Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

    Report Post
    Results 1 to 16 of 16
    1. #1
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2097
      Likes Given
      1495

      Default Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      TANZANIA sasa imekuwa nchi ya misiba na tunadiriki kusema kwamba mara nyingi misiba hiyo imekuwa ya kujitakia. Haipiti siku kabla vyombo vya habari havijatangaza habari za vifo vya mamia ya watu vinavyotokana na ajali barabarani katika kila kona ya nchi yetu. Ajali za vyombo vya majini, kama ilivyo kwa vyombo vya safari za anga na reli zimezidi kuongezeka na kujenga dhana miongoni mwa wananchi kuwa, siyo tu ajali zimekuwa sehemu ya utamaduni wetu, bali pia kwamba ajali hizo kamwe haziepukiki.

      Tumeshindwa kupata muarobaini wa kupunguza, kama siyo kukomesha ajali hizo zinazopoteza maisha ya Watanzania. Badala ya kufanya uamuzi mgumu wa kuchukua hatua stahiki dhidi ya vyanzo vya ajali hizo na kusimamia sheria za usafirishaji kwa kuhakikisha sheria hizo zinauma kila upande pasipo woga wala upendeleo, viongozi wetu wamebaki kuwa vinara wa kutoa rambirambi kwa wafiwa. Tunathubutu kusema kwamba vifo vingi vinavyotokana na ajali hizo vimetokea kwa sababu Serikali imeshindwa kutimiza wajibu wake.

      Juzi mchana utamaduni huo wa ajali ulijirudia baada ya miili ya abiria wapatao 50 kuopolewa wakiwa wamefariki dunia na wengine 137 kuokolewa wakiwa majeruhi baada ya meli ya Skagit iliyokuwa imebeba abiria kutoka Dar es Salaam kwenda Zanzibar kuzama karibu na Kisiwa cha Chumbe, kilomita 19 kutoka Bandari ya Malindi, mjini Zanzibar. Hata hivyo, kumekuwapo na mkanganyiko kuhusu idadi kamili ya watu waliokuwa katika meli hiyo, kwani jana mamlaka husika zilikuwa zikitoa kauli zilizokuwa zinatofautiana au zinakinzana.

      Hii ni ajali ya pili mbaya kutokea visiwani humo katika kipindi cha miezi 10 tu tangu ilipotokea ajali nyingine ya MV Spice Islander Septemba 2011 ambapo watu wapatao 240 walikufa na wengine zaidi ya 1,500 hawajulikani walipo hadi leo baada ya meli hiyo kuzama ikiwa safarini kuelekea Pemba ikitokea Bandari ya Malindi, Unguja na tume iliyoundwa na Rais Mohamed Shein kuchunguza ajali hiyo ilitoa ripoti iliyosema kuwa, meli hiyo ilikuwa imebeba mizigo na abiria kuliko uwezo wake.

      Hata hivyo, siyo mara ya kwanza kwa meli hiyo iliyozama juzi kukumbwa na misukosuko ikiwa imebeba abiria baharini. Mei mwaka huu, abiria wapatao 300 walinusurika kufa baada ya meli hiyo kushika moto katika eneo la Nungwi ulioanzia kwenye injini wakati ikielekea Unguja kutoka Pemba. Zipo taarifa kutoka shirika moja la kimataifa kuwa, meli hiyo ilinunuliwa mwaka 2011 kutoka Marekani, lakini wataalamu walionya mwaka 2006 kwamba meli hiyo ilikuwa haifai tena kubeba abiria.

      Jambo moja linalojitokeza hapa ni kwamba meli zinazosafirisha abiria katika maziwa na bahari zetu siyo salama na hazifai tena kwa sababu zimechakaa, hivyo kustahili tu kuuzwa kama vyuma chakavu. Inashangaza kuona serikali zetu katika pande zote mbili za Muungano hazithamini maisha na ustawi wa watu wake na hazioni umuhimu wa kununua meli zilizo salama kwa ajili ya usafiri wa wananchi.

