ndio maana TAIFA letu alikuendelezwa kiviwanda na kilimo tofauti kabisa na Kenya ambayo walijuwa ni KOLONI lao.
Hivyo hata utata huu baina yetu na Malawi kuhusu mpaka unafuata mkondo huo huo ndio maana unaona humu Waingereza walikuwa na tabia ya leo kuzungumzia ili kesho lile wakitumia maneno tofauti kabisa kwa issue hiyo hiyo ya mpaka na actually walikuwa wanaweka mpaka kwenye ramani wakitumia a dotted line (maana yake ni mpaka bado haujafafanuliwa vizuri i.e bado kitendawili) unlike Msumbiji ambayo mipaka yake na Malawi kwenye Ziwa Nyasa unaonyeshwa na solid line maana yake ni unaeleweka vizuri hauna shaka.
Kitakacho kuja kutuokoa ni sheria ya UN ya mwaka 1992 (sina hakika na mwaka) ambayo unasema hivi: Nchi zinazo pakana na MAZIWA basi ni lazima Ziwa ligawanwe katikati kama ni nchi mbili, kama ni nchi nne basi kila moja inufaike na robo ya ziwa, tukiwabana Wamalawi katika kipengere hicho basi tutakuwa saved by the BELL. Wakitutilia mkwara basi yatawakuta yaliyo wahi kutokea mashariki ya kati between Waarabu na Waisrael wakati wa vita vya 1967, Waarabu wakajikuta wanapotesa Jerusaleem, Golan Heights na Sania.
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By mndwadage
mkuu tatizo la Tanzania ni siasa hata kwenye maswala ya utendandaji,hawa wamalawi ilikua ni kuwasogezea vifaa vya kijeshi na wanajeshi kadhaa wawe wanapiga jeramba pembezoni mwa ziwa. sidhani kama Malawi wengethubutu kukanyaga hata fukwe za Tanzania.!!
Huu mgogoro umekuwepo kwa miongo mingi, kwa nini sasa hivi Malawi ndo wameamua kukomaa? Hii ndiyo ishu ya msingi. Ina maana Malawi wamejiandaa hata kwa vita. Je sisi tulijiandaa? Baada ya kuapishwa, Joyce Banda amechukua hatua kadhaa za kuwafurahisha "wazungu" ikiwemo kuridhia ndoa za jinsia moja. Tuna uhakika gani kwamba tutakuwa tunapigana na Malawi na sio Mataifa ya Ulaya-hasa yenye makampuni yanayotafuta mafuta na gesi Z. Nyasa?
Nihitimishe kwa kusema, vita na Malawi haitakuwa rahisi kama wengi wanavyopenda tuamini maana hata umoja tuliokuwa nao wakti wa vita vya Kagera haupo kwa sasa na hakuna jitihada za kuujenga. Pia, nadhani sasa UwT wamepata kazi mahsusi ya kufanya, kaz ambayo miaka yote tumekuwa tukiwategemea waifanye.
"There is a very thin line between inflation and extortion."-Sooth.
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By Bukyanagandi
Hapo kwenye nyekundu mkuu - tumefika hapa tulipo kwa sababu hiyo hiyo Waingereza walijuwa fika kwamba Tanganyika wataitawala kwa dhamana ya UN, ndio maana TAIFA letu alikuendelezwa kiviwanda na kilimo tofauti kabisa na Kenya ambayo walijuwa ni KOLONI lao.
Hivyo hata utata huu baina yetu na Malawi kuhusu mpaka unafuata mkondo huo huo ndio maana unaona humu Waingereza walikuwa na tabia ya leo kuzungumzia ili kesho lile wakitumia maneno tofauti kabisa kwa issue hiyo hiyo ya mpaka na actually walikuwa wanaweka mpaka kwenye ramani wakitumia a dotted line (maana yake ni mpaka bado haujafafanuliwa vizuri i.e bado kitendawili) unlike Msumbiji ambayo mipaka yake na Malawi kwenye Ziwa Nyasa unaonyeshwa na solid line maana yake ni unaeleweka vizuri hauna shaka.
Kitakacho kuja kutuokoa ni sheria ya UN ya mwaka 1992 (sina hakika na mwaka) ambayo unasema hivi: Nchi zinazo pakana na MAZIWA basi ni lazima Ziwa ligawanwe katikati kama ni nchi mbili, kama ni nchi nne basi kila moja inufaike na robo ya ziwa, tukiwabana Wamalawi katika kipengere hicho basi tutakuwa saved by the BELL. Wakitutilia mkwara basi yatawakuta yaliyo wahi kutokea mashariki ya kati between Waarabu na Waisrael wakati wa vita vya 1967, Waarabu wakajikuta wanapotesa Jerusaleem, Golan Heights na Sania.
Mkuu Bukyanagandi, naamini hii issue tumeijadiri vya kutosha na kwa kuwa Membe ameisha itolea majibu nadhani tusubiri tione muafaka utakuwaje, ingawa baada ya tamko la Membe bungeni kuhusu hii issue nilisikia vyombo vya habari hasa vya Malawi kuwa "kwa nini Tanzania walikuwa kimya kuzungumzia habari ya mpaka ila baada ya kuona tumeanza utafiti wa mafuta - ndio wao (Tanzania) wanaleta longolongo, sisi Wamalawi tutaendelea na Mipango yetu".
Nina amini watawala wetu wamesoma comments zetu kwa kuwa najua wapo kwenye JF, hivyo watatenda kwa jinsi watakavyoona inafaa na kwa ubavu tulio nao.
