Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ukweli kuhusu mpaka wa Tanzania na Malawi

    Report Post
    Page 2 of 28 FirstFirst 123412 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 546
    1. #1
      Mtoto wa Mkulima's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2007
      Posts : 962
      Rep Power : 812
      Likes Received
      39
      Likes Given
      0

      Default Ni lake Nyasa au Lake Malawi?

      Wakubwa niwekeni sawa, nilikuwa nauliza Ziwa Nyasa ni Ziwa Nyasa au Ziwa Malawi? Na je, Kwanini Ziwa Victoria liendelee kuitwa Ziwa Victoria na si Ziwa Nyanza? Au ndio kuwaenzi watawala wetu wazungu?

      Lake Nyasa or Lake Malawi?
      The name of the lake itself is also disputed. Malawi claims the lake is named 'Lake Malawi' while international maps and other countries (most notably Tanzania) claim the name of the lake to be 'Lake Nyasa'. The origins of the dispute in the name have their background in geopolitical disputes that began prior to Malawi's independence in 1964, when it was previously known as Nyasaland.

      Further complications emerged for different political reasons in the 1960s, when the then President Banda (of Malawi) became the only African leader to establish diplomatic relations with white South Africa. This was fiercely repudiated by other African leaders, including the then President Nyerere (of Tanzania). The contrasting attitudes and policies gave further impetus to disputes between the two governments, on the name of the lake itself, and the boundary between the two countries.

      At present, the dispute between the two governments is largely dormant. Intergovernmental relations between Malawi and Tanzania are largely cordial.


      Tanzania-Malawi dispute
      The partition of the lake area between Malawi and Tanzania is disputed. Tanzania claims international borders through the lake along the lines of the borders between the German and British territories before 1914; Malawi, meanwhile, claims the whole non-Mozambican lake, including the waters next to the Tanzanian shore. The foundations of the dispute were set when the British colonial government, which had recently captured Tanganyika from Germany, put the water under the jurisdiction of Nyasaland without a separate administration for the Tanganyika portion. The dispute has led to conflicts in the past, though for several years Malawi has declined to enforce its claims to the disputed portion.

      Occasional flare-ups in in the 1990s and in recent times have impacted fishing rights, particularly of Tanzanian's who reside on the lake shore, who have occasionally been accused of fishing in Malawian waters.
      Quote By Mwawado
      Habari hiyo hata Mimi nimewahi kuisikia, hata ukiangalia Ramani ya ziwa hilo linaitwa Ziwa Malawi tofauti na hapo zamani tulipoliona kwenye ramani kama ziwa nyasa. Nashindwa kuelewa kwa dhati kama mpaka umegawanywa upya ama ndio yale yale ya kuambiwa kuwa Mlima Kilimanjaro upo Kenya.Inapaswa mipaka ya nchi yetu iwekwe wazi ili kutokuja kupoteza maeneo na Vivutio vyetu vya asili.

      Mpaka wa Tanzania na Malawi una matatizo ya muda mrefu, nakumbuka mwaka 1978 kulikuwa na kurushiana risasi kati ya Majeshi ya Tanzania na Malawi, kwa siku mbili mfululizo kulikuwa na amri ya kutokuwasha Taa katika Mji wa kyela mkoani Mbeya, Kipindi hicho nilikuwa Mbeya, Mkuu wa Mkoa wa mbeya kwa Wakati Huo Mzee Richard Wambura alisema Mwl Nyerere ameamuru majeshi yetu yarudishe mapigo kama itaonekana Banda ataingiza majeshi Kyela. Serikali ya Banda ilikuwa inadai maeneo ya Matema Beach, Mto Songwe mpaka Ipinda yapo ndani ya Ardhi ya Malawi.

      Sasa inawezekana kabisa tumelitoa kwa hiyari ziwa liwe upande wa Malawi nasi tumebakiwa na Bandari tupu ya Itungi,ambayo sasa nafikiri haina hata meli moja baada ya TACOSHILI kufa.
      Quote By Gamba la Nyoka
      Kama serikali imelitoa hilo ziwa kwa Wamalawi pasipo kuhusisha maoni ya Watanzania, basi serikali inalo la kujibu. Huwezi kuwaambia wananchi waliokaa pale miaka nenda rudi eti, hayo maji usiyaguse ni ya wamalawi hayo.

