Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

    Report Post
    Page 1 of 10 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 196
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,613
      Rep Power : 46736
      Likes Received
      16712
      Likes Given
      8547

      Default Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

      Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

      Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

      SAY NO TO SERIKALI TATU!!

      Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com


    2. #2
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,660
      Rep Power : 4023
      Likes Received
      2943
      Likes Given
      5072

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Serikali tatu si zitaongeza ulaji zaidi maana kutakuwa na uwigo mpana wa kucheza kwa wale kina Drogba wa siasa za Tanzania? Well, ni ulaji tu kwa kwenda mbele!
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    3. #3
      Hercule Poirot's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Location : Mwisho wa Dunia
      Posts : 220
      Rep Power : 463
      Likes Received
      40
      Likes Given
      49

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      huo ndo maana ya muungano..tatizo la wenzetu tumeshawapatia/wamejipa vielelezo vingi vya kujitambua kama taifa huru..ni kiasi cha wao kujitangaza kama nchi tu basi.. Hapo ndio ugumu wa kuwaambia tuunde serikali moja unapokuja kwani wameshaonja tamu ya madaraka mjj

    4. #4
      Kakati's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th April 2009
      Posts : 119
      Rep Power : 542
      Likes Received
      11
      Likes Given
      13

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Tuwaulize watanzania na wazanzibari kwa kura ya maoni wantaka muungano wa namna gani. Hakuna lisilojadilika wala lisiloweza kubadilika. Mimi ningependelea serikali moja. Pia sijui kwa nini tunadhani serikali tatu zitakuwa na gharama, sio lazima. Inategemea tutakavyogawa madaraka na ukubwa wa vyombo tutakavyoviweka. Jamani hii ni nafasi ya kumaliza hili suala. Tutaendelea na mijadala ya kero za muungano hadi lini. Tuwe wakweli na wawazi. Hata kuvunja huu muungano sio tusi kama kama lengo litakuwa kuanza upya na kuwa muungano wa maana zaidi. Au kuwa na nafasi nzuri ya muungano wa eneo kubwa zaidi ulio imara EAC
      Development is unfortunately not about obeying law but refusing any traces of the unjust part of it.

    5. #5
      Communist's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,924
      Rep Power : 0
      Likes Received
      641
      Likes Given
      811

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      saddam likes this.


    6. #6
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,550
      Rep Power : 1065
      Likes Received
      1285
      Likes Given
      619

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Kwanza Mzee Mwanakijiji Muungano wa serekali tatu ni wazo la kinafiki kwa wasioutaka huo muungano kwa dhati kwani si tu gharama zitaongezeka bali tutakaribissha mivutano isiyokwisha na serekali ya muungano itakuwa inaelea tu juu kwa juu...

      I support you kuwa muungano wa kweli ni wa serekali moja....lazima kila mmoja akubbali kupoteza autonomy ndiyo sacrifice ya muungano vinginevyo ni kichekesho cha serekali mbili kitaendelea....moja ya wote na nyingine ya wachache....Umefika mda watanganyika tuamke sasa na tusimamie hili...ama serekali moja au kila mtu akusanye kilicho chake
      ....
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    7. #7
      MAMENGAZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 718
      Rep Power : 572
      Likes Received
      104
      Likes Given
      89

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Mkirua hata mimi nakuunga mkono, hapa hakuna cha serikali mbili wala tatu zitatuchanganya tuu, iwe serikali moja, kama haiwezekani basi Tanganyika ifufuke na Zanzibar waendelee na nchi yao

    8. #8
      Mzalendo JR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2012
      Posts : 911
      Rep Power : 536
      Likes Received
      277
      Likes Given
      213

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Serikali tatu mantiki yake ni nini hasa? Mgogoro utarudi tena juu ya nyadhifa katika serikali ya Muungano tena kwa kasi na muungano ndio unajifukia kaburini. Mi nadhani tuendelee na serikali mbili ila marekebisho makubwa katika mambo ya yautengenezao huu muungano.

