Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

    Report Post
    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast
    Results 21 to 40 of 52
    1. #1
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 719
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano



      Na Salma Said,


      Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi kwa upande wa Zanzibar, Mansour Yusuf Himidi, amesema atasimamia mtazamo wake kuhusu muundo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unaofaa hata kama itapelekea kuvuliwa uwanachama.

      Mwandishi wa DW Zanzibar, Salma Said, amefanya mahojiano na Mansour Yussuf Himidi, ambaye ni waziri katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na pia Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuhusiana na kauli za Katibu Mwenezi wa chama hicho, Nape Nnauye, na wajumbe wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi, kumtaka arudishe kadi ikiwa hakubaliani na sera ya sasa ya serikali mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


      Habari hii kwa kirefu na audio clip, soma post HII


      Na Mwinyi Sadallah | 6th August 2012 | Nipashe


      Waziri asiye na Wizara Maalum wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Mansoor Yussuf Himid, amependekeza kuwepo na Muungano wa mkataba kati ya Tanzania bara na Zanzibar.

      Mansoor alitoa matamshi hayo wakati akichangia hoja kwenye semina ya mjadala wa mchakato wa ukusanyaji maaoni ya uundwaji wa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muugano Tanzania uliofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani Zanzibar.

      Alisema ipo haja ya kuwa na Muungano wa mkataba ili kuondokana na malalamiko mengi ambayo yanalalamikiwa katika Muungano wa sasa.

      Katika maelezo yake, Mansoor alisema bado ataendelea kuwa muumini wa mfumo wa serikali mbili chini ya mkataba na si kama ilivyo sasa ili kuipa fursa zaidi Zanzibar kujijenga na kujitegemea kiuchumi.

      Alisema si dhambi Zanzibar na Tanganyika chini ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zote zikawa na viti viwili katika Umoja wa Mataifa (UN).

      Alieleza kuwa kuna baadhi ya viongozi kwa malengo yao binafsi wanajaribu kuwajengea hofu wenzao na kuwazuia kutoa maoni yao kwa upana kama raia huru kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

      Aliongeza kuwa hajawahi hata mara moja kukataa Muungano, ila mara zote amekuwa akihimiza mabadiliko ya kimfumo katika Muungano huo na kwamba anaamini kuwa kufanya hivyo si uadui wala usaliti.

      “Hata NEC ya CCM ilipoanzisha mchakato wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kulienezwa hofu kila mahali, nashukuru tumefanikiwa kuunda GNU, sasa imesimama na kusomga mbele, kila mmoja anaona fahari, faida na tija ya jambo hilo,” alisema.

      Hata hivyo, kauli ya Mansoour ya kutaka Muungano wa mkataba na suala zima la kila upande kuwa na kiti UN, inamaanisha kwamba Zanzibar inapaswa kuwa huru.

      Alisema awali suala la kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa lilipoibuliwa na Rais Jakaya Kikwete, kulikuwa na mtazamo hasi kwa baadhi ya wanasiasa waliokuwa wakiamini kuwa kuundwa kwa GNU kungetoa mwanya wa kuwarejesha watawala waliopinduliwa Januari 12,mwaka 1964 na kulipizana visasi.

      “Hata wenzetu wa CUF kabla ya GNU, walikuwa wakipinga kila kitu kizuri cha SMZ, baada ya kushirikishwa serikalini hata yale waliyokuwa wakiyapinga wakati ule, sasa wanayaunga mkono, kuyasimamia na kuyashangilia,” alisema Waziri Mansoor.

      Akizungumzia umuhimu wa dhana ya Muungano alisema hapendi uvunjike na kwamba mara zote amekuwa akitaka hoja na haja ya Muungano huo kufanyiwa marekebisho ya msingi na kuwa chini ya mkataba.

      Waziri huyo wa SMZ ambaye pia ni Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki kwa tiketi ya CCM, aliongeza kuwa ikiwa maoni yake yatachukuliwa na chama chake kuwa ametenda dhambi, atakuwa tayari kukabiliana na adhabu yoyote atakayopewa.

      “Niko tayari kuadhibiwa kwa kutoa maoni ninayoyaamini kama ni ya kujenga, nafikiri nimetumia haki yangu ya Kikatiba na kiraia, nataka Zanzibar iwe na nyenzo zake za kiuchumi kwa maendeleo ya watu wake, sijali na wala sitawasikiliza wanaoeneza maneno ya uzushi,” aliongeza Waziri Mansoor.

      Alisema kila Mzanzibari anayo haki ya kutoa maoni yake bila mtu mwingine kuzuia utashi wake huku akisisitiza kuwa hiyo ndiyo demokrasia anayoijua yeye ndani ya chama chake.

      Hata hivyo, aliipongeza CCM kuwa ina mwelekeo, viongozi wake wana uwezo wa kuvumiliana na kupima mabadiliko ya nyakati.

      “Ninakiheshimu sana chama changu, ninakipenda, ndicho kilichonilea, bado ni imara sana, kuna watu wanataka kukichafua, kufika kwetu hapa ni kutokana na utashi wa viongozi wake kuwa na dira na uvumilivu,” alisema.

      TUME YA WARIOBA YATUPIWA LAWAMA

      Tume ya kukusanya maoni ya Katiba inayoongozwa na ya Jaji Joseph Warioba, imetupiwa lawama kwa kushindwa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya baadhi ya viongozi wa CCM wanaowatisha wanachama wasitoe maoni ambayo yanatofautiana na msimamo wa chama hicho.

