Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 35
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,141
      Rep Power : 3542
      Likes Received
      3032
      Likes Given
      460

      Default Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?




      Na Joster Mwangulumbi - Imechapwa 11 July 2012

      ULIMBOKA ni neno la Kinyakyusa lenye maana ya Mungu uniponye. Neno hilo ndilo linatumika kama jina na ukoo wa Dk. Steven.

      Mtu akiwa kwenye matatizo, shida, mashaka au mateso huomba huruma ya Mungu amponye. Kwa huruma na upendo, Mwenyezi Mungu ndiye aliwashika wasamaria wema, kwa mkono wake wa miujiza, akawaongoza, bila kujijua kwenda kumwokota na kumfikisha hospitalini Dk. Steven Ulimboka aliyepigwa na kutupwa katika msitu wa Mabwepande akaachwa afe.


      Mungu aliyewaongoza wasamaria wema kumwokoa na kumfikisha Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha mifupa (MOI), ndiye amemtia nguvu, anazungumza sasa kwa ‘ufasaha’ alivyopigiwa simu na ofisa wa ikulu, alivyotekwa, alivyoteswa usiku kucha na alivyookotwa.


      Hivi sasa anapata matibabu katika hospitali moja nchini Afrika Kusini, akisubiri ubuponyi yaani uponyaji kamili kutoka kwa Mwenyezi Mungu mwenyewe.

      Katika mkanda wa mahojiano maalum akiwa MOI, Dk. Ulimboka haachi chembe ya shaka kwamba mkasa huo ulipangwa na kuratibiwa na kikosi maalum cha ‘mauaji’ ambacho kina maslahi na mgomo wa madaktari ambao umedumu kwa wiki tatu sasa.

      Sehemu ndogo ya maelezo ya Dk. Ulimboka ni kama ifuatavyo….

      …Kazi yao ilikuwa siyo kufanya kazi kama askari, eeh its like they acted under instructions.

      Eeh, yaani unajua, kwa muda kama siku tatu mfululizo, huyu bwana alikuwa anajaribu kuwasiliana na mimi lakini kwa bahati mbaya ratiba yangu ilikuwa haiwezekani kumwona.


      Nilishawahi kumwona zamani, kwenye mgogoro ule mwingine, lakini this time of course alikuwa serious akinitafuta akisema kwamba anataka some hearing ili aweze kushauri. Huyu bwana anafanya kazi ikulu.


      Aah, mimi kwa sababu namfahamu kutokana na incident ya kwanza sikuwa na muda. Lakini jana aka-insist sana na akakaa Hugo pale muda mrefu sana, sisi tulikuwa tumekaa Leaders Club.


      Baadaye nikamwambia Deo kuna jamaa mmoja – ambaye Deo anamkumbuka sana kwa sababu mara zote huwa tunakwenda naye – anataka kutuona. Basi tukawaacha wenzetu wanafanya kazi nyingine, tukaondoka mimi na Deo around saa tano, ilikuwa na robo (5.15).


      Naye akatuarifu kuwa pale Hugo alipokuwa amekaa wanafunga, akawa ameenda kule juu sehemu inaitwa Stereo, akaniambia yupo pale. Mimi nikawasha gari hadi pale, nikaangalia meza ya kwanza pale sikumwona. Tulipoingia pale hatukumwona.

      Nikazunguka sikumwona, nikampigia simu akaniambia, nakuja hapo sasa hivi.


      It took like twenty to thirty minutes tangu aliposema anakuja. Tukaamua kuwasha gari ili kurudi pale Leaders lakini tukaona kama hilo haliwezi kuwepo. tukaishia pale Tunisia Road kuna kontena, tukakaa pale. Sasa akawa anapiga simu akisema anakuja kuna vitu anamalizia; tukawa tunawaza ni vitu gani?


      Basi tukiwa tumekaa, ghafla tukamwona anafika, kwa gari. Akasema uko na Deo, nikasema eeh. Basi tukaanza mazungumzo.


      Kitu ambacho nili-notice, while tukiwa tuna-discuss naye, akitaka kujua namna gani tuweke understanding; matatizo yetu ni yapi, which are the priority areas, eeh kama alivyosema yeye mwenyewe ili aweze ku-advise, kwa sababu wakati mwingine…


      Sisi tukasema mambo yote yanafahamika. Tukaongea naye kwa muda mfupi tu, akawa anaandika kwenye diary yake, kwa hiyo pia alikuwa very bussy communicating, unaona.


      Kwenye simu yake sasa, tukafika kwamba tumemaliza. Ila sisi tulikuwa tuna vinywaji kwa sababu ilikuwa siyo rahisi sana tumwache yeye aondoke sisi tuendelee kubaki. Yeye alikuwa anakunywa maji akasema bwana mi naondoka.


