Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

    Report Post
    Page 5 of 5 FirstFirst ... 345
    Results 81 to 97 of 97
    1. #1
      Salary Slip's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2012
      Posts : 1,336
      Rep Power : 690
      Likes Received
      648
      Likes Given
      380

      Default Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Kuibuka kwa kashifa mpya inayomhusu katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini inaacha maswali mengi kuliko majibu. Katibu mkuu huyo anadaiwa kuipa tender kampuni ya PUMA ya kuiuzia IPTL mafuta mazito ya kufua umeme kinyume cha sheria ya manunuzi ya umma. Taarifa zinasema aliingilia uamuzi wa TANESCO wa kuipa kampuni nyingine kazi hiyo kwa kile kinachodaiwa ni tofauti ya bei.

      Hata hivyo gazeti la Nipashe la leo trh 26/07/2012 ambalo pia linapatikana online limetoa taarifa ambayo mimi imenishangaza kuwa waziri mkuu anafanya juhudi za kumtetea katibu mkuu huyo. Taarifa katika gazeti hilo zinasema Waziri Mkuu amekutana na wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya Nishati na Madini akiwasihi waachane na mpango wao wa kutaka katibu mkuu huyo awajibishwe. Swali, kwanini waziri mkuu anamtetea mtu aliyevunja sheria badala ya kumshauri raisi amuwajibishe? Je ametumwa? Na kama ametumwa ni nani kamtuma na kwa faida ya nani?

      Watanzania hebu tutafakari mambo haya yafuatayo alafu tujiulize ni kwanini raisi na waziri mkuu wasijiuzulu au wawajibishwe
      1. Kwanini wizara hii imekuwa kinara wa ufisadi tangu Kikwete aingie madarakani na ni hatua gani za kuridhisha zimechukuliwa mpaka leo?
      2. Hivi viongozi hawa wakuu na bodi ya wakurugenzi wa TANESCO hawakujua kuwa shirika linahujumiwa ktk bei ya mafuta mpaka huyu katibu mkuu mpya bwana Maswi alipoingia ufisini na kama walijua mbona walikaa kimya?Ina maana na wao wanapata taarifa hizi kupitia vyombo vya habari?
      3. Ni hatua gani zilichukuliwa dhidi ya watuhumiwa wa richmond?
      4. Kwanini mamlaka ya uteuzi ambayo ni raisi huwa haichukuia hatua kwa wakati mpaka bunge limshinikize?
      5. Kwanini waziri mkuu anamtetea mtu alievunja sheria badala ya kushauri awajibishwe?
      6. Watendaji wa wizara na TANESCO kutokuwa na hofu ya ufisadi ni nani anawapa kiburi na kuwalinda licha ya mlolongo wa matukio ya wenzao kuwajibishwa?
      7. Je, wanayafanya haya kwa maelekezo ya wakubwa na ndio maana hawana hofu licha ya kujua hatari inayowakabili?
      8. Je, ni kweli wakubwa wao wa kazi wanakuwa hawajui kinachoendelea mpaka taarifa hizi zifike kwenye vyombo vya habari?
      9. Waziri mkuu hata kama hana mamlaka juu yao na labda hapati ushirikiano mbona hajiuzulu?
      10. Mkurugenzi mkuu TANESCO amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi; Je katibu mkuu wa wizara ambae kwa mazingira ya sasa nae ni mtuhumiwa ni sahihi kuendelea kuwepo ofisini mpaka leo? Au mpaka bunge lije juu?Hii sio aibu na fedheha kwa mamlaka ya uteuzi?

      Maswali ni mengi kuliko majibu.Wahusika mjitafakari na muwajibike. Tumechoka kila siku wizara moja tu.

      Unahitajika uchunguzi huru tena wa vyombo vya nje maana hata kwenye richmond uchunguzi wa ndani ulificha baadhi ya taarifa kwa kile kilichodaiwa kuokoa serikali.
      Last edited by Salary Slip; 27th July 2012 at 10:01.
      Maarifa, BAK, Mr Rocky and 7 others like this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #81
      armanisankara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2011
      Posts : 273
      Rep Power : 676
      Likes Received
      43
      Likes Given
      108

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Quote By Salary slip
      Kuibuka kwa kashifa mpya inayomhusu katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini inaacha maswali mengi kuliko majibu. Katibu mkuu huyo anadaiwa kuipa tender kampuni ya PUMA ya kuiuzia IPTL mafuta mazito ya kufua umeme kinyume cha sheria ya manunuzi ya umma. Taarifa zinasema aliingilia uamuzi wa TANESCO wa kuipa kampuni nyingine kazi hiyo kwa kile kinachodaiwa ni tofauti ya bei.

