
By
Tumaini Makene
Wakuu na Mods
Njia ya muongoni fupi sana. Wabunge wa CHADEMA wasiokuwa na majina wamefika Ndago saa 8.30 mchana?????!!!!!!
Wakuu, kuna Operesheni ndogo kwa Mkoa wa Singida yakiwa ni maandalizi ya operesheni kubwa kwa mikoa mitano, Singida, Iringa, Dodoma, Manyara na Morogoro, kama ilivyoazimiwa na Kamati Kuu mapema wiki hii.
Kazi hiyo iko chini ya timu inayoongozwa na Kamanda Mwita Mwikabwe Waitara, yeye ndiye mratibu wa ziara hii fupi na leo ilianzia katika Wilaya ya Iramba, Jimbo la Iramba Magharibi, ambapo mikutano ya hadhara imefanyika katika maeneo ya Ndago na Kinampanda.
Kulikuwa na taarifa tangu siku tatu zilizopita, timu ikiwa bado Dar es Salaam, kuwa kuna kikundi cha vijana wamekodiwa, wananunuliwa pombe, wakiandaliwa kufanya fujo ili mkutano huo usifanyike kisha ionekane CHADEMA wameshindwa kufanya mkutano kwa Mwigulu Nchemba. Bahati mbaya sana kitumbua chao kimeingia mchanga. Nafikiri hata huyu mleta maada ni sehemu ya hiyo propaganda.
Sasa wakati mkutano umefunguliwa tu, Kamanda Mwita akawa-preempty kwa kuwaambia kuwa taarifa hizo tayari zinajulikana na polisi wawe makini. Haa! Jamaa waka-panic. Walikuwa mbele kabisa pale. Wakaanza kurusha maneno, wanapiga makelele, wanazunguka zunguka pale mbele ya hadhara. Mbele ya polisi. No action.
Kelele za kundi lile, hazikuwa zikivumilika. Wananchi hawakukubali uvunjifu wa amani wa makusudi uliokuw aukifanywa mbele ya polisi. Yaani sinema ile ilikuwa Ilemela-type, kule ambako wabunge wa CHADEMA walivamiwa, kukatwa mapanga mbele ya polisi wenye silaha. Brothers, huwezi kuamini lile kundi likajitenga pembeni na kuanza kurusha mawe.
Wananchi wengi waliokuwa pale mkutanoni kwa mamia, hawakukubali ufidhuli ule. Wakawafukuzilia mbali wale wahuni. Mkutano ukaendelea kwa amani kabisa, kisha tukaelekea mkutano wa pili Kinampanda, ambako John Mnyika, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi na Mbunge wa Ubungo, amemaliza kupiga nondo kama alivyopiga Ndago.
Wananchi wamemskiliza John kwa makini, sasa kazi zinanunuliwa. Nondo zinawagusa wananchi wa Iramba Mashariki, yakiwa ni maandalizi ya Opereseheni kubwa inayokuja mikoa hii muda si mrefu.
Follow Us Here