      Kwenye ile line ya yeye kusema anaondoka tu, hapo hapo wakatokea watu kama wanne watano hivi, wakasema, wakaja straight kwenye meza yetu, as if they were directed. Wakasema upo chini ya ulinzi, yaani mimi hapa. Kama mtu hakujui hawezi kuja saa 5 usiku kuja kukukamata.


      They came direct towards me, nikauliza kwani kuna kosa gani? Wakanipiga mtama nikaanguka barabara ya lami. Nilichokifanya kitu cha kwanza ni kutoa simu na kumpa Deo. Sasa they pushed me na kufanikiwa kuchukua simu moja na wallet yangu.


      Nilichowahi ni kuchomoa simu yangu kumpa Deo. Wakaniburuza huku wakini-push again na kuvuka barabara hadi kwenye gari ile, ilikuwa haina namba ile, ni kama Starlet hivi. Nikaamua tu kubaki patient.


      Wakafungua lango la nyuma wakanitupa huko. Wakaja wakanitupa huko. Basi mmoja akaingia upande wangu wa kulia mwingine wa kushoto. Wakaanza kunipiga ngumi, wakanipiga ngumi; mwingine akanipiga vichwa, naona, wengine wana kama dude fulani kama la plastiki hivi, wananipiga kichwani. Wananiambia tulia tutakuua sisi. Kama una ndugu zako aga kabisa kwa sababu leo hurudi.


      Unatuletea usumbufu sana wewe… sasa nikawa najiuliza usumbufu gani? Kwa sababu hata hapo usumbufu, wewe unajua unachokifanya kwa hiyo tunataka kukomesha hiyo tabia. Wakanipiga kwenye gari hiyo huku inakwenda, ilikuwa inaenda mwendo wa kasi sana. Nikafanikiwa kuchungulia hivi nikagundua tuko maeneo ya Victoria…

      …Hata na ile miguu wakafunga sana. Basi wakaendesha gari, wakaendesha this time muda mrefu sana. Sikuwa najua wanaenda wapi. Walipokuja kunishusha, wakaanza kunipiga tena.

      Sasa kwa sababu I was helpless nimefungwa, basi nikawa napigwa nageuka hivi, nikigeuka hivi, nikaona wananipiga kwa sikio la huku, wengine wakawa wananipiga sikio la huku walinipiga sana kama half an hour hivi, and then I think I lost consciousness.


      Unaona na nilikuwa na-bleed sana wakati ule. Kwa hiyo nilichofanya nikawa napata feelings hawa watu they are carrying me somewhere.


      Nikafika mahali nikaona kama vile wamenitupa kwenye shimo hivi. Sijui kama wanataka kunifukia? Unaona, nikawaambia why I are you burring me alive?...

      Katikati ya mateso kama aliyopata Dk. Ulimboka kuna uponyaji. Kwa kuteswa kwake Yesu Kristo binadamu wamepona (biblia).

      Kwa kujichoma moto, mmachinga wa Tunisia baada ya mgambo na polisi kuvuruga biashara yake, nchi nzima iliwaka moto na Watunisia wakapata demokrasia.

      Kutokana na maandamano katika viwanja vya Tahrir na serikali kujibu kwa risasi, Misri iliwaka moto, hatimaye imefanya uchaguzi huru.

      Watu wote wasio na hofu ya Mungu, ndio wanaweza kujisikia raha kuteka watu wasio na hatia na kuwatesa, wakati mwingine, kwa kufurahia vipande vya fedha.


      Yuda Isikarioti alifurahia vipande 30 vya fedha kwa kazi ya kumsaliti Yesu. Aliishia wapi? Kwa kuteswa kwake Dk. Ulimboka, Mungu atawatia adabu walioratibu mpango huo.





    2. Study Abroad

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,141
      Rep Power : 3542
      Likes Received
      3032
      Likes Given
      460

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Tahrir = ? then Ulimboka?

    4. #3
      Richard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2006
      Location : LANGLEY
      Posts : 2,224
      Rep Power : 1087
      Likes Received
      482
      Likes Given
      1645

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Nilimsahau Deo, ntamuongeza kwenye orodha ya wahusika wakuu kule kwenye ile movie inayotayarishwa yaitwa "Mabwepande and The Wrath of Pliers".
      Jasusi likes this.
      When thinking about my risk assessment, I always remember:
      HAZARD and the RISK .

    5. #4
      kadoda11's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : planet earth
      Posts : 1,375
      Rep Power : 699
      Likes Received
      349
      Likes Given
      183

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      picha linaendelea......
      "The only true wisdom is in knowing you know nothing"

    6. #5
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? ataendeleza migomo? vipi huyu alikuwa chadema?

      Nasikia kuna kada wa CCM kauliwa Singida, vipi? mnasemaje kuhusu hilo?
      Richard likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,607
      Rep Power : 2889
      Likes Received
      3822
      Likes Given
      12192

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      Vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? ataendeleza migomo? vipi huyu alikuwa chadema?

