Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 37
    1. #1
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Leo Mwigulu Mchemba ameomba mwongozo kuhusu ushahidi wa John Mnyika alioufikisha kwenye ofisi za Bunge.

      Cha msingi hapa ni kwamba Job Ndugai ameeleza kuwa wabunge waache tabia ya uongo na kujiamini kwamba wana ushahidi. Ndugai ameeleza kwamba wote ambao waliwahi kufikisha ushahidi kwa Spika Hakuna hata mmoja aliyeleta ushahidi unaokidhi vigezo vya ushahidi.

      Kuhusu ushahidi alioleta Mnyika, Ndugai kasema kwamba Mnyika ameleta maelezo ya utangulizi na wala si ushahidi halisi. Hivyo, kwa suala hili la Mnyika ameamua kulifikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge na huko Mnyika ataandikiwa barua kama hatua ya kwanza.

      Binafsi hapa sina matatizo na uamuzi wa Job Ndugai, uamuzi wa kiti cha Spika. Sitetei uhalisi wa ushahidi aliowasilisha John Mnyika.

      Hoja yangu ni jinsi Ofisi ya Spika inavyoshughulikia masuala haya.

      Tangu Bunge hili la 10 limeanza chini ya Anne Makinda kama Spika, sikumbuki ni idadi gani ya wabunge hasa wa CHADEMA wameombwa kuleta ushahidi na wakaleta. Kwa kutaja ninaojua ni Godbless Lemma, Zitto Kabwe, Ezekah Wenje nk.

      Lakini leo ni miezi 17 imepita tangu mtu wa kwanza kuambiwa alete ushahidi na haukushughulikiwa. Ushahidi huo ni ule wa Godbless Lemma ambaye sasa hauhitajiki kwa sababu mbunge hoja yake inakufa anapokoma kuwa mbunge na hivyo suala la Lemma limefungwa hivyo.

      Lakini bado kuna ushahidi mwingi wa wengine una zaidi ya mwaka hatuoni kasi yoyote ya kushughulikia.

      Sasa umekuja ushahidi wa John Mnyika. Haujamaliza hata siku mbili Kiti cha Spika kimetoa maamuzi kwamba upelekwe Kamati ya Maadili na haki ili Mnyika aanze kuwajibika kwa kuandikiwa barua. Narudia simetetei Mnyika na inawezekana kabisa ushahidi wake ni hafifu na ikibidi ni wa uongo.

      Taaabu yangu ni kwamba kiti cha Spika kimeonyesha double standards ambazo watazania wote tunaendelea kuangalia kana kwamba tunaangalia ngumi za jogoo wawili wakipigana na kama vile sisi haituhusu.

      Iwapo John Mnyika ataandikiwa barua, bais huo ni ushahidi tosha kwamba Spika amefanya amevunja katiba. Je, Spika kavunja katiba kwa namna gani?

      Ibara ya 9(h) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema hivi: { Kwa hiyo, Mamlaka ya Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo zinaondolewa nchini }.

      Ibara ya 13(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema hivi: {Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria}.

      Wakati humohumo katibani Ibara ya 13(2) inasema hivi: {Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake}.

      Kama yapo mengine yanayotaja neno ubaguzi au upendeleo basi mtaonyesha lakini kwa hoja yangu hapa inanitosha. Sasa ubaguzi unaokatazwa na katiba unaigusaje issue hii ya ushahidi wa John Mnyika?

      Ubaguzi ni kwamba Ofisi ya Spika wa bunge lilelile ameonyesha sura mbili kwa suala lilelile yaani kushughulikia ushahidi. Ni kweli kuwa kanuni hazitaji ni lini na kwa haraka gani Spika anatakiwa kushughulikia masuala haya ya kuuanika ushahidi au kuushughulikia.

      Lakini hapa tumeona kuwa suala la ushahidi wa John Mnyika Spika hakusubiri hata masaa 48 yapite.

