Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

    Report Post
    Page 27 of 27 FirstFirst ... 17252627
    Results 521 to 529 of 529
    1. #1
      Fang's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 5th November 2008
      Location : Limited
      Posts : 484
      Rep Power : 10089
      Likes Received
      273
      Likes Given
      1281

      Default Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      The topic speaks for itself.

      The main thread can be found here:
      http://www.jamiiforums.com/great-thi...05-2012-a.html

      Update:
      Quote By Mwali View Post
      Kama kuna member yoyote anaswali kwa waalikwa wetu (lenye kuhusiana na mjadala huu), naomba aliwekwe kwenye thread ya side comment. NItachagua maswali matatu ambayo yatakua hayaja ulizwa na yenye kuonekana kua na mantiki. Karibuni.
      Quote By Mwali View Post
      Taarifa kwa waalikwa na members wote wanao fatilia mjadala huu: Itakapo fika saa kumi na mbili East African Time (18:00 EAT) tutachukua break ya masaa mawili na kurudi tena saa mbili kuendelea na mjadala. Hii ni kuwapa fursa wale walio funga waweze kufuturu. Asanteni kwa uvumilivu.


      Quote By Roulette View Post
      Tumepigiwa sim na Matola, anaomba mjadala uendelee kesho. Alijitolea kwa kuchangia katika mjadala huu kupitia internet cafe kwa muda wa masaa sita, ila sasa anaona it's getting too late. Kesho asubuhi nitarudi kuwajulisheni muda kamili wa kuendelea mjadala. In the mean time tuendelee kukusanya comment na masuali ya members wote katika thread ya "side comments"
      Update Muhimu sana:

      Quote By Matola View Post
      Jamani wana JF kuna mambo ni personal zaidi, lakini hili lililonipata naona ni janga, mama yangu mzazi amefail step na alikuwa amefanyiwa oparesheni ya neuron surgeon sasa ametonenesha ile sehemu aliyofanyiwa oparesheni, nimeshinda MOI leo na sikuweza kufanya chochote, Nampenda Mama yangu siwezi kumteleza.

      Natumia fursa hii kuwaomba radhi wana JF kwamba wanisamehe kwa kutokupatikana leo, nadhani kwa waelewa wanajuwa vyema uchungu wa Mama. Roulette mimi ndio nimerudi nyumbani sasa hivi wakati waliofunga wanajiandaa kupata daku. tusameheehane ndugu zangu, nina majonzi
      .

      UPDATES - QUESTIONS FROM MEMBERS;

      Quote By Mr Rocky View Post
      Kuongeza fedha katika Mfuko wa Uwezeshaji Kiuchumi wa wajasiriamali wadogo (Mfuko wa JK) kiasi cha Shilingi bilioni 10.5 kupitia benki ya NMB. ilitoa kiasi cha Shilingi bilioni 10.5 kupitia benki ya NMB (Shilingi bilioni 5.25) na CRDB (Shilingi bilioni 5.25). Kiasi hiki kiliwezesha kutolewa kwa mikopo ya Shilingi bilioni 37.17 ikiwa in asilimia 118 ya Shilingi 31.5 zilizotengwa kutolewa na benk hizo mbili.


      Qn;
      Zomba tueleze nani alipata hizi bilions ulizotaja katika aya yako hii Sio kusifia tuu na kusema kuwa mkopo huu ulisaidia nani alizipata na zimesaidia nini na kwa nini hadi sasa hata marejesho hayaonekani Mikopo hii ililengwa kuwasaidia wale wajasiriamali wadogo klujikwamua na kufanya biashara katika hali nzuri ila zilitolewa na kuishia kwenye mikono ya watu ambao mnawajua ninyi ila mmekaa kimya wala hamtaki kutujuza ni akina nani. Na wala hamjasema lolote kuhusu kurejeshwa kwa mkopo huo ili uwasaidie wengine ambao wanauhitaji.

      Qn;
      Kuhusu sheria na utawala, kwa mara ya kwanza Tanzania tumeona ingezeko la mahakimu, majaji, na kupunguwa kwa kesi kwa kiasi kikubwa sana mahakamani.

