Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

    Report Post
    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast
    Results 21 to 40 of 59
    1. #1
      Nyenyere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 1,881
      Rep Power : 0
      Likes Received
      487
      Likes Given
      689

      Post Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Kama habari iliyoandikwa na mwandishi Exavery Mzuzu wa Dira ya Mtanzania itakuwa kweli, basi sakata la zabuni ya mafuta TANESCO litachuma mapesa mengi kuliko linavyodhaniwa kuokoa. Mwandishi huyu anaripoti kuwa makampuni yaliyoshinda zabuni kabla ya kutenguliwa na katibu mkuu Maswi yamekimbilia mahakamani kudai fidia. Sasa sijui hili suala kisheria limekaaje, maana hawa PUMA walichofanya ni kuchungulia wenzao wametoa offer kiasi gani halafu wao wakashuka chini yao. Je hii siyo unfair competition?

      Pia hivi hatuoni kuwa kuna madhara makubwa sana kama tutaruhusu individuals kuingilia michakato ya kisheria kwa kigezo cha kuokoa "maslahi ya taifa?" Kitendo hiki hiki tunachokiona ni cha kishujaa leo hii, baadaye kitatuumiza vibaya sana. Ni uzalendo huu huu ndio uliogeuka mwiba mchungu kwa Mh. Lowasa. Kwani ilikuwa ni lazima mshindi wa zabuni apatikane kama makampuni yaliyoomba yalitoa bei kubwa? Sheria za manunuzi ya umma zinasemaje kuhusu hili? Kwa nini zabuni isingetangazwa tena ili kuruhusu makampuni zaidi kushiriki (wakiwemo PUMA)?

      Kauli aliyotolewa na waziri kuwa wanaodhani bodi haitaingiliwa wanajidanganya inaiweka wapi bodi. Je, kautamaduni haka kakijichimbia mizizi si ndio itakuwa loophole ya ufisadi? Tunashangilia leo bila kujua nini kinakuja kesho. Si lazima itokee kwa waziri aliyepo sasa, inaweza kutokea hata katika wizara nyingine pia, na tutapaswa kuwaelewa na kuheshimu uzalendo wao.

      Suala jingine la msingi kabisa hapa: kama kweli PUMA nao walishiriki zabuni ya kwanza na bei yao ikawa juu hadi walipogundua wameshindwa ndipo wakashusha, walitaka kufanya ufisadi pia? Vipi kama makampuni mengine nayo yangepewa nafasi ku-bid kwa kigezo kuwa mshindani wao PUMA kashusha bei, je kuna uwezekano tungewezapata bei chini zaidi ya hiyo 1460/=?

      Disclaimer: Mimi si msomi wa sheria za manunuzi au sheria kwa ujumla. Hii ni tafakuri yangu tu.
      The glory of Christianity is to conquer by forgiveness - William Blake

    2. Miaka 50

    3. #21
      Ndukidi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Posts : 373
      Rep Power : 576
      Likes Received
      141
      Likes Given
      346

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Nyenyere
      Kama habari iliyoandikwa na mwandishi Exavery Mzuzu wa Dira ya Mtanzania itakuwa kweli, basi sakata la zabuni ya mafuta TANESCO litachuma mapesa mengi kuliko linavyodhaniwa kuokoa. Mwandishi huyu anaripoti kuwa makampuni yaliyoshinda zabuni kabla ya kutenguliwa na katibu mkuu Maswi yamekimbilia mahakamani kudai fidia. Sasa sijui hili suala kisheria limekaaje, maana hawa PUMA walichofanya ni kuchungulia wenzao wametoa offer kiasi gani halafu wao wakashuka chini yao. Je hii siyo unfair competition?

      Pia hivi hatuoni kuwa kuna madhara makubwa sana kama tutaruhusu individuals kuingilia michakato ya kisheria kwa kigezo cha kuokoa "maslahi ya taifa?" Kitendo hiki hiki tunachokiona ni cha kishujaa leo hii, baadaye kitatuumiza vibaya sana. Ni uzalendo huu huu ndio uliogeuka mwiba mchungu kwa Mh. Lowasa. Kwani ilikuwa ni lazima mshindi wa zabuni apatikane kama makampuni yaliyoomba yalitoa bei kubwa? Sheria za manunuzi ya umma zinasemaje kuhusu hili? Kwa nini zabuni isingetangazwa tena ili kuruhusu makampuni zaidi kushiriki (wakiwemo PUMA)?

