Re: Zitto: Sijahongwa, ni siasa za urais na hasira za posho!

By
Tumaini Makene
Kimbunga
Mwita Maranya kakwambia nusu ya ukweli unaopaswa kuambiwa, kutokana na namna unavyojenga hoja zako hapa mara kwa mara. Unataka kujua msimamo wa chama juu ya ufisadi wenu wa kitaasisi (institutionalized fraud) kupitia mfumo wa posho? Usisumbuke mkuu, pata nakala ya ilani ya CHADEMA!
Kupinga mfumo wa posho na badala yake kuhitaji uhuisho wa mishahara kwa watumishi wa kada zote, ni kwa CHADEMA ni suala la kisera mkuu. Hivyo kama Mwita Maranya ni mwanachama/mpenzi makini kama ulivyokiri wewe hapa, basi tayari msimamo wake unaujua kupitia msimamo wa chama katika suala hili.
Jifunze kuitafuta na kuisema kweli tupu. Fanyia kazi ushauri wa Mwita Maranya.
Mkuu Tumaini Makene nashukuru umenjibu vyema. Mimi siku zote nimekuwa sifahamu msimamo wa CDM kuhusu posho manake mara wanazikataa mara wanashutumiana. Sasa nisaidie jambo moja: Ni kwamba Zitto alikataa posho ikiwa ni msimamo wake binafsi na wala si msimamo wa CDM? Kwamba msimamo wa CDM ni kuhuisha mishahara na posho.
CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.
Follow Us Here