Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

    Report Post
    Page 10 of 16 FirstFirst ... 89101112 ... LastLast
    Results 181 to 200 of 304
    1. #1
      n00b's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2008
      Posts : 768
      Rep Power : 9825
      Likes Received
      1442
      Likes Given
      166

      Default JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Tanesco, Robert Mboma amekataa kuhudhuria mkutano wa waandishi wa habari unaotarajia kumsimamisha kazi mkurugenzi mtendaji wa Tanesco, William Mhando.

      Uamuzi wa kumsimamisha kazi Mhando unatokana na bifu linalosemekana kuwapo kati ya Mhando na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi; lakini katibu mkuu huyo ametumia udhaifu wa serikali na tanesco kumwadhibu Mhando.

      Inasemekana sababu inayotolewa na Katibu Mkuu ni kwamba Mhando alimdharau kwa kutompa taarifa kabla ya Tanesco kutangaza mgawo wa umeme wa hivi karibuni. Kwa mantiki hiyo, akamlima Mhando barua akisema anahujumu shirika. Hata hivyo, wananchi na watumishi wa Tanesco wanajua kuwa anayehujumu Tanesco ni serikali, ambayo inalinyima shirika hilo pesa ilizoahidi kwa ajili ya miradi ya uzalishaji na usambazaji wa umeme, na kulizuia shirika hilo kuuza umeme kwa faida, kwa sababu za kisiasa.

      Inasemekana hatua dhidi ya Mhando inatokana na woga wa waziri na katibu mkuu juu ya mjadala mkali unaotarajiwa kuibuka bungeni wakati wa kujadili bajeti ya wizara yao. Mhando anatolewa kafara kisiasa, lakini taarifa zinasema naye amejibu barua ya katibu mkuu kueleza jinsi asivyohujumu shirika hilo. Habari zaidi baadaye.

      source east africa radio breaking news

      Breaking news:mkurugenzi mtendaji wa tanesco william mhando asimamishwa kazi


      Bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mhandisi WILLIAM MHANDO (pichani) ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa dhidi ya Menejimenti ya TANESCO.

      Taarifa hiyo imetolewa na mwenyekiti wa bodi hiyo Jenerali Mstaafu ROBERT MBOMA ambapo katika taarifa yake amesema maamuzi hayo yamefikiwa katika kikao cha dharura kilichofanyika jana kujadili masuala mbalimbali ikiwemo tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.


      Taarifa zinasema katika kikao hicho, Bodi iliona tuhuma hizo ni nzito hivyo ni vyema zikafanyiwa uchunguzi huru na wa kina mara moja
      KWA HABBARI KAMILI BOFYA HAPA
      I seriously mean it when I say, 'Get a life'

    2. Miaka 50

    3. #181
      satellite's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th November 2010
      Location : HOMELAND SECURITY
      Posts : 546
      Rep Power : 541
      Likes Received
      94
      Likes Given
      60

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Mhoja
      Si vizuri kudisplay secrets letters bila ya kuzidowngrade. Secret information ni muhimu kwa usalama wa taifa. Je ni nani aliyezidisclose hizo barua?
      Kaka hapo usalama wa taifa upi unaouzungumzia?hapa hakuna cha kuficha kwenye maslahi ya taifa yaaani unapenda nchi iwe gizani?

    4. #182
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By SOLOMO
      Haya yote ni masuala ya UMIMI! Huyo Katibu Mkuu anasema umeme unakatwa wakati wa BUNGE, anamaanisha nini!? yaani Mhando angekata Umeme wakati BUNGE halipo katika vikao vyake ingekuwa sawa? Tutaona mengi sana Tanzania. Njia ipo lakini namna ya kufikia njia hiyo ndio kimbombo! the problem is on the system and not personalities!
      Anasema ni hujuma na ndio akakata wakati wa bunge na si kwamba bunge likiwa halipo ndiyo iwe sawa. Msome vizuri.