      Kuna kero, ila kumbukeni hakuna serikali ya Tanganyika. Iundwe kwanza ili kuivunja serikali ya muungano kwani kwa sasa muungano upande wa Tanganyika ilibidi kuua serikali ya Zanzibar na kua na serikali moja tu kama Nchi moja. Hii haiingii akilini kua kuna SMZ na Muungano, huu muungano ni wa chi zipi? Currently ni SMS Vz Jamhuri? Did jamhuri exist befor muungano? SMZ existed and it exits, now where is Tanganyika?

      Kuwe na serikali MOJA tu ja MUUNGANO na si vinginevyo, au la Tanganyika kwanza.....
      "Happiness is what you think, what you say, and what you do are in harmony"

    9. #9
      Lubaluka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 473
      Rep Power : 608
      Likes Received
      22
      Likes Given
      19

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Kwa hilo Mwanakijiji nakuunga mkono...... Nisingependa kuona serikali tatu maana mbali na mzigo ni matatizo, migogoro na kero kila kukicha.... Hapo ni swala moja tuuu.. Muungano nchi moja (Tanzania) au kila mtu kivyake (Tanganyika & Zanzibar) full stop!!!!! no more... no less....
      Always The Silence of Our Friends Hurts more than the Noise of Our Enemy.

    10. #10
      JingalaFalsafa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2012
      Location : Africa.
      Posts : 352
      Rep Power : 432
      Likes Received
      229
      Likes Given
      89

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Serikali moja, Nchi moja, Taifa moja.
      Na hakuna maana nyingine ya MUUNGANO ZAIDI YA HIYO! Vinginevyo ni UNAFIKI UNAFIKI UNAFIKI MTUPU! Mianya ya migogoro kati yetu chanzo chake kikubwa ni kuwepo kwa "Union Affairs against Non-Union Affairs" sasa tuifute kabisa hii aidha kwa kuwepo kwa serikali moja, ama kuvunja kabisa kamuungano kakinafiki tulichonacho, No More Options! Tatizo tunanakilishwa kila kitu na wazungu, tuwe na namna yetu katika kuchambua na kufanya maamuzi yetu binafsi.
      Mungu wetu anaita!

    11. #11
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,823
      Rep Power : 0
      Likes Received
      565
      Likes Given
      295

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Hakuna suluhisho zaidi ya kuvunja muungano.
      Mikael P Aweda likes this.

    12. #12
      mlanguzi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 15th July 2012
      Posts : 181
      Rep Power : 385
      Likes Received
      10
      Likes Given
      0

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Quote By mzee mwanakijiji View Post
      tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

      Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (ccm na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

      Tuwasaidie zanzibar watoke kwenye muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

      Say no to serikali tatu!!

      Iambie tume ya warioba - hatutaki serikali tatu!!
      sioni mantikia ya hoja hii. Wabara karibu watapigana vita vya wenyewe kwa wenyewe. Washaanza chadema vs ccm.zanzibar hali shwari tusitake kuwaingiza zanzibar matatizo

    13. #13
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,351
      Rep Power : 1572
      Likes Received
      813
      Likes Given
      622

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Naomba na sisi tusioutaka muungano tupewe nafasi.

      Muungano ni ridhaa ya watu wahusika. Kama hiyo ridhaa haijawekwa hadharani kuwa tuliridhiana kuwe na Muungano basi ni batili.

      Kama hali ndiyo hiyo ya wimbo wa waasisi wa muungano, ipo nafasi nzuri tu ya kuyarejea hayo maridhiano na kuyatakari kama yanafaa au hayafai. Mara nyingi it is better to start from the beginning when and where there was Tanganyika and Zanzibar.