      Kauli aliyotolewa na waziri kuwa wanaodhani bodi haitaingiliwa wanajidanganya inaiweka wapi bodi. Je, kautamaduni haka kakijichimbia mizizi si ndio itakuwa loophole ya ufisadi? Tunashangilia leo bila kujua nini kinakuja kesho. Si lazima itokee kwa waziri aliyepo sasa, inaweza kutokea hata katika wizara nyingine pia, na tutapaswa kuwaelewa na kuheshimu uzalendo wao.

      Suala jingine la msingi kabisa hapa: kama kweli PUMA nao walishiriki zabuni ya kwanza na bei yao ikawa juu hadi walipogundua wameshindwa ndipo wakashusha, walitaka kufanya ufisadi pia? Vipi kama makampuni mengine nayo yangepewa nafasi ku-bid kwa kigezo kuwa mshindani wao PUMA kashusha bei, je kuna uwezekano tungewezapata bei chini zaidi ya hiyo 1460/=?

      Disclaimer: Mimi si msomi wa sheria za manunuzi au sheria kwa ujumla. Hii ni tafakuri yangu tu.
      As long as mkono yupo kwenye hilo sakata, ni lazima waende mahakamani, kwani si ndio huko anakopatia hela yake kwa kushirikiana na majaji wapuuzi.

    4. SMU
      #22
      SMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2008
      Location : Mavurunza
      Posts : 4,534
      Rep Power : 3811
      Likes Received
      1312
      Likes Given
      1916

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Lu-ma-ga
      Lakini pia mkumbuke kuwa ki-mkataba anayetakiwa kununua mafuta kwenda IPTL ni serikali wala si TANESCO walikuwa wanafanya hivyo kuhalalisha wizi na kurahisisha migawo.kwa maana nyingine hiyo tender ni batili pia kwani TANESCO alijitwalia jukumu lisilo lake
      Hili ni jipya sasa. Kama hili unalosema ni la kweli basi tuna tatizo kubwa zaidi.

      Shida yangu kubwa katika suala hili ni kampuni ya PUMA kutoshindanishwa na makampuni mengine kabla ya kupewa zabuni hiyo (hata kama anayenunua ni serikali na sio tanesco!).
      "Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau

    5. #23
      Mtumpole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2010
      Location : Dreamland
      Posts : 525
      Rep Power : 548
      Likes Received
      93
      Likes Given
      327

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Lu-ma-ga
      Lakini pia mkumbuke kuwa ki-mkataba anayetakiwa kununua mafuta kwenda IPTL ni serikali wala si TANESCO ....
      Tena ni WIZARA YA NISHATI NA MADINI.
      Mwenye dhambi hana raha

    6. #24
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 7,999
      Rep Power : 12012
      Likes Received
      5321
      Likes Given
      5154

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Ndukidi
      Kama nilivyomuelewa waziri, alisema kuwa Puma walikuwapo kwenye bidding ya kwanza na kwa bei hiyo hiyo ya chini wakatoswa.Haya makampuni mengine wakapewa kwa mkataba wa 1500 Tshs kwa lita arround there, lakini ilipofika kwenye malipo wakawa wanalipwa 1800 tshs kwa lita. Nadhani tatizo liko hapo maana yake walikiuka mkataba tayari. Labda tufuatilie tena kuujua ukweli kwenye hili.
      Ndugu yangu Ndukidi kuna mahali nimemweleza mleta thread Nyenyere kwamba lazima kuna mambo ambayo yamejificha ambayo sisi hatuyajui. Kwakuwa sitaki kuamini kwamba katibu mkuu Maswi aliamua kubatilisha zabuni hiyo na kuwapa Puma bila kujiridhisha kama taratibu zilifuatwa.
      Kama maelezo yako ni sahihi basi hapa kuna mengi yaliyofichika katika zabuni hii ambayo kama kweli wanakwenda mahakamani, basi yatawekwa hadharani na ndipo tuatajua nani ni nani katika sakata hili.

      Kama walishinda zabuni kwa bei ya sh.1,500 kwa lita lakini wakalipwa Tsh.1,800 basi hapo ni wazi kwamba kulikuwa na harufu ya rushwa, na huenda PUMA walienguliwa kimizengwe toka hatua za awali ili kukamilisha dili.
      SMU likes this.
      Honesty is a very expensive GIFT. Do not expect it from cheap people.