      Hata hivyo gazeti la Nipashe la leo trh 26/07/2012 ambalo pia linapatikana online limetoa taarifa ambayo mimi imenishangaza kuwa waziri mkuu anafanya juhudi za kumtetea katibu mkuu huyo. Taarifa katika gazeti hilo zinasema Waziri Mkuu amekutana na wajumbe wa kamati ya kudumu ya bunge ya Nishati na Madini akiwasihi waachane na mpango wao wa kutaka katibu mkuu huyo awajibishwe. Swali, kwanini waziri mkuu anamtetea mtu aliyevunja sheria badala ya kumshauri raisi amuwajibishe? Je ametumwa? Na kama ametumwa ni nani kamtuma na kwa faida ya nani?

      Watanzania hebu tutafakari mambo haya yafuatayo alafu tujiulize ni kwanini raisi na waziri mkuu wasijiuzulu au wawajibishwe
      1. Kwanini wizara hii imekuwa kinara wa ufisadi tangu Kikwete aingie madarakani na ni hatua gani za kuridhisha zimechukuliwa mpaka leo?
      2. Hivi viongozi hawa wakuu na bodi ya wakurugenzi wa TANESCO hawakujua kuwa shirika linahujumiwa ktk bei ya mafuta mpaka huyu katibu mkuu mpya bwana Maswi alipoingia ufisini na kama walijua mbona walikaa kimya?Ina maana na wao wanapata taarifa hizi kupitia vyombo vya habari?
      3. Ni hatua gani zilichukuliwa dhidi ya watuhumiwa wa richmond?
      4. Kwanini mamlaka ya uteuzi ambayo ni raisi huwa haichukuia hatua kwa wakati mpaka bunge limshinikize?
      5. Kwanini waziri mkuu anamtetea mtu alievunja sheria badala ya kushauri awajibishwe?
      6. Watendaji wa wizara na TANESCO kutokuwa na hofu ya ufisadi ni nani anawapa kiburi na kuwalinda licha ya mlolongo wa matukio ya wenzao kuwajibishwa?
      7. Je, wanayafanya haya kwa maelekezo ya wakubwa na ndio maana hawana hofu licha ya kujua hatari inayowakabili?
      8. Je, ni kweli wakubwa wao wa kazi wanakuwa hawajui kinachoendelea mpaka taarifa hizi zifike kwenye vyombo vya habari?
      9. Waziri mkuu hata kama hana mamlaka juu yao na labda hapati ushirikiano mbona hajiuzulu?
      10. Mkurugenzi mkuu TANESCO amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi; Je katibu mkuu wa wizara ambae kwa mazingira ya sasa nae ni mtuhumiwa ni sahihi kuendelea kuwepo ofisini mpaka leo? Au mpaka bunge lije juu?Hii sio aibu na fedheha kwa mamlaka ya uteuzi?

      Maswali ni mengi kuliko majibu.Wahusika mjitafakari na muwajibike. Tumechoka kila siku wizara moja tu.

      Unahitajika uchunguzi huru tena wa vyombo vya nje maana hata kwenye richmond uchunguzi wa ndani ulificha baadhi ya taarifa kwa kile kilichodaiwa kuokoa serikali.
      Africa hatuna utamaduni wa viongozi wetu kujiuzulu ingekua America au Europe sawa

    4. MI6
      #82
      MI6's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th July 2012
      Posts : 138
      Rep Power : 371
      Likes Received
      16
      Likes Given
      10

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Kama utafikiria hili jambo vizuri utagundua kuna njama kubwa ya kumchafua Maswi kwa kuwa anasimamia ukweli na maslahi ya taifa.
      Daima tz anayefanya mema na haki hapendwi na pia hupuuzwa kwa kila asemalo na afanyaloo..
      rmashauri likes this.

    5. #83
      aminiusiamini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2011
      Posts : 313
      Rep Power : 453
      Likes Received
      72
      Likes Given
      60

      Default

      Ni kweli maswi alifanya right thing kununua mafuta rahisi kuliko yale ya mhando.
      Tatizo la watanzania nini? Yule aliyeokoa hela za walipa kodi au yule aliyefuata sheria na kutia hasara nchi?
      rmashauri likes this.