      Ni gharama nafuu sana kwa kila nchi kuwajibika na watu wake na rasilimali zake. Itatujengea kuheshimiana

      SAY NO TO IMPOSED MUUNGANO AND DISMENTAL IT.
      Ukweli utakuweka huru daima

    14. #14
      Mtanzania1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th December 2010
      Location : Kalenga, Liringa
      Posts : 992
      Rep Power : 627
      Likes Received
      125
      Likes Given
      94

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Mkuu Mzee Mwanakijiji hoja yako ni ya msingi sana lakini itakuwa ngumu sana kuietekeleza. nasema hivyo kwa sababu tumeshuhudia siku za karibuni watu wakiacha kazi za ujuzi na taaluma wakijiingiza kwenye siasa na hii yote si kwa sababu kwamba ni wazalendo sana bali walifanya hivyo kwa ajili ya matumbo yao (ni kazi inayoongoza kwa maslahi makubwa sasa nchini). Tumeshuhudia pia kuongezwa kwa mikoa na wilaya ambayo na hii yote imekuwa ni kutaka kuongeza wigo wa nafasi za kisiasa bila kujali hali za wananchi. Kwa sababu nchi hii maamuzi yote yanafanywa na wanasiasa kwa manufaa yao (kama kujiongezea posho wao na kuwanyima madaktari) utekelezaji wa jambo hili utakuwa mgumu sana kwa sababu unagusa maslahi ya watoa maamuzi (wanasiasa) na hawatakubaliana na hilo bila kujali itikadi zao za vyama.......wao watapendelea mfumo wa huu uliopo sasa au serikali tatu au kuuvuja muungano kwa sababu nafasi zao hazitaathirika sana ............. Hivyo kuendelea na hoja ya serikali moja kutaka kuuvunja muungano haraka sana.............na kama kwa miujiza ikiwezekana basi tutapiga hatua sana....matumizi ya uendeshaji yatapungua......wanasiasa wengi kama wahadhiri, waganga wa jadi, madaktari, wasanii, wahandisi nk watarudi kwenye kazi zao za ujuzi na taaluma kwani nadhani nazo zitaanza kulipa pia kwani keki ya taifa nayo itaanza kugawiwa kwa usawa
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      Ukifanya jambo la werevu utaitwa mwerevu, ukifanya jambo la kijinga basi utaitwa mjinga pia

    15. #15
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,512
      Rep Power : 14624
      Likes Received
      2344
      Likes Given
      1529

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      NO TO SERIKALI TATU!!
      Hatutaki serikali tatu!
      wala mbili! = moja
      Kaizer and Nguruvi3 like this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    16. Iza is offline
      Iza
      #16
      Iza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th January 2009
      Location : palipo na Internet
      Posts : 1,649
      Rep Power : 861
      Likes Received
      235
      Likes Given
      370

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Bara wananchi wengi wangependa kueendelea na muungano na hawa jamaa zetu, binafsi nilipenda serikali moja lakini kwa mambo yanavyokwenda haswa toka nimsikie Mama Karume...Tume ikifika nilipo ni mwendo wa kukataa muungano..

      Lakini pia tusaidiane katika hili,...inapotokea kwenye kura ya maoni kwakuwa na wingi wa watu bara wakataka serikali moja lakini huko visiwani wasitake hata huo muungano Let alone serikali moja...hapo itakuwaje? Je yatachukuliwa maoni kiujumla wake au ndo kama ilivyokuwa '92 kuhusu vyama vingi...
      Fikiria kwa u-makini...!

    17. #17
      MAMMAMIA's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 25th February 2008
      Location : Near You
      Posts : 3,794
      Rep Power : 3261
      Likes Received
      1496
      Likes Given
      1206

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano.
      Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!
      Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
      Hapo kwenye RED - Kuwakataza wananchi kujadili maslahi ya taifa lao ni KULAZIMISHANA na pia kung'ang'ania serikali tatu ni KULAZIMISHANA. Kwa nini kulazimishana huku? Kwa faida ya nani?

