Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA wagundua mtambo wa kuingiliana kwa mawasiliano

    Report Post
    Results 1 to 3 of 3
    1. #1
      abdulahsaf's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st August 2010
      Posts : 860
      Rep Power : 723
      Likes Received
      123
      Likes Given
      1

      Default CHADEMA wagundua mtambo wa kuingiliana kwa mawasiliano

      Saturday, July 21, 2012 1:52 PM
      CHAMA CHA DEMOKRASIA na Maendeleo (Chadema), kimedai kugundua mtambo unachochea uvunjifu wa amani unaotumika kupitia mawasiliano ya simu za mkononi ambao unamilikiwa na mtoto wa kigogo wa CCM
      Hayo yalisemwa jana mbele ya vyombo vya habari jijini Dar es Salaam na mjumbe wa Kamati Kuu wa CHADEMA, Mabere Marando

      Marando aliviambia vyombo vya habari kuwa, mtambo huo unafanya kuingiliana kwa mawasiliano ya simu ambapo anayekupigia si mlengwa

      Alifafanua kuwa, mtambo huo una uwezo wa kufanya kupigiwa simu au kupokea ujumbe mfupi wa maneno na namba ambayo unaifahamu ambapo aliyetuma ama kupiga simu si mtu ambaye unamfahamu mwenye namba hiyo

      Marando alisema mitambo hiyo ya inayomilikiwa na mtoto mmoja wa kigogo ambaye hajamtaja jina alisema aliinunua nchini Israeli ambapo kuna kampuni mbili alizozitaja kwa majina ya Nice System na Verinty System, ambazo zimefanikiwa kutengeneza mitambo yenye uwezo wa kuingilia kwa mawasiliano kati ya mtu na mtu kwa umbali wa kilometa tano

      Alisema mitambo hiyo ndiyo ilitumiwa kusambaza ujumbe mfupi wa vitisho kwenye simu ya mbunge wa Iramba Magharibi, Mh.Mwigulu Nchemba.

      Alifafanua mfumo uliotumika kuingiliana unaitwa sms proofing, na kwamba inaweza kutumiwa na idara za kiusalama kwa sababu maalum tu.

      Pia alisema chama hicho kilisikitishwa na taarifa walizozipata kuwa mwanasheria mkuu wa serikali Jaji George Werema kuwaagiza watumishi wa ofisi yake kuandaa mashtaka kwa ajili ya tukio hilo la kuwahusisha wabunge wa CHADEMA na meseji hizo badala ya kushughulika na watu walioingilia mawasiliano yao.

      Wiki iliyopita mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu, alisimama bungeni na kuomba mwongozo wa Spika akidai kuwa amepokea ujumbe mfupi wa simu kutoka kwa baadhi ya wabunge wa CHADEMA, akitishiwa kuuawa.


    2. #2
      rodrick alexander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Posts : 729
      Rep Power : 516
      Likes Received
      172
      Likes Given
      341

      Default Re: CHADEMA wagundua mtambo wa kuingiliana kwa mawasiliano

      inashangaza sana kwani mpaka sasa hivi tcra wameshindwa kununua mtambo ambao utaonyesha idadi ya simu na sms zinazotumika na makampuni ya simu ili waweze kukusanya kodi inayostahili badala yake tunasikia taarifa juu ya mtambo wa kuingilia mawasiliano tcra mnafanya nini?

    3. #3
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,507
      Rep Power : 21688
      Likes Received
      13814
      Likes Given
      18061

      Default Re: CHADEMA wagundua mtambo wa kuingiliana kwa mawasiliano

      wamegundua?
      au wamekamata?
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...