    6. #84
      Dina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th September 2008
      Location : Ulimwenguni
      Posts : 1,114
      Rep Power : 766
      Likes Received
      291
      Likes Given
      172

      Default

      Quote By Mkandara
      Swali nimeuliza hamkulijibu.. Why Tanesco ndio wanunue mafuta kwa ajili ya IPTL? Kwa nini IPTL wenyewe wasinunue mafuta wanakotaka wao sii lazima Puma. Mafuta is part of their expenses, wayanunue wao kisha wao wawauzie Tanesco umeme.

      Jibu ni moja tu IPTL na mashirika yote ya kuzalisha umeme ni mali za viongozi wetu.. we are all paying for their expenses lakini hamtaki kutazama huko na sasa mnawavutia na bomba la gas watumalize vizuri. Tunagom,bana na Tanesco lakini hatutaki kutazama IPTL na Symbions na mashirika haya yalokuwa ya dharura leo ndio yameshika uchumi wa nchi..
      Kwangu mimi hii ni dawa chungu sana kuimeza. Kuna hoja kubwa sana ya msingi, ni kwa nini wananunuliwa mafuta? Na maana yake ni nini, kuwa ndani ya mikataba hiyo tulijifunga kuwanunulia hayo mafuta for the foreseable future kiasi kwamba hakuna jinsi ya kujichomoa? Na je ndio wote tumekubali upofu wa moja kwa moja kuwa haya makosa hayawezekani kurekebishwa? Au ndio ile kauli ya Pinda kuwa tukifurumua nchi itayumba?

    7. #85
      Salary Slip's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2012
      Posts : 1,336
      Rep Power : 690
      Likes Received
      648
      Likes Given
      380

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Quote By MI6
      Kama utafikiria hili jambo vizuri utagundua kuna njama kubwa ya kumchafua Maswi kwa kuwa anasimamia ukweli na maslahi ya taifa.
      Daima tz anayefanya mema na haki hapendwi na pia hupuuzwa kwa kila asemalo na afanyaloo..
      Binafsi nina kila sababu ya kumuunga mkono Mwasi kwa uamuzi wake ila tunahitaji uchunguzi kwasababau hakuna mwenye uhakika kama Maswi alisukumwa na uzalendo au la?Nimesoma mwanahalisi la trh 25/07/2012 na kukuta mambo ya utata kuhusu huyo Mwasi na uamuzi wake.Kwahiyo hapa kinachohitajika ni tume huru ya uchunguzi?

      kwa upande wa TANESCO hakuna atakaekubali dhuluma hii, nami si waungi mkono hata kidogo.

    8. Miaka 50

    9. #86
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,770
      Rep Power : 7662
      Likes Received
      4929
      Likes Given
      4509

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Quote By Dina
      Kwangu mimi hii ni dawa chungu sana kuimeza. Kuna hoja kubwa sana ya msingi, ni kwa nini wananunuliwa mafuta? Na maana yake ni nini, kuwa ndani ya mikataba hiyo tulijifunga kuwanunulia hayo mafuta for the foreseable future kiasi kwamba hakuna jinsi ya kujichomoa? Na je ndio wote tumekubali upofu wa moja kwa moja kuwa haya makosa hayawezekani kurekebishwa? Au ndio ile kauli ya Pinda kuwa tukifurumua nchi itayumba?
      na kwa muda tu, kama vile tunavyokodisha Limo au costa bus kwa dharura zetu na ilikuwa kwa miaka miwili tu.. Sasa ajabu ni kwamba tumeikata miaka 7 na inaonekana limeisha kuwa jambo la kawaida tu..hakuna tena dharura ila ndio maisha na wabunge wanabishana tu nani kanunua mafuta ghali au rahisi wakati bill ya kila siku ni mabillioni ya fedha na kampuni kama hizi uchwara lini BP ikabadilisha jina kuwa Puma Energy kama sii kamba zao... Tutumie umeme tusitumie IPTL wanalipwa kwa siku na gharama ni zetu.. Sasa janga kubwa kweli liko wapi?..
      Exploration of reality

    10. #87
      rmashauri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Location : Ng'wanza Sukuma
      Posts : 2,860
      Rep Power : 1200
      Likes Received
      350
      Likes Given
      680

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Quote By Salary slip
      Kuibuka kwa kashifa mpya inayomhusu katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini inaacha maswali mengi kuliko majibu. Katibu mkuu huyo anadaiwa kuipa tender kampuni ya PUMA ya kuiuzia IPTL mafuta mazito ya kufua umeme kinyume cha sheria ya manunuzi ya umma. Taarifa zinasema aliingilia uamuzi wa TANESCO wa kuipa kampuni nyingine kazi hiyo kwa kile kinachodaiwa ni tofauti ya bei.......................