      Hili linathibitishwa na ukweli kwamba MV Liemba iliyozama katika Ziwa Tanganyika miaka michache baada ya Uhuru halijapata meli nyingine hadi leo. Kama hiyo haitoshi, MV Bukoba iliyozama katika Ziwa Victoria mwaka 1996 na kuua watu 1,000 haijapata mbadala wake hadi leo, huku MV Victoria iliyoanza kutumika katika ziwa hilo tangu miaka ya 60 ikisubiriwa kuzama na kuua maelfu ya abiria wakati wowote kutokana na kuzeeka kupita kiasi. Ni jambo la ajabu kwamba Ziwa Nyasa limekosa meli kwa miongo mingi sasa na kuacha wananchi wakiweka maisha yao rehani kwa kutumia usafiri usio salama.

      Tunazishauri serikali zote mbili zitambue kwamba majuto ni mjukuu, kwa maana ya kuhakikisha kwamba vyombo vya usafiri vinakuwa salama badala ya kusubiri kutokea kwa ajali na kuwa wepesi wa kutoa rambirambi na hata kuamuru bendera zote nchini zipeperushwe nusu mlingoti.
      Mr Rocky, Remmy and Kongosho like this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    2. Miaka 50

    3. #2
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,350
      Rep Power : 7770
      Likes Received
      1546
      Likes Given
      1801

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      The silly government!

    4. #3
      paty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : never never land
      Posts : 1,025
      Rep Power : 975
      Likes Received
      270
      Likes Given
      62

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Hii ni hatari ya sisi wenyewe kukubali kuwa dampo la vitu vya bei laisi vilivyokwisha thamani na vilivyo chini ya kiwango, ni hatari sana, ...ivi mamlaka husika huwa zinafanya kazi gani?

      Hizi tume zinazoundwa baada ya majanga huwa zinaishia wapi? Maana kila mwaka tatizo ni lile lile na wananchi wanazidi kupoteza maisha, inasikitisha sana, nadhani viongozi wanapaswa kuwajibika na wananchi tuache haraka zisizo kuwa na maana, kama usafiri ni hatarishi hakuna haja ya ku risk maisha yako
      Young Master likes this.
      CHADEMA mwendo mdundo - T 2015 CDM

    5. #4
      Never give up's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th September 2009
      Location : miles from nowhere
      Posts : 3,641
      Rep Power : 1221
      Likes Received
      723
      Likes Given
      586

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      ...na wengine zaidi ya 1,500 hawajulikani walipo!!!!!!

    6. #5
      SnowBall's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th September 2011
      Location : Amsterdam, Nertherlands
      Posts : 2,628
      Rep Power : 24025
      Likes Received
      2399
      Likes Given
      3298

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Kuna mambo maishani lazima uwe makini tu..hayataki ubabaishaji!..na miongoni mwao ni hili la 'Usafirishaji wa Abiria'..kiukweli usipokuwa makini hapa kila siku itakuwa Misiba tu!..Hakuna mbadala..tuache lipualipua..kama tunawatakia mema watu wetu tujitoe kikweli kikweli..bahati mbaya kwa nchi yangu Tanzania kila kitu hatuwezi..lol!
      Young Master likes this.
      ..''I wasted time, and now those time waste me''...Shakespear


    7. #6
      bombu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Posts : 1,036
      Rep Power : 879
      Likes Received
      497
      Likes Given
      592

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Tatizo kubwa ni kuwa wamiliki wa vyombo vyenyewe ndo hao hao wanaoturushia rambirambi zao kupitia runingani, na kutuambia hizo ni ajali kama ajali zingine, eti ni ajali za kimaumbile. Inanishangaza sana kuona kuwa baada ya tukio moja mambo husahaulika na ratiba za ovyo ovyo huendelea, huku tukidhani kuwa hiyo ni bahati mbaya.