      Hivyo, hii ni nafasi ya kulichukulia jambo hili kuwa ni la katiba. Kuna watu watakuja na hoja kwamba Bunge lina kinga. Hawa ni wale ambao hawajui maana ya kinga na hawajsoma utaratibu wa kinga au sheria ya kinga.

      Hakuna mtu hapa nchini aliye juu ya katiba. Hakuna taasisi iliyo juu ya Katiba, siyo Ikulu au Ofisi ya Bunge, siyo Rais wan chi siyo Spika au Naibu Spika. Kinga ya bunge ni kinga kwa ajili ya kuendesha majadiliano maadamu majadiliano hayo hayavunji haki ya mtu yeyote duniani.

      Bunge, mbunge, Spika, Naibu Spika wote hao waliapa kulinda katiba na si kuvunja hata kipengele kimoja.

      Je, uvunjaji wa Katiba ni uhalifu wa aina gani? Kwa kiingereza wapo wanaouita “treason”. SIna hakika kama “Uhaini” ndilo neno sahihi kwa dhambi ya uvunjaji wa katiba.

      Kuvunja katiba si lazima uvunje vipengele vyote. Na mara nyingi si rahisi kuvunja katiba yote maana hiyo sasa itakuwa si uvunjaji wa katiba bali hayo ni “Mapinduzi” kama mapinduzi yoyote duniani.

      Kuvunjwa katiba ni pale kinapovunjwa kipengele kimoja au kadhaa vya katiba.

      Kwa hoja hii ya John Mnyika, vipengele vyote vinavyozuia ubaguzi ndani ya Jamhuri yetu vimevunjwa. Hii sasa ni kesi ya kikatiba. Mahala pake ni mahakamani. John Mnyika akipata barua basi huo ndiyo mwanzo wa kulipeleka suala hilo Mahakamani.

      Ninaweza kutaja mifani mingi ya mambo ya mabunge ya Commonwealth kufikishwa mahakamani lakini hata hapa Augustine Mrema alishawahi kupinga adhabu yake bungeni kwa kwenda mahakamani. Japo Mrema alishindwa kwenye kesi ile iliyoendeshwa na Jaji Katiti lakini Mahakama haikuzuia case ile eti tu kwa sababu ni jambo limetokea bungeni.

      Hata msingi wa kesi ya Mrema ilijikita kwenye misingi ya Katiba kwamba pamoja na kutoridhika na adhabu ya kufungiwa ile adhabu ilikuwa inamnyima haki yake ya kikatiba kushiriki vikao vya Bunge. Pendekezo ambalo lilikataliwa na Jaji Katiti kwamba kuhudhuria vikao vya Bunge si haki ya kikatiba.


      Hivyo, watanzania tuamke tulitizame jambo hili kwa muono huo na si kulalamika kama tumeishiwa hoja. Tunajadili katiba mpya na hivyo kesi kama hizi ni kipimo kwetu kuona kama kweli tunaelewa tunalojadili au la.

      Hatuwezi kuendelea kuona Spika akivunja katiba kwa kutoa upendeleo na ubaguzi ambao umekatanzwa na vifungu tele vya katiba yetu. Sasa tujikite wote tulitizame kuwa ni jambo la katiba.

      Wabunge wa CHADEMA watumie nafasi yao kulipeleka hili suala Mahakamani maana nis suala la kuvunjwa kwa katiba. Ushahidi upo mwingi tu kuonyesha Bunge ni taasisi inayoendekeza ubaguzi. Ukianzia na suala la Tundu Lissu ambapo Spika alilidanganya Bunge kuwa Tundu Lissu ni mshtakiwa wa mauaji. Kuna suala la kufikishwa kwa ushahidi wa Zitto Kabwe. Kuna suala la ushahidi kuhusu uongo wa Waziri Mkuu kuhusu mauaji ya Arusha hadi Lemma amepoteza ubunge.