      Nasikia kuna kada wa CCM kauliwa Singida, vipi? mnasemaje kuhusu hilo?
      Go to hell!

    9. #7
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,146
      Rep Power : 1527
      Likes Received
      754
      Likes Given
      590

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      Vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? ataendeleza migomo? vipi huyu alikuwa chadema?

      Nasikia kuna kada wa CCM kauliwa Singida, vipi? mnasemaje kuhusu hilo?
      Zombie ni kitu kisicholewa kitu kwa sababu ya hali yake kwa kukosa utimilifu wa kibinadamu
      Ukweli utakuweka huru daima

    10. #8
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,059
      Rep Power : 12246
      Likes Received
      6010
      Likes Given
      6835

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? Ataendeleza migomo? Vipi huyu alikuwa chadema?

      Nasikia kuna kada wa ccm kauliwa singida, vipi? Mnasemaje kuhusu hilo?
      nagombea ubunge kilwa kupitia ccm naomba sapoti yako
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    11. #9
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By Mimibaba
      Zombie ni kitu kisicholewa kitu kwa sababu ya hali yake kwa kukosa utimilifu wa kibinadamu
      Kweli mimi silewi. Jamani mpaka ulewe ndio uwe na "utimilifu'? huo ni ukosefu wa maadili.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    12. #10
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By TIMING
      nagombea ubunge kilwa kupitia ccm naomba sapoti yako
      Timing ikikaa sawa tutakupigia debe, usiwe na shaka.
      TIMING likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    13. #11
      Mimibaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2009
      Posts : 3,146
      Rep Power : 1527
      Likes Received
      754
      Likes Given
      590

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      Kweli mimi silewi. Jamani mpaka ulewe ndio uwe na "utimilifu'? huo ni ukosefu wa maadili.
      Kwani wewe ni Zombie?
      Ukweli utakuweka huru daima

    14. #12
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By Jasusi
      Go to hell!
      Kwi kwi kwi teh teh teh! Ya ngapi?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    15. #13
      Baba V's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Location : Buguruni Mnyamani
      Posts : 10,723
      Rep Power : 30185
      Likes Received
      4616
      Likes Given
      3477

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Watashindana naye, hawatashinda!!, ndo wanazidi kujitengenezea anguko

    16. #14
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,663
      Rep Power : 1907
      Likes Received
      1561
      Likes Given
      676

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      Vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? ataendeleza migomo? vipi huyu alikuwa chadema?

      Nasikia kuna kada wa CCM kauliwa Singida, vipi? mnasemaje kuhusu hilo?
      Kada wa ccm? Unamuuliza nani hapa jamvini? Nenda lumumba

    17. #15
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,644
      Rep Power : 4014
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      Vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? ataendeleza migomo? vipi huyu alikuwa chadema?

      Nasikia kuna kada wa CCM kauliwa Singida, vipi? mnasemaje kuhusu hilo?
      Hizi siasa za maji taka zinatupeleka wapi? Uhuni unaingizwa kwa makusudi kwenye siasa. Ipo siku tutakosa wote maana haitawezekana kufungana. Kwanini tusihimizane kutafuta maendeleo tunahimizana kumalizana kisiasa tu? kama leo ntaambiwa niiongoze system, economic intelligence would be my first priority...watu wakila na kushiba hakutakuwa na kelele za hovyo za kisiasa
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    18. #16
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By Precise pangolin
      Kada wa ccm? Unamuuliza nani hapa jamvini? Nenda lumumba
      Jibu ya Uli basi au hata hayo niende Lumumba?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    19. #17
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,663
      Rep Power : 1907
      Likes Received
      1561
      Likes Given
      676

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By zomba
      Jibu ya Uli basi au hata hayo niende Lumumba?
      Kwani jack zoka na Ahmed Msangi wanasemaje iwapo ataendelea na mgomo?

    20. #18
      Kasimba G's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 852
      Rep Power : 592
      Likes Received
      252
      Likes Given
      265

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Nisha jua real id ya huyo zoba!

    21. #19
      PakaJimmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 14,678
      Rep Power : 22518
      Likes Received
      6327
      Likes Given
      2831

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Hii story ya Ulli inaingia moja kwa moja katika 'lane' ya kumbukumbu mbaya kabisa za taifa hili chini ya JK. SOON waliomtesa watamwona mtaani, si katika hali waliyomwacha nayo pale Mabwepande, bali ktk hali mpya na ya uzima tele.

    22. #20
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Msaliti wa Dk. Ulimboka yuko ikulu?

      Quote By Precise pangolin
      Kwani jack zoka na Ahmed Msangi wanasemaje iwapo ataendelea na mgomo?
      Kwanza jibu maswali yangu halafu uulize lako. Ngoja nikukumbushe:

      Vipi hali yake, hajambo> anarudi lini? ataendeleza migomo? vipi huyu alikuwa chadema?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    23. Miaka 50
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...