      Waziri wa Miundombinu na Mwasiliano wa Zanzibar, Rashid Seif Suleiman, alisema tume hiyo ina kila sababu za kuchukuliwa hatua za kisheria kwa sababu wanachofanya ni kosa chini ya Sheria ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

      Alisema kitendo hicho kinapora uhuru wa wananchi kutoa maoni juu ya aina ya mfumo wa Muungano wanaoutaka.

      Seif alikuwa anachangia mada juu ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyowasilishwa katika semina ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Aboubakar Khamis Bakary, mjini hapa.

      “Nadhani Sheria ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba inakataza mtu au taasisi kumzuia mtu mwingine kutoa maoni yake au kumlazimisha aseme anavyotaka yeye, sasa hawa viongozi wa CCM wanaotaka kuwanyang’anya kadi wawakilishi wao wanakiuka sheria hii,” alisema Waziri Seif.

      Alisema ataendelea kuishangaa Tume ikiwa itaendelea kushindwa kukemea au kuwachukulia hatua wale wote wanaotoa vitisho dhidi ya watu wenye mitazamo tofauti na ya CCM katika Katiba mpya.

      Seif alisema kila mtu yuko huru kutoa maoni yake mbele ya tume hiyo na kwamba si haki kwa mtu au chama chochote cha siasa kuwakataza wanachama wake kutoa maoni yanayogusa mitazamo yao binafsi tofauti na ya vyama vyao.

      Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Zanzibar, Asha Bakar Makame, aliwataka viongozi wenzake ndani ya CCM kutowatisha wanachama wenye maoni tofauti na chama hicho katika suala la mabadiliko ya Katiba.

      Asha alisema ni jambo la kushangaza katika ukuaji wa demokrasia wanapojitokeza watu kuwazuia wengine kuwa na mawazo huru kwenye mchakato wa kupata Katiba mpya.

      "Jamani tusitishane, kama CCM kila mtu ni CCM hapa hakuna mtu asiyenijua msimamo wangu kuhusu Chama, ninakipenda na nitakitetea, lakini si vizuri kuanza kutishana kwa kuambiana huyu hivi huyu vile, haifai jamani,” alisema.

      Asha alikumbusha kwamba wakati wa kutafuta maridhiano ya kisiasa Zanzibar, wapo wana-CCM na viongozi waliopinga suala hilo, lakini hakuna mtu aliyeadhibiwa kwa kuvuliwa uanachama na kuwataka viongozi kuwavumilia wanachama na wafuasi wengine wa CCM katika suala zima la maoni tofauti kuhusu Muungano.

      Mwakilishi wa Kwamtipura, Hamza Hassan Juma, alisema Rais Kikwete, hajazuia kutoa maoni tofauti na msimamo wa CCM juu ya suala hilo na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano huo na kuwa wavumilivu.

      Hamza aliongeza kwamba CCM bado ni bora, hivyo kisiogope mageuzi kama ilivyotokea wakati wa mageuzi kutoka demokrasia ya chama kimoja kuingia mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992.

      Mzenji73 and Daudi Mchambuzi like this.

    2. RukaaJuu Final

    3. #21
      Joseph's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd August 2007
      Location : Zanzibar
      Posts : 2,701
      Rep Power : 1148
      Likes Received
      698
      Likes Given
      423

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Kama CCM walishindwa kuvuana magamba basi hata hili litapita tu kama kawaida yao hivyo hapa hakuna jipya.
      You can never have someone praise you,nor will anyone condemn you,never in the past,not at present and never will be in the future.

    4. #22
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 719
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Vigogo wa wasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar sasa wasanifiwa na Nape mtu asaijuwa Zanzibar historia yake ndewe wala shikio Inaoneka na Muungano utamalizwa na kuvunjwa na wana wa Mapinduzi.

    5. #23
      Mzenji73's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th January 2009
      Posts : 204
      Rep Power : 823
      Likes Received
      33
      Likes Given
      53

      Default Re: Mahojiano Mh Mansour/Nape

      Quote By Nnauye Jr
      Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
      UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
      "Wallahi inanishangaza! wataka kutwambia 'platforms' zote alizotumia Mh Mansour kuelezea msimamo wake (na kwa kweli msimamo wa waZnz wengi wetu) ni kuropoka barabarani! ama kweli hizi ni dharau za mwisho! yaani pahala patakatifu kwenu nyie ccm ni huko dodoma tu? ..... nashangazwa na uoni wako hapa Mh. hivi hujui nani anaelazimisha huu muungano?? salaale! kwa uchache tu, hukumbuki 'hali ya hewa kuchafuka Znz, enzi za Mh Jumbe? ..... hukijui kipi kilowafukuzisha CCM maalim Seif na wenzake ..... hukumbuki vipi ajenda tu iloanzishwa bungeni ya G55, ile ya kudai Tanganyika? na mengineo mengi ....

      Mh Muungano mnaulazimisha nyinyi viongozi wa CCM wa Tanganyika mkishirikiana na vibaraka wenu wachache waliopo hapa Znz, sisi tulio wengi hatuutaki huu muungano, na kwa kweli ushafika wakati hamna njia tena ya 'kuulinda kwa nguvu zenu zote' ..... hauishi tena katika nyoyo zetu, kama ni muungano uwe wa kimkataba, habari ndio hio.

      Mtuwacheee Tupumueeeeeeeeeee! "

    6. #24
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,726
      Rep Power : 2267
      Likes Received
      601
      Likes Given
      783

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Simple life is healthier than egoism.