      CHADEMA wakienda mahakamani tutakuwa tumenyoosha adabu kwamba katiba si ya kuchezewachezewa kwa dhana ya kwamba kuna chama kina wabunge wengi na kinaweza kujivunia hilo kwa kudhani kiko juu ya katiba kwa sababu Rais, Spika, Naibu Spika wanatoka chama hicho.

      Ninaamini wanasheria mliomo humu JF na kokote mnalijua hili kunizidi.

      CHADEMA mkishindwa hapa basi inabidi watu tufungue macho na kuwakamia nyinyi wala si Anne Makinda au Job Ndugai. Mara nyingi mmekuwa mkitutangazia magazetini kuhusu upendeleo wa Spika na mnamuacha hivyohivyo wakati uwezo uko mikononi mwenu.

      Mwaka jana Tundu Lissu alitutangazia kuwa amempeleka Spika Anne Makinda kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge baada ya kuzuia swali lake kwa kisingizio kwamba ana kesi Mahakamani wakati Tundu Lissu hakuwa na kesi ya mauaji ya Tarime. Tukasubiri kwa hamu matokeo ya kesi ile maana tulijua hapa ndipo Spika Anne Makinda angekiona cha moto maana ushahidi wa hili ilikuwa wazi na asingekwepa kibano kile.

      Lakini kwa mshangao wa watu kama mimi hadi leo hakuna lolote kuhusu suala lile kana kwamba Kamati ya Kanuni za Bunge haikumjadili Spika Makinda kwa kumpendelea Waziri Mkuu na kumzuia Tundu Lissu kujibu swali.

      Hivyo ndivyo ninaona dawa inaweza kupatikana kwa masuala haya kwani tumechoshwa na marudio ya haya mambo.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      POMPO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 2,955
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1090
      Likes Given
      625

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Mkuu katiba hiyo hiyo inasemaje kuhusu kuingilia mhimili mwingine? I mean Bunge VS Mahakama?
      Nikupateje and IFUNYA like this.

    4. mob
      #3
      mob's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2009
      Posts : 594
      Rep Power : 599
      Likes Received
      103
      Likes Given
      32

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      mkuu umenena ninachokiona wanapendeleana wakiamini na sisi huku hatujui mambo ila inabidi waelewe watanzania wa leo sio wa mwaka 67
      Nikupateje likes this.

    5. #4
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Quote By POMPO
      Mkuu katiba hiyo hiyo inasemaje kuhusu kuingilia mhimili mwingine? I mean Bunge VS Mahakama?
      Mkuu POMPO,

      Neno "Mhimili" halimo ndani ya Katiba.

      Tusirefushe thread wakati nimeshaeleza ndani ya post yangu kwamba Maamuzi ya mashauri ya kikatiba ni mahakamani.

      Nikaonyesha jinsi kesi ya Augustine Lyatonga Mrema akiwa mbunge wa Temeka, ilivyokubaliwa Mahakamani na akashindwa kwa msingi wa kushindwa kujieleza Mahakamani lakini si kwa msingi wa case kukataliwa kwa sababu ya neno "Mhimili".
      Last edited by Nikupateje; 12th July 2012 at 15:05.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    6. #5
      buyegiboseba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Posts : 535
      Rep Power : 510
      Likes Received
      139
      Likes Given
      39

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Tusubiri kwanza maamuzi ya hiyo kamati ndo tutajadili hiki ulichokipendekeza
      Nikupateje likes this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Bobuk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 2,056
      Rep Power : 920
      Likes Received
      829
      Likes Given
      0

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Hivi na ile KESI ya kupinga uteuzi wa Wabunge wa East Africa imefikiwa wapi?

      Maana CCM kwa wingi wao walipindisha sheria za utezi wa wabunge hao.

