Sasa hivi wanafunzi kata ya ilemela mkoa wa mwanza wapo katika maandamano wakiwa na mabango tofauti yenye maandishi "tunataka haki zetu" wakielekea mahakama ya mwanzo wilaya ya ilemela kufungua kesi zidi ya waalimu kwa kukataa kuwafundisha...
UPDATES:
Wanafunzi wa shule za Msingi za Temeke wakiingia kwenye ofisi za Manispaa ya Temeke kufuatia mgomo wa walimu ulioanza rasmi jana na kuwasababishia kukosa masomo. Picha na Elizabeth Edward - Gazeti la Mwananchi
- TBC1 imeripoti kuwa Ruvuma walimu wamegoma na imethibitisha vurugu kutokea mkoani Mbeya na kuwa nako walimu wamegoma.
Wanafunzi wa shule za msingi Bwawani na Kijichi Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, wakiandamana jana Jumatatu Julai 30, 2012, kupinga haki yao ya msingi ya kupata elimu kuvurugwa kufuatia mgomo wa walimu ulioanza rasmi jana. Wanafunzi hao waliandamana umbali wa kilomite 10 hadi ofisi za Afisa elimu wa manispaa hiyo na kueleza "kesi" yao ambapo wameitaka serikali kumalizana na walimu ili wao wasome.
Eddy Kinawiro huku Kimara wanafunzi wa Shule ya Msing Kimara B wamerudi wote kutokana na kuwa shuleni hakuna walimuLucas Sabuni Baadhi ya S/M Nzega mjini wanafunzi wamerudi majumbani hakuna walimu mashuleni.Simon Mwangoka Mwasile Shule ya secondary Uyole na shule ya msingi Itezi zilizoko katika jiji la mbeya wamegoma 99% nimeshuhudia mwenyewe kwa kutembelea maeneo husika.



Reply With Quote

Follow Us Here