    7. #25
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1844
      Likes Received
      593
      Likes Given
      413

      Default Re: Mahojiano Mh Mansour/Nape

      Quote By Nnauye Jr
      Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
      UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
      Tunagombea Muungano barabarani kwa faida ya nani..... tumeletewa Tume sema kila kitu unachokitaka na usichokitaka kuhusu Muungano.

      Hapa limejitokeza kundi kama wasemaji wa wananchi kuhusu hatima ya Muungano.

    8. Miaka 50

    9. #26
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 719
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default Mansoor Yussuf Himid: Msimamo wangu juu ya Muungano hautabadilika



      Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Mansoor Yussuf Himid amesema potelea mbali kama ni kufukuzwa katika chama chake cha CCM lakini hatasita kuitetea Zanzibar

      Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Mansoor Yussuf Himid amesema yupo tayari kunyanganywa kadi ya chama hicho lakini hataregeza msimamo wake juu ya kuitetea Zanzibar katika Muungano. Kauli ya Mansoor imekuja siku chache baada ya chama hicho wilaya ya mjini kutoa maamuzi ya kuwataka viongozi wenye kupingana na msimamo wa chama kurejesha kadi za chama hicho au kuacha tabia hiyo mra moja.

      Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Radio ya Ujerumani (DW) jana Mansoor alisema kamwe hawezi kuogopa vitisho vinavyotolewa na watu wenye kujipa madaraka na udikteta ambao hawataki mabadiliko wala mawazo tofauti. Mansoor aliahidi kuendelea na msimamo wake katika kudai mabadiliko katika muundo wa Muungano na kusema kwamba msimamo wake hautabadilika licha ya vitisho vya baadhi ya Viongozi wa Chama hicho.

      “Nimesema hayo tokea muda mrefu chama hiki kimetukuka na kina heshima na maadili yake ni baadhi ya watu wanataka kutuziba midomo lakini Mimi sijasema leo nimesema tokea 2008-2009 juu ya msimamo wangu juu ya mfumo wa muungano na leo naendelea kusema tena hata ikipidi kunyanynganywa kadi mimi narejea tena kuwa mfumo huu wa serikali mbili sikubaliani nao na nitaendelea kusema ahivyo hivyo siwezi kubadilisha maoni yangu leo baada ya kuwa na msimamo miaka yote hayo” alisisitiza Himid ambaye ni Mjumbe wa NEC.

      Aidha alisema Chama Cha Mapinduzi wilaya ya mjini hakina mamlaka ya kuitisha kikao na kutoa maamuzi kama hayo ambapo alisema ni watu wachache wenye nia ya kutaka kuwanyamazisha watu wenye maoni tofauti na wao. “CCM wilaya ya mjini hawana mamlaka hayo, lakini pia hawana uwezo wa kutunyamazisha kwani CCM haijakataza wanachama wake kuwa na mawazo tofauti sasa nashangaa hao wanaosema sisi tumekiuka msimamo wa Chama ni msimamo upi maana mchakato wa katiba upo huru na kila mtu anatakiwa kutoa maoni yake” Alisema Himid.

      Katika kuonesha kukasirika kwake na uamuzi huo wa kutaka kuwanyanganya kazi, Muweka Hazina huyo wa CCM alisema kwamba ni jambo la aibu kwa CCM Wilaya ya Mjini kufanya vitendo vya kibaguzi na vya udikteta kutaka kuwafunga midomo watu wasitoe maoni yao. Alisema hakuna makosa kwa wana CCM kuwa na mawazo tofauti kwani kila mmoja ana haki ya kutoa maoni na kueleza msimamo wake na tabia ya kikundi cha watu kujiona wao ndio wenye mamlaka na wenye chama ni kosa na halipaswi kuachiwa.
      “Hao ni ni wabaguzi hawataki watu waseme ukisema unaonekana msaliti, hao ni watu wenye mawazo mgando hawataki kusikiliza fikra nyengine wanataka wanachosema wao ndio kiwe hicho hicho hilo haliwezekani na hatutakubali” Alisisitiza.

      Hata hivyo alisema zama za kusema tunakwenda na fikra za mwneyekiti umepitwa na wakati na sasa jamii kubwa inakwenda na vijana amabo wanataka mabadiliko nchini hivyo aliwashauri wana CCM kuwaachia watu watoe maoni yao kwa uhuru kwani katiba tayari imetoa uhuru huo hivyo CCM hawawezi kuwa juu ya sheria.

      “Hii nchi sio ya CCM peke yake hapa kuna CUF kuna Chadema na pia kuna vyama vyengine lakini wengine hawana hata vyama sasa hatuwezi kuendelea na watu ambao hawataki kuwa na mabadiliko wenye mawazo mgando …zama hizo zimeshapitwa na wakati wakati wa kwenda na fikra za mwenyekiti umekwisha” alisema Mansoor ambaye ni Waziri aisye na wizara maalumu.

      Mmweka Hazina huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, alisema kitendo kilichofanywa cha kutishiwa kunyanganywa kadi ya CCM na baadhi ya viongozi hao ni cha fedheha na kimekitia aibu Chama cha CCM mbele ya wana jamii.
      Himid alisema yeye ametokana na mifupa ya Chama cha Afro Shiraz (ASP) hivyo suala la kuwepo kwa dhana ya wanachama wa madaraja ndani ya CCM halipo kwa kuwa Chama hicho kinaheshimu misingi ya haki za binadamu na kuwataka wenye kudhani kwamba wao ndio wana mamalaka zaidi kuliko wengine waache tabia hiyo.

