Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Rais Kikwete punguza safari za nje

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 23
    1. #1
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Rais Kikwete punguza safari za nje

      Tumepata kuandika na leo tunaandika tena tukimsisitiza Rais Jakaya Kikwete na washauri wake kupunguza safari za nje ya nchi kikazi wakati taifa likiwa kwenye hali tete.

      Licha ya misafara yake kulalamikiwa ndani na nje ya nchi kwa sababu ya kuongozana na msururu wa watendaji ambao wengine hawana umuhimu, safari hizo hazizingatii utulivu wa nchi.

      Ni mara kadhaa wananchi wamewahi kuhoji majukumu ya rais na wasaidizi wake kwa sababu sio lazima kila safari nje ya nchi anatakiwa aende, ndiyo maana wapo wasaidizi wake katika ngazi mbalimbali ambao wanaweza kumwakilisha. Pamoja na ushauri tunaompa rais kupitia vyombo vya habari hususani magazeti, watendaji wake huibuka na kumjibia kwamba safari hizo zina tija hivyo lazima asafiri, wanasahau kwamba wasaidizi wanaweza kwenda ili rais abaki nchini kumaliza kero za waliomwajiri kupitia sanduku la kura.

      Tunafahamu kwamba nyingi ya safari hizo ni kutembeza bakuli kuomba msaada ambao hana muda wa kufuatilia matumizi ya fedha hizo kwa sababu anakuwa nje ya nchi. Kwetu tutaendelea kulisema tukiamini ipo siku rais Kikwete ataona umuhimu wetu japo atakuwa amechelewa.

      Wataalamu wanasema msafara wa watu 20 ambayo ni idadi ya kawaida kwa msafara wa rais Kikwete hasa anapokwenda nje ya nchi wastani wa matumizi kwa siku huweza kufikia dola 15'000 za maarekani ambazo ni zaidi ya sh milioni 20.

      Sasa gharama hiyo ni kwa siku, wakati mwingine ziara zake huchukua hadi siku 10 au zaidi na idadi ya wasindikizaji huweza kuongezeka hadi kufikia 40; tutafakari ni kiasi gani taifa linapoteza fedha nyingi pasi na sababu za lazima? Takwimu zinaonyesha mpaka sasa rais na wapambe wake wamesafiri zaidi ya mara 320 tangu aingie madarakani Desemba mwaka 2005 tukisema kila safari amekaa huko kwa siku tano, tunaona jinsi Taifa letu linavyotiwa umaskini na wachache wanaozunguka meza ya rais.

      Tunaamini kwamba matatizo yanayotokea hivi sasa kama mauaji ya raia kule Songea, migogoro kwenye Bodi ya Pamba, mfumko wa bei unaosababisha kuyumba kwa uchumi wetu, migomo ya walimu wanaodai marupurupu, madaktari na mengine mengi angeweza kuyasimamia kwa karibu zaidi na kuyamaliza.

      Alipata kunena aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Hayati Daudi Balalli akiishauri serikali kuacha kuwa omba omba badala yake tutangulize uzalendo kwa kulinda maliasili.

      Source: Tanzania Daima - Jumanne julai 17,2012
      Life without problems never make a strong and good person!


    2. #2
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,722
      Rep Power : 68646
      Likes Received
      7102
      Likes Given
      5609

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      sweetlady leo umeingia kwenye siasa
      huku unaweza jikuta unapigwa ban bure bora twende kwenye jukwa letu la chit chat bana
      Maana huchelewi kukasirika na kujikuta umetukana
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    3. #3
      Nyani Ngabu's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,521
      Rep Power : 0
      Likes Received
      9766
      Likes Given
      696

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Hivi kati ya Kikwete na Membe nani anasafiri zaidi kumshinda mwenzake?

    4. #4
      james chapacha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 508
      Rep Power : 465
      Likes Received
      104
      Likes Given
      25

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Eti anaenda kuemea!!!!!!!!!!!na cha ajabu zaidi anayekupa misaada anapanda daladala,anayeenda kuomba anakwenda na taxi.

    5. #5
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,542
      Rep Power : 1269
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      29

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      nyie watu ni bora kumuomba mchungaji asihubiri siku ya jumapili kuliko kumwomba JK asisafiri
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune



    6. #6
      King Kong III's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Enaboishu-Umenyeni
      Posts : 12,401
      Rep Power : 5162
      Likes Received
      3345
      Likes Given
      2738

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Hiv hili swala halipo mahakamani kweli? Maana naogopa kuchangia nisije nikaingilia uhuru wa mahakama!

    7. #7
      nipeukweli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th July 2012
      Posts : 318
      Rep Power : 412
      Likes Received
      117
      Likes Given
      80

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      uuuuwiii this coconut head!