      Hili suala ni lazima serikali ilitolee kauli haliwezi kuwa kimya kimya milele!
      Quote By Ruge Opinion
      Miaka ya 1970 Kamuzu Banda, rais wa Malawi, alitangaza kuwa lile ziwa lote ni la Malawi na akaanza kuwabugudhi Watanganyika waliokutwa kwenye ziwa. Nyerere akasogeza majeshi pale na kumtumia ujumbe Kamuzu aache uchokozi. Kamuzu akanywea.

      Tangu hapo hakujawahi kuwapo maelewano rasmi.

      Hilo ziwa lilikuwa linajulikana kama ziwa Nyasa kutokana na wenyeji pande zote mbili kuwa Wanyasa. Malawi vile vile ilikuwa inajulikana kama Nyasaland. Walipopata uhuru wakabadili jina na kujiita Malawi. Kwa hiyo na jina la ziwa wakalibadilisha bila makubaliano na sisi. Kwa hiyo kwao ni Ziwa Malawi na kwetu ni Ziwa Nyasa.
      Quote By kajembe
      Mgogoro huo ulianza enzi ya Kamuzu Banda alipokuwa raisi. miaka ya sitini Kamuzu alikuwa anazungumza kwenye redio yao, Malawi Broadcasting Corporation kutoka Blantyre, Malawi, na kusema ziwa lote ni la Malawi na pia wilaya ya Rungwe na hadi Mbeya ni sehemu ya Malawi.

      Kuna siku mwezi wa September 1968 Nyerere alimwita Banda ni kichaa. Alikasirika sana kwa sababu ya madai ya Mzee Kamuzu kwamba sehemu za Tanzania ni za Malawi. Alidai hata Mbamba Bay na sehemu zingine mkoani Ruvuma karibu na Ziwa Nyasa kwamba ni za Malawi. Pia alidai jimbo lote, Eastern Province, la Zambia. Kaunda alimjibu Banda na kusema ni shauri yake akitaka kuanzisha vita.

      Kabla ya mgogoro huo, Banda alikuja Tanzania na kukutana na Nyerere mwaka 1962 na kumwambia hakuna nchi ya Mozambique. Alimwambia Nyerere wagawane nchi hiyo. Alimwambia Nyerere sehemu ya kaskazini ya Mozambique, sehemu ya Wamakonde jimbo la Cobo Delgado, "ni lako" Nyerere. Ni sehemu ya Tanzania. Sehemu za Mozambique zilizobaki ni za Malawi, Rhodesia na Swaziland. Nyerere alimpuuza tu.

      Baada ya miaka michache, 1968, Kamuzu akatangaza na kusema sehemu zetu za Tanzania nilizozitaja hapo juu ni sehemu za Malawi.

      Mzee Kamuzu alikuwa ni mkorofi sana.

      CHANZO CHA MGOGORO

      Mgogoro wa ziwa umetokana na uamuzi wa wakoloni wa Kiingereza kuliweka ziwa hilo chini ya utawala wao wa Nyasaland wakati walipokuwa wanatawala nchi hiyo na ilipokuwa ni British Protectorate. Walifanya uamuzi huo baada ya Wajerumani kushindwa katika vita kuu ya kwanza na Waingereza walipoichukua German East Afrika - iliyokuwa inaitwa Deutsch Ostafrika katika Kijerumani - na kuwa koloni yao ya Tanganyika. Kabla ya hapo, kutokana na makubaliano kati ya Waingereza waliokuwa watawala wa Nyasaland na Wajerumani waliokuwa watawala wa nchi yetu, mpaka wa ziwa ulikuwa kati ya ziwa. Na ndiyo mpaka huo tu ambao ni halali pamoja na jina kuitwa Nyasa, siyo Malawi.