    9. #7
      aduwilly's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2009
      Posts : 708
      Rep Power : 660
      Likes Received
      109
      Likes Given
      39

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Unadhani MAHAKAMANI ndo kupo salama, ubaguzi ni kila pala kaka, we kamua zako ugali tu cku ziende ungojee kifo tu, ukitaka haki duniani unajipotezea muda tu kwani hutaipata popote pale

    10. #8
      Matola's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 12,465
      Rep Power : 0
      Likes Received
      5425
      Likes Given
      3612

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Nitarudi hapa.

    11. #9
      Gulwa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th June 2008
      Posts : 138
      Rep Power : 584
      Likes Received
      46
      Likes Given
      0

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Mahakama zetu zinaaminika? Majaji wetu niwaadilifu kiasi gani? Je uteuzi wao si wa kisiasa zaidi? Tafakari

    12. #10
      POMPO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 2,955
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1090
      Likes Given
      625

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Quote By Nikupateje
      Mkuu POMPO,

      Neno "Mhimili" halimo ndani ya Katiba.

      Tusirefushe thread wakati nimeshaeleza ndani ya post yangu kwamba Maamuzi ya mashauri ya kikatiba ni mahakamani.

      Nikaonyesha jinsi kesi ya Augustine Lyatonga Mrema mwaka ilivyokubaliwa Mahakamani na akashindwa kwa msingi wa kushindwa kujieleza Mahakamani lakini si kwa msingi wa case kukataliwa kwa sababu ya neno "Mhimili".
      Nimekusoma mkuu, ila mahakam zetu si unazijua? altenative ni NGUVU YA UMMA tu ifanye kazi
      Nikupateje and IFUNYA like this.

    13. #11
      Makala Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2011
      Posts : 1,559
      Rep Power : 702
      Likes Received
      320
      Likes Given
      0

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Ni suala la msingi sana,hata leo hii mi sijamwelewe J.Ndugai. Anadai ushahidi haujajitosheleza kwani amejadili na nini? Je,yeye anajua nini kuhusu EPA? Yeye anao ukweli kadiri gani kuhusu EPA na anawaambia nini Watanzania?

    14. #12
      Ukwaju's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : Dodoma
      Posts : 3,414
      Rep Power : 1117
      Likes Received
      627
      Likes Given
      821

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Jamaa yangu mbona umetutoa kwenye utamu unatuleta huku ambako siko (tuanchokifuata ni kweli MWIGULU kamsamehe MNYIKA? basi)
      Haya mambo unayoyaleta kabisa hayaingiliani na Mihimili mitatu
      Nakuuliza ni nani anayelivunja Bunge na wote wakarudi majimboni kuomba kura upya?
      usiwape wasomaji habari za uchochezi, eti waende mahakamani wakashtakiwe Anne na Job
      turudishe kwenye mada
      Sending by: BlackBerry 8100 Smartphone using JamiiForum

    15. #13
      kimeloki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th July 2012
      Posts : 554
      Rep Power : 455
      Likes Received
      56
      Likes Given
      6

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Kiti cha spika inawayawaya.

    16. #14
      JamboJema's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 14th June 2011
      Location : Mwanza
      Posts : 736
      Rep Power : 548
      Likes Received
      75
      Likes Given
      216

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Double starndard ipo na inategemewa. Ninachowasihi hawa jamaa ni kuwa makini na 'actions' zao dhidi ya CDM...wanawapaisha bila kujijua. Kwa sasa ilivyo, hata kama Mnyika kawasilisha ushahidi 'nyanya' vipi, jamii itaamini anaonewa kama ilivyofanyika kwa Zitto alipomtuhumu Karamagi.
      Ni huyu huyu Ndungai alimtoa nje Lisu eti kwa kuwasha 'mic'. Alipobanwa kuwa hakuna kifungu kinachosema hilo ni kosa akabadilika...... Ni aibu tupu. Wanatakiwa wawe na weledi zaidi kupambana na CDm ili CDM waonekane 'malimbukeni' lakini kwa mwendo huu watashangaa wanabaki wenyewe!
      Uchakavu wa Mahakama si nafuu ya hukumu!