      Je ongezeko hilo linareflect hali halisi ya mahamaka zetu na mlundikano wa kesi? je hao mahakimu na majaji walioongezeka kuna vitendea kazi kuwawezesha kuhimili hali ya nchi yetu? Maana kuna wilaya ambhazo hazina mahakama za mwanzo au hata majengo kuendeshea kesi mbalimbali. Au inabidi hakimu aendeshee kesi zake kwenye ghala (refer Magu)?

      Je budget ya kuendesha shughuli za mahakama inatolewa kwa wakati kukidhi uhalisia na mahitaji ya hizo mahakama? Au ni kuongeza tuu majaji na mahakimu bila kujali kama kuna majengo au vitendea kazi kuendesha hizo kesi?

      Quote By Edson View Post
      swali 1. ni kwa nini utawala wa raisi kikwete umegubikwa na hsutuma za rushwa na ufisadi? na je kwa mtizamo wa zomba ni kweli kikwet kama raisi hana makucha ya kuwadhibiti hawa wala rushwa? kama anayo kwa nini hali iko hivi na kama hana kwa nini asiachie ngazi

      swali la 2. raisi kiwkte kwa kiwango kikubwa ameshindwa kuboresha sekta ya afya na kwa kuzingatia mvutano uliopo na na madaktari na hivyo wengi wameamua kuondoa na kwenda nje ya nchi. Nini maoni ya zomba katika hili. ni kweli haiwezekani kuboresha mazingira na malipo ya wafanyakazi wa sekta ya afya?

      swali la 3. kwa maoni yako zomba ningependa kujua je demokrasia inakua au inadidimizwa nchini? na vipi kuhusu haki za binadamu je serikali ya kikwete inajali haki za binadamu? jibu swali hili kwa kutumia mifano hai
      Quote By Elizabeth Dominic View Post
      Mwali mimi nitaomba uwaulize washiriki kuhusu dhana ya udhaifu wa Kikwete. Je wanakubaliana nayo?

      Kama ndiyo ni kwanini kama siyo ni kwanini? Nauliza hivyo kutokana na pamoja kuwa Marais waliopita kuwa na mapungufu mengi lakini haijapata kutokea Taifa kuwa kwenye hali ya mkanganyiko kama sasa, kuanzia sekta ya Afya na mgogoro wa madaktari.

      Ukija kwenye Uchumi pia nayo utaona uhujumu uchumi mkubwa unaohusisha viongozi mbalimbali ambapo wanagusa nyanja zote Usafiri, elimu, ujenzi, utalii nakadhalika sasa ukijumuisha yanayotokea kiuhalisia naomba wainyambue hoja ya Udhaifu. Asante
      Quote By matumbo View Post
      Mwali swali langu ni kuwa...Kikwete amefanikiwa vipi kutekeleza kauli mbiu za "ajira milioni moja kwa vijana" "kilimo kwanza" ?
      Quote By FJM View Post
      Ningetaka kujua toka kwa Zomba yafuatayo:
      1. Inflation rate ilikuwa ngapi 2006 na sasa ikoje?
      2. Gini Coeefficent ilikuwaje 2006 na sasa mambo yako vipi?
      3. Miradi ya barabara iliyokuwa under pipeline 2006
      4. Miradi mipya ya barabara iliyoanza (from scrach) tangu 2006
      5. GDP growth rate na Inflation kwa hii miaka 1995, 2005 na 212.
      Quote By M'Jr View Post
      Asante Mwali pamoja na wageni wetu zomba na Matola,

      Mi napata tabu kidogo, ni kweli kwamba wakati wa utawala wa Nyerere ni kweli tulikuwa tuna export sana hasa mazao na tulifikia kuwa tunaongoza kwenye export ya zao la katani Duniani.

      Sitaki kwenda mbali sana lakini kwa mtazamo wa sasa inaonekana sio tu kwamba hatuexport tena ila hata chakula tu cha kututosheleza hakipo (Tukumbuke miaka miwili iliyopita) Kwahiyo mkuu zomba je kwa mtazamo wako unataka kunambia leo hali ya kilimo nchini ni mbaya kuliko wakati wa Nyerere?