      Uamuzi wa Waingereza kuliweka ziwa hilo chini ya utawala wao Nyasaland haukubadilisha mpaka wa ziwa kihalali kwa sababu mipaka yote ya nchi zetu ilikubaliwa wakati bara letu lilipogawanywa na wakoloni. Ni mipaka hiyo ambayo hata sisi tuliikubali baada ya kupata uhuru na hakuna hata nchi moja ambayo ina haki peke yake ya kubadilisha mipaka hiyo. Hata Waingereza hawakuwa na haki ya kulikiweka Ziwa Nyasa chini ya ukoloni wao Nyasaland kwa sababu walivunja makubaliano yao na Wajerumani ambayo yalisema mpaka wa ziwa ni kati ya ziwa hilo: nusu ni sehemu ya Deutsch Ostafrika ambayo sasa ni Tanganyika, na nusu nyingine ni ya Nyasaland chini ya utawala wa Waingereza.

      Hata wilaya ya Rungwe ambayo ilijumuisha Kyela na Ileje ilikuwa inatawaliwa kutoka Nyasaland mara tu baada ya Wajerumani kushindwa vita kuu ya kwanza na Waingereza walipopewa madaraka ya kutawala nchi ambayo ilikuwa ni koloni ya Wajerumani; yaani nchi yetu ya Tanganyika.

      Deutsch Ostafrika - German East Africa - ilikuwa ni nchi tatu: Tanganyika, Ruanda na Urundi (nchi ambazo zilibadili majina na kuitwa Rwanda na Burundi mwaka 1962 baada ya kupata uhuru).

      League of Nations - jumuiya ya mataifa iliyoitangulia United Nations - iliwapa Wabeligiji Ruanda na Urundi. Koloni hizo mbili za Wabeligiji zilikuwa zinatawaliwa kutoka Leopoldville, mjii mkuu wa Belgian Congo, nchi ambayo pia ilikuwa inatawaliwa na Wabeligiji. Mpango huo ni kama vile wilaya ya Rungwe ilipowahi kutawaliwa kutoka Karonga na Waingereza waliokuwa wanatawala wa Nyasaland na baadaye kiuchukua nchi yetu ya Tanganyika kutoka kwa Wajerumani.

      Baada ya vita kuu ya kwanza, na Wajerumani kushindwa vita hiyo, waziri mkuu wa Uingereza, Lloyd George, kwenye mkutano wa League of Nations alimwambia raisi wa USA, Woodrow Wilosn, kwamba aichukue German East Africa, yaani nchi yetu, na kuiweka chini ya utawala wa Merikani baada ya Wajerumani kuipoteza nchi hiyo katika vita kuu ya kwanza. Lakini President Wilson alikataa. Angekubali, nchi yetu ingetawaliwa na USA na tungekuwa koloni ya USA. Baada ya Rais Wilson kukataa kuichukua nchi yetu, Lloyd George akakubali na kusema ataichukua Tanganyika na kuiweka chini ya utawala wa nchi yake ya Uingereza. Tuliponea chupuchupu kuchukuliwa na Wamerika. Nchi yetu ingechukuliwa na Wamerika, labda tusingepata uhuru. Wamerika wangeing'ang'ania nchi yetu kama vile walivyo ng'ang'ania nchi zingine walizochukua bila kuzipa uhuru.

      Kuhusu Ziwa Nyasa, kwa kifupi ni kwamba mpaka halali uko kati ya Ziwa. Ni mpaka ambao Wajerumani na Waingereza walikubaliana kuzigawa koloni zao: Nyasaland kuwa ya Waingereza; nchi yetu, Deutsh Ostafrika, kuwa ni ya Wajerumani. Walikubaliana kwamba mpaka wa ziwa ni kati ya ziwa hilo. Upande mmoja tu, Waingereza, hawakuwa na haki ya kubadili mpaka kati ya Tanganyika na Nyasaland walipolikweka ziwa hilo chini ya utawala wao Nyasaland.

      Nukuru kutoka kitabu cha Nyerere and Africa: End of an Era, ukurasa 484:

      "Dr. Banda also claimed substantial parts of Tanzania, including - Rungwe district - and the rest of Mbeya Region in southwestern Tanzania, as Malawian territory. He also claimed the entire Eastern Province of Zambia, provoking a curt response from Zambia’s president, Dr. Kenneth Kaunda, who challenged Banda to 'Go ahead and declare war on Zambia.'

