Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 28
    1. #1
      Kijakazi's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 26th June 2007
      Posts : 1,421
      Rep Power : 0
      Likes Received
      375
      Likes Given
      10

      Default Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Maoni ya Mzee Kingunge alipoulizwa kwa nini anafikiri Afrika bado iko nyuma!

      Alisema

      " Wakati wazungu walipofanikiwa na mapinduzi ya viwanda waasia wakajiuliza (wajapani) hivi ni nini siri ya mafanikio yao (yani wazungu) wakagundua kwamba siri yao iko kwenye maarifa, wakajifunza maarifa na wakatoka, wakaja wakorea wakajiuliza swali hilo wakagundua kwamba ni maarifa wakaiga wakatoka, wataiwani na wasingapore hivyo hivyo na sasa wachina nao wamegundua siri ya wazungu ni maarifa wameiga wanatoka ila Afrika akasema TUNAFIKIRI SIRI YA MAFANIKIO YA MZUNGU IKO KWENYE LUGHA YAKE NA RANGI YAKE kwa hiyo tunafanya kila tuwezalo kuwekeza katika hayo mambo mawili na ndio kilichotufikisha hapa tulipo"

      Hayo ni maneno ya Mzee Kingunge, nini maoni yako, unaafiki naye?
      Leonard Akaro and Kizotaka like this.

    2. FemaTV & Radio

    3. SMU
      #2
      SMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2008
      Location : Mavurunza
      Posts : 4,531
      Rep Power : 3810
      Likes Received
      1311
      Likes Given
      1916

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Kwenye suala la maarifa yupo sahihi.

      Nyerere alisema "umasikini wa mawazo ndio umasikini mbaya san
      Richard likes this.
      "Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau

    4. #3
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 11,914
      Rep Power : 24137
      Likes Received
      4637
      Likes Given
      2628

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By Kijakazi

      Hayo ni maneno ya Mzee Kingunge, nini maoni yako, unaafiki naye?
      Yeye alifanya nini kama sio kuiga kuva manguo ya kichina


      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    5. #4
      NATA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2007
      Posts : 4,255
      Rep Power : 8416
      Likes Received
      1133
      Likes Given
      390

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Wao si ndio wasisi, wamefanya nini kuwekeza katika maarifa hadi sasa wanamiaka 100+++.lol!

    6. #5
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 589
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Ameshazeeka huyo apumzike sasa!

    7. Miaka 50

    8. #6
      BIG X's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2011
      Location : WHITE HOUSE
      Posts : 767
      Rep Power : 414
      Likes Received
      197
      Likes Given
      168

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Nimependa hayo maneno, yanafanana na hali halisi.
      GOOD JUDGEMENT COMES FROM EXPERIENCE, BUT EXPERIENCE COMES FROM BAD JUDGEMENT.

    9. #7
      Joseph's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd August 2007
      Location : Zanzibar
      Posts : 2,661
      Rep Power : 1139
      Likes Received
      678
      Likes Given
      417

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Hivi huyu mzee mpaka leo bado ni mbunge wa kuteuliwa na Rais?
      You can never have someone praise you,nor will anyone condemn you,never in the past,not at present and never will be in the future.

    10. #8
      KOMBESANA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2009
      Posts : 525
      Rep Power : 610
      Likes Received
      114
      Likes Given
      1460

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Kingunge amekata shauri ama ameokoka?Sababu ninazo:
      Kingunge kasoma Russia yaani USSR tena Taasisi ya Heshima iitwayo Patrice Lumumba.Huyu ana uhuru wa kutuambia yeye binafsi kaiga nini USSR.
      Huyu ni aina ya wapanga mikakati wakubwa wa CCM na Serikali yake kwa miaka mingi.Wakati CCM ikiwekeza kwenye lugha na rangi ya wakoloni alikuwa wapi?
      Kingunge NGOMBALE Mwiru aidha sasa kachoka mno kimawazo ama vijana wanaotawala hawamjali tena ndiyo maana anabwatuka.
      Huyu hataki kusema kuwa kuna mdudu UFISADI anayetafuna na kudumaza maendeleo kwa sababu hata yeye alionja asali pale Ubungo Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani.Hana jipya!
      August likes this.

    11. #9
      Msalagambwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th July 2012
      Posts : 535
      Rep Power : 452
      Likes Received
      177
      Likes Given
      527

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Mjinga anapumua ujinga tu

    12. #10
      Kijakazi's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 26th June 2007
      Posts : 1,421
      Rep Power : 0
      Likes Received
      375
      Likes Given
      10

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By Safari_ni_Safari
      Yeye alifanya nini kama sio kuiga kuva manguo ya kichina

      Sasa si ameshakupa jibu? na yeye si ni mwafrika kwa hiyo anaangukia humo humo!Kwa hiyo swali lako halina mantiki!