      Hivi karibuni chama cha mapinduzi CCM wilaya ya mjini kilitoa tamko la kuwataka wajumbe wa baraza la wawakilishi, akiwemo Muweka Hazina wa CCM Zanzibar, Mansoour na makamo mwenyekiti wa CCM Zanzibar kuacha mara moja kukiuka maadili ya chama chao kwa kuwa na mtazamo hasi dhidi ya muungano. Jana akihojiwa na DW, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisikika akisema kwamba viongozi wanaokwenda kinyume na madili ya chama chao watatakiwa kwenda kujieleza katika vikao na iwapo watathibitika wamekwenda kinyume basi watanyanganywa kazi au kufukuzwa.

      Nape alisema mwana yoyote CCM hawezi kwenda kinyume na maadili ya chama chake na iwapo atakuwa na msimamo mwengine usiokuwa wa chama hicho basi atatakiwa kuwasilisha maoni yake ndani ya vikao na iwapo maoni hayo wajumbe hawatayaridhia basi atalazimika kurejesha kazi ya chama hicho iwapo yeye hatokubaliana na msimamo wa kikao. Akijibu suala hilo Himid alisema kuwa Nape hawezi kugawa matabaka wanachama wa CCM, wale wa Tanzania Bara na Zanzibar kwani wote ni wanachama wanahaki sawa mbele ya sheria na katika CCM.

      “Sisi Watanzania hatuna uhuru, yeye amegawa kwa utabaka, sisi ni watu wazima tuna haki na uhuru, Nape hawezi kutwambia sisi watu wazima kwamba tukasema anayotaka yeye, ule wakati wa ndio Mwenyekiti haupo kila mtu ana haki yake kutoa maoni na hata Tume ya Jaji Warioba inasema hivyo” Alisema Himid. Na kuongeza kwamba. “Mimi naichukulia kuwa hii ni njama ya kutaka kuwaziba midomo Wazanzibari, hatujakiuka miongozo wala sheria tutaendelea kusema kutaka mabadiliko ya muundo wa Muungano, hii nchi asilimia kubwa ni vijana na vijana wanataka mabadiliko na hilo haliwezi kukwepwa” Aliongeza.

      Licha ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa mbali ya kueleza msimamo wa Chama hicho, lakini amesema wanachama wake hawafungiki kuwa na maoni na mitazamo tofauti katika mchakato wa katiba mpya.

      “Mie nadhani kuna baadhi ya watu wana fikra za udikteta, haiwezekani twende kwenye kutoa maoni tukasema tunataka Serikali mbili kama ilivyosema CCM sisi ni watu wazima tuna haki zetu na tusichaguliwe la kusema na kwa nini tuzibwe au tufungwe midogo?” Alihoji.

      Mansoor amesema msimamo wake kuhusu mfumo wa muundo wa Muungano utabakia kama ulivyo kutaka kuwepo kwa mabadiliko makubwa katika muundo huo kwani kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko kutoka Zanzibar ambayo hayapatiwi ufumbuzi kutokana na kuwepo kwa muundo dhaifu wa Muungano. Alisema hakuna mtu mwenye nia ya kuvunja Muungano, lakini ni lazima kukawepo kwa Muungano wenye maslahi ambayo hautakuwa na kero na ndio maana wamekuwa wakitoa maoni ya kutaka mabadiliko ya muundo na sio kuvunja.

      “Mimi pia nakubali muungano una manufaa, lakini sikubaliani na mfumo wa Muungano na ndio maana tunasema kwa mfumo huu sebu(sitaki)” alisema Mweka Hazina wa CCM Zanzibar.

      Tokea kuanza kwa machakato wa katiba wazanzibari wengin wamekuwa na maoni ya aina mbili tofauti ambapo wapo wengine wakitaka muungano kama ulivyo uendelee na wengine wakisema wanataka muungano wa serikali mbili zenye mamlaka kamili na zenye kuirejeshea Zanzibar ya kuingia mikataba na nchi za nje na baadae kuwe na mkataba.


      Kwa kusikiliza mahojiano ya Mhe: Mansoor Bonyeza hapa.

    10. #27
      Nambombe's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th May 2012
      Posts : 155
      Rep Power : 383
      Likes Received
      12
      Likes Given
      6

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By Mtu wa Pwani
      kama uamsho wazanzibari sote ni uamsho. mmemsikia Nassor Moyo, waziri wa sheria wa Jamhuri ya mungano wa mwanzo, mama Fatma Karume mke wa muasisi wa dola ya zanzibar, makamo wa CCM zanzibar na Rais mstaafu Karume, mwanasheria mkuu zanzibar, DPP zanzibar, wawakilishi zanzibar na wengineo.

      kwa sasa hakuna anaeweza kuzuia nguvu ya wimbi la mabadiliko


      wimbo ni mmoja tu kwa sote:

      "tunataka nchi yetu sasa tumechoka "
      Wa tanganyika mbona munakuwa wanyonge hivyo, jamani watanganyika wenzangu nielezeni faida ambayo sisi tunapata kwenye huu muungano

    11. #28
      ngonyani's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th October 2011
      Posts : 11
      Rep Power : 386
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Tuachiwe...tupumuwe

    12. #29
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,659
      Rep Power : 717
      Likes Received
      291
      Likes Given
      36

      Default re: Mansoor Yussuf Himid: Msimamo wangu juu ya Muungano hautabadilika

      Hivi ninani akisema anaweza kusikilizwa kama si wananchi? Nape na kundi lake kutisha watu wenye mawazo tofauti na chama chao itakimaliza ccm kwa kasi ya ajabu, huu si wakati wa kutisha watu, Nampongeza waziri alie heshimu hisia zake mwenyewe,