      And President Nyerere dismissed Banda’s claim to large chunks of Tanzanian territory as 'expansionist outbursts, which do not scare us, and do not deserve my reply.' The outlandish claim also drew a sharp response from Nyerere who said Dr. Banda was 'insane.' But, he warned, 'Dr. Banda must not be ignored; the powers behind him are not insane.'"


      Akizungumza ktk chuo kikuu cha Dar es Salaam, November 1997, Mwalimu Nyerere alisema

      "In 1961 we became independent. In 1962, early 1962, I resigned as prime minister and then a few weeks later I received Dr. Banda. Mungu amuweke mahali pema (May God rest his soul in peace). I received Dr. Banda. We had just, FRELIMO had just been established here and we were now in the process of starting the armed struggle.

      So Banda comes to me with a big old book, with lots and lots of maps in it, and tells me, 'Mwalimu, what is this, what is Mozambique? There is no such thing as Mozambique.' I said, 'What do you mean there is no such thing as Mozambique?' So he showed me this map, and he said: 'That part is part of Nyasaland (it was still Nyasaland, not Malawi, at that time). That part is part of Southern Rhodesia, that part is Swaziland, and this part, which is the northern part, Makonde part, that is YOUR part.'

      So Banda disposed of Mozambique just like that. I ridiculed the idea, and Banda never liked anybody to ridicule his ideas.
      So he left and went to Lisbon to talk to Salazar about this wonderful idea. I don’t know what Salazar told him. That was ‘62."
      Quote By Simba mnyama
      Wana-JF,

      Mgogoro wa mpaka katika Ziwa Nyasa unaonesha ngoma bado mbichi kabisa. Hebu tusome hizi habari kutoka Malawi:

      Lake Malawi/Nyasa row: Time to show strong leadership
      By Cedrick Ngalande August 6, 2012
      At around the time of independence quite a few people in Tanzania wanted to claim a huge part of Lake Malawi or Lake Nyasa . Cool heads eventually prevailed, as most Tanzanians, including the legendary President Julius Nyerere, understood the importance of respecting boundaries emanating from colonial times. During most of Dr Kamuzu Banda’s rule, Tanzania never really pushed this crazy idea of dividing up the lake. The issue was almost forgotten during the rule of Dr Bakili Muluzi and thereafter. In fact, Dr Bingu wa Mutharika commissioned a company to start exploring oil in the lake. Tanzania said nothing at that time. Now we have a new president and all of sudden the Tanzanians are demanding that our government stop all exploration activities in the lake until all border issues have been clarified. Why now? Folks, there is a reason why we have tradition. Tradition may appear useless and outdated but it is important because it usually become established after a long experience. In politics there is what is known as ‘presidential protocol’. These are small things which over the years have proven to be niceties a president must or must not do in order to represent his/her country correctly.

      Test for President Joyce Banda to diplomatically manage the dispute on the boundary You would think some of them are not important but they are. Here are a few of them – presidents never bow for other presidents in public; presidents never escort anybody to their car; presidents walk with their arms spread outwards apparently projecting power and being in control; presidents usually put on a solid color (one color) necktie because it portrays power; when two presidents greet each other while facing the camera, each of them jostle to be on the right side so that his palm will face the camera- another sign of power, apparently; when in company of other presidents, they try to be the last one to enter the door – a fatherly gesture; there is an interesting video clip of Chairman Yassier Arafat and PM Ehud Barak jostling to be the last one to enter a room at Camp David. The sight of President George W Bush gently pushing PM Gordon Brown into Number 10 Downing Street before himself angered some British political experts. Statesmanship is a game because image is everything in international politics.