    13. #11
      MVUMBUZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th January 2011
      Posts : 2,583
      Rep Power : 1088
      Likes Received
      682
      Likes Given
      374

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Aliwahi kuwa mshauri wa marais waliomtangulia mbona hakuweza kutoa ushauri ili na sisi tuwe kama hao aliowataja. Hizi ni busara za kujipendekeza ambazo hazisaidii kwa sasa.
      August likes this.

    14. #12
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 11,914
      Rep Power : 24137
      Likes Received
      4637
      Likes Given
      2628

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By Kijakazi
      Sasa si ameshakupa jibu? na yeye si ni mwafrika kwa hiyo anaangukia humo humo!Kwa hiyo swali lako halina mantiki!
      Kwa hiyo ameongea ili iweje........akufurahishe ama vipi?

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    15. #13
      Kijakazi's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 26th June 2007
      Posts : 1,421
      Rep Power : 0
      Likes Received
      375
      Likes Given
      10

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By Safari_ni_Safari
      Kwa hiyo ameongea ili iweje........akufurahishe ama vipi?
      Labda! mimi sijui, nimenukuu tu alichokisema!

    16. #14
      Ndoa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2011
      Posts : 624
      Rep Power : 501
      Likes Received
      119
      Likes Given
      46

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Huyo mzee hana lolote! Si alikuwa madarakani mihula yote, alikuwa hayaoni hayo maarifa?

    17. #15
      Borat69's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th June 2012
      Location : Global Citizen
      Posts : 698
      Rep Power : 488
      Likes Received
      279
      Likes Given
      77

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Kwa hili inawezekana Mzee Kingunge yuko sawa. Si unaona baadhi ya dada zetu siku hizi wanavyokimbilia kuzaa na wazungu hata vibabu ili wapate watoto machotara na kuwaweka kwenye blogs kuwa ndio watoto wanaovutia. Hao hao dada zetu wanajichukia kupita kiasi mpaka inafikia kujichubua na kuharibu ngozi zao nzuri za kiafrika kwa kutaka kuwa wazungu..inasikitisha sana. Mzee Kingunge might have a point there.
      "Our Lives begin to End the Day We Become Silent About Things that Matter"-Dr Martin Luther King Jr.

    18. #16
      HOMOSAPIEN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st March 2011
      Posts : 483
      Rep Power : 508
      Likes Received
      131
      Likes Given
      42

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By webondo
      Ameshazeeka huyo apumzike sasa!
      Umesema kweli hata uwezo wake wa kufikiri umepungua kabisa,maneno haya hakustahili kuyasema yeye kwani ni lipi alilowezesha kufikia maarifa,wakati wake na Nyerere kulikuwa na vyuo vikuu vingapi?.na sasa amezeeka kaachana na siasa vipo vingapi.nani anayejaribu kufikia maarifa.
      THE FUTURE ALWAYS START TOMORROW AND NOT TODAY

    19. #17
      August's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2007
      Posts : 2,744
      Rep Power : 1162
      Likes Received
      251
      Likes Given
      2511

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By Kijakazi
      Maoni ya Mzee Kingunge alipoulizwa kwa nini anafikiri Afrika bado iko nyuma!

      Alisema

      " Wakati wazungu walipofanikiwa na mapinduzi ya viwanda waasia wakajiuliza (wajapani) hivi ni nini siri ya mafanikio yao (yani wazungu) wakagundua kwamba siri yao iko kwenye maarifa, wakajifunza maarifa na wakatoka, wakaja wakorea wakajiuliza swali hilo wakagundua kwamba ni maarifa wakaiga wakatoka, wataiwani na wasingapore hivyo hivyo na sasa wachina nao wamegundua siri ya wazungu ni maarifa wameiga wanatoka ila Afrika akasema TUNAFIKIRI SIRI YA MAFANIKIO YA MZUNGU IKO KWENYE LUGHA YAKE NA RANGI YAKE kwa hiyo tunafanya kila tuwezalo kuwekeza katika hayo mambo mawili na ndio kilichotufikisha hapa tulipo"

      Hayo ni maneno ya Mzee Kingunge, nini maoni yako, unaafiki naye?
      mbona yeye mwenyewe anapenda rangi nyeupe kama wale watu wa maeneo ya ziwa victoria, mwanzo nilifikiri mzee atakuwa mtu wa musoma au mwanza kumbe nanjilinji kilwa

    20. #18
      bensonlifua92's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th December 2010
      Posts : 82
      Rep Power : 444
      Likes Received
      32
      Likes Given
      32

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By Ndoa
      Huyo mzee hana lolote! Si alikuwa madarakani mihula yote, alikuwa hayaoni hayo maarifa?

