Ki ukweli, Tanzania tunahitaji miaka 50 ili kujiendesha wenyewe bila misaada!
Kuhusu mikopo, hata USA wanakopa, hivyo Tanzania sidhani kama tunaweza kukwepa kukopa!
Nikirudi kwenye misaada, kutokana na mfumo tulioachiwa na wakoloni (ukoloni mambo leo) ni vigumu sisi kusimama peke yetu kwa kipindi hiki, wengine watadai kuwa tuna resources nyingi ambazo zikitumika vizuri tunaweza kujiendesha bila kutegemea misaada, lakini swali la kujiuliza ni je, vifaa, teknolojia na ujuzi wa kuvuna na kutumia hizo resources tunao?
Jibu ni HAPANA, na ili tuwe na huo uwezo naamini tutahitaji miaka 50! Hii haijalishi ni chama gani kipo madarakani, iwe CCM, CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI, au hata tukikodisha chama cha siasa kutoka nje. etc.
Kitu cha ajabu ni kuwa hata South Africa naye anategemea msaada japo ni kwa asilimia kidogo ukilinganisha na Tanzania!
Follow Us Here