    17. #15
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Quote By Gulwa
      Mahakama zetu zinaaminika? Majaji wetu niwaadilifu kiasi gani? Je uteuzi wao si wa kisiasa zaidi? Tafakari
      Unapotafakari kuhusu imani kuhusu mahakama zetu usiache kutafakari hukumu ya kesi ya Ubunge ya John Mnyika iliyofunguliwa na Hawa Ng'umbi.

      Usisahau pia hukumu kesi ya Oscar Mukasa wa CCM kupinga ubunge wa Dr. Mbasa wana-CHADEMA mbunge wa Biharamuro.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    18. #16
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,163
      Rep Power : 12557
      Likes Received
      5736
      Likes Given
      748

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Mahakama gani wataenda kila siku wanasema hawana imani na mahakama. na polisi.

    19. #17
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Quote By Ukwaju
      Jamaa yangu mbona umetutoa kwenye utamu unatuleta huku ambako siko (tuanchokifuata ni kweli MWIGULU kamsamehe MNYIKA? basi)
      Haya mambo unayoyaleta kabisa hayaingiliani na Mihimili mitatu
      Nakuuliza ni nani anayelivunja Bunge na wote wakarudi majimboni kuomba kura upya?
      usiwape wasomaji habari za uchochezi, eti waende mahakamani wakashtakiwe Anne na Job
      turudishe kwenye mada
      Mkuu sikiliza,

      Inawezekana aliyeanzisha ile thread alituma wakati nina-edit hii yangu. Lakini nimesoma thread yake sielewi kwa nini ameamua kuongopa kwani nimesikiliza Mwigulu tangu wakati anaomba mwongozo na sikusikia maneno ya kusamehe.

      Hivyo, thread ile ama mleta mada alikurupuka ama amedhamiria kupotosha kilichoelezwa.


      Suala la kuvunja Bunge hilo si mada yangu. Tusirefushe thread kwa kuleta hoja ambazo mngeweza kuanzisha thread nyingine ingekuwa ni efficient step.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    20. #18
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Quote By Ritz
      Mahakama gani wataenda kila siku wanasema hawana imani na mahakama. na polisi.
      Maadam hukanushi hoja zangu basi nakukaribisha kwa mara ya kwanza umekubaliana na hoja yangu.
      Sijatamka neno "Polisi" kwenye thread yangu.

      Na zaidi, kwa sababu hoja zenu zimeanza kujirudia soma post namba 15 hapo juu nilivyomjibu mwenzako.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    21. #19
      Biohazard's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 1,365
      Rep Power : 991
      Likes Received
      308
      Likes Given
      210

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      HApo umenena mkuu
      Nikupateje likes this.

    22. #20
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 846
      Rep Power : 963
      Likes Received
      538
      Likes Given
      592

      Default Re: John Mnyika na CHADEMA nendeni Mahakamani. Anne Makinda na Job Ndugai wamevunja Katiba bungeni

      Quote By Bobuk
      Hivi na ile KESI ya kupinga uteuzi wa Wabunge wa East Africa imefikiwa wapi?

      Maana CCM kwa wingi wao walipindisha sheria za utezi wa wabunge hao.


      Quote By buyegiboseba
      Tusubiri kwanza maamuzi ya hiyo kamati ndo tutajadili hiki ulichokipendekeza
      Mkuu buyegiboseba,

      Nakubaliana na wewe. Ndiyo maana nimeleta thread kiasi kwamba wenye mawazo kama wewe muweze kuiboresha na pia mtumie muda wenu kuwaelimisha kama wenzako hapo juu ambao wanaleta kesi ya ubunge wa East Africa ambapo tukiishia kutaja kesi basi tutataja nyingi na mimi nimetaja ya Mrema nikidhani ilikuwa ni rahisi kueleweka.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    23. Study Abroad
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...