    7. #25
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 7,999
      Rep Power : 12012
      Likes Received
      5321
      Likes Given
      5154

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Ndukidi
      As long as mkono yupo kwenye hilo sakata, ni lazima waende mahakamani, kwani si ndio huko anakopatia hela yake kwa kushirikiana na majaji wapuuzi.
      Aiseeee......
      Honesty is a very expensive GIFT. Do not expect it from cheap people.


    8. #26
      Twasila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2011
      Posts : 436
      Rep Power : 494
      Likes Received
      58
      Likes Given
      0

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By simplemind
      Lowest bidder shall not be neccesarily be accepted.
      Not lowest bidder but lowest eavluated bidder. The difference between the two is yawnimg.

    9. #27
      Twasila's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2011
      Posts : 436
      Rep Power : 494
      Likes Received
      58
      Likes Given
      0

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Mr. Maswi is not the CEO of TANESCO. Which law gives him the powers to vary the decision of TANESCO's tender award? Haya shauri zetu!!

    10. #28
      Lu-ma-ga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 1,851
      Rep Power : 814
      Likes Received
      527
      Likes Given
      8

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Twasila
      Mr. Maswi is not the CEO of TANESCO. Which law gives him the powers to vary the decision of TANESCO's tender award? Haya shauri zetu!!
      Ki-mkataba mwenye mamlaka ya kununua mafuta na kusupply IPTL ni serikali kupitia Wizara ya nishati na madini

    11. #29
      Lu-ma-ga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 1,851
      Rep Power : 814
      Likes Received
      527
      Likes Given
      8

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Kama ulisikiliza vizuri siku waziri nanfanya majumuisho ya hotuba yake alisema hivi: KI-mkataba mwenye mamlaka ya kuuza mafuta IPTL ni wizara ya nishati na madini.Na akasema kuwa mkataba waliweka kama silaha yao ya mwisho kuitoa ktk sakata hili wengi hawakujua kuwa si TANESCO anajulikana ki-mkataba kuwa ni mnunuzi isipokuwa ni wizara,kwa maana nyingine TANESCO walikuwa wanatumika kurahisisha wizi

    12. #30
      Ston Merchant's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st August 2011
      Location : Samunge
      Posts : 248
      Rep Power : 444
      Likes Received
      40
      Likes Given
      29

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Ndahani
      Acha liwalo na liwe...inanikumbusha hadithi ya mtu aliyejitosa kwenye mto wenye maji yenye kasi huku akiwa hajui kuogelea wala majaaliwa yake.
      kma Chemba..
      " Umeme hauna kiuno lakini Unakatika. "

    13. #31
      Nyenyere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 1,881
      Rep Power : 0
      Likes Received
      487
      Likes Given
      689

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Quote By Lu-ma-ga
      Kama ulisikiliza vizuri siku waziri nanfanya majumuisho ya hotuba yake alisema hivi: KI-mkataba mwenye mamlaka ya kuuza mafuta IPTL ni wizara ya nishati na madini.Na akasema kuwa mkataba waliweka kama silaha yao ya mwisho kuitoa ktk sakata hili wengi hawakujua kuwa si TANESCO anajulikana ki-mkataba kuwa ni mnunuzi isipokuwa ni wizara,kwa maana nyingine TANESCO walikuwa wanatumika kurahisisha wizi
      Kwa hiyo mawaziri waliotangulia wana kesi ya kujibu!
      The glory of Christianity is to conquer by forgiveness - William Blake

    14. #32
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,662
      Rep Power : 718
      Likes Received
      291
      Likes Given
      36

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Vipi unaogopa mahakama? yes hofu yako ina maana saana but haina msingi sana, issue hapa ni wanasiasa ccm na wafanyabiashara ccm, na Waathirika ni Maskini watanzania,tusubiri tuone, may be ni upepo tu coz tanzania kila siku lazima issue ya kifisadi itoke

    15. #33
      MVUMBUZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th January 2011
      Posts : 2,586
      Rep Power : 1090
      Likes Received
      685
      Likes Given
      374

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Hii yote ni kitu gani kama siyo vita ya wenye nguvu wachache kupigania rasilimali za watanzania kwa manufaa binafsi? UDHAIFU wa serikali kushindwa kununua mafuta yenyewe ndio unaotufikisha hapa. Hii public and private partneship(PPP) imevaa joho lingine la ufisadi. System hii inaanzishwa tena bila kufanya utafiti wa efficiency yake huku lengo likiwa kuwapa ulaji mafisadi wachache kwa kigezo cha kufanya kazi na private sector.
      Nyenyere likes this.