      Lol, tumebaki tukiziumiza keyboard zetu, ilhali mambo yanazidi kutuwia ugumu. Ingawa wakati mwingine jamani ajali twazisababisha sie abiria na mizigo yetu. Tu watu wabinafsi wenye kujijali, hakuna anayefumbua macho na kuutazama uhalisia wa mambo. Utakuta mtu yuko radhi asafiri akiwa amening'inia kwa madai kuwa ana haraka ya aendako.

      kweli tunatakiwa kufumbua macho na kuona thamani ya roho na nafsi zetu. Tujithaminishe kabla hatujapangwa pamoja na mizigo yetu. Ni kawaida kwa vyombo vyetu vya usafiri kujaza kupita ukomo wake, na hili ni tatizo kubwa kuliko yote.
      Young Master likes this.
      Knowledge is knowing that a tomato is a fruit, but Wisdom is knowing not to put it in a fruit salad

    8. #7
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,214
      Rep Power : 46194
      Likes Received
      6565
      Likes Given
      5321

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Wanasubiri kuunda tume watu wale pesa za kufanya kazi za tume na mapendekezo yake nayo yatawekwa kama yalivyowekwa yale ya Mv Spice maana Tanzania kwa tume hatuna mshindani na zote report zake hazifanyiwi kazi
      Tumebaki tunasema ajali haina kinga wakati tunaona kwa macho yetu kuwa hivi vyombo ni vichakavu havifai hata kubeba abiria kwa namna yoyote
      Young Master likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    9. #8
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2097
      Likes Given
      1495

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Quote By Mr Rocky
      Wanasubiri kuunda tume watu wale pesa za kufanya kazi za tume na mapendekezo yake nayo yatawekwa kama yalivyowekwa yale ya Mv Spice maana Tanzania kwa tume hatuna mshindani na zote report zake hazifanyiwi kazi
      Tumebaki tunasema ajali haina kinga wakati tunaona kwa macho yetu kuwa hivi vyombo ni vichakavu havifai hata kubeba abiria kwa namna yoyote
      Usemayo ni kweli kabisa mkuu...Hakuna kinachoshindikana katika hii dunia na waswahili husema kinga ni bora kuliko tiba. Kwa mtazamo wangu nadhani kinga ya kwanza ya ajali kama hizi za uzembe ingepaswa kuwekwa na serikali kwa kuhakikisha kuwa vyombo vya majini vinavyoingia nchini kwetu ni mpya na zenye viwango vinavyokubalika kimataifa na sio kuruhusu nchi yetu kugeuzwa kama dampo la vyuma chakavu na machinjio ya watu

      Siwalaumu sana watanzania kwa kupanda usafiri huo kwa sababu kwanza kabisa usafiri wa majini ni usafiri wa gharama nafuu ambao hutumika na watu wengi hasa wa kipato cha chini...Ni watanzania wachache wenye uwezo wa kusafiri kwa ndege. Kama wakisema wasipande hizo meli kwa sababu zimechakaa unadhani watasafiri kwa njia gani wakati huo usafiri wa meli ndio wanaoutegemea ndio ambao pia wana uwezo wa kuumudu?
      Mr Rocky likes this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    10. #9
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,214
      Rep Power : 46194
      Likes Received
      6565
      Likes Given
      5321

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Quote By Young_Master
      Usemayo ni kweli kabisa mkuu...Hakuna kinachoshindikana katika hii dunia na waswahili husema kinga ni bora kuliko tiba. Kwa mtazamo wangu nadhani kinga ya kwanza ya ajali kama hizi za uzembe ingepaswa kuwekwa na serikali kwa kuhakikisha kuwa vyombo vya majini vinavyoingia nchini kwetu ni mpya na zenye viwango vinavyokubalika kimataifa na sio kuruhusu nchi yetu kugeuzwa kama dampo la vyuma chakavu na machinjio ya watu

      Siwalaumu sana watanzania kwa kupanda usafiri huo kwa sababu kwanza kabisa usafiri wa majini ni usafiri wa gharama nafuu ambao hutumika na watu wengi hasa wa kipato cha chini...Ni watanzania wachache wenye uwezo wa kusafiri kwa ndege. Kama wakisema wasipande hizo meli kwa sababu zimechakaa unadhani watasafiri kwa njia gani wakati huo usafiri wa meli ndio wanaoutegemea ndio ambao pia wana uwezo wa kuumudu?