      A country’s image depends a lot on the demeanor of its leader. President Barak Obama likes to pat other leaders on their back after greeting them; you thought that was an unplanned coincidence? Just remember, how your father used to pat you on the back when you were a good boy!
      It is said that Bill Clinton failed to get a good deal at his summit with Boris Yelsin in Moscow because President Clinton having sprained his ankle arrived in Moscow on a wheelchair. The sight of a sick American president is said to have psychologically emboldened Boris Yelsin. Ghana is said to have regained its respect in West Africa when President J.J. Rawlings arrived at the 25th Organization of African Unity meeting in Togo in July 2000 in a military uniform portraying a very youthful image. The presidency is acted on a world stage. What a president says and does is very important! When Joyce Banda took over the presidency, she made it appear like Malawi will now be doing everything the donor community tells her to do. In fact some British newspapers were so pleasantly surprised with this that they called us ‘a donor fearing nation’. President Joyce Banda went to London and even bowed before Queen Elizabeth, a very strange gesture considering that both are heads-of-state. Well, all these words and actions have now collectively given an image of a weak leadership in Malawi. The world has sensed blood. Now Tanzania has decided it is time to split up the lake. Notice that they did not bring up this crazy idea when Muluzi or Mutharika were in charge. If we dignify Tanzania’s unreasonable request, one wonders what the next thing will be. Are they now going to claim Chitipa? Will Mozambique now claim Mulanje Mountain?

      Government must make clear that no part of Malawi is up for discussion – full stop! It is time to show strength. Tell Tanzania that Lake Malawi was, is and will always be Malawian. Surprisingly, after all these arrogant statements by the Tanzania government, our government’s response is at best a whimper. The minister of foreign affairs has issued a statement saying the issue will be settled ‘amicably’. Really, Mr. Minister? What could be an amicable statement? Are you planning to even dignify Tanzania’s unreasonable demand? Do you plan to divide up the lake? How can you have an amicable settlement to an
      ONE OF THE STRONGEST WEAPONS IS DIALOGUE

    2. Miaka 50

    3. #21
      Mtanzania's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2006
      Location : UK
      Posts : 5,280
      Rep Power : 5568
      Likes Received
      289
      Likes Given
      77

      Default Re: Ni kweli kuwa Tanzania haina haki na ziwa Nyasa?

      Quote By hume
      Kwa maana hiyo Tanzania inakiri kuwa hatuna sehemu kwenye ziwa nyasa OR sorry wenye ziwa lao wanaliita ziwa Malawi.

      Wenye kujua historia, neno Ziwa Nyasa tulilitoa wapi? Au tulibatiza mali za watu?

      Kama mtu mmoja alivyoshauri, tubadili contents kwenye jiografia ili ieleweke Ziwa Nyasa haliexist!
      Mwanzoni hilo ziwa lilikuwa linaitwa lake Nyasa ikiwa ni kutokana na Nyasaland ambayo ndio malawi ya sasa. walipobadili jina na kuwa Malawi wakataka kubadili na ziwa kuwa Lake Malawi
      lakini kwa Tanzania tumeendelea na jina lile la mwanzo.

      Nafikiri ni sawa na lake Tanganyika, lingebadilishwa kuwa Lake Tanzania.

      Olgah alivyosema ni sawa, kuna mazungumzo yanaendelea, ila nijuavyo mimi yameanza siku nying mno, maana toka mdogo nasikia wanaongea, sijui watamaliza lini?

    4. #22
      Mwiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Posts : 4,593
      Rep Power : 2085
      Likes Received
      223
      Likes Given
      19

      Default Re: Ni kweli kuwa Tanzania haina haki na ziwa Nyasa?

      Ahsanteni sana walioweza kuibua suala hili bungeni, ni juzi tu katika ile hoja ya Tunapata faida gani niligusia na hili salamu zipelekwe bungeni, naona zimefika.

      Sasa nasema kama Mtanganyika, tunataka kuona mpaka unapakwa rangi ya manjano na unakatiza katikati ya ziwa kama ilivyo kwa upande wa msumbiji, hivi vikao hapa si sehemu yake ni kuamuliwa tu na ndivyo ilivyo la si hivyo tutangaze vita vya maji, maana Misri wako tayari kupigana kama maji ya Ziwa Viktoria yatazuiliwa kutiririka kwenye mto Nile, huko kwao wakihisi yanapungua tu wanaulizia kuna nini tunawajibu safari hii mvua sio nyingi.

      Sasa hapa kwenye Ziwa Nyasa kuna uhai na mauti kwa Watanganyika wa mikoa inayopakana na ziwa hili, kama Banda alitangaza vita wakati huo sasa ni wakati wa Tanzania kuelekeza mizinga Malawi, maana wazungu wakikosea tu na kusema kuna mafuta na Uranium katika ziwa Nyasa basi Malawi hatowachia uzi tena atadai na ukingo wa ziwa uliopakana na Tanganyika pia ni wa kwake ni bora kukinga kuliko kutibu.

