Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 50
    1. #1
      hippocratessocrates's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2012
      Posts : 1,493
      Rep Power : 2122
      Likes Received
      575
      Likes Given
      164

      Default MGOMO WA MADAKTARI TZ- Wana JF tuna maoni gani?

      Nianze kusema kuwa mimi ni daktari, na ningependa kwa pamoja tusio madaktari na madaktari tujadiliane katika uzi huu, si kwa kuonyesha hisia (hasira,matusi,kejeli n.k), kupoteza muda, kupotosha madai na taarifa na bali kwa kuona mapungufu ya chanzo cha mgomo kabla ya kujadili madhara yake, ili wote kama watanzania(na wasio watanzania pia) kuliweka sawa hili na kulisaidia Taifa.

      MADAI NA UFAFANUZI:
      -Uwajibishwaji wa watendaji wakuu wa W/Afya
      Ufafanuzi: Kutokana na ubadhirifu uliothibitika, hatua za kinidhamu zilipaswa kufuatwa.

      -Uboreshwaji wa Huduma za Afya katika hospitali.
      Ufafanuzi: Upatikanaji wa vifaa kazi, madawa na mazingira ya Hospitali ili kutoa huduma stahiki wa wagonjwa. Yaani
      Upatikananji wa vitendea kazimachine za upimaji moyo, kifua, sukari, uzito, urefu n.k), Mashine za Oxygen, vifaa vya kuongezea maji na damu mwilini n.k .
      Upatikanaji wa nyenzo(Machine kama vile CT Scan, MRI, Mashine za mionzi yaani X-ray, mashine za matibabu yaani mionzi ya kutibu saratani)
      Mazingira-Kuongeza vitanda, mashuka, huduma za chakula kwa wagonjwa wasio na ndugu n.k

      -Posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (Risk allowance) 30% au Chanjo
      Ufafanuzi: Katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuambukizwa Kifua kikuu(TB), Homa ya Ini (Hepatitis), UKIMWI (HIV/AIDS) tunapaswa kujikinga dhidi ya magonjwa haya tunapokuwa tukitibu wagonjwa na hivyo ni vyema serikali kutoa chanjo au isipowezekana kutoa chanjo na itoe posho tajwa kujikinga, mfano chanjo ya Homa ya ini pekee kwa mwaka ni mara 3 na inagharimu 45,000 (30USD) kwa kila chanjo.

      -Posho ya kuitwa kazini(On call allowance)-5%
      Ufafanuzi: Kisheria(Sina uhakika na kifungu), Muda wa kuitwa kazini au katika kada/sekta nyingine huitwa “Overtime” ni asilimia tano(5%) ya mshahara na hivyo, sheria ifuatwe katika hili.

      -Posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu(Hardship allowance)-40%
      Ufafanuzi: Si madaktari wote(yaani madaktari 1500) wafanyao kazi katika hospitali za serikali wanafanya kazi katika mazingira magumu bali, wachache hasa walio vijijini na hivyo, ili kuwapa motisha na kuonyesha njia ya motisha ili madaktari wasibaki mijini tu na hivyo kuwafanya waende vijijini ili kuepuka usumbufu wa wagonjwa kusafiri toka mkoahadi mkoa kwa matibabu, posho ya mazingira magumu itolewe kwa madaktari hawa walio vijijini na si wote.

      -Posho ya Usafiri(10%) au mkopo wa magari.
      Ufafanuzi: Kwa madaktari wale kukaa mbali na hospitali, wapatiwe posho hii au mkopo wa gari(NA PESA HII IKATWE KATIKA MSHAHARA). Hii ikiwa na maana daktari aliye zamu na anayeishi(mfano) bunju na kufanya kazi Muhimbili, au anayeishi Vikindu na kufanya kazi Amana, anayeishi kimara mwisho na kufanya kazi Temeke nk katika mikoa mingine anayetakiwa kufika usiku saa nane na hakuna usafiri anaweza kufika kwa wakati.

      -Posho ya makazi (30%) au kupatiwa nyumba.
      Ufafanuzi: Kisheria (“Doctor is equal to high government officer and is entitled to a house”).Nitapokuwa na vifungu vya sheria nitathibitisha hili. Na kwa kuwa jambo hili lipo kisheria basi na sheria ifuatwe(na ndio Seriakali ilisema inajenga nyumba 700 za madaktari), lakini isipowezekana kwa daktari kupatiwa nyumba(kwa ambao hawana) basi posho ya asilimia 30% itumike kama mbadala.

      -Wafanyakazi wote wa Sekta ya Afya wapewe kadi za kijani za bima ya Afya.
      Ufafanuzi: Kwa wafanyakazi wa sekta ya Afya yaani madaktari, wauguzi, wafamasia, watu wa maabara, nk. Wapewe bima za Afya wakipata huduma sawa na ile wanayotoa.