      Kama si hujuma hayo mafuta aliyapata wapi baadae? Huyo Mhando inamaana aliwaambia kabisa kateni na wao wakobungeni na ndipo watakapo zitowa pesa mbio mbio, akili yake yote ilkuwa kwenye 10% na wala si kwenye kuwatumikia Watanzania.
      Last edited by zomba; 15th July 2012 at 16:59.
      NasDaz likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    5. BAK
      #183
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,633
      Rep Power : 44971
      Likes Received
      8386
      Likes Given
      8363

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Mhoja
      Si vizuri kudisplay secrets letters bila ya kuzidowngrade. Secret information ni muhimu kwa usalama wa taifa. Je ni nani aliyezidisclose hizo barua?
      Hivi kuna usalama wa Taifa nchini mwetu? Unafanya kazi zipi, tangu lini na kwa faida ya nani?
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    6. #184
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By mwanza
      yaani kitendo cha kukatika umeme bungeni ilikuwa ni aibu kubwa sana,Mhando alitakiwa kulijua hilo hata ikiwezekana kujaza maji kwa ndoo ilimradi umeme upatikane. tatizo hilo ndio linaonekana dharau na kuihujumu serikali.
      Mkuu Mwanza, kiukweli nimecheka nilipoisoma hii!, haswa hii ya ikibidi kujaza maji kwa ndoo!.

    7. #185
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Tutafika
      Tanesco ni "roho" ya serikali. Inabeba uchumi wa nchi, inabeba usalama wa taifa! Haiwezekani kwa mtu mwenye akili timamu akaweka "roho" ya serikali mikononi mwa mfanyabiashara! Kwa mtetezi wa ccm kama wewe kutoa maoni haya, unadharirisha chama!

      Kinachotakiwa serikali izalishe umeme na itoe huduma kwa wananchi kama inavyotoa huduma ya ulinzi (polisi, JWTz). Kinachoweza kushindikana ni nini?

      Hapa simaanishi huduma iwe 100% bure kama ulinzi ulivyo, (hasa kipindi hiki ambapo hatuna fedha ya kutosha) bali kuwe na kiwango cha umeme ambacho ni basic kwa kila mtu kitolewe bure, watu walipie matumizi ya ziada!

      Kwa mantiki hii, tanesco iwe wizara kamili na iendeshwe kwa kodi zetu!
      Kwanza hiyo niliyokuwekea nyekundu badilisha sio kiswahili sahihi kuandika namna hiyo.

      Halafu uelewe kuwa usalama wa taifa ni jukumu la kila raia hata huyo Mhando ni raia na sasa anashutuma za hujuma kwa serikali. Kwa hiyo usiniambie kuwa Bakhresa hana uwajibikaji kwa usalama wa taifa hili.

      Kuna vigezo vya "security clearance" kwa kila sehemu na unyeti wake na anaweza kuchambuliwa na vigezo hivyohivyo vilivyotumika kumchambuwa Mhando na kumuweka sehemu nyeti halafu akawa hafai kuiendesha kwa tuhuma za hujuma. Bakhresa leo hii anaendesha shughuli nyeti zaidi ya Mhando, anauza chakula Tanzania na Afrika Mashariki nzima. Huoni unyeti wake kiusalama? licha wa taifa wa kimataifa. Mhando ana kigezo gani cha kuwa ana ubora wa usalama wa taifa zaidi ya Bakhresa? kuwa makini kidogo.
      Last edited by zomba; 15th July 2012 at 17:19.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    8. RukaaJuu Final

    9. #186
      Nteko Vano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2012
      Location : Dar es salaam
      Posts : 428
      Rep Power : 450
      Likes Received
      90
      Likes Given
      26