      Samahani nimechagua tu kuku-quote wewe ila wengi wamekuwa na mawazo au mtizamo kama wako dhidi ya huyu mzee wetu Kingunge Ngombare Mwiru

      Ni kweli kuwa mzee wetu huyu anahusika kwa sehemu kubwa sana kwa taifa letu hili kuwa hivi lilivyo leo kwa kuzingatia nafasi na heshima aliyokuwa amepewa tangu ujana wake alipojitokeza kuwa mtu maarufu hapa TZ na nadhani hadi nchi majirani zetu....., Nakumbuka jina Kingunge kuna wakati lilimaanisha mtu mzito/kigogo..., Mfano utasikiwa watu wanasema aaah!! jamaa yule bwana ni Kingunge kwelikweli.. au utasikia Kingunge wa Tanzania ni..., au Kingunge wa Kenya ni..., Uganda..., n.k. Hii yote nimeamua tu kuonyesha jinsi mzee wetu alivopata fursa ktk taifa letu. Kwa bahati mbaya kabisa inawezekana kuwa mzee wetu huyu kwa makusudi, au kutotambua hiyo fursa, au kwa kubanwa na mfumo au vinginevyo kabisa mawazo anayoyatoa hapo juu kama aliyatambua akiwa bado yungali na nguvu hayajalisaidia taifa letu kwamba sisi hatukuiga MAARIFA ya wazungu badala yake tumeiga LUGHA yao....kwa mujibu wa mzee Kingunge...

      Pamoja na udhaifu wake huo, mimi naona nimshukuru mzee Kingunge kuwa hajataka kuondoka ktk taifa hili bila kutuachia kipande cha maneno haya ya hekima...kwamba tunatakiwa tuige MAARIFA ya wazungu ili tuendelee... Ni wajibu wetu badala ya kumbeza tuu tuchukue haya maneno yake na tuyafanyie kazi..tuweke strategic plans and action plans on how we can make these words BECOME true and reality ktk nchi yetu. Siyo sahihi sana kumpuuza kabisa mzee wetu huyu, huenda ametambua makosa yake na anaona basi atupe hayo yatusaidie. Hata mwalimu Nyerere alikiri kuwa wakti wake walifanya mazuri na makosa pia..akatushauri tuchukue mazuri tuyaendeleze na makosa yao iwe ni fursa ya kujifunza na kufanya marekebisho twende mbele...Ila akatushangaa pia kuwa tunaacha yale mazuri na tumeamua kuchukua makosa yao....


      Mimi nataka niongezee kidogo ktk hayo maneno ya huyu mzee si kwamba tunaiga lugha ya wazungu na kupenda rangi yao tu..Sisi TUNADHANI ILI TUENDELEE TUNAHITAJI MISAADA YA HAWA WAZUNGU...na mbaya zaidi sisi tunadhani tunahitaji KUPIGA DEBE LA NGUVU KUZUNGUKA HUKU NA KULE ILI KUTAFUTA MISAADA YA WAZUNGU... Cha kushangaza kama mzee Kingunge alivosema HATUHANGAIKI KUTAFUTA HAYO MAARIFA YANAYOWAFANYA WAZUNGU WAWE NA MAENDELEO... aaaaah bali kwetu muhimu ni MISAADA eti tunajivuna na kusema MISAADA YA MASHARTI NAFUU.. Nadhani tunajidanganya wenyewe. Hivi hata ukipewa misaada kama huna MAARIFA itakufaa nini?

      Kingine ambacho mzee hajakisemea ni kuwa SISI AU NISEME BADHI YETU (kwa bahati mbaya sana sasa ndo inaonekan ndo style ya viongozi wetu kuchangamkia uongozi) TUNATAMANI KUWA MATAJIRI BILA KUZALISHA... njia ambayo imechaguliwa ni ya kwa kupitia UFISADI... Hivi kuna msomi hapa anaweza niambia kuwa mtu anapoamua kufisadi fungu lililotengwa kwa project/program fulani hapo kweli anaelewa maana ya jambo analofanya? Hapo kweli mtu huyo ni msomi kweli.... Angalia yanayotokea sasa bungeni hivi hawa wabunge wetu wanajua kweli umaana wa wao kuwa viongozi. Fuatilia utagundua kuwa PESA ya serikali kwa ngazi zote ziko kwenye misukosuko mikubwa ya mbinu nyingi na kabambe watu wazifisadi na wafiche au wajipatie mitaji ya makampuni yao ya kishetani....