      -Pendekezo la mshahara kuwa mil. 3.5/=kwa mwezi.
      Ufafanuzi: Kama vile mishahara katika Serikali inavyotegemea
      *Muda wa masomo wa fani.
      *Kiwango cha elimu.
      *Ugumu wa masomo wa fani husika.
      *Ugumu wa kazi.
      *Muda unaotumika kazini.
      Hivyo kwa kuzingatia haya, pendekezo la mshahara tajwa utolewe kwa madaktari lakini kama ikishindikana basi Mwajiri(Seerikali) na itoe pendekezo lake.

      MAKOSA:
      Jumla ya madaktari wote katika hospitali zaSerikali ni 1500, hii ikiwa ni takwimu ya Wizara ya Afya yam waka 2011 na ikijumuisha zaidi ya madaktari 300 waliofukuzwa na 150 waliokwenda nje tayari hadi leo trh 17.07.2012. Hivyo tafsiri iliyotumika ni ;
      -Daktari hayuko entitled kupata nyumba kama high government official kama ilivyoainishwa kisheria
      -Daktari hatakiwi kulipwa overtime (call allowance)mara baada ya muda wa kazi kwa aslimia tano ya mshahara
      -Tafsiri ya kuwa madaktari wote huwa wanakuwa zamu za usiku (overtime) na hivyo kuwekakiasi cha posho tajwa juu kuwa ya madaktari wote na kila siku!
      -Tafsiri ya pesa ya mazingira magumu kwa madaktari wote(KWANI SI MADAKTARI WOTE WAKO MAZINGIRA MAGUMU YA VIJIJINI)
      -Tafsiri ya kutaka posho ya mazingira hatarishi pekee badala nyenzo za kujikinga na chanjo
      -Tafsiri kuwa wafanyakazi wengine wa sekta ya afya hawakujumuishwa katika madai.
      -Tafsiri ya pendekezo la mshahara tajwa kuwa ni SHURUTI ya kurudi kazini.
      -Tafsiri ya kuwa PENDEKEZO la mshahara haliwezi kupungua!
      Last edited by hippocratessocrates; 18th July 2012 at 14:51.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Ninaweza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2010
      Location : bukonda moyo
      Posts : 2,163
      Rep Power : 869
      Likes Received
      315
      Likes Given
      719

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Selikalini hajabakiwa mtu mwenye hekima wala busara, wanasubiri msaada wa watu wa marekani kutatua mgogoro huu.

    4. #3
      Nyakageni's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,248
      Rep Power : 0
      Likes Received
      769
      Likes Given
      52

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      i tried to be a doctor and failed, sasa nawaheshimu tu!

    5. #4
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Hii mijadala bado inaendelea?

      Vipi hali ya Ulimboka? hajambo?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    6. #5
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,687
      Rep Power : 1913
      Likes Received
      1583
      Likes Given
      676

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Quote By zomba
      Hii mijadala bado inaendelea?

      Vipi hali ya Ulimboka? hajambo?
      Mkuu jikite kwenye hoja hiyo hapo juu suala la ulimboka halikuhusu tokea Jana unaulizia mbona sisi hatukuulizi kuhusu kugomea sensa

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Chibenambebe's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th March 2012
      Posts : 118
      Rep Power : 384
      Likes Received
      18
      Likes Given
      2

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Hali tutegemee kuwa mbaya zaidi kwa kipindi kifupi kijacho kwa sababu waliotangulia kuondoka hakika wamekwenda kuwaandalia wenzao makao hivyo wengi najua watafuata.

    9. #7
      RGforever's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2011
      Posts : 2,089
      Rep Power : 1131
      Likes Received
      413
      Likes Given
      105

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Inauma sana daktari anauwezo wa kumtibu mgonjwa halafu hana kifaa....

    10. #8
      Shine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 9,180
      Rep Power : 2428
      Likes Received
      944
      Likes Given
      377

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Quote By Ninaweza
      Selikalini hajabakiwa mtu mwenye hekima wala busara, wanasubiri msaada wa watu wa marekani kutatua mgogoro huu.
      Sijui na lile sakata la meli za iran kutumia bendera ya Tz likinuka serikali ndo itahamia wapi kuombaomba?

    11. #9
      Ronal Reagan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 2,630
      Rep Power : 959
      Likes Received
      615
      Likes Given
      256

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Hippo,
      Tuliwaelewa na kuwanunga mkono toka zamani tu. Hoja zenu nyingi zina mantiki na mashiko na serikali badala ya kujibu hoja kwa hoja ikaishia kwenye siasa mbuzi na vitisho.

      Kukosekana kwa daktari kunahatarisha afya na pengine kusababisha kifo, lakini je! kukosekana kwa mwanasiasa kuna madhara gani? Na nini tija yao (wanasiasa) ikiwa nchi imeuzwa, hali ya uchumi ni mbaya, dhuluma na ufisadi vimeongezeka?

      Yet they fetch 10m per month + unlawful allowances to icing their daylight robbery.

      I prefer to have doctors than silly politicians in my team
      Simplicity. and Malekelo like this.