      Kuna waliotoa rai ya kura ya maoni, matokeo yake yatakuwa kwa kasima gani - Tanzania Bara 50+1 na Zanzibar 50+1 iwe ndio uamuzi wa wengi juu ya kile watakachoamua au Tanzania yote wakiamua 50+1 iwe ndio imepita?

      Kwa mtazamo wangu ni kuwa MUUNGANO UMESHAKUA KIROBA CHA MISUMARI, hakibebeki tena. Uamuzi wowote utakaoamuliwa sasa - iwe serikali 1,2,3...au kanda 7 au serikali 30 (yaani kila mkoa na serikali yake)...bado kero za Muungano zitazidi na hivyo kuzidi kutobebeka.

      Kwa maoni yangu, suluhisho pekee la kutatua kero za Muungano ni kuvunja Muungano.
      "JF - SAUTI YA WASIO NA SAUTI ............ na wapayukaji"

    18. #18
      Isalia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 486
      Rep Power : 482
      Likes Received
      76
      Likes Given
      0

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Kila mmoja ana mawazo yake kheri muungano uvunjike kuliko serekali moja na hilo halitokuwa maisha hata watanganyika wote wapige kura yakutaka serekali moja mtu anakuja eti z'bar inabebwa kwa lipi au kuwekwa makao makuu yote tanganyika ndio kubebwa na kupewa 4.5% katika pesa za muungano au kutopewa kabisa ndio kubebwa kama mmechoka kubeba kateni ubeleko

    19. #19
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2547
      Likes Given
      3632

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Tusikubali kwenda serikali tatu. Kwa vile tumekatazwa kutaka kuvunja Muungano - japo waliotukataza hawana uwezo huo - na kwamba tunaweza kujadili "muundo" bora wa Muungano. Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja". Haya mambo ya serikali mbili nchi mbili au serikali tatu nchi mbili hayaingii kichwani na ni jitihada za kujaribu kuibeba Zanzibar. Wakati umefika tudai uwepo wa serikali moja tu ya kitafa kwenye nchi moja.

      Ninafahamu kabisa matokeo ya watu wa bara kutaka hili. Jambo pekee ambalo tusikubali kuuziwa (CCM na upiinzani wanataka hili) ni serikali tatu. Serikali tatu ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba na wala hatupaswi kuubeba. Nawasihi wenzangu tukate kuongezewa mizigo. Tuwe na serikali moja, taifa moja na nchi moja. Sasa kama hili lina maana Zanzibar iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" na bara iwe "serikali moja, taifa moja na nchi moja" basi na iwe.

      Tuwasaidie Zanzibar watoke kwenye Muungano kama hawataki serikali moja kwani mbili hawataki na tatu tutajipa mzigo zaidi!

      SAY NO TO SERIKALI TATU!!

      Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
      Mwanakijiji,

      ..mimi nataka serikali moja, serikali ya Tanganyika.

      ..pia nitapendelea serikali hiyo iwe ndogo and more efficient than hii tuliyonayo.

      ..zaidi sitaki kusikia suala la serikali za majimbo huku Tanganyika. wanaotaka serikali za majimbo ndiyo hao hao wanaotaka muungano wa serikali 3. Ukizingatia kwamba wanataka tuwe na majimbo 10 then tunaelekea kuwa na jumla ya SERIKALI KUMI NA TATU.
      Nguruvi3 and Crucifix like this.

    20. #20
      Crucifix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 1,570
      Rep Power : 806
      Likes Received
      431
      Likes Given
      321

      Default Re: Muundo Bora wa Muungano: Wabara tudai "serikali moja, nchi moja, taifa moja"!

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      T Ninawasihi watu wa bara kudai "Serikali moja, taifa moja, na nchi moja".

      Iambie tume ya Warioba - hatutaki serikali tatu!!
      Hapo kwenye red umenikera hadi mwisho wa kukereka. Sisi sio wa bara; ni WATANGANYIKA!
      rogers26tz likes this.
      Jesus, Adoramus te. Dominus meus et Deus meus

    Page 1 of 10 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...