    8. #8
      Zipuwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Posts : 2,206
      Rep Power : 875
      Likes Received
      310
      Likes Given
      123

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      kumshauri mtu miguu imelambwa na mbwa ni kazi bure
      Maisha yetu ni mafupi lazima tuyatete kwa namna yeyote ile!

    9. #9
      Brightman Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2009
      Posts : 747
      Rep Power : 671
      Likes Received
      96
      Likes Given
      26

      Default

      Quote By sweetlady View Post
      ............safari hizo zina tija.......

      Source: Tanzania Daima - Jumanne julai 17,2012
      Kumbe majibu yapo!
      Kwani huyu mhariri anataka nani aende kutembeza hilo bakuli kama si mkulu wa kaya..!
      Last edited by Brightman Jr; 17th July 2012 at 17:57.

    10. #10
      mito's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th June 2011
      Posts : 1,178
      Rep Power : 640
      Likes Received
      480
      Likes Given
      1573

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Muhimu hapo ni kwamba apunguze safari ili kuokoa pesa za walipa kodi. Kimsingi suala la yeye kuwepo au kutokuwepo halizuii shughuli za serikali kufanyika, labda kusaini miswada (kuwa sheria) na kusaini wafungwa wa murder wanyongwe ndo kutamsubiria
      Haki ya mtu haipotei, inacheleweshwa tu!

    11. #11
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By Nyani Ngabu View Post
      Hivi kati ya Kikwete na Membe nani anasafiri zaidi kumshinda mwenzake?

      Kikwete atakuwa anasafiri zaidi kuliko Membe.....mimi huwa nahisi wakati mwingine anamwomba Membe apumzike yeye aende badala yake!
      Life without problems never make a strong and good person!

    12. #12
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By mito View Post
      Muhimu hapo ni kwamba apunguze safari ili kuokoa pesa za walipa kodi. Kimsingi suala la yeye kuwepo au kutokuwepo halizuii shughuli za serikali kufanyika, labda kusaini miswada (kuwa sheria) na kusaini wafungwa wa murder wanyongwe ndo kutamsubiria
      Haswaaa wala hujakosea hapo red.....ndio mana tunamwomba apunguze safari manake zina gharimu vinginevyo afute wizara ya mambo ya nje manake ni kama vile haina kazi!
      mito likes this.
      Life without problems never make a strong and good person!

    13. #13
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By Negembo View Post
      Kumbe majibu yapo!
      Kwani huyu mhariri anataka nani aende kutembeza hilo bakuli kama si mkulu wa kaya..!
      Kutembeza gani bakuli kila siku?.......hatukatai kuwa JK ni omba omba ila basi ifike mahali akishatembeza bakuli apumzike aangalie kama bakuli aliloleta limefanya yale aliyokusudia.....huoni kama hizo safari zake zinamaliza hata hilo bakuli?
      Life without problems never make a strong and good person!

    14. #14
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By Zipuwawa View Post
      kumshauri mtu miguu imelambwa na mbwa ni kazi bure

      Tehe! AU amekula miguu ya kuku lol
      Life without problems never make a strong and good person!

    15. #15
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By nipeukweli View Post
      uuuuwiii this coconut head!

      Watanzania tuna hasara kweli!
      Life without problems never make a strong and good person!

    16. #16
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By mtotowamjini View Post
      nyie watu ni bora kumuomba mchungaji asihubiri siku ya jumapili kuliko kumwomba JK asisafiri
      Kweli asee manake asiposafiri ataumwa ila bora kusema kuliko kunyamaza!
      Life without problems never make a strong and good person!

    17. #17
      BINARY NO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 555
      Rep Power : 488
      Likes Received
      141
      Likes Given
      64

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Aibu kwa Taifa km hili kuomba

    18. #18
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By King Kong III View Post
      Hiv hili swala halipo mahakamani kweli? Maana naogopa kuchangia nisije nikaingilia uhuru wa mahakama!
      Ngoja tumuulize Kova na Makinda !
      Life without problems never make a strong and good person!

    19. #19
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,371
      Rep Power : 36544
      Likes Received
      7503
      Likes Given
      4604

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Quote By BINARY NO View Post
      Aibu kwa Taifa km hili kuomba
      Yaani ni zaidi ya aibu......rasilimali tulizonazo tunawapa wageni wanaondoka nazo afu sie tunapeleka bakuli.....nahisi watakuwa wanatucheka sana ila ndiyo kama hivyo ukila na kipofu usimshike mkono!
      Life without problems never make a strong and good person!

    20. #20
      Msolopagazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th November 2010
      Posts : 492
      Rep Power : 532
      Likes Received
      49
      Likes Given
      19

      Default Re: Rais Kikwete punguza safari za nje

      Vasco da Gama wacha aendelee na uvumbuzi

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...