    12. #10
      Simplicity.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th August 2011
      Posts : 494
      Rep Power : 491
      Likes Received
      70
      Likes Given
      68

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Madai yalieleweka na yanaeleweka. Sasa jinsi ulivyoandika hapo serikali haikuelewa nini? siasa uchwara wanazozifanya zitawatokea puani.

    13. #11
      MWAKIKALI's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th June 2012
      Posts : 13
      Rep Power : 352
      Likes Received
      4
      Likes Given
      4

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Nchi nyingi zilipata ukombozi wa kweli baada ya uonevu wa kiwango cha juu kwa wananchi uliofanywa na serikali, ukisoma historia ya ufaransa na mfalme louis, baadhi ya nchi za kiarabu africa. Na tanzania uhuru wetu upo jirani zaidi ya ilivyotabiriwa. Thanx god, nimeishi kuuona ukombozi wa kweli wa taifa letu, nakupenda tanganyika.

    14. #12
      hippocratessocrates's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2012
      Posts : 1,493
      Rep Power : 2122
      Likes Received
      575
      Likes Given
      164

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Sidhani kama kulikuwa na dai lisilo na umuhimu, kama pande zote mbili zingejishusha na kwa busara kubwa kutatua mgogoro kwa kusikiliza madai lakini kama tungejifunza "to priotize our priorities"..na katika hili huduma bora na za msingi zifanyiwe kazi kwa uharaka na kisha madai mengine..

    15. #13
      Makene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,185
      Rep Power : 671
      Likes Received
      206
      Likes Given
      155

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      imesemwa kila mara kwa madai ya madaktari wao si wafanyakazi pekee.
      Hii ina maana tu iwapo serikari itathibitisha ya kwamba polisi wanalazimika kulinda maandamano kwa fimbo na si silaha za moto, walimu wanaweza kufundisha bila chalk,na kupima matokeo ya kazi yao bila mitihani kwa wanafunzi wao, hata wakulima wa jembe la mkono ndio wenye hali njema kiuchumi na wanaweza kulima bila mbolea na mbegu bora.
      Serikari haina uwezo wa kufilisika, kwa maana ya kuacha ufahari na kuweka matabaka.
      Serikari inatimiza andiko, mwenye hana hata kidogo alichonacho atanyanganywa.

    16. #14
      hippocratessocrates's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2012
      Posts : 1,493
      Rep Power : 2122
      Likes Received
      575
      Likes Given
      164

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Mkuu Makene umenena, ni kweli wengi tunahalalisha ubaya kuendelea kutokea kwa sababu ya ubaya mwingine utaofanyika sehemu nyingine, kwa kusema tu madaktari si wanyakazi pekee na wakati toka uhuru hadi leo TZ yetu ina madaktari 1500 tena wengine wakiwa wamehamia na kuendelea kuhamia sekta binafsi, kuhama nchi na wengine wakifukuzwa..sijui kama hatuoni kama tunaleta chuki na kinyongo kwa wale wachache wanaobaki!

    17. #15
      hippocratessocrates's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2012
      Posts : 1,493
      Rep Power : 2122
      Likes Received
      575
      Likes Given
      164

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Brain drain???

    18. #16
      hippocratessocrates's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2012
      Posts : 1,493
      Rep Power : 2122
      Likes Received
      575
      Likes Given
      164

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      brain drain has peaked up,,,

    19. #17
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 484
      Rep Power : 669
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Serekali haijui kwamba inafanya battle na the cream of tanzanian education..!

    20. #18
      Wanitakiani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th April 2008
      Posts : 632
      Rep Power : 698
      Likes Received
      129
      Likes Given
      20

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Natamani Watanzania wote wangesoma huu uzi. Bahati mbaya wanasiasa wamewekeza kwa Watz wengi walio wajinga na wasio na upeo wa kupambanua mambo. Madai ya madaktari ni kwa ajili ya kuwanusuru watz wenzao lkni hoja imepotoshwa. Inasikitisha sana!
      Laughing Faces Do Not Mean That There Is Absence of Sorrow! But it Means That They have The Ability to Deal With It!

    21. bdo
      #19
      bdo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2006
      Posts : 892
      Rep Power : 886
      Likes Received
      140
      Likes Given
      73

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Quote By zomba
      Hii mijadala bado inaendelea?

      Vipi hali ya Ulimboka? hajambo?
      unaumia sana maana hadi sasa hujasikia habari mbaya ya afya yake
      Last edited by bdo; 19th July 2012 at 01:51.

    22. #20
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,084
      Rep Power : 12251
      Likes Received
      6014
      Likes Given
      6851

      Default Re: Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari.

      Quote By zomba
      Hii mijadala bado inaendelea?

      Vipi hali ya Ulimboka? hajambo?
      dogo.... i am sure kuna wakati you read what you write or listen to your inner self and realize that you are sitting on a glass sofa

      jah bless your intelligence as time goes by....

      brotherly advice
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...