      Mwali sina uhakika kama ulitualika na sisi but kama hukutualika sorry
      Quote By gfsonwin View Post
      swali langu kwa zomba na Matola-Hivi je nini umekuwa mchango wa vyama upinzani katika kuboresha utawala wa raisi kikwete? lijibiwe katika nyanja zote yaani elimu, afya ulinzi, kijamii nk. asanteni
      Quote By Nzi View Post
      Swali kwa Zomba - Ndugu Kikwete alishawahi kutoa ahadi ya kutengenesha biashara na siasa (wakati wa mdahalo wa urais - 2010) ili kupunguza mgungano wa kimaslahi kwa mtu ambaye ni mfanyabiashara na anataka kuingia kwenye siasa. Aliahidi kuja na sera na sheria ya kutekeleza ahadi hiyo. Swali, unalizungumziaje suala hili? je, huoni hili ni pigo kubwa katika suala zima la uongozi bora na uwajibikaji kwa wanasiasa?!
      Quote By mwaJ View Post
      7. Kuimairisha upatikanaji wa haki kwa watu wenye ulemavu na wazee

      Maswali kwa Zomba:

      • Kukamilika kwa sera ya wazee

      Je? Hiyo Sera inatekelezwa? Imewanufaisha wazee wa nchi hii? Toa mifano hai.


      • Kukamilisha sera ya watu wenye ulemavu

      Je? Hiyo Sera inatekelezwa? Ni kwa nini mauaji ya walemavu wa ngozi yameongezeka kipindi cha Kikwete?


      • Kupitishwa kwa sheria ya walemavu 2010

      Je? Hiyo sheria inatekelezwa? Ni kwa nini hata shule zenye watoto wenye ulemavu bado hazina mazingira rafiki kwa walemavu?


      • Kukarabati nyumba za vyuo vya ufundi kwa watu wenye uelemavu.

      Toa mifano hai ukilinganisha na vyuo vya ufundi vilivyopo nchini.


      • Kukarabati majengo ya makazi ya wazee

      Ni majengo ya wapi hayo yaliyokarabatiwa? Ni mwaka huu tumewaona na kuwasikia wazee wanaoishi katika kambi ya wazee Morogoro wakilalamika kuhusiana na mazingira magumu wanayoishi.


      • Kuhamasisha jamii kuhusiana na utoaji wa huduma kwa watu wenye ulemavu na wazee.
      • Kutoa nyenzo (vifaa) za kujimudu kwa watu wenye ulemavu na wazee.
      • Kuwajengea uwezo wazee na watu wenye ulemavu kwa kuwapa mitaji midogo midogo.

      Naomba utoe mifano hai kwa bullets 3 hapo juu.
      Quote By platozoom View Post
      Swali kwa Matola unafikri ni changamoto zipi alizokutana nazo JK ambazo zimekwamisha utekelezaji wa ahadi zake.

      Swali kwa zomba ukitilia maanani mabadiliko ya katiba yanayokuja ambayo pengine yakaongeza au kuondoa kikomo cha kugombe urais ......unafikiri JK anastahili kuongezewa kipindi kingine cha miaka mitano? na kwa nini?

      Mwali swali langu kwa Matola na zomba tena:

      Katika miaka ya karibuni hasa katika kipindi cha JK kumekuwa na mijadala mikali sana ya udini (sio dini) miongoni mwa wanasiasa hata viongozi wenyewe wa dini juu ya mgawanyo wa madaraka na utoaji wa nafasi za elimu na ajira kwa vigezo vya dini ya mtu!

      Swali: Mnafikiri ni kwa kiasi gani utawala wa JK umelishughulikia kwa namna ya kutoacha mpasuko katika Taifa?

      Nini mchango wa Utawala wake katika mgawanyiko huu?

      Naunganisha na maswali yangu ya awali:

      Swali kwa Matola unafikri ni changamoto zipi alizokutana nazo JK ambazo zimekwamisha utekelezaji wa ahadi zake.

      Swali kwa zomba ukitilia maanani mabadiliko ya katiba yanayokuja ambayo pengine yakaongeza au kuondoa kikomo cha kugombe urais ......unafikiri JK anastahili kuongezewa kipindi kingine cha miaka mitano? na kwa nini?


      Quote By SnowBall View Post
      zomba alitakiwa aongee from his perspectives na ku'compare' na 'international standards'..sasa kuorodhesha asilimia tu pamoja na maelezo mengi hakuleti tija ya mjadala!..