    16. #34
      Fofader's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2011
      Posts : 502
      Rep Power : 487
      Likes Received
      105
      Likes Given
      54

      Default

      Hii ya mahakamani ndio itakuwa nzuri. Mahakamani maswali mengi ya msingi yataulizwa. Tutajua mengi zaidi!!
      Nahisi kwamba kinachojulikana mpaka sasa ni tip of an iceberg.

    17. #35
      timbilimu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Location : DSM
      Posts : 2,672
      Rep Power : 977
      Likes Received
      584
      Likes Given
      10

      Default

      Quote By Mtumpole
      Tena ni WIZARA YA NISHATI NA MADINI.
      Watanzania wenzangu mgogoro hapa siyo Wizara ama Tanesco analipa pesa za mafuta,kiini cha tatizo ni Mkataba mzima kati ya Serikali/Tanesco na IPTL. Naiona Dowans nyingine ikikamua pesa za bure za walipa kodi wa nchi hii.

    18. #36
      WildCard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd April 2008
      Posts : 6,455
      Rep Power : 1980
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      59

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Nilidhani tungeangalia uwezekano wa kuzirudisha bilioni 6 za kila mwezi zilizokwapuliwa na mafisadi hawa kwa kipindi chote hiki kwa kuwa mkataba walioingia na TANESCO ambao ni batili tokea mwanzo kumbe bado tunaleana tu!

    19. #37
      akilipana's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th October 2009
      Posts : 57
      Rep Power : 498
      Likes Received
      3
      Likes Given
      10

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Bodi kitu gani bana? Bodi ya korosho ya M/kiti Ana si yala tu mapesa? Inamsaidiaje mkulima. Bodi ziwe na wataalamu siyo wanasiasa

    20. #38
      Ngatele's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th January 2011
      Posts : 31
      Rep Power : 428
      Likes Received
      4
      Likes Given
      6

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Maswi hakununua mafuta bali alielekeza yanununliwe PUMA, serikali kama financier ingependa kupata value for money though wizara haikuwa mnunuzi. RITA walielekezwa waishauri TANESCO watumie section 42 ya emergency procurement baada ya kuonekana hitaji la kuwasha mitambo ya IPTL ambayo iko chini ya RITA lakini Mhando akafanya mchakato wa kawaida wa kuitisha tenda kabla ya maelekezo kutoka RITA, note that Maswi baada ya kufahamu kuwa PUMA wana bei ya chini alielekeza mafuta yanunuliwe kwao under emergency situation ambapo bodi ya zabuni haihusiki.

      Cha kutazama hapa ni kama TANESCO walipeleka taarifa PPRA kulingana na Section 31(3) ya PPA 2004 na pia kama taarifa pia ilipelekwa kwa Paymaster General ili baadaye uchunguzi ufanyike kama kweli kulikuwa na emergency situation na kama haikuwepo njia nyingine ya ushindani ingetumika mafuta yangenunuliwa kwa bei gani? na kama itakuwa ya chini ya iliyotumika, ile tofauti ya total amount itabidi Mhando ailipe.

      Kwa ujumla msimamizi wa manununzi ya taasisi ni Accounting Officer kwa hivyo yeye ndiye atawajibika kama hakufuata sheria ya manunuzi. Wizara ilitoa pesa na yeye alipaswa kuzingatia sheria na vingenevyo kushauri yapasayo kufanywa but in total value for money iwe achieved na si emergency situation itumike kuwaambia wazabuni niwekee za kwangu knowing that ni lazima mafuta yanunuliwe because there is an emergency!!!!

    21. #39
      LIWALONALIWE's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th July 2012
      Posts : 29
      Rep Power : 900
      Likes Received
      7
      Likes Given
      0

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Liwalo na liwe

    22. #40
      sosoliso's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Mwembekiuno
      Posts : 2,836
      Rep Power : 17963
      Likes Received
      1622
      Likes Given
      1562

      Default Re: Walioshinda Zabuni TANESCO wakimbilia Mahakamani!

      Ninachoona hapa ni vita vya kupigania maslahi binafci.. Inanikumbusha kasheshe ya kuchelewa project ya vitambulisho vya taifa pamoja ni hii ya karibuni iliomuondoa Nundu na Mfutakamba.. Masharti na vigezo havizingatiwi kabisa..!

    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...