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Mtoto wa Kishua
      Leo kwa mara ya kwanza nimetambua kwamba , utetezi mwngi humu ni wa majungu na kutotambua facts za kila kinacho zungumzwa,nadhani sitaamini chohocte kinacho jadiliwa humu. Kwa mimi niliye fanya kazi na Mhando naweza sema, ni mhujumu mkubwa wa nchi hii na hafai na kama atatolewa ni jambo kubwa sana katika kuendeleza nchi hii katika masuala ya nishati ya umeme. Huyu mtu asikilizi mtu, wala hana muda wa kufanya kazi zaidi ya kusafiri na kukwepa wageni na wawekezaji wanao kuja kwa nia nzuri ya kuwekeza.KUna project nyingi zilikuja kwa ajili ya kuokoa hilo shirika lakini hakua na muda zaidi ya kukwepa nakukimbia officini huku shirika halina pesa. Kitendo chake cha kufanya mamamuzi bila kumshirikisha Katibu mkuu ni kutokana na yeye kutamba kwamba kapewa rungu na raisi ,kwa hiyo hakuna mtu naweza mgusa, baada ya raisi kumuamini huyu jamaa. Hakuna bifu ni kubweteka kwa huyu Mhando na ni janga la taifa kama atarudishwa hapo.
      Ninachofahamu mimi hata akisafiri habebi ofisi lazima atakaimishwa mtu ambaye angeweza kuongea na wawekezaji. Hata hivyo project kama hizo wanapokuja wawekezaji mara nyingi kunakuwa na jopo linalokuwa linajadiliana na wawekezaji kama vile waziri au naibu waziri, katibu mkuu au naibu wake, mkurugenzi na bodi yake au principal officers. Wakishafikia makubaliano ndipo mkurugenzi anapewa majukumu rasmi. Hivyo basi hizo project kufeli knawiri sio tatizo lake ni tatizo la mfumo mzima wa serikali na inawezekana kuna maslahi binafsi kwa baadhi ya miradi.

    10. #187
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By BAK
      Hivi kuna usalama wa Taifa nchini mwetu? Unafanya kazi zipi, tangu lini na kwa faida ya nani?
      Upo tena sana tuu, labda tulirekebishe vizuri jina lake, ni USALAMA WA SERIKALI YA CCM, unafanya kazi ya kuhakikisha serikali iko salama, tangu vyama vingi vilipoanza, kwa faida ya chama tawala!
      BAK likes this.

    11. #188
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Gosbertgoodluck
      Zomba, nakubaliana na wewe kwa asilimia 100. Ila hujanijibu kuhusu UHURU kwamba kwa nini asipewe Bw. Mhando? Tambua kwa sasa, CEO wa TANESCO anafanya kazi kwa maelekezo ya wakubwa pale juu. Inawezekana na kuna mambo ambayo yeye na Menejimenti yake wanatamani kuyafanya ili kuboresha utendaji wa shirika lakini hawadiriki kufanya kutokana na wasiwasi wa kuingiliwa na wakubwa. Mimi nadhani wakubwa wa-define targets na kuwawekea sheria na taratibu then waiache TANESCO ijiendeshe kibiashara tuone kama itashindwa. Sina uhakika sana lakini nilipotaka kujua siri ya mafanikio ya mashirika ya ndege kama Kenya Airways na Ethiopian Airline, niliambiwa kwamba serikali zao zimeyapatia mashirika hayo uhuru mkubwa wa kujiendesha kibiashara na zenyewe zinakula faida tu. Kinachotazamwa hapa ambacho ndiyo muhimu ni efficiency.
      Kama ni hivyo huyo Mhando ndio mpumbavu kuwekwa kikaragosi na yeye kukubali. Lakini sikubali kuwa kama shirika utaliendesha vizuri atatokea kidudu mtu kutoka juu huko akatia lake atajulikana tu kuwa ni mkorofi.

      Mhando hawezi na wasifanye makosa tena ya kuweka mtu kama Mhando.

      Wanipe mimi halafu waone aniingilie katibu Mkuu au Waziri au Rais. Kazi yangu wao wangoje matokeo according to plan ya uendeshaji ntakayowakabidhi ikifika muda na nimeshindwa kuitekeleza wana haki ya kunifukuza. Kabla ya hapo haingilii mtu.

      Huyo Mhando anaonesha hana hata plani ya utendaji wake.
      Last edited by zomba; 15th July 2012 at 17:17.
      The Boss likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    12. BAK
      #189
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,633
      Rep Power : 44971
      Likes Received
      8386
      Likes Given
      8363

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Pasco
      Upo tena sana tuu, labda tulirekebishe vizuri jina lake, ni USALAMA WA SERIKALI YA CCM, unafanya kazi ya kuhakikisha serikali iko salama, tangu vyama vingi vilipoanza, kwa faida ya chama tawala!
      Ungekuwepo ndege ya nchi ya kigeni isingeingia nchini na kuzoa wanyama wetu kimya kimya, mafisadi wa EPA, Rada, Kiwira, Dowans n.k. wasingekuwa wanapeta uraiani na mabilioni yao waliyoyapata kifisadi bali wangekuwa wanaozea lupango. Rasilimali za nchi (Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gas n.k.) zisingekuwa zinaibiwa mchana kweupe na kutokuwa na maslahi yoyote kwa Tanzania na Watanzania pamoja na malalamiko mengi toka kwa Watanzania miaka nenda miaka rudi. Hakuna usalama wa Taifa nchini bali kuna Usalama wa mafisadi.
      Pasco likes this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    13. #190
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Josephine
      Pasco,umejitahidi sana kuitetea serikali na kutuamoinisha kuwa Mhando alistahili adhabu.