      Watanzania hebu tutafakari mambo haya yafuatayo alafu tujiulize ni kwanini raisi na waziri mkuu wasijiuzulu au wawajibishwe
      1. Kwanini wizara hii imekuwa kinara wa ufisadi tangu Kikwete aingie madarakani na ni hatua gani za kuridhisha zimechukuliwa mpaka leo?
      Mkuu ufisadi katika wizara hii haujaanzia kwa Kikwete, tangu enzi za Mkapa sema tu kuwa kipindi cha Mkapa hata wabunge walikuwa hawaruhusiwi kuhoji kama ilivyo leo. Mkapa aliwafunga mdomo wabunge wa CCM. Kumbuka NetGroup Solution, mikataba feki ya madini, mkataba wa IPTL umesainiwa enzi za Mkapa, kujiuzia Kiwira kwa bei sifuri n.k

      Binafsi namtetea Maswi alifanya kitendo cha uzalendo sana, afterall kaipa tenda kampuni ya serikali na kwa bei nafuu tunataka nini zaidi ya hicho jamani?
      Haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote (Mithali 14:34)

    11. #88
      mcubic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2011
      Posts : 350
      Rep Power : 486
      Likes Received
      65
      Likes Given
      53

      Default My short conversation with Hon Zitto In Twitter

      Kufuatia sakata la baadhi ya wabunge kushutumiwa kwamba wamekula mlungula ili wafanikishe kumuwajibisha waziri wa Nishati na madini na Katibu mkuu wa wizara hiyo, kwa kukiuka sheria za manunuzi ya umma, Nilimtweet Mheshimiwa Zitto Kabwe kuhusiana na kadhia hiyo., Ilikuwa hivi

      Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
      Spika ni vema aikubali hoja ya ndg. Vita Kawawa kwamba suala la tuhuma kwa baadhi ya wabunge kuhongwa na #tanesco lijadiliwe mahususi >>

      Me
      @zittokabwe nakufuatilia sana mheshimiwa,, but kama vile utoe kauli maana these statement they meant u....tunapata shida ss wafuas wako


      Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
      @Me usiwe mfuasi wangu. Fuata 'principles' ninazoamini. 'Justice' ndio msingi hapa. Sitatolea kauli tuhuma za kubumbabumba.


      Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
      >> kwenye mjadala mahususi ushahidi utatolewa na watuhumiwa kujieleza. Vinginevyo hizi ni siasa tu zenye malengo Maalumu dhidi ya mtu fulani


      Mheshimiwa Zitto aliendelea kutweet kwa kumquote Nguli wa mashahiri wa kiswahili Shabani Robert akionesha kushikilia msimamo wa yale anayoaamini.


      Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
      Shabaan Robert alisema, "msema kweli huchukiwa na rafiki zake, sitaona wivu juu ya wale wapendwao na marafiki zao siku zote,">>
      Zitto Zuberi Kabwe@zittokabwe
      >> 'siwezi kuikana kweli kwa kuchelewa upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga.

    12. #89
      Mahesabu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2008
      Location : manzese
      Posts : 3,034
      Rep Power : 1318
      Likes Received
      218
      Likes Given
      677

      Default Re: My little conservation with Hon Zitto In Twitter

      KONSAVESHENI au KONVAZESHEN????
      mcubic likes this.

    13. #90
      rugumisa's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th May 2012
      Posts : 38
      Rep Power : 358
      Likes Received
      8
      Likes Given
      12

      Default Re: My little conservation with Hon Zitto In Twitter

      zitto ni fisadi.wapambe wake mteteeni tu.