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By Sooth
Huu mgogoro umekuwepo kwa miongo mingi, kwa nini sasa hivi Malawi ndo wameamua kukomaa? Hii ndiyo ishu ya msingi. Ina maana Malawi wamejiandaa hata kwa vita. Je sisi tulijiandaa? Baada ya kuapishwa, Joyce Banda amechukua hatua kadhaa za kuwafurahisha "wazungu" ikiwemo kuridhia ndoa za jinsia moja. Tuna uhakika gani kwamba tutakuwa tunapigana na Malawi na sio Mataifa ya Ulaya-hasa yenye makampuni yanayotafuta mafuta na gesi Z. Nyasa?
Nihitimishe kwa kusema, vita na Malawi haitakuwa rahisi kama wengi wanavyopenda tuamini maana hata umoja tuliokuwa nao wakti wa vita vya Kagera haupo kwa sasa na hakuna jitihada za kuujenga. Pia, nadhani sasa UwT wamepata kazi mahsusi ya kufanya, kaz ambayo miaka yote tumekuwa tukiwategemea waifanye.
Yaani tuombe Mungu vita isiwepo, maana inaaminika kuwa vita ya Kagera iliturudisha nyuma x 10 kimaendeleo, na imajine wakati inawezekana Nyerere alikuwa mwadilifu, sasa kwa hawa Manyang'au/kupe, tunaweza kukuta tunarudi nyuma kimaendeleo x 10,0000 hadi nchi ikauzwa
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
By Mzee Mwanakijiji
Nadhani watu wanazungumzia kupeleka wanajeshi kule kwa urahisi sana. Hupeleki wanajeshi kwenye mpaka wa nchi nyingine bila kuwa tayari kupigana vita. Kuna vitendo ambavyo kisheria vikifanyika vinachukuliwa kuwa ni "act of war". Tanzania haipaswi kupeleka wanajeshi wake karibu na mpaka na Malawi bila kuwa tayari kwenda vitani. Swali, Watanzania mko tayari kwa vita siyo kwenda kujionesha tu. Nani kawaambia ati mkipeleka wanajeshi basi wamalawi watanywea? Na wenyewe si wana jeshi?
Unafikiri kuwa na wingi wa jeshi na silaha ndio kushinda vita? Lakini kubwa zaidi ni kuwa viongozi wetu tayari hawana ile cloud ya kuwa viongozi wa wakati wa vita. Kama kwenye amani wametutawala hivi wakati wa vita itakuwaje? Njia pekee ya kuleta hiyo heshima ni sisi kutangaza tunaanza utafiti wetu wa mafuta kwenye nusu yetu tukiheshimu mipaka yetu na hatutagusa nusu ya Malawi. Malawi watakuwa wametupiwa mpira!
Kama wao wanaamini ziwa zima ni lao basi wao ndio wafanye hatua ya kwanza vita.... hapo ndio JWTZ linapoenda kulinda mpaka wetu!
Nakuunga Mkono Asilimia mia moja. Ikiwezekana na sisi tubadili jina la ziwa liwe ziwa Tanzania, au na sisi serikali itangaze kwamba ziwa lote ni letu (a bit late and ridiculous already).
Kama kweli tunaamini kwamba Malawi ni bwana mdogo kwetu, yeye ndiye anatakiwa kulalamika na aje kuomba majadiliano sio sisi, kuna watu humu ndani jana siku nzima walikuwa wanatokwa mapovu kwamba tutangaze vita. nilikuwa sijaona busara zako Mwanakijiji. respect.
Hivi usalama wa taifa wapo kweli? Kusema kweli security kwenye mipaka imeshuka, wahamiaji haramu kila siku wala hawaogopi tena, pia tuangalie usikute ni propaganda ya ccm ili kutusahaulisha matatizo yetu na kuzuia uchaguzi 2015
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
[QUOTE=Mzee Mwanakijiji. Tanzania haipaswi kupeleka wanajeshi wake karibu na mpaka na Malawi bila kuwa tayari kwenda vitani. Swali, Watanzania mko tayari kwa vita siyo kwenda kujionesha tu. Nani kawaambia ati mkipeleka wanajeshi basi wamalawi watanywea? Na wenyewe si wana jeshi?
Njia pekee ya kuleta hiyo heshima ni sisi kutangaza tunaanza utafiti wetu wa mafuta kwenye nusu yetu tukiheshimu mipaka yetu na hatutagusa nusu ya Malawi. Malawi watakuwa wametupiwa mpira!
Kama wao wanaamini ziwa zima ni lao basi wao ndio wafanye hatua ya kwanza vita.... hapo ndio JWTZ linapoenda kulinda mpaka wetu![/QUOTE]
Wkati tunajiandaa kufanya utafiti ni lazima tuwazuie wao kuendelea na shughuli hiyo. Nakubaliana na wewe kuwa hakuna haja kupeleka majeshi ila kukaa mkao wa kula ni lazima maana kama chakula ndo kinaiva iweje ujiandae na jambo lingine?
vita sio cinema za rambo...............nafikiri hatua za kusuluhisha migogoro inafuatwa, tuwe na subira tunaone mwisho wake
Mkuu Che wa TZ nakubaliana na wewe,vita si mchezo. Tunakumbuka vita ya Amini tuliambiwa tufunge mkanda kwa miezi 18, matokeo yake? Zaidi ya robo karne wa-TZ wameendelea kufunga mikanda. For sure that was a U-Turn as far as our economy was concerned! With economic hardships faced by this country,are we ready for war?
Re: Njia rahisi ya kuleta 'sense' kwa Wamalawi: Tanzania itangaze kuanza utafiti wa mafuta Ziwa Nyas
hivi ni kweli mpaka sasa hatujui msimamo wa malawi?tunapoteza fedha kwenda kuzungumza na mvamizi wa ardhi yetu?hebu tangazeni tenda ya uchimbaji mafuta kwa mchina au mrusi ,tuache siasa.
Follow Us Here