Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

    Report Post
    Page 39 of 40 FirstFirst ... 2937383940 LastLast
    Results 761 to 780 of 783
    1. #1
      Kyindokyakombe's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 97
      Rep Power : 375
      Likes Received
      95
      Likes Given
      2

      Default Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

      Kuanzia leo Julai 30, 2012; Gazeti la MwanaHalisi limefungiwa na serikali kwakuwa linadaiwa kuandika habari za uchochezi.

      CHANZO: TBC1

      Quote By Profesy
      JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

      WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

      TAMKO LA SERIKALI

      GAZETI LA MWANAHALISI LAFUNGIWA


      Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelifungia kutochapishwa gazeti la MwanaHalisi kuanzia 30 Julai, 2012 kwa muda usiojulikana kutokana na mwenendo wake wa kuandika habari na makala za uchochezi, uhasama na uzushi likiwa na nia ya kusababisha wananchi kukosa imani na vyombo vya dola hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini.

      Katika matoleo yake hivi karibuni, gazeti la MwanaHalisi toleo Na. 302 la Jumatano Julai, 11 – 18, 2012 na toleo Na. 303 la Jumatano Julai 18 – 24, 2012 na toleo Na. 304 la Jumatano Julai 25 hadi 01 Agosti, 2012 na mengine yaliyotangulia yamekuwa yakichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.

      Mhariri wa gazeti la MwanaHalisi, ameitwa na kuonywa mara nyingi, lakini hataki kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii, pia hazifuati weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.

      Mhariri, mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi yetu ambacho kinatoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutonukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru.

      Uamuzi wa Serikali
      Serikali imeamua kulifungia kutochapishwa kwa muda usiojulikana gazeti la MwanaHalisi, kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976, kifungu Na. (25) (i), adhabu hiyo itaanza tarehe 30 Julai, 2012 kwa mujibu wa Tangazo la Serikali (Government Notice) Na. 258 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali na kutolewa jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Julai, 2012.

      Serikali inawataka wamiliki, wahariri na wanahabari kuzingatia sheria, uzalendo, weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari katika kutekeleza wajibu wa kuhabarisha, kuelimisha na kutoa burudani kwa wananchi.

      Kama ilivyoelezwa Bungeni wakati wa kuwasilisha Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivi karibuni waandishi na watangazaji wa habari wanatakiwa kuhakikisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoandaa vinazingatia taaluma na kuweka mbele maslahi ya Taifa letu na uzalendo. Uhuru na haki ya vyombo vya habari uendane na wajibu.

      Kuanzia sasa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo kwa maksudi vitatoa taarifa za uchochezi ambazo zitahatarisha hali ya amani na utulivu uliopo nchini mwetu.

      Imetolewa na

      OFISI YA MSAJILI WA MAGAZETI
      WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
      30 Julai, 2012
      Committee to Protect Journalists (CPJ) Statement;

      Tanzanian authorities ban weekly indefinitely

      Nairobi, July 30, 2012--The Tanzanian government today banned indefinitely the critical Swahili-language weekly MwanaHalisi, accusing the paper of publishing seditious articles, according to local journalists and a statement by the information ministry.

      The ministry claimed that MwanaHalisi's four July editions contained seditious and false material but did not specify particular articles. Under the 1976 Newspaper Act, Tanzanian authorities can suspend a newspaper at will if they deem that it has "seditious intent," according to CPJ research. MwanaHalisi Chief Editor Jabir Idrissa told CPJ that the paper is considering filing an appeal.

      Idrissa and other local journalists said they suspect the ban is related to a series of articles in MwanaHalisiconcerning the kidnap and torture in late June of physician Steven Ulimboka. Unknown assailants kidnapped and beat Ulimboka on the outskirts of the main commercial city Dar es Salaam after he led a doctors' strike, according to news reports. MwanaHalisi's reports suggested involvement by authorities, citing phone records of an alleged security officer, Idrissa said. Tanzanian security services and President Jakaya Kikwete have denied government involvement, according to local and international reports.

      "Once again, Tanzanian authorities have wielded an archaic newspaper act and vague, unsupported accusations of sedition to censor reporting that is merely critical of the government," said CPJ East Africa Consultant Tom Rhodes. "Authorities should reverse this ban immediately and allow MwanaHalisi to report on the Ulimboka case without fear of reprisal."

      Over the past year, Tanzanian authorities have called MwanaHalisi's editors in for questioning every two or three weeks over their articles, Idrissa said.

      Tanzanian authorities used the Newspaper Act to suspend MwanaHalisi in October 2008 for three months for articles considered seditious and insulting to the president. During the 2010 election campaign, Sethi Kamuhanda, the permanent secretary of the ministry of information, visited print media houses to warn them that the government would close down any media that portrayed the government negatively, according to local journalists.



      For more data and analysis on Tanzania, visit CPJ's Tanzania page here.