    13. #30
      Makupa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 2,176
      Rep Power : 810
      Likes Received
      251
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Nnauye Jr
      Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
      UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
      Mkuu wangu wa kazi kichama , wewe huwa mawazo yako unawasilisha wapi, kwanini unalizimisha binadamu mwenzakao aamini unachokiamini wewe

    14. Deo
      #31
      Deo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th November 2008
      Posts : 521
      Rep Power : 641
      Likes Received
      89
      Likes Given
      7

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Ashakum si matusi; Wanaopenda sana kuvunja muungano ni wenye asili ya uarabu na uarabu koko, hiyo wanafanya kwa maslahi mapana zaidi. Zaidi wengi wao wanatumika na zaidi wanawatumia nywele ngumu kuwa makuwadi wao hasa kwa kuangalia kipengele cha dini. Walio, na waliokuwa kwenye madaraka pia wana nia ya kuuvunja muungano.

      Kwa kifupi, maslahi makubwa hasa kwa nchi za kiarabu ni ya kisiasa, magharibi kama ipo ni kiuchumi, na kwa wazanzibari wengi wanaotaka kuvunja hawajui lakini kwa tabaka la hapo juu ni uchumi uchwara, kiaiasa na kidini.

      Historia ni mwalimu mzuri; ingefaa sana wazanzibari wakafundishwa historia yao ya ukweli na siyo ya kupotosha au kuipaka sukari. Tangu kabla ya mwarabu, baada ya mwarabu, kufika kwa wazungu na uhuru, mapinduzi na muungano.

      Muungano ukivunjika kama alivyosema mzee kifimbo, wengi wa wazanzibari nyewele ngumu watakuwa watumwa, na watawatumikia waarabu na waarabu koko.

      Mungu isaidie Zanzibar

    15. #32
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,457
      Rep Power : 1189
      Likes Received
      1434
      Likes Given
      937

      Default Re: Mahojiano Mh Mansour/Nape

      Quote By Nnauye Jr
      Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
      UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
      Mimi huwa nadhania ndiyo sina maslahi na Muungano, kumbe ni wengi wanamtazao kama wangu, to me hata Muungano ukifa kesho sina cha kupoteza wala cha kuongeza. Nijuavyo mimi hata wanaotaka muungano usife hawataki tuu kwamba Historia iandikwe kwamba muungano ulikufa wakiwa wao madarakani lakini in reality hakuna Mtu mwenye shida na Muungano.
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    16. #33
      Kijana Msomali's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th May 2012
      Posts : 92
      Rep Power : 1361
      Likes Received
      68
      Likes Given
      42

      Default Re: Mahojiano Mh Mansour/Nape

      Quote By Nnauye Jr
      Kuna watu wamefilisika kimawazo wanaoeneza upuuzi kuwa kuna watu wanalazimisha na kung'ang'ania Muungano! Ili iweje? Ili tupate nini?!? Its a matter of nguvu ya hoja sio hoja ya nguvu!
      UKISIKILIZA VIZURI NILICHOSEMA, UPO UTARATIBU WA KUFIKISHA MAWAZO KWA KIONGOZI WA CCM, SIO KUROPOKA BARABARANI! LAKINI SWALI LANGU KUBWA HAPA....... NANI ANALAZIMISHA MUUNGANO? ILI APATE NINI?NASEMA WANAOSAMBAZA MAWAZO HAYO WAMEFILISIKA KIMAWAZO TENA SANA!
      Well Said Nnauye Jr lakini katiba ya Jamhuri Muungano wa Tanzania haimzuii raia yeyote kutoa maoni ama fikra zake ikiwa TU hayo maoni yake ama hizo fikra zake hazivunji sheria za nchi ama haki za mtu mwingine. Kwa nini viongozi wengi wanaogopa kuujadili muungano hata kwa constructive way?

    17. #34
      Kijana Msomali's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th May 2012
      Posts : 92
      Rep Power : 1361
      Likes Received
      68
      Likes Given
      42

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By Deo
      Ashakum si matusi; Wanaopenda sana kuvunja muungano ni wenye asili ya uarabu na uarabu koko, hiyo wanafanya kwa maslahi mapana zaidi. Zaidi wengi wao wanatumika na zaidi wanawatumia nywele ngumu kuwa makuwadi wao hasa kwa kuangalia kipengele cha dini. Walio, na waliokuwa kwenye madaraka pia wana nia ya kuuvunja muungano.

      Kwa kifupi, maslahi makubwa hasa kwa nchi za kiarabu ni ya kisiasa, magharibi kama ipo ni kiuchumi, na kwa wazanzibari wengi wanaotaka kuvunja hawajui lakini kwa tabaka la hapo juu ni uchumi uchwara, kiaiasa na kidini.

      Historia ni mwalimu mzuri; ingefaa sana wazanzibari wakafundishwa historia yao ya ukweli na siyo ya kupotosha au kuipaka sukari. Tangu kabla ya mwarabu, baada ya mwarabu, kufika kwa wazungu na uhuru, mapinduzi na muungano.

      Muungano ukivunjika kama alivyosema mzee kifimbo, wengi wa wazanzibari nyewele ngumu watakuwa watumwa, na watawatumikia waarabu na waarabu koko.

      Mungu isaidie Zanzibar

      Deo Mimi ni mfuasi mzuri wa Muungano, ila hayo mawazo yako yamekaa kibaguzi sana, ungetumia njia nyingine kuwasilisha mawazo yako natumai hadhira ingekuelewa vizuri. Ni dhambi kubwa kujaribu kuulazimisha ulimwengu kuwa wanaopinga muungano ni waarabu.