      Nachokifahamu watendaji hawa wa Tanesco wanafanya kazi katika mazingira magumu sana,kwani katika mambo ya utaalamu siasa zinapoingia ni tatizo kunwa sana.

      Naungana na wengi waliosema alipaswa kujihudhuru mapema sana.

      Tatizo la viongozi hawa ni fadhila wanazopata katika nafasi zao Mf.Mhando anaenda kufanya check up na clinic nje ya nchi kila baada ya mda flani,bado anatunzwa kwa kununuliwa mahitaji makubwa na shirika hii ni hatari sana,watu wanaona hawezi kuachia nafasi zao.
      Mkuu Josephine, siitetei serikali, natetea kufuatwa kwa sheria taratibu na kanuni, ila pia hizo check up sio fadhila, ni stahili halali zinazoendana na post hiyo hata ningekuwa mimi, maadam niliomba kazi, kwanini niachie?. Kuachia ngazi katika mazingira fulani, nako pia ni udhaifu!.

    14. #191
      mafian's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Posts : 45
      Rep Power : 389
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default

      Mhh.....

      Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

    15. #192
      manuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2009
      Posts : 712
      Rep Power : 656
      Likes Received
      263
      Likes Given
      185

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Hivi hii ni nchi ya kina nani?
      TO BE HURT ITS YOUR OWN WILLING

    16. #193
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By BAK
      Ungekuwepo ndege ya nchi ya kigeni isingeingia nchini na kuzoa wanyama wetu kimya kimya, mafisadi wa EPA, Rada, Kiwira, Dowans n.k. wasingekuwa wanapeta uraiani na mabilioni yao waliyoyapata kifisadi bali wangekuwa wanaozea lupango. Rasilimali za nchi (Dhahabu, Almasi, Tanzanite, Uranium, Gas n.k.) zisingekuwa zinaibiwa mchana kweupe na kutokuwa na maslahi yoyote kwa Tanzania na Watanzania pamoja na malalamiko mengi toka kwa Watanzania miaka nenda miaka rudi. Hakuna usalama wa Taifa nchini bali kuna Usalama wa mafisadi.
      Wao ndio walisimamia hiyo ndege ni ya nchi rafiki!, wale twiga sio wetu ni twiga wa nanii ndio aliwatoa kama zawadi kwa yule rafiki yake kumshukuru kwa zile three pieces!. Pesa za rada na EPA walisimamia na ndizo zilizotumika kuimarisha chama na kumuingiza pale mahala!, Kiwira si ni A.B., Dowans pia ni yetu!. Hizo rasilimali, haziibiwi, bali tunawasimamia wazihamishie mahala more secure bali bado ni zetu!,. Kazi ya usalama wa taifa, ni kuhakikisha taifa liko salama, hayo yote uliyoyataja, hakuna hata moja linalohatarisha usalama wa taifa la CCM, yote hayo yanaimarisha zaidi usalama hivyo kiukweli vijana wanafanya kazi nzuri, ndio maana mpaka sasa Tanzania ni nchi ya amani na utulivu sana tuu!. Labda tuu kuna chama fulani cha siasa kinajipanga kuhatarisha usalama wa Taifa la CCM kwa mwaka 2015, Nape ameshakitaja, kitashughulikiwa kabla ili hata baada ya 2015, amani, utulivu na ustawi wa taifa la CCM viendelee kudumu!.
      kaburungu likes this.

    17. #194
      Ndinani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Posts : 2,950
      Rep Power : 1532
      Likes Received
      745
      Likes Given
      237

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Huyu Mhando kazi ndio basi aende akaombe shamba la mkonge alime huko kwao Muheza; nasema hivyo kwasababu nakumbuka mgosi Nundu nae alivyoanza kutoa barua kwenye vyombo vya habari kama njia ya kujihami wakati wa sakata lake wizara ya uchukuzi, lakini njia hiyo ndio iliyomtosa!! Mhando nae kwa kuvujisha hizi barua kwenye media kutoka kwa katibu wake mkuu ndio kutamponza.
      nyumba kubwa likes this.