      Swali langu..na naomba Mwali ulichukue..ni hivi:

      Kwa kuwa tumeamua kuwa na Kauli Mbiu ya Kilimo Kwanza..na kwa kuwa karibu watu wetu 80% wanategemea kilimo..na kwa kuwa Ukiinua Kilimo obviously utakuwa umeinua Uchumi wa Mtanzania..Je? Kwa karibu miaka mitano tangu hii Kauli Mbiu ilipoanzishwa nini Mafaniko yake na nini kiwango cha Utekelezaji wake??
      Quote By FJM View Post
      Kwenye hoja ya ahadi za rais zomba amesema kuwa ahadi za rais zimetekelezwa. Ningetaka kujua ufafanuzi kwa haya yafuato:

      1. Ahadi zote 69 ziligharimu kiasi gani?
      2. Bajeti ya ahadi hizo ilipitishwa katiba kikao gani cha bunge?
      3. Na hela hizo zilikuwa za ndani (domestic revenue) au misaada/loans? Na kama ni misaada/loans toka wapi?
      Quote By Shark View Post
      Hivi karibuni kikwete alikaririwa akisema kua hajui hata umaskini wa watanzania unatokana Na nini?

      Zomba, unafikiri ni sahihi hili??
      Quote By Ngongo View Post
      Qn;
      Naomba Mkuu zomba kuuliza swali dogo sana.Rais Kikwete ameteua majaji wengi kwa nia ya kukabiliana na mlundikano wa kesi.

      Bahati mbaya teuzi hizi haziendani na ongezeko la ujenzi wa mahakama,vitendea kazi vya kisasa kama computer amabazo zingesaidia kuongeza kasi ya usikilizwaji wa kesi.Majaji wengi hawana ujuzi wa kutosha na hata hukumu zao tayari zimezua maswali mengi miongoni mwa wataalamu wa sheria.

      Qn;
      Ujenzi wa UDOM umekomba fedha za NSSF na kusabisha shirika hilo matatizo makubwa ya cash flow na hatimaye sisi wanachama wa NSSF tunalazimika kulipwa fedha zetu tutakapofikisha miaka 60 haijalishi umefukuzwa kazi ukiwa na miaka 20 au 30 !.

      [1] Inafahamika wazi ajira za sekta binafsi hazina usalama mtu unafanyakazi miaka yako sita au kumi unatambaa au unakimbizwa.

      [2] Umri wa kuishi mTanzania ni chini ya miaka 50 ?

      [3] Maamuzi ya ujenzi wa Udom na Daraja la kigamboni wanachama wa NSSF na PPF hawakushirikishwa.

      zomba huoni Kikwete na serekali yake wanastahili kushtakiwa kwa kutuweka sisi wanacha wa hiyo mifuko ya hifadhi ya jamii katika hali ya ngumu kwa nia ya kujipatia ujiko wa kisiasa ?.Katiba mpya kipengele cha kumshitaki Rais anayechezea uhai wa wananchi wake kiwekwe.
      Quote By ruttashobolwa View Post
      Hili swali liende kwa zomba ,tume shuhudia jk akibadilisha baraza la mawaziri pamoja na mawaziri kwa tuhuma za ufisadi lakini hatuoni hatua yeyote inayo chukuliwa kuwa chukulia hatua za kisheria au kuhakikisha pesa zilizo chukuliwa zinarudishwa.

      -Je tuendelee kuona mafisadi wanatamba mtaani na kukimbia na pesa za wananchi?

      -Kuna ugumu gani kuwa kamata mafisadi hao na kuwachukulia hatua?
      Quote By Kibanga Ampiga MKoloni View Post
      Swali langu:

      Je kwa kuwa Bunge la Tanzania chini ya RAISI KIkwete na SPIKA Makinda na Majority ya wabunge wa CCM wamekuwa wakipitisha miswada yenye kukandamiza wananchi, Wapinzani wanapojaribu kuhoji kuna kuwa na upinzani mkubwa kutoka kwa SPIKA. Mafano:-
      1. Upandishaji wa Bei ya Mafuta taa huku tukijua kuwa Idadi ya Magari tanznaia hayafiki hata 1 Milioni na watanzania zaidi ya 45 Milioni wakitegemea mafuta taa.

