Re: Hivi daktari ana thamani kuliko binadamu wengine??? POLISI NA JESHI WAKIGOMA ITAKUWAJE??

By
chilisosi
Naomba mnijibu jamani, kwa nini hawa madaktari wantumia uhai wetu kuomba nyongeza ya mshahara
Kwani wao ni bora kukliko hawa wafuatao
POLISI
WANAJESHI
WALIMU Nk
Daktari alipwe shs 10,000,000 halafu mwalimu aliyemfundisha alipwe laki nne??
Halafu wanatumia kisingizio cha huduma bora kudai mihela.
Hebu nisaidieni mawazo yenu
Kuwa mkweli; Tanzania siyo nchi ya kijamaa tena, kwa hiyo kila kazi inalipwa kulingana na thamani yake. Iwapo unajua kuwa uhai wako unategema hao madakatari, basi walipe vizuri kwani kwa tamko hilo ni kukiri kuwa taaluma yao ni ya muhimu. Iwapo unaamni taaluma ya daktari siyo ya muhimu, na hivyo uhai wako hauhitaji taaluma yao basi usillamike wanapogoma. Hebu fikiria tena iwapo wabunge watagoma hata kwa mwaka mzima, je utaathirika vipi?
Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo
Follow Us Here