    18. #195
      BONGOLALA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2009
      Posts : 4,902
      Rep Power : 1477
      Likes Received
      1014
      Likes Given
      128

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Hivi kuna anayejua kwa siku,mwezi tanesco hukusanya kiasi gani cha bill?naona huwa ni siri labda badra atujuze humu jf!

    19. #196
      chuwaalbert's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th September 2010
      Posts : 295
      Rep Power : 500
      Likes Received
      52
      Likes Given
      129

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Hapa wanapeperusha uelekeo wa majadiliano ya Wizara ya Nishati na madini!

    20. #197
      Atukilia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2009
      Posts : 280
      Rep Power : 578
      Likes Received
      83
      Likes Given
      49

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Mo-TOWN
      Nakushauri Next time jaribu kuwa integrative zaidi katika kuchanganua mambo. Fahamu kuwa nje ya darasa the line btn operational na strategic issue si tu inategemea issue husika bali pia ni nyembamba sana kuliko maelezo.

      Tanesco si shirika au kama kampuni ya bia kiwango cha public interest kwa Tanesco ni kikubwa kuliko maelezo. Na kwa maana hiyo sina uhakika kama unafahamu kuwa umeme ni strategic issue kwa nchi. Vile kwa darasani ni rahisi kusema kuwa kina cha maji kimepungua ghafla na sio ktk real life never...kina cha maji kinakuwa monitored na kupungua kwake haliwezi kuwa swala la dharura.
      Kwani mimi nazungumzia umeme kwa ujumla wake au tukio la kupungua maji kwa ghafla kwenye bwawa la mtera kutokana na matumizi kuongezeka? Ni Kweli wana monitor maji kila siku lakini kumbuka baada ya masika maji yalikuwa bado yapo chini ya kiwango hivyo matumizi yakiongezeka kidogo impact yake inakuwa kubwa. Mimi nadhani badala ya kubishana kuhusu bwawa la Mtera serikali iwekeze kwenye vianzo vipya vya umeme kama Stigler Gorge na Kiwira. Vinginevyo kila mwaka tutabadili CEO na kumbuka kadri life span ya CEO inavyokuwa fupi ndio na compensation yake inavyozidi kuwa kubwa
      There is a thin line between madness and creativity

    21. #198
      Gosbertgoodluck's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 2,863
      Rep Power : 1149
      Likes Received
      334
      Likes Given
      4

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Pasco
      Wao ndio walisimamia hiyo ndege ni ya nchi rafiki!, wale twiga sio wetu ni twiga wa nanii ndio aliwatoa kama zawadi kwa yule rafiki yake kumshukuru kwa zile three pieces!. Pesa za rada na EPA walisimamia na ndizo zilizotumika kuimarisha chama na kumuingiza pale mahala!, Kiwira si ni A.B., Dowans pia ni yetu!. Hizo rasilimali, haziibiwi, bali tunawasimamia wazihamishie mahala more secure bali bado ni zetu!,. Kazi ya usalama wa taifa, ni kuhakikisha taifa liko salama, hayo yote uliyoyataja, hakuna hata moja linalohatarisha usalama wa taifa la CCM, yote hayo yanaimarisha zaidi usalama hivyo kiukweli vijana wanafanya kazi nzuri, ndio maana mpaka sasa Tanzania ni nchi ya amani na utulivu sana tuu!. Labda tuu kuna chama fulani cha siasa kinajipanga kuhatarisha usalama wa Taifa la CCM kwa mwaka 2015, Nape ameshakitaja, kitashughulikiwa kabla ili hata baada ya 2015, amani, utulivu na ustawi wa taifa la CCM viendelee kudumu!.
      Hapo kwenye rangi nyekundu sikubaliani na wewe. Ni kosa sana kusema nchi yetu ni ya AMANI. Ninachoweza kukubali ni UTULIVU. Huwezi kuwa na watu wenye hali ngumu ya maisha kiasi hiki halafu ukasema nchi ina amani. Kila kukicha maisha yanaendelea kuwa magumu, bei za bidhaa kama vyakula na other basic social services zinaongezeka kila kukicha halafu useme nchi ina amani!!!!! Hapana Pasco, kilichopo sasa hivi ni utulivu ambao tusipoangalia unaweza kuwa na kishindo kikubwa.
      Pasco and kaburungu like this.
      "Before God we are all equally wise and equally foolish"