      2. Hifadhi ya Jamii, kwamba hakuna tena kuchukua mafao yako pindi unapoacha kazi mpaka hapo utakapo fikisha umri wa miaka 55/60 hata kama umefanya kazi kwa muda mwezi mmoja.

      Je ni kwa nini RAISI kikwete amekuwa ni mwepesi kusign hii miswada bila kusikiliza maoni ya wananchi?
      jmushi1, kiraia, zomba and 17 others like this.
      ...To Defeat your Enemy, become your own Enemy...


    2. #521
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 11,333
      Rep Power : 34416
      Likes Received
      10550
      Likes Given
      14628

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      zomba mimi na Kongosho na Mr Rocky tunapenda kukupongeza sana kwa juhudi zako za kuitetea serikali za hali ya juu. ambazo kwakweli umeweza kutuletea data ambazo zipo na kutuonyesh jinsi ambavyo serikali yetu inapotosha hali halisi. Yaani hela inayoombwa ama inayotafutwa inatafutwa with purpose fulan lkn kumbe haitumiki hivyo kwasababu ingekuwa inatumika hivyo basi data zilizopo zingeonyesha hali halisi tofauti na hivi sasa zilivyokaa kiunadharia. Mipango yao ni mizuri lakin si inayotekelezeka.

      however siyo kwamba tunapinga kila kitu hapana vingine umesema viko sahhih lakin vingine ni sahihi kwenye makabrasha lakin siyo ukweli kwenye field. big up brother.
      Mr Rocky and Matola like this.
      "thought takes man out of servitude into freedom"
      'daima tudumu katika upendo'

    3. #522
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,053
      Rep Power : 14671
      Likes Received
      2955
      Likes Given
      2099

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      Quote By gfsonwin View Post
      zomba mimi na Kongosho na Mr Rocky tunapenda kukupongeza sana kwa juhudi zako za kuitetea serikali za hali ya juu. ambazo kwakweli umeweza kutuletea data ambazo zipo na kutuonyesh jinsi ambavyo serikali yetu inapotosha hali halisi. Yaani hela inayoombwa ama inayotafutwa inatafutwa with purpose fulan lkn kumbe haitumiki hivyo kwasababu ingekuwa inatumika hivyo basi data zilizopo zingeonyesha hali halisi tofauti na hivi sasa zilivyokaa kiunadharia. Mipango yao ni mizuri lakin si inayotekelezeka.

      however siyo kwamba tunapinga kila kitu hapana vingine umesema viko sahhih lakin vingine ni sahihi kwenye makabrasha lakin siyo ukweli kwenye field. big up brother.
      Ungeonesha kama nilivyoonesha mimi unavyosema havipo sahihi, badala ya kurusha shutuma bila ushahidi.

      Isitoshe, mimi hapa nilikuwa siitetei Serikali ila namtetea Kikwete na kuonesha mipango na maboresho aliyoyafanya amabyoo yote yamefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

      Siitetei Serikali nzima kwa kuwa najuwa bado kuna watu Serikalini ambao sio safi na saa nyingine huhisi wanafanya makusudi kabisa kuupaka matope uongozi wa Kikwete.

      Kikwete kama Kikwete kafanya mema mengi sana katika uongozi wake kwa manufaa ya umma. Lakini ukumbuke katika kila msafara wa mamba kenge hakosi.

      Hujasikia Mchungaji au Sheikh akazaa mtoto jambazi? na wema wote na mafunzo mema yote lakini hayakosekani hayo. Cha msingi ni kutazama Kikwete kama Kikwete anafanya nini? ni mengi sana mema. Lakini Kikwete atapomteua kiongozi mwengine halafu huyo afanye madudu halafu umlaumu Kikwete? itakuwa humtendei haki Kikwete. Tazama aliyeteuliwa katumwa afanye nini na yeye kafanya nini. Kama katumwa kufanya mabaya na Kikwete basi hapo Kikwete atakuwa haepuki lawama, lakini kama Kikwete kasema nataka ununuliwe mtambo wa kufulia nguo Muhimbili wa kisasa, huyo alietumwa akaenda akaununuwa substandard na akala rushwa ya asilimia 10, hapo utamlaumu Kikwete?
      Last edited by zomba; 30th July 2012 at 07:44. Reason: typo
      Chilisosi, Fang and gfsonwin like this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    4. #523
      SoNotorious's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2011
      Posts : 796
      Rep Power : 520
      Likes Received
      192
      Likes Given
      261

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      JK legacy yake itakuwa ni matuta alojenga kwenye highway zetu, jk ni comic dunia haijawhi kuona.