    5. #23
      Ben Saanane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th January 2007
      Posts : 6,729
      Rep Power : 32787
      Likes Received
      4995
      Likes Given
      6457

      Default Re: Ni kweli kuwa Tanzania haina haki na ziwa Nyasa?

      Hivi admin,uliongea nini vile kuhususu kutumia alama au picha za Viongozi wa taifa kama logo?

    6. #24
      Ulimakafu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2011
      Location : Itabanya Balasi
      Posts : 10,945
      Rep Power : 2603
      Likes Received
      690
      Likes Given
      1615

      Default Ni Ziwa Nyasa au Ziwa Malawi?

      Wadau mi huwa naona kuna mkanganyiko wa kuitwa/kutambuliwa kwa jina la Ziwa letu maarufu Nyasa,vyombo vingine(hata ramani) huonyesha Ziwa Malawi. So kipi ni kipi?

    7. #25
      Vin Diesel's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st March 2011
      Posts : 5,866
      Rep Power : 19947
      Likes Received
      2792
      Likes Given
      1615

      Default Re: Ni Ziwa Nyasa au Ziwa Malawi?

      kuna ramani zinazoonesha ni ziwa nyasa na zingine zaandika ziwa malawi.
      Ramani zilizochapwa malawa zinaandika ziwa malawi.
      zilizochapwa Tz zaandika nyasa.
      Simulated Automated Breakthroughs....

    8. RukaaJuu Final

    9. #26
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,710
      Rep Power : 1287
      Likes Received
      490
      Likes Given
      173

      Default Re: Ni Ziwa Nyasa au Ziwa Malawi?

      Mara Nyingi haya maziwa yaliyopewa majina ya nchi ni kiashirio cha kuwa Upande mkubwa wa ziwa upo katika nchi hiyo.

      Hilo ziwa Lilikuwa linaitwa Ziwa Nyasa wakati Malawi ikiitwa NyasaLand, Malawi walipopata uhuru na kuiita nchi yao Malawi basi walikuwa kwenye mchakato wa kulibadilisha hilo ziwa kuwa Ziwa Malawi, kwa hiyo kimataifa (Official) hilo ni ziwa Malawi japo ni ngumu sana kwa jamii yote ikubali kwa muda mfupi jina jipya kwakitu kikubwa kama hicho.

      Hata Tanzania tulikuwa na Nafasi hiyo ya Kulibadilisha Ziwa Tanganyika na kuwa Ziwa Tanzania lakini ni vitu ambavyo vinasumbua sana

      kwa hiyo ya MAlawi sio mara ya Kwanza, maana hata Ziwa Victoria ilikuwa ikiitwa Lake Nyanza

    10. #27
      kituro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 173
      Rep Power : 464
      Likes Received
      14
      Likes Given
      0

      Default Re: Ni Ziwa Nyasa au Ziwa Malawi?

      Majina yote ni sahihi iwe malawi au nyasa yote yanamanisha kitu kilekile nyasa ni malawi (nyasaland) kwahiyo haijalishi umeita jina gani maana inabaki ileile!.

    11. #28
      kituro's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 173
      Rep Power : 464
      Likes Received
      14
      Likes Given
      0

      Default Re: Ni Ziwa Nyasa au Ziwa Malawi?

      Ndugu zetu wa kyela tunawapenda sana lakini msipokaa sawa mtachukuliwa na wamalawi kwakuwa watasema bonde la nyasa ni lao nanyi mnaishi katika bonde la ziwa malawi (malavi).
      Ulimakafu likes this.

    12. #29
      Kakalende's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st December 2006
      Posts : 2,916
      Rep Power : 1229
      Likes Received
      382
      Likes Given
      374

      Default Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Mwaka jana kuna chi 2 za Amerika Kusini; Nicaragua/Honduras, nusura waingie vitani baada ya mojawapo kufuata ramani ya Google na kutangaza kuwa ndio mpaka wao rasmi.

