Kweli Mkuu gfsonwin
manake ukitoe kwa Walimu O'& A-Level, kwa ma lecturers na baadae kwa mwajiri na viongozi kitalegea 'nut' zake.
Ukichukulia kuwa watumiaji wengine wanakuwa na ile "nitakipata lini tena"
Kisiwe kigezo cha mafanikio!. Sifa na Jhudi za mtu ndiyo viwe vigezo!, mh...! lakini kwa viongozi wetu nina wasiwasi.
Mh. Diana Chilolo nae kala rushwa?
Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde
One man's good fortune is another man's misfortune
Hesabu za Tanesco hukaguliwa na Kamati ya Zitto. Suala la misumari na mbao za kichina toka kwa Chief mkwawa zinatakiwa zihojiwe na kamati ya Zitto. Zito hachomoi hapa, ameliibia taifa vya kutosha. Huwa anatumia tactic ya kuwa MBOGO ili aonwe kwa uharaka. Zinaanza kumtokea puani sasa. Lazima azitapike
Wewe WATANABE lazima umetumwa, naona unajaribu sana kumuunganisha January Makamba kwenye hii issue lakini hautafanikiwa.
Wengine someni maelezo haya:
---------------------------------------------------------------------------------------
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ambaye awali alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, alisema ni sahihi kamati hiyo kuvunjwa, kwa sababu imekithiri vitendo vya rushwa.
“Wakati mimi nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, vilikuwapo vitendo vya rushwa, si kwa wajumbe wote ila baadhi yao walikuwa vinara, kutokana na hali hiyo nilivipigia kelele na nimepata shida sana kupambana navyo,” alisema na kuongeza:
“Tuliweka msimamo ndani ya Kamati kwamba vitendo hivyo havikubaliki hata kidogo na ilifikia hatua nilienda kuwashitaki kwa Spika, Anne Makinda, kuhusu tabia ya baadhi ya wajumbe kupokea rushwa na alikubaliana na mimi kisha naye alikemea vitendo hivyo.
“Kusema ukweli tulifanikiwa kuvidhibiti kutokana na msimamo wa pamoja tuliokuwa nao. Baadhi ya wajumbe wa kamati wakalalamika kwanini nimeenda kusema kwa Spika, unajua ni wabunge wachache ndiyo wanaoharibu sifa ya wabunge wengine.
“Kwa hiyo, wananchi wasidhani wajumbe wote wa Kamati ya Nishati na Madini ni wala rushwa, hapana, wanaofanya vitendo hivyo ni wachache kama nilivyosema hapo mwanzo.
“Mimi nataka uchunguzi huo ufanywe haraka na wote wanaohusika wajulikane.”
Katika hatua nyingine, alisema wakati akiwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, kuna baadhi ya watu walikwenda kwa baba yake, Yusuph Makamba kwa ajili ya kumshawishi alegeze msimamo wake.
“Unajua Kamati hii ina ‘deal’ na mambo makubwa na yenye maslahi ya watu, kwa hiyo usipokuwa makini kama kiongozi wa kamati au mjumbe wa kamati, watu wengi watakufuata na kukushawishi kwa fedha,” alisema na kuongeza:
“Mimi nilikuwa na msimamo wangu na ndio maana hata watu wengine wakawa wanaogopa kuanza kunifuata na kunieleza wanayotaka niyafanye.
“Nakumbuka siku moja, kabla ya kwenda katika mdahalo wa Star Tv kuna watu walimfuata mzee Makamba na kutaka anishawishi nisizungumzie mradi mmoja wa umeme ambao ulikuwa na walakini.
“Lakini Mzee Makamba akawajibu kwamba mimi sikai kwake na nimehama tangu nikiwa na umri wa miaka 18, kwa hiyo hana namna yoyote ya kufanya. Kwa hiyo mtu unatakiwa uwe na msimamo na ifikie hatua wakuogope.”
Source: Spika Makinda ang
Follow Us Here