    18. Deo
      #35
      Deo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th November 2008
      Posts : 521
      Rep Power : 641
      Likes Received
      89
      Likes Given
      7

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By Kijana Msomali
      Deo Mimi ni mfuasi mzuri wa Muungano, ila hayo mawazo yako yamekaa kibaguzi sana, ungetumia njia nyingine kuwasilisha mawazo yako natumai hadhira ingekuelewa vizuri. Ni dhambi kubwa kujaribu kuulazimisha ulimwengu kuwa wanaopinga muungano ni waarabu.

      Nashukuru
      , Kijana Msomali, kwa kweli siyo niayangu kuweka mawazo yangu katika taswira ya kibaguzi, lakini nimeandika hivyo kwa kutazama namna mambo yanavyokwenda.

      Pia ninajua historia kamili ya Zanzibar, hivyo natambua nani youpo kazini na tangu lini. Ina uma sana pale ambapo watu wengi wanaingizwa kwenye mkumbo kwa kutokufahamu kwao na kwa makusudi, na hasa viongozi wao wanapo fanya shughuli zao kwa maslahi binafsi.

      Kumbuka historia ya Zanzibar imepotoshwa kwa makusudi.
      Utawala wa Mkapa ulimaliza masomo yanayoweza vijana kujua historia yao, na kuwajengea uzalendo na hii ilifanywa kwa makusudi, na lengo nikutufanya watumwa kwenye nchi yetu. Na ndivyo ilivyo sasa hapa Tanzania.
      Kwa kila Mzalendo lazima atapenda sana Muungano.

      Labda asielewe manufaa yake

    19. #36
      zethumb's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 286
      Rep Power : 499
      Likes Received
      38
      Likes Given
      85

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By Mzenji73
      MUUNGANO WA SERIKALI MBILI MWISHO CHUMBE 2015 – WAZANZIBARI

      NIMESIKILIZA kwa makini sana maelezo ya Mhe Mansour Yussuf Himid na maelezo ya Nape Mnauye, nikarudia kusikiliza tena kwa mara ya pili ili kuweza kujiridhisha na kufahamu kwa undani hoja za kila mmoja. Hata hivyo, mawazo ya Nape, yamepitwa na wakati.


      Kwa ufupi nimegundua kwamba viongozi wa CCM kwa upande wa Bara, yaani Tanganyika bado wanakasumba ile ile ya Nyerere, kutaka kuimeza Zanzibar. Kwa kauli ya Nape, si kweli kuwa Chama chao kina wigo wa kweli wa Demokrasia na uhuru wa kutoa maoni.


      Aidha, nimegundua kuwa wanaamini Zanzibar ni mali yao waliyorithi kutoka kwa Nyerere na kusahau wajibu wao wa kuitetea Tanganyika yao na kuimarisha zaidi utawala wa Taifa la Tanganyika, kama wanavyofanya baadhi ya viongozi wa CCM wanaoumizwa na Zanzibar.


      Nape, kauli yake iko wazi katika kudai kuendeleza kuitawala Zanzibar, ikibidi hata kwa mabavu na nguvu. Kwa mujibu wa kauli ya Nape, ni wazi kwamba Chama cha CCM, hakina nia njema kwa Zanzibar, kuona ina utawala wenye mamlaka yake kamili.


      Nilipokuwa namsikiza nimejiuliza, hivyo kwanini Viongozi wa CCM Tanganyika, wanaumizwa na Zanzibar kuliko Tanganyika yao? Na hapa nimepata picha kwamba hata hizi vurugu na uonevu wa wananchi wa Zanzibar, unasimamiwa na CCM Tanganyika.


      Nape Mnauye, anajaribu kuwatisha baadhi ya viongozi wa CCM wa Zanzibar kwa madai ya kupingana na sera za Chama chao. Mansour Yussuf Himid, amesema wazi kuwa sera za CCM si Katiba ya nchi wala si Sheria za nchi ni utaratibu wa Chama tu.


      Nakumbuka mwanzoni mwa miaka ya 1980 Julius Nyerere, alisema kuwa Katiba si MSAAFU kwamba haibadiliki. Nape, anashikilia kwamba suala la Muungano kwa sera ya sasa ya CCM ni Serikali mbili.


      Mansour, anakubali hilo na wala hakatai, ila anazungumzia mustakabali wa Zanzibar, kufuatana na mabadiliko ya Katiba mpya, hapo baadae. Hapa nimeamini CCM Tanganyika ni mafisadi wa kauli na imani zao.


      Nape, anasema mwenye mawazo au maoni wayapeleke katika vikao halali vya CCM, ili yajadiliwe badala ya kuzungumza barabarani. Nape, amesahau kuwa Mansour amekuwa akizungumza kauli hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu ndani ya Baraza la Wawakilishi.


      Mansour, amezungumza hayo katika mjadala wa rasimu ya Katiba chini ya Samuel Sitta, mwaka jana 2011 na amekuwa akirudia kauli yake ya kukataa Muungano wa Serikali mbili mara kwa mara ndani ya Baraza la Wawakilishi, hadi kudiriki kusema kuwa Muungano huu wa sasa ni BUTU.


      Mansour kwa mara ya mwisho nimemsikia tena juzi katika Kongamano lililodhaminiwa na Norway, akisema kuhusu Muungano na muundo wa muungano wenye maslahi kwa Zanzibar. Inashangaza kuwa sehemu zote hizo Nape Mnauye, anaziona ni barabarani.