    14. #91
      Mjuni Lwambo's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 25th April 2012
      Location : Lyamidati-Shinyanga.
      Posts : 1,678
      Rep Power : 691
      Likes Received
      437
      Likes Given
      365

      Default Huyu siyo kigwangala ninayemfahamu

      Jana nilipigwa na butwaa alipoinuka mbunge wangu kuchangia ktk wizara ya nishati na madini. kwanza, Mh. Kigwangala kabla hajasema lolote alitamka kuunga mkono hoja zaidi ya mara moja, hili si la kushangaza kwa kuwa imekuwa ni pai ya wabunge wa chama chake kuunga mkono kitu chochote tu bora liende. Kilichonishangaza mimi kwa Mbunge wetu huyu wa Nzega ni msisitizo aliokuwa nao ktkt kuunga mkono hoja. alirudiarudia kuunga mkono na kisha kuanza kumwaga sifa kwa mawaziri husika. Mimi binafsi pamoja na wananzega wenzangu tumesikitishwa na mchango huo wa mwakilishi wetu. Kwa muda sasa tangu tumchague tumekuwa na matumaini mno na mheshimiwa Hamisi. Amekuwa mstari wa mbele kutetea hasa kuhusu mzozo wa kampuni ya kigeni RESOLUTE inayochimba madini ktk jimbo letu. Je? mh. anataka kutuambia kuwa sasa mgogoro huo umekwisha?. Mh., ktk suala hili ulijitoa mhanga kutetea wanyonge hadi ikafika kipindi ukasumbuliwa na polisi kama mtoto mdogo sasa imekuwaje?. ni nini kimekubadilisha mpaka kuchangia michango butu namna hiyo bungeni?. unasema kiwango wanachotoa wachimba madini wa kigeni kwamba kimeongezeka kutoka aslimia tatu mpaka kufikia nne, Je? hili nalo ni jambo la kujivunia wakati nchi zingine wanalipa nusu kwa nusu. Kwa kweli sifichi aliyechangia jana tarehe 27/07/2012 ktk bajeti na wizara ya nishati na madini siyo KIGWANGALA ninae mfahamu.

    15. #92
      Chief's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2006
      Posts : 955
      Rep Power : 854
      Likes Received
      96
      Likes Given
      229

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Quote By Bantugbro
      Mkuu Mkandara, kwa jinsi ninavyoelewa ni kwamba IPTL iko chini ya RITA (mufilisi) kutokana na kesi iliyofungiliwa na TANESCO miaka kama 3-4 iliyopita. Jaji wa hiyo kesi alikubali kwamba kwa kuwa IPTL iko chini ya mfilisi wakati mitambo yao bado ni mizima hivo basi haina budi TANESCO waendelee kuitumia hiyo mitambo kuzalisha umeme lakini mafuta wanunue wao. Kumbuka pia kipindi hicho kuna baadhi ya wabunge wa CDM walioshauri kuwa serikali iitaifishe kabisa hiyo mitambo.
      Ninavyofahamu, tangu siku ya kwanza, mkataba unasema serikali ndiyo inunue mafuta. Ndio maana siku za nyuma serikali ilikuwa inahaha kubadili mitambo hiyo badala ya kutumia mafuta itumie gasi ya songosongo ili kupunguza gharama. Sijui huu mpango umekufia wapi..


    16. #93
      Chief's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2006
      Posts : 955
      Rep Power : 854
      Likes Received
      96
      Likes Given
      229

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Quote By Salary slip
      Soma vizuri acha kukurupuka.
      Nimekusoma vizuri. Naamimi nafahamu kiswahili


    17. #94
      George Smiley's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th October 2011
      Posts : 374
      Rep Power : 456
      Likes Received
      184
      Likes Given
      108

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      hii nayo itapita

    18. #95
      republicoftabora's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th May 2012
      Posts : 57
      Rep Power : 365
      Likes Received
      14
      Likes Given
      10

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Ishapita

    19. #96
      Vijijini Lawama's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 117
      Rep Power : 383
      Likes Received
      38
      Likes Given
      11

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Ngoja nitulie kwanza ndo nisome huu uzi. tuliishaongea sana lakini du serikali inapoongozwa na watu wasojali ndo hivo. wait a bit i shall come sometimes to read and comment..........

    20. #97
      Mwanaharakatihuru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2012
      Posts : 474
      Rep Power : 0
      Likes Received
      114
      Likes Given
      14

      Default Re: Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

      Nashawishika kusema hakuna aisiye fisadi viwango tu vinatofautiana hata kujamiikaforum wakati wa muda wa kazi ufisadi tu zitto anaweza akawa fisadi ngojea list ya membe

    Page 5 of 5 FirstFirst ... 345

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...