      ###
      CPJ is a New York-based, independent, nonprofit organization
      that works to safeguard press freedom worldwide.
      Wajameni serikali hii inataka kutufunga mdomo tuendelee kuwa gizani tusijue madudu yao.

      Pole sana KUBENEA tupo na wewe habari zako za kiuchunguzi zinatusaidia sana na ndizo zinazotufungua macho tujue nchi yetu inavyoliwa.

    2. Miaka 50

    3. #761
      TUMBIRI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 1,856
      Rep Power : 3634
      Likes Received
      1114
      Likes Given
      284

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Last edited by TUMBIRI; 2nd August 2012 at 14:36.
      Hadha Min Fadhil Rhabi - Hizi ni Rehema za Mwenyezi Mungu

    4. #762
      FreedomTZ's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th July 2012
      Posts : 147
      Rep Power : 374
      Likes Received
      22
      Likes Given
      45

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Quote By Ndibalema
      Nanona sasa tunapitia katika kipindi cha udickteta.
      Haswaaa. Ni kile kipindi cha mpito alichosema spika Anna Makinda
      Ndibalema and Sangarara like this.
      "Freedom is never voluntarily given by the oppressor; it must be demanded by the oppressed"
      Martin Luther King, Jr

    5. #763
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,354
      Rep Power : 12596
      Likes Received
      5872
      Likes Given
      781

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Hivi nani aliwambia UN wapo kwa ajili ya kusaidia watu...mnapoteza muda wenu subiri majibu ya UN wataiwekea vikwanzo Tanzania kama Iran.

    6. #764
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,370
      Rep Power : 1212
      Likes Received
      1214
      Likes Given
      1591

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Quote By OLEWAO
      Ushauri, Kwakuwa serikali imetumia mabavu yake kukandamiza uhuru wa kupata habari; hasa kwa waandishi wazalendo kama hawa wa mwanahalisi waliotufungua macho juu ya utekwaji na hatimaye uteswaji wa dr ulimboka na pia vitisho kwa viongozi wa vyama vya upinzani ambao ni wapigania masilahi ya watanzania; Napendekeza vyombo vyote vya habari binafsi viungane na kutoa tamko la pamoja la kususia habari yoyote inayoihusu serikali ya kikwete ili kushinikiza kufunguliwa kwa gazeti la mwanahalisi kwakuwa wahenga walishasema, ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji nywele zako. Coz wakitoka mwanahalisi watakuja mwananchi n.k. Tafakari.
      Hii walitakiwa waifanye Jana.

    7. #765
      Kimboko's Avatar
      Member Array
      Join Date : 16th November 2010
      Posts : 42
      Rep Power : 440
      Likes Received
      6
      Likes Given
      7

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Quote By nasema hili
      Tatizo la watendaji wetu wanatumwa nao wadhaifu wenzao nao wanaenda kichwa kichwa kuuza sura kwenye TV, Hivi nani anatoa hukumu, mahakama au huyo aliyeshika magazeti??? @#%&^*#@%^&* Sana.

    8. RukaaJuu Final

    9. #766
      POMPO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 3,036
      Rep Power : 1192
      Likes Received
      1122
      Likes Given
      649

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      kati ya haO WADAU ongezea na JAMIIFORUMS Tunalaani
      "Tumefika hapa kutokana na UDHAIFU wa Rais Jakaya Kikwete.." J.J. Mnyika, Bungeni,June,2012.

    10. #767
      Curriculum Specialist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2007
      Posts : 1,923
      Rep Power : 1605
      Likes Received
      564
      Likes Given
      183

      Default

      Quote By Mundu
      Ni mkakati mzuri, lakini Tanzania magazeti yasipogusa habari za Serikali yataandika kuhusu nini? Kwa kuwa habari nyingi za nchi hii kwenye magazeti zimejikita kuandika habari za mijini tu, ambazo Serikali ni mchangiaji mkubwa wa habari hizi...basi ushauri wangu, waandishi waanze kuandika habari za jamii, hususan za wananchi wanaoishi vijijini...zinaweza zikaonekana ni habari za kitabaka lakini mwisho wake zitaanza kuzoeleka na kuonekana ni habari muhimu na ndizo zinazopaswa kuandikwa, ili kumkomboa mtanzania mnyonge katika ujinga, umasikini, maradhi, dhuluma n.k
      Waandike habari za CWT, CHADEMA M4C, Maendeleo ya Dr. Ulimboka, zinalipa sana!waachane habari za kiserikali! Hasa zinazohusu mawaziri, Watumie Tbccm tu kwa taarifa zao, ambayo wananchi tumeisusia kitambo!