      Nape, anavyo amini sehemu halali iliyotoharika kwa viongozi wa CCM kuzungumzia na kuujadili Muungano ni katika vikao vya CCM tu, wala si mahali pengine. Kumbe jamaa huyu ni mjinga sana na viongozi wote wa CCM Tanganyika wenye mawazo kama ya Nape, nawaweka kapu moja ya wajinga.


      Na hapa nazidi kupata picha kwamba matatizo ya muda mrefu kwa Zanzibar, yamekuwa yakichangiwa na Tanganyika, kwa ushirikiano wa baadhi ya Viongozi wachache wa CCM Zanzibar, wanaokubali kuburuzwa na kutawaliwa na Tanganyika.


      Kwa taarifa yenu mwaka huu mmeula na chua ‘JINGA LIKIEREVUKA MWEREVU YU MASHAKANI’ ikiwa tuliweza kufikia maamuzi ya kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, naamini na uwezekano wa kuipata Zanzibar yetu, iliyo-huru upo, kupitia viongozi na nguvu ya wananchi wa Zanzibar.


      Nape Mnauye, kazi waliyofanya Jumuiya ya Uamsho, ilikuwa kazi ya kigoma cha kuamsha kula daku, ilikuwa ni kazi maalumu waliyopewa na Wazanzibari. Tunakuhakikishia muda si mrefu kwamba Muungano wa Serikali mbili utakuwa mwisho CHUMBE.


      WATUACHE TUPUMUWEE..
      ni vema tu bwana Mzenji73, ninacho shindwa kuelewa ni kuwa wazenj wengi ukiwemo wewe mna amini kuwa wa bara tunafaidi sana huu muungano na tunaishi kwa jasho la watu wachache wa zenj (about 3million with over 35million!). cha kujiuliza ni je zanzibar kuna nini? Mzee Nyerere mnatakiwa nyie wazenj mheshimu sana kwa mengi aliyowafanyia kwa huo muda aliokuwa madarakani maana nina amini bila yeye kufanikisha muungano mnaouponda sasa hivi mngelikuwa mmechinjana vyakutosha na bara tungelikua na wakimbizi chungu mbovu kutoka visiwa hivyo! anyway ni muda muafaka kwenu sasa kuchagua kwenda Oman au kuendelea na udugu uliojengeka (japo nyie mwajiita wakaazi na kubagua wabara huko visiwani),

    20. #37
      Macos's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2008
      Posts : 777
      Rep Power : 718
      Likes Received
      167
      Likes Given
      13

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By masopakyindi
      watu kama huyo yusufu himid ndo ndumila kuwili, kutumikia mabwana wawili na kujaribu kufaidi kote.
      Aondoke katika gari kubwa la ccm kabla ya kutoswa kwa aibu.
      Kama hakubliani na ser za ccm si aingie uamsho tu na aandamane?
      bado kuna watu wana mawazo ya kale..wanafikiri huu muungano hauwezi kujadiliwa...wanafanya kama ni biblia ama quraan...
      Ccm kuweka sera ya muungano isiyo taka mabadiliko ndio imezaa uamsho, na ndio iliyo zaa g55 ya kina kiseka na marmo.
      Mansour ana yo haki ya kujadili na kukosoa ikiwa sera ya chama chake haindani na wakati wa sasa na matazamio ya wengi..
      Wahafidhina wasio taka mabadiliko ndani ya ccm ..na watu kama kina nape ni watu ambao ukiwatoa katika siasa basi hawawezi kufanya kazi aina nyengine..watu kama hawa ni wachumia tumbo kwa kutumia siasa
      siasa sio dini..na muungano sio dini unaweza kujadiliwa...na kinyume chake utavunjika tu....hata kama dola itatumika.lakini watu wataukataa mpaka kitaeleweka
      kwa watu makini kuna haja ya kuujadili muungano ili uwe wa usawa na wenye misingi imara..
      Sera ya ccm ya serikali 2 ni kioja kwa wenye kufikiri
      ila ni nzuri kwa wenye maslahi binafsi

    21. #38
      Macos's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2008
      Posts : 777
      Rep Power : 718
      Likes Received
      167
      Likes Given
      13

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By deo
      ashakum si matusi; wanaopenda sana kuvunja muungano ni wenye asili ya uarabu na uarabu koko, hiyo wanafanya kwa maslahi mapana zaidi. Zaidi wengi wao wanatumika na zaidi wanawatumia nywele ngumu kuwa makuwadi wao hasa kwa kuangalia kipengele cha dini. Walio, na waliokuwa kwenye madaraka pia wana nia ya kuuvunja muungano.

      Kwa kifupi, maslahi makubwa hasa kwa nchi za kiarabu ni ya kisiasa, magharibi kama ipo ni kiuchumi, na kwa wazanzibari wengi wanaotaka kuvunja hawajui lakini kwa tabaka la hapo juu ni uchumi uchwara, kiaiasa na kidini.

      Historia ni mwalimu mzuri; ingefaa sana wazanzibari wakafundishwa historia yao ya ukweli na siyo ya kupotosha au kuipaka sukari. Tangu kabla ya mwarabu, baada ya mwarabu, kufika kwa wazungu na uhuru, mapinduzi na muungano.

      Muungano ukivunjika kama alivyosema mzee kifimbo, wengi wa wazanzibari nyewele ngumu watakuwa watumwa, na watawatumikia waarabu na waarabu koko.