      Mkuu Young_Master nchi ya kitu kidogo kila kitu kinawezekana
      Kuanzia waziri mpaka mtu wa chini pale TRA anayetoa mzigo bandarini wanajua uhalisia wa vyombo vyetu ndani ya bahari
      Wanajua hiki chombo ni cha mwaka gani na kilipaswa kuwa wapi wakati huo
      Hakuna kwenye uafadhali sio kwenye ndege wala sio meli au vyombo vvya usafiri majini wala sio barabarani
      Na hii ni kutokana na kuwa na watu wasiojali wanapitisha na kukubali vyombo hivyo vitumike kuwasafirisha watu
      Angalia mabasi yanavyoua watu yakipata ajali kwa kuwa bodi zake ni kama karatasi hivyo likipata ajali ni kuwa bodi inakatika na kuhama kabisa
      Angalia vinoah vilivyoruhusiwa kubeba abiria ambavyo hata mbuzi akilitwanga bodi lake kwa pembe zake kisawa sawa analitoboa ila vimejaa barabarani kubeba abiria
      Kwa hapa Arusha kwa sasa angalia barabara ya Namanga wamezitoa zile 504 zilizokuwepo vinoah kwa sasa ndo vimejaa
      Angalia karatu na Babat kwa sasa
      Mkuu kila mahali ni pabaya hakuna kwenye usalama kabisa
      Young Master likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    11. #10
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2097
      Likes Given
      1495

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Quote By Mr Rocky
      Mkuu Young_Master nchi ya kitu kidogo kila kitu kinawezekana
      Kuanzia waziri mpaka mtu wa chini pale TRA anayetoa mzigo bandarini wanajua uhalisia wa vyombo vyetu ndani ya bahari
      Wanajua hiki chombo ni cha mwaka gani na kilipaswa kuwa wapi wakati huo
      Hakuna kwenye uafadhali sio kwenye ndege wala sio meli au vyombo vvya usafiri majini wala sio barabarani
      Na hii ni kutokana na kuwa na watu wasiojali wanapitisha na kukubali vyombo hivyo vitumike kuwasafirisha watu
      Angalia mabasi yanavyoua watu yakipata ajali kwa kuwa bodi zake ni kama karatasi hivyo likipata ajali ni kuwa bodi inakatika na kuhama kabisa
      Angalia vinoah vilivyoruhusiwa kubeba abiria ambavyo hata mbuzi akilitwanga bodi lake kwa pembe zake kisawa sawa analitoboa ila vimejaa barabarani kubeba abiria
      Kwa hapa Arusha kwa sasa angalia barabara ya Namanga wamezitoa zile 504 zilizokuwepo vinoah kwa sasa ndo vimejaa
      Angalia karatu na Babat kwa sasa
      Mkuu kila mahali ni pabaya hakuna kwenye usalama kabisa
      Usemayo ni kweli kabisa mkuu na hayo maeneo yote uliyoyataja nayafahamu na ni kweli yanaongoza kwa huo usafiri mbomvu wa vinoah na watu wanautumia sana huo usafiri wa noah kwa sababu ndio ndio usafiri wa haraka ukilinganisha na mabasi. Lakini nani alaumiwe kama sio serikali?
      Mr Rocky likes this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    12. #11
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,533
      Rep Power : 1263
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      28

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      sio tu kwamba hizi meli/boti hazistahili kuwepo majini kwa sababu ya ubovu wake bali pia zinakuaga over loaded..unakuta meli yenye uwezo wa kupakia abiria 200 unakuta zingine zina mpaka watu 350 hao wengine wanawekwa kihuni huni kwa hiyo sasa unakuta meli ikija kuzama wakicheki kwenye rekodi wanapewa idadi na information za watu ambao sio zote ni sahihi..kuna wengine nina uhakika wamekufa na wako majini mpaka sasa ambao hawakurekodiwa kwenye system...hilo ni tatizo la kiuongozi na serikali inabidi iwe makini kusimamia haya mashirika/kampunia husika
      Young Master likes this.
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    13. #12
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,214
      Rep Power : 46194
      Likes Received
      6565
      Likes Given
      5321