    22. #199
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Gosbertgoodluck
      Hapo kwenye rangi nyekundu sikubaliani na wewe. Ni kosa sana kusema nchi yetu ni ya AMANI. Ninachoweza kukubali ni UTULIVU. Huwezi kuwa na watu wenye hali ngumu ya maisha kiasi hiki halafu ukasema nchi ina amani. Kila kukicha maisha yanaendelea kuwa magumu, bei za bidhaa kama vyakula na other basic social services zinaongezeka kila kukicha halafu useme nchi ina amani!!!!! Hapana Pasco, kilichopo sasa hivi ni utulivu ambao tusipoangalia unaweza kuwa na kishindo kikubwa.
      Mkuu Gosbert Goodluck, kubali kataa, Tanzania ni nchi ya amani!, kinyume cha amani ni vita!. Kwa vile hatuna vita, then tuna amani!. Watanzania ni watu wapole, watu wa amani na ni watulivu sana!, hata bei zi pande mpaka mbinguni, hutufanyi jambo lolote la kuvuruga amani iliyopo!. Ndio maana nimeeleza usalama wa taifa la CCM wako macho kufuatilia hiki chama kinachotaka kutishia usalama wa CCM mwaka 2015, na watakishughulikia kabla ya 2015, ili kuhakikisha hata baada ya 2015, usama wa taifa la CCM unaendelea ili kuienzi amani na utulivu uliopo!.
      Kingcobra and kaburungu like this.

    23. #200
      Kingcobra's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th January 2011
      Posts : 713
      Rep Power : 564
      Likes Received
      128
      Likes Given
      14

      Default Re: JF EXCLUSIVE: Sababu ya Kuachishwa kazi Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO

      Quote By Pasco
      Mkuu Gosbert Goodluck, kubali kataa, Tanzania ni nchi ya amani!, kinyume cha amani ni vita!. Kwa vile hatuna vita, then tuna amani!. Watanzania ni watu wapole, watu wa amani na ni watulivu sana!, hata bei zi pande mpaka mbinguni, hutufanyi jambo lolote la kuvuruga amani iliyopo!. Ndio maana nimeeleza usalama wa taifa la CCM wako macho kufuatilia hiki chama kinachotaka kutishia usalama wa CCM mwaka 2015, na watakishughulikia kabla ya 2015, ili kuhakikisha hata baada ya 2015, usama wa taifa la CCM unaendelea ili kuienzi amani na utulivu uliopo!.
      Pasco, amani unayozungumzia hapa ni ya kisiasa na kama ulivyosema ni kinyume cha vita. Lakini kwa maana pana zaidi ambayo kwa kweli ndiyo viongozi wetu wanapaswa kuitafuta kwa udi na uvumba ni amani inayotokana na wananchi kuridhika na hali iliyopo na kuendelea kuwa na matumaini na mwenendo wa serikali yao katika kuwaletea maendeleo. Hali hiyo, kwa nchi yetu ni kama an ideal situation ambayo haiwezi kufikiwa. Hivi sasa ukitembea mitaani watu wengi wanang'unika juu ya utendaji mbaya wa serikali na kasi ya kuongezeka kwa pengo kati ya matajiri na maskini. Kwa sisi tunaopata kuongea hata na watendaji waandamizi wa serikali na hata chama tunajua kwamba manung'uniko yapo hata kwa watendaji hao lakini hawapo tayari kujitokeza hadharani. Manung'uniko hayo yanatengeneza bomu taratibu na ushahidi mzuri ni nchi Ivory Coast ambayo nayo ilisifiwa sana kwa hiyo inayoitwa amani kumbe in actual fact hakukuwa na amani. Ilipolipuka, watu walianza kuchinjana kwa kiwango ambacho mtu yeyote asingetarajia.
      Pasco and kaburungu like this.
      "The richest man is not he who has the most, but he who needs the least"

    Page 10 of 16 FirstFirst ... 89101112 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...