      Mungu isaidie zanzibar
      mungu isaidie zanzibar ili watu kama hawa wanao fananisha kila kitu cha zanziabar ni warabu( japo ndani ya nyoyo zao wanamaanisha waislam)wasipate lengo la kuwagawa wazanzibari..
      Sasa tatizo la muungano sio la kundi moja tu hata ccm nao wamechoka...
      Wanaotaka mabadiliko ni wazenji wote...na wale ambao hawataki ni wale ambao wanafaidi kwa posho za muungano..hawa ndio wanao penda hali ya sasa isibadilike.
      Hakuna mwarabu wala mzungu kuna wazanzibari tu
      tukubali sasa upepo umebadilika...sababu zilizokuwapo nyuma ya pazia la muungano halipo tena
      ni nyerere kutumiwa na mabeberu kuzuia zanzibar kuwa 'cuba' hii ndio sababu ya muungano huu.
      Nyerere hakua na haja ya kuungana kwani alishawahi kutamka kwamba angekua na uwezo basi angevisokomeza visiwa hivi baharini
      kauli hizo zipo..na vijana wanazijua ...sio warabu ama nani siasa hizo zimeshashindwa

    22. #39
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,437
      Rep Power : 2887
      Likes Received
      4802
      Likes Given
      2863

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Tatizo linabaki pale pale. Wzba ukisoma hoja zao hawana kitu unachoweza kusema wanakijua na wanakisimamia.
      Kuna mtu kaandika hapo juu mwisho wa serikali 2 Chumbe. Hajasema serikali 3 au mkataba mwisho Chumbe. Sasa hapa najiuliza hivi wenzetu wanataka muungano uvunjike au wanadai kitu kingine?

      Lakini pia soma hoja za WZNZ hawana mbadala au hatima kuhusu suala hili. Wao wamebaki kulalamika ili hali wanakila uwezo wa kumaliza kadhia ya muungano. Ni wao kuamua tu hata leo, wanakila silaha ya kisheria. Hawataki!

      Wanasema mwisho chumbe! hawasemi pesa za bure asilimia 7 mwisho chumbe, hawasemi ajira na fursa za biashara mwisho chumbe, hawasemi nyaya za umeme mwisho chumbe, hawasemi elimu ya bure mwisho chumbe.
      Lakini basi hata kama mwisho ni chumbe wanauwezo wa kuzuia hilo? Maana jeshi linalomlinda rais wa Zbar limevuka Chumbe, mishahara ya BLW imevuka Chumbe!!!!

      Tunasubiri kidogo tu, makontena ya ZNZ kuja bara mwisho Chumbe, Ajira za ZNZ bara mwisho Chumbe nk. Ni suala la muda tu mtaonja machungu ya Tanganyika! Mtazamia Tanganyika kama mnavyozamia Ulaya.
      Mtabaki kusafisha baraza za Waarabu na wajomba zao! Angalia orodha ya akina Kussa nk. na jiulize wewe nywele za kipili pili una ZNZ?

      Anyway mimi bado namuomba Nape anijibu maswali niliyomuuliza.

      LET ZNZ GO!

    23. Deo
      #40
      Deo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th November 2008
      Posts : 521
      Rep Power : 641
      Likes Received
      89
      Likes Given
      7

      Default Re: Himid: Hata nikivuliwa uwanachama wa CCM, sitabadili mawazo yangu kuhusu Muungano

      Quote By Macos
      mungu isaidie zanzibar ili watu kama hawa wanao fananisha kila kitu cha zanziabar ni warabu( japo ndani ya nyoyo zao wanamaanisha waislam)wasipate lengo la kuwagawa wazanzibari..
      Sasa tatizo la muungano sio la kundi moja tu hata ccm nao wamechoka...
      Wanaotaka mabadiliko ni wazenji wote...na wale ambao hawataki ni wale ambao wanafaidi kwa posho za muungano..hawa ndio wanao penda hali ya sasa isibadilike.
      Hakuna mwarabu wala mzungu kuna wazanzibari tu
      tukubali sasa upepo umebadilika...sababu zilizokuwapo nyuma ya pazia la muungano halipo tena
      ni nyerere kutumiwa na mabeberu kuzuia zanzibar kuwa 'cuba' hii ndio sababu ya muungano huu.
      Nyerere hakua na haja ya kuungana kwani alishawahi kutamka kwamba angekua na uwezo basi angevisokomeza visiwa hivi baharini
      kauli hizo zipo..na vijana wanazijua ...sio warabu ama nani siasa hizo zimeshashindwa
      Je ni nini nafasi ya Shirazi kama taifa, Oman, wale waOman waliotangaza uhuru na wakati wa mapinduzi (matukufu) walikimbia na mpaka leo wanajitambua kama waZanzibari? Nini nafasi ya Iran? Libya ilikuwa na interest ambayo Gadafi amekufa nayo. Bado mataifa mengi ya kiarabu yana interest na roots zao hapo, hawa vipi?

      Usisahau mabepari uchwara wanaotaka kulichuuza nchi yenu ambao wao ni wazanzibari?

      Ni matajiri wangapi duniani wanaona fursa ya kujiendeleza hapo Zanzibar tena kwa kusaidiwa na mataifa yao?

      Hawa wote wana mawakala wao hapo.

      Ni muhimu sana kujua historia kama nilivyosema hapo juu na Nyerere anajua historia hiyo. Ndio maana walioendesha mauaji ya halaiki siku ya mapinduzi (yanayosemekana ni matukufu) walilenga kundi fulani la watu kwa sababu fulani. Kwa nini mpaka leo hamtukuzi uhuru uliotangazwa na Sultani mwaka 1963?


    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...