    5. #524
      Chilisosi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2008
      Posts : 1,814
      Rep Power : 0
      Likes Received
      386
      Likes Given
      501

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      Quote By zomba View Post
      Ungeonesha kama nilivyoonesha mimi unavyosema havipo sahihi, badala ya kurusha shutuma bila ushahidi.

      Isitoshe, mimi hapa nilikuwa siitetei Serikali ila namtetea Kikwete na kuonesha mipango na maboresho aliyoyafanya amabyoo yote yamefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

      Siitetei Serikali nzima kwa kuwa najuwa bado kuna watu Serikalini ambao sio safi na saa nyingine huhisi wanafanya makusudi kabisa kuupaka matope uongozi wa Kikwete.

      Kikwete kama Kikwete kafanya mema mengi sana katika uongozi wake kwa manufaa ya umma. Lakini ukumbuke katika kila msafara wa mamba kenge hakosi.

      Hujasikia Mchungaji au Sheikh akazaa mtoto jambazi? na wema wote na mafunzo mema yote lakini hayakosekani hayo. Cha msingi ni kutazama Kikwete kama Kikwete anafanya nini? ni mengi sana mema. Lakini Kikwete atapomteua kiongozi mwengine halafu huyo afanye madudu halafu umalumu Kikwete? itakuwa humtendei haki Kikwete. Tazama aliyeteuliwa ktumwa afanye nini na yeye kafanya nini. Kama katumwa kufanya magaya na Kikwete basi hapo Kikwete atakuwa haepuki lawama, lakini kama Kikwete kasema nataka ununuliwe mtambo wa kufulia nguo Muhimbili wa kisasa, huyo alietumwa akaenda akaununuwa substandard na akala rushwa ya asilimia 10, hapo utamlaumu Kikwete?
      Hapo umeongea point,
      Kweli nimeamini hata milembe kuna wengine wamepelekwa kwa kusingiziwa tu, I mean jamii haikuwaelewa wanataka nini wakizani vichaa.
      Llkiani pamoja na kuwa kikwete kachagua waziri aliyeenda kufanya madudu kwa nini kikwete akae kimya mpaka vyombo vya habari na wabunge wapige kelele? unakumbuka ilichukua muda gani kumuondoa ekelege? mpaka wabunge wakataka waziri mkuu ajiuzuru?? hapo nani ana kosa. nazani kosa ni kukaa kimya bila kukemea wazembe.

    6. #525
      Zohali's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 28th July 2012
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      Kwangu mimi serikari kwa kipindi 2005-2015 imefanikiwa zaid katika sehemu ya uhuru wa watu kutoa maoni na kusema madukudu yao ni moja kati ya sehemu walio jitahidi.,
      zomba likes this.


    7. #526
      kelvin shayo's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 27th July 2012
      Posts : 8
      Rep Power : 348
      Likes Received
      0
      Likes Given
      5

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      kwakweli kikwete anapewa kazi nzito na kuonekana sio mtenda mema kwasababu ya watendaji wake wanamuangusha sanaa

    8. #527
      kelvin shayo's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 27th July 2012
      Posts : 8
      Rep Power : 348
      Likes Received
      0
      Likes Given
      5

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      halafu watu tumekuwa tukitoa maoni mengi ila maoni yetu hayawi implemented na serikali its like tunajifurahisha kuongea and actions are not there at all.