      Hawa jamaa wa Google, msitari wa mpaka wamechora na rangi nyekundu kisha wanaonyesha LAke Nyasa yote imebaki Malawi, hii imekaaje? Nadhani hili la ugomvi wa mpaka halina itikadi, nakumbuka miaka ya nyuma enzi za Hayati Mwalimu nusura tuzipige na Malawi wakati wa Dr. Banda kwa ajili ya mpaka huu.

      Last edited by Kakalende; 3rd August 2012 at 16:16.
      Mwali and kachwamayebe like this.
      Volunteers are not paid -- not because they are worthless, but because they're priceless!

    13. #30
      Jackbauer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : CTU
      Posts : 4,873
      Rep Power : 1691
      Likes Received
      1348
      Likes Given
      277

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Waziri muhusika hana habari,mbunge hajui na mkuu wa mkoa ana majukumu mengi!

    14. #31
      Kakalende's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st December 2006
      Posts : 2,916
      Rep Power : 1229
      Likes Received
      382
      Likes Given
      374

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Je, Mh. Membe aliliongelea hili kwenye mawasilisho yake Bungeni? au kama liliwahi kusemewa wadau tuleteeni hapa maelezo ya serikali yenu na hatua gani zimechukuliwa kurekebisha mpaka.
      Volunteers are not paid -- not because they are worthless, but because they're priceless!

    15. #32
      pumbatupu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th July 2011
      Posts : 258
      Rep Power : 448
      Likes Received
      77
      Likes Given
      53

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Itakuwa vizuri waki'declare' hivyo ili tupigane manake yale mabomu ya mbagala na g'mboto hayana pa kutumika..nadhani itakuwa muafaka kuanza kuyatumia sasa kuliko hivi yanavyotuua wenyewe..
      maisha ni ubatili mtupu, hebu ishi kama marehemu mtarajiwa..

    16. #33
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,726
      Rep Power : 10177
      Likes Received
      5673
      Likes Given
      12666

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Quote By pumbatupu
      Itakuwa vizuri waki'declare' hivyo ili tupigane manake yale mabomu ya mbagala na g'mboto hayana pa kutumika..nadhani itakuwa muafaka kuanza kuyatumia sasa kuliko hivi yanavyotuua wenyewe..
      wanajeshi wetu wanapiga watu mitaani tu
      Jephta2003 and lutondwe like this.
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    17. #34
      Never give up's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th September 2009
      Location : miles from nowhere
      Posts : 3,640
      Rep Power : 1221
      Likes Received
      723
      Likes Given
      585

      Default

      Quote By Jackbauer
      Waziri muhusika hana habari,mbunge hajui na mkuu wa mkoa ana majukumu mengi!
      hawachelewi kusema mwenye ushahidi atuletee

    18. #35
      dudus's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 2,302
      Rep Power : 1007
      Likes Received
      1291
      Likes Given
      522

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Quote By Kakalende
      Mwaka jana kuna chi 2 za Amerika Kusini; Nicaragua/Honduras, nusura waingie vitani baada ya mojawapo kufuata ramani ya Google na kutangaza kuwa ndio mpaka wao rasmi.

      Hawa jamaa wa Google, msitari wa mpaka wamechora na rangi nyekundu kisha wanaonyesha LAke Nyasa yote imebaki Malawi, hii imekaaje? Nadhani hili la ugomvi wa mpaka halina itikadi, nakumbuka miaka ya nyuma enzi za Hayati Mwalimu nusura tuzipige na Malawi wakati wa Dr. Banda kwa ajili ya mpaka huu.
      Nitashangaa kama Jenerali Shimbo na JWTZ yake watakuwa hawalijui hili na kama wanalijua ni hatua gani wamechukua so far. Hii ndio kazi yao ya msingi waliyoajiriwa na watanzania kuifanya na si kuingilia siasa za ndani au kutisha wananchi.

