TULIWASILISHA KATIBA YETU KWA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA pamoja na maombi ya usajili WA muda Kama taratibu za ofisi yake zinavyoamuru.
Msajili aliipitia na kutupatia MAAGIZO Kama si USHAURI WA kuifanyia marekebisho aliyoyaona Kabla ya kutoa rasmi kwa ajili ya wanachama wetu na wananchi WA Tanzania kwa ujumla.
Soon baada ya kukamilisha zoezi la Uhakiki WA kudumu linaloendelea hivi sasa katika mikoa ya Dodoma, Tabora, Lindi, Mtwara na Dar ES Salaam mnamo tar. 17-08-2012, Katiba yetu itakua Tayari kwenye website ya Chama ambayo ni
adctz.
Kwa matakwa AMA mahitaji niliyoyaona kwa baadhi/wengi WA wanaJamii walioonyesha kuvutiwa na Chama chetu sio vibaya nikawapatia mambo MUHIMU YALIYOMO KWENYE KATIBA YETU:
1. Ukomo WA Uongozi: Vipindi viwili vya miaka mi5 mi5 kwa uongozi WA Kitaifa.
2. Kiongozi kutangaza Mali zake ndani ya KIPINDI cha MIEZI MITATU mara baada ya kuchaguliwa.
3. Kufukuzana: Kutakua na CHOMBO cha Kutatua migogoro ya chama nje ya chama kitakachokuwa CHINI ya Uongozi WA Mwanasheria AMA jopo la wanasheria ili kukwepa personal interest ie: makundi hivyo suala la kutimuana kiholela halitokuwepo katika chama Chetu.
4. KATIBA pia itatambua Uwepo WA MwenyeziMungu, Itasaidia kupata viongozi waadilifu, wachamungu hivyo kupunguza matendo yote maovu ie: Ufisadi, Wizi WA Mali za Umma, Udikteka etc.
5. Walemavu wasipungue asilimia TANO (5%) katika ngazi zote za Uongozi. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna zaidi ya walemavu millioni NNE (4mil.) NCHINI Tanzania.
6. Asilimia hamsini ya wanawake katika ngazi zote za Uongozi.
Hayo ni baadhi tu ya maeneo muhimu yaliyopo kwenye KATIBA yetu.
KARIBUNI ADC - DIRA ya mabadiliko.
Follow Us Here