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Quote By Young_Master
      Usemayo ni kweli kabisa mkuu na hayo maeneo yote uliyoyataja nayafahamu na ni kweli yanaongoza kwa huo usafiri mbomvu wa vinoah na watu wanautumia sana huo usafiri wa noah kwa sababu ndio ndio usafiri wa haraka ukilinganisha na mabasi. Lakini nani alaumiwe kama sio serikali?
      So mkuu Young_Master sio kwamba wahusika hawaoni kinachoendelea
      Wanaona na wanajua kuwa vyombo fulani havifai kusafirisha abiria au vinabeba abiria kupita uwezo wake
      Ila nani wa kukemea iwapo kuanzia msimamizi, meneja, mkata ticket lao moja kuwa wanataka faida
      MV Bukoba, Mv Spice na hata hii iliyozama inasemekana ni kubeba abiria na mizigo kupita uwezo wake na ubovu mwingine ambao unajulikana kwa wote
      Ila nani amfunge paka kengele kusema kuwa umezidisha abiria washushe au hiki chombo hakiruhusiwi kuondoka bandarini kwa kuwa kimejaa kupita kiasi
      Kuanzia msimamizi hapo na wahusika wote washakunja chao mfukoni hawana haja nyie abiria mtajua wenyewe mkifika au msifike shauri yenu
      Mabasi yanaondoka stendi yanajulikana kabisa ni mabovu may be tyres zimeisha kabisa au kuna sehem imefungwa fungwa na kamba au mpira kwenye engine linaachiliwa na kubeba roho za watu hakuna anayejali abiria jiombee mwenyewe ufike salama na Mungu anajua kuwa nyie mnasafiri so ni lazima awafikishe salama
      Trafic wanaona na wanajua kabisa chombo ni kibovu ila kwa kuwa nae kashakunjiwa wala haoni
      Madereva wanaovertake maeneo hatari yenye milima na kona za hatari traffic wapo wala hawajali wao wakikusimamisha wakunjie 5000 yao wakati mnasalimiana basi nenda mheshimiwa safari njema kabisa
      lori limetoka mnadani limejaza mizigo na juu kabisa ya hiyo mizigo wanakalishwa akina mama ambao gari likiyumba tuu kidogo hawawezi hata kujitetea
      Wakikutana na polisi we jua tuu kukunja mkono wala kosa halitaonekana( sawa ni shida ya usafiri huko wanakotoka ila je usalama wa hao wasafiri uko wapi)
      likianguka na kuua hizo ni kudra za mwenyezi Mungu ajali haina kinga
      Tufike mahali tuseme basi na hizi ajali hao waliopewa dhamana waone kuwa maisha ya watu yanayopotea yana thamani kama yao ambao wanapanda V8 na VX na kupita nazo mtaani kwa mbwembwe
      Young Master likes this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    14. #13
      Globu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2011
      Location : Giningi
      Posts : 4,911
      Rep Power : 3317
      Likes Received
      545
      Likes Given
      32

      Default

      Quote By Never give up
      ...na wengine zaidi ya 1,500 hawajulikani walipo!!!!!!
      Wamekufa.

    15. #14
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2097
      Likes Given
      1495

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Quote By Globu
      Wamekufa.
      Probably
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    16. #15
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,554
      Rep Power : 2090
      Likes Received
      1097
      Likes Given
      1575

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Nkicheki miaka ya MV Victoria, hata sipati hamu ya kupanda vyombo hivi vya kitz, practically primitive, we meli ya miaka ya 60, itakuwa na nini la kuifanya iendane na mazingira ya sasa?
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    17. #16
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,132
      Rep Power : 7423
      Likes Received
      2097
      Likes Given
      1495

      Default Re: Meli zetu hazifai kubeba abiria, ni vyuma chakavu

      Quote By Genecius Kaiza
      Nkicheki miaka ya MV Victoria, hata sipati hamu ya kupanda vyombo hivi vya kitz, practically primitive, we meli ya miaka ya 60, itakuwa na nini la kuifanya iendane na mazingira ya sasa?
      nadhani hilo swali ingekuwa ni bora kama wangeulizwa hao waheshimiwa wanaopiga meza za bungeni kila siku halafu hatuoni wanachofanya zaidi ya kuangamiza maisha ya wananchi kwa uzembe wao kila kukicha.
      genekai likes this.
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...