Jioni hii live tbc waziri tibajuka anena kiprofesa.
Maneno ya nguvu kuwa
"hakuja nyumbani kutoka un ili aje kupambana na maskini bali kaja kupambana na umaskini"
Jioni hii live tbc waziri tibajuka anena kiprofesa.
Maneno ya nguvu kuwa
"hakuja nyumbani kutoka un ili aje kupambana na maskini bali kaja kupambana na umaskini"
Huyu mama anafaa kuwa rais jamani
Honestly i declare it
Halafu wewe unafaa kuwa PM wake!
...------------------------------------------------.---------------------------------------------------------------------..Rather Kill a FRIEND than Risk Missing an ENEMY
mama mnafiki huyu, kelele nyingi zisizo na manufaa.
"Serikalii hii ni IMPOTENT kuanzia yule wa juu hadi walioko chini" by Dr. Slaa
Hata yule jamaa wa msoga alianza hivyo hivyo ...mara ooh "Maisha bora kwa kila mtanzania..mara ari mpya, kasi mpya.. mara sijui nini" ...mwishowe wengi tukaingia mkenge na jamaa akajizolea ushindi wa kishindo. Matokeo yake kila mtu sasa anajuta.
Nshomile bwana. Kiswahili maneno matatu, kinatupiwa kiingereza. Hotuba yake itapita haraka maana magamba yatakuwa yanaitikia tu.
Kizuri ni kizuri tu lakini bora ni zaidi ya kizuri.....Laiti km huyu MAMA PROF TIBAIJUKA angekua ndani ya CCM ile ya NYERERE nadhani angekua fanya makubwa...Huyu MAMA anahujumiwa na serikali dhaifu japokua system inajaribu kumpunguzia kasi lakini chenye ubora kinaonekana..Tukumbueke kati ya wizara nyeti inayomgusa kila MTANZANIA mojawapo ni hii...Sheria zimevunjwa wenye haki wakanunuliwa nawenye fedha,ARDHI yao ikaporwa,maeneo yaliyotengwa kwa shughuli mahsusi km vile viwanja vya mipira, vikauzwa kwa wenye fedha,maeneo ya fukwe tunajua sheria inasema watu wanapaswa kujenga kuanzia hatua ngapi lakini serikali apo nyuma haikuona ilo lakini nakumbuka alipokuja huyu MAMA mwanzono kabisa alisema atavunja maeneo yote na kweli wamekiona...Tunakupa moyo MAMA tenda kazi kwa manufaa ya waTanzania na sio nini CCM inataka japo unagusa interest zao lakini MUNGU yupo na wewe....Km uliweza kuishauri KENYA kuhusu KIBERA kwanini nyumbani ushindwe
Huyu mama tangu awe na hiyo wizara sioni alichofanya, wenje kamwambia u profesor wake hauna maana kama anaitwa kwenda kumaliza migogoro ya ardhi na haendi ni profesor wa nini, hajakanyaga jiji la mwanza toka awe waziri wa ardhi licha ya kuitwa na wabunge wa mwanza! haoni hata mwanza ni jiji ambalo linachangamoto kibao za ardhi na makazi, mama wa watu kakomaa na kigamboni utafikiri tanzania ardhi pekee iko kigamboni tu!! Profesor.
Ni kweli kwamba kila mmoja wetu anaudhaifu wake as a human being lakini Prof. Tibaijuka kathibitisha kuwa ni msomi anaejua anachokifanya. Tuseme mapungufu yake lakini kwa leo tumpe hekoo yake
Ni mzuri ndani ya system mbovu na fedha kidogo so we should not expect much from her.
'Our Problems can be solved,our challenges can be met'- Obama
Jamani tuseme ukweli huyu mama ni professor wa ukweli kashuka nondo za ukweli, na yote anayozungumza anarefer internationally how they do, kile ukweli tumpongeze kwa hili. Na anaonekana amejipanga sana. Kuwa kiongozi sio kulalamika ila kutoa suluhu. Mama nakukubali. Hongera
Yes Indeed huyu mama leo ameongea kizalendo sana,ana vision ya mbali sana.Kwa kweli kama yeye ndio aliyewashauri NAIROBI WAJENGE METROPOLIAN CITY NA WAKAMSIKILIZA NA KUFANYA IMPLIMENTATION.Sisi tukienda nairobi tunapasifia.We need to have nidhamu ya kazi na focus.Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni(Fidia zilipwe kutokana na market values zilizopo na yeye ameadmit).Huyu mama kwa miaka miwili na nusu aliyokaa tu katika hiyo wizara,amedhubutu na kufanya maamuzi magumu.Tumuombee sana huyu mama na watendaji wenzake waweze kurudisha nidhamu katika hii wizarailiyokuwa imejaa uozo.
Mimi siangalii CCM wala CDM lakini lazima nikiri kwamba mama Tibaijuka anauwezo mkubwa sana. Tukumbuke hii miradi imesimama kwa muda gani, tukumbuke nani alishakuwa na ujasiri wa kubomoa nyumba za mafisadi, tukumbuke nani ana uwezo wa kutoa elimu bungeni na bunge lote likakaa midomo wazi, n.k
Miradi anayotaka kufanya huyu mama tuiunge mkono na sio kuitathmin kiCCM zaidi. Huyu mama na uwezo, ni msomi na ni mzalendo.
Hatakwepa kuwa kashindwa kupambana na umasikini na sasa anapambana na masikini, bei ya kiwanja inapofika 10Milions, Ulanguzi wa viwanja vya makazi, makazi holela vimemshinda sasa anapambana na maskini kwa kumuacha maisha yamtungwe KO
sidhani kam ayalikuwa mawazo yake.Yangekuwa ndio mawazo yake angekuwa ameandika paper na kuwaachia ccm>From wat i know UN habitat wana researches nyingi sana za watafiti mbalimbali na yeye anaweza aiwepo kati ya researchers.So kama aliwabembeleza kenya wafanye pilot project huku wakipewa mihela sidhani kama ingeshindikana .Kenya tayari wana real estate industry iliyokomaa sana zaidi ya tanzania na wasingekuwa tayari ziachia hela kwa kitu wanachokijua zaidi.
SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.
Uhaya si issue unless someone has an inferior brain! Nilisikiliza hotuba yake yoote, nadhani Watanganyika tumeona ni aina gani ya viongozi wa kuikomboa hii nchi! 1)Elimu iliyotukuka,2)) uzalendo, 3) proven expertise! vyote vitatu kwa pamoja. Sio kina wengine, wenye baadhi ya hivi lakini si vyote. We have no more time to give people a try @ presidency level.
Agreed ! Tena pale anapita kimya kimya akiwa anakwenda kwao kula ndizi.
Huwezi kuwa makini ukafanya lolote la maana ndani ya CCM hasa ya Dhaifu. Huyu kule kashahaidiwa, na kukatiwa kiamba kule uarabuni ili kivukoni ikikamilika tu basi next time utamuona ktk magazeti yupo bichi hawaii amekula pensi huku akijipoza kwa juisi ya madafu..! Zile mbwembwe za ukuta sijui Palm beach umeshasikia utekelezaji ???
Follow Us Here