      Kuna mamo mengi mzee wetu hakuyasema ila TUUUNGANE NAYE KTK HUO HUO UDHAIFU WAKE TUNAOUONA KUWA TUIGE YALE MAARIFA na siyo hizi harakati na mashindano tunayoyashuhudia ya kufisadi taifa letu kwa kila mbinu kwanza hata huyo FISADI kama anaona mbali hata hiyo pesa anayokwapua haifaidi..ni nyingi mno kwa mahitaji yake hapa TZ... ni lawama za bure na tamaa ya bure tu anajipatia... Pia ni ulofa wa hali ya juu na ndhani wazungu wanatushgaa na kutucheka sana... HIVI INAINGIA AKILINI KWELI TUNAPOKEA MISAADA TOKA KWA WAZUNGU AU TUNAIBA PESA YETU WENYEWE KISHA BAADHI WANAKWENDA FICHA KTK MABENKI YAO WAZUNGU HUKO ULAYA AU SIJUI USA HIVI WANADHANI HIYO PESA INAKAA TU BURE, INAKWENDA FANYA BIASHARAAA...NA HATA HAWA WATU WAKITAKA KUITUMIA NI KTK WOGOWOGA TU SASA RAHA HAPO IKO WAPI YA MTU KUWA NA MAPESA MENGI YA KIFISADI...Kwanini udharilike ukipita njiani watu wanakuona wewe ni FISADI, watoto wako wakitanua jamii inawaona ni za kifisadi... usituringie... na zaidi sana kuna CHUKI KUBWA SANA inajengeka sasa ktk jamii juu ya hao MAFISADI na watoto wao na wajukuu wa MAFISADI na hasa vijana..hapo hiyo si hatari huko mtaani jamani...

      TUIGE MAARIFA na tuwe na MIKAKATI na MIPANGO KAZI na tuache KUTEGEMEA MISAADA haina tija kama hatuna MAARIFA... tuache UFISADI na tusiwe na TAMAA BILA KUZALISHA na tuache UVIVU tupambane na maadui wote wa maendeleo kwa kuchapa MZIGO/KAZI..

      ASANTENI SANA

    21. #19
      Kakubilo Kasota's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th March 2012
      Posts : 166
      Rep Power : 395
      Likes Received
      53
      Likes Given
      21

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Huwa sielewi, sijui tumelogwa? mbona hawa watu wakiisha toka kwenye system ndo huwa na mawazo mazuri? Nakumbuka Sumaye naye sikumoja aliwahi kusema, taifa haliwezi kuendela kama hatuuzi vitu nje ya nchi, kama tunanunua zaidi bila uuza then hatutakuwa na fedha za kigeni, aliendelea zaidi kwa kudai tujenge zaidi viwanda ili tupate vitu vya kuuza, ni huyu hyu aliyekuwa waziri mkuu wa muda mrefu kupita yeyote aliyewahi kukalia kiti hicho, swali, kwanini viongozi wengi wa magamba huwa wanaona kikwazo cha matatizo yetu mara baada ya kuachia madaraka?

      Bila kujali historia yake huyo mzee (ambayo kwakweli huwa nasikia kichefu chefu, hasa baadhi ya kauri zake) aliyo yasema ndio ukweli, hivi mwaka 1988 pale kambi ya jeshi kibaha, wanajeshi wale (mainjinia) si waliweza kutengeneza Gari na wakalipa jina la Nyumbu? nakumbuka liliingia hadi kwenye maonesho ya sabasaba, enzi hizo maonesho yale yalikuwa na mvuto sana, hivi kama akina kingunge wangewaendeleza watu wale, leo situngekuwa tunatengeneza ndege? CDM, mkiingia madarakani 2015, endelezeni hili tafadhari!

    22. #20
      Domy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th December 2011
      Location : EARTH
      Posts : 1,861
      Rep Power : 1739
      Likes Received
      437
      Likes Given
      36

      Default re: Tujikumbushe kauli hii ya Mzee KINGUNGE

      Quote By NATA
      Wao si ndio wasisi, wamefanya nini kuwekeza katika maarifa hadi sasa wanamiaka 100+++.lol!
      Walichukua zabuni ya kukusanya ushuru Ubungo terminal

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...