
By
ukwelikitugani
Mfa maji haachi kutapatapa,Wahenga walisema. Imekuwa kawaida kwa CCM, Bwana Kikwete na wana-Propaganda wake kutafuta mchawi wa migomo na migogoro mbalimbali badala ya kutafuta suluhisho la kudumu la ufumbuzi wake. Mtakumbuka matukio kadhaa yalitokea,mfano:
1. Maandamano ya Wanavyuo,kudai mikopo na kuboreshwa mazingira.. Walijitokeza watetezi wengi na makada wa CCM kudai ati ni Chadema wanaohusika. (impact yake- ccm kupoteza kukubalika vyuoni).
2. Ukaja mgomo wj madaktari na crucifiction ya bwana-Daktari Ulimboka. Hapa Kikwete, CCM yake na vibaraka wao TISS waliwatuhumu Chadema kuwa nyuma ya wadai haki zao (madaktari). (Impact yake- CCM kuonekana bulshit katika jamii ya madaktari)!
3. Mgomo wa Walimu.. Hali inavyoelekea,si punde itatamkwa Chadema wapo nyuma ya wadai haki hawa. Natamani sana wataalam wa propaganda wa bwana JMK na chama lake wajitokeze na kuwakemea walim waache kutumiwa na CHADEMA..
My take:- Ni uwezo mdogo wa kiuongozi na utawala alionao kikwete,kukimbilia visingizio kama chaka la kuficha udhaifu.
:- Natoa wito kwa walim kwa kuwa wapo wengi,na wana mtandao mkubwa kila kona ya nchi, basi wawe mashuhuda wa kuwa CHADEMA ndio watetezi wa haki kwani hata CCM wanakiri hivyo,na kubwa zaidi thamani yenu mbele ya chama tawala ni ndogo mno.
Follow Us Here