    11. #768
      Kapo Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2011
      Posts : 374
      Rep Power : 495
      Likes Received
      37
      Likes Given
      0

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Serikali imeshikwa patamu,haki itapatikana tu

    12. #769
      Juaangavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2009
      Posts : 582
      Rep Power : 602
      Likes Received
      42
      Likes Given
      10

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Mtu ukikata tamaa na ukaamini umefika mwisho wa kuruhusu ubongo wako kutafuta suluhu yaan ile halisi ya chanzo cha matatizo yanayokuzunguka, unakuwa hayawani.
      My take, tunaelekea kuna watu ndani ya system wapo ktk stage hiyo. Mungu asipotuepusha kuna siku mtu ataamlisha vifaru viingiye barabara kuzuia wanafunzi wanaodai haki yao ya kufundishwa. Tafakari

    13. #770
      LE GAGNANT's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 1,228
      Rep Power : 710
      Likes Received
      222
      Likes Given
      184

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Gazeti la Annur wanaliogopa.

    14. #771
      bashemere's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th July 2012
      Posts : 175
      Rep Power : 380
      Likes Received
      20
      Likes Given
      44

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      tena kwa sababu tz ina uhusiano wa kujificha na iran afadhari watufungie misaada maana ccm wakula hiyo misaada

    15. #772
      nyanungu magena's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th November 2010
      Posts : 52
      Rep Power : 441
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      wanaogopa sana,ila waliomtesa uliomboka kwa matesa ya namna ile hata shetani aligeuka pembeni na kusema mimi cjawatuma kufanya hivi.

    16. #773
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      593
      Likes Given
      76

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Usemi wa kwamba ukweli UNAUMA ndo unajidhihilisha hapa;why mwanahalisi tu sio majira wala uhuru?may god curse this

    17. #774
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,619
      Rep Power : 15263
      Likes Received
      3732
      Likes Given
      2868

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini


      Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mkajanga


      MCT yasikitishwa kufungiwa MwanaHalisi


      Baraza la Habari Tanzania (MCT), limesema limesikitishwa na kitendo cha kufungiwa kwa gazeti la MwanaHalisi kwa kipindi kisicho na ukomo na kwamba haliungi kusimamishwa wala kufungiwa kwa chombo chochote cha habari kwa sababu yeyote ile.

      Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mkajanga, alisema baraza linaamini makosa na matatizo ya kitaaluma hayawezi kumalizwa katika kufungia magazeti ama aina yeyote ya chombo cha habari.

      “Kufunga ama kusimamisha vyombo vya habari ni ukiukwaji wa wazi wa uhuru wa vyombo vya habari kwa sababu kunawanyima wateja wa chombo hicho haki yao ya kupata habari za chaguo lao,” alisema.

      “Kunawanyima raia ambao wamekuwa wakitumia chombo hicho haki ya kueleza maoni yao, kunanyima uhuru wa kujieleza na kukwaza demokrasia, hivyo kusimamishwa kwa gazeti la MwanaHalisi ni jambo la kusikitisha,” aliongeza.

      Aidha MCT ilisema sheria ambayo serikali imeitumia kulifungia gazeti hilo ni ile ambayo imekuwa ikilalamikiwa na wadau wa vyombo vya habari.

    18. #775
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      593
      Likes Given
      76

      Default

      Ipo siku tutashinda ubabe huu:lets unite

    19. #776
      mchemsho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Posts : 2,016
      Rep Power : 810
      Likes Received
      271
      Likes Given
      22

      Default Re: kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi Tanzania yashitakiwa UN na Mabalozi nchini

      Liwalo na liwe, swala hili limeamuriwa na waziri, marufuku kujadiliwa...poor kikwete

    20. #777
      Njaa Mbaya's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th July 2012
      Posts : 155
      Rep Power : 378
      Likes Received
      26
      Likes Given
      88

      Default Re: Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

      Aisee yaani CCM sijui unaweza kuilezea kwa maneno gani ukaipatia juu ya UDHAIFU wake maana sioni maneno ya kutumia

    21. #778
      bob giza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2010
      Posts : 267
      Rep Power : 514
      Likes Received
      5
      Likes Given
      2

      Default Re: Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

      Quote By denoo49
      masafa yake ni mwenge, ubungo, buguruni na mbagala. Nauli 400, haina msaada kwenye tuta.
      umesomeka afande...ova

    22. #779
      bob giza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2010
      Posts : 267
      Rep Power : 514
      Likes Received
      5
      Likes Given
      2

      Default Re: Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

      Quote By Remote
      104.4 fm kwa dsm
      nashukuru sana mkuu!!

    23. #780
      brasy coco's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2012
      Posts : 338
      Rep Power : 424
      Likes Received
      58
      Likes Given
      9

      Default Re: Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

      Me nashindwa kuelewa ina maana hii serikali inajiamulia tu ina maana waziri yeye ndo mahakama?? Kama kuna habri ya uchochezi kwanini wasipeleke kesi mahakamani?? Walijua kabisa kesi atashinda mwanahalisi sababu anasema kweli me sikubaliani na hawa madikteta washenzi kabisa wanafanya Nchi kama yao......................na hawa wengne hawapendi nao wangegoma kuandika habari yeyeto ya serikali au kufanya maandamano nasi tutakuwa nyuma yao

    Page 39 of 40 FirstFirst ... 2937383940 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...