    9. #528
      salva mwanaharakati's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 27th July 2012
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      2

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      nawasalimu katika jna la MUNGU muumba wa mbingu na nchi!
      kwa habari yatathmini ya utawala wa huyu kiongozi wa sasa wa Taifa letu, nimepitia maoni na maswali mengi ya wachangiaji wenzangu nimejifunza mengi, kwa kuzingatia ukweli kwamba; mahitaji ya watanzania katika maisha ya kila siku hasa kwa mambo makuu matatu, malazi...chakula na mavazi, ambayo ni ya msingi sana kiasi haipashwi mtu kuyakosa. pia kwamba, mchango wa serikali yetu katika kuwawezesha raia wake kupata mahitaji hayo ( ikumbukwe huu ni wajibu kwa serikali zote duniani ) unaweza kupimwa kwa hali halisi ya wepesi au ugumu wa maisha katika jamii, hili halihitaji shahada kuliamua kwani hata watoto wa fukara wanaweza kulichabua kwa uhalisi kwa kiwango cha weledi wao na likaeleweka, na kwamba;

      `uwiano wa nini kimefanikiwa na nini hakijafanikiwa kwa kiwango tarajiwa kiutawala ni vema ukazingatia uhalisi wa mambo toka katika jamii husika, na hasa kuzingatia tija kwa wananchi na hali ya uendelevu wa yale yaliyotekelezwa na pia ukweli kama namna yalivyotekelezwa hayana madhara / hasara kwa wananchi?

      sasa basi; nawashangaa wote ambao wanamacho bali hawaoni, wanamasikio hawasikii, tena wana akili nao hawatafakari na kuona uhalisi, bali kwa akili mbovu wanakandamiza mzani upande mmoja. hawaoni hali mbaya katika mandhari ya miji na vijiji, hawaoni misiba ya albino isiyo kwisha, hawaoni mauaji ya raia wasiomakosa, wala matendo ya upendeleo ya spika bungeni ambayo yanampaka aibu kama kanuni ya dhambi inavyo taka ( mwisho ni aibu halafu mauti), pia hawaoni jirani anpokosa kuhudhuria chooni bila ugonjwa wa kumzuia kufanya hivyo bali kuto kula. hawaoni meeeengi yanayoendelea kwenye jamii wanayoishi,hata viwanda vilivyoporwa na wachache wasio na tija kwa umma bali kwa wachache, tena waliodhurumu mafao ya wafanyakazi katika viwanda baadhi hadi leo wanakufa tu hawayaoni haya, sera na mikataba mibaya itakayo tuumiza hata wakitoka madarakani hamvioni wala kusikia pia heee!

      pia hasikii; vilio vya kudai haki vinazidi kula uchao ( madaktari, walimu, wafanyakazi kwa jumla na hata raia wengine) hawasikii wazazi wa albino wakilia msiba wala albino anaye omba ulinzi hawamsikii jamani!, hata kelele za migodini kusiko na haki kwa wazawa hawasikii, yaani hata malalamiko juu ya uporwaji madini katika taifa letu wapi jamani!, hasikiki hata mama anayeporwa mtoto ndani ya vyombo vya sheria tena hadharani huku tukisikia wengine daah! MUNGU wasaidie!

      sasa wanaamua kutotafakari haya yote kwa kuwianisha na hayo mazuri yasiyo na mashiko, wanayabebea bango kana kwamba yapo pekee katika jamii isiyo na hayo matatizo hapo juu. ILA NAFASI WANAYO WABADILIKE ILI WENZAO WANAPOCHUKUA HATAMU KUONGOZANCHI ANGALAU WAONEKANO WANAMAWAZO YALIYOPONDEKA NA MOYO UNAOTUBU KWA UBAYA HUU.

      KWA HAKIKA; mapumba ni mengi kuliko mchele katika utawala huu wa kikatili unaojificha kwenye kauli zisizotosha kuwaficha kama serikali sikivu na kiongozi anaye jali. haya hayaondoi ukweli un aokua kila siku na ndio utakao wamaliza.
      MUNGU Ni mwaminifu Tanzania itabadilika na kufika inakotakiwa si muda mrefu. ameni.

    10. #529
      Ndibalema's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2008
      Location : Mbagala
      Posts : 6,733
      Rep Power : 2031
      Likes Received
      1699
      Likes Given
      1697

      Default Re: Mjadala: Side Comments: Tathmini ya Utawala wa Rais Kikwete (2005-2012)

      Nadhani hajui dira ya hii nchi
      aliingia madarakani akiwa hajui anaenda kufanya nini kwa watanzania
      "Makalio ya sufuria hayaogopi moto"

    Page 27 of 27 FirstFirst ... 17252627

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...