    19. #36
      LordJustice1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 2,069
      Rep Power : 2301
      Likes Received
      409
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By Kakalende
      Je, Mh. Membe aliliongelea hili kwenye mawasilisho yake Bungeni? au kama liliwahi kusemewa wadau tuleteeni hapa maelezo ya serikali yenu na hatua gani zimechukuliwa kurekebisha mpaka.
      Jana Membe amedai eti kuna kamati imeteuliwa kuhusu suala hilo! Pinda pia aliwahi kudai eti kuna timu ya wataalamu imepelekwa kukutana na wenzao wa Malawi! Hata hivyo niliwahi kusoma kitabu kimoja kilichoandikwa "Boundaries of East Africa" mwandishi aliandika ku-suggest kwamba kisheria Tanzania haina hata tone la la maji Ziwa Nyasa (wamalawi huliita Lake Malawi)! Wamalawi wamekuwa wajanja sana kusambaza Ramani hapa nchini zinazoonesha upuuzi kama huo! Mimi nionavyo, hakuna haja ya kujadiliana na wamalawi, ni vema tukakaa kwenye "state of conflict" tukawa na sehemu ya Ziwa kuliko tukaingia kwenye mjadala na kulikosa kabisa lile Ziwa!
      andate and nyabhera like this.

    20. #37
      TANMO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Tanzagiza
      Posts : 5,046
      Rep Power : 7769
      Likes Received
      1808
      Likes Given
      3439

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Hivi kuna faida gani kuingia vitani kugombania mipaka ilhali kwa kiasi kikubwa wakazi wa maeneo husika wanaingiliana kwenye shughuli zao za kila siku? Mmalawi akitaka mafuta ya taa anakuja Tanzania kuchukua, hivyo hivyo kwa mtanzania anayeishi mpakani. Hebu tujifunze kutumia Diplomasia jamani.

      Nguvu zenyewe za kupigana hatuna, mpaka leo tumeshindwa kupigana na maradhi, na umasikini. Adui ujinga ndiyo anatupiga kila kukicha, hadi Rais wa nchi naye ujinga umemshinda nguvu na sasa ndiyo unaomuongoza kwenye kila analofanya na kusema..
      Do Something......

    21. #38
      LordJustice1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 2,069
      Rep Power : 2301
      Likes Received
      409
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By Never give up
      hawachelewi kusema mwenye ushahidi atuletee
      JK kama angekuwepo wakati wa uhuru tungenyang'anywa hata Mlima Kilimanjaro na Wakenya! Sidhani kama ana uwezo wa kuilinda na kuitetea mipaka yetu!
      JODY BYABATO likes this.

    22. #39
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,617
      Rep Power : 22059
      Likes Received
      998
      Likes Given
      785

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Hao google wana yao uku mambo shwari wamalawi wanakwao nasi kwetu.Uku ritui,mbambabay,manda na itungi operation zaendelea hawa jamaa hatuna kwele nao kabisa.
      Kwanza karonga yote wanaoishi apo ni watz so suala la mpka kwao sio issue kabsaaa
      Iyokopokomayoko likes this.

    23. #40
      Arafat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2009
      Posts : 2,372
      Rep Power : 962
      Likes Received
      583
      Likes Given
      576

      Default Re: Mpaka wa Tanzania na Malawi - Google Earth

      Quote By LordJustice1
      Jana Membe amedai eti kuna kamati imeteuliwa kuhusu suala hilo! Pinda pia aliwahi kudai eti kuna timu ya wataalamu imepelekwa kukutana na wenzao wa Malawi! Hata hivyo niliwahi kusoma kitabu kimoja kilichoandikwa "Boundaries of East Africa" mwandishi aliandika ku-suggest kwamba kisheria Tanzania haina hata tone la la maji Ziwa Nyasa (wamalawi huliita Lake Malawi)! Wamalawi wamekuwa wajanja sana kusambaza Ramani hapa nchini zinazoonesha upuuzi kama huo! Mimi nionavyo, hakuna haja ya kujadiliana na wamalawi, ni vema tukakaa kwenye "state of conflict" tukawa na sehemu ya Ziwa kuliko tukaingia kwenye mjadala na kulikosa kabisa lile Ziwa!
      Labda wanalindwa na hawa hapa:

      Ruhanjo , Ex-TISS Bosi Mr. EM, Waziri Mkulo ............!
      Siku tutakapoacha kuwa mashabiki wa wanasiasa ndio siku hatua ya kwanza ya kujikomboa itakapo anza

    Page 2 of 28 FirstFirst 123412 ... LastLast

    LinkBacks (?)


    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...